mapengo junior
JF-Expert Member
- Jun 28, 2011
- 1,135
- 276
- Thread starter
- #41
SIMULIZI..... PENZI CHUNGU
MWANDISHI.. HALFANI SUDY
SEHEMU YA 28
Hamadi! Kumbe alikuwa Mhudumu wa Guest ile.
Mhudumu yule wa kiume wa nyumba ile ya kulala wageni aliingia kwa kasi sana, akiwa na gazeti la Dumizi mkononi. Sasa alikuwa anatazamana na Suto uso kwa uso. Macho ya Suto yalitua katika lile gazeti. Akajua kuna hatari!
"Bila shaka ni Suto Sutani"
Mhudumu alisema kwa dharau kidogo. Suto aliuficha kwa nyuma mkono wake wa kushoto, akificha kile kisu.
"Suto umefanya hapa ndio kichaka wauaji, ufanye mauaji huko na kuja kujificha hapa" Mhudumu alisema huku akibonyazabonyaza simu yake, bila shaka akitafuta namba fulani za kupiga.
Suto alijua licha ya kuvaa kofia na miwani lakini yule Mhudumu alikuwa ameshamgundua. Akamwangalia yule mhudumu huku akisikitika, Akijua Mhudumu kajiongeza mwenyewe kwenye orodha isiyomhusu, orodha ya kifo ! Suto hakujibu, Suto alitenda.
Kwa kasi ya haraka aliutoa ule mkono wenye kisu kule nyuma, na kwa kasi ileile na nguvu zake zote alididimiza kile kisu katika tumbo pana la yule Mhudumu, Mhudumu alishikwa na mshangao sambamba na maumivu, hakutegemea kama Suto ana kisu, hakutegemea kama Suto atafanya kitendo kama kile kwa muda ule na kwa kasi ile. Mhudumu alishikilia tumbo lake lililobaki na jeraha baya sana. Mhudumu yule alikufa akiwa anashangaa uwezo wa Suto katika uuaji.
Suto Sutani aliona pale siyo sehemu salama tena kwake. Alichukua begi lake dogo la visu, alipita mlango wa nyuma wa nyumba ile ya kulala wageni na kutokomea. Akiuacha ndani mwili usio na roho wa Mhudumu yule mbea.
***************
Inspekta Jasmine alikuwa ofisini kwake ndani ya makao makuu ya Polisi, Posta. Mara simu ya mezani iliita.
"Hallo Afande"
"Hallo Afande"
"Yametokea mauaji Gongo la mboto"
" Saa ngapi?"Inspekta Jasmine aliuliza kwa fadhaha.
" Kama masaa matatu yaliyopita"
"Naelekea huko, ramani sahihi ya nyumba yalikofanyika mauaji utanipa njiani"
"Sawa Afande"
Simu ikakatwa.
Inspekta Jasmine alichukua gari na askari watano, walielekea Gongo la mboto.
Waliwasiri Gongo la mboto, na kwa msaada wa yule askari aliyekuwa anakaa jirani na ile Guest, walifika hadi katika nyumba ya wageni yalipotokea mauaji. Nyumba aliyokuwepo Suto Sutani, adui namba moja wa Inspekta Jasmine masaa matatu yaliyopita. Walikuta kundi dogo la watu.
Inspekta Jasmine na wale askari watano waliingia moja kwa moja ndani ya nyumba ile ya kulala wageni. Walimkuta Mhudumu pale kaunta na yule askari aliyepiga simu. Askari aliyeamini kuwa muuaji kwa kadri ya sifa alizopewa na Mhudumu ni Suto, na kuamua kumpigia moja kwa moja Inspekta Jasmine.
"Habari yako"
"Nzuri Afande"
"Meneja yuko wapi"
"Hapana Meneja hapa nipo mimi tu"
"Hebu nielezee mazingira ya tukio"
"Tuliamka asubuhi vizuri na Mhudumu mwenzangu wa kiume anayeitwa Jerry, baada ya kufanya usafi wa nje, Jerry aliniaga kuwa anaenda kununua gazeti, baada ya muda mfupi alirudi anakimbia na kuelekea uwani, mimi nilidhani kashikwa na tumbo la kuhara, kwahiyo anakimbilia chooni. Yalipita masaa kadhaa Jerry sikumuona. Ilivyofika saa nne asubuhi, muda wa wateja kukabidhi vyumba. Nikaanza kupita chumba kimoja baada ya kingine. Nilipofika chumba namba nane niliukuta mlango ukiwa wazi, nilipoingia ndani, ndipo nilikutana na maiti ya Jery sakafuni......Jerry aliuwawa kwa kuchomwa kisuuu oooooh masikini Jery" Mhudumu alisimulia kwa uchungu na simanzi, huku machozi yakimtiririka. Inspekta Jasmine hakujari kabisa kilio cha Mhudumu yule. Pamoja na kilio chake aliendelea kumhoji.
"Uliandika jina la mteja aliyepanga katika chumba namba nane?"
"Ndio afande"
"Anaitwa nani?"
Mhudumu akipekua kitabu harakaharaka.
"Ana...anaitwa Susa Zamani"
Hii Simulizi ndio kwanza inaanza.....
ITAENDELEA KESHO
MWANDISHI.. HALFANI SUDY
SEHEMU YA 28
Hamadi! Kumbe alikuwa Mhudumu wa Guest ile.
Mhudumu yule wa kiume wa nyumba ile ya kulala wageni aliingia kwa kasi sana, akiwa na gazeti la Dumizi mkononi. Sasa alikuwa anatazamana na Suto uso kwa uso. Macho ya Suto yalitua katika lile gazeti. Akajua kuna hatari!
"Bila shaka ni Suto Sutani"
Mhudumu alisema kwa dharau kidogo. Suto aliuficha kwa nyuma mkono wake wa kushoto, akificha kile kisu.
"Suto umefanya hapa ndio kichaka wauaji, ufanye mauaji huko na kuja kujificha hapa" Mhudumu alisema huku akibonyazabonyaza simu yake, bila shaka akitafuta namba fulani za kupiga.
Suto alijua licha ya kuvaa kofia na miwani lakini yule Mhudumu alikuwa ameshamgundua. Akamwangalia yule mhudumu huku akisikitika, Akijua Mhudumu kajiongeza mwenyewe kwenye orodha isiyomhusu, orodha ya kifo ! Suto hakujibu, Suto alitenda.
Kwa kasi ya haraka aliutoa ule mkono wenye kisu kule nyuma, na kwa kasi ileile na nguvu zake zote alididimiza kile kisu katika tumbo pana la yule Mhudumu, Mhudumu alishikwa na mshangao sambamba na maumivu, hakutegemea kama Suto ana kisu, hakutegemea kama Suto atafanya kitendo kama kile kwa muda ule na kwa kasi ile. Mhudumu alishikilia tumbo lake lililobaki na jeraha baya sana. Mhudumu yule alikufa akiwa anashangaa uwezo wa Suto katika uuaji.
Suto Sutani aliona pale siyo sehemu salama tena kwake. Alichukua begi lake dogo la visu, alipita mlango wa nyuma wa nyumba ile ya kulala wageni na kutokomea. Akiuacha ndani mwili usio na roho wa Mhudumu yule mbea.
***************
Inspekta Jasmine alikuwa ofisini kwake ndani ya makao makuu ya Polisi, Posta. Mara simu ya mezani iliita.
"Hallo Afande"
"Hallo Afande"
"Yametokea mauaji Gongo la mboto"
" Saa ngapi?"Inspekta Jasmine aliuliza kwa fadhaha.
" Kama masaa matatu yaliyopita"
"Naelekea huko, ramani sahihi ya nyumba yalikofanyika mauaji utanipa njiani"
"Sawa Afande"
Simu ikakatwa.
Inspekta Jasmine alichukua gari na askari watano, walielekea Gongo la mboto.
Waliwasiri Gongo la mboto, na kwa msaada wa yule askari aliyekuwa anakaa jirani na ile Guest, walifika hadi katika nyumba ya wageni yalipotokea mauaji. Nyumba aliyokuwepo Suto Sutani, adui namba moja wa Inspekta Jasmine masaa matatu yaliyopita. Walikuta kundi dogo la watu.
Inspekta Jasmine na wale askari watano waliingia moja kwa moja ndani ya nyumba ile ya kulala wageni. Walimkuta Mhudumu pale kaunta na yule askari aliyepiga simu. Askari aliyeamini kuwa muuaji kwa kadri ya sifa alizopewa na Mhudumu ni Suto, na kuamua kumpigia moja kwa moja Inspekta Jasmine.
"Habari yako"
"Nzuri Afande"
"Meneja yuko wapi"
"Hapana Meneja hapa nipo mimi tu"
"Hebu nielezee mazingira ya tukio"
"Tuliamka asubuhi vizuri na Mhudumu mwenzangu wa kiume anayeitwa Jerry, baada ya kufanya usafi wa nje, Jerry aliniaga kuwa anaenda kununua gazeti, baada ya muda mfupi alirudi anakimbia na kuelekea uwani, mimi nilidhani kashikwa na tumbo la kuhara, kwahiyo anakimbilia chooni. Yalipita masaa kadhaa Jerry sikumuona. Ilivyofika saa nne asubuhi, muda wa wateja kukabidhi vyumba. Nikaanza kupita chumba kimoja baada ya kingine. Nilipofika chumba namba nane niliukuta mlango ukiwa wazi, nilipoingia ndani, ndipo nilikutana na maiti ya Jery sakafuni......Jerry aliuwawa kwa kuchomwa kisuuu oooooh masikini Jery" Mhudumu alisimulia kwa uchungu na simanzi, huku machozi yakimtiririka. Inspekta Jasmine hakujari kabisa kilio cha Mhudumu yule. Pamoja na kilio chake aliendelea kumhoji.
"Uliandika jina la mteja aliyepanga katika chumba namba nane?"
"Ndio afande"
"Anaitwa nani?"
Mhudumu akipekua kitabu harakaharaka.
"Ana...anaitwa Susa Zamani"
Hii Simulizi ndio kwanza inaanza.....
ITAENDELEA KESHO