Riwaya: Mke wa Rais

Riwaya: Mke wa Rais

Sawa mkuu ukicheki kwenye episode zilizopita hapo juu nimeweka
 
Yaani nyie kina shunie mnajishunisha mmeshindwa kwenda kumfariji ibra kabisa,acheni roho mbaya nyie kina dada khaaa
 
MKE WA RAIS

Mwandishi IBRAHIM MASIMBA

Ilikuwa lazima ampata yule mwanamke, ilikuwa lazima amtie mikononi. Alitaka kujua wapi ilipo VICTORIA BASE, Alihisi ni sehemu sahihi kwake. Hakutaka kulala wala kurudi nyumbani hadi pale ambapo atampata yule ambaye amemuua Sohwa. Akaondoka eneo la tukio huku akishuhudia gari ikiendelea kuteketea. Hilo likampa uhakika kuwa hakuwa pake yake, hakuwa peke yake kwa minajilo ya kufuatiliwa na wanausalama ama majasusi wanaohusika na mpango ovu dhidi ya nchi ya Tanzania. Akatembea huku maneno ya dereva tax yakijirudia, yakipita kichwani hasa pale alipoambiwa sehemu hiyo hawafiki watu wala magari. "Kwa nini wasifike watu? Kwa nini yasifike magari? Wanaokaa huko sio watu? Wanafikaje huko kama magari hayatakiwi? Hapana nilazima nifike, tena usiku huu huu iwe kwa mtutu au kwa hiyari ya mwanamke yule. Aliwaza Muddy Huku akiipungia mkono tax moja iliyokuwa ikipita mbele yake.

******

Wa kwanza kuingia alikuwa Jenipher, akashangazwa na ukimya wa pale ndani. Cha kwanza alichokifanya ni kuingia ndani ya chumba ambacho walimuacha Muddy. Aliusukuma mlango taratibu na kuruhusu macho yake yatembee ndani ya chumba kile. Kwa kuwa chumba kilikuwa giza hakuweza kuona kitu, akaufungua mlango zaidi na kuingia ndani, bado ukimya uliendelea kutawala, akaiendea swichi ya kuwashia taa.. Sekunde mbili baadae alikuwa akiangaliana na kitanda kitupu pasipo uwepo wa Muddy. Hilo likamshangaza Jenipher, Muddy alikuwa mgonjwa, Muddy hakuwa na nguvu za kupambana kwa muda huu kama alivyoeleza Mwanaharamu. Kitendo cha Muddy kutoweka ndani pasipokuonekana uwepo wa mvurugano ndani ya chumba. Hapo pakatoa imani kuwa Muddy hakuwa ametekwa bali alikuwa amekwenda sehemu. Sehemu ambayo haikuwa nzuri na haikuwa na usalama kwake. Ile kauli ya mwanaharamu kuwa Muddy asingekuwa na nguvu ya kupambana kutokana na kuchomwa sindano yenye sumu kali, ilimpa hofu, hofu ya kutokurejea tena kwa muddy. Wakati akiliwaza hilo mlango ukasukumwa, Akaingia Neema Habibu (r.i.p luv) naye akaungana na Jenipher kushangaa.. kushangaa kutokuwepo kwa Mohammed. Punde Mwanaharamu naye akaingia, alipozisoma nyuso za wasichana wale akagundua kile ambacho kilikuwa ndani yao. Hakuongea kitu zaidi ya kuitoa simu yake kisha kubofya namba kadhaa muda mfupi simu yake ilikuwa sikioni. Punde wakausikia mlio wa simu ukitokea ndani ya chumba kile kuonyesha kuwa Simu ya Mudy ilikuwa ndani ya chumba kile tena kitandani. Wakatizamana kabla ya Mwanaharamu kupiga hatua kuifuata pale kitandani. Alipoifikia akaichukua na kuitizama.. kutizama kwake akakutana na kitu cha kutisha, kitu ambacho kilimfanya ashtuke, mashtuko ambao ulipokelewa na wasichana wale. Macho ya Mwanaharamu yalikuwa yakitizamana na picha ya kichwa kitupu cha Sohwa Richardson. Haukufichika mshtuko kwa kuwa hakukitegemea kitu kile. Neema na Jenipher wakasogea.. macho yao yakatizama kwenye kioo cha simu ya Muddy, ukelele ukasikika kutoka kwa Neema Huku Jenipher akijibweteka chini kama mzigo. Hakutarajia kukutana na kitu kile. Ulikuwa ni muda mfupi tu tokea walipoachana jana. Leo alikuwa akiangaliana na kichwa cha rafiki yake akiwa ameuawa kinyama. Jenipher akasimama na kuuendea mkoba fulani ambao ulikuwa ndani ya chumba kile. Alipoufikia akauchukua na kuufungua. Akakitoa kitu kama cd na kurudinayo mpaka pale waliposimama Neema na Mwanaharamu. Akanyoosha mkono kumkabidhi Ile disc. Baada ya hapo mwanaharamu akaiendea kompyuta na kuitumbukiza ile disc. Punde yakaja maandishi makubwa yaliosomeka kama VICTORIA BASE.. Wote wakatizamana. Baada ya maandishi yale yakafuatia maandishi marefu sana.. ilikuwa makala ambayo ilikuwa ikieleza mazingira na ulinzi ambao ulikuwa ukiendelea ndani ya kambi hiyo iitwayo Victoria. Ilikuwa kambi ambayo ipo nje kidogo ya jiji la Vancouver katika mji mdogo wa victoria. Lilikuwa eneo ambalo lilikuwa likilindwa na mashirika makubwa ya kijasusi, mashirika ambayo haikujulikana kwa wananchi kwa nini hutumia ulinzi kiasi kile. Yalikuwa maelezo mengi yaliowaburudisha sana, kila mmoja alimshukuru Sohwa kwa kile alichokifanya. Kwa mara ya pili mwanaharamu akaitizama picha ya kichwa cha Sohwa iliotumwa kupitia simu ya Muddy. Kwa mara ya kwanza akajikuta akiiapia ile picha.

"Kazi ulioifanya ni kubwa sana Sohwa, hii inaonyesha hukuwa mbaguzi kwa watu weusi. Ulipigana kwa kuisaidia afrika licha ya uzungu wako. Umehatarisha maisha yako sababu ya Tanzania. Tangulia Sohwa, nenda ukiamini kuwa aliyeufanya unyama huu yupo nyuma yako anakufuata. Hata kama sio kwa mkono wangu basi utakuwa mkono wa mmoja kati yetu. HUKUSTAHILI KUFA KIFO HIKI". Wote wakasimama na kutizamana kwa muda kisha Mwanaharamu akasema.. "Acha nikamrudishe Muddy hapaswi kupambana kwa sasa." Akatoka nakuubamiza mlango.

**********

Ukimya na minong'ono kwa mbali ndio sauti pekee zilizosikika baada ya kushuka nje ya hoteli. Akatembea kama mteja wa kawaida akaongoza moja kwa moja mpaka ndani ya hoteli. Akapanda ngazi mpaka mapokezi ambao alipokelewa na msichana ambaye hakuwa mmoja kati ya wale ambao aliwakuta. Akasogea karibu kabisa na kwa sauti ya unyenyekevu Muddy akasabahi.

"Habari mrembo? "

"Salama tu kaka, lakini mbona miye sio mrembo!" Akajibu mwanadada yule huku tabasamu likichanua.

"Aliyekwambia wewe sio mrembo amekudanganya, tena ulivyoumbwa natamani kama tungekuwa wote kitandani muda huu." Mudy akaongeza na kumfanya yule msichana aangue kicheko kikubwa. Muda wakati akiongea na msichana yule wa mapokezi, macho yake yalikuwa yakizunguka pande zote pasipokumuona mtu anayemhitaji.

"Kuwa na mimi haiwezekani, kama unahitaji chumba nikusaidie. Safari hii akajibu yule msichana huku akiwa tofauti na mwanzo. Muda huu alikuwa hataki kabisa utani. Macho yake yalikuwa yakimtizama Muddy kama ukiyaangalia kwa uoga, lakini kwa Mudy aligundua macho yale yalikuwa yakitizama mahali, na si kutizama tu, bali yalikuwa yakipokea amri kutoka kule jicho la Mhudumu lilipokuwa likitizama.

MUDDY NAYE AKAGEUKA
 
MKE WA RAIS

MWANDISHI IBRAHIM MASIMBA

Muddy akageuka kufuata uelekeo wa macho ya binti yule. Uelekeo ambao ulibadilisha sura ya mwanamke yule. Lakini cha ajabu hakumuona mtu wala kukiona kitu. Hapakuwa na kile alichokihisi, hakuona mtu ambaye alitarajia. Akageuka katika muda ule ule wa sekunde mbili. Akakutana na tabasamu tena la mwanadada yule. Muddy hakuongea kitu bali aliondoka pale akiwa kwenye tahadhali kubwa. Aliamini kuna macho ya watu mahala yakimtizama. Mikono ikawa tayari kwa mapambano huku miguu ikiwa tayari kwa mateke. Akamuacha mwanadada yule akishindwa kuuficha mshangao wake. Hakumjali na hakumtilia manane. Safari yake ikaishia upande wa bar katika hoteli ile. Alichokifanya nikutafuta sehemu nzuri yenye uwezo wa kumuonyesha mlangoni mwa hoteli. Akakaa hapo kisha kumuita mhudumu ambaye alikuwa umbali wa hatua mbili. Mhudumu akasogea kwa hatua za madaha, alipomfikia Muddy akainama kumsikiliza. Wakati binti yule akiinama, macho ya Muddy yakavutiwa na kitu ambacho kilikuwa ndani ya mavazi ya mwanadada yule. Nyaya ndogo nyembamba zisizoonekana zilipita katika mavazi yake. Nyaya za mawasiliano yanayotumiwa na wanausalama wengi duniani.

"Naomba Nisaidie Maji."hatimaye Muddy akatamka. Binti hakujibu kitu bali aliondoka na punde akarudi akiwa ameshikilia chupa ya maji mkononi. Alipofika akaiweka juu ya meza na kuondoka bila kuongea kitu. Hilo lilikuwa jipya kwa Muddy, hakuna mhudumu wa aina ya binti yule aliemhudumia muda mfupi uliopita. Wakati wahudumu wakisifiwa kwa ukarimu, huyu alikuwa tofauti kabisa. Alionekana hakuwa mmoja kati ya wafanyakazi, bali yuko pale kwa kazi nyingine tofauti. Hata mawasiliano ya siri ambayo yalifungwa kwenye mavazi yake lilikuwa ni jibu tosha kwa Muddy kuwa pale amehudumiwa na Jasusi. Hilo likampa umakini, macho yake yakatua juu ya watu wawili ambao walikaa kwa pembeni yake. Mmoja kati ya watu hawa alikuwa ni yule mwanadada, mwanadada ambaye alimuhitaji kwa Safari ya VICTORIA BASE. Hakuonyesha kama alimuona na hakuonyesha kama alikuwa akimfuatilie Yeye. Bali alimuona akipiga soga na mtu ambaye alikaa naye. Umakini ukaongezeka, mkono wake ukashuka taratibu na kuigusa bastola yake. Hapo akaendelea kujiweka tayari tayari. Akaendelea kutizama kwa chati, akitizama kuelekea kule mlangoni na mara moja moja akimtizama yule mhudumu.

Punde akawaona watu wawili waliokuwa wamekaa pembeni yake wakiinuka, kisha akawaona wakitoka pale na kuelekea nje kabisa. Hilo halikumfanya Mudy asimame kwa muda ule, bado macho yake yalikuwa yakimtizama yule mhudumu. Alitaka kujua kitu, kitu ambacho kingemhakikishia ukweli kama kina muunganiko kati yao. Macho yake sanifu yakatembea kwa umakini usoni kwa mwanadada yule. Akitafuta kukiona kile ambacho hakikuwa rahisi kukiona. Kila alipojaribu kuangalia hakukiona kitu kutoka kwa mwanadada yule. Bali akashangazwa na tabasamu, tabasamu usoni kwa mwanadada yule
Halikuwa tabasamu la kumpumbaza Mohamed, halikuwa tabasamu la kufurahia kitu, la hasha, lilikuwa tabasamu lenye dhihaki juu ya Muddy. "Amenitambua mimi ni nani, lakini hata kama mwenzake ataondoka huyu ndiye atakaye nipeleka."aliwaza Muddy huku sasa akihamisha macho na kutizama mlangoni. Hapo macho yake yakakutana na mtu mwingine akiingia.. "Mwanaharamu!" Akanong'ona Muddy. Yeah alikuwa akitizamana na Bhatalon Nemisis (mwanaharamu) wakati akiingia pale bar. Akamuangalia mpiganaji yule kwa muda mrefu akajikuta akisahau kuwa palikuwa na mtu ambaye alikuwa akimfuatilia. Hata alipokuja kugeuka kutizama pale hakumuona tena yule mhudumu bali kulikuwa na sura mpya. Alikuwa ametoweka katika aina fulani ambAyo hakuitegemea kabisa. Akarudisha macho kutizama pale alipo mwanaharamu. Naye hakumuona alikuwa ametoweka. Muddy akawaza na kuwazua, punde alikuwa akisimama naye akitoka nje ya bar. Kwa mara ya pili akielekea pale mapokezi.

*******

Aliingia pale bar mapema sana, aliingia kama wateja wengine na kuvuta kiti kishakukaa. Akamuita mhudumu na hata alipokuja kuhudumiwa hakuona cha ajabu kuhudumiwa na Jasusi. Aliujua mpango mkakati wa mataifa haya matano kuhusu kilichotokea Tanzania, hivyo hakushangazwa na kurundikwa kwa majasusi wa hali ya juu katika kila hoteli hasa baada ya kugundulika uwepo wa wapelelezi kutoka Afrika. Wakati akiendelea kuwepo hapo ndipo alipomuona Mudy akiingia pale bar. Baada ya Muddy kuingia haukupita hata sekunde tano wakaingia watu wawili tena wanawake. Uingiaji wa wanawake wale ulimvutia sana Mwanaharamu, kwani walionyesha hata wao ni wa moja katika kile ambacho kinatendeka Kuhusu Tanzania. Macho yake yakaifanyakazi ya kuwatizama wale watu wawili. Aliwatizama kwa muda kisha akaamua kutoka ndani ya bar na kurudi kwa mara ya pili. Alitoka akipitia mlango mwingine na akarudi kupitia mlango wa kawaida, hapo ndipo alipoonana na Mudy na hapo ndipo alipomuona Mhudumu Yule akitoka. Naye akaamua kuunga kwa kumfuatilia nyuma.
 
nisaidieni kuelewa huyu mwanaharamu kajiungaje na kina muddy?
Jaribu kufuatilia episode zilizopita kulikuwa na mtu ambaye alikuwa akikutana na Mudy katika mazingira fulani huku Muddy akijiuliza maswali mengi kuhusu mtu huyo. Ingawa huko alikuwa yeye katika sura nyingine (wataalam wa tasnia ya ushushushu wanatambua) kin
rudia mkutano wa Nairobi kenya. Vitengo havifanyi kazi ya kuwatangazia fulani anakwenda sehemu. (Kumbuka KIKOSI CHA KISASI cha Elvis Musiba kuhusu yule msichana ambaye alikuwa akimuokoa willy gamba katika maeneo hatari) ujasusi uko hivyo
 
MKE WA RAIS

Mwandishi Ibrahim Masimba

Phone 0743990480

*******

Hakumuona mwanaharamu, hakuwaona mabinti wawili na kingine hakumuona mwanadada aliekuwa akihudumu. Wote walitoweka katika mazingira tatanishi, lakini kule kumuona Nemisis the bastard maeneo yale akatambua kila kitu kilikuwa mikononi kwa mwanaharamu, kila kitu kilikuwa kimesimamiwa na kichaa mwanaharamu katika fani ya ujasusi. Hakuinuka kwa haraka, bali bado alikaa akiendelea kutizama mlangoni. Watu walikuwa wakiingia na wengine kutoka, katika hali ya kustaajabisha kama sio kushangaza, akamuona Bastard akiwa sambamba na mwanamke aliyekuwa akihudumu muda mfupi uliopita. Mwendo wao na hatua zao hazikuwa na urafiki kati yao. Mudy ni jasusi alieiva kisawa sawa, alitambua kile ambacho bastard amefanya. Moyoni akatabasamu akaiona safari ya kuelekea Victoria Base imefika. Akaendelea kuwasindikiza kwa macho, baada ya kupotea katika upeo wa macho yake naye akasimama kuelekea tena pale mapokezi. Tabasamu lilikuwa usoni huku mluzi ukisikika mdomoni.. Hakuwa na wasiwasi, hakuwa na hofu wala woga, alikuwa akitembea kama yupo juu ya ardhi ya Tanzania, Ardhi iliobarikiwa kuwa na vitu vingi lakini visivyo na msaada kwa watu wake kutokana na tamaa kutoka kwa viongozi wakuu. Akapokelewa tena na msichana yule, msichana ambaye hapo mwanzo hakumuonyesha ushirikiano. Hakutaka kusimama hapo zaidi ya kuchukua ufunguo na kupandisha ngazi kuelekea chumbani kwake, muda wote hakutaka kuwaza wapi alipoelekea mwanaharamu sambamba na mwanamke yule mateka. Yeye shida yake ilikuwa kwa yule mwanamke mwingine, mwanamke ambaye alikuwa akimfuatilia hapo mwanzo, mwanamke ambaye alihusika kuvamiwa kwa dereva tax kisha kuawa. Mwanamke ambaye alimuona kwa macho yake. Akazimaliza ngazi na kuifuata korido ambayo ilimfikisha mlangoni mwa chumba chake, kabla hajafungua aliupita kwanza mlango na kupitiliza mbele kana kwamba anaelekea eneo tofauti la hoteli ile. Hakuwa na wasiwasi wowote bali alitaka kujua kama yupo peke yake ama kuna watu waliokuwa wakimfuatilia kwa nyuma. Hazikupita dakika mbili akawaona watu watatu wakitembea kuelekea mlangoni mwa chumba chake, akatulia huku macho yake yakicheza kila sehemu. Akawaona mmoja kati ya watu wale akiuendea mlango na kuugusa, akatulia kwanza, muda mfupi akamuona mtu yule akichomoa kitu mfukoni, akaonekana akichomeka kwenye kitasa, mlango ukafunguka akashuhudia mtu yule akiingia huku wale wawili wakibaki pale pale wakitizama huku na huko. Muddy akaendelea kutulia hapo. Sekunde kumi na tano baadae akamuona mtu yule akitoka kisha kuufunga mlango, wakaondoka wote watatu. Baada ya watu wale kuondoka Mudy akaamua kurudi pale chumbani.

Aliufungua mlango taratibu, akaingiza uso kisha ukafuatia mwili. Macho yake yakatizama kila upande na kona ya chumba kile. Hapo macho yake yakakiona kitu, kitu ambacho kilitegwa penbeni kabisa kwa kitanda. Akaanza kuipiga hatu ya kwanza, akaipiga ya pili kukifuata kitu kile, lakini kabla hajakifikia masikio yake yakanasa kitu, kitu ambacho kiliufanya mkono wake ushuke mpaka alipoihifadhi bastola yake. Ilikuwa michakato ya miguu ya mtu nje ya mlango wa chumba. Hakutaka kudharau mawazo yake, kushuka kwa mikono yake kukaambatana na kugeuka nyuma.. akashtuliwa na mlango kusukumwa kisha mtu mmoja kuingia huku mkononi akiwa amekamatia Bastola. Hakufanikiwa kumfikia, kwani muda ule ule mtu yule akaruka hewani na kumzoa Muddy, wote wakaenda chini mithili ya mafurushi. Bastola ikamponyoka Muddy na kuangukia umbali wa hatua nne. Hapo ndipo zilipoanza kupigwa pale chini, yalikuwa mapigano makali, mapigano ambayo yalionyesha kuelemewa kwa Mohammed. Alikutana na kisiki cha mpingo, alipigwa ngumi na mateke na hata aliporusha ngumi, alihisi nguvu kumuishia huku macho yake yakiingia giza. Kila sekunde alikuwa akipoteza fahamu, hakuwa Mohammed yule, hapa alionekana kama mlevi na asie na chochote.. akatulia huku damu zikimvuja mdomoni na puani. Hakuwa na uwezo huo tena

Muda mfupi wakaingia watu wengine wanne, kila mmoja alieingia aliuadhibu mwili wa Mohamed ambao ulikuwa umelala bila kuwa na fahamu. Baada ya kuhakikisha Mudy ametokota na hakuwa na madhara tena wakamfunga kamba miguuni na mikononi kisha akatiwa kwenye mifuko maalum, baada ya hapo akabebwa begani na kutolewa kama mzigo. Walipita naye mapokezi na kutoka naye nje kabisa ya hoteli. Wakaelekea mpaka sehemu ambayo walipaki magari yao. Mlango mmoja wa gari ukafunguliwa Mudy akatupwa kama furushi, kisha mlango ukafungwa tena, muda mfupi msululu wa magari ulikuwa ukiliacha Jiji la Vancouver safari hii wakielekea ViCtoria Base. Licha ya mudy kupoteza, fahamu lakini bado majasusi wale hawakutaka kufanya ujinga. Ingawa Muddy alikuwa ndani ya mifuko maalumu ya kuwekea maiti lakini bado wanaume watatu wenye bunduki kubwa za kivita walikuwa wametulia pembeni ya mwili wake huku midomo ikielekezwa kwake.

**********

Kilikuwa chumba kidogo sana na chenye kiza kizito sana, harafu ya kifo, damu, mikojo na kinyesi ilisikika kila upande. Maji machafu yaliomwagwa chini hakikuwa kitu kigeni katika chumba kile. Chini ya sakafu ya chumba kile ulionekana mwili wa mwanamke uliolazwa pasipokuwa na hata nguo moja. Ulionekana kama mwili usiokuwa na uhai, ulionekana ni mwili wa mtu ambaye alipata mateso makali sana. Hakuonyesha kama alikuwa na Uhai, damu zilikuwa zikichuruzika mwilini kama maji, mwili wake mzuri ulikuwa umejaa majeraha kila kona, majeraha ambayo hayakumpa nafasi ya kuishi tena. Hakuwa mwingine bali Sylvia Badenshok mwanamke aliyekuwa ametekwa na Nemisis the bastard wakati alipokuwa akihudumu katika hoteli fulani. Licha ya kuteswa kwa kila njia lakini hakuinua kinywa chake kujibu maswali alioulizwa. Muda wote alikuwa akiteswa huku akiwetemea mate wetesaji. Hakufumbua mdomo juu ya wapi ilipo kambi ya victoria, hakufumbua mdomo wa kutaja ni wapi walipo viongozi waliokuwa wamepanga kufanya mapinduzi. Kikubwa alichowaambia ni kwamba Watakufa hata kabla hawajafanikisha wanachokitaka kwani Ilikuwa Vigumu kupambana na Majasusi wale kisha kurudi hai. Yalikuwa maneno ambayo hayakukubalika ndani ya Kichwa cha Mwanaharamu. Hakuwahi kushindwa kufanya kitu na kikafeli.
 
We ni noma mkuu, una kipaji haswa. Ila naomba unisaidie, Canada wanaongea kiswahili? Maana naona wote wanatiririka kiswahili
 
Back
Top Bottom