Riwaya: Mke wa Rais

Riwaya: Mke wa Rais

Ibra Mkuu wangu, lete Hiyo hiyo iliyotayari, weekend ngumu sana hii, very sorry for Yanga.
 
MKE WA RAIS

Miili ya watu watatu walikuwa wamelaliana. Walikuwa chini kila mmoja akivuja damu kusababisha Sehemu waliolala kutengeneza kidimbwi kidogo. Kidimbwi ambacho kiliutengeneza mfereji mdogo Uliokuwa ukititirisha damu. Damu ilikuwa mbichi, damu bado ilikuwa ikinukia kuonyesha kuwa watu hawa hawakuuawa katika Muda mrefu. Macho yake yakakisanifu chumba kile kwa umakini wa hali ya Juu, alikuwa akitafuta wapi Risasi imetoka. Wapi muuaji alikaa kabla hajatekeleza haya Mauaji. Macho yaliozoea kuona asichokiona mtu mwingine yakaushuhudia Uwazi, uwazi katika Dirisha. Uwazi wa kusogezwa kuonyesha kuwa muuaji alikuwa ni mwenyeji, mwenyeji wa Eneo lile pia kuonyesha kuwa alikuwa muuaji aliefuzu. Kuuona Upenyo pamoja na Watu watatu Chini, akakihisi kitu, kitu ambacho hakuwa na shaka nacho. Jina la Sohwa lilikuwa kichwani mwake. Alimjua Sohwa kwa Utaalam wake katika kutekeleza kile alichopanga. Hakukuwa na Mwingine katika jiji la vancouver mwenye uwezo wa kufanya hili. Hakuwa Jenifer, hakuwa Jenifer kwa kuwa Muda Waliopishana haukuwa muda wa kumpa mtu nafasi ya kukifanya kile. Hakutaka kuupoteza Muda pale Hotelini. Hakutaka polisi wamkute katika Eneo lile. Hakutala kuharibu kile ambacho amekianza. Alijua anapambana na KGB, alitambua anapambana na CIA na pia alifahamu kuwa anapambana na Mossad. Dakika mbili baadae alikuwa akiiacha hoteli, akiiacha kama mtu wa kawaida. Hakuonekana kama ni tishio. Hakuonyesha kama ni Mtu mwenye jina. Na mwisho hakuwa mtu wa kuonyesha kuwa alikuwa mtu maarufu.

Alitembea huku akiangalia huku na kule, alitambua alikuwa akilindwa na kufuatiliwa na macho ya mtu fulani akiwa sehemu fulani. Kingine kilicho mshangaza ni kutokumuona Jenifer mpaka wakati huo, hakujua wapi alipoelekea lakini hilo halikumtia Hofu kwa kuwa alimtambua Jenifer. Dakika sita mbele alikuwa akiingia ndani Ya hoteli Nyingine. Hpteli ambayo ilikuwa bora kwake. Bado kitendo kilichofanywa chumbani kwake kiliendelea kujirudia. Hakujua kwa nini Sohwa aliamua kuua. Hakujua kusudio la mauaji yale.

Akapokelewa na Mhudumu wa mapokezi akiwa katika tabasamu mwanana. Tabasamu ambalo lilipokelewa vizuri na Mohamedi. Maongezi yakafanyika na Chumba kupatikana. Muda mfupi baadae Muddy alikuwa ndani Ya chumba fulani kipana. Chumba ambacho kilimpa nafasi ya kuweka vitu vyake katika Usiri Mkubwa. Bastola zake zilikuwa kitandani, alifanya kila kitu baada ya kujua kuwa hapakuwa na camera wala kitu chochote ambacho angekitilia shaka.

Baada ya kupanga vitu vyake katika mpangilio timamu aliona kwanza aingie bafuni na kuoga kisha akapate Chakula kabla hajajua nini cha kufanya.

******

macho yake yalikuwa kama yamefumbwa na kuonekana kama alikuwa ndotoni. Alionekana amelala lakini sio kulala kwa Starehe bali Shida. Alikuwa ni Mwanaume anayekaribia Umri wa maika hamsini na tano. Alikuwa amelala juu ya kitanda katika Jumba ambalo lilionekana kulindwa kama Ikulu.. Huyu Alikuwa ni makamu wa Rais Wa Jamhuri Ya Muungano Wa Tanzania MH DUNSTIN KILOWOKO. Alikuwa katika chumba cha hoteli moja nchini Canada. Alikuwa Yeye na watu wake ambao walikuwa katika mpango wa kuingusha serikali iliyokuwa ikiongozwa na Rais RASHID OMARY OTHMAN. Bado kila kitu kilichokea kilikuwa kikijirudia kichwani mwake. Bado alikuwa akiukumbuka mpango huo ambao ulikuja Kufeli Siku ya mwisho. Akakumbuka pale ambapo aliuanzia mpango hup hadi kufikia hapo. Akakumbuka alipokuwa karibu na mke wa Mheshimiwa Rais na kufanikiwa kumrubuni mpaka kuanzisha Mahusiano na Meja Jeneral Comrade Agwe kabla ya kuuawa na watu waliozaniwa kuwa ni kutoka Idara Ya Usalama Wa Nchi. Hakujua kipi kilichotokea mpaka Meja Jenerali Igwe kuuawa. Hakujua kipi ambacho kilikuwa nyuma ya tukio hilo wakati kila kitu kilikuwa kimepangwa na kupangika kwa msaada wa Majasusi kutoka katika Nchi saba tofauti. Wakati hilo likiwa halijapoa likatokea la kutokea baada ya Mke Wa Rais Kuuawa Ndani Ya Ikulu. Ingawa Usiku Ule Mke wa Rais alipelelwa Masaki, lakini kitu cha kushangaza ni kule kusikia kuwa mke Wa Rais ameuawa Ikulu. Hapo ndipo Mipango Yao ilipoharibika.

Alikuwa akiangaza macho yake huku mawazo yakiwa hayapo pale hotelini. Bado alikuwa na hamu pamoja na tamaa ya kuiongoza Tanzania. Kulifikiria Hilo akamkumbuka mtu mmoja, Mtu ambaye alikuwa ametumwa kwa Mission Moja ndani Ya Tanzania. Huyu alikuwa ni mwanadada Neema Mtobwa. Mtoto wa mwandishi Wa Riwaya Za kipelelezi Africa. Akaichomoa Simu yake na kuitafuta namba ya Neema. Muda Mfupi simu ilisikika ikiita Upande wa Pili. Licha ya kuita Sana lakini haikuwa imepokelewa. Akiwa anarudia tena ukaingia Ujumbe kwenye Simu, Ujumbe ambao ulimgutusha na kuutia mwili wake baridi. Ujumbe ambao ulimfanya ashindwe kuhema vizuri na wakati ule ule akafumba macho na Kutulia.
 
MKE WA RAIS

11

Alikuwa ametulia Chumbani kwake akiipitia kompyuta yake mpakato. Alikuwa akisoma kile ambacho kingemuwezesha kuifanya kazi yake bila kujulikana. Punde camera zake alizotega kwenye Chumba Cha Mohamedi zikamletea picha. Picha ambazo alizitambua tu pale watu wawili walipoonekana kupitia camera alizotega wakiingia ndani Ya Jengo. Uingiaji wa watu hawa haukumpa shida ya kugundua kuwa hawa ni nani, hawa ni wakina nani na kwa nini wameingia chumba kile. Kwa kuwa alifanyakazi ya Kijasusi kwa Muda mrefu sana haikumpa tabu kugundua aina Ya Watu wale. Akatamani kukifanya kitu, kitu ambacho kingeweza kumshtua Mohamed. Hakujua kwa nini alipanga kufanya hivyo lakini alijikuta akiinuka na kukiendea kitanda chake. Akavuta Sehemu Moja pembeni mwa kitanda kile, ghafla sehemu moja ilifunguka na kuacha uwazi. Alikuwa akitizamana na silaha zake. Alikuwa akitizamana hazina ya Silaha. Hakutaka kuchelewa. Sekunde mbili baadae Alikuw nje ya Chumba chake akiuparamia ukuta wa Hoteli na Kutua Kwa Nje. Mavazi ya Mafundi wa hoteli ile yalikuwa mwilini mwake yakimhifadhi na kumpa nafasi ya kufanyakazi yake kwa Urahisi. Huyu Alikuwa Sohwa, Sohwa Richardson. Alitaka kumtumia Mohamedi Ujumbe. Ujumbe katika aina ya kuuawa. Ujumbe ambao kwa jasusi yoyote angeweza kuutambua na kuijua maana halisi. Mara hii alikuwa kwenye lifti akielekea Ghorofa ya Tano. Kiunoni alikuwa amechimbia Bastola yake yenye kiwambo cha kuzuia Sauti. Lifti ikamfikisha, akashuka na kuusogea upande wa pili Wa Ghorofa.

Punde alikuwa akitizamana na Dirisha la kioo. Akatoa vitu fulani katika mfupo wa Suruali aliovaa, sekunde mbili baadae kioo cha Dirisha kilikuwa kimesogea na kuacha uwazi wa kuweza kupitisha mdomo wa bastola ndogo. Ndicho kilichofanyika na ndicho alichokifanya. Punde mdomo wa bastola Ulikuwa umepenya na Nukta nne baadae Bastola ikakohoa Mara tatu. Hakutaka kuangalia kile kilichotokea, alichofanya nikuondoka Eneo lile kwa mwendo wa Taratibu bila kuzua Taharuki. Ndivyo ilivyokuwa.

******

alifumbua macho akiangaza huku na huko. Hakujua alikuwa sehemu gani wala Hakujua amefikaje hapo. Akahitaji utulivu wa akili yake kufikiria ni Vipi amefika pale. Mavazi Meupe ya kidaktari kwa watu anaowaona pale kulimpa jibu kuwa alikuwa Hospitali, tena akiwa amelazwa juu ya kitanda kuonyesha ameletwa hapo akiwa hajitambui. Akaendelea kuangaza macho yake ndani ya Chumba kile kilichosheheni vitu mbali mbali vya kitabibu. Punde akaikumbuka Simu, simu ambayo alimpigia Neema Mtobwa. Simu ambayo haikupokelewa, lakini licha ya kutokupokelewa simu Hiyo hiyo ilimletea Ujumbe ambao ulimshtua na kumtetemesha sana. Kufikia hapo akajua kwa nini yuko pale Hospitali. Kufikia hapo akaona umuhimu wa Kuongea na Viongozi wa nchi husika ambao walikuwa waratibu wa mapinduzi. Wakati akifikiria Hilo akamuona mwanadada mrembo akiingia mle ndani akiwa katika mavazi Ya kidaktari. Huyu alikuwa mwanamke Mrembo kuwahi kumuona. Licha ya Urembo huo na vazi lile la Kidaktari, lakini Sura Yake haikuwa ngeni Machoni mwake. Ilikuwa Sura ya mtu anayemfahamu lakini Hakujua aliwahi kumuona wapi. Tabasamu Mwanana liliuchukua Uso Wa mwanadada yule. Hata pale alipokifikia kitanda Cha Mheshimiwa Makamu Wa Rais bado tabasamu halikubanduka Usoni Mwake. Akainama na kuongea kitu na Mgonjwa Yule, lakini Bado makamu wa Rais alionekana kuwa katika mawazo mazito, mawazo ambayo yalikuwa Juu ya mwanamke Huyu aliyesimama mbele yake. Ingawa alikuwa katika mavazi ya Kidaktari lakini bado sura yake ilikuwa ikimtatiza. Akainua Macho kutaka kumuangalia daktari Yule. Akainua macho kutegemea kumuona hapo. Haikuwa hivyo, haikuwezekana na hapakuwa na Mtu mbele yake. Daktari wa kike alikuwa ametoweka katika aina ambayo hakuwahi Kuiona. Muda huu huu alikuwa akitabasamu mbele yake, lakini ndani ya Sekunde Hii hii alikuwa ameoweka katika aina fulani ambayo ilimtisha. Kuondoka kwa binti yule kimazingara kulifuatiwa na wanaume wawili kuingia ndani. Hawa walikuwa watu wake, hawa walikuwa watu wake katika ule mpango wa mapinduzi. Wote waliingia wakiwa katika wasiwasi mkubwa. Wasiwasi Ambao ulionekana Machoni na hata kwenye Nyuso Zao.

Wakaongoza mpaka kilipo kitanda alicholazwa mheshimiwa. Wakatizamana kwa Muda, Kisha kwa sauti ya kukata tamaa akanena. ''Ni muda wa kulipa kila tulichokifanya katika Nchi yetu. Nadhani kuna kila dalili za uwepo wa Mohamedi Hapa nchini. Washirika wetu wanaondelea kuuawa huu ni Mkono wa Mohamed. Bila kumzuia Huyu Mwana Haramu basi tutajikuta tukirudishwa Nchini na kwenda kuhukumiwa. Muda mfupi kabla ya kufika kwenu alikuwepo Daktari wa kike hapa. Huyu Binti Nadhani nishawahi kumuona Sehemu lakini bado sijakumbuka ni Sehemu Gani. Kumbukumbu na Hisia kuhusu Huyu ninahisi Huyu ni Jasusi, na kama Ni jasusi Tutakuwa tumekwisha. Maana ondoka yake hapa ili niduwaza na kunipumbaza. Aliondoka mfano wa kimbunga kama sio kivuli. NIMEJIKUTA NAOGOPA SASA
 
MKE WA RAIS

Nimeanza Kuogopa. Huyu binti nadhani namjua. Wote wakamuangalia Mheshimiwa kwa kumkazia macho Usoni mwake. Hawakuongea chochote mlango ukafunguliwa kisha watu watatu wakaingia. Mwanaume mmoja na wanawake wawili. Mwendo wao na maumbile yao walionyesha wao ni watu gani. Walipoingia hawakuongea chochote na mtu yeyote, bali waliongoza mpaka sehemu fulani ambayo ilionekana kutegwa kitu fulani mfano wa Camera. Punde watu wale wakaonekana kufungua kitu, kila mmoja akikaza macho kuangalia kitu kile. Kitu ambacho kilipofika mikononi kwa Mtaalam Wa IT hakikuchelewa kufunguka na wakati ule ule picha ya mwanadada aliyevalia mavazi Ya Kidaktari ikatamalaki. Wote wakaongeza umakini kuiangalia Sura yake. Punde wakashtuliwa na Sauti kutoka nyuma yao, Sauti iliowagutusha na kuwageuza Shingo zao na kuruhusu macho kumtazama wa Nyuma Yao. Wakakutana na Sura ya mmoja wa wahaini akiwa amepigwa na butwaa akitizama kile walichokuwa wakitizama. Ikatia shaka na kutia wasiwasi, tena wasiwasi mkubwa. ''Jenipher'' ndio sauti pekee kutoka kwa mtu aliyesimama Nyuma Yao. Alikuwa Makamu Wa Rais, wazi wazi alikuwa akitetemeka. Kugundua kuwa mwanadada Yule ni Jenipher kulimfanya ashindwe kuamini kama alikuwa pale kama Daktari. Hakuwahi Kumsikia tokea alipokamatwa kwenye mkasa ule wa Nitakufa na Wewe. Kwa nini Jenipher Yupo hapa Canada? Kwa nini amenitembelea Mimi? Amejuaje kama niko Hapa Nchini na Hapa Hospitali? Ameondokaje katika Upeo wa macho Yangu bila kumuona? Yalikuwa maswali lukuki yakipishana kichwani kwa Mheshimiwa Kilowoko.

Alikuwa amelowa Jasho, alikuwa akitetemeka kwa woga. Watu wale kutoka CIA na KGB wakasimama kisha kumuomba wakae ili kuzungumza. Walikuwa wakitizama pasipokuongea Chochote, macho sita ya watu watatu yalikuwa usoni mwa Mzee Kilowoko. Macho Yenye maswali lukuki, maswali ambayo yalihitaji majibu kutoka kwa Mzee. Ukimya Ukatawala tena na tena. HakUkuwa na Yoyote alienyanyua Mdomo kuongea Chochote. Wote walikuwa wakishangazwa na Ukimya Wa Mzee Kilowoko. Mara Wakauona mlango wa Chumba kile ukifunguliwa Tena, Akaingia mwanamke yule yule, mwanamke ambaye walikuwa wanamjadili, mwanamke ambaye amesababisha Ububu kwa Mzee Kilowoko, Mwanamke Mrembo kwa kumtizama kila anapotembea. Naam, huyu alikuwa ni kama malaika machoni kwa Dimitrovic. Licha ya kumuona kama malaika kwa umbo, sura na mwendo lakini macho ya malaika huyu yalisadifu kitu Ushetani. Macho yasio na mzaha, macho yasio na utani na mwisho ni macho yaliobeba utawala fulani katika kujiamini. Akatembea kwa mwendo wake wa kawaida, tabasamu pana la kuvutia likiifanya Sura Yake iwe nzuri Zaidi. Akawafikia, akawaangalia na baada ya kufanya kilichomleta mle ndani Akatoka bila kuongea na Mtu yoyote Yule. Mkono wa Sohwa Ulikuwa Umeshuka kiunoni alipohifadhi bastola, lakini alipomuona Jenifer akitoka ndani ya Chumba naye akaamua kutoka kumfuatilia kwa Nyuma.

Akaifungua mlango na kutoka kama mtu wa kawaida. Akaangalia kwa chati eneo lote lakini alikuta patupu. Aliwaona watu wengine tofauti na yule mwanadada.

Akaendelea kusogea kwa taratibu akionekana kuchezea Simu lakini macho yake yakiwa katika kutafuta kile ambacho alikihitaji. Mpaka anafika Nje Ya Jengo la Hospitali Ile, hakufanikiwa Kumuona Jenipher. Akasimama kwa muda akiangalia na kuzungusha macho yake katika kuhakiki kila Sura ambayo Ilikuwa ikipita mbele yake. Kitu ambacho hakukitegemea akashuhudia macho yake yakikutana na Sura za Watu wawili, Moja ya mtu ambaye anamsaka na Nyingine Ilikuwa Sura Ya Mohamed. Kila mmoja alikuwa amesimama umbali wa hatua hamsini kutoka alipo mwenzake. Hawakuwa wakitizamana na wala hawakuonekana kama ni Wa moja. Lakini kwa nini wote wawe hapa? Huyu mwanamke ni nani? Na kwa nini Mohamedi Yupo hapa? Kwa nini Kilowoko alionyesha kuogopa baada ya kumuona Huyu Mwanamke? Akajiuliza maswali huku akitamani kujua, angekua kwa vipi? Lilikuwa ni swali Gumu Sana. Hakuna Jasusi Yoyote Duniani Mwenye akili ndogo anayewaza kuandamana na mwanamke anayesakwa. Hakuna Jasusi ambaye anajitanabahisha kwa Watu kuwa yeye ni nani. Kwa Nini Hawa wako pamoja? Bado halikuwa swali lenye kupata Jibu. Mlio ukasikika kwenye simu yake, akaitoa kutoka mfukoni na kuiangalia, aliporudisha Macho kutizama pale walipokuwa wamesimama Muddy Na Jenipher Hawakuwepo. Palikuwa patupu, waliondoka wakipotea katika aina ambayo ilimpa majibu.

Ni wakati Huo Sohwa Alipohitaji Kukutana na Mohamed. Ndipo hapo sohwa alipohotaji kuujua uwepo Wa Mohamed katika Nchini Ya Canada. Ingawa Alishaunganisha matukio na kuhisi kilichopo, lakini alitaka kukutana na Mohamed. Akaondoka Kurudi ndani Huku Hamu Yake ya kutaka kulijua hili suala ikaongezeka.

******
 
MKE WA RAIS

***

Ulikuwa Usiku tulivu, Usiku ambao ulimkuta Mohamed akiwa ametulia ndani ya Club Moja ya Usiku akipata kinywaji Chake huku akiangalia huku na huko. Alikuwa pale yapata dakika ishirini akisubiri kile ambacho aliahidiwa Na Jenifer. Kila wakati macho yake yalikuwa yakiburudishwa na kile alichokuwa akikiangalia. Wasichana waliovaa uchi hakushindwa kuwatupia macho katika aina ambayo Ilimvutia hata mwenyewe. Ukiondoa hilo lakini Jicho lake hakuliondoa sehemu. Sehemu ambayo alitarajia kumuona Jenifer akitokea pale. Lakini Haikuwa Hivyo, Muda uliendelea kupotea na Jenifer Hakuwa ametokea. Kitu kama wasiwasi kikaendelea kutanda Moyoni na hata mawazoni mwake, kuchelewa kurudi Kwa Jenifer kilikuwa kitu kilichomshangaza sana. Hakikuwahi wala Haikuwahi kutokea. Akajipa dakika zaidi Za kusubiri. Akatulia akiendelea kumimina kinywaji mdomoni, Punde akahisi kama mkono wa binadamu ukimgusa begani. Taratibu Mohamed Akageuza Shingo na kumtizama mtu huyo. Akakutana na tabasamu zuri, tabasamu ambalo humvutia kila Lijali. Mbele yake alikuwa amesimama binti alievaa kinguo kifupi, kinguo ambacho kiliiacha mikanda Ya Chupi aina Ya Bikini kuonekana kwa Urahisi. Mohamed hakukurupuka kuongea, bado alikuwa akilisanifu Umbo la mwanadada yule. Jicho lake lilikuwa likishuka na kupanda na kuishia kifuani. Kifuani paliposimama kitu mfano Wa Embe. Embe dodo. Hapo akatuliza macho na muda katika kutizama mahali hapo. Sio kwamba alivutiwa sana na Kifua cha binti yule. La hasha, kilichomfanya akazie macho Eneo lile ni kile kinguo alichovaa binti yule. Kinguo ambacho kilitengenezwa kwa kamba. Lakini ndani ya kamba hizo kulipitishwa waya mwembamba sana. Kengele ya hatari ikalia kichwani kwake. Akatambua na kugundua mwanamke aliembele yake ni Shushushu. Akarejesha Jicho lake chini na kukitizama kinguo kile usawa wa kiuno. Hapo akakiona kitu ambacho alitarajia kukiona. Kilikuwa Chombo cha mawasiliano, chombo kilichotengenezwa mfano wa kifungo. ''karibu Mrembo.'' hatimaye Mohamed akanena kwa sauti ndogo. Binti hakuuliza wala kuitikia bali alikivuta kiti na kusogea karibu na Mohamed kisha kukaa huku akiuruhusu Mwili wake ugusana na Mohammed. Hilo likafanikiwa. Muda mfupi mhudumu akafika na kupewa agizo la kuleta kile ambacho mrembo yule alihitaji. Hata kinywaji kilipoletwa mazungumzo yakaendelea Zaidi na Zaidi. Binti alikuwa mzungumzaji mzuri sana, alitokea kumvutia Mohamed kwa Uchangamfu wake. Licha ya kuvutiwa na maongezi ya mwanadada yule, lakini muda wote alikuwa akitizama mbele kama ataweza kumuona Jenifer.

Safari alimuona kweli, alimuona akitokea akiwa tofauti na alieondoka mwanzo. Huyu alikuwa Jenifer alievalia mavazi tofauti na yale aliondoka nayo Muda Mfupi Uliopita. Tabasamu likaupamba uso wake, tabasamu lenye Ujumbe ndani yake. Sekunde mbili mbele Mudy alikuwa akiinuka kuelekea msalani. Haukuwa msalani kama alivyoaga kwa mwanadada Yule, bali ilikuwa safari ya kuonana na Jenifer. Akatembea akikongoja kana kwamba alikuwa amelewa kwa kiwango cha Juu. Macjo yake yalikuwa yakiangaza mfano Wa bundi. Alikuwa akitizama kila upande, alijua wapo na walikuwa wakimuangalia. Alijua lazima atakuwa akifuatiliwa. Haukuwa Uongo, mbele Yake akatokea mtu anayemfahamu. Mtu ambaye aliwahi kuwa Mkuu wa kitengo Cha kijasusi ndani Ya Idara Ya Usalama Wa Taifa. Huyu alijulikana kama Muuaji Asiye na Huruma. Kwa nini yuko Hapa? Naye ni mmoja kati yao? Yalikuwa maswali mawili ambayo hakuupata muda kutafuta majibu. Ndio kwanza wakapitana pasipokuangaliana. Kipara kilichotengenezwa kichwani kwa Muddy kilimfanya awe Tofauti Sana. Akakiendea Choo kimoja wapo kati ya Vyoo vingi ndani Ya club Ile. Akaufungua mlango Taratibu lakini kwa Tahadhali Kubwa. Akatanguliza Uso na Kuchungulia kwa ndani. Macho yake yakapokewa na kitu cha ajabu, kitu kilichomsisimua Mwili wake. Mwanaume mmoja alikuwa amelala katikati Ya Dimbwi la Damu. Mohamed akaurudisha mlango na kurudi pale alipomuacha Yule msichana, lakini safarii Hakuwepo. Alikuwa ameondoka akiacha kikaratasi Cha Sehemu ambayo anaishi. Muddy akakichukua kikaratasi kile na kukiweka mfukoni.

Dakika mbili baadae alikuwa akiondoka ndani ya Club kuelekea kule alipoelekezwa. Bastola Tatu Zilikuwa Mwilini katika Sehemu Tofauti. Umbali wa hatua Hamsini mbele akamuona Jenipher, hakumuangalia, hakutaka kuchelewa. Akaondoka akiacha Ishara, Ishara ambayo ilieleweka kwa Mlengwa. Akajipakia ndani ya Tax kisha safari Kuelekea anapoishi mwanamke Yule ikaanza. Muda Wote alikuwa akiangalia huku na huko kuangalia kama kuna Jambo lolote linaendelea. Naam, hakuwa mbali na hisia zake, Magari mawili kutoka Gari yao aliliona Gari jingine Likifuatia. Hili alikuwa akilitambua kwa kuwa hata mchana wa leo aliliona pale hotelini. Baada ya Dakika Tano Tax ikasimama mbele ya Hotel moja kubwa sana. Mohamed Akalipa, kisha akaongoza kuingia ndani ya Hoteli. Wakati Anaukaribia mlango Wa Chumba alichoelekezwa, akashangaa kumuona mtu yule yule akitoka. Lakini Safari hii hakupita Hivi hivi, bali aligeuka na Kumuangalia Muddy KisHa AKATABASAMUUU
 
Back
Top Bottom