Mbwa wa geti
Sehemu ya sita
Hakupiga hatua nne,akasikia mtu yule akimpa tahadhari
“Huwezi kupata huo mlango wa chemba..”
Yule mtu hakungoja swali kutoka kwa Zedi,taratibu akaanza kumfuata Zedi kisha akampita na kumuomba wafuatane,Zedi akatii lakini hakuwa na imani sana na mtu yule hivyo akawa makini sana na nyendo zake na za mtu yule.
Safari yao ilikuwa ni ya kimyakimya,katikati ya pori lile na nusu walitembea nusu walikimbia ili mradi lengo lao lilikuwa ni wawahi kufika.
Safari yao iliwafikisha kwenye mfuniko wa mkubwa wa chemba ya maji machafu yatokayo ndani ya ngome ile ya Kabah,walishirikiana kufungua chemba ya ile na kabla ya Zedi hajajitosa ndani,mtu yule akamshika bega la kulia kisha akasema
“Naitwa Mao Waira,nikutakie safari njema na tukutane Nairobi…””
Alimaliza kuongea mtu yule aliejitambulisha kwa jina la Mao Waira.
Zedi akaliweka kichwani jina lile kisha akazama chembani na Mao Waira akaifunga kwa juu na kuanza kurudi kambini kwao kwa kasi ya umeme.
*****
Kitu ambacho Kabah hakutaka kuamini ni kusikia eti Zedi hajaonekana kote ndani ya ukuta unao izunguka ngome ile ile iliokatikati ya pori nene la Kenya national park.Kichwa kilimuuma,aliiona hatari ya kuanzisha Vita na Zedi aliehuru,na mara kwa mara alijilaumu kwa kushindwa kumuua Zedi mapema.
Hadi inafika ahsubuhi Kabah alikuwa hajapata kusikia habari yoyote kutoka kwa vijakazi wake ya kuwa Zedi ameonekana au mwili wake au hata nyayo zake,Kabah alijikuta akizunguka peke yake pasi kufanya kitu ndani ya ofisi yake,hakuwa amedhania Zedi aweza kuwa na uwezo wa kuruka ngome ile au Zedi anao uwezo wa kuwapiga chenga vijana wake mahiri kwa namna ya ajabu kiasi kile.
Kabah hakutaka kushindwa,aliagiza vijana mahiri waingie msituni kumsaka Zedi,lakini pia alinyakuwa simu yake iliokuwa mezani na kupiga pahali na kutoa maelekezo Zedi atafutwe Nairobi nzima ikibidi na viunga vyake.
Zedi alihisi kama kuna kitu kinamtekenya ndani ya sikio,na kwa pupa akakurupuka,lakini halikuwa sikio tu baadhi ya maeneo ya mwili yalikuwa yameanza kushambuliwa na sisimizi waliokuwa wameanza kumtambaa mwilini baada ya kukaa eneo lile la pango kwa muda mrefu.
Akasimama na kujikung’uta,kisha akaanza kufuata njia ile ya kipango kile ambacho hakujua kinaishia wapi.
Akasonga mbele hatimae akajikuta akitabasamu peke yake,mbele aliona mwanga, hivyo aliamini huko mbele ataiona dunia na ndivyo ilikuwa,alijikuta akaitokeza nje ya pango lile na kwa mbali aliona makazi ya watu na barabara iliokuwa ikipitisha magari.
Taratibu akaanza kufuata uelekeo wa barabara,na hapo akaamua kujitizama na akaona hatamaniki kwa mavazi na uchafu,lakini pia alijiona alivyo konda.
Alizifikia nyumba za wakazi wa eneo lile,na kilionekana kuwa ni kijiji cha wafugaji kilichokuwa pembezoni mwa hifadhi ile ya Nairobi.
Waliowengi kijijini pale,walionekana kumshangaa,lakini macho ya huruma yalikuwa yakimlaki kwa viulizo,hatimae Zedi alimfikia mzee mmoja na kuuliza,aliambiwa yupo Nanyuki nje kidogo ya jiji la Nairobi na pembeni ya hifadhi ya Nairobi national park.
Zedi alidanganya masahibu yaliomkuta na alidai yeye ni mtalii kutoka Tanzania na aliachwa na wenzie baada ya Simba kuwakimbiza huko porini.
Kama ujuavyo jamii nyingi za wafugaji,roho ya upendo imewajaa,ndivyo walivyo mwamini Zedi na wakampa chakula na kisha vijana rika sawa na Zedi wakavunja mabegi yao na kumpa Zedi nguo za nzuri na viatu,na Zedi alishukuru kwa ukarimu wa watu wa Nanyuki.
Ni wakati anaaga ili aondoke ndipo akapata jambo jipya kutoka kwa wakazi wa Nanyuki,wakazi wale walimpa tahadhari,maana kumekuwa na upotevu wa watu kijijini pale hasa vijana tena wengi hupotea nyakati za jioni na usiku,lakini kubwa zaidi ni kuwa hivi sasa serikali imetangaza hali ya hatari kwa wakazi wote wa nchi ya Kenya,ya kuwa kuna jamii ya wadudu wasioeleweka chanzo chake wamekuwa wakishambulia wanyama na binadamu kwa muda mchache sana.
Zedi hakuwa mgeni na wadudu wale,aliwajua na hapo akaona anakazi ya kufanya ili kulipa wema wa Wakenya.
Akawatoa hofu,na kisha akasaidiwa kupata usafiri wa kumfikisha jijini Nairobi kwa kupitia Nyeri,jambo moja hakujua aendako si salama kwake na Kama angelijua ni heri angelitafuta njia ya kurudi Tanzania kumsaidia mwanae anae teseka mikononi mwa ***** Tausi.
****
Tausi kilio kwake kilikuwa ni kama ratiba ya kila saa kwake,na sasa alikuwa analia kwa kuingiliwa kimwili na rafiki wa kabah.
Kabah na rafiki zake walimgeuza mtumwa wao wa ngono,kila walipojisikia walifika na kumwingilia kimwili Tausi,iwe kwa lazima ama hiyari,rafiki huyu wa Kabah alikuwa amemlagai kwa paketi mbili za madawa ya kulevya aina ya heroine na kwa kuwa Tausi aliyahitaji basi akafanya vile rafiki yule alivyotaka,hakuwa na pa kusemea wala hakuwa na kulilia maana Kabah alijua rafiki zake wanamwingilia mpenzi wake huyo na yeye alibariki,pengine ndo ilikuwa ni tabia yao,lakini Tausi aliona ule ni udhalilishaji kwake lakini anelikwenda wapi,ikiwa hakuna mtu anae msikiliza au kumruhusu japo kutoka nje ya geti ya jumba lile la kifahari.
Alijinyanyua kutoka pale alipokuwa amelazwa na rafiki wa kabah ambae yeye alimtambua kama Burizozo.
Akaelekea sebuleni na huko akatoka nje ya jumba lile na kisha akamuita mlinzi mmoja aliekuwa eneo lile.
“Temba!! Mwanangu yuko wapi!?”
“Tausi mimi kwa sasa sijui ila atakuwa anamezeshwa mzigo huko ili,,,,,”
Tausi hakutaka Temba amalize kuongea,akaweka viganja vya mikono yake mdomoni,kuziba sauti ya kilio isitoke,kisha akakimbia kurudi ndani,na huko kilifuatia kilio kingine cha kwikwi na akasahau kama aliingiliwa kimwili na rafiki wa kabah dakika chache zilizopita.
Temba alibaki akimtizama mwanamke yule akiishia ndani,na hapo akili yake ikaingiwa na roho ya huruma,alitamani kumsaidia,lakini aliona sio muda sahihi wa kufanya hivyo,akageuka ili arudi lindoni kwake na bila kutarajia akijikuta akitazamana na Kabah aliekuwa ameingia pale uwani kwa kutumia mlango mdogo wa geti uliokuwa wazi.
Temba alitoa heshima kwa bosi wake huyo,ambae kiumri alikuwa ni mdogo kwa Temba,lakini shauri ya pesa ilimfanya Kabah atukuzwe na kila mtu akiwemo Temba aliekuwa mlinzi mkuu wa mali za magendo za Kabah na siku ambayo hawakuwa na kazi basi Temba alisimamia ulinzi ndani ya jumba lile la kifahari lililokuwa mjini Dodoma maeneo ya area c.
Kabah alimtizama Temba kwa dakika moja bila kusema kitu na kisha kama aliegutushwa kutoka usingizini alimwambia Temba wanakazi ya kufanya muda huo na haraka Temba aandae vijana mahiri wa kazi.
Temba alijua ni nini walipaswa kufanya wakati huo nae hakuwa na namna akaingia kazini muda huo huo na vijana wake wa kazi ambao walijipachika jina la MBWA WA GETI wakiwa na maana wanasimamia masilahi ya bosi wao na hakuna mtu wa kuingilia awe askari au mtu wa kawaida ni lazima achungulie kaburi akikutana na vijana hawa.
*****
Kabah aliingia ndani huku akimwacha Temba ama Mbwa wa geti akiandaa vijana kwa kazi maalumu,alipoingia ndani tu moja kwa moja alielekea chumbani kwake na huko akachukua simu yake aliotumia kuwasiliana akiwa Tanzania na akampigia mtu anaemfahamu yeye akamweleza kupotea kwa Zedi na kisha akaagiza mipaka yote iwekwe nzi wa kunusa harufu ya mtu kama Zedi,vijana wakapangwa wakamgojea Zedi.
Alishuka chini na kumkuta Tausi akiwa amejiinamia sebuleni
Itaendelea
Jiunge nami whatsapp 0658564341
Ama nitext 0758573660
Asalaam Kudo