MKE WA RAIS
100
Hapakuwa na Dalili ya Uwepo wa Jenifer. Jenifer alikuwa ametoweka. Hakuwepo pale wala hakuonekana. Kilikuwa kitu cha ajabu sana, kitu ambacho hakuna hata mmoja ambaye alikiamini. Atakuwa amekwenda wapi? Ametekwa ama ameondoka katika kujihami na Risasi zilizokuwa zikivulumishwa? Kama ameondoka, ameondoka vipi wakati hakuonyesha kuwa na fahamu. Wakaangaliana tena na tena bila kupata kile walichokuwa wakikiuliza. Wakainuka na kuanza kutoka nje huku kila mmoja akiwa hanajibu kuhusu wapi alipokwenda Jenifer.
*****.
Zilikuwa sauti za watu, sauti ambazo mwanzo alihisi labda ni wapita njia. Lakini Lugha iliyokuwa ikitumika na harafu ambayo ilikuwa ikipita katika matundu ya puani yake yalimfanya aliondoe wazo hiko haraka. Wazo la kwamba alikuwa sehemu jirani na barabarani. Harufu ya kinyesi na mikojo kilikuwa kitu pekee kilichomjulisha na kumtambulisha wapi alipo. Akafumbua macho yake kwa taratibu. Akakutana na kile ambacho hakukijua. Alikuwa amelazwa Chini ya sakafu katika Chumba ambacho kilikuwa kichafu sana. Chumba kilichotapakaa kinyesi na mikojo. Chumba ambacho hakikufaa kulazwa kwa mtoto nzuri kama Jenifer. Mwili wake wakike ulitakiwa kulazwa sehemu ya Gharama. Lakini leo alikuwa amelazwa Juu ya Kinyesi. Juu ya mikojo, alifungiwa ndani Ya Chumba kichafu kisichopendeza. Akaendelea kufumbua macho yake akiangaza huku na huko. Alikutana na vitu ambavyo vilimtisha. Alikuwa akitizamana na matone ya Damu. Matone ambayo kwa sehemu nyingine kulikuwa na mfano wa madimbwi. Kilikuwa ni chumba ambacho kilionyesha ni mahakama ya kifo. Akaendelea kutizama kila upande wa chumba kile. Bado kile alichokutana nacho kilimtisha. Akaamua kuinuka na kukaa kitako, mara akayahisi maumivu kichwani, hapo akaupeleka mkono wake sehemu hiyo akakutana na umajimaji, umajimaji ambao ulimpa majibu kuwa ni Damu. Kufikia hapo akavuta kumbukumbu, kumbukumbu ambayo ilishapotea baada ya kushambuliwa usiku uliopita. Hakufika popote katika kuirudisha kumbukumbu ya usiku wa Jana. Akakiona kitasa cha mlango kikitingishwa. Akarudi chini na kutulia kanakwamba Hakuwa yeye aliekuwa amekaa kitako. Akausikia mlango ukifunguliwa kisha hatua za watu zikasikika zikisogea pale alipo. Akaendelea kujikausha huku akiuandaa Mwili wake na mapambano iwapo itabidi kuwa hivyo. Ni kweli hatua zikasogea na kumfikia, mara akaihisi mikono ya kiume ikimtomasa hapa na pale katika mwili Wake. Mikono ambayo ilikosa adabu na kuingia mpaka ndani ya blauzi aliyovaa na kuanza kuchezea matiti yake mazuri. Bado Jenipher aliendelea kutulia, bado hakuonyesha kama Amesharudi katika fahamu. Mkono ukaendelea kushuka na kushuka, akahisi mkanda wa Suruali yake ukifunguliwa. Hapo hakutaka Kuruhusu hilo, hakutaka kulikubali kwa Gharama yoyote. Akakusanya nguvu zake na kuulegeza mwili wake. Punde alikuwa akiinuka sambamba na mapigo kadhaa mujarabu. Yalikuwa mapigo sahihi yaliokwenda sehemu Sahihi. Mapigo ambayo hayakutoa nafasi kwa yoyote mle ndani Kujitetea. Wote walikuwa wametambarajika wakiwa hawana uhai. Wote walitulia. Akaurudisha mkanda sehemu yake kisha kuokota bastola mbili ambazo zilikuwa pembeni yake. Baada ya hapo aliwapejuwa wale maiti na aliporidhika na alichokipata akaanza kupiga hatua kufuata mlango ili atoke na kupotea Eneo lile. Akaufungua mlango vizuri, akachungulia kwa Chati, hapo akakutana na Ukimya wa hali ya juu. Hapakuwa Dalili ya kuwepo kwa mtu. Lakini hakutaka kuuamini Ukimya ule. Hakutaka kuamini kwa kuwa alijua alikuwa akipambana na Watu ambao ni Zaidi Ya maneno. Bastola ikatangulia mbele, kikafuatia kichwa kisha kiwiliwili. Alikuwa akitembea mbele na Nyuma, alikuwa akiangalia katika pembe zote. Akafakiniwa kupita kizingiti, hata alipouanza mlango wa pili bado Ukimya ulizidi kutamalaki. Hakulijali hilo bado aliendelea kutembea, bado aliendelea kusonga mbele. Akaupita mlango wa pili, mbele yake kulikuwa na Korido ndefu ambayo ilikuwa ikielekea sehemu ambayo hakuijua. Mbele kidogo Akakutana na Neno CIA MISSIONS. Moyo ukamdunda na Umakini Ukaongezeka. Alikuwa Ndani Ya Jengo la Shirika la Kijasusi la Marekani. Alikuwa ndani Ya Shirika ambalo ni Hatari sana kwa Uchunguzi. Alipipiga hatua kama kumi hivi, Akajihisi hakuwa peke yake, akahisi uwepo wa mtu nyuma yake, mtu ambaye hakuwa akimuona.:. Naam hakukosea na hakuwa mbali na wazo lake, Jenifer akageuka