Riwaya: Mke wa Rais

Riwaya: Mke wa Rais

Pole kiongozi Ila tumehusiwa kuwatendea wema viumbe hao kwani wametokana na Ubavu wetu pia ni dhaifu ukilazimisha kumnyoosha basi utamkata
Pole sana
binti alishaamua kuniacha lakini nashangaa alipokuja kuniletea fujo
 
Hii story nzr sana ila ibra ndo anazingua adi watu wameondoa atention kutoka na story yenyewe inavyoletwa kidogokidogo
 
MKE WA RAIS

kilikuwa kikao cha asubuhi, kikao ambacho hakuna mjumbe hata mmoja aliekitarajia. Kila mmoja alikuwa amelala akiamini kila kitu kimetulia, lakini taarifa ya kuuawa kwa watu wao wanne katika sehemu mbili tofauti iliwashtua na kuwafanya waitane asubuhi hii. Kila mmoja macho yake yalikuwa yakiongea, hakukuwa na hata mmoja ambaye hakushtushwa na taarifa ile. Chumba chote kilikuwa kimya kikifikiria hili na lile. Bado hawakutaka kuamini kama Kuna watu wanaweza kuwaua watu wao Bila wao kuuawa. Kingine ambacho kiliwashangaza na kuwaacha midomo wazi ni kule kuachwa hai kwa kijana Juma Hassan. Kwa nini wengine wauawe lakini huyu ameachwa hai? Kuna kitu gani hapa kati? Yalikuwa maswali mazito sana, Maswali ambayo hayakuwa na Majibu. Mara mlango Ukasukumwa wakaingia watu wengine wapatao sita, kila mmoja akaelekea na kuchukua sehemu yake kisha kukaa. Macho ya wajumbe wote wakageuka kutizama kule alipokaa kijana Juma Hassan. Kila mmoja alikuwa na maswali mazito, maswali ambayo yaliulizwa kwa macho badala ya Mdomo. Ishara za kijasusi Zikamfanya Juma Hassan kusimama na kuelekea mbele ya chumba kile ambacho kiligeuka kama ukumbi wa mkutano. Hakutaka kusita kuongea chochote, aliongea tokea pale alipoanza kufanya mawasiliano na mtu ambaye alidhani ni Neema Mtobwa kwa kuwa alikuwa akitumia akitumia namba yake. Akaeleza jinsi alivyogingewa mlango na mwaname na mwisho akamaliza pale alipomuona mwanaume akiingia na hakujua tena kilichoendelea baada ya kupigwa pigo ambalo hakulielewa lilipotokea.

Kumaliza maelezo kwa nyuma kulifuatiwa na Bumbuwazi, bumbuwazi na kengele za hatari kulia vichwani mwao. Maelezo ya Juma na kile walichokipata kutoka Tanzania juu ya kuawa kwa vijana wao, kitendo cha muuaji kuitumia namba ya Neema kukutana na vijana wao kisha kuwaua ni kitu ambacho kiliwatisha na kuwasisimua, kitu ambacho walikiona ni kama kuvuliwa nguo mbele za watu. Ilikuwa dharau gani mtu akuulie watu wako katika himaya yako? Huyu ni nani? Na anafanya hivi kwa kumpigania nani? Je Huyu ni Mohamed? Yote yalikuwa maswali ambayo hayakupatiwa majibu kwa wakati Ule. Muda mfupi baadae walikuwa ndani ya chumba cha wataalam wa IT ndani ya kitengo cha kijasusi Cha CIA. Wote walikuwa wamemzunguka mwanadada Shunie ambaye alikuwa akijaribu kuitafuta namba ya Marehemu Neema Mtobwa. Alitaka kujua ilitumika lini na ilitumiwa na nani. Kila mmoja alikuwa akihema kwa utulivu, macho yao yalikuwa mbele yakitizama kwenye computer. Punde kila mmoja alikuwa akihamaki baada ya Computer Kuleta majibu kuwa Namba hiyo Bado inatumika na mara ya mwisho kutumika ni Leo hii katikati ya Jiji la Vancouver kwenye Hotel Moja ya Nyota tano.

Wote wakaendelea kutizamana huku kila mmoja akifikiria kitu Cha kufanya. Ilikuwa ni ajabu sana Neema kufanya uasi wakati walimuamini sana. Kila mmoja alikuwa akiwaza lake na kila mmoja alikuwa akiwaza nini kifanyike. Kila mmoja alikuwa akihisi labda Neema ametekwa, kila mmoja alikuwa akihisi hivyo kwa kuwa hakuna anayeweza kuwagundua kiurahisi. Muda Mfupi baadae kiongozi wa mkutano ule akakumbuka kitu, kitu ambacho kilimpa Tabasamu la kushangaza mbele ya Wenzake. Akaichomoa Simu kutoka mfukoni mwake akaandika namba fulani kisha kuiruhusu simu moja kwa moja akaweKa Simu Sikioni.

''KGB MOSCOW RUSIA''. ilisikika sauti upande wa pili.

''Sohwa Richardson Anahitajika Canada Mchana wa leo. Ofisi imuandalie ndege''. Alijibu Yule Mjumbe wa kikao kile na kukata simu.

******

ulikuwa mchana wa saa nane, ndege ndogo ya kirusi ilikuwa ikitua katika uwanja wa ndani wa polisi nchini Canada. Baada ya ndege kutua akashuka mwanadada Mrefu mweupe wa kawaida na kupokelewa na watu wasiopungua watano. Baada ya kumpokea mwanadada yule wakampakia ndani ya Gari na safari Ya kuelekea Hotelini ikaanza. Alionekana Muda Wote kama mtulivu, hakutaka kuongea kitu. Muda wote alikuwa kimya akiangalia hapa na pale. Alikuwa Mwanadada Sohwa Richardson, Jasusi kutoka kitendo cha Ujasusi ndani Ya KGB. Ukimuangalia alikuwa ni mwanamke mpole na mkimya lakini alikuwa ni mwanamke mbaya kuliko Hata Shetani. Alikuwa ameshafanya mission nyingi sana katika nchini mbali mbali. Mission kubwa ambayo nusura iondoke na maisha yake ni Ile ambayo ilifanyika katika Nchini ya Mexico. Bila utaalam wake wa kutumia silaha na mapigano ya mikono nadhani asingeweza kuwa hai mpaka Muda huu. Lakini Leo hii alikuwa Nchini Canada kwa wito kutoka kwa mkuu wake wa kitengo. Mkuu wake kikazi ambaye kauli yake ni kama Amri. Akaruhusu macho yake ya burudishwe na mandhari Nzuri ya Jiji la Vancouver, Mandhari Ambayo ilikuwa akivutia kutizamwa. Haikuchukua Muda Mrefu Gari ilikuwa Ikisimama Nje ya Hotel kubwa na Ya kifahari. Wakashuka wale wajumbe wakiwa sambamba na Sohwa. Wakawa wanaingia katika Hoteli ile. Wakati Watu wale Wakiingia, Mohamedi naye Alikuwa akitoka katika Jengo la Hotel ile. Macho Yake yakatizamana na Mwanamke Yule, Wakatambuana na Kujuana, lakini hawakusalimiana Bali wakapitana.

PATAMU HAPO
 
MKE WA RAIS

Walitambuana na kuonana, lakini wakapitana bila hata ya kusalimiana. SOHWA lilikuwa ni Neno lililojirudia Kichwani kwa Mohamed. MOA ni neno ambalo lilipita kichwani kwa Sohwa. Wakapitana kanakwamba hawajuani na licha ya kupitana lakini pia hakuna ambaye aligeuka kumtizama mwenzake. Wote walikuwa wakitembea kuelekea kule aendako. Sohwa alishangazwa na Uwepo wa Mohamedi katika Eneo lile. Alijua Lazima kuna jambo, jambo ambalo ni kubwa sana. Ilikuwa ni nadra sana kumuona Jasusi kutoka Africa kuja katika nchi fulani bila kuwepo kwa issue maalum. Kwa mara ya kwanza akaufikiria wito kutoka kwa kiongozi wake wa KGB kisha akaunganisha hili na lile akapata Jibu kuwa kuitwa kwake pale Canada panahusiana na Uwepo wa Mohamed pale Nchini. Hakujua kwa nini amewaza hivyo lakini alihisi huo ndio usahihi. Ugumu wa kupambana na Mohamedi akauona, ugumu ambao sio kimapambano, bali walikuwa marafiki. Marafiki ambao hapo awali wakati wapo kwenye Mafunzo Nchini Cuba Walianzisha Mahusiano ya kimapenzi. Ni Hawa waliohatarisha maisha yao katika kupambana na watu ambao walikuwa waasi katika Nchi Ya Ufaransa. Leo walikuwa wamekutana tena, wamekutana katika mission moja wakiwa upande tofauti. Ilitia Raha na iliburudisha vichwani Mwao.

Viongozi wa mission ya Mapinduzi katika nchi ya Tanzania walikuwa wameketi tena kwa mara ya pili tena safari hii wakiwa na mwanadada Sohwa. Bado walikuwa katika Chumba kile kile Cha Wataalam Wa Teknolojia. Mwanadada Shunie alikuwa Nyuma ya Computer akifanya kile ambacho alikifanya kwanza. Muda mfupi baadae walikuwa katika ukumbi wa mkutano. Safarii hii waKikabidhi Jukumu la kupatikana mtu anayetumia Namba ya Neema Mtobwa Mikononi kwa Sohwa. Aliambiwa kila kitu kuhusu kilichokuwa kikifanyika katika nchi ya Tanzania. Wakamueleza jinsi walivyozidiwa nguvu na wapiganaji waliokuwa wakimtii Rais. Na wakamaliza kueleza ni vipi waliamua kuwatorosha wale wote waliokuwa wamepanga kuipindua Serikali ya Jamhuri Ya Muungano wa Tanzania. Sohalwa aliwasikiliza kwa makini na mwisho wa maelezo Yao alikuwa amejua kwa nini Mohamed alikuwa pale. Akakubali kulifanya hilo akiomba apewe wiki mbili katika kulikamilisha hilo suala. Baada ya makabidhiano hayo Sohwa akaonyeshwa ni wapi kilipo chumba ambacho atatumia kwa wakati wote atakapo kuwa pale canada.

*****
Kumuona Sohwa katika Eneo lile la hotel kulimpa Mohamedi picha tofauti kichwani mwake. Alijua ni lazima Sohwa Yupo pale kwa Mission, Mission ambayo hakuwaza wala kufikiria kuihusisha na Mission yao. Alichokifanya baada ya pale nikumtumia Jenifer Ujumbe mfupi kumueleza Juu ya Uwepo wa Mtu mwingine hatari katika Eneo la Hotel. Baada ya kuutuma Ujumbe ule akaendelea na safari Yake. Ilikuwa safari ya kuelekea katika ofisi za ubalozi wa Tanzania. Muda wote alikuwa akiangaza huku na huko kutizama kama alikuwa anafuatwa, lakini hakukuwa na hilo. Barabara zote zilikuwa zimechangamka kila mtu alionekana akiwa na pilika zake. Akaivuka mitaa mitatu na alipoingia mtaa wa nne akamuona mtu mmoja akitokea kwa mbele yake. Huyu alikuwa akionekana mtu wa kawaida kwa mavazi, lakini kutembea kwake alionekana ni mtu wa aina tofauti. Huyu alionekana kama mcheza sinema hasa kwa ule mwendo wake. Hakuna jasusi katika dunia hii asiemtambua jasusi mwenzake. Mohamed alimgundua mtu yule. Alimgundua hasa walipokuwa wanapishana. Ingawa mtu yule alikuwa akitembea kawaida lakini ule mshangao wake usoni ulimpa Mudy majibu kwamba alikuwa akifuatiliwa na alikuwa amejulikana. Hilo halikumtia Hofu wala kumuogopesha, bali aligutuliwa katika hilo pale mlio fulani ulipolia kutoka mfukoni mwake. Akaichomoa simu na kuutazama ujumbe huo. ''Kuna mgeni mmoja wa kiume Chumbani kwako''. Ulisomeka Ujumbe ulionekana kutumwa na Jenipher. ''Msalimie mwambie anisubiri''. Lilikuwa jibu lililomsisimua Jenipher. Akaurudia mara mbili kuusoma kisha akajiinua pale na kuufungua mlango wake na kutoka nje. Alitembea kama mteja wa kawaida na kuupita mlango wa Chumba cha Mudy. Kuupita mlango ule akaongoza akishuka chini kabisa, hapo akakutana na watu wawili ambao macho yao wote yalielekezwa ulipo mlango Wa Chumba Cha Mudy. Akawapita na hawa, akawapita bila kuwatizama Usoni, Muda Ule Ule akamuona Mohamed akiingia. Akamkazia macho katika kumpa Ishara fulani. Mohamed Akaipokea Ishara Kisha wakapishana wote mmoja Akitoka na Mwingine Akiingia. Mudy akazipanda ngazi Moja baada ya Nyingine. Punde akauona mlango Wa Chumba Chake Ukiwa Wazi. Mkono ukashuka pale ilipohifadhiwa bastola yake, akaendelea kupiga hatua akizuga kama alikuwa anaupita mlango, lakini katikati kasi Ambayo haikutegemewa, Akauvaa mlango na kuangukia ndani. Bastola Mkononi akitizamana na watu watatu, watu ambao wote kwa pamoja walikuwa wamelala katikati Ya Dimbwi la Damu. Mohamed Akashangaaa
 
Back
Top Bottom