ibra87
R I P
- Jul 22, 2015
- 5,614
- 5,360
- Thread starter
- #621
MKE WA RAIS
******
alikuwa yule yule, yule aliepishana naye muda mfupi uliopita. Lakini safari hii akimuangalia na kutabasamu. Tabasamu halikumfanya Mohamedi ashindwe kugundua kile kilichopo nyuma yake. Nyuma ya tabasamu la urafiki, tabasamu linaloongea na kufikisha ujumbe sehemu nyingine. Licha ya tabasamu lote, lakini halikumyumbisha wala kumshtua Mohammed. Ndio kwanza alikuwa akiikwea Lifi kuelekea pale alipoambiwa afike. Pale alipotakiwa kwenda kuitafuta Zabibu. Yeah! Hilo ndilo ambalo lilipita katika kichwa cha Mohamedi. Lifti ikamuacha atelemke na kuambaa na korido moja matata sana. Alitembea kwa kujiamini, mikono yake ilikuwa tayari kuifikia bastola endapo angetakiwa hilo. Bado hapakuwa na upinzani wala hakumuona mtu wa kumtilia mashaka. Hapo akajipa imani ya kuamini, hatua nne kabla ya kuifikia sehemu Husika akahisi kitu, kitu ambacho hakikuwa cha kupuuzwa. Akagundua hakuwa peke yake, alikuwa akifuatiliwa na Mtu. Mkono ulikuwa ukishuka sekunde hii, sekunde ya pili Alikuwa akigeuka kwa Silika ya Aina yake. Lakini akakuta patupu. Koridoni hapakuwa na mtu wala paka. Kwa mara ya kwanza hisia zake zilimpoteza. Alichokifanya ni kupuuza, sasa alikuwa akielekea kwenye mlango wa Chumba kile alichoambiwa afike kwa mujibu wa kile kikaratasi alichokikuta pale Alipotoka.
Akauendea mlango na kuusukuma baada ya kunyonga kitasa, akaukuta ukiwa mgumu kuonyesha kuwa ulikuwa umefungwa kwa ndani. Nukta ya kwanza alikuwa iliukuta mkono wake ukiwa mfukoni, na Nukta ya pili ukatoka ukiwa umeshikilia Lundo la funguo. Akauchagua Mmoja na kuutumbukiza kwenye kitasa. Muda mfupi alikuwa ndani akitizamana na mwanamke alielala Chali kitandani akiwa Uchi wa nyama. Hakuonyesha kutingishika wala kugeuza shingo kuangalia mlangoni anapotokea Mohamed. Bado alionyesha kutulia kana kwamba hapakuwa na chochote kile. Hilo kidogo likampa hofu Mohammed. Kwa nini aonyeshe kutokujali ujaji wangu humu chumbani? Kwa nini haonyeshi kama kile alichokuwa anakionyesha kule club? Ana nini? Amefanywa nini? Yalikuwa maswali yaliokosa majibu wakati Mohamed akitizamana na Umbo la mwanamke Mrembo akiwa ametulia uchi juu ya kitanda. Mguu ulikuwa Huku na mwingine kule. Mohamed akakaza macho kutizama, Ghafla akaliona lile ambalo aliliwaza. Damu ilikuwa ikichuruzika kutoka pale kitandani kuelekea pembeni kabisa ya Kitanda. Mkono ulikuwa tayari umekamatia bastola yake katika utimamu. Akazipiga hatua kwa kuhesabu moja baada ya nyingine, macho yake yalikuwa yakiangaza chumba kizima yasimuone mtu. Akainua kichwa kulitizama Dali la Chumba kile. Akakiona kipande cha Sillingboard kikiwa kimewekwa pembeni. Upenyo mdogo wa kumpitisha Mtu ukionekana. Muddy akajua kuwa tayari mwanamke yule alikuwa ameuawa. Ameuawa na mtu aliyepita katika upenyo ule anaoutizama. Akatingisha kichwa huku akimsogelea mwanadada yule. Macho yakagota kwenye mpini wa kisu ubavuni kwa mwanadada yule. Hakutaka kusubiri, alirudi nyuma kisha kukiacha chumba kile huku mawazo mazito yakiwa kichwani. Alimtambua muuaji na alimtambua yeye alikuwa nani. Lakini kwa nini kila akiniona anatabasamu? Na kwa nini huwa anaua mtu ambaye alikuwa na miadi nami? Yeye anamsaidia nani? Kila kitu kilikuwa gizani, hakutaka kuamini kama mauaji yanayofanywa na Mtu yule ni vita ya kuwasaidiwa wao.
******
ukumbi ulikuwa kimya kila mmoja akiangalia mbele ya meza kuu. Waziri wa mambo ya Kigeni wa marekani na wenzake wa Urusi, Uingereza na Italia walikuwa wametulia wakiangaliana na wajumbe kutoka Tanzania wakiongozwa na Makamu Wa Rais Mzee Kilowoko. Waziri mkuu na mawaziri wengine wa Serikali ya Jamhuri Ya Muungano Wa Tanzania. Ukiwaondoa hao wengine waliokuwepo ni Mke wa Rais Wa Jamhuri Ya Muungano Wa Tanzania sambamba na watu wengine ambao hawakuwa wakijulikana. Kila mmoja alikuwa kimya akisikiliza maoni Juu Ya mpango mkakati wao waliouleta kuhusu kupewa nguvu ya kifedha na kiusalama kama maandalizi Ya kuipindua iliopo madarakani. Ulikuwa ni mkakati Uliosukwa kwa Muda Mrefu. Watu wengi walikuwa wamepandikizwa katika kufanikisha hilo. Ulikuwa ni Mkutano Uliofanywa kwa kificho Sana kwa Siri Nzito. Baada ya Muda wa majadiliano na mikakati ya kufanikisha mapinduzi Hayo, Nchi hizo nne zikaamua kutuma watu wao ambao kazi yao ilikuwa ni Kuratibu Mapinduzi na Kuhakikisha wanaua kila mtu ambaye angeonekana kuwazibia katika mpango huo. Ni katika Mkutano Huo uliozalisha mahusiano kati ya Mke wa Rais na mtu mmoja ajulikanae kwa Jina la Comrade Robert ambaye alikuwa ni Meja General Mstaafu katika jeshi la nchi. Uhusiano Huo Ulikuwa wa Siri sana, siri ambayo hata mheshimiwa Rais Hakuwa ameigundua. Uhusiano Huo Ukaanza kuleta mabadiliko makubwa kwa Mke Wa Rais, kila wakati alikuwa akiondoka Ikulu bila taarifa huku muda mwingi akimtumia Mkurugenzi Wa Idara ya Usala,a Wa Taifa kufanikisha hilo. Ni wasiwasi Huo Na mashaka kwa Mheshimiwa Rais ndipo alipoamua Kuwaajili Vijana Watatu ambao aliwaamini kwa kuwa walikuwa ni Watiifu kwa Rais. Hapo ndipo Alipowachagua captain George, Kanali Jamilah na Liutenant Sevenlee katika kufuatilia kilichopo nyuma ya safari hizo
******
alikuwa yule yule, yule aliepishana naye muda mfupi uliopita. Lakini safari hii akimuangalia na kutabasamu. Tabasamu halikumfanya Mohamedi ashindwe kugundua kile kilichopo nyuma yake. Nyuma ya tabasamu la urafiki, tabasamu linaloongea na kufikisha ujumbe sehemu nyingine. Licha ya tabasamu lote, lakini halikumyumbisha wala kumshtua Mohammed. Ndio kwanza alikuwa akiikwea Lifi kuelekea pale alipoambiwa afike. Pale alipotakiwa kwenda kuitafuta Zabibu. Yeah! Hilo ndilo ambalo lilipita katika kichwa cha Mohamedi. Lifti ikamuacha atelemke na kuambaa na korido moja matata sana. Alitembea kwa kujiamini, mikono yake ilikuwa tayari kuifikia bastola endapo angetakiwa hilo. Bado hapakuwa na upinzani wala hakumuona mtu wa kumtilia mashaka. Hapo akajipa imani ya kuamini, hatua nne kabla ya kuifikia sehemu Husika akahisi kitu, kitu ambacho hakikuwa cha kupuuzwa. Akagundua hakuwa peke yake, alikuwa akifuatiliwa na Mtu. Mkono ulikuwa ukishuka sekunde hii, sekunde ya pili Alikuwa akigeuka kwa Silika ya Aina yake. Lakini akakuta patupu. Koridoni hapakuwa na mtu wala paka. Kwa mara ya kwanza hisia zake zilimpoteza. Alichokifanya ni kupuuza, sasa alikuwa akielekea kwenye mlango wa Chumba kile alichoambiwa afike kwa mujibu wa kile kikaratasi alichokikuta pale Alipotoka.
Akauendea mlango na kuusukuma baada ya kunyonga kitasa, akaukuta ukiwa mgumu kuonyesha kuwa ulikuwa umefungwa kwa ndani. Nukta ya kwanza alikuwa iliukuta mkono wake ukiwa mfukoni, na Nukta ya pili ukatoka ukiwa umeshikilia Lundo la funguo. Akauchagua Mmoja na kuutumbukiza kwenye kitasa. Muda mfupi alikuwa ndani akitizamana na mwanamke alielala Chali kitandani akiwa Uchi wa nyama. Hakuonyesha kutingishika wala kugeuza shingo kuangalia mlangoni anapotokea Mohamed. Bado alionyesha kutulia kana kwamba hapakuwa na chochote kile. Hilo kidogo likampa hofu Mohammed. Kwa nini aonyeshe kutokujali ujaji wangu humu chumbani? Kwa nini haonyeshi kama kile alichokuwa anakionyesha kule club? Ana nini? Amefanywa nini? Yalikuwa maswali yaliokosa majibu wakati Mohamed akitizamana na Umbo la mwanamke Mrembo akiwa ametulia uchi juu ya kitanda. Mguu ulikuwa Huku na mwingine kule. Mohamed akakaza macho kutizama, Ghafla akaliona lile ambalo aliliwaza. Damu ilikuwa ikichuruzika kutoka pale kitandani kuelekea pembeni kabisa ya Kitanda. Mkono ulikuwa tayari umekamatia bastola yake katika utimamu. Akazipiga hatua kwa kuhesabu moja baada ya nyingine, macho yake yalikuwa yakiangaza chumba kizima yasimuone mtu. Akainua kichwa kulitizama Dali la Chumba kile. Akakiona kipande cha Sillingboard kikiwa kimewekwa pembeni. Upenyo mdogo wa kumpitisha Mtu ukionekana. Muddy akajua kuwa tayari mwanamke yule alikuwa ameuawa. Ameuawa na mtu aliyepita katika upenyo ule anaoutizama. Akatingisha kichwa huku akimsogelea mwanadada yule. Macho yakagota kwenye mpini wa kisu ubavuni kwa mwanadada yule. Hakutaka kusubiri, alirudi nyuma kisha kukiacha chumba kile huku mawazo mazito yakiwa kichwani. Alimtambua muuaji na alimtambua yeye alikuwa nani. Lakini kwa nini kila akiniona anatabasamu? Na kwa nini huwa anaua mtu ambaye alikuwa na miadi nami? Yeye anamsaidia nani? Kila kitu kilikuwa gizani, hakutaka kuamini kama mauaji yanayofanywa na Mtu yule ni vita ya kuwasaidiwa wao.
******
ukumbi ulikuwa kimya kila mmoja akiangalia mbele ya meza kuu. Waziri wa mambo ya Kigeni wa marekani na wenzake wa Urusi, Uingereza na Italia walikuwa wametulia wakiangaliana na wajumbe kutoka Tanzania wakiongozwa na Makamu Wa Rais Mzee Kilowoko. Waziri mkuu na mawaziri wengine wa Serikali ya Jamhuri Ya Muungano Wa Tanzania. Ukiwaondoa hao wengine waliokuwepo ni Mke wa Rais Wa Jamhuri Ya Muungano Wa Tanzania sambamba na watu wengine ambao hawakuwa wakijulikana. Kila mmoja alikuwa kimya akisikiliza maoni Juu Ya mpango mkakati wao waliouleta kuhusu kupewa nguvu ya kifedha na kiusalama kama maandalizi Ya kuipindua iliopo madarakani. Ulikuwa ni mkakati Uliosukwa kwa Muda Mrefu. Watu wengi walikuwa wamepandikizwa katika kufanikisha hilo. Ulikuwa ni Mkutano Uliofanywa kwa kificho Sana kwa Siri Nzito. Baada ya Muda wa majadiliano na mikakati ya kufanikisha mapinduzi Hayo, Nchi hizo nne zikaamua kutuma watu wao ambao kazi yao ilikuwa ni Kuratibu Mapinduzi na Kuhakikisha wanaua kila mtu ambaye angeonekana kuwazibia katika mpango huo. Ni katika Mkutano Huo uliozalisha mahusiano kati ya Mke wa Rais na mtu mmoja ajulikanae kwa Jina la Comrade Robert ambaye alikuwa ni Meja General Mstaafu katika jeshi la nchi. Uhusiano Huo Ulikuwa wa Siri sana, siri ambayo hata mheshimiwa Rais Hakuwa ameigundua. Uhusiano Huo Ukaanza kuleta mabadiliko makubwa kwa Mke Wa Rais, kila wakati alikuwa akiondoka Ikulu bila taarifa huku muda mwingi akimtumia Mkurugenzi Wa Idara ya Usala,a Wa Taifa kufanikisha hilo. Ni wasiwasi Huo Na mashaka kwa Mheshimiwa Rais ndipo alipoamua Kuwaajili Vijana Watatu ambao aliwaamini kwa kuwa walikuwa ni Watiifu kwa Rais. Hapo ndipo Alipowachagua captain George, Kanali Jamilah na Liutenant Sevenlee katika kufuatilia kilichopo nyuma ya safari hizo