Mbwa wa geti
Sehemu ya nane
Rpc akachanganyikiwa na hapo akaona anachezewa shere ndani ya mkoa wake,hiyo ni dharau akanyanyua simu na kupiga makao makuu.
*****
Kabah alikuwa amezungukwa na vijana kama sita hivi na vijana wote hawa walikuwa na T-shirt nyeusi zenye kichwa cha mbwa alieachama,wlikuwa ni vijana wa kikundi cha mbwa wa geti wakiongozwa na Temba.
Temba alikuwa anamkabidhi Kabah majalada kadhaa alioyachukua kutoka kwa askari wasaliti waliokuwa ndani ya jeshi.
Kabah aliyatia moto huku akitabasamu.
“hakuna kosa lolote?” aliuliza Kabah.
“Hatuna huo utaratibu wa kuacha nyayo mkuu” alijibu Temba kwa kujivuna
Wakiwa katikati ya maongezi gari ya Burizozo rafiki mkubwa wa Kabah ikaingia na kisha akateremka akiwa na picha mbili kashikilia,alipokifikia kile kikundi akamkabidhi zile picha Kabah na kusema
“Hawa wameagizwa kutoka makao makuu na wataingia hapa usiku huu,watafikia hotel ya perugina”
Kabah alicheka kisha akachukua picha zile na kumkabidhi Temba,Temba akazitazama kisha akaguna jambo lililofanya macho yote yamtazame.
“Kama huyu kweli yupo basi anatakiww kufa ndani ya usiku wa leo kabla hajapiga hatua yoyote ile” alisema Temba
“unamfahamu?!”aliuliza Kabah
“Ndio”
Burizozo akamtazama Temba kisha akamsukuma kwa kidole cha shahada huku akisema
“mh unalipwa kwa kazi kama hii,sitaki kusikia unanbia upuuzi huo wafe leo ama kesho,kikubwa wafe”
Temba alimtazama Burizozo aliekuwa anamwagiza Temba kwa dharau ,alitamani amshambulie japo kwa kichwa tu lakini haikuwezekana na hakuhitaji hilo litokee kwa wakati huo.
Wakati Burizozo akiongea na vijana wa Temba na Temba mwenyewe,Kabah alikuwa anaongea na simu kutoka kenya,simu ile ilimchamganya,tayari Zedi alikuwa ameanza kuleta madhara upande wake,kwa hasira akaioki bastola yake na kumpiga risasi ya kifua kijana wa Temba na kumuua papo hapo,jambo lile likamkera zaidi Temba na hata vijana wake hawakuonekana kulifurahia ila wakapata ishara kutoka kwa Temba ya kuwa watulie wasifanye lolote wakati huo zaidi walimchukua kijana mwenzao na kuelekea kumpeleka kuzika na kikao kile kikaishia pale huku Burizozo akimchukua Kabah wakaingia ndani huku nyuma waliacha maagizo kwa vijana ya kuwashugulikia wapelelezi kutoka makao makuu.
***
Wakati Temba akiwadhani tukio lile halikuonwa na watu wengine alikosea sana.
Siku ya tukio
Watu wawili walikuwa wamekalia viti ndani mgahawa bora na wa kisasa uliokuwa pembeni kidogo ya mataa,mgahawa huu uliitwa Destination.
Walikuwa wamependeza huku muda mwingi nyuso zao zikiwa zimepambwa kwa tabasamu la upendo.
“u mzuri sana mwanamke wewe,yaani natamani uwe wangu milele” alizungumza mwanaume aliekuwa amekaa kwa kuelekea upande wa barabara.
“mh Ziga mpenzi acha kunipamba hivyo mwenzio naona aibu” aliongea mwanamke kwa madeko huku akiachia kicheko laini kilichousisimua mwili wa komando Ziga ambae kwa sasa anahudumu ofisi kuu hapo alikuwa likizo yeye na mpenzi wake huyo waliekutana kwenye hekaheka za kikosi cha pili.
“Mina sio siri umeuteka moyo wangu huwa natamani kuwa nawe kila sekunde itambaayo,pua zangu hunusa harufu ya ngozi yako hata kama ukiwa umbali wa anga ama haki…..”
Pah,pah..
Wapenzi wale haraka walisahau mideko yao na nyuso zao wakazielekeza kule walikosikia mlio wa risasi na hapo wakashuhudia mparanginyiko wa watu waliokuwa wanakatiza barabarani huku madereva nao wakinusuru roho zao kwa kuvunja sheria za mataa.
Ziga akasimama huku mkono wake ukiwa unaelekea kiunoni,lakini Sajini Mina akawahi kumshika na kumzuia na kisha akamwambia
“mpenzi sio kila muda ni kazi,tupo likizo tuwaachie wenyewe na yaezekana ni uporaji tu huo mmh”
Ziga akimtizama mpenzi wake huyo na pasi kusema kitu alikaa.
Ni wakati anakaa tu ukaanza tena mrindimo wa risasi na kitendo kile kikaibua mashaka kwenye fikra zao,maana gari moja imeshambuliwa na watu wa aina mbili tofauti.
Mrindimo ule ulipokoma,wakasimama na kuondoka maana hata wahudumu wa mgahawa ule haikujulikana walikoelekea.
Ni wakati wanaanza kundoka ndipo wakashudia magari mengi ya polisi yakifika eneo lile na ulinzi kuimarishwa.
“Hebu ngoja niangalie kuna kitu gani kinaendelea pale” alisema Ziga huku akishuka ndani ya gari na kujichanganya na raia waliokuwa wameanza kujaa eneo lile.
Katika machache alionasa ni kuhusu faili lililopotea na pia alijua walioshambuliwa ni askari wa mkoani,Ziga aliona awaachie wenyewe akarudi ndani ya gari kisha wakaondoka kuelekea kwenye hotel waliofikia.
Usiku wa siku hiyo uliwakuta wapenzi wale wakiwa wanaogeshana ndani ya hotel kubwa na ya kisasa ilioko pembeni kidogo ya mji,hotel ya perugina.
Nb:wakati huu wa Ramadan tujaribu kufungua nyoyo zetu katika kuonesha tupo pamoja kila hatua
Utaonekana mnafiki na dhambi itakuandama kama kila siku unasoma hapa afu hata hukoment wala hulike.
Ila unangoja shetani akutumie siku nikiwa kimya kwa sababu mbalimbali basi uje hapa kutukana na kukejeli......
Zika unafiki leo sapoti kazi zetu waandishi hata kama haijakufurahisha sema ili tuumize kichwa kukufanya utabasamu kila usomapo
S
Asalaam kudo