vinneboy
JF-Expert Member
- Aug 12, 2015
- 478
- 436
- Thread starter
- #81
SLAVE SEX(mtumwa wa ngono)……(15)
MTUNZI….EMMANUEL F. KWAY
Contact…+255718 862176
AGE….(18+)
ILIPOISHIA.
Hayo ndiyo maneno aliyoongea Pedeshee Kway
huku kioo cha gari kikipanda juu,hakutania alitoa
gari kwa kasi na kumuacha Gloria akiwa hospitalini
asijue wapi aelekee kwa sababu alikuwa bado
mgeni wa jiji la Afrika kusini.
SONGA NAYO.
Jambo lililokuwa limemtokea Gloria bado
hakuliamini kama lilikuwa ndoto au kweli,hata siku
moja hakuamini kuwa Pedeshee Kway angemgeuka
kiasi hicho na kumuacha kwasababu ya mimba
aliyokuwa nayo,ghafla akajiangalia tumboni na
kuchukizwa na mtoto aliyembeba,alimuona ndiye
aliyetia dosari katika maisha yake ya raha
mustarehe.Alitamani kitu kinachotokea kisiwe cha
ukweli bali ndoto ili ashtuke.Ni kweli alilishuhudia
Landcruiser V8 linatoka nje ya geti likikunja kona
na kutokomea, hapo ndipo aliposhtuka kama mtu
aliyetoka usingizini,aliweka mikono yake kichwani
na kujikuta akilengwa na machozi hofu
ilimtanda,hapo ndipo picha ya mume wake Nickson
ikamjia kichwani na kujiona jinsi gani alivyokuwa
mwanamke mpumbavu.
Gloria alijutia na kutamani siku zirudi nyuma lakini
haikuwezekana alikuwa ameshachelewa, alitamani
arudi nyumbani haraka ili akamuombe msamaha
Nickson ili warudiane ingawa hakuamini kama
angesamehewa kutokana na unyama aliomfanyia
wa kumuweka kituo cha polisi.
“Lazima nimuombe msamaha Nickson wangu”
Aliwaza Gloria huku akiwa amekaa chini.Wakati
tukio zima linatokea la kuachwa na Pedeshee Kway
na gari kuna Mzee Mmoja aliliona na alitaka kujua
nini hatma yake.Alisogea karibu na Gloria kwa
huruma na kumshika bega la kulia.
“Hallo”
Mzee huyo Mweusi tii alimsalimia Gloria,huku
akimtizama usoni.
“Sorry for what happened”(samahani kwa
yaliyotokea)
Mzee huyo alisema huku akizidi kumsogelea Gloria
karibu nayeye akajikuta amechuchumaa.
“Am Mr.Zuma”
Alijitambulisha Mzee huyo lakini Gloria hakusema
lolote.
“Can you speak zulu?so that you tell me”(Unaweza
kuongea kizulu ili uniambie)
“No tafadhali go”
Gloria akachanganya kiswahili na kuongea kwa
hasira na kwa wakati huo hakutaka kuongea na
mtu yoyote Yule,alichokuwa anafikiria kichwani
kwake ni kuitoa mimba ya mtoto huyo,aliamini
kuwa ndiye aliyemzibia sterehe yake aliyoonjeshwa
kidogo.
Ghafla akasimama na kurejea hospitalini ili
kuzungumza na daktari juu ya kutoa mimba,kwa
kiingereza kibovu alichokua anazungumza
kilieleweka.
“Why are you aborting?”
Daktari alimuuliza tena swali Gloria kwa mara
nyingine,akitaka kujua ni kwanini anataka kuitoa
mimba kubwa kama hiyo.
“Because me mmhhh, I hate children is me and
Father of the the children don’t like me,okay”
Gloria alizidi kuunga unga na kuvuta maneno ya
kiingereza akijaribu kuyaunga na gundi ili
afanikiwe.Lakini daktari alimuelewa japo kwa shida.
“Are you sure?” (Una uhakika)
“Yes,Yes my doctor”
Gloria akajibu kwa ujasiri kwa bahati nzuri alikuwa
anapochi na ndani yake alikuwa na Dollar elfu
mbili, hiyo aliamini ingetosha kabisa kuuwa kiumbe
chake kilichokuwa tumboni kilichomsababishia
asitishiwe huduma.
Dokta akatoka nje baadaye alirudi na vifaa vya
kazi.Jambo la kutoa mimba katika nchi ya Afrika
Kusini lilipigwa vita na jambo hilo lilikuwa ni kosa
la jinai,lakini kutokana na tamaa ya pesa Dokta
Vunga akajikuta amepatwa na tamaa.
Dola elfu moja ikamfanya atake kuuwa mtoto
aliyefikisha miezi mitano tumboni.Ghafla baada ya
Gloria kupanda kitandani akaingia mwanaume
mweusi.
“Vipi bwana mbona unaingia bila utaratibu?,hapa
sio chooni”
Dokta Vunga akauliza kwa Jazba.Gloria akageuka
na kuona sura ya mzee aliyekutana naye muda
mfupi uliopita.
“Naomba jambo unalotaka kulifanya uliache mara
moja,.kwa sababu nitakushtaki sasa hivi”
“Jambo gani?”
“Unajifanya hujui,unataka kumfanyia nini huyu
Mwanamke aliyelala hapo kitandani?”
“Nampima tu Malaria naomba utoke nje”
Mabishano hayo yalifanyika kwa lugha ya kizulu.
“Unampima Malaria na mikasi?sasa subiri nipige
simu polisi ili….”
“Ngoja kwanza basi”
Dokta Vunga aliogopa mno kusikia habari za
polisi,alihisi kinyesi kinambana, Mwanamke
aliyelala juu ya kitanda ameipanua miguu yake
alikuwa mbioni kwenda kufanya kitendo cha kuuwa
mtoto tumboni.
Ilibidi aghairi ghafla baada ya kusikia neno
polisi,akakumbuka ndugu zake na wadogo zake
waliokuwa wakimtegemea na aliamini kitendo cha
kushtakiwa kingemfanya afungwe kama sio
kunyongwa.
“Nachotaka mimi huyo binti umuache kama alivyo”
“Hilo?hilo ondoa shaka”
Dokta Vunga akabadilisha msimamo
wake.Mr.Zuma alijikuta anaingiwa na huruma na
kutaka kujua nini chanzo cha Mwanamke huyo
kutaka kuuwa kiumbe kisicho na hatia,akamshawi
shi watoke hospitali ili watafute sehemu
waongee.Gloria kwa shingo upande akainuka na
wote wakatoka nje mpaka kwenye gari la kifahari
Lamborghin,lilikuwa gari la kisasa Mr.Zuma
akawasha gari hilo na kuligeuza huku akianza
kumzoea Gloria taratibu.
“Tell me,why are you crying?”(Nambie kwanini
unalia)
Mr.Zuma akamuuliza Gloria ambaye badala ya
kujibu akazidi kulia zaidi,hii ikamfanya Mr.Zuma
azidi kutaka kujua kiundani,picha ya mwanaume
aliyekuwa anamfokea na kuondoka na Landcruiser
v8 ikamjia kichwani.
“Who was that Man,is he your husband?”(Yule
mwanaume ni nani,ni mumeo)
Mr.Zuma alizidi kuuliza wakiwa wanazidi kusonga
mbele.wakapita barabara ya Kuelekea Stellenbosch
wakanyoosha wakafika mpaka paar,gari lilizidi
kutembea kwa kasi, urefu wa kilomita nyingi
mpaka wakafika Hermanus,wakaacha lami na
kuingia kwenye barabara iliyochongwa vizuri ikiwa
na majani mazuri pembeni yake,urefu wa mita mia
mbili arobaini gari la kifahari likasimama nje ya
geti kubwa.
Mr.Zuma akatoa Rimoti na kubonyeza, lango
likajifungua lenyewe.Gloria alistaajabu mno,hasa
baada ya kuona mbele yake jumba kubwa kupita
kiasi, nje kulisheheni magari tofauti ya
kifahari,Kichwani kwake alikuwa ana vitu vingi sana
anavifikiria,vitu alivyokuwa anaviona
vilimchanganya akili yake akabaki na kazi ya
kugeuza shingo yake,kwa mbali kidogo aliona kuna
uwanja mkubwa kiasi huku ndani yake wakiwemo
Farasi weupe wanatembea huku na kule.
“Welcome home”(Karibu nyumbani)
Mr.Zuma alizungumza na kushuka garini
akamfungulia Gloria mlango wote wakashuka na
kutembea,namna alivyopokelewa Mr.Zuma alizidi
kustaajabu ghafla akajihisi yupo peponi,lilikuwa ni
jumba kubwa la kisasa.Wakaingia wote ndani
wakakaribishwa kwenye kiti na wafanyakazi wa
ndani baada ya muda mfupi Juisi ililetwa.Mr.Zuma
akawa ana kazi ya kumsaili Gloria akimuhoji
maswali mawili matatu,alifurahi mno alivyojua ni
mtanzania.
“Bongo,nilishawahi ishi kule ujue,nimekaa Tabata
pale jijini Dar es salaam,Arusha sakina nimekaa
sana, Moshi Marangu,nikaendaga mpaka mulima
Kilimanjaro,nikapanda mpaka juu Kibo na
Mawenzi”
Mr.Zuma alizungumza Kiswahili, Gloria
akashangazwa.Na wakaanza kuongea.
“Hukuniambia ilikuwaje,pale hospitalini,Yule jamaa
ni nani? Mumeo?”
“Ndio,ni mume wangu kaikataa hii mimba na
isingekuwa wewe ningesha muuwa huyu mtoto”
Gloria hakuona haya yoyote, aliyoongea hayakuwa
na ukweli hata kidogo.
“Usijali kabisa,mimi nitakusaidia”
“Sawa,nitashukuru”
Hapo ndipo mazoea yakawa yameanza.Uzuri wa
Gloria ulizidi maradufu siku hadi siku,kila alipopita
mbele yake Mr.Zuma alibaki akishindwa kuelewa ni
kitu gani akifanye,katika maisha yake ni kweli
hakuwahi kuona mwanamke mzuri kama Gloria.
Uzuri wa Gloria uliunyanyasa Moyo wa
Mr.Zuma.Pamoja na kusaidiwa na Mr.Zuma na
kupewa msaada lakini hakuacha kumkumbuka
Mume wake Nickson na alitamani kurudi Tanzania
dakika hiyo hiyo ili akamuombe msamaha mume
wake,alijiona mkosaji na alistaili moto wa
Sheteni.Siku hiyo usiku Mr.Zuma alirudi akiwa
amelewa chakali, akangia chumbani kwa Gloria na
kuufungua mlango akamkuta amelala.
Gloria akashtuka kutoka usingizini na kuwasha
switch ya kitandani.
“Vipi?”
“Viiiipi Nini,tulia ivyo ivyoooo”
Mr.Zuma alivua nguo zake na kumsogelea Gloria
karibu akimlazimisha kufanya naye ngono huku
akimuhaidi angempa pesa nyingi endapo atakubali
tendo hilo litokee.
“kiasi gani?”
Gloria aliuliza kwa sauti ya puani huku
akirembua,udenda ulimtoka.
“Dollar elfu kumi”
“Ni ndogo mbona”
Gloria akatingisha kiberiti.
“Dollar laki tano”
Moyo wa Gloria ukapiga paa! Dola laki tano
hazikuwa ndogo kwake japokuwa hakuelewa ni
kiasi gani cha pesa endapo akizibadilisha, bila
kuuliza akajikuta anamsogelea Mr.Zuma na kuutoa
ulimi wake nje,ndimi zao zikagusana wakaanza
kulana denda.
BILA KUSAHAU KWAMBA HADITHI HII INAPATIKANA
YOTE WATSAP NA INBOX KWA TSHS 3000/- KWA
MWEZI.mawasiliano namba 0718 862176.
(BADO SHINDANO LINAENDELEA LA STORY ZA
KWAY SHINDA PESA KWA MAELEZO ZAIDI INGIA
KWENYE UKURASA WA STORY ZA KWAY ILI UPATE
MAELEKEZO)
Sasa unaweza kusoma hadithi za mtunzi kway
insta@storyzakway
ITAENDELEA.
MTUNZI….EMMANUEL F. KWAY
Contact…+255718 862176
AGE….(18+)
ILIPOISHIA.
Hayo ndiyo maneno aliyoongea Pedeshee Kway
huku kioo cha gari kikipanda juu,hakutania alitoa
gari kwa kasi na kumuacha Gloria akiwa hospitalini
asijue wapi aelekee kwa sababu alikuwa bado
mgeni wa jiji la Afrika kusini.
SONGA NAYO.
Jambo lililokuwa limemtokea Gloria bado
hakuliamini kama lilikuwa ndoto au kweli,hata siku
moja hakuamini kuwa Pedeshee Kway angemgeuka
kiasi hicho na kumuacha kwasababu ya mimba
aliyokuwa nayo,ghafla akajiangalia tumboni na
kuchukizwa na mtoto aliyembeba,alimuona ndiye
aliyetia dosari katika maisha yake ya raha
mustarehe.Alitamani kitu kinachotokea kisiwe cha
ukweli bali ndoto ili ashtuke.Ni kweli alilishuhudia
Landcruiser V8 linatoka nje ya geti likikunja kona
na kutokomea, hapo ndipo aliposhtuka kama mtu
aliyetoka usingizini,aliweka mikono yake kichwani
na kujikuta akilengwa na machozi hofu
ilimtanda,hapo ndipo picha ya mume wake Nickson
ikamjia kichwani na kujiona jinsi gani alivyokuwa
mwanamke mpumbavu.
Gloria alijutia na kutamani siku zirudi nyuma lakini
haikuwezekana alikuwa ameshachelewa, alitamani
arudi nyumbani haraka ili akamuombe msamaha
Nickson ili warudiane ingawa hakuamini kama
angesamehewa kutokana na unyama aliomfanyia
wa kumuweka kituo cha polisi.
“Lazima nimuombe msamaha Nickson wangu”
Aliwaza Gloria huku akiwa amekaa chini.Wakati
tukio zima linatokea la kuachwa na Pedeshee Kway
na gari kuna Mzee Mmoja aliliona na alitaka kujua
nini hatma yake.Alisogea karibu na Gloria kwa
huruma na kumshika bega la kulia.
“Hallo”
Mzee huyo Mweusi tii alimsalimia Gloria,huku
akimtizama usoni.
“Sorry for what happened”(samahani kwa
yaliyotokea)
Mzee huyo alisema huku akizidi kumsogelea Gloria
karibu nayeye akajikuta amechuchumaa.
“Am Mr.Zuma”
Alijitambulisha Mzee huyo lakini Gloria hakusema
lolote.
“Can you speak zulu?so that you tell me”(Unaweza
kuongea kizulu ili uniambie)
“No tafadhali go”
Gloria akachanganya kiswahili na kuongea kwa
hasira na kwa wakati huo hakutaka kuongea na
mtu yoyote Yule,alichokuwa anafikiria kichwani
kwake ni kuitoa mimba ya mtoto huyo,aliamini
kuwa ndiye aliyemzibia sterehe yake aliyoonjeshwa
kidogo.
Ghafla akasimama na kurejea hospitalini ili
kuzungumza na daktari juu ya kutoa mimba,kwa
kiingereza kibovu alichokua anazungumza
kilieleweka.
“Why are you aborting?”
Daktari alimuuliza tena swali Gloria kwa mara
nyingine,akitaka kujua ni kwanini anataka kuitoa
mimba kubwa kama hiyo.
“Because me mmhhh, I hate children is me and
Father of the the children don’t like me,okay”
Gloria alizidi kuunga unga na kuvuta maneno ya
kiingereza akijaribu kuyaunga na gundi ili
afanikiwe.Lakini daktari alimuelewa japo kwa shida.
“Are you sure?” (Una uhakika)
“Yes,Yes my doctor”
Gloria akajibu kwa ujasiri kwa bahati nzuri alikuwa
anapochi na ndani yake alikuwa na Dollar elfu
mbili, hiyo aliamini ingetosha kabisa kuuwa kiumbe
chake kilichokuwa tumboni kilichomsababishia
asitishiwe huduma.
Dokta akatoka nje baadaye alirudi na vifaa vya
kazi.Jambo la kutoa mimba katika nchi ya Afrika
Kusini lilipigwa vita na jambo hilo lilikuwa ni kosa
la jinai,lakini kutokana na tamaa ya pesa Dokta
Vunga akajikuta amepatwa na tamaa.
Dola elfu moja ikamfanya atake kuuwa mtoto
aliyefikisha miezi mitano tumboni.Ghafla baada ya
Gloria kupanda kitandani akaingia mwanaume
mweusi.
“Vipi bwana mbona unaingia bila utaratibu?,hapa
sio chooni”
Dokta Vunga akauliza kwa Jazba.Gloria akageuka
na kuona sura ya mzee aliyekutana naye muda
mfupi uliopita.
“Naomba jambo unalotaka kulifanya uliache mara
moja,.kwa sababu nitakushtaki sasa hivi”
“Jambo gani?”
“Unajifanya hujui,unataka kumfanyia nini huyu
Mwanamke aliyelala hapo kitandani?”
“Nampima tu Malaria naomba utoke nje”
Mabishano hayo yalifanyika kwa lugha ya kizulu.
“Unampima Malaria na mikasi?sasa subiri nipige
simu polisi ili….”
“Ngoja kwanza basi”
Dokta Vunga aliogopa mno kusikia habari za
polisi,alihisi kinyesi kinambana, Mwanamke
aliyelala juu ya kitanda ameipanua miguu yake
alikuwa mbioni kwenda kufanya kitendo cha kuuwa
mtoto tumboni.
Ilibidi aghairi ghafla baada ya kusikia neno
polisi,akakumbuka ndugu zake na wadogo zake
waliokuwa wakimtegemea na aliamini kitendo cha
kushtakiwa kingemfanya afungwe kama sio
kunyongwa.
“Nachotaka mimi huyo binti umuache kama alivyo”
“Hilo?hilo ondoa shaka”
Dokta Vunga akabadilisha msimamo
wake.Mr.Zuma alijikuta anaingiwa na huruma na
kutaka kujua nini chanzo cha Mwanamke huyo
kutaka kuuwa kiumbe kisicho na hatia,akamshawi
shi watoke hospitali ili watafute sehemu
waongee.Gloria kwa shingo upande akainuka na
wote wakatoka nje mpaka kwenye gari la kifahari
Lamborghin,lilikuwa gari la kisasa Mr.Zuma
akawasha gari hilo na kuligeuza huku akianza
kumzoea Gloria taratibu.
“Tell me,why are you crying?”(Nambie kwanini
unalia)
Mr.Zuma akamuuliza Gloria ambaye badala ya
kujibu akazidi kulia zaidi,hii ikamfanya Mr.Zuma
azidi kutaka kujua kiundani,picha ya mwanaume
aliyekuwa anamfokea na kuondoka na Landcruiser
v8 ikamjia kichwani.
“Who was that Man,is he your husband?”(Yule
mwanaume ni nani,ni mumeo)
Mr.Zuma alizidi kuuliza wakiwa wanazidi kusonga
mbele.wakapita barabara ya Kuelekea Stellenbosch
wakanyoosha wakafika mpaka paar,gari lilizidi
kutembea kwa kasi, urefu wa kilomita nyingi
mpaka wakafika Hermanus,wakaacha lami na
kuingia kwenye barabara iliyochongwa vizuri ikiwa
na majani mazuri pembeni yake,urefu wa mita mia
mbili arobaini gari la kifahari likasimama nje ya
geti kubwa.
Mr.Zuma akatoa Rimoti na kubonyeza, lango
likajifungua lenyewe.Gloria alistaajabu mno,hasa
baada ya kuona mbele yake jumba kubwa kupita
kiasi, nje kulisheheni magari tofauti ya
kifahari,Kichwani kwake alikuwa ana vitu vingi sana
anavifikiria,vitu alivyokuwa anaviona
vilimchanganya akili yake akabaki na kazi ya
kugeuza shingo yake,kwa mbali kidogo aliona kuna
uwanja mkubwa kiasi huku ndani yake wakiwemo
Farasi weupe wanatembea huku na kule.
“Welcome home”(Karibu nyumbani)
Mr.Zuma alizungumza na kushuka garini
akamfungulia Gloria mlango wote wakashuka na
kutembea,namna alivyopokelewa Mr.Zuma alizidi
kustaajabu ghafla akajihisi yupo peponi,lilikuwa ni
jumba kubwa la kisasa.Wakaingia wote ndani
wakakaribishwa kwenye kiti na wafanyakazi wa
ndani baada ya muda mfupi Juisi ililetwa.Mr.Zuma
akawa ana kazi ya kumsaili Gloria akimuhoji
maswali mawili matatu,alifurahi mno alivyojua ni
mtanzania.
“Bongo,nilishawahi ishi kule ujue,nimekaa Tabata
pale jijini Dar es salaam,Arusha sakina nimekaa
sana, Moshi Marangu,nikaendaga mpaka mulima
Kilimanjaro,nikapanda mpaka juu Kibo na
Mawenzi”
Mr.Zuma alizungumza Kiswahili, Gloria
akashangazwa.Na wakaanza kuongea.
“Hukuniambia ilikuwaje,pale hospitalini,Yule jamaa
ni nani? Mumeo?”
“Ndio,ni mume wangu kaikataa hii mimba na
isingekuwa wewe ningesha muuwa huyu mtoto”
Gloria hakuona haya yoyote, aliyoongea hayakuwa
na ukweli hata kidogo.
“Usijali kabisa,mimi nitakusaidia”
“Sawa,nitashukuru”
Hapo ndipo mazoea yakawa yameanza.Uzuri wa
Gloria ulizidi maradufu siku hadi siku,kila alipopita
mbele yake Mr.Zuma alibaki akishindwa kuelewa ni
kitu gani akifanye,katika maisha yake ni kweli
hakuwahi kuona mwanamke mzuri kama Gloria.
Uzuri wa Gloria uliunyanyasa Moyo wa
Mr.Zuma.Pamoja na kusaidiwa na Mr.Zuma na
kupewa msaada lakini hakuacha kumkumbuka
Mume wake Nickson na alitamani kurudi Tanzania
dakika hiyo hiyo ili akamuombe msamaha mume
wake,alijiona mkosaji na alistaili moto wa
Sheteni.Siku hiyo usiku Mr.Zuma alirudi akiwa
amelewa chakali, akangia chumbani kwa Gloria na
kuufungua mlango akamkuta amelala.
Gloria akashtuka kutoka usingizini na kuwasha
switch ya kitandani.
“Vipi?”
“Viiiipi Nini,tulia ivyo ivyoooo”
Mr.Zuma alivua nguo zake na kumsogelea Gloria
karibu akimlazimisha kufanya naye ngono huku
akimuhaidi angempa pesa nyingi endapo atakubali
tendo hilo litokee.
“kiasi gani?”
Gloria aliuliza kwa sauti ya puani huku
akirembua,udenda ulimtoka.
“Dollar elfu kumi”
“Ni ndogo mbona”
Gloria akatingisha kiberiti.
“Dollar laki tano”
Moyo wa Gloria ukapiga paa! Dola laki tano
hazikuwa ndogo kwake japokuwa hakuelewa ni
kiasi gani cha pesa endapo akizibadilisha, bila
kuuliza akajikuta anamsogelea Mr.Zuma na kuutoa
ulimi wake nje,ndimi zao zikagusana wakaanza
kulana denda.
BILA KUSAHAU KWAMBA HADITHI HII INAPATIKANA
YOTE WATSAP NA INBOX KWA TSHS 3000/- KWA
MWEZI.mawasiliano namba 0718 862176.
(BADO SHINDANO LINAENDELEA LA STORY ZA
KWAY SHINDA PESA KWA MAELEZO ZAIDI INGIA
KWENYE UKURASA WA STORY ZA KWAY ILI UPATE
MAELEKEZO)
Sasa unaweza kusoma hadithi za mtunzi kway
insta@storyzakway
ITAENDELEA.