Riwaya: Siri

SIRI
PART 1: SEASON 4
MTUNZI: PATRICK CK
Eneo lote la kuzunguka
kitalu 7 kulikuwa na giza
lililosababishwa na kukatika
kwa umeme baada ya nguzo
kulipuliwa na mlipuko.Kaiza na
watu wake waliacha gari lao
umbali wa mita mia mbili
wakatembea kwa miguu
wakiwa katika tahadhari
kubwa.Kila alipojaribu kupiga
simu kwa watu wake
waliokuwa wakilinda nyumba
ile hazikuwa zikipokelewa hii
ikazidi kumpa hofu.Walifika
katika geti la kuingilia ndani ya
ile nyumba na kukuta mtu wa
kwanza akiwa amelala chini
amekwisha kufa.Wakamgeuza
wakamtazama alikuwa
amepigwa risasi katika paji la
uso.
“Damn !! Kaiza akasema
kwa hasira
Waliendelea kuzunguka
ukuta uliozunguka ile nyumba
na kukuta miili ya watu kumi na
tatu.
“Hii ni mara ya kwanza
tukio kama hili linatokea katika
idara yetu.Nani kawaua watu
hawa wote? akajiuliza Kaiza na
kumpigia simu Zakaria
akamtaka afike pale kitalu 7
kwani wao tayati walikwisha
fika.Haraka haraka
akawaelekeza watu aliokwenda
nao waingize miili yote ndani
kisha akawasiliana na Devotha
kumjulisha kile alichokikuta
“Devotha ni hali ya
kusikitisha sana iliyoko hapa.P3
Unit imekwisha.Watu kumi na
tatu wote wameuawa
isipokuwa Zakaria peke
yake.Kitu cha kushangaza
karibu wote wamepigwa risasi
za kichwa.Inaonekana wauaji
walikuwa wanawalenga
vichwani bila wao kuwa na
taarifa ndiyo maana wameweza
kuua timu nzima”akasema
Kaiza
“Kaiza hili unaloniambia
limenipa mstuko
mkubwa.Haijawahi kutokea
toka idara hii ianzishwe
kupoteza watu wengi kiasi
hicho.Haraka sana mili yote ya
waliouawa iondolewe hapo na
kuletwa hapa kitalu 2
tuihifadhi.Vipi hapo maeneo ya
karibu hakuna taharuki
yoyote?Hakuna wananchi
wanaoishi maeneo ya karibu
ambao wamefika eneo la tukio
baada ya kusikia milio ya risasi?
“Eneo liko kimya kabisa
Devotha na inaonekana
majirani wa eneo hili
hawafahamu
kilichotokea.Ninahisi wauaji
walitumia bunduki zenye
viwambo vya kuzuia sauti na
kuua watu wetu kimya
kimya”akajibu Kaiza
“Sawa Kaiza hakikisha miili
hiyo inaondolewa haraka sana
eneo hilo” akasema Devotha na
kukata simu
“Haya ni majabu.Hadi
nitakapoiona miili ya watu wetu
ndipo nitakapoamini kama hii
ninachoambiwa na Kaiza ni kitu
cha kweli.P3 Unit ni kikosi
tegemezi kabisa katika idara
yetu na kina watu waliopata
mafunzo ya hali ya juu nje ya
nchi.Ni watu ambao tumekuwa
tunawatumia katika operesheni
mbalimbali na hawajawahi
kushindwa au kuuawa hata
mmoja wao.Imetokeaje leo
wakauawa wengi kiasi
hicho?.Huyu MathewMulumbi
ni kiumbe wa aina gani
anayeweza kuwaua watu wote
hao kirahisi namna
hii?akajiuliza Devotha
“Nilitegemea suala hili
lingekuwa dogo na kumalizika
bila matatizo lakini sasa tayari
limechukua sura mpya na
limekuwa kubwa.Ameingia
MathewMulumbi na kuharibu
mchezo wote.Ngoja nimjulishe
rais hiki kilichotokea” akawaza
Devotha na kumpigia simu Dr
Evans
“Devotha habari za usiku
huu.Mambo yanakwendaje
hapo.Kila kitu kimekwenda
vizuri?akauliza Dr Evans
“Mheshimiwa rais mambo
yanakwenda
vyema.Tumefanikiwa
kumuhamisha Olivia na kumleta
hapa kitalu 2 kama
ulivyoelekeza.Vile vile tayari
tumempata Agrey Themba na
hivi tuongeavyo yuko njiani
analetwa hapa kitalu 2”
akasema Devotha
“Very good.Vipi kuhusu
MathewMulumbi?Uliweka
kikosi cha kumsubiri pale kitalu
7?akauliza Dr Evans
“Mheshimia rais tumepata
mafanikio katika sehemu zote
lakini kuna tatizo kidogo katika
upande wa Mathew”
“Kuna tatizo gani
Devotha?Mmeshindwa kumpata
Mathew?Hajafika kitalu
7?akauliza Dr Evans
“Mheshimiwa rais hivi sasa
Kaiza na timu ndogo
nimewatuma waende kitalu 7
baada ya kupokea taarifa
kutoka kwa mmoja wa watu
wetu aliye ndani ya P3 unit
kwamba kumetokea wamavizi
na wameua watu wetu.Kaiza
amefika hapo na taarifa
aliyonipa ni mbaya sana.Watu
kumi na tatu wameuawa
isipokuwa mmoja tu” akasema
Devotha na kumstua Dr Evans
“Kikosi kizima kimeuawa?
Imewezekanaje wakauawa
wote?akauliza
“Amesalia mmoja tu
mheshimiwa rais”
“Kusalia mtu mmoja si
hoja.Ninachotaka kufahamu ni
namna hawa watu
walivyouawa.P3 Unit ni kikosi
maalum katika idara yetu
chenye mafunzo ya hali ya juu
na ndicho kikosi
tegemeo.Wamefanya
operesheni nyingi na hakuna
opereseni hata moa waliyowahi
kumpoteza mtu.Nini kimetokea
hadi wauawe wote?Una hakika
ulipeleka P3 unit kweli?
“Ndiyo mheshimiwa rais
kikosi kilichokwenda kulinda
pale kitalu 7 ni P3 unit”akajibu
Devotha
“MathewMulumbi
!!Mathew!!!..akasema Dr Evans
huku akisikika akigonga meza
kwa hasira
“Ni kiumbe wa aina gani
huyu?akauliza Dr Evans na
ukapita ukimya
“Devotha huyu mtu tayari
amevuka mpaka na kama
tusipokuwa waangalifu
atavuruga kila kitu.Hiki
alichokifanya leo ni tangazo la
vita hivyo tunapaswa kumsaka
kwa kila uwezo tulio nao na
kuhakikisha anapatikana.Bila
kumpata MathewMulumbi
tumekwisha.Nataka mpaka
kufikia kesho asubuhi nipate
mikakati yako namna ya
kumpata Mathew.Kama hauna
mikakati au uwezo wa kumpata
nieleze ukweli ili niweze
kutumia vyombo vingine
kumpata lakini nina imani na
idara yako kuwa hamuwezi
kushindwa kumpata Mathew.”
akasema Dr Evans
“Sawa mheshimiwa rais
tutafanya hivyo.”akasema
Devotha
“Devotha kwa sasa baada
ya kumpata Agrey Themba
hakikisha unamfungua
Olivia.Nina uhakika mkubwa
kwamba kwa kumumia baba
yake lazima atafunguka kila
kitu.Hakikisha kabla ya
mapambazuko uwe tayari
umefahamu kila kitu kuhusu
Olivia na IS” akasema Dr Evans
na kukata simu
 
SIRI
PART 1: SEASON 4
MTUNZI: PATRICK CK
Mathewalipunguza
mwendo wa gari alipoliona
bango kubwa limeandikwa
Zawama Saccos katika mtaa wa
Msanzi na mbele kidogo
akaliona jengo la ghorofa
ambalo halijamaliziwa.Mbele ya
jengo hilo kulikuwa na jengo
lingine la ghorofa lililokuwa na
maduka akasimamisha gari
karibu na uzio wa jengo lile
linaloendelea kujengwa
akashuka.Aliangaza pande zote
kuhakiki usalama
wake,kulikuwa na magari
machache yakipita
barabarani.Kuzunguka jengo
lile kulikuwa na uzio wa mabati
akaingia ndani ya uzio akaliona
gari moja likiwa limeegeshwa
akalisogelea na kuchungulia
ndani hakukuwa na mtu
akaingia ndani ya lile jengo
akaanza kuchunguza kama kuna
mtu yeyote mle ndani.Alilikagua
jengo lote lakini hakukuwa na
mtu yeyote,akashuka na
kwenda katika lile gari
akakinyonga kitasa mlango
ulikuwa umefungwa.Akatoa
simu na kumpigia Lucy Themba
mke wa Agrey
“Mathewumekwisha fika
mahala hapo?akauliza Lucy
“Ndiyo mama nimekwisha
fika”
“Umempata
Agrey?Amekwisha fika
hapo?akauliza kwa wasi wasi
“Mama nataka kufahamu
mzee aliondoka nyumbani na
gari ya aina gani?
“Aliondoka na gari lake aina
ya landcruiser V8 rangi nyeusi’
akasema Lucy na
Mathewakabaki kimya
“Mathew” akaita Lucy
“Sawa mama
ahsante.Nitakupigia simu muda
si mrefu lakini kwa sasa
naomba usimueleze mtu yeyote
suala hili” akasema Mathewna
kukata simu
“Tayari wamemchukua
Agrey.Hili suala linazidi kuwa
gumu.Naamini watu hawa
waliomchukua Olivia ndio hao
hao waliomteka baba yake.Ni
kikundi gani hiki? Nini hasa
malengo ya kuwateka Olivia na
baba yake?Ninaanza kupata
picha kwamba suala hili ni zaidi
ya fedha.Baada ya Olivia
kutekwa tuliamini kwamba
watekaji walifanya vile ili
kujipatia fedha kutoka kwa
familia yake lakini sasa baada
ya baba yake pia kutekwa
ninaanza kuhisi kwamba hili
suala ni kubwa zaidi ya
tunavyolichukulia.Ngoja niende
kwa Lucy nitapata majibu yote”
akawaza Mathewna kuingia
katika gari lake akaondoka
kuelekea nyumbani kwa Agrey
Themba
“Ninajaribu kuunganisha
matukio yote yanayohusiana na
kutekwa kwa Olivia lakini bado
sipati picha nzuri ila
ninachoweza kukipata mpaka
hapa nilipofika ni kwamba kuna
mtu au watu walio karibu na
familia ya akina Olivia ambao
wanahusika katika tukio hili.Ni
Lucy pekee anayeweza kusaidia
kupata ufumbuzi wa suala hili
kama atakuwa tayari kunieleza
ni nani waliyempa taarifa za
mimi kwenda kumuokoa
Olivia”akawaza Mathew
Kabla hajafika nyumbani
kwa bilionea Agrey Themba
akampigia simu Lucy
akamjulisha kwamba
amekaribia kufika nyumbani
kwake hivyo awataarifu walinzi
wake.Alipofika getini tayari
taarifa zake zilikuwa kwa
walinzi wakamfungulia geti
akaingia ndani na kumkuta
Lucy Themba akiwa
amesimama katika kibaraza
akimsubiri.Alihisi
kuchanganyikiwa baada ya
kumuona Mathewakishuka
garini peke yake
“Mathew,yuko wapi
agrey?akauliza Lucy
“Mama tunaweza
kuzungumza ndani tafadhali?
Mathewakaomba.Lucy
akamuongoza wakaingia ndani
“Mathewnaomba
usiniambie umemkosa Agrey”
akasema Lucy midomo ilikuwa
inamtetemeka
“Mama nimekosa
Agrey.Samahani sana
nilichelewa kufika mahala
walikopanga
wakutane.Nilichokikuta pale ni
gari la Agrey ulilosema
aliondoka nalo hapa
nyumbani”akasema Mathew
“Ouh Agrey…Agrey mume
wangu .........akalia Lucy
Mathewakamfuata
“Mama usipige kelele
tafadhali.Unatakiwa kuwa na
nguvu hasa katika kipindi hiki
kigumu” akasema Mathew.
“Mathewmambo gani haya
yanatutokea?Alianza Olivia na
sasa amefuata baba yake.Nani
hawa wanatuandama namna
hii?akasema Lucy akiendelea
kulia
“Mama kuna jambo nataka
kulifahamu kutoka kwako
ambalo litatupa mwangaza
kuhusiana na matukio haya
yanayoendelea ndani ya familia
yako.Nitakuomba unieleze
ukweli bila kunificha” akasema
Mathew
“Kitu gani unataka
kukifahamu Mathew?akauliza
Lucy
“Mama nimefika mahala
ambako ninaamini Olivia
alikuwa amefichwa,nimekuta
nyumba ikiwa tupu ila kuna kila
dalili kwamba Olivia alikuwepo
pale lakini alihamishwa .Nikiwa
bado natafakari kuhusu suala
lile la Olivia likajitokeza suala la
Agrey.Alipotekwa Olivia
tulidhani kwamba watekaji
wana lengo la kujipatia fedha
lakini baada ya kutekwa baba
yake pia nimetafakari na kuona
suala hili ni zaidi ya
fedha.Lengo la watekaji si
kujipatia fedha kuna jambo
lingine kubwa zaidi ya
fedha.Kikubwa zaidi
nilichokipata katika matukio
haya mawili ni kwamba kuna
watu au mtu ambaye yuko
karibu yenu sana anashirikiana
na watekaji.Ukiacha wewe na
Agrey sikuwa nimemueleza mtu
mwingine kama ninafahamu
alipo Olivia na ninakwenda
kumuokoa.NInajiuliza kama
sikumweleza mtu mwingine juu
ya jambo hili mtu aliyempigia
simu Agrey na kujifanya ni
mimi alipata wapi taarifa
zangu?Jibu ninalolipata ni
kwamba mtu huyo alipata
taarifa hizo za mimi kwenda
kumuokoa Olivia kutoka hapa
kwenu.Endapo nikimfahamu
huyo mtu tutakuwa tumepata
mwanga mkubwa sana na
itatusaidia katika kumpata
Olivia na baba yake.Mama
nimekuja hapa kuomba
unieleze ukweli nani ambaye
mlimueleza kuhusu mimi
kufahamu mahala alipo Olivia?
akauliza Mathew.Lucy Themba
akafuta machozi na kusema
“Hakuna mtu yeyote
tuliyemueleza kuhusu suala la
wewe kufahamu mahala alipo
Olivia.Tunaofahamu ni mimi na
Agrey hakuna mtu mwingine
anayejua” akasema Lucy
Themba
“Mama hili ninalokuomba
unieleze ni la muhimu sana na
ninakuhakikishia kwamba
kama tukimfahamu mtu huyo
tutakuwa tumempata Olivia na
baba yake.Ninaomba mama
usinifiche kitu hata kama
umemueleza mwanao au mtu
wako wa karibu niambie
usihofu.Nina uhakika mkubwa
kwamba kuna mtu ambaye
yuko karibu yenu anashirikiana
na watekaji na ndiyo maana
Olivia alihamishwa haraka
mahala alipokuwa amefichwa
baada ya kupata taarifa
kwamba ninakwenda
kumuokoa.Kama mtu huyo
asingekuwa na taarifa hizo hivi
sasa ningerejea na Olivia lakini
nimemkosa baada ya
kuhamishwa na taarifa za mimi
kwenda kumfuata Olivia
naamini wamezipata toka
hapa.Mama kama kweli unataka
tumpate Olivia na baba yake
naomba uniambie nani ulimpa
taarifa za kwamba ninakwenda
kumfuata Olivia Kigamboni?
“Mathewhakuna mtu
yeyote
tuliyemueleza.Ninakuhakikishia
baba hakuna mtu yeyote
ambaye tumemueleza.Kama
kungekuwa na mtu yeyote
ningekwisha kueleza”
“Mama fikiria tena tafadhali
ni muhmu sana.Kumbuka hata
kama kulikuwa na mtu yeyote
karibu yenu wakati
mnazungumza wewe na Agrey”
“Hakuna
Mathew.Ulipoondoka tulikuwa
na wageni wetu
uliowaacha,wakaja tena
wengine na walipoondoka mimi
na Agrey tukaenda chumbani
kwetu na hatukuzungumza
kuhusu suala lako” akasema
Lucy
“Mama nisikilize
vizuri.Wewe na familia yako
tayari mko katika hatari na mtu
ambaye anayaweka maisha
yenu hatari yuko karibu yenu
na kama tukiweza kumfahamu
basi tutaweza kuwapata Olivia
na Agrey.Kwa sasa wakati
tukiendelea kumtafuta mtu
huyo ni nani nitakuondoa hapa
na kukupeleka sehemu salama
ambako utakaa hadi hapo suala
hili litakapopatiwa ufumbuzi”
“Hapana Mathewsiendi
kokote.Kama kuna mtu ambaye
anaiandama familia yetu basi
aje aniulie hapa hapa nyumbani
kwangu,siendi kokote” akasema
Lucy
“Mama uko katika hatari
kubwa.Ninataka kukusaidia
uwe salama wakati tunaendelea
kuwatafuta Olivia na baba yake”
“Mathewnimekwambia
siendi kokote.Kama yupo huyo
ambaye anaiandama familia
yetu anifuate hapa hapa
sintamuogopa”
“Mama ninataka nikupeleke
sehemu sal…………”
“Mathewstop! Nimesema
siendi sehemu yoyote.Tafadhali
kama una hakika yupo mtu
ambaye anaiandama familia
yetu basi mtafute na hakikisha
unampata lakini mimi
nitaendelea kukaa hapa hapa
kwangu nikiwasubiri mume
wangu na mwanangu kama
watapatikana” akasema Lucy
“Olivia na Agrey
watapatikana mama lakini
nitahitaji sana ushirikiano wako
ndiyo maana ninataka uniambie
kama kuna mtu ambaye
umemueleza kuhusu mimi.Ni
huyo pekee atakayelifumbua
fumbo hili”akasema Mathew
“Mathewnimekwambia
hakuna mtu yeyote
tuliyemwambia kuhusu wewe”
“Sawa mama
nimekuelewa.Nitatafuta namna
nyingine ya kufanya kuweza
kumfahamu mtu huyo na kwa
kuwa umekataa wazo langu la
kukuondoa hapa kukupeleka
sehemu salama ninakushauri
uimarishe ulinzi hapa nyumbani
kwako usipokee simu ya mtu
usiyemfahamu na usimueleze
mtu yeyote jambo lolote
kuhusiana na mimi.Ukipigiwa
simu hata na simu ya mumeo au
ya mwanao kwamba uende
sehemu Fulani tafadhali
usifanye hivyo nijulishe
kwanza.Nitakupa namba ya
simu ya siri ambayo mimi na
wewe tutakuwa
tunawasiliana”akasema
Mathew
“Mathewtafadhali watafute
Agrey na Olivia.Nitakufa kama
hawatapatikana” akasema Lucy
“Usihofu mama ninakuahidi
kuwatafuta Agrey na Olivia na
ninakuhakikishia kwamba
lazima watapatikana lakini
ninaomba sana ushiriiano wako
mkubwa hasa katika kumtafuta
mtu huyu ambaye yuko karibu
yenu ambaye ndiye anayeratibu
matukio haya ya utekaji ndani
ya familia yako” akasema
Mathewna kumpa Lucy
maelekezo kadhaa halafu
akaondoka kurejea nyumbani
kwake
Baada ya Mathewkuondoka
Lucy akachukua simu na
kumpigia Dr Evans
“Lucy habari za usiku
huu?akauliza Dr Evans
“Habari si nzuri Dr Evans”
“Nafahamu Lucy,hata mimi
mpaka sasa sijalala ninaendelea
kuwasiliana na viongozi wa
jeshi la polisi kila mara kupata
ripoti za maendeleo ya
uchunguzi.Usiwe na hofu
yoyote ninakuhakikishia
kwamba Olivia atapatikana”
akasema Dr Evans
“Dr Evans tatizo limezidi
kuwa kubwa.Agrey naye
ametekwa usiku huu”
“Agrey ametekwa?akauliza
Dr Evans kwa mshangao kana
kwamba hajui chochote
kilichotokea
“Ndiyo ametekwa usiku
huu”
“Oh my God ! Ametekwa
vipi?Wamekuja hapo nyumbani
watekaji wakamchukua?Hebu
nieleze mazingira ya kutekwa
kwake Lucy” akasema Dr Evans
“Mapema leo jioni alikuja
kijana mmoja akajitambulisha
kwetu kwamba anaitwa
MathewMulumbi akadai
kwamba yeye ni mpelelzi na
anafahamu mahala alipo Olivia
akatuomba tumpe ruhusa ya
kwenda kumuokoa Olivia,Agrey
alisita lakini mimi nikamuamini
na kumtaka akafanye uchunguzi
wake na amlete Olivia
nyumbani.Saa kadhaa baada ya
Mathewkuondoka,Agrey
alipigiwa simu na mtu mmoja
aliyejitambulisha kuwa ni
MathewMulumbi na
akamueleza Agrey kwamba
amefanikiwa kumpata Olivia
lakini amejeruhiwa na anahitaji
msaada hivyo akamtaka Agrey
amfuate akamuelekeza sehemu
ya kumkuta.Sote tuliamini
kwamba ni MathewMulumbi
lakini baadae baada ya Agrey
kuondoka nikapigiwa simu na
MathewMulumbi akaniambia
kwamba amemkosa Olivia
ndipo hapo
nilipostuka.Mathewalikana
kupiga simu yoyote
nikamuelekeza aende mahala
yule jamaa alikopanga akutane
na Agrey akalikuta gari la Agrey
lakini yeye mwenyewe
hakuwepo na simu yake
haipatikani tena.Tayari mume
wangu ametekwa” akasema
Lucy na kuanza kudondosha
machozi
“Lucy nyamaza
kulia.Umefanya vyema kunipa
taarifa hizi.Kwa maelezo
uliyonipa ni wazi huyo
MathewMulumbi anaonekana
anahusika katika tukio hilo la
kutekwa kwa Agrey.Huyo ndiye
atakayekuwa mshukiwa wetu
wa kwanza na anatakiwa
afanyiwe uchunguzi mkubwa
kujua uhusika wake katika
sakata hili na nitaomba
ushirikiano wako mkubwa Lucy
ili tuweze kumpata.Kesho
nitatuma timu ya wapelelezi
hapo kwako na utampigia simu
Mathewutamuomba muonane
nyumbani kwako na akishafika
atakamatwa atahojiwa na
ataonyesha watu
anaoshirikiana nao.Lucy
nakuhakikishia kwamba
tukimpata huyu jamaa
tutakuwa tumewapata Olivia na
baba yake.Huyo jamaa
anafahamu kila kitu
kinachoendelea” akasema Dr
Evans
“Hata mimi ninahisi huyu
Mathewsi mtu mzuri.Agrey
alinionya kuhusu kumuamini
lakini sikutaka kumsikia
niliamini tumepata mkombozi
wa kutusaidia kumpata
mwanetu.Yote haya ni makosa
yangu. Ahsante sana Dr Evans
kwa kunifumbua macho kuhusu
huyu jamaa.Hata usiku huu
amekuja hapa na akanitaka eti
anipeleke sehemu salama
nilikataa kata kata kwamba
siwezi kutoka nyumbani
kwangu.Sikujua kumbe alikuwa
na malengo yake shetani yule”
akasema Lucy Themba kwa
hasira
“Ulifanya vyema Lucy
kumkatalia kwani kama
ungekubali hata wewe nadhani
ungeungana na akina Agrey”
akasema Dr Evans
“Lakini huyu jamaa anataka
nini kwetu?
“Mathewni mpelelezi kama
alivyojitambulisha kwenu na
ninaamini kuna watu ambao
wanamtumia kufanya haya
aliyoyafanya.Tukimpata
atahojiwa na atawataja wale
ambao wamemtuma afanye
matukio haya mabaya.Lucy
narudia tena kukuhakikishia
tutawapata Olivia na Agrey”
“Nashukuru sana Agrey
tafadhali naomba ufanye kila
uwezalo kuwapata Olivia na
Agrey.Nitakufa kama
wasipopatikana” akasema Lucy
“Niamini mimi Lucy,watu
hawa watapatikana” akasema
DrEvans na kuagana na Lucy
Themba
 
SIRI
PART 1: SEASON 4
MTUNZI: PATRICK CK
Mathewalipunguza
mwendo wa gari alipoliona
bango kubwa limeandikwa
Zawama Saccos katika mtaa wa
Msanzi na mbele kidogo
akaliona jengo la ghorofa
ambalo halijamaliziwa.Mbele ya
jengo hilo kulikuwa na jengo
lingine la ghorofa lililokuwa na
maduka akasimamisha gari
karibu na uzio wa jengo lile
linaloendelea kujengwa
akashuka.Aliangaza pande zote
kuhakiki usalama
wake,kulikuwa na magari
machache yakipita
barabarani.Kuzunguka jengo
lile kulikuwa na uzio wa mabati
akaingia ndani ya uzio akaliona
gari moja likiwa limeegeshwa
akalisogelea na kuchungulia
ndani hakukuwa na mtu
akaingia ndani ya lile jengo
akaanza kuchunguza kama kuna
mtu yeyote mle ndani.Alilikagua
jengo lote lakini hakukuwa na
mtu yeyote,akashuka na
kwenda katika lile gari
akakinyonga kitasa mlango
ulikuwa umefungwa.Akatoa
simu na kumpigia Lucy Themba
mke wa Agrey
“Mathewumekwisha fika
mahala hapo?akauliza Lucy
“Ndiyo mama nimekwisha
fika”
“Umempata
Agrey?Amekwisha fika
hapo?akauliza kwa wasi wasi
“Mama nataka kufahamu
mzee aliondoka nyumbani na
gari ya aina gani?
“Aliondoka na gari lake aina
ya landcruiser V8 rangi nyeusi’
akasema Lucy na
Mathewakabaki kimya
“Mathew” akaita Lucy
“Sawa mama
ahsante.Nitakupigia simu muda
si mrefu lakini kwa sasa
naomba usimueleze mtu yeyote
suala hili” akasema Mathewna
kukata simu
“Tayari wamemchukua
Agrey.Hili suala linazidi kuwa
gumu.Naamini watu hawa
waliomchukua Olivia ndio hao
hao waliomteka baba yake.Ni
kikundi gani hiki? Nini hasa
malengo ya kuwateka Olivia na
baba yake?Ninaanza kupata
picha kwamba suala hili ni zaidi
ya fedha.Baada ya Olivia
kutekwa tuliamini kwamba
watekaji walifanya vile ili
kujipatia fedha kutoka kwa
familia yake lakini sasa baada
ya baba yake pia kutekwa
ninaanza kuhisi kwamba hili
suala ni kubwa zaidi ya
tunavyolichukulia.Ngoja niende
kwa Lucy nitapata majibu yote”
akawaza Mathewna kuingia
katika gari lake akaondoka
kuelekea nyumbani kwa Agrey
Themba
“Ninajaribu kuunganisha
matukio yote yanayohusiana na
kutekwa kwa Olivia lakini bado
sipati picha nzuri ila
ninachoweza kukipata mpaka
hapa nilipofika ni kwamba kuna
mtu au watu walio karibu na
familia ya akina Olivia ambao
wanahusika katika tukio hili.Ni
Lucy pekee anayeweza kusaidia
kupata ufumbuzi wa suala hili
kama atakuwa tayari kunieleza
ni nani waliyempa taarifa za
mimi kwenda kumuokoa
Olivia”akawaza Mathew
Kabla hajafika nyumbani
kwa bilionea Agrey Themba
akampigia simu Lucy
akamjulisha kwamba
amekaribia kufika nyumbani
kwake hivyo awataarifu walinzi
wake.Alipofika getini tayari
taarifa zake zilikuwa kwa
walinzi wakamfungulia geti
akaingia ndani na kumkuta
Lucy Themba akiwa
amesimama katika kibaraza
akimsubiri.Alihisi
kuchanganyikiwa baada ya
kumuona Mathewakishuka
garini peke yake
“Mathew,yuko wapi
agrey?akauliza Lucy
“Mama tunaweza
kuzungumza ndani tafadhali?
Mathewakaomba.Lucy
akamuongoza wakaingia ndani
“Mathewnaomba
usiniambie umemkosa Agrey”
akasema Lucy midomo ilikuwa
inamtetemeka
“Mama nimekosa
Agrey.Samahani sana
nilichelewa kufika mahala
walikopanga
wakutane.Nilichokikuta pale ni
gari la Agrey ulilosema
aliondoka nalo hapa
nyumbani”akasema Mathew
“Ouh Agrey…Agrey mume
wangu .........akalia Lucy
Mathewakamfuata
“Mama usipige kelele
tafadhali.Unatakiwa kuwa na
nguvu hasa katika kipindi hiki
kigumu” akasema Mathew.
“Mathewmambo gani haya
yanatutokea?Alianza Olivia na
sasa amefuata baba yake.Nani
hawa wanatuandama namna
hii?akasema Lucy akiendelea
kulia
“Mama kuna jambo nataka
kulifahamu kutoka kwako
ambalo litatupa mwangaza
kuhusiana na matukio haya
yanayoendelea ndani ya familia
yako.Nitakuomba unieleze
ukweli bila kunificha” akasema
Mathew
“Kitu gani unataka
kukifahamu Mathew?akauliza
Lucy
“Mama nimefika mahala
ambako ninaamini Olivia
alikuwa amefichwa,nimekuta
nyumba ikiwa tupu ila kuna kila
dalili kwamba Olivia alikuwepo
pale lakini alihamishwa .Nikiwa
bado natafakari kuhusu suala
lile la Olivia likajitokeza suala la
Agrey.Alipotekwa Olivia
tulidhani kwamba watekaji
wana lengo la kujipatia fedha
lakini baada ya kutekwa baba
yake pia nimetafakari na kuona
suala hili ni zaidi ya
fedha.Lengo la watekaji si
kujipatia fedha kuna jambo
lingine kubwa zaidi ya
fedha.Kikubwa zaidi
nilichokipata katika matukio
haya mawili ni kwamba kuna
watu au mtu ambaye yuko
karibu yenu sana anashirikiana
na watekaji.Ukiacha wewe na
Agrey sikuwa nimemueleza mtu
mwingine kama ninafahamu
alipo Olivia na ninakwenda
kumuokoa.NInajiuliza kama
sikumweleza mtu mwingine juu
ya jambo hili mtu aliyempigia
simu Agrey na kujifanya ni
mimi alipata wapi taarifa
zangu?Jibu ninalolipata ni
kwamba mtu huyo alipata
taarifa hizo za mimi kwenda
kumuokoa Olivia kutoka hapa
kwenu.Endapo nikimfahamu
huyo mtu tutakuwa tumepata
mwanga mkubwa sana na
itatusaidia katika kumpata
Olivia na baba yake.Mama
nimekuja hapa kuomba
unieleze ukweli nani ambaye
mlimueleza kuhusu mimi
kufahamu mahala alipo Olivia?
akauliza Mathew.Lucy Themba
akafuta machozi na kusema
“Hakuna mtu yeyote
tuliyemueleza kuhusu suala la
wewe kufahamu mahala alipo
Olivia.Tunaofahamu ni mimi na
Agrey hakuna mtu mwingine
anayejua” akasema Lucy
Themba
“Mama hili ninalokuomba
unieleze ni la muhimu sana na
ninakuhakikishia kwamba
kama tukimfahamu mtu huyo
tutakuwa tumempata Olivia na
baba yake.Ninaomba mama
usinifiche kitu hata kama
umemueleza mwanao au mtu
wako wa karibu niambie
usihofu.Nina uhakika mkubwa
kwamba kuna mtu ambaye
yuko karibu yenu anashirikiana
na watekaji na ndiyo maana
Olivia alihamishwa haraka
mahala alipokuwa amefichwa
baada ya kupata taarifa
kwamba ninakwenda
kumuokoa.Kama mtu huyo
asingekuwa na taarifa hizo hivi
sasa ningerejea na Olivia lakini
nimemkosa baada ya
kuhamishwa na taarifa za mimi
kwenda kumfuata Olivia
naamini wamezipata toka
hapa.Mama kama kweli unataka
tumpate Olivia na baba yake
naomba uniambie nani ulimpa
taarifa za kwamba ninakwenda
kumfuata Olivia Kigamboni?
“Mathewhakuna mtu
yeyote
tuliyemueleza.Ninakuhakikishia
baba hakuna mtu yeyote
ambaye tumemueleza.Kama
kungekuwa na mtu yeyote
ningekwisha kueleza”
“Mama fikiria tena tafadhali
ni muhmu sana.Kumbuka hata
kama kulikuwa na mtu yeyote
karibu yenu wakati
mnazungumza wewe na Agrey”
“Hakuna
Mathew.Ulipoondoka tulikuwa
na wageni wetu
uliowaacha,wakaja tena
wengine na walipoondoka mimi
na Agrey tukaenda chumbani
kwetu na hatukuzungumza
kuhusu suala lako” akasema
Lucy
“Mama nisikilize
vizuri.Wewe na familia yako
tayari mko katika hatari na mtu
ambaye anayaweka maisha
yenu hatari yuko karibu yenu
na kama tukiweza kumfahamu
basi tutaweza kuwapata Olivia
na Agrey.Kwa sasa wakati
tukiendelea kumtafuta mtu
huyo ni nani nitakuondoa hapa
na kukupeleka sehemu salama
ambako utakaa hadi hapo suala
hili litakapopatiwa ufumbuzi”
“Hapana Mathewsiendi
kokote.Kama kuna mtu ambaye
anaiandama familia yetu basi
aje aniulie hapa hapa nyumbani
kwangu,siendi kokote” akasema
Lucy
“Mama uko katika hatari
kubwa.Ninataka kukusaidia
uwe salama wakati tunaendelea
kuwatafuta Olivia na baba yake”
“Mathewnimekwambia
siendi kokote.Kama yupo huyo
ambaye anaiandama familia
yetu anifuate hapa hapa
sintamuogopa”
“Mama ninataka nikupeleke
sehemu sal…………”
“Mathewstop! Nimesema
siendi sehemu yoyote.Tafadhali
kama una hakika yupo mtu
ambaye anaiandama familia
yetu basi mtafute na hakikisha
unampata lakini mimi
nitaendelea kukaa hapa hapa
kwangu nikiwasubiri mume
wangu na mwanangu kama
watapatikana” akasema Lucy
“Olivia na Agrey
watapatikana mama lakini
nitahitaji sana ushirikiano wako
ndiyo maana ninataka uniambie
kama kuna mtu ambaye
umemueleza kuhusu mimi.Ni
huyo pekee atakayelifumbua
fumbo hili”akasema Mathew
“Mathewnimekwambia
hakuna mtu yeyote
tuliyemwambia kuhusu wewe”
“Sawa mama
nimekuelewa.Nitatafuta namna
nyingine ya kufanya kuweza
kumfahamu mtu huyo na kwa
kuwa umekataa wazo langu la
kukuondoa hapa kukupeleka
sehemu salama ninakushauri
uimarishe ulinzi hapa nyumbani
kwako usipokee simu ya mtu
usiyemfahamu na usimueleze
mtu yeyote jambo lolote
kuhusiana na mimi.Ukipigiwa
simu hata na simu ya mumeo au
ya mwanao kwamba uende
sehemu Fulani tafadhali
usifanye hivyo nijulishe
kwanza.Nitakupa namba ya
simu ya siri ambayo mimi na
wewe tutakuwa
tunawasiliana”akasema
Mathew
“Mathewtafadhali watafute
Agrey na Olivia.Nitakufa kama
hawatapatikana” akasema Lucy
“Usihofu mama ninakuahidi
kuwatafuta Agrey na Olivia na
ninakuhakikishia kwamba
lazima watapatikana lakini
ninaomba sana ushiriiano wako
mkubwa hasa katika kumtafuta
mtu huyu ambaye yuko karibu
yenu ambaye ndiye anayeratibu
matukio haya ya utekaji ndani
ya familia yako” akasema
Mathewna kumpa Lucy
maelekezo kadhaa halafu
akaondoka kurejea nyumbani
kwake
Baada ya Mathewkuondoka
Lucy akachukua simu na
kumpigia Dr Evans
“Lucy habari za usiku
huu?akauliza Dr Evans
“Habari si nzuri Dr Evans”
“Nafahamu Lucy,hata mimi
mpaka sasa sijalala ninaendelea
kuwasiliana na viongozi wa
jeshi la polisi kila mara kupata
ripoti za maendeleo ya
uchunguzi.Usiwe na hofu
yoyote ninakuhakikishia
kwamba Olivia atapatikana”
akasema Dr Evans
“Dr Evans tatizo limezidi
kuwa kubwa.Agrey naye
ametekwa usiku huu”
“Agrey ametekwa?akauliza
Dr Evans kwa mshangao kana
kwamba hajui chochote
kilichotokea
“Ndiyo ametekwa usiku
huu”
“Oh my God ! Ametekwa
vipi?Wamekuja hapo nyumbani
watekaji wakamchukua?Hebu
nieleze mazingira ya kutekwa
kwake Lucy” akasema Dr Evans
“Mapema leo jioni alikuja
kijana mmoja akajitambulisha
kwetu kwamba anaitwa
MathewMulumbi akadai
kwamba yeye ni mpelelzi na
anafahamu mahala alipo Olivia
akatuomba tumpe ruhusa ya
kwenda kumuokoa Olivia,Agrey
alisita lakini mimi nikamuamini
na kumtaka akafanye uchunguzi
wake na amlete Olivia
nyumbani.Saa kadhaa baada ya
Mathewkuondoka,Agrey
alipigiwa simu na mtu mmoja
aliyejitambulisha kuwa ni
MathewMulumbi na
akamueleza Agrey kwamba
amefanikiwa kumpata Olivia
lakini amejeruhiwa na anahitaji
msaada hivyo akamtaka Agrey
amfuate akamuelekeza sehemu
ya kumkuta.Sote tuliamini
kwamba ni MathewMulumbi
lakini baadae baada ya Agrey
kuondoka nikapigiwa simu na
MathewMulumbi akaniambia
kwamba amemkosa Olivia
ndipo hapo
nilipostuka.Mathewalikana
kupiga simu yoyote
nikamuelekeza aende mahala
yule jamaa alikopanga akutane
na Agrey akalikuta gari la Agrey
lakini yeye mwenyewe
hakuwepo na simu yake
haipatikani tena.Tayari mume
wangu ametekwa” akasema
Lucy na kuanza kudondosha
machozi
“Lucy nyamaza
kulia.Umefanya vyema kunipa
taarifa hizi.Kwa maelezo
uliyonipa ni wazi huyo
MathewMulumbi anaonekana
anahusika katika tukio hilo la
kutekwa kwa Agrey.Huyo ndiye
atakayekuwa mshukiwa wetu
wa kwanza na anatakiwa
afanyiwe uchunguzi mkubwa
kujua uhusika wake katika
sakata hili na nitaomba
ushirikiano wako mkubwa Lucy
ili tuweze kumpata.Kesho
nitatuma timu ya wapelelezi
hapo kwako na utampigia simu
Mathewutamuomba muonane
nyumbani kwako na akishafika
atakamatwa atahojiwa na
ataonyesha watu
anaoshirikiana nao.Lucy
nakuhakikishia kwamba
tukimpata huyu jamaa
tutakuwa tumewapata Olivia na
baba yake.Huyo jamaa
anafahamu kila kitu
kinachoendelea” akasema Dr
Evans
“Hata mimi ninahisi huyu
Mathewsi mtu mzuri.Agrey
alinionya kuhusu kumuamini
lakini sikutaka kumsikia
niliamini tumepata mkombozi
wa kutusaidia kumpata
mwanetu.Yote haya ni makosa
yangu. Ahsante sana Dr Evans
kwa kunifumbua macho kuhusu
huyu jamaa.Hata usiku huu
amekuja hapa na akanitaka eti
anipeleke sehemu salama
nilikataa kata kata kwamba
siwezi kutoka nyumbani
kwangu.Sikujua kumbe alikuwa
na malengo yake shetani yule”
akasema Lucy Themba kwa
hasira
“Ulifanya vyema Lucy
kumkatalia kwani kama
ungekubali hata wewe nadhani
ungeungana na akina Agrey”
akasema Dr Evans
“Lakini huyu jamaa anataka
nini kwetu?
“Mathewni mpelelezi kama
alivyojitambulisha kwenu na
ninaamini kuna watu ambao
wanamtumia kufanya haya
aliyoyafanya.Tukimpata
atahojiwa na atawataja wale
ambao wamemtuma afanye
matukio haya mabaya.Lucy
narudia tena kukuhakikishia
tutawapata Olivia na Agrey”
“Nashukuru sana Agrey
tafadhali naomba ufanye kila
uwezalo kuwapata Olivia na
Agrey.Nitakufa kama
wasipopatikana” akasema Lucy
“Niamini mimi Lucy,watu
hawa watapatikana” akasema
DrEvans na kuagana na Lucy
Themba
 
SIRI
PART 1: SEASON 4
MTUNZI: PATRICK CK
“Lucy amekana kabisa
kumueleza mtu yeyote kuhusu
mimi na mpango wa kwenda
kumuokoa Olivia mahala
alikofichwa.Japo anakakataa
hawajamueleza mtu lakini
naamini kabisa kwamba taarifa
ile imevuja kutokea kwao na
ndiyo maana watekaji
wakawahi kumuhamisha Olivia
toka sehemu walikkokuwa
wamemficha.Kwa nini hataki
kuwa muwazi ili niweze
kuwasaidia yeye na familia
yake? Hata hivyo bado sijakata
tamaa nitaendelea kumsaka
mtu huyo hadi nimfahamu
kwani ndiye anayefahamu
walipo Olivia na baba yake
Agrey.Ngoja nikatulize akili
nilitafakari jambo hili nijue
namna ya kufanya” akawaza
Mathew.
Saa nane za usiku akafika
nyumbani kwake akafungua
mlango wa gari Bravo akashuka
“Thank you
Bravo.Umefanya kazi nzuri sana
leo” akasema Mathewna
kumrejesha Bravo katika
nyumba yake,akaingiza ndani
silaha zake
“Wale jamaa walikuwa na
bunduki kali nimezitazama
zilikuwa ni M4 Cabin.Ni
kampuni ya ulinzi au ni kikundi
cha watu wamekodishwa
kuifanya ile kazi?Kama ni
kampuni ya ulinzi wanawezaje
kuwa na silaha za namna
ile?Serikali
wanafah…….Mathewakatolewa
mawazoni baada ya simu yake
kuita alikuwa ni Ruby
“Hallo Ruby” akasema
Mathew
“Mathewunaendeleaje?Nim
ekuwa na wasiwasi sana
nilikutafuta lakini simu yako
haikuwa ikipatikana.Uko wapi
mida hii?
“Nimerejea nyumbani
kwangu muda mfupi uliopita”
“Umefanikiwa kumpata
Olivia?akauliza Ruby
“Hapana sikufanikiwa
kumpata”akajibu Mathewna
kumueleza Ruby kila kitu
kilichotokea katika ile nyumba
alimokuwa amefichwa Olivia.
“Dah! Akasema Ruby
“Kitu nilichokigundua
kufuatia kilichotokea usiku
huu,kuna mtu wa karibu sana
na familia ya akina Olivia
ambaye anashirikiana na
watekaji na huyo ndiye
aliyewapa watekaji taarifa
kwamba ninakwenda
kumuokoa Olivia wakamuondoa
haraka sana kabla sijawasili.Ili
kuwapata Olivia na baba yake
lazima kumfahamu mtu huyo
ambaye yuko karibu na familia
yao na anafahamu kila
kinachoendelea.Hapo ndipo
nilipofikia kwa usiku huu Ruby”
akasema Mathew
“Pole sana
Mathewjapokuwa haujampata
Olivia lakini ulichokigundua
kuhusu uwepo wa mtu mwenye
ukaribu na familia ya Olivia ni
kitu
kikubwa.Mathewnimekupigia
kukujulisha kuhusu jambo moja
muhimu
nililoligundua.Uliponipigia simu
na kunipa taarifa za tukio hili
nilirejea nyumbani mara moja
kuangalia ujumbe uliotumwa
katika kompyuta yangu.Kama
nilivyotegemea kirusi chetu
kimefanikiwa kuiba mafaili
mengi na kuyatuma katika
kompyuta yangu.Toka nimerudi
nimekuwa nikiyapitia mafaili
hayo na sijafanikiwa
kuyamaliza ni mengi
sana.Mathewsuala hili ni kubwa
zaidi ya tunavyofikiri” akasema
Ruby
“Kwa nini unasema hivyo
Ruby? Umegundua nini?
akauliza Mathew.
“Mafaili yaliyotumwa
kwangu yanaonyesha kwamba
yanatoka katika idara ya siri ya
usalama wa ndani wa taifa”
akasema Ruby
“Ruby subiri kidogo
unasema kuna kitu kinaitwa
idara ya siri ya usalama wa
ndani wa taifa?Sijawahi kusikia
kitu kama hicho”
“Hata mimi ni mara yangu
ya kwanza kufahamu kwamba
kuna idara ya siri ya usalama
wa ndani wan chi.Inaonekana
haina muda mrefu toka
kuanzishwa kwake na
inaendeshwa kwa siri bila
kujulikana”akasema Ruby
“Je Olivia ametekwa na
idara hii ya
serikali?Mathewakauliza
“Nashawishika kuamini
hivyo kwa sababu namba zile
ulizompa Olivia zimepigwa
kutoka idara hiyo ya serikali
hivyo ni wazi wao ndio
waliomteka Olivia.Hata kama si
wao basi kuna kitu
wanakifahamu kuhusu Olivia”
akasema Ruby.Ukapita ukimya
mfupi
“Awali nilidhani watekaji
walikuwa na shida na fedha
lakini baada ya tukio la kutekwa
Agrey Themba nilianza kuhisi
suala hili ni zaidi ya kutaka
fedha.Nilikuwa najiuliza
maswali kuhusiana na silaha
walizokuwa nazo wale watu
niliowaua kule Kigamboni usiku
huu sasa nimepata jibu kwa nini
walikuwa na bunduki nzito
kama zile.” akasema Mathew
“Mathewswali linaloibuka
hapa,nini sababu ya serikali
kuwateka Olivia na baba
yake?akauliza Ruby
“Hilo ni swali zuri kwa
kuanzia
uchunguzi.Ninavyofahamu
mimi serikali wanaweza
wakateka mtu kama ni hatari
pale anapoonekana ni hatari
kwa usalama wa nchi”
“Unadhani familia ya Olivia
ni hatari kwa usalama wa
nchi?akauliza Ruby
“Nimekuwa na ukaribu na
Olivia kwa miezi kadhaa
sasa,mambo yake mengi
ninayafahamu chumba chake
ninaingia kama
kwangu,sijawahi kuhisi hata
mara Olivia anaweza kuwa
hatari kwa usalama wa
nchi.Hata kwa kumuangalia
machoni Olivia hawezi kuwa
hatari kwa usalama wan
chi.Hata hivyo bado swali
linabaki pale pale kwa nini
idara hii nyeti ya serikali
wamteke Olivia?Naamini ipo
sababu kubwa”akasema
Mathew
“Mathewhili suala ni
kubwa.Tunapaswa kulichimba
kwa undani sana hadi tupate
sababu ya Olivia na baba yake
kutekwa na idara ya serikali
ambayo inahusika na usalama
wa ndani ya nchi.Ninakuja Dar
es salaam”
“Unasema
Ruby?Mathewakauliza
“Ninakuja Dar es
salaam.Siwezi kukuacha
ukaifanya kazi hii peke
yako.You need help and I’m the
one to help you so I’m coming
to Dar es salaam”
“Ruby ahsante sana kwa
kujitolea kuja Dar es salaam
lakini sidhani kama kuna
ulazima wa kuja huku.Sitaki
uingie katika hatari
Ruby.Unaweza ukanisaidia hata
ukiwa huko London”
“Hapana Mathewlazima nije
Dar es salaam.Wewe ni rafiki
yangu na siogopi kuingia katika
hatari kwa kukusaidia.Hili suala
ni kubwa Mathewhivyo kubali
au kataa unanihitaji
sana.Unamuhitaji vile vile papii
Gosu Gosu kwa ajili ya
kusaidiana naye.Mathewwatu
waliomteka Olivia ni taasisi ya
serikali na tayari
wameshakufahamu na hivi
tuzungumzavyo watakuwa
wanakutafuatilia sana hivyo
unahitaji mtu kama Gosu Gosu
kwa ajili ya kusaidiana
naye.Tayari nimepata tiketi
katika ndege ya shirika la ndege
la Misri itakayoondoka kesho
saa mbili za asubuhi hapa
London kupitia Cairo na saa
moja za jioni nitakuwa Dar es
salaam jiandae kunipokea”
akasema Ruby
“Ahsante sana Ruby sijui
nikushukuruje kwa kuamua
kuja kunisaidia.Ni wazi
ninakuhitaji sana katika suala
hili.Nitawasiliana pia na Gosu
gosu ambaye kwa sasa yuko
Dubai.Atakuja na kwa pamoja
tutatengeneza timu nzuri ya
kulishughulikia suala hili”
akasema Mathew
“Mathewnakuhakikishia
kwamba tutalimaliza suala
hili.Nina imani kubwa sana na
wewe na hatujawahi kushindwa
chochote tukiwa pamoja.Najua
Olivia ana umuhimu mkubwa
kwako hivyo binafsi nitajitolea
kila niwezalo kuhakikisha
anapatikana akiwa hai yeye na
baba yake”
“Nakushukuru sana
Ruby.Tafadhali naomba
unitumie orodha ya vitu vyote
unavyovihitaji ili kesho asubuhi
nianze maandalizi” akasema
Mathewna kuandika orodha ya
vitu ambavyo Ruby angevihitaji
halafu wakaagana
“Ni mara ya kwanza
ninasikia kuna idara ya siri ya
usalama wa ndani wa nchi.Zipo
taasisi mbali mbali za serikali
zinazohusiana na masuala ya
usalama wa nchi kama jeshi la
polisi idara ya usalama wa taifa
n.k.Nini hasa majukumu ya
idara hii ya siri ya usalama wa
ndani wa nchi.Ninapata ukakasi
kuhusiana na malengo ya
kuanzishwa kwake wakati zipo
taasisi zenye kushughulikia
masuala haya ya usalama wa
nchi kwa ujumla wake.Kwa
kuwa tayari Ruby anayo mafailli
yaliyoibwa na kirusi kutoka
katika idara hii tutachunguza na
tujue kazi zake ni zipi
hasa.”akawaza
Mathewakachukua simu na
kutafuta namba za Gosu Gosu
akampigia
“Hallo Mathewhabari za
Dar es salaam?akauliza Gosu
Gosu
“Huku kwema kabisa Papii
Gosu Gosu,mambo
yanakwendaje hapo Dubai?
“Kila kitu kinakwenda
vizuri kabisa mkuu”
“Gosu Gosu nimekupigia
usiku huu ninakuomba kesho
uje Dar es salaam kuna kazi
imejitokeza”
“Kazi gani mkuu wangu ya
kibiashara?
“Si kibiashara Gosu
Gosu.Kuna mtu wangu wa
karibu sana anaitwa Olivia
Themba ametekwa jana na
watu wasiojulikana hivyo
nimejikuta sina namna zaidi ya
kuingia katika opresheni ya
kumtafuta.Ninahitaji sana
msaada wako.Nimezungumza
na Ruby atakuja kesho saa moja
za joni hivyo nakuomba na
wewe uje ili tuunde timu nzuri
ya kuhakikisha tunamsaka
Olivia na kumpata”
“Usihofu Mathewnitakuja
kesho.Kuna ndege ya Emirates
itaondoka hapa Dubai kesho saa
nne na robo kuja Dar es salaam
nitakata tiketi niweze kuja na
ndege hiyo.Nitakujulisha kila
kitu kuhusiana na safari yangu
kesho asubuhi”
“Sawa Gosu
Gosu.Nashukuru sana “
akasema Mathewna kukata
simu
“Kwa ukubwa wa suala hili
ninawahitaji sana Ruby na Gosu
Gosu.kwa upande wangu
umakini mkubwa sana
unatakiwa kuanzia sasa.Hawa
jamaa tayari wamenifahamu na
lazima watakuwa
wananifuatilia kwani tayari
nimekuwa mtu hatari kwao”
akawaza Mathew
 
SIRI
PART 1: SEASON 4
MTUNZI: PATRICK CK
Agrey Themba alishushwa
katika gari akiwa amefungwa
pingu mikononi na kufunikwa
mfuko mweusi
kichwani.Hakuweza kuona
chochote zaidi ya kusikia
milango ikifunguliwa na
kufungwa.Watu waliokuwa
wamemshika mikono
wakamkalisha katika kiti
wakamfungua pingu alizokuwa
amefungwa mkononi
wakaifunga mikono yake katika
pingu zilizokuwa
zimeunganishwa na meza.
“Jamani nimewakosea
nini?akauliza Agrey lakini
hakuna aliyemjali wala kumjibu
“Kama kuna kuna mtu
kawatuma mwambieni
anisamehe asinitese kiasi
hiki.Kama kuna mtu yeyote
nim…………” akasema Agrey
Themba na kunaswa kofi zito
“Shut up !! akasema jamaa
aliyemnasa kofi.Bado alikuwa
na mfuko kichwani hakuweza
kumuona mtu yeyote.
“Mnanipiga nimewakosea
nini jamani? Niambieni
tafadhali kama kuna kitu
nimewakosea.Niambieni kama
mnahitaji fedha nitawapa kiasi
chochote mnachokihitaji ili
mradi mniache salama”
akasema Agrey lakini hakuna
aliyemjibu akasikia mlango
ukifungwa na chumbani mle
kukawa kimya.
“Nilifanya ujinga mkubwa
sana kumuamini mtu yule
aliyepiga simu akasema yeye ni
Mathewna amempata
Olivia.Nilitakiwa kuwasiliana
kwanza na polisi lakini
nikafuata maelekezo yake
aliyoyatoa na ndiyo sababu ya
kufika hapa nilipofika.Naamini
hii yote ni michezo ya
MathewMulumbi.Toka mwanzo
sikuwa nimemuamini kabisa na
ndiyo maana nilisita
aliponiambia anataka kusaidia
kumtafuta Olivia.Lucy ndiye
ameyataka haya yote kwa
kumuamini haraka haraka na
kukubali kumpa ruhusa
akamtafute Olivia.Naamini
Mathewndiye anayehusika
katika tukio la kutekwa kwa
Olivia na sasa wameniteka
mimi.Nini hasa anakihitaji
kutoka kwetu?Shida yake ni
fedha au kuna kitu kingine ?
akajiuliza Agrey Themba
“Lakini anajidanganya bure
yule kijana kwani hatafika
mbali na uhalifu huu
anaoufanya.Jeshi la polisi
wanaendesha operesheni
kubwa ya kuhakikisha Olivia
anapatikana na baada ya kupata
taarifa kwamba na mimi pia
nimetekwa nyara msako
utaongezeka zaidi na lazima
watamkamata.Mpaka kesho
asubuhi nitakuwa tayari
nimejulikana kuwa nimetekwa
hivyo nguvu itakuwa kubwa
zaidi ya kunitafuta mimi na
Olivia” akawaza Agrey Themba
Devotha Adolph akiwa
ofisini kwake mlango
ukafunguliwa akaingia Dennis
“Karibu Dennis” akasema
Devotha
“Madam nimekuja kukupa
taarifa kwamba kila kitu tayari
na Agrey yuko katika chumba
E1 kama ulivyoelekeza”
“Ahsante Dennis.Kazi
nzuri.Hakukuwa na tatizo lolote
wakati wa kumchukua?
“Kama nilivyokueleza
simuni kwamba hakukuwa na
tatizo lolote alikuja mwenyewe
hadi eneo la tukio tukamchukua
kwa wepesi bila purukushani
zozote isipokuwa mlinzi
anayelinda jengo lile
tumelazimika kumkata pumzi
na ametupwa baharini”
“Good job Dennis.Unaweza
kwenda sasa lakini muwe
katika utayari kwani muda
wowote kunaweza kujitokeza
kazi ya kufanya”
“Sawa Madam” akajibu
Dennis na kuondoka.Devotha
akayaelekza macho yake katika
luninga kubwa ukutani
iliyokuwa inaonyesha picha
kutoka katika kamera zote
zinazoizunguka nyumba
ile.Katika kamera ya lango kuu
la kuingilia ndani ya nyumba ile
ziliingia gari tatu
“Kaiza anarejea na miili ya
wenzetu.Sikutegemea kabisa
kama suala hili lingebadilika na
kuwa namna hii.Tayari
limekuwa kubwa na maisha ya
watu wetu yamekatishwa
kikatili sana na huyu shetani
MathewMulumbi.Bado najiuliza
amewezaje kuua watu kumi na
tatu?Alikuwa peke yake au kuna
watu anashirikiana nao?
Akajiuliza
Mlango ukagongwa
akaingia Kaiza akamtazama
Devotha ambaye sura yake
ilionyesha majonzi makubwa
“Nimerejea Devotha”
akasema Kaiza
“Niambie hali mliyoikuta
huko” akasema Devotha
“Ni hali yakusikitisha
sana.Karibu kikosi chote
kimeteketea.Kwa inaonekana
walikuwa wanauawa kimya
kimya bila kuwa na
taarifa.Karibu wote wamepigwa
risasi kichwani.Baada ya
kufanya mauaji hayo wauaji
waliingia ndani ya nyumba
kwani tumekuta mlango uko
wazi.Ilikuwa vyema tuliwahi
kumuondoa Olivia na kila kitu
kilichokuwamo.Inaonekana
lengo lao lilikuwa ni Olivia”
akasema Kaiza.
“Kaiza ni wakati wako wa
kufahamu kuhusu suala hili.Mtu
aliyefanya mauji haya anaitwa
MathewMulumbi”
“Unamfahamu?akauliza
Kaiza
“Nilipigiwa simu na rais
akanitaka nimuhamishe Olivia
pale kitalu 7 haraka na kuondoa
kila kitu kwani kuna mtu tayari
amekwisha fahamu mahala
alipo Olivia. Baada ya
kumuhamisha Olivia nilikwenda
kuonana na rais” akasema
Devotha na kumueleza Kaiza
kila kitu alichozungumza na
rais.
“Nimestushwa sana kwa
taarifa hii.Nina wasiwasi huyu
jamaa anashirikiana na mtu
katika idara yetu?akasema
Kaiza
“Kwa nini unahisi hivyo
Kaiza?
“Mpango huu ulikuwa ni wa
siri kubwa.Devotha hainiingii
akilini huyu jamaa agundue
kuhusu mpango huu wa siri
kama hana mtu anayeshirikiana
naye ndani ya idara yetu”
akasema Kaiza
“Hicho unachokisema
kinawezekana Kaiza hata mimi
nimekuwa nina mawazo kama
hayo.Lakini kwa mujibu wa
maelezo ya rais ni kwamba
Mathewaliweza kugundua
mahala alipo Olivia kutokana na
zile namba ambazo Olivia
alitupa tuzipige na mifumo yetu
yote
ikajifunga.Mathewalimueleza
Agrey kwamba namba zile
alizompa Olivia ni programu
maalum ambayo
ingemuwezesha kujua mahala
aliko Olivia pindi anapozipiga
na sisi tulizipiga tu bila kuchuua
tahadhari hivyo
Mathewakagundua mahala
namba zile zilikopigwa.Hayo ni
maneno ya Mathewjapo siamini
sana katika programu hiyo
lakini tutafahamu kila kitu pale
tutakapomtia mik………………”
akanyamza Devotha simu yake
ilipoita akaichukua na mpigaji
alikuwa ni Dr Evans
“Rais anapiga” akasema
Devotha na kuipokea ile simu
“Mheshimiwa rais”
akasema Devotha
“Devotha mnaendeleaje?
“Tunaendelea vyema
mheshimiwa rais.Miili ya P3
Unit imewasili muda si mrefu”
akasema Devotha
“Devotha nimezungumza na
Lucy Themba muda mfupi
uliopita akanipa taarifa kuwa
Agrey ametekwa na watu
wasiojulikana nikamuhakikishia
kwamba lazima aliyefanya
hivyo ni
MathewMulumbi.Nimemuomba
kesho asaidiane nasi katika
mpango wetu wa kumpata
Mathew.Andaa kikosi cha watu
watano au zaidi waende
nyumbani kwa Agrey kesho
asubuhi,Lucy atampigia simu
Mathewna kumtaka waonane
na akifika pale nyumbani kwa
Lucy hakikisheni mnamkamata
Mathew.Nimewapeni njia rahisi
ya kuweza kumpata
Mathew.Baada ya kumkamata
mpelekeni kitalu 1 hakikisheni
anahojiwa na anaeleza kila
kitu.Sitaki tena kusikia kwamba
mmeshindwa kumkamata
MathewMulumbi.Hii ni nafasi
ya dhahabu imepatikana
itumieni vyema” akasema Dr
Evans.
“Ahsante sana mheshimiwa
rais kwa nafasi hii kubwa
tuliyoipata ninakuahidi
kwamba hakutafanyika kosa na
lazima Mathewatapatikana”
akasema Devotha
“Vipi kuhusu Olivia
mmekwisha anza kumfanyia
mahojiano?
“Tunajipanga ili tuanze
kazi.Nitakupa mrejesho kila
tutakachokuwa tunakipata”
akasema Devotha
“Devotha nasisitiza tena
umakini mkubwa katika suala
hili.Tulichokifanya kumteka
Olivia na baba yake ni siri
kubwa sana lakini tayari kuna
mtu amekwisha ifahamu hivyo
lazima kwa namna yoyote ile
tumtie mikononi mwetu ili
kuendelea kuhakikisha kwamba
siri yetu inabaki salama.Endapo
tutashindwa kumdhibiti
Mathewtutajiweka katika
mazingira magumu.Dhumuni la
kuanzisha idara hii ni
kushughulika na mambo
ambayo idara nyingine za ulinzi
na usalama wa nchi haziwezi
kuyaona.Kwa sasa
MathewMulumbi ni hatari sana
kwa usalama wa nchi hivyo
fanyeni kazi yenu kuhakikisha
nchi inakuwa
salama.Kilichotokea kitalu 7
sitaki kukisikia tena.Maelezo ya
Mathewyanaonyesha kwamba
ni mtu hatari hivyo
mnapokwenda kukabiliana
naye hakikisheni mnakuwa na
kikosi kilichokamilika chenye
watu wenye uwezo wa hali ya
juu.P3 Unit ni kikosi kilichopata
mafunzo ya hali ya juu sana
lakini jana wameuawa kama
kuku.Imeniumiza sana.Ni
gharama kubwa imetumika
kuwapatia mafunzo lakini
wanakufa kifo ambacho naweza
kusema kwamba ni kifo cha
aibu.Inawezekanaje mtu mmoja
akawashinda watu kumi na tatu
na wote wana silaha kali?Sitaki
jambo kama hilo lijitokeze tena”
akasema Dr Evans
“Mheshimiwa rais
nimekuelewa na
ninakuhakikishia kwamba
hakutakuwa na uzembe
wowote.Tunaipa uzito mkubwa
sana operesheni hii”
“Good.Nipeni taarifa baadae
mtakachokipata kwa
Olivia.Devotha nataka mpate
taarifa zote tunazozihitaji
kutoka kwa Olivia.Nilikupa
idara hiyo uiongoze kwa sababu
ninakuamini kwamba unao
uwezo wa kuongoza idara kama
hiyo.Nataka Olivia aongee na
aseme kila kitu.Don’t be soft on
her make her talk !’ akasema Dr
Evans na kukata simu. Devotha
akamueleza Kaiza kile
alichoelekezwa na rais
“Kwa mpango huu tayari
ninaiona picha ya huyo
Mathewmikononi
mwetu.Nitaandaa kikosi kidogo
lakini kizito na
Mathewhataweza kufanya
chochote.Hesabu hilo
limekwisha Devotha”
“Kaiza endapo tutamkosa
Mathewsafari hii rais hataweza
kutuvumilia tena.Kuna
uwezekano mkubwa akatafuta
watu wengine kuchukua nafasi
zetu.Kaiza bado ninaihitaji hii
kazi hivyo basi nakuomba
ufanye kila lililo ndani ya uwezo
wako kuhakikisha
MathewMulumbi anapatikana
kesho.Tukimpata
Mathewhatutakuwa na kitu cha
kuhofia tena lakini kama
tukimkosa tutakuwa
tumejiweka katika nafasi mbaya
kwanza kama idara na pili rais
hatatuamini tena” akasema
Devotha
“Nimekuelewa Devotha
naomba nikutoe hofu kwamba
MathewMulumbi ana muda
mfupi sana kutoka sasa kabla ya
kutua mikononi mwetu”
akasema Kaiza
“Good.Ni wakati sasa wa
kumuhoji Olivia.Nitaifanya
shughuli hiyo mimi
mwenyewe.Agrey Themba
tayari amekwishafikishwa hapa
yuko E1.Kabla ya
mapambazuko lazima tuwe
tumepata kila taarifa
tunayohitaji kutoka kwa
Olivia.Tonight she must talk !!
akasema Devotha.
“Devotha kwa nini usinipe
mimi nafasi hii
nikamuhoji.Nakuhakikishia
lazima atafunguka kila kitu”
akasema Kaiza
“Maneno aliyonieleza Dr
Evans usiku huu
yamenikumbusha mimi ni nani
hadi akaniteua kuwa
mkurugenzi wa idara hii
muhimu kabisa.Alinichagua
kutokana na uwezo wangu
mkubwa nilio nao lakini katika
sakata hili ninaonekana
kupwaya hadi akaamua
kunikumbusha majukumu
yangu.Leo nitamuonyesha
Olivia kwa nini niliaminiwa na
rais akanichagua kuongoza
idara hii” akawaza Devotha na
kuchukua simu akapiga
“Cindy shughulikia miili
yote iliyoletwa ihifadhiwe
katika kontena lile maalum
lenye baridi hadi
tutakapomaliza shughuli yetu”
akasema Devotha akatoka mle
katika ofisi yake akiwa na Kaiza
wakaenda katika chumba
kimoja kilichokuwa na
kompyuta tatu.Olivia
alionekana kupitia moja ya
kompyuta akiwa amefungwa
katika kiti.Devotha akamtazama
kwa hasira halafu akasema
“It’s time.Hakuna muda wa
kupoteza”
Akatoka ndani ya chumba
kile akaenda katika chumba
alimofungwa Olivia akapitisha
kadi katika mlango ukafunguka
akaingia ndani.Chumba
kilikuwa cheupe na Olivia
alikuwa amefungwa mikono
kwa nyuma katika kiti.Mbele
yake kulikuwa na meza na viti
viwili.Devotha akavuta kiti
akaketi
“Hallo Olivia” akasema
Devotha na kwa mbali
akatabasamu na vishimo
vikaonekana katika mashavu
yake.Olivia akamtazama
hakusema kitu
“Olivia I’m back again”
akasema tena Devotha na
kuendelea kumtazama Olivia
“Mazungumzo yetu ya awali
hayakumalizika vizuri na safari
hii nimekuja kumaliza
mazungumzo yetu.Sikuwa
nimejitambulisha kwako pale
awali.Ninaitwa Devotha Aldoph
ni mkurugenzi wa idara ya siri
ya usalama wa ndani wa
nchi.Kazi yetu ni kuhakikisha
nchi inakuwa
salama.Tunashughulika na
mambo yale yaliyofichika
kabisa ambayo ni hatari kwa
usalama wa nchi” akasema
Devotha na kumtazama Olivia
kwa sekunde kadhaa halafu
akasema
“Niliaminiwa na kupewa
kuongoza idara nyeti kama hii
nikiwa mwanamke wa kwanza
kabisa kuongoza idara nyeti
kama hii hapa nchini.Unadhani
kwa nini niliaminiwa na
kupewa idara hii
niiongoze?akauliza lakini Olivia
hakujibu kitu
“Nitakupa jibu.They call me
a female devil.Ninaitwa hivyo
kutokana na ujasiri wangu wa
kutoogopa kitu au mtu
yeyote.Ninapokuwa katika
kutekeleza majukumu yangu ya
ulinzi wa nchi sisiti kutoa roho
ya mtu na ndiyo maana
nikaitwa shetani wa kike.Usione
sura yangu ikitabasamu lakini
mimi ni mkatili mno.Kwa
kukupa mfano tu nilimuua kaka
yangu ambaye ndiye ndugu
yangu wa pekee aliyebaki baada
ya kujiunga na makundi ya
uhalifu.Sikusita kuondoa uhai
wake.Nataka upate picha kama
niliweza kuondoa uhai wa kaka
yangu ambaye nimezaliwa naye
tumbo moja nitashidwaje
kukukata kichwa
chako?Nitashindaje kuiteketeza
familia yako?
Devotha alipotaja familia Dr
Olivia akamtazama kwa hasira
“Nakuonya usithubutu
kuigusa familia yangu”
“Taratibu Olivia.Sijasema
nitaiteketeza familia yako lakini
endapo italazimu kufanya hivyo
sintasita kuwateketeza mmoja
baada ya mwingine huku
ukishuhudia.Sitaki tufikie huko
nataka tuzungumze tumalize
haya mambo bila ya kufungua
ukurasa mpya.Ninataka
kuzungumza nawe kwa amani
na ukinipa ushirikiano
ninakuahidi Olivia nitakuacha
huru”
“Nini hasa mnachokitafuta
kwangu?akauliza Dr Olivia
“Rais amekwisha nieleza
kila kitu ulichomueleza kuhusu
mahusiano yako na IS na kila
kitu ulichokifanya”
“Sikumueleza chochote
kuhusu mimi na
IS.Nilichomweleza ni kwamba
ni kweli nilikwenda Kinshasa
kuonana na Seif Almuhsin lakini
sikumueleza kwa nini”
“Unafahamu kama Seif
Almuhsin ni mmoja kati ya watu
muhimu sana katika mtandao
wa IS?
“Ndiyo ninafahamu”akajibu
Olivia
“Kama ulifahamu yule ni
mtu hatari kabisa kwa nini basi
ukaenda kukutana naye
Kinshasa?Are you one of
them?akauliza Devotha
“What if I’m one of
them?akauliza Dr Olivia
“IS ni kikundi cha kigaidi
ambacho kimekuwa kikipigwa
vita duniani kote.Wamekuwa
wakifanya mashambulio ya
kigaidi sehemu mbali mbali
duniani na kuua watu wasio na
hatia.Kwa sasa IS wameanza
kujipenyeza barani Afrika na
wanataka kuotesha mizizi yao
Tanzania jambo ambalo katu
hatuwezi kulikubali hivyo kama
wewe ni mmoja wao basi
jihesabu kwamba wewe ni adui
yetu na utaeleza kila kitu
kuhusiana na mikakati ya
kikundi hicho.Nat…..”Kabla
Devotha hajamaliza Dr Olivia
akamkatisha
“Hey ! Let’s make this
short.Hauwezi
kuniogopesha.Ulisema rais
amekueleza kila kitu
nilichozungumza naye hii
inanipa picha kwamba wewe na
rais ni watu wa karibu
sana.Nataka kufahamu where is
Edger Kaka?
“Olivia nani kakuaminisha
kwamba Edger kaka yuko
hai?Nani wamekutuma
uanzishe kashfa hii?Nini hasa
malengo yenu?Ni moja ya
mipango ya IS kutaka kuleta
machafuko hapa
nchini?akauliza Devotha
“Nimekwisha muonya rais
kwamba kama asiponieleza
mahala alipo Edger kaka
mwanae atakufa.Amechomwa
sindano yenye virusi na
mwenye dawa ya kumponya ni
mimi mwenyewe ambaye
nimevitengeneza virusi hivyo
kwa hiyo msisitize kwamba
ninamtaka Edger kaka ama
sivyo atampoteza mwanae na
hii itaendelea kwa familia yake
yote hadi pale atakaponieleza
wapi alio Edger Kaka”
“Olivia kwa nini unafanya
hivi kwa nchi yako?Wamekupa
nini watu unaoshirikiana nao
kiasi cha kukubali kutumika
namna hii? Akauliza Devotha
“Nieleze tafadhali watu
unaoshirikiana nao ni akina
nani? akasema Devotha
“Devotha nimekwisha
kwambia kwamba unapoteza
muda wako bure siwezi
kukueleza chochote.Mtu
ninayeweza kuzungumza naye
ni rais pekee.Ninaamini lazima
atakuja kwangu akilia na
atanieleza mahala alipo Edger
Kaka”
“Olivia ninasema kwa mara
ya mwisho Edger amekwisha
fariki dunia miaka mitatu
ilopita.Hayupo tena duniani
unachoweza kukipata ni mifupa
yake tu.Ondoa ujinga huo
kichwani mwako kwamba
Edger yuko hai.Muda wa mzaha
umekwisha sasa nataka
unieleze nini hasa sababu ya
wewe kwenda kukutana na Seif
almuhsin jijini
Kinshasa?Mazungumzo yetu
rasmi yataanzia hapo”akasema
Devotha
“Devotha nimekwambia
siwezi kuzungumza chochote na
mtu kama wewe.Ninayeweza
kuzungumza naye ni rais peke
yake wewe ni mtu mdogo sana
kuzungumza nami” akasema Dr
Olivia
“Olivia wewe ni mwanamke
mwenzangu na sitaki nikufanyie
ukatili.Sitaki kutumia nguvu
kukulazimisha uongee lakini
kwa kuwa umeonyesha
kwamba hauko tayari kwa
mazungumzo ya amani basi
tutaufungua ukurasa mpya”
akasema Devotha na kufungua
moja ya kabati jeupe akatoa
kisanduku cheupe akakiweka
mezani akakifungua na kutoa
vitu mbalimbali akaviweka
mezani.Akachukua kisu kikali
na kumsogelea Olivia
“Olivia nilikwambia muda
wa mzaha umekwisha na sasa
nataka ufunguke kabla sijaanza
kukuharibu.Umekwenda
Kinshasa kukutana na Seif
Almuhsin ambaye anatumiwa
na IS kusajili vijana
wanaokwenda kupatiwa
mafunzo ya ugaidi na kupeleka
katika sehemu mbali mbali
duniani kupambana.Kama
haitoshi tumekuta mawasiliano
yako na Sayid Omar ambaye
anatajwa kama mfadhili
mkubwa wa kikundi cha
IS.Ukaribu huu na watu wa IS
unatufanya tuamini
unashirikiana nao.Nataka
unieleze mipango yenu yote
mliyopanga kuitekekeleza hapa
Tanzania ” akasema
Devotha.Olivia hakumjibu
chochote alikuwa kimya
akimtazama
“Olivia umesikia
nilichokuuliza….” Akasema
Devotha
“Nimekwambia siwezi
kuzung………..” kabla Olivia
hajamaliza sentensi yake
Devotha akakizamisha kisu
katika paja la Olivia
“Aaaagghhh !! Olivia
akapiga ukelele mkubwa
“Huo ni mwanzo tu Olivia
kama hautafunguka nitaendelea
kukuharibu” akasema Devotha
na kuchukua kichupa kidogo
akapuliza mahala alipochoma
kisu na Olivia akapiga tena
ukelele kwa maumivu makali
aliyoyapata
“Talk to me!! Akasema
Devotha lakini Olivia aliendelea
kulia
“Olivia usipofunguka
nitakuacha upoteze damu na
ufariki dunia.Hebu pata picha
mama yako atajisikiaje akipata
taarifa kwamba umefariki
dunia? Rafiki yako
MathewMulumbi pia ataumia
sana” akasema Devotha na
Olivia akastuka baada ya
kusikia jina la Mathewlikitajwa
“Usistuke Olivia
tunafahamu kila kitu kuhusu
maisha yako.Utafunguka au
tuendelee na huu
mchezo?akauliza Devotha lakini
Olivia hakumjibu kitu.Bado
damu iliendelea kumwagika
katika jeraha
“Good.Tunaendelea na
zoezi letu hadi pale
utakaposema basi” akasema
Devotha na kuchukua mkasi
akamtazama Olivia halafu
akachukua dawa katika
sanduku akamuwekea katika
jeraha lile lililokuwa linavuja
damu.Devota akalishika sikio la
Olivia na kujiandaa kulikata
kwa mkasi mara akakumbuka
kitu
“Olivia u mwanamke
mrembo na sitaki kuuharibu
uzuri wako.Yupo mtu ambaye
anapaswa abebe mzigo wako
wa adhabu”akasema Devotha
na kuielekea kamera
“Nipe E1”akasema na katika
moja ya kuta za chumba kile
ikatokea picha kubwa ya mtu
akiwa ndani ya chumba ameketi
kitini akiwa amefungwa mikono
na pinguu iliyo juu ya meza na
kichwani alikuwa amevishwa
mfuko mweusi
“Huyu umuonaye pichani
ndiye atakayebeba mateso yote
badala yako hivyo ni jukumu
lako kumuokoa na utamuokoa
pale utakapofunguka kila kitu”
akasema Devotha na kuamuru
mtu yule ndani ya chumba
avuliwe mfuko kichwani.Olivia
akapatwa na mstuko mkubwa
“Baba?! Akasema akiwa
hayaamini macho yake
“This is not true.Baba yangu
hayupo hapa” akasema Olivia
“Olivia unachokishuhudia
ni kitu cha kweli kabisa na si
picha ya kutengeneza.Yule ni
baba yako Agrey Themba.Huyu
ni mtu wa kwanza tumemleta
hapa aje akusaidie kubeba
mateso yako hivyo kama
unampenda na unataka
kumuokoa funguka na utueleze
ukweli wote” akasema Devotha
“Please don’t hurt
him.Don’t touch my father.Don’t
touch my family.Hangaikeni na
mimi lakini familia yangu
waacheni kabisa hawahusiki na
chochote!
“Olivia unaipenda sana
familia yako nao wanakupenda
pia na ndiyo maana tunawaleta
hapa ili waweze kukuonyesha
upendo wao na kukusaidia
kubeba mateso yako”akasema
Devotha na kuigeukia kamera
“Guys he’s all yours”
akasema Devotha na watu
watatu waliojazia miili
wakajitokeza na kuanza
kumtandika makonde
Agrey.Yalikuwa ni makonde
mazito na damu nyingi ikaanza
kumtoka.Olivia akafumba
macho asione kilichokuwa
kinaendelea kwa baba yake.
“Stop ! akasema Devotha
“Olivia umeona mateso
anayoyapata baba yako.Kwa
nini ukakubali baba yako
ateseke kiasi hiki?Tell me
everything and we’ll let your
father go!! Akasema Devotha
Olivia akafumbua macho na
kumtazama baba yake ambaye
uso wake ulikuwa umechafuka
kwa damu akahisi kitu kama
kisu kinaukata moyo
wake.Akamtazama Devotha na
kusema
“Go ahead kill him !
“Unasemaje Olivia ?akauliza
Devotha.Hakutegemea kusikia
kauli kama ile
“Umedhamiria kumpa
mateso baba yangu huku
niishuhudia ili kunilazimisha
niweze kufunguka na kukueleza
yale uyatakayo.Umekosea sana
njia hiyo haitaweza kusaidia
chochote kwani sintawaeleza
chochote.Anzeni kumuua
yeye,muendelee na watu
wengine wa familia yangu na
mwisho mnimalizie mimi.Go
ahead kill him ! akasema Dr
Olivia kwa ukali.Devotha
akamuangalia kwa hasira
“Olivia unajifanya shujaa
sana? Akauliza Devotha
“Kill him” akasema Dr
Olivia.
“You think this is a joke?
Let me show you it’s not a joke”
akasema Devotha na kutoka
mle chumbani kwa hasira na
baada ya dakika kama nne
akaonekana katika chumba
alimo Agrey Themba.
“Olivia nimekuja
kukuonyesha kwamba sisi
hatutanii” akasema Devotha na
Agrey aliposikia jina Olivia
likitajwa akainua
kichwa.Hakuweza kumuona
aliyekuwa anaongea kutokana
na damu nyingi kumtiririka
usoni kufuatia kipigo kizito
alichopigwa.Devotha akachukua
bastora na kumlenga Agrey
“Olivia I’ll count to
three”akasema Devotha
“Three”
“Jamani naomba msiniue
sina kosa lolote!! Akasema
Agrey kwa taabu
“Two! Devotha akaendelea
kuhesabu huku akimtazama
Olivia kupitia luninga
iliyokuwamo ndani ya kile
chumba
“Please forgive me my
father.I love you” akawaza
Olivia na kufumba macho
asishuhudie kifo cha baba yake.
“One! Akasema Devotha na
mlio wa risasi ukasikika.Baada
ya sekunde kadhaa Olivia
akafumbua macho na
kumtazama baba yake akiwa
bado amekaa kitini
“Thank you God ! akasema
kwa sauti ndogo.Devotha
hakumpiga risasi Agrey alipiga
pembeni
“Olivia nilitaka
kukuonyesha kwamba sisi
hatuna utani.Next time I won’t
miss.Uko tayari kufunguka
?akauliza Devotha.Olivia
hakujibu kitu.Ukasikika mlio
mwingine wa risasi.Devotha
alimpiga Agrey Themba risasi
katika paja.Agrey akapiga kelele
kubwa
“Are you ready to talk
Olivia? Devotha akamuuliza
Olivia kupitia kamera.Olivia
alihisi maumivu makali kwa
ndani kumuona baba yake
akipata mateso makali namna
ile
“Bila Edger kupatikana
sintakuwa huru.Ili niweze
kujinasua kutoka katika mikono
ya IS lazima nihakikishe Edger
kaka anapatikana.Natakiwa
kuendelea na msimamo wangu
ili kujilinda na kuilinda familia
yangu dhidi ya IS.Najua
hawawezi kumuua baba ila
watamtesa sana kunilazimisha
nifunguke”akawaza Olivia
“Olivia !! akauliza Devotha
kwa ukali lakini Olivia hakujibu
kitu aliendelea
kumtazama.Mara ukasikika
mlio mwingine wa
risasi.Devotha alimpiga Agrey
risasi katika paja la mguu
mwingine.
“My God please save my
father” akaomba Olivia akiwa
amefumba macho alihisi
uchungu mkubwa lakini
hakufumbaa kinywa chake
kusema chochote.Devotha kwa
hasira akaitupa chini bastora
ile.
“Mpelekeni mkamtibu
haraka sana ! Devotha
akawaelekeza wale jamaa
waliokuwemo mle ndani
akatoka kwa hasira na kwenda
katika chumba walimo akina
Kaiza
“Huyu ni mwanamke wa
aina gani ?Kwa nini imekuwa
ngumu kumfungua? Akauliza
Devotha akiwa amejishika
kiuno
“Devotha kwa namna
nilivyomuona Olivia hatupaswi
kutumia nguvu.Nashauri
tumuendee taratibu tunaweza
kufanikiwa
kumfungua.Kumbuka huyu
tayari ni mshirika wa IS hivyo
amekwisha kula kiapo cha
kutokusema chochote.Kama
ameweza kushindwa kufunguka
hata baada ya kushuhudia baba
yake akipigwa risasi mbili
hakuna tunachoweza kufanya
kumfungua.Hata tukimpa
mateso ya aina gani hataweza
kufunguka”akasema Kaiza
“Kaiza we must break her
before sunrise.Kila kitu lazima
kimalizike usiku wa leo kwa
sababu kesho itaamshwa na
taarifa mpya za kupotea kwa
Agrey Themba na mambo
yatazidi kuwa magumu.Hatuna
muda wa kusubiri wala
kubembeleza.Tutatumia kila
njia hadi afunguke”akasema
Devotha
“Devotha tunatakiwa kukaa
chini na kutafuta namna ya
kumfungua Olivia.Kutumia
nguvu hatutaweza
kamwe.Nashauri tubadili
mbinu” akasema Kaiza.Devotha
akainamisha kichwa akafikiri
“Unashauri nini?akauliza
Devotha
“Tusitumie nguvu
hatutaweza kupata
chochote.Nashauri kesho
tumueleze Agrey kila kitu
kuhusiana na Olivia na yeye
ndiye atakayekwenda
kuzungumza na mwanae
kumtaka aeleze ukweli.Kwa njia
hii naamini Olivia anaweza
akafunguka lakini kwa kutumia
nguvu hatutapata kitu” akasema
Kaiza.
“Hilo linaonekana ni wazo
zuri.Lakini vipi kama rais
akitaka kujua tumefikia wapi?
“Mwambie bado
tunaendelea na mahojiano”
akasema Kaiza
“Sawa nakubaliana na
ushauri wako wa kumtumia
Agrey.Tuma mtu akamtibu
Olivia jeraha lake katika paja”
akasema Devotha na kuelekea
ofisini kwake
“Sasa ninaamini kweli
Olivia ni mshirika wa IS.Tayari
amekwisha ingiwa na ile roho
ya kikatili kama waliyo
nayo.Hata baba yake
alipotishiwa kuuawa
hakuonyesha kujali.Hapa kuna
kazi ngumu sana
kumfungua.Hili suala
litakwenda mbali zaidi. Halafu
Olivia bado anaendelea
kusisitiza kuhusu Edger Kaka
kwamba yuko hai.Ukimtazama
machoni anamaanisha kile
anachokiongea.Kwa nini
amlenge rais DrEvans
kuhusiana na suala hili hadi
kufikia hatua ya kumchoma
mwanae sindano yenye virusi ili
kumshinikiza aweze
kumuonyesha mahala alipo
Edger? Kuna kitu chochote Dr
Evans anakifahamu kuhusu kifo
cha Edger?Hainiingii akilini
Olivia aweke msisitizo mkubwa
namna hii na hata kuhatarisha
maisha yake kwa jambo ambalo
hana uhakika nalo.Yawezekana
kweli kuna kitu kuhusiana na
kifo cha Edger” akawaza
Devotha
“Niachane na mawazo hayo
ya Edger nijielekeze katika
jukumu langu kuhakikisha
Olivia anafunguka kuhusu yeye
na kikundi cha IS na mipango
yao hapa Tanzania.Nilitegemea
lingekuwa suala rahisi na
ningeweza kupata kirahisi
taarifa kutoka kwa Olivia lakini
limegeuka na kuwa suala gumu
na kadiri muda unavyokwenda
ndivyo linavyozidi kuwa
gumu.Ngoja nipumzishe kichwa
changu kwanza hadi asubuhi
yawezekana nikapata
ufumbuzi” akawaza Devotha
 
SIRI
PART 1: SEASON 4
MTUNZI: PATRICK CK
Saa kumi moja za alfajiri Dr
Evans akampigia simu Dr
Stanslaus Mbeula
“Mheshimiwa rais habari za
asubuhi” akasema DrMbeula
“Habari yako Dr
Mbeula.Mnaendeleaje huko?
“Mheshimiwa rais
tumefanya kazi usiku kucha”
akasema Dr Mbeula
“Kuna chochote
mmekigundua” akauliza Dr
Evans
“Mheshimiwa rais
tumegundua virusi fulani katika
damu ya Coletha lakini
tunaendelea kuvichunguza
zaidi.Baada ya kufanya kazi
usiku kucha tumechukua
mapumziko mafupi tutarejea
tena baadae kuendelea
kuchunguza zaidi” akasema Dr
Mbeula
“Dr Mbeula nakushukuru
sana kwa kazi kubwa
mliyoifanya.Vipi Coletha
anaendeleaje?
“Coletha anaendelea vyema
japo usiku hali yake ilikuwa
inabadilika badilika lakini hadi
ninaondoka hospitali muda
mfupi uliopita hali yake ilikuwa
inaendelea vyema”
“Dr Mbeula ninaomba
tafadhali mfanye juu chini
kutambua virusi hivyo ni vya
aina gani ili kuokoa maisha ya
mwanangu.Kama zoezi litakuwa
gumu naomba unijulishe ili
nimpeleke Coletha nje ya nchi”
akasema Dr Evans
“Mheshimiwa rais usiwe na
shaka.Tutakaporejea
tutaendelea na uchunguzi wetu
kuhusiana na virusi hivyo nina
hakika tutafanikiwa kupata
dawa yake baada ya
kuvitambua.Hata hivyo
mheshimiwa rais nina swali
nataka kuuliza”
“Uliza Dr Mbeula” akasema
Dr Evans
“Ulifahamuje kama
mwanao Coletha ana
maambukizi ya virusi hivi?
akauliza Dr Mbeula.Swali lile
likamfanya Dr Evans akae
kimya kwa muda halafu
akasema
“Dr Mbeula kwa sasa
naomba nisiliongelee hilo
suala..Naomba ujitahidi kwa
kadiri uwezavyo kuhakikisha
unapambana na virusi
hao.Tafadhali naomba uokoe
maisha ya mwanangu
nakutegemea sana Dr Mbeula”
“Nakutoa hofu mheshimiwa
rais mimi na wenzangu
tutafanya kila lililo ndani ya
uwezo wetu kuhakikisha
tunalipatia ufumbuzi suala hili
lakini mheshimiwa rais
nimeuliza swali hilo ili kujua
asili ya virusi hivi” akasema Dr
Mbeula
“Dr Mbeula baadae
nitakuita ikulu tutazungumza
vizuri lakini kwa sasa endeleeni
na jitihada za kupambana na
vizuri hao”
“Sawa mheshimiwa rais
nitawasiliana nawe tena baadae
kukujulisha maendelo yetu”
akasema Dr Mbeula akaagana
na rais.
“Olivia ! Olivia ! kwa nini
umemfanyia hivi Coletha? Sisi
ni kama ndugu tumekukosea
nini hadi ukatufanyia hivi?
Akawaza Dr Evans akiwa
amekaa kitandani akachukua
simu na kumpigia Devotha.Simu
iliita bila kupokelewa akapiga
tena ikapokelewa.Devotha
alizungmza kwa sauti ya
uchovu.
“Hallo mheshimiwa rais”
“Devotha umelala?
“Ndiyo nilikuwa
nimejipumzisha mheshimiwa
rais”
“Samahani kwa
kukuamsha.Nataka kujua zoezi
limekwendaje?akauliza
“Mheshimiwa rais zoezi
lilikuwa gumu kidogo tofauti na
tulivyotegemea.Olivia amegoma
kabisa kufunguka hata baada ya
kumpiga risasi baba yake”
“Agrey amepigwa risasi?!
Dr Evans akastuka
“Nilimpiga risasi katika paja
na haina madhara kwani
haikugusa mfupa,lengo lilikuwa
kumfanya Olivia aogope na
afunguke.Pamoja na kitendo
hicho bado Olivia aligoma
kabisa kufunguka na alidiriki
hata kutamka kwamba kama
ninataka kumuua baba yake
nifanye hivyo kwani hatanieleza
chochote.Mheshimiwa
rais,Olivia anashirikiana na
magaidi hivyo haitakuwa rahisi
kufunguka kwani magaidi hula
kiapo cha kutokusema
chochote.Tumefikiria kubadili
mbinu na kumtumia baba yake
Agrey.Tutamueleza kila kitu
kuhusu mwanae na yeye ndiye
atakayemshawishi afunguke”
akasema Devotha
“That’s a mistake
Devotha.Mkiwakutanisha Olivia
na baba yake lazima atamueleza
kwamba mimi niko nyuma ya
mpango huu jambo ambalo
sitaki Agrey alifahamu.Agrey ni
zaidi ya rafiki tumetoka mbali
hivyo sitaki afahamu kabisa
uhusika wangu katika suala hili
hivyo nataka asikutanishwe na
Olivia kabisa.Tafuteni mbinu
nyingine za kuweza kumfungua
Olivia na si mbinu hiyo ya
kumkutanisha na baba
yake.Devotha mnazo mbinu
nyingi sana kwa nini
mnashindwa
kuzitumia?Hakikisha jua
halizami leo bila kupata taarifa
zote kutoka kwa Olivia.Jambo
lingine nawasisitiza kuhusu
kumpata MathewMulumbi”
Akasema Dr Evans
“Tumejipanga vizuri kwa
ajili ya suala hilo mheshimiwa
rais.Mara tu
kutakapopambazuka kikosi
kilichoandaliwa kitakwenda
kuonana na Lucy Themba na
kila kitu kitakwenda kama
ulivyoelekeza.Mheshimiwa
kuna jambo lingine ambalo
nataka kulifahamu.Wakati
ninamuhoji Olivia alirudia tena
ile kauli yake kwamba
unafahamu kuhusu Edger kaka
kuwa hai.Kuna chochote
unakifahamu kuhusu Edger
mheshimiwa rais?Nimeuliza
hivi kutokana na msisitizo
mkubwa aliouweka Olivia
katika suala hili kwani hata
ukimtazama usoni wakati
akizungumza haonekani
kutania” akasema Devotha
“Devotha hata mimi suala
hili limenishangaza sana.Ni
mara ya kwanza nimelisikia
kwa Olivia.Edger Kaka
amekwisha fariki miaka mitatu
iliyopita na hakuna namna
yoyote anayoweza
kurudi.Sielewi hili suala la
kwamba Edger yuko hai kalitoa
wapi.Mimi ninachofahamu
Edger alikwisha fariki
dunia.Kingine cha ajabu ni yeye
mwenyewe Olivia ndiye
aliyeutambua mwili wa Edger
hospitali iweje leo ageuke na
kudai Edger hakufa? Hapo
ndipo unapoweza kuamini
kwamba hili ni jambo
linalotengenezwa kunichafua
mimi na serikali yangu.Olivia na
mtandao wake kuna kitu
wanakitafuta ndiyo maana
wakaanzisha kitu kama hiki.Hii
ni kashfa mbaya kabisa Devotha
na inaweza kuleta machafuko
makubwa kwa nchi ndiyo
maana nataka kwa namna
yoyote ile lazima Olivia ateswe
hadi afunguke ni akina nani
anaoshirikiana nao katika
kutunga uongo huu” akasema
Dr Evans
“Mheshimiwa rais
nimekuelewa lakini ukijipa
dakika chache kutafakari kile
anachokisema Olivia utapata
picha kwamba hajakurupuka
kudai kwamba Edger Kaka yuko
hai.Huu ni mpango ambao
umekuwa na maandalizi
makubwa hadi kuandaa kirusi
hicho na unaonekana si mpango
wa muda mfupi.Wamechukua
muda mrefu
kuuandaa.Ninachojiuliza kwa
nini wakulenge wewe moja kwa
moja?Mheshimiwa rais kama
kuna kitu chochote
unakifahamu kuhusu suala hili
nieleze tafadhali inaweza
ikasaidia kupata ufumbuzi wa
hili jambo kwani Olivia
amesisitiza kwamba
atazungumza pale
atakapopatikana Edger Kaka”
akasema Devotha
“Devotha narudia tena
sifahamu chochote kuhusu
jambo hili.Kama ningefahamu
chochote ningekueleza”
“Sawa mheshimiwa rais”
“Nipigie simu mara kwa
mara kunijulisha
mnavyoendelea” akasema Dr
Evans na kukata simu
“Olivia amekosa nini katika
maisha yake hadi akakubali
kujiunga na magaidi ambao
wamembadilisha na kumfanya
amekuwa mkatili kiasi
hiki?Hawa magaidi wanatumia
mbinu gani kuwaharibu watu
akili na kuwageuza kuwa
wakatili kama walivyomfanya
Olivia?Nimemshuhudia Olivia
toka akiwa mtoto na sikuwahi
hata mara moja kuhisi kama
siku moja angegeuka na kuwa
mtu katili namna
hii.Ametengeneza virusi
ambavyo vinaweza kumuua
Coletha ambaye ni sawa na
mdogo wake.Amemtumia
mwanangu ninayempenda
kunishinikiza eti nimrejeshe
Edger Kaka.Kwa nini hili suala
la Edger kaka amelikazania
sana wakati anafahamu kabisa
Edger Kaka amekwisha fariki na
kuoza kabirini?Halafu kwa nini
ananilenga mimi moja kwa
moja kwamba ninafahamu
mahala alipo
Edger?Najilazimisha kuamini
Olivia amechanganyikiwa lakini
haonekani kama mgonjwa wa
akili.Hapo ndipo linapokuja lile
wazo langu kwamba lengo lake
na watu anaoshirikiana nao ni
kutaka kuleta machafuko hapa
nchini kwa kuuaminisha umma
kwamba Edger hajafa na mimi
ninafahamu mahala alipo na
kwa kuwa Edger alikuwa na
watu wengi wanaompenda hasa
vijana yataibuka machafuko na
wao watapata nafasi ya
kujipenyeza hapa nchini
kufanya wanachokitaka.Huu ni
mpango wa IS ili waweze
kuingia hapa nchini na kuotesha
mizizi.Olivia amelipwa shilingi
ngapi hadi akubali kufanya kitu
cha namna hii? Katu sintakubali
watu hawa wafanikiwe lengo
lao.Lazima kuwaondoa haraka
sana nikianza na Olivia
mwenyewe na kupitia kwake
lazima atawataja wale wote
anaoshirikiana nao” akawaza Dr
Evans
 
SIRI
PART 1: SEASON 4
MTUNZI: PATRICK CK
Saa kumi na mbili na dakika
nne simu ya Mathewikaita
alikuwa ni Lucy
Themba.Mathewakaipokea
haraka haraka ile simu
“Mama shikamoo”
“Marahaba
Mathewhujambo baba”
“Sijambo kabisa
mama.Unaendeleaje?akauliza
“Hivyo hivyo mwanangu”
“Kuna taarifa zozote
zimepatikana toka wakati ule
tulipoachana?
“Hakuna taarifa zozote
baba,nimelia hadi machozi
yamekauka”
“Pole sana mama”
“Mathewnimekupigia
kukuomba uje hapa nyumbani
kwangu mapema asubuhi hii
kuna suala la muhimu sana
nataka kuzungumza nawe”
“Jambo gani mama?
“Ulisema kuna mtu wa
karibu na familia yetu ambaye
anashirikiana na watekaji?
“Ndiyo mama ninahisi
hivyo kuna mtu yuko karibu
yenu ambaye anashirikiana na
watekaji”Mathewakajibu
“Nadhani tayari
nimekwisha mfahamu”akasema
Lucy na Mathewakashusha
pumzi
“Una hakika mama?
“Ndiyo Mathewnadhani
“Unaweza ukanitajia mtu
huyo ni nani?akauliza Mathew
“Naomba uje hapa
nyumbani tuzungumze
Mathew”
“Sawa mama ninakuja hapo
nyumbani muda si mrefu”
“Nashukuru sana” akasema
Lucy na kukata simu
“Jana nimemuomba sana
Lucy Themba anieleze kama
kuna mtu walimpa taarifa zangu
akakataa kata kata kwamba
hakuna mtu
yeyote.Inawezekana baada ya
kukaa na kutafakari
amenielewa na tayari kuna mtu
amemuhisi.Ngoja nikamsikilize
mara moja” akawaza Mathewna
kuamka akaanza kujiandaa kwa
ajili ya kwenda kuonana na
Lucy Themba.
Hakuchukua muda mrefu
kujiandaa kabla hajatoka
akamuelekeza Derick
msimamizi mkuu wa nyumba
yake aandae vyumba viwili
kwani kuna wageni watafika
pale nyumbani jioni ya siku
ile.Baada ya kutoa maelekezo
yale akaondoka kuelekea kwa
Lucy Themba.Akiwa njiani
akampigia simu Ruby
“Ruby nimepigiwa simu na
Lucy Themba ameniambia kuna
mtu anamuhisi kushirikiana na
watekaji.Niko njiani
ninakwenda kuonana naye”
akasema Mathew
“Mathewuliniambia
kwamba ulimuomba sana
akwambie kama kuna mtu
aliyemweleza kuhusu wewe
akakataa.Kitu gani kimemfanya
abadili mawazo asubuhi hii?
“Yawezekana baada ya
kutafakari sana kuna kitu
amekigundua na anataka
kunieleza.Vipi mipango ya
safari? Akauliza Mathew
“Ninaondoka asubuhi hii
kuja Dar es salaam kama
nilivyokuahidi.Nipokee uwanja
wa ndege saa moja za jioni”
akasema Ruby
“Usihofu Ruby nitakuwepo
uwanjani kukupokea” akasema
Mathewakaagana na Ruby
Mathewaliwasili nyumbani
kwa bilionea Agrey Themba
akafunguliwa geti akaingia
ndani akashuka garini na
kwenda kugonga kengele ya
mlango mkubwa wa kuingilia
sebuleni.Akatoka msichana wa
kazi akamkaribisha
ndani.Wakati akimsubiri Lucy
akaletewa kikombe cha kahawa
akaendelea kunywa
taratibu.Akiwa ameyaelekeza
macho yake luningani
akitazama vipindi vya asubuhi
mara ghafla wakajitokeza watu
watano wote wakiwa na
bunduki.Mathewalihisi kama
yuko ndotoni lakini ile haikuwa
ndoto bali ni kitu cha kweli
kabisa alikuwa amezungukwa
na watu wenye silaha.
“MathewMulumbi uko chini
ya ulinzi.Tafadhali piga magoti
na inua mikono yako juu!
Akasema jamaa mmoja kwa
sauti kali.Mathewakawatazama
wale jamaa kama vile anatafuta
nafasi hata ndogo aweze
kuitumia
“Mathewhakuna
utakachoweza kufanya kwa
sasa.Piga magoti inua mikono
yako juu tafadhali” akasema
yule jamaa na vyuma vikasikika
katika zile bunduki za wale
jamaa.Mathewhakuwa na ujanja
akapiga magoti na kuinua
mikono juu.Kwa mzoefu wa
mambo haya kama
Mathewunaposikia vyuma vile
vimelia huna budi kutii amri
utakayopewa.Mmoja wa wale
jamaa akamsogelea huku
wenzake wakiwa katika
tahadhari kubwa na akamshika
MathewMikono na kumfunga
pingu kisha akamsachi na
kuichukua bastora yake na vifaa
vingine kama simu ambayo
ilizimwa haraka.Bila kupoteza
muda Mathewakafunikwa
mfuko kichwani akazungushwa
upande wa nyuma kulikokuwa
na magari matatu akaingizwa
katika gari la kati kati kisha
magari yale yakaondoka.Kaiza
ambaye alikuwa amepanda gari
la mbele kabisa akampigia simu
Devotha baada ya kuyaacha
makazi ya Agrey Themba.
“Devotha kazi
imekwisha.Tumempata
MathewMulumbi” akasema
Kaiza
“Unasema kweli Kaiza?
Akauliza Devotha
“Ndiyo Devotha.Tunaye
MathewMulumbi na hivi
tuongeavyo tunayaacha makazi
ya Agrey tunaelekea kitalu 1”
“Nimekosa neno la kuongea
Kaiza.Hakukutokea machafuko
yoyote?
“Hakukuwa na machafuko
yoyote.Tulimstukiza kiasi
kwamba alishindwa hata
kunyoosha mkono kuishika
bastora yake”
“Good job Kaiza.Ninaelekea
kitalu 1 kushuhudia
MathewMulumbi akifikishwa
pale.Huyu mtu ni hatari sana”
akasema Devotha na kukata
simu bila kupoteza muda
akampigia simu rais Dr Evans
“Devotha
unasemaje?akauliza Dr Evans
“Mheshimiwa rais
nimekupigia kukujulisha
kwamba tayari tumempata
MathewMulumbi”
“Mmempata
MathewMulumbi?
“Ndiyo mheshimiwa
rais,tumempata Mathewhivi
sasa anapelekwa kitalu 1”
“Kazi nzuri sana
Devotha.Huyo ndiye aliyekuwa
anatunyima usingizi na baada
ya kumpata sasa tunaweza
kupumua.Devotha hakikisha
unatumia vyema nafasi hii
kumfungua Olivia.Naendelea
kukumbusha tena kwamba
MathewMulumbi ni mtu hatari
hivyo kila aina ya tahadhari
inapaswa kuchukuliwa” Dr
Evans akamuelekeza Devotha
mambo kadhaa wakaagana
 
SIRI
PART 1: SEASON 4
MTUNZI: PATRICK CK
Wakati suala la kutekwa
kwa Dr Olivia Themba
likiendelea kuchukua sura
mpya baada ya baba yake Agrey
Themba naye kutekwa,katika
mpaka wa Namanga basi la
Mkombozi luxury linalofanya
safari zake kati ya Dar es salaam
na Nairobi lilifanikiwa kuvuka
mpaka na kuingia
Tanzania.Abiria walipewa
dakika chache za kujisaidia na
mmoja kati ya abiria
waliokuwamo ndani ya basi hilo
akashuka na kuwasha simu
yake akatafuta namba Fulani
akapiga
“Hallo” akasema mtu
aliyepokea simu upande wa pili
“Fahad nimekupigia
kukujulisha kwamba
tumekwisha vuka mpaka na
tayari tumeingia Tanzania”
akasema mtu yule aliyepiga
simu
“Karibuni sana
Tanzania.Tunawasubiri Dar es
salaam.Maandalizi yanaendelea
kwani kila kitu kinatakiwa
kumalizika usiku wa leo”
akasema Fahad na kukata simu
MPENZI MSOMAJI SIRI KUBWA
BADO IMETANDA KATIKA
SUALA LA KUTEKWA DR
OLIVIA NA BABA YAKE AGREY
THEMBA.USIKOSE SEHEMU
IJAYO………………
 
Ahsanteni Sana Shunie na Erick Emily.....Kwa sasa tunaweza sema hakuna arosto ni mwendo wa mperampera..Tukutane mchana kwenye Season 5 ndani ya Siri. Na ahsante sana Kulubule kwa kuanzisha huu uzi tutaendelea kushirikiana.
Be blexxed
 
Ahsanteni Sana Shunie na Erick Emily.....Kwa sasa tunaweza sema hakuna arosto ni mwendo wa mperampera..Tukutane mchana kwenye Season 5 ndani ya Siri. Na ahsante sana Kulubule kwa kuanzisha huu uzi tutaendelea kushirikiana.
Mchana umefika tyr mkuu....tunasubiria muendelezo tu.
 

Similar Discussions

Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…