SLAVE SEX(mtumwa wa ngono).......(19)
MTUNZI....EMMANUEL F. KWAY
Contact...+255718 862176
AGE....(18+)
ILIPOISHIA.
“Ndio”
Gloria akarudi na kubadili nguo,ambapo alivaa dera
na kitambaa kichwani wakaongozana mpaka
kanisani,Mchungaji Patrick alikuwa teyari yupo
kanisani anahubiri neno la Mungu,wakaingia mtu
na mke wake na kuketi viti vya nyuma kutokana
na umati wa watu uliofurika siku hiyo ya Jumapili.
SONGA NAYO.
Siku hiyo ilikuwa furaha kubwa sana kwa Nickson
Shayo,kufanikiwa kumpeleka mke wake Gloria
kanisani ili tu akasikilize neno la Mungu,Mchungaji
Patrick mtumishi wa Mungu alikuwa mbele ya
madhabau anahubiri neno la kiroho,aliongea
mambo mengi sana hususani swala zima la ndoa.
“Bwana apewe sifa”
Mchungaji Patrick alisema na waumini wakaitikia
kwa sauti “AMEEEEN” kisha kuendelea,
“Mathayo mtakatifu sura ya kwanza mstari wa kumi
na nane; kuzaliwa kwake yesu kristo kulikuwa
hivi.Mariam Mama yake alipokuwa ameposwa na
Yusufu,kabla hawajakaribiana alionekana ana
mimba kwa uwezo wa Roho mtakatifu,Halel
uyaa,Bwana yesu asifiwe sana”
“Ameeeeen”
Waumini waliitikia na Mchungaji Patrick akaanza
kuelezea maana ya neno hilo la Mungu.
Mchungaji Patrick alikuwa ni mwenye jina kubwa
sana alikuwa ni kipenzi cha watu, sababu ya roho
yake nzuri ya kuwasaidia wasiokuwa
navyo,aliwasaidia maskini na kila baada ya mwisho
wa mwisho alikwenda mahospitali kutoa misaada
na kupita vituo vya watoto yatima,jina lake
likavuma zaidi na hata alipoomba msaada nje ya
nchi kuhusiana na pesa alipatiwa mara moja,
alikuwa akitembelea gari la kifahari aina ya
HAMMER III original, mbali na hapo alikuwa akiishi
katika nyumba kubwa ya kifahari aliyojengewa na
usharika.
Wanawake wajane walimpenda na kila walipomfuata
basi hawakulalamika tena,baada ya neno kuisha
alitembea mpaka ofisini kwake, huko aliketi na
mlango wake ukagongwa baada ya kuweka makalio
yake chini.
“Ingia”
Mchungaji Patrick alisema na hapo sura ya
mwanamke mnene kiasi aliyevalia dera zito
kuingia.
“Mama Isack karibu,bwana asifiwe”
“Hakuna cha bwana asifiwe hapa,juzi nimekuja
hapa nikakuta foleni au na wengine unawafanya
kama unavyonifanya?”
Mama Isack alijibu kwa swali, huku akimsogelea
Mchungaji Patrick karibu.
“Lak.....”
Kabla ya kumalizia neno lake akashtukia Mama
Isack kashamvaa mdomoni na kutoa ulimi wake,
wakaanza kulana denda,mbali na kazi ya utumishi
wa Mungu, Mchungaji Patrick alikuwa anapenda
ngono kupita kiasi,aliwalaghai wanawake wajane
kisha kufanya nao uzinzi,hakuna mtu aliyeweza
kujua siri hiyo kuwa mchungaji anayeaminika
karibia jiji zima anajiusisha na mambo
yasiyompendeza Mungu,hakuna mtu hata mmoja
angekuamini endapo ungemshtaki, kutokana na
sura ya upole wake.Mchungaji Patrick alikuwa ni
simba aliyejifika ngozi ya kondoo.
“Umefunga mlango lakini?”
“Achana naooo bwanaaa pati”
“Hapana ngoja nikafunge kwanza”
Mchungaji Patrick bila haya, akatembea mpaka
mlangoni na kufunga mlango kwa funguo,akafungu
a redio na kuweka kanda aliyojirekodi anaomba na
kuimba ili atakaye pita ajue yu kwenye maombi
kumbe anafanya tendo baya la umalaya.
Mchungaji Patrick alimsogeza Mama Isack mpaka
karibu kabisa na meza na kumpandisha juu yake,
hapo alimnyonya mama huyu Shingo yake huku
mkono wake kupita chini kabisa ya pango akiwa
kama anatafuta kitu,
dera likapitishwa shingoni likatolewa na kutupwa
chini Mama Isack akabakiwa na chupi,waliendelea
kulana denda mfululizo na Mchungaji Patrick
akatoa fimbo ya Musa nje, ikiwa imesimama Wima,
hapo hapo akamuweka Mama huyu sawa mikono
yake akaizungusha kiunoni mwake akawa
anamvuta karibu yake zaidi,Mambo yakawa tayari
mchungaji alishika miguu ya MAMA huyu Mjane na
kuanza kumsulubu vya kutosha.
“Ahhhssss Mchungaji...Mhhhh aaaah haaa...po
haaa...po mmmh aaaah mhhhhhh”
Hizo ndizo kelele za puani alizokuwa anatoa Mama
Isack akiwa sayari nyingine, macho yake
anayazungusha huku na kule anakatika juu ya
Meza,alikishika kichwa cha Mchungaji Patrick
Vizuri kabisa huku akiwa anamng’ang’nia
shingoni,akaachia ukulele wa nguvu.
“Baba ni katika jina la Yesu,naomba umfungue
huyu Mama kuanzia leo,na ujidhihirishe leo kuwa
wewe ndiye simba wa Yuda.....”
Hayo ndiyo maneno yaliyokuwa yakisikika kutokea
ndani ya chumba cha Mchungaji Patrick.Hakuna
hata mmoja aliyejua kuwa ilikuwa ni kanda na
Mchungaji Patrick alikuwa ofisini kwake ana fanya
mambo yasiyo staili endapo angekutwa na
waumini wake.
“Leo mchungaji atakuwa ameshukiwa na roho
mtakatifu”
Muumini mmoja alimuuliza mwenzake.
“Ni kweli,hawa ndiyo watu wa Mungu
bwana,Mchungaji Patrick ni mtu mzuri sana tangu
nimlete hapa mke wangu,aisee imekuwa miujiza
sana,hatimaye ananiheshimu yaani ikifika tu
Jumapili huyo mwenyewe ananihamsha,Kwa kweli
bwana apewe sifa”
“Amen”
Watu wengi walifurika nje ya mlango wa mchungaji
Patrick,hasa hasa wanawake wajane na wake za
watu,jambo hilo halikuwashtua watu sababu
walisema kuwa wanaenda kuombea waume zao
watulie na Mchungaji Patrick ndiye alikuwa
mwenye miujiza hiyo,
kuna wengine walidiriki hata kumuita Mesiya
wakijaribu kumfananisha na Mungu.
Katika kundi la watu waliokuwa nje wanasubiri
huduma ya Mchungaji Patrick alikuwepo Nickson
na Mke wake Gloria.Nickson alitaka kwenda
kumuonesha Mchungaji Patrick mke wake ili
waombewe na amuombee kiumbe kilichokuwa
tumboni mwa Gloria,alijisikia faraja sana kwenda
katika nyumba ya ibada na aliamini miujiza
ingetokea,
alishasikia kwa watu miujiza ya Mchungaji Patrick.
Ghafa mlango wa mchungaji ukafunguliwa
akatokeza Mama mweupe mnene akiwa amevalia
dera.
“Bwana Yesu asifiwe”
Mama Isack alisalimia.
“Ameeen”
Waumini waliokuwa nje wakaitikia kwa
pamoja,akaingia mwingine kuomba msaada wa
kiroho, msichana huyo naye alikaa kwa mchungaji
nusu saa lizima,ivyo ndivyo ilivyokuwa lakini
wakiingia jinsia ya kiume hata dakika kumi zilikuwa
haziishi.
Zamu ya Nickson na Gloria ikawa imefika
wakaingia na kufunga mlango.Macho ya mchungaji
Patrick yakatua juu ya uso mzuri mweupe wa
kung’ara ambao ulipakwa mafuta ya
kunukia,Mchungaji Patrick alipagawishwa na Uzuri
wa mke wa mtumishi wake Nickson.
“Bwana Yesu asifiwe mchungaji”
Nickson alisalimia na kumshtua Mchungaji Patrick
aliyekuwa ameduwaa.
“Ameen,Wewe ndiye Mr.Nickson,si ndo wewe?”
“Ndiye mimi baba Mchungaji”
“Bwana asifiwe sana”
“Amen mchungaji”
Hakuna kitu kingine zaidi alichofanya
Nickson,alimtambulisha Mke wake kwa mchungaji
Patrick wakapeana mikono,Nickson akazidi
kumshukuru mchungaji Patrick kisha baada ya
hapo wakafumba macho wakasali kwa pamoja.
Katikati ya maombi Mchungaji Patrick akafumbua
macho yake ili kutathmini uzuri wa Gloria,akawa
ana kazi ya kumkagua kuanzia juu mpaka chini,
tamaa ikamuingia ya kimwili,pepo baya la ngono
likaanza kufanya kazi yake,akazidi kurefusha
maombi ili azidi kumkagua Gloria zaidi na zaidi.
“Katika jina la Yesu mwanao mpendwa tunaomba
na kukushukuru AMEEEN”
“Ameen”
Mchungaji Patrick alimaliza na wote wakaitikia,Nick
son akahisi moyo wake umekuwa mweupe na
ameutua mzigo.Hakuelewa ni kitu gani kinaendelea
ndani ya mchungaji wake.
***
Maisha yalizidi kuendelea kama kawaida nyumbani
kwa Nickson huku mimba ya Gloria ikizidi kuwa
kubwa na tumbo lake kutokeza mbele,Nickson
alikuwa akisubiri kwa hamu sana siku ya
kujifungua kwa Mke wake,alikuwa akiomba ruksa
mara kwa mara ofisini ili awahi kwa mke wake,hilo
alikubaliwa.
Kwa ajili ya msaada zaidi Nickson akaamua
kumpigia Mama yake simu aliyekuwa mkoani
Kilimanjaro ili aweze kufika Dar es salaam mara
moja,na hiyo ndiyo ilikuwa mila na destuli.
Mama akawa ameingia siku ya Jumanne Nickson
baada ya kutoka ofisini akanyoosha mpaka Ubungo
Terminal kwenda kumpokea Mama, walivyoonana
wote walifurahi sana.
*****
Kila kilichoendelea nchini Tanzania Mr.Zuma
alipewa taarifa,Gloria aliwasiliana na Bwana Zuma
kisiri sana.
“Najifungua mwezi ujao,utakuja?”
Gloria aliuliza akiwa simuni.
“Nitakuja,kwanini nisije?”Mr.Zuma akajibu kwa
swali.
“Nitafurahi sana kukuona”
“Sio kuniona tu,nitakuja tutakaa kisha tuondoke
sote kuja Afrika Kusini”
“Nitafurahi mno”
“Sawa utaniambia hospitali utakayo fikia na kila
kitu”
“Ondoa shaka”
Gloria akakata simu.Ivyo ndivyo ilivyokuwa licha ya
kukaa na Nickson lakini hakuwa na mapenzi naye
hata kidogo,hakutaka kulionesha swala hilo wazi
wazi.
Alivyokuja Mama yake na Nickson akajifanya
kumchangamkia kumbe moyoni alichukia vibaya
sana.
“Subiri,hawa dawa yao ngoja aje Zuma,wataipata
freshi shenzi zao,nawaachia mtoto mimi nasepa
zangu”
Mambo hayo yalitiririka ubongoni mwa Gloria
akiwa mezani na Nickson pamoja na Mama yake
mkwe!
Hatimaye miezi tisa ikawadia, na siku za
Kujifungua kwa Gloria zikafika,Nickson hakutaka
mke wake apate shida, mara moja akamuwaisha
hospitali ya Aghakhan hata kabla hajajifungua
mtoto.Hakuacha kumuomba Mungu siku zote ili
mtoto wake wa kwanza azaliwe salama,Siku hiyo
yeye na Mama yake walisali na walimuweka Gloria
katika Mikono ya Mungu.
***
“Ng’aaaaaa ng’aaaaaa ng’aaaaaaaaaaa”
Ilikuwa ni sauti ya kichanga kutoka ndani ya
chumba ambacho wanaume hawaruhusiwi
kuingia,wakunga wakigongana vikumbo huku na
kule,usiku wa saa saba.
“Embu mwangalie mtoto wa kike au wa kiume?”
Mkunga alimuuliza mwenzake.
“Huyu wa kike na ana afya nzuri,hongera Mama
umejifungua mtoto wa kike”
“Ahs....ante”
Gloria alipatiwa mtoto wake akambeba, aliachia
tabasamu na kumnyonyesha hapo hapo.
Alijifungua salama salmin, tena bila operesheni ya
aina yoyote ile.
Asubuhi yake Gloria akaamishwa chumba kingine,
akapelekwa kwenye wodi la akina mama
waliojifungua.Nickson na Mama yake walikuwa
teyari wamefika hospitali.
Na Mr.Zuma alikuwepo Tanzania aliingia siku mbili
kabla,na ndiyo hapo Gloria alipompigia simu ili aje
kumshuhudia mtoto wake.
Naye mara moja akawasha gari ya kukodi,
akielekea hospitali ya aghakhani,akaulizia ilipo
nayeye akafika.Nickson,Mama Nickson na
Mr.Zuma wakafika chumba alicholazwa Gloria kwa
pamoja.
“Gloriaaaaaa,Real?”
Mr.Zuma aliruka kwa furaha mpaka kwenye kitanda
cha Gloria na kuanza kumpiga mabusu mengi
mfululizo,jambo hilo likashuhudiwa na Nickson
pamoja na Mama yake, wote wakabaki vinywa
wazi!
BILA KUSAHAU KWAMBA HADITHI HII INAPATIKANA
YOTE WATSAP NA INBOX KWA MALIPO YA TSHS
3000/- KWA MWEZI,mawasiliano namba +255718
862176
Sasa unaweza kusoma hadithi za mtunzi
kway@storyzakway
ITAENDELEA.