Riwaya: Mkono Wa Chuma

Riwaya: Mkono Wa Chuma

Heshima yenu wakuu. Kwanza poleni na pia samahanini sana kwa kuwaacha kimya kimya kwa muda mrefu bila taarifa rasmi. Majukumu mengine yalinibana, na hivyo sikuweza kabisa kujumuika nanyi hapa jukwaani, ila sasa nimerejea.

Riwaya ambazo nakumbuka hatukufika nazo mwisho bila shaka ni mbili, yani 'Mkono wa Chuma' na 'Mtoto wa Baba Paroko'. Kwa upande wa mkono wa chuma nimeona mkuu SPYMATE ametoa taarifa hapo juu, na ni kweli hayo ndio maelezo ya huyo Alex Kileo mwenyewe. Kabla sijapotea jukwaani nakumbuka nliwahi kumcheki kwenye simu kumuuliza kama anaiuza sehemu iliyobakia, nkiwa na lengo la kuinunua na kuileta hapa, ila alisema 'haiuzwi' na akaahidi tena kua ni lazima ataiendeleza mpaka mwisho, pindi atakapomaliza changamoto zake 'personal' zinazomkabili. Baadae ndio akaleta hiyo taarifa kama ilivyowasilishwa hapo juu.

Kwa upande wa 'Mtoto wa Baba Paroko' nlifanya pia mawasiliano na mtunzi mwenyewe Lello, akasema hiyo itaendelea kama kawaida, na wala haitakua kwenye kitabu. Isipokua kwa sasa anabanwa na zoezi la kuandaa kitabu cha 'Mimi na Rais (the President and I)', na punde atakapomalizana na hilo zoezi atapata wasaa mzuri wa kuiendeleza 'Mtoto wa Baba Paroko'.

Hivyo kwanza niwape pole ya arosto ya muda mrefu, lakini pia niwaombe tuwe wavumilivu wakati tukiendelea kusubiri muendelezo wa hizo riwaya. Tuko pamoja wakuu
Heshima chief na pia bila samahani nasubiri
 
Nimefurahi sana kuona kuwa Nina mashabiki wengi.

Jiandaeni kwa story Kali zaidi
Kuna group wanadai hii story ulikuwa unacopy nje ya nchi na kuitafsiri, mtunzi kasimama kuendelea, nawe huna uwezo wa kuendelea hata nusu episode. nimebaki njia panda
 
Kuna group wanadai hii story ulikuwa unacopy nje ya nchi na kuitafsiri, mtunzi kasimama kuendelea, nawe huna uwezo wa kuendelea hata nusu episode. nimebaki njia panda
Duu yajayo yanafurahishaa....mko tayari wapenda hadithi?????
 
Kuna group wanadai hii story ulikuwa unacopy nje ya nchi na kuitafsiri, mtunzi kasimama kuendelea, nawe huna uwezo wa kuendelea hata nusu episode. nimebaki njia panda
Sio kwel, mimi ndio mmiliki halali wa hii riwaya, ila nina matatizo yangu binafsi ndio yamefanya stori imesimama.



uwa sina kipaji cha kukopi, na uwa naandika papo kwa papo na kutuma, uwa sina uhariri
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom