Kudo
JF-Expert Member
- Nov 2, 2017
- 1,809
- 6,081
- Thread starter
- #301
“Noooo, Khajat!! Huyu aliyejulikana kama Joan alipiga kelele baada ya kuona Khajat ametuwa chini kama mzigo baada ya kuwa amerushwa juu. Wakati anataka kukimbilia pale alipokuwa ameangukia Khajat, Joan alishikwa na mshangao alipomwona mzee mmoja wa makamu akienda pale alipoangukia Khajat na kumchukua. Ilikuwa ni kitendo cha kasi na wepesi sana. Ilikuwa kama vile Mwewe amchukuavyo kifaranga. Yule mzee alitoweka kwenye majengo yaliyokuwa jirani. Kuona hivyo Joan akakimbilia sehemu ambayo mzee yule alikuwa ameingia na Khajat. Vilikuwa ni vitendo vya haraka, hivyo wakati Joan na yeyé akiwa anapotelea kwenye lile jengo ndipo gari la jeshi la FRPI lilipopiga breki kwa fujo eneo hilo. Wanajeshi kadhaa walishuka na kuanza kukimbilia alipokuwa ameelekea Joan.
“Shiiiiiiii! Yule mzee alisema mara baada ya Joan kutokezea kwenye chumba ambacho alikuwa amemlaza Khajat na kuanza kumpa huduma ya kwanza.
“Mzee Kasheba! Joan alisema
“Kaa hapo Joan, huyu anahitaji huduma ya haraka kama kweli tunataka aendelee kuishi! Alisema mzee Kasheba.
“Wako wanakuja huko nje! Joan alisema. Punde kidogo wakasikia mlango wa jengo hilo ukigongwa kwa nguvu.
“Oooooh shiiit! Mzee Kasheba alisema kwa mshituko.
* * *
“Wote wako hapa sipokuwa watu wawili tu ndiyo wanakosekana! Alisema askari huyu mwenye cheo cha juu jeshini huku jicho lake moja la kushoto likiwa na bandeji nyeupe iliyochafuka damu.
“Umeshajua ni nani wanakosekana, unajua inatakiwa tukamilishe kazi hii ndani ya masaa machache yajayo??!! Alisema Joseph Katanga. Ambaye alikuwa amechafuka sana, mavazi yake ya kijeshi yakiwa na matone na michirizi mingi ya damu.
“Kwa orodha iliyokuwa imetolewa mwezi wa nne siku chache kabla operesheni hii haijaanza wanaokosekana hapa ni Khajat na Joan! Alisema huyu mwanajeshi mwenye jicho lenye bandeji
“Watafutwe, hii ni sumu ambayo hapo baadae itatuathiri. Halafu Nataka kujua kwa nini wao hawakuwa na watu wa kuwachukua wakati mambo yalipoanza? Alisema Joseph Katanga. Wakati wakiongea hayo mara kaingia mtu mwingine aliyekuwa amevaa kiraia, wote wakampigia saluti. Hakujisumbua kuitikia saluti zao. Alikuwa jamaa mrefu, mzungu, mwenye kipara kinachong’aa. Aliwaangalia kwa muda bila kusema neno, halafu akatoa tabasamu la dhihaka. Hapo meno yake yaliyoungua na jino moja la dhahabu pembeni vilionekana.
“Nasikia kuna wasichana wawili wamekosekana, jitahidi watafutwe haraka. Nataka hili jambo limalizike ndani ya muda mfupi ujao ili tumiliki mambo kama tulivyopanga” Alisema huyo mtu mwenye meno machafu kwa ghadhabu.
“Tayari tumeshawaombea hifadhi Tanzania, hivyo tunangoja hao wawili wapatikane ili malengo yetu yatimie. Nawapa masaa kumi na mbili muwe mmekamilisha” Alisema huyo mzungu aliyejulikana kwa jina la KK na kutoka nje ya chumba kile huku nyuma akiwaacha Joseph Katanga na askari mwingine.
“Tumeua zaidi yawatu 200 usiku wa kuamkia leo, hebu hivi vitoto visituharibie kazi. Huyo Joan ni mjuu wa mzee Kasheba. Hebu nenda kaangalie, kama wako kwake muue yeyé halafu walete. Sitojali ukweli kuwa nirafiki yangu lakini kama hafuati nisemacho sheria hufuata mkondo wake. Fanya haraka nataka kufunga kazi hii haraka iwezekanvyo, halafu nianze kuangalia kwenye TV jinsi suala hili litakavyoongelewa! Katanga alisema huku macho yake yakionekana kuwa machovu na mekundu. Hii ni kutokana na kazi aliyokuwa ameifanya usiku kucha. Kazi ya kuongoza jeshi la FRPI kuwauwa watu wote wa jamii ya Hema na kuhakikisha hakuna mfugaji anabaki eneo hilo. Lilikuwa ni zoezi kubwa na gumu, waliua kadiri walivyoweza na kwa namna yoyote ile.
Yule askari alipiga saluti na kuondoka na vijana wengine kumi, walielekea nyumbani kwa Mzee Kasheba kuona kama wanaweza kuwapata Joan na Khajat.
*****************
Goma, DRC – 2017
Alhamisi, Saa 4:30 usiku
NDEGE maalum iliyokuwa imebeba makomandoo watano, ilikuwa ikipita juu ya anga la Goma - Congo DRC. Anga lililokuwa limefunikwa na mawingu mazito, meusi ambayo mra kwa mara yalikuwa yakimulikwa na mwanga wa radi. Ndege hiyo ilikuwa na jumla ya abiria sita pamoja na rubani, japo ilikuwa na uwezo wa kubeba abiria kumi na mmoja. Makomandoo wote walikuwa na vifaa vyao tayari kwa kuruka toka kwenye ndege hiyo hadi kwenye kambi maalum ya jeshi la serikali ambayo ilikuwa eneo hilo la Kivu Kaskazini.
Ilipofika eneo fulani, ndege hiyo maalum ilitoa mlio maalum, hivyo makomandoo wote wakajua walikuwa wamefika sehemu waliyotakiwa kudondoshwa. Kila mtu akaanza kuweka sawa begi lake wakati ndege hiyo ilipokaribia sehemu ambayo makomandoo hao wangedondoshwa kwa miavuli.
“Haya makamanda tuko eneo husika. Nitahesabu hadi tano, kisha nitafyatua mlango nanyi mtaruka. Mlango utakuwa wazi kwa sekunde thelathini halafu nitaufunga. Kila la kheri makamanda!” Kapteni Ambrose ambaye ndiye alikuwa rubani wa ndege hiyo alisema kwa sauti ya juu.
Makomandoo walikuwa kimya kila mmoja akiwa tayari kwa tukio.
“Moja…mbiliii…tatuuu…nnneeee… Tano twendeeee!”
Mlango ulifyatuka makomandoo wakajiachia hewani.
Ilitokea kama sadfa tu neno “shiiiiiit!” likasikika.
“Nini tena?” Kapteni Ambrose alihoji kwa hamaki baada ya kusikia komandoo mmoja akisema shiiiit!
“Limechanika, anyway ngoja niende. See you Kapteni!” alisema komandoo huyo aliyekuwa amesema shiit hapo awali, baada ya kubaini kuwa parachuti lake lilikuwa limechanika sehemu ya katikati
“High risk (ni hatari sana), ngoja kidogo!” Kapteni Ambrose alipiga kelele kumzuia yule komandoo asiruke. Lakini alikuwa ameshachelewa, yule komandoo alikuwa ameshajiachia angani!
* * *
Alhamisi, Saa 5:15 usiku
Komandoo wa kwanza alitua kwa kukimbia kwenye shamba kubwa la kahawa, zao ambalo ni maarufu eneo hilo. Dakika tano baadaye makomandoo wote isipokuwa mmoja tu walikuwa wameshafika sehemu waliyokuwa wakitarajiwa kutua. Hapo walipokelewa na wanajeshi watatu wenye vyeo vya juu wa jeshi. Makomandoo waliopokelewa ni Twaha Mchopa, Musa Buti, Mark Muga na Emily Otieno.
“Poleni kwa safari!” alisema ofisa mmoja aliyejitambulisha kwa jina la Meja Jean Francis Kabananga.
“Asante. Ila tuna wasiwasi na mwenzetu sijui amepatwa na madhila gani!
“Nilitaka kuuliza, maana tuliambiwa mko watano!? Meja Kabananga alisema
“Tulimsikia akilalamika akiwa angani, inaonyesha alipata changamoto ndogo, ila yeyé ni mhitimu bila shaka atafika tu,” Luteni Musa Buti mmoja wa wale makomandoo alisema. Yeye ndiye kiongozi wa wenzie kwenye misheni hii.
“Kwani hapatikani kwenye mawasiliano?” Meja Kabananga alihoji wakati wakielekea kwenye magari matatu ya kijeshi yaliyokuwa yamepaki eneo hilo.
“Dakika tatu baada ya kutua tulikuwa na mawasiliano naye. Akatuambia kwa sababu ya kuharibika parachuti lake amedondokea mbali na sehemu iliyokusudiwa. Na kama unavyoona hali hii ya upepo mkali na mvua hizi bila shaka unaweza kuelewa mtu akikutwa na ajali ya kuharibikiwa parachuti angani!” alisema Luteni Musa Buti.
“Okay, maadam ana ramani tutamngoja hapo kambini, ni kilomita kumi toka hapa. Twendeni maana mnasubiriwa kwa hamu kubwa sana na mkuu!” Meja Kabananga alisema kwa Kiswahili chake cha Kikongo. Mvua nzito ilikuwa bado ikiendelea kunyesha. Milio ya bunduki na risasi vilisikika kwa mbali, kitu kilichowaambia wale makomandoo kuwa walikuwa wameingia kwenye uwanja wa vita.
“Nasikia milio ya mashine huko! Mchoppa alisema
“Nakwambia hapa limeshakuwa swala la kawaida. Wakati wote ni wakati wa mapambano. Hali iliyofanya raia na askari wazoee tu sasa! Alisema afisa mmoja wa jeshi. Ardhi ilikuwa imelowa chepechepe!
Alhamisi, Saa 5:15 usiku.
Kilomita nane toka mahali ambapo Meja Kabananga alikuwa anawapokea wale makomandoo, huyu naye alikuwa amepokelewa kwa namna yake. Baada tu ya kutua chini, Komandoo Pablo Mahene alishtukia anamulikwa na mwanga mkali sana usoni. Wakati bado anahangaika namna ya kujitoa kwenye parachuti alishtukia anachomwa na kitu kama sindano shingoni. Fahamu zikamtoka.
“Ndiyo mkuu, kama tulivyotarajia, aliangukia eneo lilelile,” alisema jamaa mmoja mrefu sana, mweusi sana, mwenye jicho moja bovu. Wakati huu walikuwa kwenye gari moja la jeshi lililokuwa likiendeshwa kwa kasi sana kama wako kwenye barabara ya lami.
“Vema, kazi nzuri! Sasa watajua kuwa Jose Katanga karudi. Watafidia muda wote ambao nilikuwa nje ya uwanja!” Ulisema upande mwingine kwenye redio ile ya mawasiliano.
“Haya ndiyo mambo tulikuwa tunayakosa bosi, huu msisimko umerejea tena!” Alisema yule jamaa mrefu, mweusi, mwenye jicho bovu.
“Mwiteni mzee Kasheba amuhoji huyo jamaa!” Joseph Katanga alisema
“Shiiiiiiii! Yule mzee alisema mara baada ya Joan kutokezea kwenye chumba ambacho alikuwa amemlaza Khajat na kuanza kumpa huduma ya kwanza.
“Mzee Kasheba! Joan alisema
“Kaa hapo Joan, huyu anahitaji huduma ya haraka kama kweli tunataka aendelee kuishi! Alisema mzee Kasheba.
“Wako wanakuja huko nje! Joan alisema. Punde kidogo wakasikia mlango wa jengo hilo ukigongwa kwa nguvu.
“Oooooh shiiit! Mzee Kasheba alisema kwa mshituko.
* * *
“Wote wako hapa sipokuwa watu wawili tu ndiyo wanakosekana! Alisema askari huyu mwenye cheo cha juu jeshini huku jicho lake moja la kushoto likiwa na bandeji nyeupe iliyochafuka damu.
“Umeshajua ni nani wanakosekana, unajua inatakiwa tukamilishe kazi hii ndani ya masaa machache yajayo??!! Alisema Joseph Katanga. Ambaye alikuwa amechafuka sana, mavazi yake ya kijeshi yakiwa na matone na michirizi mingi ya damu.
“Kwa orodha iliyokuwa imetolewa mwezi wa nne siku chache kabla operesheni hii haijaanza wanaokosekana hapa ni Khajat na Joan! Alisema huyu mwanajeshi mwenye jicho lenye bandeji
“Watafutwe, hii ni sumu ambayo hapo baadae itatuathiri. Halafu Nataka kujua kwa nini wao hawakuwa na watu wa kuwachukua wakati mambo yalipoanza? Alisema Joseph Katanga. Wakati wakiongea hayo mara kaingia mtu mwingine aliyekuwa amevaa kiraia, wote wakampigia saluti. Hakujisumbua kuitikia saluti zao. Alikuwa jamaa mrefu, mzungu, mwenye kipara kinachong’aa. Aliwaangalia kwa muda bila kusema neno, halafu akatoa tabasamu la dhihaka. Hapo meno yake yaliyoungua na jino moja la dhahabu pembeni vilionekana.
“Nasikia kuna wasichana wawili wamekosekana, jitahidi watafutwe haraka. Nataka hili jambo limalizike ndani ya muda mfupi ujao ili tumiliki mambo kama tulivyopanga” Alisema huyo mtu mwenye meno machafu kwa ghadhabu.
“Tayari tumeshawaombea hifadhi Tanzania, hivyo tunangoja hao wawili wapatikane ili malengo yetu yatimie. Nawapa masaa kumi na mbili muwe mmekamilisha” Alisema huyo mzungu aliyejulikana kwa jina la KK na kutoka nje ya chumba kile huku nyuma akiwaacha Joseph Katanga na askari mwingine.
“Tumeua zaidi yawatu 200 usiku wa kuamkia leo, hebu hivi vitoto visituharibie kazi. Huyo Joan ni mjuu wa mzee Kasheba. Hebu nenda kaangalie, kama wako kwake muue yeyé halafu walete. Sitojali ukweli kuwa nirafiki yangu lakini kama hafuati nisemacho sheria hufuata mkondo wake. Fanya haraka nataka kufunga kazi hii haraka iwezekanvyo, halafu nianze kuangalia kwenye TV jinsi suala hili litakavyoongelewa! Katanga alisema huku macho yake yakionekana kuwa machovu na mekundu. Hii ni kutokana na kazi aliyokuwa ameifanya usiku kucha. Kazi ya kuongoza jeshi la FRPI kuwauwa watu wote wa jamii ya Hema na kuhakikisha hakuna mfugaji anabaki eneo hilo. Lilikuwa ni zoezi kubwa na gumu, waliua kadiri walivyoweza na kwa namna yoyote ile.
Yule askari alipiga saluti na kuondoka na vijana wengine kumi, walielekea nyumbani kwa Mzee Kasheba kuona kama wanaweza kuwapata Joan na Khajat.
*****************
Goma, DRC – 2017
Alhamisi, Saa 4:30 usiku
NDEGE maalum iliyokuwa imebeba makomandoo watano, ilikuwa ikipita juu ya anga la Goma - Congo DRC. Anga lililokuwa limefunikwa na mawingu mazito, meusi ambayo mra kwa mara yalikuwa yakimulikwa na mwanga wa radi. Ndege hiyo ilikuwa na jumla ya abiria sita pamoja na rubani, japo ilikuwa na uwezo wa kubeba abiria kumi na mmoja. Makomandoo wote walikuwa na vifaa vyao tayari kwa kuruka toka kwenye ndege hiyo hadi kwenye kambi maalum ya jeshi la serikali ambayo ilikuwa eneo hilo la Kivu Kaskazini.
Ilipofika eneo fulani, ndege hiyo maalum ilitoa mlio maalum, hivyo makomandoo wote wakajua walikuwa wamefika sehemu waliyotakiwa kudondoshwa. Kila mtu akaanza kuweka sawa begi lake wakati ndege hiyo ilipokaribia sehemu ambayo makomandoo hao wangedondoshwa kwa miavuli.
“Haya makamanda tuko eneo husika. Nitahesabu hadi tano, kisha nitafyatua mlango nanyi mtaruka. Mlango utakuwa wazi kwa sekunde thelathini halafu nitaufunga. Kila la kheri makamanda!” Kapteni Ambrose ambaye ndiye alikuwa rubani wa ndege hiyo alisema kwa sauti ya juu.
Makomandoo walikuwa kimya kila mmoja akiwa tayari kwa tukio.
“Moja…mbiliii…tatuuu…nnneeee… Tano twendeeee!”
Mlango ulifyatuka makomandoo wakajiachia hewani.
Ilitokea kama sadfa tu neno “shiiiiiit!” likasikika.
“Nini tena?” Kapteni Ambrose alihoji kwa hamaki baada ya kusikia komandoo mmoja akisema shiiiit!
“Limechanika, anyway ngoja niende. See you Kapteni!” alisema komandoo huyo aliyekuwa amesema shiit hapo awali, baada ya kubaini kuwa parachuti lake lilikuwa limechanika sehemu ya katikati
“High risk (ni hatari sana), ngoja kidogo!” Kapteni Ambrose alipiga kelele kumzuia yule komandoo asiruke. Lakini alikuwa ameshachelewa, yule komandoo alikuwa ameshajiachia angani!
* * *
Alhamisi, Saa 5:15 usiku
Komandoo wa kwanza alitua kwa kukimbia kwenye shamba kubwa la kahawa, zao ambalo ni maarufu eneo hilo. Dakika tano baadaye makomandoo wote isipokuwa mmoja tu walikuwa wameshafika sehemu waliyokuwa wakitarajiwa kutua. Hapo walipokelewa na wanajeshi watatu wenye vyeo vya juu wa jeshi. Makomandoo waliopokelewa ni Twaha Mchopa, Musa Buti, Mark Muga na Emily Otieno.
“Poleni kwa safari!” alisema ofisa mmoja aliyejitambulisha kwa jina la Meja Jean Francis Kabananga.
“Asante. Ila tuna wasiwasi na mwenzetu sijui amepatwa na madhila gani!
“Nilitaka kuuliza, maana tuliambiwa mko watano!? Meja Kabananga alisema
“Tulimsikia akilalamika akiwa angani, inaonyesha alipata changamoto ndogo, ila yeyé ni mhitimu bila shaka atafika tu,” Luteni Musa Buti mmoja wa wale makomandoo alisema. Yeye ndiye kiongozi wa wenzie kwenye misheni hii.
“Kwani hapatikani kwenye mawasiliano?” Meja Kabananga alihoji wakati wakielekea kwenye magari matatu ya kijeshi yaliyokuwa yamepaki eneo hilo.
“Dakika tatu baada ya kutua tulikuwa na mawasiliano naye. Akatuambia kwa sababu ya kuharibika parachuti lake amedondokea mbali na sehemu iliyokusudiwa. Na kama unavyoona hali hii ya upepo mkali na mvua hizi bila shaka unaweza kuelewa mtu akikutwa na ajali ya kuharibikiwa parachuti angani!” alisema Luteni Musa Buti.
“Okay, maadam ana ramani tutamngoja hapo kambini, ni kilomita kumi toka hapa. Twendeni maana mnasubiriwa kwa hamu kubwa sana na mkuu!” Meja Kabananga alisema kwa Kiswahili chake cha Kikongo. Mvua nzito ilikuwa bado ikiendelea kunyesha. Milio ya bunduki na risasi vilisikika kwa mbali, kitu kilichowaambia wale makomandoo kuwa walikuwa wameingia kwenye uwanja wa vita.
“Nasikia milio ya mashine huko! Mchoppa alisema
“Nakwambia hapa limeshakuwa swala la kawaida. Wakati wote ni wakati wa mapambano. Hali iliyofanya raia na askari wazoee tu sasa! Alisema afisa mmoja wa jeshi. Ardhi ilikuwa imelowa chepechepe!
Alhamisi, Saa 5:15 usiku.
Kilomita nane toka mahali ambapo Meja Kabananga alikuwa anawapokea wale makomandoo, huyu naye alikuwa amepokelewa kwa namna yake. Baada tu ya kutua chini, Komandoo Pablo Mahene alishtukia anamulikwa na mwanga mkali sana usoni. Wakati bado anahangaika namna ya kujitoa kwenye parachuti alishtukia anachomwa na kitu kama sindano shingoni. Fahamu zikamtoka.
“Ndiyo mkuu, kama tulivyotarajia, aliangukia eneo lilelile,” alisema jamaa mmoja mrefu sana, mweusi sana, mwenye jicho moja bovu. Wakati huu walikuwa kwenye gari moja la jeshi lililokuwa likiendeshwa kwa kasi sana kama wako kwenye barabara ya lami.
“Vema, kazi nzuri! Sasa watajua kuwa Jose Katanga karudi. Watafidia muda wote ambao nilikuwa nje ya uwanja!” Ulisema upande mwingine kwenye redio ile ya mawasiliano.
“Haya ndiyo mambo tulikuwa tunayakosa bosi, huu msisimko umerejea tena!” Alisema yule jamaa mrefu, mweusi, mwenye jicho bovu.
“Mwiteni mzee Kasheba amuhoji huyo jamaa!” Joseph Katanga alisema