mapengo junior
JF-Expert Member
- Jun 28, 2011
- 1,135
- 276
- Thread starter
- #21
SIMULIZI... PENZI CHUNGU - SIMULIZI... PENZI CHUNGU
MWANDISHI.. HALFANI SUDY
SEHEMU YA 17
Inspekta Jasmine tangu alipopewa tu jukumu la kupeleleza kesi hii, hakuwa amepiga hatua yoyote.
Alishawahoji mama Suto, Suto na majirani wawili. Alijumuisha maelezo yao na kujikuta yupo palepale.
Pamoja ya kuwa majirani walikuwa hawampendi Suto lakini hawakusita kutaja sifa nzuri za Suto, mbele ya inspekta Jasmine.
Jumatatu ya leo ilimkuta Inspekta Jasmine mlangoni kwa jirani wa tatu wakina Suto.
Alikuwa anaitwa mama Siyawezi.
"Habari mama" inspekta Jasmine alisalimia.
"Nzuri mwanangu" mama Siyawezi alijibu huku akimwangalia Inspekta Jasmine kwa macho ya udadi.
"Mimi ni afisa wa jeshi la Polisi" Inspekta Jasmine alisema huku akionyesha kitambulisho.
"Nimefanya nini tena jamani ?" Mama Siyawezi alisema kwa sauti ya woga.
"Usiwe na wasiwasi mama, kuna vitu vya kawaida tu nataka kukuliza"
"Mwenzenu mimi nikisikia Polisi tu roho inaniruka, nawaogopa sana Polisi"
"Walikufanya nini Polisi hadi uwaogope kiasi hicho ?"
"Wala hawajanifanya kitu, mimi nikiona mavazi yenu tu yale yaani nachanganyikiwa, bora wewe hujayavaa, ningekukimbia hapa" Mama Siyawezi alisema huku akicheka.
"Hahaha tuendelee na kilichonileta mama"
"Sawa, nakusikiliza " Mama Siyawezi alitulia sasa.
"Unaitwa nani mama?"
"Jina nililopewa nyumbani ni Asha Msigeze, ila sahivi wananiita Mama Siyawezi, kwa kuwa nini mtoto wa kike anaitwa Siyawezi, lakini yupo Kisiju kwa bibi yake"
"Sawa mama, ulikuwa unamfahamu Suto?"
"Nisimfahamu Suto mimi, kazaliwa hapa hapa, kakulia hapa hapa, na kaulia hapa hapa!"
"Kamuua nani Suto?"
"Yaani, we askari halafu huna habari, Suto kawaua vijana watatu hapa, mwezi uliopita. Wawili kwa kisu, na mmoja kwa panga. Yule wa panga alikatwa vibaya sana. Ile picha inajirudia Kila mara nikilala, kumbe Suto alikuwa katili sana yule"
"Una hakika Suto aliwauwa wale vijana wale?"
"Nakubali sikusoma, ila picha nazielewa vizuri sana, ukiangalia mazingira tu ya siku ile, unapata jibu....Suto anahusika katika mauaji....au anawajua vizuri sana wauaji !" Mama Siyawezi alipigia msumari wa mwisho katika kaburi la Suto.
"Sawa mama Siyawezi, hivi ni nani aliyekuwa rafiki mkubwa wa Suto?"
"Mama yake" mama Siyawezi alijibu bila kufikiria.
"Hakuwa na rafiki mwengine?"
"Rafiki wa Suto ni mama yake mzazi......aaaaah lakini juzijuzi alipata rafiki mpya wa kiume"
"Ni nani?"
"Kwa jina sijui, lakini ukienda kumuuliza mama Suto atakwambia."
"Nashukuru mama, ahsante kwa ushirikiano wako"
Inspekta Jasmine alitoka nyumbani kwa mama Siyawezi na kuelekea kwa mama Suto. Nia ni kumjua huyo rafiki mpya wa Suto.
Angejua kitakachotokea, ni bora asingetoka ndani ya nyumba ile.
Alivyotoka Inspekta Jasmine, mgeni mpya wa kiume aligonga hodi katika nyumba ya mama Siyawezi, Mama Siyawezi alidhani Inspekta Jasmine amerudi tena. Alifungua mlango kwa haraka, kumbe alikuwa anaharakia kifo. Alipofungua tu mlango, alitazamana na kisu !
Itaendelea......badae
MWANDISHI.. HALFANI SUDY
SEHEMU YA 17
Inspekta Jasmine tangu alipopewa tu jukumu la kupeleleza kesi hii, hakuwa amepiga hatua yoyote.
Alishawahoji mama Suto, Suto na majirani wawili. Alijumuisha maelezo yao na kujikuta yupo palepale.
Pamoja ya kuwa majirani walikuwa hawampendi Suto lakini hawakusita kutaja sifa nzuri za Suto, mbele ya inspekta Jasmine.
Jumatatu ya leo ilimkuta Inspekta Jasmine mlangoni kwa jirani wa tatu wakina Suto.
Alikuwa anaitwa mama Siyawezi.
"Habari mama" inspekta Jasmine alisalimia.
"Nzuri mwanangu" mama Siyawezi alijibu huku akimwangalia Inspekta Jasmine kwa macho ya udadi.
"Mimi ni afisa wa jeshi la Polisi" Inspekta Jasmine alisema huku akionyesha kitambulisho.
"Nimefanya nini tena jamani ?" Mama Siyawezi alisema kwa sauti ya woga.
"Usiwe na wasiwasi mama, kuna vitu vya kawaida tu nataka kukuliza"
"Mwenzenu mimi nikisikia Polisi tu roho inaniruka, nawaogopa sana Polisi"
"Walikufanya nini Polisi hadi uwaogope kiasi hicho ?"
"Wala hawajanifanya kitu, mimi nikiona mavazi yenu tu yale yaani nachanganyikiwa, bora wewe hujayavaa, ningekukimbia hapa" Mama Siyawezi alisema huku akicheka.
"Hahaha tuendelee na kilichonileta mama"
"Sawa, nakusikiliza " Mama Siyawezi alitulia sasa.
"Unaitwa nani mama?"
"Jina nililopewa nyumbani ni Asha Msigeze, ila sahivi wananiita Mama Siyawezi, kwa kuwa nini mtoto wa kike anaitwa Siyawezi, lakini yupo Kisiju kwa bibi yake"
"Sawa mama, ulikuwa unamfahamu Suto?"
"Nisimfahamu Suto mimi, kazaliwa hapa hapa, kakulia hapa hapa, na kaulia hapa hapa!"
"Kamuua nani Suto?"
"Yaani, we askari halafu huna habari, Suto kawaua vijana watatu hapa, mwezi uliopita. Wawili kwa kisu, na mmoja kwa panga. Yule wa panga alikatwa vibaya sana. Ile picha inajirudia Kila mara nikilala, kumbe Suto alikuwa katili sana yule"
"Una hakika Suto aliwauwa wale vijana wale?"
"Nakubali sikusoma, ila picha nazielewa vizuri sana, ukiangalia mazingira tu ya siku ile, unapata jibu....Suto anahusika katika mauaji....au anawajua vizuri sana wauaji !" Mama Siyawezi alipigia msumari wa mwisho katika kaburi la Suto.
"Sawa mama Siyawezi, hivi ni nani aliyekuwa rafiki mkubwa wa Suto?"
"Mama yake" mama Siyawezi alijibu bila kufikiria.
"Hakuwa na rafiki mwengine?"
"Rafiki wa Suto ni mama yake mzazi......aaaaah lakini juzijuzi alipata rafiki mpya wa kiume"
"Ni nani?"
"Kwa jina sijui, lakini ukienda kumuuliza mama Suto atakwambia."
"Nashukuru mama, ahsante kwa ushirikiano wako"
Inspekta Jasmine alitoka nyumbani kwa mama Siyawezi na kuelekea kwa mama Suto. Nia ni kumjua huyo rafiki mpya wa Suto.
Angejua kitakachotokea, ni bora asingetoka ndani ya nyumba ile.
Alivyotoka Inspekta Jasmine, mgeni mpya wa kiume aligonga hodi katika nyumba ya mama Siyawezi, Mama Siyawezi alidhani Inspekta Jasmine amerudi tena. Alifungua mlango kwa haraka, kumbe alikuwa anaharakia kifo. Alipofungua tu mlango, alitazamana na kisu !
Itaendelea......badae