Riwaya mpya: Mbwa wa geti

Riwaya mpya: Mbwa wa geti

Mbwa wa geti

Sehemu ya saba


Alishuka chini na kumkuta Tausi akiwa amejiinamia sebuleni,akamtazama kwa dharau kisha akamsabahi,lakini salamu yake haikuitikiwa na Tausi,Kabah akakaa kwenye sofa huku akimtizama Tausi.

“naomba umuache mwanangu Kabah,mateso unayonipa yanatosha kuwa adhabu ya ujinga wangu,lakini mwache mwanangu aishi kwa amani..”
Tausi alikuwa anaongea na Kabah

“mwanao anafanya kazi kwa malipo,na malipo yake ni kete ninazo kupa kila siku,”
Yalikuwa majibu ya Kabah kwenda kwa Tausi.Tausi alinyanyua macho na kumtizama Kabah kama vile haamini alichokisikia kutoka kwa Kabah

“Naomba umwache mwanangu,kama kete ndo malipo basi naomba usinipe tena ili mwanangu aishi kwa amani Kabah please…..”

“are you sure kwamba huhitaji tena kete zangu?

“Ndio kabah”

“basi sawa mi naondoka na mwanao anakuja” kabah hakungoja neno kutoka kwa Tausi akasimama na kuchukua briefcase yake na kuondoka sebleni pale.

*****

Rpc Kambi Mabeyo,alikuwa ameshika faili maelezo kadhaa kuhusu mkakati wa ukomeshaji uuzaji wa dawa za kulevya mkoa wa Dodoma ikiwa ni kutekeleza agizo la rais la kupambana na uuzaji wa dawa za kulevya nchini.
Rpc Kambi Mabeyo alilifunga faili lile kisha akamtazama askari mkakamavu aliekuwa amesimama mbele yake akiwa ndani ya vazi lake la kazi.

“una hakika ndani ya Wiki hii utakuwa umekamilisha ushahidi wa kuwatia hatiani hawa wauzaji wa dawa hizi?!”
Lilikuwa swali la Rpc kambi kwenda kwa kijana wake aliekuwa anaongoza mpangao mzima wa kuwakamata wauzaji wa dawa za kulevya mjini Dodoma.

“Ndio afande na tumebakiza hatua ndogo sana kumjua papa wao hawa jamaa” lilikuwa jibu la Inspector Makasi kwenda kwa mkubwa wake wa kazi.

Rpc Kambi Mabeyo akimtizama kwa makini kijana wake,na hapo akaona ari ya kijana yule ndani ya uso wake,akampa nasaha kidogo na namna ya kuendesha mkakati ule bila kusingizia watu au kubugudhi watu wasio husika.

Inspector Makasi alipiga salute na kisha akaondoka ofisini pale ili kuwahi majukumu mengine ya kikazi na tayari alikuwa na kibali cha kuwakamata watu kadhaa waliokuwa wakihusika na tuhuma za uingizaji dawa za kulevya ndani ya mji ule wa Dodoma,huku maeneo kama hazina na airport yakiwa ndio senta ya biashara ile.

Jambo moja ambalo Rpc na inspector hawakujua ni kuwa muda wote wa ukusanyaji na uwasilishaji ripoti kuna mtu alikuwa akifuatilia kila hatua ya maendeleo ya kazi ile na hata wakati Inspector Makasi anatoka ofisini kwa Rpc,mtu yule aliona na aliona pia wakati Inspector Makasi anapanda gari yake aina ya Noah na vijana wengine watatu huku wakiwa na silaha za moto mikononi mwao,mtu yule aliamua kupiga simu pahali kisha akatoa maelezo machache tu na kukata simu kisha akaendelea na kazi yake.

Inspector Makasi alikuwa anaendesha noah ile tangu walipotoka ofisini kwa Rpc na sasa walikuwa wanazunguka mzunguko wa jamatini kisha wakanyoosha na barabara,wakaipita Nyerere square na wakawa wanakaribia Bank ya NBC ndipo walipata mgeni nyuma.

Ilikuwa ni pikipiki iliokuwa imebeba watu wawili na pikipiki ile ilikuwa ni BMW yenye namba za usajili kutoka uganda,watu kadhaa barabarani walikuwa wakishangaa ukubwa wa pikipiki ile.

Inspector Makasi aliiona pikipiki ile lakini hakuitilia shaka akaendelea na Safari yake huku akipanga mikakati na vijana wake.

Gari inayoendeshwa na Inspector makasi ilisimama kwenye njia panda ya dar es laam road ili kusubiri taa za kuongozea magari ziruhusu ni wakati huo ambapo kilitokea kitendo ambacho hakuna aliekitegemea.

Ile pikipiki ilikuwa ipo nyuma haraka ikapita upande wa pili kulia mwa gari ya Inspector ambako kulikuwa na magari machache sana na hapo ukasikika mlio wa risasi kutoka kwenye bunduki iliokatwa mbele na askari waliokuwa kwenye Noah ile wakashuhudia kichwa cha Inspector Makasi kikisambaratika huku damu iliochanganyikana na ubongo ikiruka huku na huko na hata waliposhuka walikuwa wamechelewa tayari pikipiki ile ilikuwa imeondoka eneo lile na wao wakaanza kushambulia kuielekea lakini tena bila kutarajia wakajikuta wakioga risasi kutoka kwenye gari nyingine iliokuwa ipo upande wa pili kama inarudi mjini huku wao walikuwa wakitoka mjini.

Kutoka kwenye gari ile walishuka watu watatu na wakaanza kushambulia kwa weledi kuelekea kwa askari wale waliokuwa wametoka ndani ya Noah na ndani ya dakika mbili tu eneo la mataa lilikuwa limebakia na maiti nne za askari polisi huku wauwaji wakiwa wanagawana njia za kukimbia.
***
Simu ya Rpc Kambi Mabeyo iliita na akaipoea,ililuwa ni sauti ya askarI wa barabarani alie kuwa pale mataa ,alieleza kwa kifupi namna tukio lilivyotokea.

Kambi mabeyo Rpc wa mkoa wa Dodoma alichanganyikiwa kusikia taarifa za kuuwawa kwa Inspector Makasi na askari wengine watatu,haraka akatoka ofisini kwake huku simu yake ikiwa sikioni alikuwa anatoa taarifa vikosi vya uchunguzi vifike eneo la tukio haraka sana.

Ndani ya dakika kumi tu tayari magari ya polisi zaidi ya manne yalikuwa yamesimama eneo lile huku magari yanayoingia na kutoka mjini yakiwa yamezuiwa kuvuka eneo lile jambo lililopelekea kuwe na foleni ndani ya mji wa Dodoma.

Hakuna askari ambae alikuwa eneo lile hakuwa na silaha,huku wakiwa wameweka ulinzi mkali eneo lile,Kambi Mabeyo haraka akaagiza kijana mmoja achukue faili ndani ya noah ile,lakini akarejeshewa taarifa ya kuwa hakuna faili hata moja ndani ya gari lile ,hapo akachanganyikiwa na akaagiza uchunguzi ufanyike kwa kina kujua wauaji na kwanini waliua japo jinsi alivyojua yawezekana ni ripoti ya madawa ndio imegarimu maisha ya vijana wake.

Swali moja lilibaki kichwani ni kwanini taarifa za kijana wake ziliwafikia wauaji ikiwa swala lile walilipeleka kwa siri mno.

Rpc akaelekea kituo kikuu cha polisi Dodoma na huko akataka apewe majalada yote ya kesi zinazohusu uuzaji na utumiaji wa dawa za kulevya,lakini ajabu nako hakukua na jalada hata moja,akaondoka bila kusema kitu hadi mkoani zilipo ofisi zake na huko akahitaji kupata jalada la mwisho lililokuwa linaandaliwa na Inspector Makasi,taarifa ikarudi ya kuwa hakuna kilichoachwa na inspector.

Rpc akachanganyikiwa na hapo akaona anachezewa shere ndani ya mkoa wake,hiyo ni dharau akanyanyua simu na kupiga makao makuu
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom