SIMULIZI; PENZI CHUNGU
MWANDISHI; HALFANI SUDY
Cha ajabu na kushangaza wote watatu walikuwa wanakoroma. Mikoromo mikali sana. Kila mmoja alikuwa anakoroma huku anatabasamu. Alikuwa anajua kuwa anamdanganya mwenzake. Nani wa kumdanganya mwenzie kati ya watu wale watatu. Wote walikuwa mashujaa katika nyanja yake.
Mikoromo bandia ya watu wale ilivuka mipaka. Sauti za mkoromo zilipita mlangoni na kutokea jikoni. Pale alikolala Suto Sutani awali. Sauti hazikukomea hapo, zilisafiri na kutoka nje ya kibanda kile. Kule nje sauti ilisafiri kwa kasi zaidi ikisaidiwa na upepo na kufika katika sikio la mnyama mkali zaidi porini, Simba!
Simba yule jike nae hakuidharau sauti ile ya mkoromo, alianza kuifuata.
Ndio! Sauti ilimfikisha mpaka nje ya kibanda walicholala kina Mzee Mapengo.
Alipofika pale nje Simba alitulia, ghafla hakuisikia tena ile mikoromo, ilikata ghafla. Simba alikaa pale nje kama dakika mbili, hali ilikuwa shwari. Simba alikizunguka kile kibanda mara tatu, alivyomaliza akatulia katikati ya mlango. Akatoa muungurumo mdogo na kuamua kuingia ndani. Mlango ulikuwa mkubwa na uko wazi, hakukuwa na zuio lolote, aliingia ndani kwa madaha makubwa sana. Alipofika pale jikoni alisita kidogo, akabadiri mtindo, sasa alikaa kitayaritayari kupambana na chochote mbele yake. Aliunguruma muungurumo mkali, akiwa katikati ya mlango wa chumba walicholala Daniel Mwaseba, Suto Sutani na Mzee Mapengo.
Alipofika pale mlangoni, macho ya Simba yaliangalia haraka haraka na kuwaona maadui zake watatu..
JIPATIE KITABU CHA PENZI CHUNGU KWA SH 8000 TU...PIGA SIMU NO 0687028898 KAMA UNAKIHITAJI.