ibra87
R I P
- Jul 22, 2015
- 5,614
- 5,360
- Thread starter
- #921
MKE WA RAIS
Mwandishi Ibrahim Masimba
******
Hakuwa kushindwa kwa njia yoyote, hata yeye hakuamini kama binti yule aliweza kuvumilia mateso yote bila kusema chochote. Alishakutana na watu wengi wenye roho ngumu lakini kwa mwanamke yule ilikuwa ni habari nyingine. Alitumia mbinu zote lakini bado hakuambulia kitu. Akamuacha akiwa amelala kama mfu, akiwa amelala kama maiti, damu zilikuwa zimeunda mfereji na kwenda kutengeneza dimbwi kubwa. Mwili wa mwanamke yule haukutamanika kutokana na majeraha.. alilala mfano wa mfu.. licha ya mateso makali aliopitia lakini kamwe hakuufungua mdomo wake kusema chochote. Kwao ilikuwa ni bora kufa kuliko kuongea chochote kile. Hata mlango ulipofunguliwa na mtu kutoka ndipo hapo Sylivia alikumbuka kuwa alikuwa na kidonge kimoja, kidonge ambacho ilikuwa silaha ya mwisho kwao katika kujiangamiza hasa pale wanahisi kushindwa kuvumilia. Mkono wake dhaifu ukatambaa taratibu kuelekea sehemu ambayo kilihifadhiwa kile kidonge. Hakujali maumivu makali aliokuwa akijisikia kwa wakati ule, hakujali jeraha kubwa la risasi ambalo lilikuwa begani. Mkono ukafika sehemu husika na kutoka na kile ambacho kilikusudiwa. Punde kidonge kikapelekwa mdomoni pasipo kuonwa na mtu yoyote. Baada ya hapo akatulia akikisikilizia kile ambacho alikitegemea. Sekunde kumi mbele shingo yake ikalegea na kugeuka huku macho yakiwa wazi. Mapovu yalikuwa yakitoka mdomoni.. alikuwa maiti. MUda ule ule mlango ukafunguliwa, akaingia Nemisis the bastard. Alikuwa amekatia vitu vya kutesea mikononi. Lakini alipousukuma mlango kisha kuruhusu macho yake yatembee juu ya mwili wa mwanamke yule akagundua kuwa hapakuwa na uhai kwa mateka wake. Akasogea zaidi na zaidi mpaka ulipolala mwili ule usio na uhai. Povu lililokuwa likishuka mdomoni lilikuwa limempa majibu, majibu ambayo hakuyapenda. Alimtegemea huyu mtu ampe japo kwa uchache kuhusu huko Victoria. Lakini kabla hajapata chochote tayari mateka wake ameshakufa. Mwanaharamu akamtiza kwa muda mrefu pasipokuongea kitu. Hakutakiwa kuwepo pale tena, hakutakiwa kuzubaa au kushangaa, alitakiwa kujua ni wapi huko victoria. Akauangalia tena mwili wa mwanamke yule, akainuka na kuufunga mlango wa chumba kile. Akaondoka eneo lile akiamua kuelekea huko, akielekea kwenye moto wenyewe. Alitaka kuifanyakazi kwa mikono yake, alitaka kuifanya kazi kwa wakati huu. Na haikuwa kazi yingine zaidi ya kuisambaratisha VICTORIA BASE.
********
Alionekana kama msichana mchafu na ombaomba, alikuwa amesimama nje ya hoteli kubwa ya kifahari akionekana kutetemeka kwa baridi. Mavazi yake chakavu hayakuwa sababu ya kuuficha uzuri wake. Mavazi yake chakavu haikuwa sababu ya kulificha umbo lake. Alikuwa mzuri, mrembo na kilakitu ambacho kilikuwa ndani yake kilikuwa kizuri. Macho yake yalikuwa yakitizama ndani ya hoteli na wakati mwingine Nje. Hakuna ambaye alimtilia manani kutokana na mavazi yake husika. Lakini haikuchukua muda msichana yule kutoweka katika namna ambay hakuna ambaye alimuona. Hakuondoka kwenda popote bali kile ambacho kilitokea muda mfupi ndani ya hotel ile ndicho kilichomuondoa. Hata pale alipowaona watu watano wakitoka ndani ya hoteli huku wamebeba mifuko maalumu ya kuwekea maiti, yeye tayari alikuwa upande wa pili wa barabara macho yake yakiangalia kitendo kilichokuwa kikitendeka. Huyu alikuwa Neema Habibu. Alikuja muda mrefu sana akitizama hiki na kile ambacho kilikuwa kikifanyika. Maneno ya mwanaharamu kuwa Muddy hakuwa na nguvu za kutosha kupambana ndiyo yaliomfanya Neema kufika hapo akiwa sambamba na Mwanaharamu. Baada ya kufika hapo, yeye alifanyakazi moja ya kuhakikisha macho yake hayabanduki kule alipokaa Muddy. Ni wakati akilifanya hilo ndipo alipowaona watu watano wakiingia, ikiwa ni baada ya kumuona Mudy akielekea mapokezi. Hata pale Muddy alipoondoka pale mapokezi na kuelekea chumbani bado alikuwa akikitizama kile kitendo. Muda mfupi baada ya Muddy kuondoka pale mapokezi, akawaona watu wale nao wakielekea mapokezi na baadae kuelekea kule ambapo alikuwa akielekea Muddy. Kengele ya Tahadhali akalia kichwani kwake. Akajua watu wale lazima wanamfuata Muddy. Akatamani kwenda huko ndani akamwambie Muddy kuwa anafuatwa. Lakini mavazi yake hayakuruhusu hilo. Wakati akifikiria kipi ambacho anaweza kufanya, akawaona watu walewale wakitoka lakini safari hii wakiwa wamebeba kitu mfano wa mtu. Hapo hisia kuwa Muddy alikuwa msambweni zilimjia. Hapo akaamua kufanya kitu, kitu ambacho kilikuwa cha hatari sana. Aliamua kuzifuatilia gari zile ili kujua ni wapi zinaelekea.
**********
Alipotoka pale kwenye chumba alichomuacha yule binti akiwa tayari na zana zake za kazi. Mwanaharamu alikuwa ndani ya tax akielekea kule ambako aliambiwa na Neema kuwa kuna kitu kinaendelea. Alikuwa na bastola tatu katika sehemu tofauti. Alikuwa na visu vitatu, magazine tatu za risasi. Gari ilikuwa akitembea katika mwendo wa kasi, muda mwingi Mwanaharamu alikuwa akiwasiliana na Neema kujua kile ambacho kilikuwa kikiendelea. Upande wa Neema hata yeye alikuwa kwenye gari akiendesha mwenyewe. Alikuwa nyuma kwa magari matano kuepuka kushtukiwa mapema. Aliiacha magari yale yatangulie kisha yeye akifuatilia kwa nyuma. Bado alihakikisha magari yale hayampotezi.. lakini mwendo wa dakika kama kumi mbele, akakiona kitu ambacho hakukitegemea. Magari matatu ambayo alitoka nayo sambamba kule hotelini yote yakasimama na magari mengine yakipita barabara nyingine. Hilo kwake hakulitegemea, hakulitegemea kwa kuwa muda ule ule akausikia mngurumo wa helkopta, sekunde tano baadae akaiona milango ya gari zile ikifunguliwa, wakashuka wale watu watano wakiwa sambamba na mfuko wao. Helkopta ikazidi kushuka. Neema akatamani kusimamisha gari lakini akaogopa kushtukiwa. Akapita akishuhudia mwili wa mtu ukipakiwa ndani ya helkopta na muda ule ule helkopta ikapaaa na kutokomea.
Mwandishi Ibrahim Masimba
******
Hakuwa kushindwa kwa njia yoyote, hata yeye hakuamini kama binti yule aliweza kuvumilia mateso yote bila kusema chochote. Alishakutana na watu wengi wenye roho ngumu lakini kwa mwanamke yule ilikuwa ni habari nyingine. Alitumia mbinu zote lakini bado hakuambulia kitu. Akamuacha akiwa amelala kama mfu, akiwa amelala kama maiti, damu zilikuwa zimeunda mfereji na kwenda kutengeneza dimbwi kubwa. Mwili wa mwanamke yule haukutamanika kutokana na majeraha.. alilala mfano wa mfu.. licha ya mateso makali aliopitia lakini kamwe hakuufungua mdomo wake kusema chochote. Kwao ilikuwa ni bora kufa kuliko kuongea chochote kile. Hata mlango ulipofunguliwa na mtu kutoka ndipo hapo Sylivia alikumbuka kuwa alikuwa na kidonge kimoja, kidonge ambacho ilikuwa silaha ya mwisho kwao katika kujiangamiza hasa pale wanahisi kushindwa kuvumilia. Mkono wake dhaifu ukatambaa taratibu kuelekea sehemu ambayo kilihifadhiwa kile kidonge. Hakujali maumivu makali aliokuwa akijisikia kwa wakati ule, hakujali jeraha kubwa la risasi ambalo lilikuwa begani. Mkono ukafika sehemu husika na kutoka na kile ambacho kilikusudiwa. Punde kidonge kikapelekwa mdomoni pasipo kuonwa na mtu yoyote. Baada ya hapo akatulia akikisikilizia kile ambacho alikitegemea. Sekunde kumi mbele shingo yake ikalegea na kugeuka huku macho yakiwa wazi. Mapovu yalikuwa yakitoka mdomoni.. alikuwa maiti. MUda ule ule mlango ukafunguliwa, akaingia Nemisis the bastard. Alikuwa amekatia vitu vya kutesea mikononi. Lakini alipousukuma mlango kisha kuruhusu macho yake yatembee juu ya mwili wa mwanamke yule akagundua kuwa hapakuwa na uhai kwa mateka wake. Akasogea zaidi na zaidi mpaka ulipolala mwili ule usio na uhai. Povu lililokuwa likishuka mdomoni lilikuwa limempa majibu, majibu ambayo hakuyapenda. Alimtegemea huyu mtu ampe japo kwa uchache kuhusu huko Victoria. Lakini kabla hajapata chochote tayari mateka wake ameshakufa. Mwanaharamu akamtiza kwa muda mrefu pasipokuongea kitu. Hakutakiwa kuwepo pale tena, hakutakiwa kuzubaa au kushangaa, alitakiwa kujua ni wapi huko victoria. Akauangalia tena mwili wa mwanamke yule, akainuka na kuufunga mlango wa chumba kile. Akaondoka eneo lile akiamua kuelekea huko, akielekea kwenye moto wenyewe. Alitaka kuifanyakazi kwa mikono yake, alitaka kuifanya kazi kwa wakati huu. Na haikuwa kazi yingine zaidi ya kuisambaratisha VICTORIA BASE.
********
Alionekana kama msichana mchafu na ombaomba, alikuwa amesimama nje ya hoteli kubwa ya kifahari akionekana kutetemeka kwa baridi. Mavazi yake chakavu hayakuwa sababu ya kuuficha uzuri wake. Mavazi yake chakavu haikuwa sababu ya kulificha umbo lake. Alikuwa mzuri, mrembo na kilakitu ambacho kilikuwa ndani yake kilikuwa kizuri. Macho yake yalikuwa yakitizama ndani ya hoteli na wakati mwingine Nje. Hakuna ambaye alimtilia manani kutokana na mavazi yake husika. Lakini haikuchukua muda msichana yule kutoweka katika namna ambay hakuna ambaye alimuona. Hakuondoka kwenda popote bali kile ambacho kilitokea muda mfupi ndani ya hotel ile ndicho kilichomuondoa. Hata pale alipowaona watu watano wakitoka ndani ya hoteli huku wamebeba mifuko maalumu ya kuwekea maiti, yeye tayari alikuwa upande wa pili wa barabara macho yake yakiangalia kitendo kilichokuwa kikitendeka. Huyu alikuwa Neema Habibu. Alikuja muda mrefu sana akitizama hiki na kile ambacho kilikuwa kikifanyika. Maneno ya mwanaharamu kuwa Muddy hakuwa na nguvu za kutosha kupambana ndiyo yaliomfanya Neema kufika hapo akiwa sambamba na Mwanaharamu. Baada ya kufika hapo, yeye alifanyakazi moja ya kuhakikisha macho yake hayabanduki kule alipokaa Muddy. Ni wakati akilifanya hilo ndipo alipowaona watu watano wakiingia, ikiwa ni baada ya kumuona Mudy akielekea mapokezi. Hata pale Muddy alipoondoka pale mapokezi na kuelekea chumbani bado alikuwa akikitizama kile kitendo. Muda mfupi baada ya Muddy kuondoka pale mapokezi, akawaona watu wale nao wakielekea mapokezi na baadae kuelekea kule ambapo alikuwa akielekea Muddy. Kengele ya Tahadhali akalia kichwani kwake. Akajua watu wale lazima wanamfuata Muddy. Akatamani kwenda huko ndani akamwambie Muddy kuwa anafuatwa. Lakini mavazi yake hayakuruhusu hilo. Wakati akifikiria kipi ambacho anaweza kufanya, akawaona watu walewale wakitoka lakini safari hii wakiwa wamebeba kitu mfano wa mtu. Hapo hisia kuwa Muddy alikuwa msambweni zilimjia. Hapo akaamua kufanya kitu, kitu ambacho kilikuwa cha hatari sana. Aliamua kuzifuatilia gari zile ili kujua ni wapi zinaelekea.
**********
Alipotoka pale kwenye chumba alichomuacha yule binti akiwa tayari na zana zake za kazi. Mwanaharamu alikuwa ndani ya tax akielekea kule ambako aliambiwa na Neema kuwa kuna kitu kinaendelea. Alikuwa na bastola tatu katika sehemu tofauti. Alikuwa na visu vitatu, magazine tatu za risasi. Gari ilikuwa akitembea katika mwendo wa kasi, muda mwingi Mwanaharamu alikuwa akiwasiliana na Neema kujua kile ambacho kilikuwa kikiendelea. Upande wa Neema hata yeye alikuwa kwenye gari akiendesha mwenyewe. Alikuwa nyuma kwa magari matano kuepuka kushtukiwa mapema. Aliiacha magari yale yatangulie kisha yeye akifuatilia kwa nyuma. Bado alihakikisha magari yale hayampotezi.. lakini mwendo wa dakika kama kumi mbele, akakiona kitu ambacho hakukitegemea. Magari matatu ambayo alitoka nayo sambamba kule hotelini yote yakasimama na magari mengine yakipita barabara nyingine. Hilo kwake hakulitegemea, hakulitegemea kwa kuwa muda ule ule akausikia mngurumo wa helkopta, sekunde tano baadae akaiona milango ya gari zile ikifunguliwa, wakashuka wale watu watano wakiwa sambamba na mfuko wao. Helkopta ikazidi kushuka. Neema akatamani kusimamisha gari lakini akaogopa kushtukiwa. Akapita akishuhudia mwili wa mtu ukipakiwa ndani ya helkopta na muda ule ule helkopta ikapaaa na kutokomea.
