ibra87
R I P
- Jul 22, 2015
- 5,614
- 5,360
- Thread starter
- #481
MKE WA RAIS
Giza likatanda usoni, kizunguzungu kikampata na muda mfupi alikuwa akianguka Chini. Akajitahidi kupambana na hali ile, haukuwa kazi rahisi. Muda mfupi alitulia na hakujua tena kinachoendelea. Ulikuwa ni kama muujiza au mchezo wa kuigiza, muda mfupi uliopita kabla walitoka wakiwa waarabu kuanzi muonekano, Nywele na ndefu. Lakini Muda huu walikuwa wakirudi kama wazungu tena tofauti na Carl pamoja na yule mwanamke. Hawa walikuwa Warusi kimuonekanma. Hawakuonyesha kuwa na wasiwasi pale walipokiendea Chumba chao. Hata walipoingia, waliingia kanakwamba hapa kuwa na mtu ndani. Hata walipouona mwili wa Jenifer ukiwa Chini umetambalajika bado hakuonyesha kujali. Bado waliuangalia mwili wa Jenipher huku wakitabasamu. Mwanamke akausogelea mwili wa Jenipher na kuupekuwa katika mavazi yake. Hapo wakakuta na bastola mbili za kirusi na magazine tatu za Risasi. Baada ya kuhakikisha hakuwa na kitu kingine walichukua kitu kama begi ambalo lilikuwa kubwa kupita kiasi. Muda mfupi baadae Jenipher alikuwa amewekwa ndani ya begi na kufungiwa humo ndani. Dakika mbili baadae watu wale walikuuwa wakiiacha hotel wakiwa na fuko lao begani. Dakika mbili tena gari moja ya kifahari Ilikuwa ikisimama mbele yao. Mlango wa nyuma ukafunguliwa kisha begi ambalo ndani yake alikuwepo Jenifer likaingizwa ndani kisha mlango kufungwa, hawakutaka kuupoteza muda, hawakutaka kuchelewa, walitakiwa kuondoka ndani ya Ardhi ya Tanzania wakiwa na mateka wao. Gari ilikuwa akikata mbuga kulitafuta Daraja la kigamboni, hawakutaka kupitia feri kuhofia kukaguliwa. Kila mmoja alikuwa makini kwa kila gari aliopita mbele yao. Bastola zao mikononi huku kila wakati wakiangalia nyuma pale walipoliweka begi. Hakuna ambaye alijiamini kirahisi katika kuondoka na mwanamke yule. Kila mmoja alikuwa akiondoka katika ardhi ya Tanzania kwa kushindwa. Muda mfupi walikuwa uhasibu wakiutafuta uwanja wa Taifa. Punde wakaibukia Tazara wakiutafuta Uwanja wa ndege. Kufikia hapo kila mmoja akatabasamu, yalikuwa matasamu ya Kufanikiwa kutoroka na mpiganaji mmoja. Hawakuuona Ugumu tena wakuondoka Tanzania kwa usalama.
Alikuwa akihisi kama yupo kwenye shimo refu sana. Akahisi ndani ya Shimo hilo kama alikuwa akirushwa na kuachiwa akijibamiza kitu ambacho alihisi ni kingo za shimo hilo. Akataka kufumbua macho yake ili kutizama na kuona wapi alipo. Hata alipofanikiwa kufumbua macho hakufanikiwa kuona chochote zaidi Ya Giza totoro. Akajaribu tena na tena katika kuangalia huko lakini ndio kwanza kiza kilitanda kila sehemu. Hakujua alipo na pia hakutambua kwa nini yuko pale. Akajituliza na kuipa Uhuru Akili yake, Uhuru wa kukumbuka ilikuwaje mpaka kufikia pale alipo. Akakumbuka walipoingia ndani ya kivuko kisha kufuatiwa na watu ambao waliwatambua kuwa ni majasusi. Akakumbuka waliposhuka upande wa pili na kuanza kuwafuatilia. Kufikia hapo akakumbuka kila kitu, alikumbuka mara ya mwisho alipoingia katika Chumba kile na kuchomwa na kitu kama sindano. Kufikia hapo hakujua tena kilichoendelea. Hapo ndipo akajua kuwa yupo mahala ambapo hapakuwa salama kwake. Kule kurushwa rushwa na kujigonga kwenye kitu kama kingo kulimpa ufahamu kuwa alikuwa akipelekwa sehemu. Sehemu ambayo aikuwa salama kwake. Akajaribu kuunyoosha mkono wake, akakutana na kitu kama Kitambaa. Hapo akagundua kuwa alikuwa ndani ya kitu kama begi. Akauruhusu mkono wake uelekee sehemu fulani ambayo alipendaga sana kuhifadhi Kisu chake. Ilikuwa sehemu ambayo haikuweza kufikiwa na mikono ya binadamu wakaida. Mkono Wake kufika pale ukakutana na kile ambacho alikuwa akikitafuta. Kisu yake ilikuwa imewekwa katika Sehemu yake. Akaichomoa kisha kuipeleka moja kwa moja katika kitambaa kile. Muda mfupi alikuwa akiona taa kupitia upenyo ambao ulitosha kumsaidia kuona alikuwa wapi. Hapo ndipo aliposhudia kuwa alikuwa ndani ya Gari na kwa muda ule walikuwa wakiipita Vingunguti. Akatambua kuwa alikuwa akisafirishwa. Akisafirishwa bila kujua wapi ambapo alikuwa akipelekwa.
Akajiondoa katika begi lile kisha kutulia akisubiri mpaka mwisho wa safari kuona wapi anapelekwa. Aliendelea kutulia mpaka pale alipoiona gari ikikatiza kushoto kuingia Uwanja wa Ndege wa mwalimu nyerere. Hapo akaamua kujiandaa kufanya kitu, kitu ambacho hakujua kitapokelewa vipi. Wakati wakiingia Eneo la uwanjani Kitu Cha ajabu kikatokea. Taa zote za uwanjani zikazimwa, Hilo likaleta mshangao kwa majasusi wale, muda mfupi walikuwa wakichupa kutoka garini na kuangukia pembeni. Kila mmoja alikuwa na bastola mkononi. Macho yao yakiwaka huku na huko, kila mmoja alikuwa akitizama katika aina fulani, aina ambayo husaidia kumuona hata sisimizi gizani. Bado hali ilikuwa ngumu na tete, wakiwa bado wamekaza macho kuangalia huku na huko, wakamuona mtu akitoka nyuma ya Gari huku akiwa kama kivuli. Ulikuwa Ushukaji thabiti, Ushukaji ambao ulipendeza lakini huku ukiogofya machoni kwa Majasusi wale. NGOMA BADO ILIKUWA MBICHI, TENA MBICHI KABISAAA
Giza likatanda usoni, kizunguzungu kikampata na muda mfupi alikuwa akianguka Chini. Akajitahidi kupambana na hali ile, haukuwa kazi rahisi. Muda mfupi alitulia na hakujua tena kinachoendelea. Ulikuwa ni kama muujiza au mchezo wa kuigiza, muda mfupi uliopita kabla walitoka wakiwa waarabu kuanzi muonekano, Nywele na ndefu. Lakini Muda huu walikuwa wakirudi kama wazungu tena tofauti na Carl pamoja na yule mwanamke. Hawa walikuwa Warusi kimuonekanma. Hawakuonyesha kuwa na wasiwasi pale walipokiendea Chumba chao. Hata walipoingia, waliingia kanakwamba hapa kuwa na mtu ndani. Hata walipouona mwili wa Jenifer ukiwa Chini umetambalajika bado hakuonyesha kujali. Bado waliuangalia mwili wa Jenipher huku wakitabasamu. Mwanamke akausogelea mwili wa Jenipher na kuupekuwa katika mavazi yake. Hapo wakakuta na bastola mbili za kirusi na magazine tatu za Risasi. Baada ya kuhakikisha hakuwa na kitu kingine walichukua kitu kama begi ambalo lilikuwa kubwa kupita kiasi. Muda mfupi baadae Jenipher alikuwa amewekwa ndani ya begi na kufungiwa humo ndani. Dakika mbili baadae watu wale walikuuwa wakiiacha hotel wakiwa na fuko lao begani. Dakika mbili tena gari moja ya kifahari Ilikuwa ikisimama mbele yao. Mlango wa nyuma ukafunguliwa kisha begi ambalo ndani yake alikuwepo Jenifer likaingizwa ndani kisha mlango kufungwa, hawakutaka kuupoteza muda, hawakutaka kuchelewa, walitakiwa kuondoka ndani ya Ardhi ya Tanzania wakiwa na mateka wao. Gari ilikuwa akikata mbuga kulitafuta Daraja la kigamboni, hawakutaka kupitia feri kuhofia kukaguliwa. Kila mmoja alikuwa makini kwa kila gari aliopita mbele yao. Bastola zao mikononi huku kila wakati wakiangalia nyuma pale walipoliweka begi. Hakuna ambaye alijiamini kirahisi katika kuondoka na mwanamke yule. Kila mmoja alikuwa akiondoka katika ardhi ya Tanzania kwa kushindwa. Muda mfupi walikuwa uhasibu wakiutafuta uwanja wa Taifa. Punde wakaibukia Tazara wakiutafuta Uwanja wa ndege. Kufikia hapo kila mmoja akatabasamu, yalikuwa matasamu ya Kufanikiwa kutoroka na mpiganaji mmoja. Hawakuuona Ugumu tena wakuondoka Tanzania kwa usalama.
Alikuwa akihisi kama yupo kwenye shimo refu sana. Akahisi ndani ya Shimo hilo kama alikuwa akirushwa na kuachiwa akijibamiza kitu ambacho alihisi ni kingo za shimo hilo. Akataka kufumbua macho yake ili kutizama na kuona wapi alipo. Hata alipofanikiwa kufumbua macho hakufanikiwa kuona chochote zaidi Ya Giza totoro. Akajaribu tena na tena katika kuangalia huko lakini ndio kwanza kiza kilitanda kila sehemu. Hakujua alipo na pia hakutambua kwa nini yuko pale. Akajituliza na kuipa Uhuru Akili yake, Uhuru wa kukumbuka ilikuwaje mpaka kufikia pale alipo. Akakumbuka walipoingia ndani ya kivuko kisha kufuatiwa na watu ambao waliwatambua kuwa ni majasusi. Akakumbuka waliposhuka upande wa pili na kuanza kuwafuatilia. Kufikia hapo akakumbuka kila kitu, alikumbuka mara ya mwisho alipoingia katika Chumba kile na kuchomwa na kitu kama sindano. Kufikia hapo hakujua tena kilichoendelea. Hapo ndipo akajua kuwa yupo mahala ambapo hapakuwa salama kwake. Kule kurushwa rushwa na kujigonga kwenye kitu kama kingo kulimpa ufahamu kuwa alikuwa akipelekwa sehemu. Sehemu ambayo aikuwa salama kwake. Akajaribu kuunyoosha mkono wake, akakutana na kitu kama Kitambaa. Hapo akagundua kuwa alikuwa ndani ya kitu kama begi. Akauruhusu mkono wake uelekee sehemu fulani ambayo alipendaga sana kuhifadhi Kisu chake. Ilikuwa sehemu ambayo haikuweza kufikiwa na mikono ya binadamu wakaida. Mkono Wake kufika pale ukakutana na kile ambacho alikuwa akikitafuta. Kisu yake ilikuwa imewekwa katika Sehemu yake. Akaichomoa kisha kuipeleka moja kwa moja katika kitambaa kile. Muda mfupi alikuwa akiona taa kupitia upenyo ambao ulitosha kumsaidia kuona alikuwa wapi. Hapo ndipo aliposhudia kuwa alikuwa ndani ya Gari na kwa muda ule walikuwa wakiipita Vingunguti. Akatambua kuwa alikuwa akisafirishwa. Akisafirishwa bila kujua wapi ambapo alikuwa akipelekwa.
Akajiondoa katika begi lile kisha kutulia akisubiri mpaka mwisho wa safari kuona wapi anapelekwa. Aliendelea kutulia mpaka pale alipoiona gari ikikatiza kushoto kuingia Uwanja wa Ndege wa mwalimu nyerere. Hapo akaamua kujiandaa kufanya kitu, kitu ambacho hakujua kitapokelewa vipi. Wakati wakiingia Eneo la uwanjani Kitu Cha ajabu kikatokea. Taa zote za uwanjani zikazimwa, Hilo likaleta mshangao kwa majasusi wale, muda mfupi walikuwa wakichupa kutoka garini na kuangukia pembeni. Kila mmoja alikuwa na bastola mkononi. Macho yao yakiwaka huku na huko, kila mmoja alikuwa akitizama katika aina fulani, aina ambayo husaidia kumuona hata sisimizi gizani. Bado hali ilikuwa ngumu na tete, wakiwa bado wamekaza macho kuangalia huku na huko, wakamuona mtu akitoka nyuma ya Gari huku akiwa kama kivuli. Ulikuwa Ushukaji thabiti, Ushukaji ambao ulipendeza lakini huku ukiogofya machoni kwa Majasusi wale. NGOMA BADO ILIKUWA MBICHI, TENA MBICHI KABISAAA
