Riwaya: Mke wa Rais

MKE WA RAIS

Mwandishi: Ibrahim Masimba

*****
Kilikuwa kitu kigumu kukiamini kwa wakati ule. Hakuamini kama mwisho wa Sohwa ulikuwa wa aina ile. Chozi likashuka huku mikono yake ikijikunja na kutengeneza kitu mfano wa ngumi. Macho yake yaliolowa machozi bado hayakuganduka kwenye kioo cha simu. Bado yalikuwa yakiitizama picha ya kutisha, picha ya mtu shujaa. Picha ya mpiganaji aliejitolea kuisaidia Tanzania licha ya kuwa katika Idara nyeti ya Ujasusi katika shirika kubwa kama KGB. Akaitamani ingekuwa ndoto, alitamani ingekuwa ni kitu kisichokuwa cha kweli. Hilo halikubadilika, bali alikuwa akiitizama kichwa cha Sohwa, kichwa kisicho na kiwiliwili. Mudy akainuka na kuuendea mkoba wake, hapakuwa na sababu ya kujificha tena ikiwa watu wanaomsaidia wanauliwa kinyama. Ni nani amemuua Sohwa? Ni vipi wamegundua kuwa yupo pamoja nao? Kwa nini wameamua kumtumia yeye picha za kifo cha Sohwa? Yalikuwa maswali lukuki yenye majibu machache. Jibu ambalo lilimfanya ajione ni mpumbavu kupoteza muda. Tayari alikuwa amejulikana, tayari alikuwa anasakwa. Kama Sohwa ameauwa kisha yeye kutumiwa picha hii ilimaanisha kwamba anajulikana na baada ya hapo kinachofuata ni mtafutano. Hilo hakuliogopa. Akaufungua mkoba wake na kutoa bastola zake mbili pamoja na vitu vingine vingi. Baada kutoa vitu vile aliupima mwili wake kama ulikuwa na nguvu za kupambana. Aliporidhishwa na hicho alichokifanya, akavaaa mavazi yake kwa haraka muda mfupi alikuwa akitoka akielekea sehemu ambayo alikuwa akiishi Sohwa. Kila alipokuwa akitembea bado picha alizotumiwa zilikuwa zikijirudia. Picha hizo zilimpa majibu kuwa watu wanaopambana nao walikuwa wanyama kupindukia.

******

Alipokelewa na ukimya wa kutisha katika nyumba ile. Hapakuwa na sauti ya kitu chochote. Ingawa ilikuwa ni asubuhi lakini hilo halikumtisha Mudy. Alitaka kumuona rafiki yake kipenzi. Alitaka kumuona mpiganaji mwenzie hata kama atakuwa mfu. Funguo zake za kufungulia aina zote za milango zikaifanya kazi yao, zikaifanyakazi ya kufungua mlango baada ya mlango. Ukimya wa jengo lile ukailazimu mikono yake kuifuata bastola ilipo na kuikamatia. Hapo akasogea kwenye sebule pana, sebule ambayo aliikuta ikiwa katika hali ambayo ilisadifu kile ambacho kilitokea hapo. Matone ya damu na mburuziko wenye damu ulionekana mbele ya Mohamed. Kengele za umakini zikazidi kugonga kichwani. Sebule yote ilikuwa ikinuka harufu ya damu. Vitu vilipasuliwa na vingine kutupwa ovyo. Mudy akatumbua mapambano ambayo yalikuwepo kabla ya kifo cha sohwa. Akaipita sebule akiufuata mburuziko ule. Bastola mkononi, bastola ikiwa tayari kwa chochote, mwili ulikuwa huru katika kupambana. Macho yaliangalia sehemu zote huku masikio yakiwa huru kunasa hata kama ni mende wanatembea. Akaufuata ule mburuziko akiamini angeweza kuukuta mwili wa Sohwa. Mburuziko ukaishia nje ya chumba ambacho mlango ulikuwa wazi. Macho yakapokelewa na mwili wa mtu uliolala katika dimbwi la damu. Akasogea huku kidole kikishula rasmi mpaka kwenye kitufe cha kufyatulia Risasi. Akasogea tena na tena. Alipofika karibu, akagundua kuwa alikuwa mbele ya mwili wa Sohwa ambao ulikuwa hauna kiwiliwili. Akahisi chozi likimtoka, chozi la kiume. Wakati anataka kuinama kuuchunguza mwili wa Sohwa, akausikia mlango wa nyumba ile ukifunguliwa, kisha zikafuatia sauti za kunong'ona. Mudy akatulia na kutega sikio. Licha ya kutega sikio lakini hakuweza kunasa kitu chochote kuhusu kinachozungumzwa na watu hao. Akiwa bado hajajua afanye nini, akasikia vishindo vikisogea kule alipo. Ukauruka mwili wa Sohwa kisha kuingia ndani ya chumba kile. Punde akawaona watu wawili wakiingia kila mmoja akiwa na SUB MACHINE GUN mikononi. Bado aliwaangalia wakati wanakuja, bado aliwasubiri wamfikie karibu. Ingawa alikuwa na uwezo wa kuwatwanga risasi lakini hakutaka kufanya hivyo, hakutaka kuharibu risasi zake. Watu wale wakatifika pale wakiwa wanaongea.

Mudy bado hakutaka kufanyakitu kwa haraka. Alihitaji kutuliza kichwa ili awezekuwamaliza kwa urahisi. Damu ya sohwa aliibeba mikononi mwake, aliapa kulipa kisasi kwa yeyote aliyehusika na kifo cha kinyama cha binti huyu shupavu. Watu wale bado waliendelea kuongea huku wakiwa wamejisahau. Mudy akautumia muda huo kujitokeza mbele yao, kilikuwa kitu ambacho kilifanyika ndani ya sekunde, muda huu walikuwa

Wamesimama wakiwa wawili, ndani ya sekunde walikuwa wamesimama wakiwa watatu, tena mtu wa tatu alikuwa mwanamume mweusi ambaye macho yake yalisadifu kile ambacho wao walikijua. Hayakuwa macho ya utani na hayakuwa macho ya mzaha. Sura yake iliongea kifo na macho yake yaliongea kukosekana kwa huruma. Haikujulikana ulikuwa muda gani lakini wote walijikuta wapo chini wakigalagala.hawakuchelewa kuinuka kwa sarakasi, lakini haikusaidia kitu, mateke mfululizo yalitosha kuwarusha tena chino. Hakusubiri wasimame, mikono yake miwili ikafanyakazi ya kunyonga shingo za wakora wale. Hakuwa na huruma tena. Alipohakikisha amewamaliza akawepekua, baada yakupata kile ambacho alikihitaji aliugeukia mwili wa Sohwa uliokuwa umelala katikati ya dimbwi la damu, akachuchumaa na kuweka kidole katikati ya dimbwi lile la damu, lakini wakati akifanya hayo mlango ukasukumwa kisha akawaona watu wakiingia katika aina ambayo ilimpendeza Moyoni na hata machoni.

KUMEKUCHA
 
[QUOT="Maarifa, post: 19173559, member: 646"]jitahidi twasubiri isije ikawa kama isindingo!!!! haiishi[/QUOTE]
Yeah Inaweza kuwa isidingo
 
MKE WA RAIS

Na ibrahim Masimba

Ulikuwa mchezo aliyoupenda na ulikuwa mchezo ambao ulikuwa ukimsisimua sana.. Hakuwahi kuogopa mapambano hata Siku Moja lakini Uingiaji wa makomandoo wale katika namna ya Zigzag kwa mara ya kwanza kulimfanya Mudy atambue Ugumu wa kitakachotokea. Alipenda sana kupambana katika aina flani ya Ugumu lakini haukuwa Ugumu wa kukabiliana na makomandoo. Akaendelea kuivuta muda, kuuvuta katika Aina fulani ya Kujipanga kuondoka pale.. Lakini angeondokaje palr? Hakutaka kufanya papara. Akaendelea kutulia.. Mara kikatokea kitu ambacho alikitarajia, kitu ambacho alijua ni mtego kwa makomandoo wale... Muda mfupi uliyopita Nyumba Ilikuwa ikiwaka taa lakini Ndani ya Muda huu jumba Zima lilikuwa giza.. Kisha Milio ya Risasi ikasikika na kufuatiwa na Mayowe ya Watu.. Damu Zilimsisimka.. Damu Zikamsimama na Hamu ya kupambana Ikaongezeka. Alikuwa akiipenda sana Michezo Ile. Mkononi kulikuwa na Bastola aina ya 38 special colt ikiwa na Risasi za Kutosha. Akasimama ili kuliacha jumba lile kabla ya Taa kuwashwa. Akainuka katika Aina ya Kipepeo na Kutembea kwa kunyata kama mfano wa paka anaponyatia paja.. Macho yake yaliyozoea giza yalikuwa yakizunguka kutizama katika kuhakikisha usalama wake.. Bastola yake Ya Kirusi Ilikuwa mbele yake kwa kila Hatua anayopiga.. Akaufikia mlango kisha akajipenyeza na kuchungulia huku na Huko.. Bado palikuwa kimya.. Hakukuwa na dalili ya Uwepo wa mtu.. Akatoka katika jumba lile mfano wa kivuli na Kuuendea mlango wa Siri ambao alikuwa na Uhakika kuwa haukuwa ukijulikana kwa Watu wengine.. Alipoufikia Akabonyeza namba fulani mara akaiona Ardhi ikifunguka akaingia ndani na Ardhi kujifunga tena.. Kutoka Hapo akatembea mpaka Chumba Maalumu cha Silaha ambacho alikigundua baada ya kutembelea pale kwa muda wote ambao Sohwa alikuwa akiishi. alichokuwa anakitaka alipokiona akakichukua na Kusogea pembeni.. Kilikuwa kitu kidogo mfano wa kisoda... kitu ambacho alikitega ndani kwa siri pasipo Sohwa mwenyewe Kugundua.kilikuwa kitu ambacho kilikuwa na uwezo wa kurekodi matukio yote iwe kwa sauti au picha za matukio yote. Baada ya kukichukua kile kitufe akaamua kupekuwa ndani ya chumba kile cha siri. MUDA WOTE alikuwa Makini kwa kila kitu. Alikuwa makini kwa kila kitu ambacho alikuwa akikishika na kuvipekua. Wakati anataka kuchukua kitu fulani ambacho kilikuwa ndani ya mtoto wa meza akashangaa kuiona simu. Simu ambayo mara nyingi ilikuwa ikitumiwa na Sohwa. Hapo akatulia huku akifikiria kwanza. Kwani SOhwa aiache simu yake tena kwakuiweka ndani ya droo? Au iliwekwa humu kama mtego baada ya kumuua? Akaunyoosha mkono kisha kuichukua simu na kuziweka katika mifuko yake ya siri. Alipomaliza Alisogea mpaka kwenye chumba cha Silaha akatupa macho yake Hapa na kule macho Yake Yakaangukia kwenye bastola Moja ya Kirusi Daringer 41 na Sem-automatic ambayo ilitengenezwa Czechslovakia.. Akazichukua na Kuzikagua aliporidhika nazo akazichomeka kwenye mavazi Yake kisha Akachukua na Visu viwili ambavyo Vilikuwa na Uwezo wa Kuua mtu kwa umbali wa hatua ishirini.. akamaliza na Mkebe uliyojaa risasi, kisha akaanza kutoka kupitia mlango wa siri ambao ulikuwa chini kwa chini. Hakuwa na mashaka yoyote kutokana na kuamini kuwa hapakuwa na mtu yoyote. Akashuka kwenye ngazi na kutokea chini kabisa ambapo palikuwa na ukumbi mkubwa ambao Sohwa aliwahi kumwambia kuwa ni ukumbi wa mikutano. Alipofika hapo akatupa macho huku na huko lakini hakuona kitu. Alipotaka kupiga hatua, akahisi kukanyaga kitu kama maji, akaupeleka mkono wake kugusa lakini alijikuta akikiangalia kidimbwi cha damu tena mbichi kuonyesha mauaji hayakufanyika muda mrefu. Akaongeza umakini akifuatilia matone yale ya damu. Matone ambayo yalionyesha kulkuwa na mtu ambaye amejeruhiwa ama kuuawa. Akahesabu hatua za miguu yake, akahesabu mpaka ishirini bila kukiona chumba amakuona ukomo wa matone yale ya damu. Hakuchoka kufuatilia, bado alihitaji kumpata mtu aliemuua Sohwa. Mbele kidogo akauona mlango wa kioo, kuuona mlango ule kulifuatana na kuona ukomo wa matone yale ya damu. Hilo lilimpa mashaka na hamaki.. bastola ikatangulia na miguu ikafuatia kwa nyuma.. hatua moja bastola hatua mbili.. akausukuma mlango ule, ukamtii kwa kufunguka.. akaingia kwa kutanguliza kichwa na macho.. kiwiliwili kikafuata.. Akajikuta akitokea kwenye ufukwe.. ufukwe wa bahari, ufukwe ambao ulikuwa kimya na ufukwe ambao haukuonyesha uwepo wa watu. MUDY akashangaaa na kutokuamini.. hapakuwa na matone ya Damu

Mudy Akatembea taratibi huku Ufukwe wote Ukiwa kimya huku miale ya Taa ikiwa ina mulika kwa mbali.. Mudy, Akaamua kutembea huku macho Yake yakizunguka Kila Pembe... Aliumaliza Ufukwe ule akaingia kwenye makazi ya Watu huku bado akiwa na tahadhali kwa Kila Hatua.. Akaumaliza Salama Mtaa wa kwanza lakini Alipoingia mtaa wa pili Akaanza kuhisi kuwa Hayupo peke Yake.. Kulikuwa na Mtu ambaye alikuwa Akimfuatilia kwa nyuma.. Sku zote hakuwa mtu wa kudharau Hisia Zake... Aliziheshimu sana.. Akaendelea kutembea kwa Mwendo wa tayari kwa mapambano... Akapiga Hatua ya Kwanza, kisha Ya pili... Hatua ya Tatu Akageuka katika Silika Huku bastola Mkononi.. Lakini Alikuwa Amechelewa, amechelewa sana... Kwani sekundi ile ile Akajikuta Ameisalimia Ardhi, mbele yake akiwa amesimama mtu, mtu ambaye hakuonyesha Huruma machoni mwake..
 
MKE WA RAIS

Mwandishi Ibrahim Masimba

Mahali: Kigamboni, Dar es salaam.

*****
Akegeuka kwa silika huku bastola mkononi ikiwa tayari kuitumia pale inatakapo mlazimu, lakini haikuwa kama Alivyotarajia. Kwani Muda ule ule akajikuta akiisalimia ardhi baada ya kupigwa mapigo kadhaa ambayo yalimuingia sawia. Hakuchelewa kusimama, kusimama kwa sababu ya kupambana, aliposimama akakutana na mtu, mtu ambaye macho yake yalisadifu kile ambacho Mudy alikitambua. Hakuwa mtu wa masihara, hakuwa mtu wa utani na hata macho yake hayakuwa na kitu ambacho kiliitwa huruma. Alikuwa akitisha na kuogopesha.. licha ya mtu huyu kutokuonyesha mzaha, lakini Mohamedi alikuwa akitabasamu, tabasamu shadidi ambalo lilikuwa ni kitu kigeni machoni kwa mtu yule. Bado wakatizamana na bado hawakusogeleana, lakini wote walikuwa wakisomana. Ulikuwa muda pekee wa Mudy kufanyakitu cha haraka ili kuondoka eneo lile. Bado kazi yake ilikuwa ngumu, bado akikuwa akipambana kuhakikisha wanarudi salama. Akakitupia jicho kidole chake ambacho kilikuwa na damu ya Sohwa, kisha akahamisha jicho lake usoni kwa mtu yule, muda huo huo akapeleka mapigo kadhaa, mapigo ambayo yalipanguswa kama uchafu, mapigo ambayo hayakugusa hata vazi la mwanamume yule. Yote yalipita hewani huku mengine yakitolewa kwa mikono. Mudy akarudi safari hii akibadilisha mapigo kwa kutumia karate na kung fu kwa pamoja. Yalikuwa mapigo yaliodumu kwa dakika tano bila pigo lolote kuingia kwa mtu yoyote. Kufika hapo kwa mara ya kwanza Mudy akakili kukutana na mtu mgumu. Hapo ndipo alipoamua kupambana pasipo kumtegea. Aliamua kutumia mapigo ya kila aina. Hilo likaonekana kufanikiwa, kufanikiwa kwa kuwa sekunde tatu tu, Alifanikisha kumuangusha mwanaume yule. Alipotaka kuinuka ilikukabiliana na mudy, akajikuta akisalimiana na mateke mfululizo, mateke ambayo yalimtupa tena chini safari hii akijibamiza kichwa ukutani. Hakuinuka kwa muda huo na hapakuwa na dalili za kuinuka tena. Mudy akamuendea na Kumkwida shingo na kuanza kumtingisha.

"Nambie umetumwa na nani?" Akauliza mudy huku akiendelea kumgongesha ukutani. Lakini mtu yule hakutoa majibu.

"Niambie nitakuua!"
Lakini bado mtu yule hakujibu. Alichokifanya Mudy ni kuchomoa bastola yake, kisha bila kuuliza akafyatua risasi ambazo zilitua kichwani na kukisambaratisha kichwa cha mtu yule. Baada ya kummaliza mtu yule, Mudy hakutaka kuchelewa, alichapua haraka na kuondoka sehemu ile akipanga kwenda kumtafuta Jenipher kwa kuwa hakuonana naye tokea walipoonana usiku uliopita akiwa sambamba na Marehemu Sohwa. Alitaka kwenda kujua nini kimesababisha na alitaka kujua ilikuwaje Sohwa akauawa kisha picha ya kichwa chake kutumiwa yeye. Kila alipokuwa akitembea alihisi labda atamuona Sohwa, alihisi labda atamuona akitabasamu, lakini Sohwa hakuwepo tena katika dunia hii. Wakati akiendelea kuwaza kuhusu kifo cha Sohwa akakunbuka kuwa alikuwa na simu ya sohwa pamoja na kitufe maalum ambacho alikitega nyumbani kwa Sohwa. Kukumbuka vitu hivyo akaamua kutafuta sehemu tofauti ili akae na kutulia kisha kuanza kufuatilia kila kitu ambacho kilitendeka ikiwa ni pamoja na mawasiliano kabla ya kifo cha Sohwa.

Uamuzi huo ukamfikisha mpaka kwenye hoteli moja ambayo ilikuwa pembezoni mwa mji wa victoria nje kidogo ya jiji la Vancouver. Ilikuwa hoteli moja ya kawaida ambayo haikuchangamka. Watu walikuwa wengi kiasi chake lakini licha ya wingi huo, lakini hapakuwa na kelele za aina yoyote. MUDY akaingia kwa mwendo wa taratibu huku macho yake yaliozoea kugundua kile kisichoonekana kwa urahisi yakizunguka huku na huko. Lakini mpaka anafika mapokezi hakugundua chochote kile ambacho kingempa mashaka. Akaongoza mpaka sehemu ambayo walisimama wadada wawili waliovalia sare.

"Habari zenu?" akasabahi

'"Nzuri, tukusaidie nini kaka? Wakajibu wote kisha kuuliza wote.

"Nahitaji chumba. Akajibu Mudy.

"Umepata kaka, lakini tungependa kujua Jina lako na wapi unatokea. Lakini pia hata ukitaka huduma ya penzi utapata." Safari hii alijibu mmoja kati ya wale wasichana.

"Naitwa James Brown, ni mwenyeji wa hapa hapa." Akajibu Mudy huku akimuangalia msichana mwingine ambaye alikuwa akiandika. Baada ya kukamilisha kilakitu na kupewa ufunguo, Mudy akaongoza akielekea chumbani kwake huku akisindikizwa na mhudumu mmoja.

Alitembea akiwa kimya mpaka walipokifikia chumba husika. Akaufungua mlango kisha kungia ndani. Hakutaka kumjali mwanamke yule. Lakini ameshaingia ndani akimuacha yule msichana nje ya mlango wa chumba chake akasikia sauti ya msichana yule ikipenya masikioni mwake.

"Kuwa makini kaka." Ya kauli ile msichana yule akaondoka akimuacha Mudy amesimama katikati ya chumba chake huku sauti ya msichana yule ikijirudia kichwani kwake. "KUWA MAKINI KAKA!" Hilo likajenga maswali kichwani mwake, akajikuta akimuhitaji yule mhudumu katika wakati ule na ndani ya muda ule. Lakini akaona afanye kwanza lile la simu ya Sohwa na kitufe kile. Baada ya maamuzi hayo, akaanza kukichunguza chumba kile kwa umakini, aliporidhika akajiweka kwenye kiti, kisha akaichomoa simu ya sohwa harafu akaiwasha. Muda mfupi baada ya kuiwasha akauona ujumbe mfupi ukiingia kwenye simu ya Sohwa. Akaufungua huku Moyo wake Ukipiga kwa mbali. Akakutana na ujumbe uliosomeka

"Naja Kuichukua Roho yako." Damu zikamsisimka. Punde ukaingia ujumbe mwingine ambao ulisomeka "Malipo ya usaliti ndio hayo" ujumbe huu wa pili ulionekana kumchanganya Mudy, kwani mtumaji aliutuma wakati ambao ulionyesha Sohwa alishauawa. Hilo likamfanya aiangalie namba ile ya mtumaji kwa makini baada ya hapo akaiandika pembeni kwa kuwa alitaka kuifanyiakazi. Baada ya hapo akaendelea kusoma kila sms. Kila namba ambayo aliitilia mashaka aliiandika pembeni tayari kwa matumizi ya baadae. Baada ya kumalizana na Simu, akakichukua kile kitufe kisha akakifungua.. wakati anaanza kuangalia kile kitufe, mlango ukagongwa..
 
a e i o u
ba be bi bo bu?
cha che chi cho chu?
tunapiga gumzo tu tukisubiri
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom