MKE WA RAIS
98
Alikiacha kifua wazi , kifua ambacho kilibeba matiti mazuri. Akayaacha matiti yaonekane kwa uwazi. Akajitokeza na kusogea pale huku akihakikisha macho ya walinzi wale yanamuangalia yeye. Hatua ya kwanza ikapita akitembea, na hata alipipiga hatu ya pili bado ilikwenda kama alivyotaka, Hatua ya tatu hakufanikiwa kuifikia. Sauti nzito ya kiume ikasikika kutokea nyuma yake. Ilikuwa sauti nzito yenye mamlaka. ''Usijali kusogea, ukifanya hivyo tutakifumua kichwa chako kwa Risasi''; sauti ikaingia ndani ya ngoma za masikio ya Jenifer, akasita kuipiga hatua ile ya Tatu. Mbele yake walinzi Watatu walikuwa wanenyoosha silaha kwake, na hata alipoangalia Nyuma aliwaona watatu wengine wakiwa na silaha zao mikononi. Jenifer Hakuonyesha kujali, hakuonyesha kuogopa bunduki za walinzi wale. Ndio kwanza alikuwa akijizungusha mfano wa changidoa, changudoa wa kiwango cha juu kama wale wa Ohio amba Africasana Pale Sinza. Mkono wake mmoja ukijuwa ukiipandisha sketi yake juu hadi kufikia Usawa wa Ilipo chupi yake. Paja lake lilikuwa likionekana waziwazi. Bado majasasi wale walikuwa wakimtizama, bado hawakuamua chochote cha kufanya, macho yao yalikuwa kwenye mapaja na kifuani kwa Jenipher. Wakasogea tena kwa tahadhali, Hatua kwa hatua kwa walinzi wa mbele na Nyuma. Wakamfikia Jenipher, wakamfikia huku kila mmoja macho yake yakionyesha kutamani kile ambacho yalikuwa yakikishuhudia. Sekunde mbili tatu walikuwa wakimshikashika Jenipher maeneo katika maeneo tofauti mwilini.
Hawakulijua walilokuwa wakilitenda, hawakuwa wakijua kile ambacho kingewatokea. Muda mfupi kitu kama mlio wa Alam Ukasikika kutoka kwa mmoja kati yao. Wakaipoteza Dakika katika kushangaa hilo. Lilikuwa nikosa kwa jasusi kama Jenipher. Mkono wake ukashuka kwa wepesi na kuifikia bastola. Sekunde ya pili cheche zilikuwa zikionekana huku walinzi wa nne kati ya Sita wakianguka Chini kila mmoja akiwa na Tundu la risasi Utosini. Kilikuwa kitu kilichofanywa katika Muda ambao haukutegemewa na Walinzi wale. Hata pale wengine wawili waliobaki walipotaka kujitetea hawakufika popote. Risasi nyingine zikazama Vifuani na kuwatupa chini. Hakusubiri hapo, akasonga mbele akielekea ndani ya Jengo lile. Muda mfupi alikuwa akichupa na kuangukia upande wa ndani. Akatulia kwa muda kama angewaona watu wakielekea pale, lakini utulivu bado Ulibaki pale pale. Hapakuonekana mtu, wala kitu Chochote kile. Bado utulivu ulikuwa pale pale. Akajiinua hapo na kusogea sehemu Nyingine. Kila wakati alikuwa akisoma Jina La Cosmass Derick kujua wapi chumba chake kilipo. Akaufikia Mlango wa kuingilia ndani kabisa ya Jengo. Akakinyonga kitasa akashangaa kuuona mlango ukifunguka ''HATARI'' Llilikuwa neno la kwanza kugonga kichwani kwa Jenipher. Hakujali, akaingia taratibu kisha kuurudisha Mlango bila kutoa Sauti. Akageuka Kuendelea na Safari ya kuitafuta lifi. Alikuwa akitembea safari hii bastola mbili mkononi. Akaifikia lift na kujitumbukiza Humo ndani, Muda mfupi baadae alikuwa akipelekwa Ghorofa ya Saba ambayo ndipo alipokuwa Akiishi aliyekuwa Gavana. Lift ikafika sehemu yake na Muda ule ule mlango Wa Lifti ukafunguka Jenipher akashuka. Wakati akishuka na kunyoosha kwenda upande mwingine, akapishana na watu watatu nao wakiingia kwenye Lifti. Kati ya hao mmoja alikuwa Sohwa, wakatizamana kwa nukta mbili kisha Kila mmoja akaushika uelekeo wake. Wakati Sohwa akielekea ndani ya lifti, Jenipher alikuwa akielekea Sehemu yake. Hakushangaa kumuona Sohwa hapo, na Hakushangaa hilo kwa kuwa, alishatambua kila kitu kilichokuwa kikiendelea. Sohwa Alikuwa mwenzao na Sohwa alikuwa kiunganishi katika Mpango wao wa kurudi na Wahaini. Akaendelea kutembea bila wasiwasi. Alijua alikuwa na Mtu, alikuwa na Jicho linalomtizama. Hakumuamini Mohamed Pale mwanzo alipomtambulisha kwa Sohwa lakini Kumuona Sohwa ndani ya Jengo Hili, kulimpa Imani, Nguvu na Uwezo wa kusonga mbele. Mbele katika kumchukua Yule mmoja, Mmoja ambaye atafuatiwa na Wengine kisha Wengine tena. Hilo ndilo wazo la Jenipher, Sohwa na Mohamed, Wazo la Tanzania kwanza na Wengine baadae. Aliufikia mlango wa chumba hicho kwa Urahisi Zaidi, akasimama Nje Ya Mlango kwa nukta kama kumi, Kisha akaushika Mlango na kunyonga kitasa. Mlango Ukamtii na Kumkaribisha Ndani, ndani ambapo alipokelewa na kile kilichofanya kengele ya Hatari Ilie kichwani Mwake. Kabla hajajua kipi cha kufanya, Akahisi kitu kizito kikitua Kichwani, kitu ambacho kilimpeleka Chini na kumpeleka katika giza, Giza ambalo lilimpoteza na kuhisi hakuwa katika Uso wa Dunia hii. JENIPHER AKATULIA TULIII