HaMachiach
JF-Expert Member
- Dec 15, 2015
- 3,445
- 6,207
- Thread starter
- #61
MAGNUM22
Sehemu 9
Mikikimikiki ilikuwa kwa watu sita tu kwa muda huu, hakuna mwingine aliyejua nini kinaendelea kaetika eneo hilo. Gina alikuwa akizungusha macho huku na kule kujua ni wapi mwanamke yule wa kizungu kapotelea, Chiba alikuwa akifanya juu chini kutafuta mawasiliano mengine ambayo aliyanasa yakiwaunganisha watu hao, Kamanda Amata akitaka kuhakikisha muuaji hafanikishi azma yake yeye akiwepo hapo. Upande wa pili, Martin Gupter akiwa anahaha kutafuta shabaha maridhawa kummaliza mtu wake, Fredy akiwa anajaribu kumpa tumaini Martin kumaliza kazi huku akijipanga ni jinsi gani ya kumuokoa mtu huyo, Amanda akiwa tayari katoweka ukumbini na kupotea kusikojulikana, ilikuwa ni shida. Wanausalama wengine wakiwa wanaendelea kufanya kazi zao za kiusalama wakiwa wanajua hali ni shwari kama walivyo hakikishiwa.
Kamanda Amata akaingia ndani ya jingo lile, akaifiki lifti na kujaribu kuibonyeza hapa na pale.
“Steppppssss!!!!” sauti ya Chiba akamfikia kutoka nyuma. Watu katika jingo hilo hawakuelewa kinachoendelea, wakaona ni kama moja ya muvi za Hollywood. Amata akakamata ngazi na kuanza kupanda kwa kasi huku akikimbia kuelekea juu, nyuma yake akifuatiwa na Chiba.
“Wana sekunde tano tu,” Chiba akamwambia Amata.
“Twendeeeee!!!!” Amata akapiga kelele na kuendelea kukimbilia kule juu.
* * *
Wakati picha ikiwa tayari kupigwa pale mbele ya jengo la mkutano, mabodigadi walikuwa makini kabisa kuangalia kila mtu na kila mpiga picha maana walikuwa wakijua kuwa aina ya budnuki huwa kama kamera. Gina akiwa anajua nini alichotumwa, akaivaa miwani yake na kuangaza huku na huko, miwani ile iliweza kusogeza taswira ya kila mtu anayekuwa mbele yake. Ni hapo alipoinua uso wake juu kutaza lile jingo baada ya kusikia mazungumzo ya Amata na Chiba. Kitu cha kung’aa kilimulika usoni mara moja akili yake ikamwonesha hatari, hakusubiri nini wala nini. Kutoka yeye mpaka pale waliposimama Rais wa Gambia na wa Tanzania ilikuwa ni kama mita nne hivi, na walinzi wengine walikuwa wamezunguka huku na huko. Alichosikia sikioni mwake ni jina lake.
“Dowwwwwwnnnnn!!!!!” akapiga kelele huku akijirusha mzima mzima na kuitawanya miguu yake hewani. Mguu mmoja ukatua kifuani mwa Rais wa Gambia na mwingine kifuani mwa Rais wa Tanzania, kutokana na nguvu ya kiki hiyo maraisa wale wte wakaenda chini. Mmoja wa walinzi wa Rais wa Gambia alikuwa makinia sana, wakati Gina akijichota kujiinua huku akipiga kelele, tayari alikwishachomoa bastola na kumlenga sawia, akaachia risasi mbili na zikamwishia Gina mgongoni. Gina akaenda chini pamoja na marais wale. Kingine kilichoshuhudiwa ni Aide de Camp wa Rais wa Gambia aliyesimama nyuma ya bosi wake akipigizwa mlangoni na damu nyingi zikimvuja shingoni, akaanguka akiwa hana uhai. Walinzi wa maraisa wakavamia eneo haraka na bundukia zikawa nje waziwazi, wanajeshi na polisi tayari wakazingira eneo na marais pamoja na wageni wakaondosha haraka katika eneo lile.
Madam S hakuwa mbali sana, alijishika kichwa alipomwona mlinzi yule akiinua bastola kumlenga Gina, hakuweza kufanya chochote lakini alitamani kuwahi au kumkataza, akachelewa.
Masikini binti yangu!!!! Akajisemea moyoni huku akijisika kichwani na mara baada ya viongozi wale kuondolewa, alishuhudia Gina akiwekwa kitandani huku akivuja damu mgongoni na kinywani, akiingizwa kwenye gari la wagonjwa pamoja na yule ADC wa Gambia.
* * *
Kamanda Amata alifika juu ya kabisa ya ghorofa, kwa mguu wake akaupiga mlango kwa nguvu nao ukafunguka na kujipigiza upande wa pili. Martin aliposikia kishindo hicho akageuka na kumwona jamaa huyo akimjia kasi, hakutaka kuipoteza nafasi. Akarudisha jicho kwenye lensi na kuweka shabaha, akapachika dole lake la shahada na kuvuta trigger, bunduki ile ikatema, na risasi ikahama kwa kasi kuelekea kule ilikoagizwa. Martin aliinuliwa na teke moja la nguvu lililotua ubavuni mwake, akabingirika na kusimama kabla hajakaa sawa, akajikuta akipata shambulizi la ghafla, akapepesuka na kushindwa kujielewa, kamanda Amata akaenda hewani na kumpa double kiki za kifua, zikamsumkuma na Martini akajigonga kwa nyuma kwenye ukingo wa ghorofa akayumba na kujirusha kwenda chini.
“Amejiuaaa!!!” Chiba akapiga kelele akiwa tayari kafika kwenye ule ukingo na bastola mkononi.
Martini alidaka waya wa umeme, akauachia na kudaka nyaya za simu, zikakatika, akashuka nazo mpaka kwenye jengo la pili, akaruka sarakasi maridadi kabisa na kujikuta chini. Dakika hiyo hiyo, gari lililokuwa likiendeshwa na Fredy likafunga breki kali na mlango wa ubavuni ukafunguka, Martini akajitoma ndani huku rsasi ya askari mmoja ikifumua kiatu chake. Fredy akapiga norinda na kuweka gari sawa, akabadili gia na kuondoka kwa kasi. Akafuata barabara ya kuelekea ikulu, na kisha kukamata ile ya Agha Khan kwa kasi ya ajabu, akanyoosha na kupitiliaza mpaka kwenye barabara ya Ocean na kupitiliza bila kukunja kutoka kwenye ukingo wa bahari gari lile likapaa hewani na kutua majini.
Askari waliokuwa wakilifukuza kwa pikipiki na gari ,ahiri za polisi, wakasihia hapo na kushuhudia gari lile likizama taratibu majini na kupoteleamo.
“Wamechagua kifo chao!” askari mmoja akasikika huku akipanda pikipiki lake tayari kwa safari ya kurudi.
Kamanda Amata na Chiba wakawasili eneo hilo na kukuta askari wale wakiwa wamezubaa kutazama majini.
“Vipi?” akauliza.
“Gari limetumbukia baharini na kuzama!”
“Wamechagua kifo chao!” mwingine akadakia.
Kamanda Amata akajua wazi kuwa upeo wao wa kufikiri umeishia hapo, akainua simu na kupiga kwa Inspekata Simbeye.
“Ee Kijana!” Inspekta akaitikia.
“Nahitaji boti na wazamiaji kama sita hivi wafike eneo lote la bahari ya Dar Es Salaam hususan Ocean Road mpaka Msasani na Kunduchi haraka nataka wajlitafute gari la jamaa wametumbukiza baharini,” akamwambia.
“Clear!” akajibu na kukata.
Amata na Chiba wakaingia garini na kurudi, hawakubakia eneo lile kwani tayari walikwishawapa kazi vijana.
“Dah! Washenzi wametuzidi kete!” Amata akasema huku akiendesha gari kwa kasi ya ajabu.
“Yule mwanamke atakuwa karudi Kunduchi, kwa sababu mizigo yake bado ipo pale…” Chiba akasema.
“Sasa ili kumuwahi, inabidi kutumia pikipiki,” Amata akamwambia wakati akisimamisha gari mbele ya ukumbi ule uliokuwa ukifanyika mkutano. Chiba akatelemka na moja kwa moja akaliendea pikipiki kubwa la polisi na kulipanda, baada ya mazungumzo mafupi na askari huyo, akaliwasha na kutokomea. Kamanda Amata akageuza gari na kurudi moja kwa moja mpaka Ofisi Ndogo ambako huko alikutana na Madam S akiwa kasawajika uso wote. Akaingia na kujitupa kitini mara moja, akiwa amechoka vibaya mno.
“Wapo salama?” akamuuliza Madam S.
“Yes, Gina amefanya kazi kubwa sana kuwasevu, alijitoa mhanga kiukweli,” Madam S akamsimulia Amata kilichojiri huku chini. Amata akabaki kustaajabu mambo yaliyofanywa na mwanamke huyo, “kwa hiyo mzima au amekufa?” akauliza kwa hamaniko kubwa.
“No ni mzima, bullet proof ilimsaidia sana, ila kama mlengaji angepiga kichwa hatungekuwa na Gina tena,” Madam S akamwambia, “Hata hivyo risasi ya muuaji imeondokana na maisha ya mtu…”
“Nani?”
“ADC wa Gambia…” akamjibu. Kamanda Amata akabaki kimya kwa sekunde kadhaa.
“Muuaji ametoroka, ni mwanaume wa Kizungu, bunduki yake ipo garini na risasi aliyotumia tuna ganda lake pia,” akamwambia.
“Lazima asakwe, popote duniani, na atiwe mkononi, endelea na Chiba mi ninaelekea Ikulu mara moja lakini tukutane hapa jioni nitawatumia taarifa” akamwambia na kuagana naye. Kamanda Amata akatoka na kuingia garini mwake akawasha na kuelekea Kunduchi ambako Chiba alikuwa ametangulia kwanza.
Huko Kunduchi Chiba aliwasili na kuweka pikipiki yake vizuri, hakusubiri kuuliza wa kusabahi mtu, mbio zake zikaishia katika mlango ule ule aliyoingia mwanzo, akanyonga kitasa bastola mkononi, akaingia, peupe, hakuna mtu. Akatazama kile chumba, hakuna mzigo hata mmoja. Akashusha bastola yake na kuiweka kiunoni mara akasikia vishindo vya watu nyuma yake alipotazama ni walinzi wa hoteli ile.
“Hamjamwona huyu mwanamke akitoka?” akauliza.
“Alitoka asubuhi sana hapa, na hajarudi,” mmoja akajibu huku mwingine akitazama huku na huko.
“Shit!” akachukua simu yake na kupiga namba fulani akaiweka sikioni.
“Hayupo, na kila kitu chake hakipo,” akamwambia Kamanda Amata.
“Ok rudi tukutane Hospitali ya Lugalo, Gina yuko pale” akamwambia.
“Yupo hospitali? Mzima au?” Chiba akauliza.
“Mzima kabisa,” Amata akamjibu lakini ilionekana wazi kuwa hakuridhika au kuamini jibu hilo.
* * *
Ndani ya Hospitali ya Lugalo jeshini, Gina alihifadhiwa ndani ya chumba cha peke yake, macho yake alikuwa ameyafumba na kubaki kimya kabisa. Kilichomgutusha ni mlango uliofunguliwa taratibu na watu wawili wakaingia ndani yake. Akafumbua macho yake taratibu na kutazama, aliwajua, Amata na Chiba.
Chiba alikuwa wa kwanza kukifikia kitanda cha mwanamke huyo na kumwacha Amata nyuma.
“Uko sawa?” akamwuliza.
“Ndiyo niko sawa, hakika ililikuwa ni pumzi yangu ya mwisho, nisingeweza kuwaona tena ndugu zangu na wapenzi wangu kama nyie,” Gina akasema huku akimkumbatia kwa nguvu Chiba na kisha Amata.
“Hauna majeraha yoyote? Au maumivu?” Amata akauliza.
“Ni hapa tu kwenye kiungo cha paja na kiuno kwa sababu nilianguka vibaya, ile risasi ilipoteza taiming yangu… vipi mmepata mshenzi yule?” akawauliza.
“Ah wapi! Wametoroka, wale jamaa wanaiujua kazi yao vyema sana, hawabahatishi,” Amata akajibu.
“Dah! Tunafanyaje?”
“Aluta continua, yaani mapambano yanaendelea. Kama hakuna la ziada wakuruhusu…” Amata akamwambia Gina huku akiketi juu ya kitanda kile.
“Wangeniruhusu mapema tu, ila niliwaomba wasubiri kidogo,” Gina akajibu huku akitoka kitandani na kuketi juu yake.
“Umekuwa shujaa Gina,”
“Ilibidi, kama ningechelewa kidogo tu basi rais wa gambia angekuwa hana uhai, nilijua wazi kuwa risasi ile ingenipata mimi na kutoniletea madhara, lakini yule mlinzi wa rais aliponifyatulia risasi ndipo akanipotezea malengo na badala yake ile risasi ikamwaribu vibaya ADC, amekufa, hana uhai,” Gina akajibu huku akiangusha machozi.
“Usilie Gina, hii ndiyo kazi yetu, uhai wetu u mkononi na tunauweka rehani siku zote, kumbuka kiapo chetu daima, for my people, for my nation,” Amata akamwambia.
* * *
Katika kilindi cha bahari, Martin, Fredy na Amanda walikuwa wakiendelea na safari yao. Chombo ambacho walikuwa wakikitumia ardhini kama gari la kisasa aina ya Lexus mara hii kilikuwa nyambizi ndogo ya kisasa aina ya Violina. Kama ni teknolojia, basi hapa ilitendewa haki kwani chombo kimoja kiliweza kubadilika mara tatu.
Mara baada ya kulitumbukiza gari hilo majini pale Ocean Road hakikuchukua hata dakika moja kumezwa na maji na kutoonekana tena. Kikiwa chini ya maji kiligeuka na kuwa nyambizi ndogo yenye kasi ya ajabu. Fredy alikiongoza na kwenda kukiweka katika pwani ya Kunduchi kama Boti ya kawaida mara baada ya kukiibua majini. Hawakukaa sana Amanda ambaye alitoroka katika ukumbi wa mikutano aliungana nao na safari ya kutoroka nchi ikaanza rasmi. Chombo kile kikazama tena majini na kusafiri chini kwa chini huku kikiongozwa kwa satelaiti ambayo iliwajulisha mahali walipo na upande gani wanaelekea.
“Asante sana Fredy,” Martin akashukuru.
“Asante ya nini?
“Ya nini? Fredy, kiukweli nilijua leo niko matatani, sijamwelewa yule jamaa…”
“Jamaa gani?” Amanda akadakiza swali.
“Kule ghorofani, nimepambana na mtu mmoja mwepesi sana wa mapigano, sikumjibu chochote kwa sababu nilijua wazi kuwa nikionesha umahiri wangu, nitapoteza muda na kuongeza nafasi ya kukamatwa, nikakubalia anipige name nilipopata upenyo ni kajirusha chini, si kwamba nilimkimbia bali wakati mwingine hata kukimbia ni silaha,” Akaeleza, “Nilikuwa nawaza nikifika chini nitawatoroka vipi askari na watu waliopo huko, bahati nzuri na wewe unafika, hakika ni pona yangu…” Kamalizia.
“Sasa tumefanikiwa kuua au?” Amanda akauliza.
“Sidhani, nilichokishuhudia ni mtu aliyeruka kuwaokoa wale marais, nafikiri kama ni kuua atakuwa amekufa mtu mwingine ila si mlengwa…” akamjibu.
“Safari hii tumekutana na wajuvi,” Fredy akawaambia, “sehemu zote tulizopita hatukuwa kujulikana wala nini lakini hapa nashangaa, yaani wana intelijensia ya hali ya juu, na hata bomu tulilotega kule nyumbani sidhani kama litafanya tuliyokusudia,” akamaliza kusema na kuhamishia macho yake katika luninga iliyokuwa mbele yake ikimwonesha ni wapi wanapita. Chombo hiki kilikuwa kikisafiri kilomita moja tu kutoka nchi kavu hivyo kamera yake ndogo ambayo huwa juu inaweza kupata picha nzuri na vizuri ya wapi wanapita.
“Tunakaribia kufika mpaka wa Tanzania na Kenya,” Fredy akawaambia.
“Oh asante Mungu, siitaki kabisa hii nchi…” Martin akawaambia, “tukivuka mpaka nambie,” akamwambia Fredy.
“Ili iweje?” Amanda akauliza.
“Ili ninywe pombe,” akajibu na kujilaza kitini.
“Mmmmm hapo sawa, jamani mkumbuke tunapiga nanga Mombasa, tajiri anatusubiri katika Hoteli ya Likoni High Class,” Amanda akawaambia wenzake nao wakaitikia.
* * *
HOTELI YA LIKONI HIGH CLASS
NDANI YA HOTELI hii, katika apatimenti inayojitegemea na yenye kila kitu cha thamani, watu watatu walikuwa wameketi kimya wakitazama matangazo ya luninga kutoka vituo vya Tanzania. Habari iliyokuwa ikitawala ni juu ya tukio la mchana wa siku hiyo la kukoswakoswa kuuawawa kwa marais wa Gambia na Tanzania kwa kuwa haikujulikana rasmi ni yupi aliyekusudiwa.
Sasa ilikuwa ni hotuba ya Rais wa Tanzania akihutubia taifa mubashara kupitia kituo hicho kutoka Ikulu ya Dodoma ambako yeye na mgeni wake walipelekwa kwa siri siku hiyo hiyo.
“…ni tukio ambalo hatukulitegemea, ni magaidi waliojaribu ama kuniua mimi au mwenzngu Rais wa Gambia na mwenyekiti wa Umoja wa nchi za Afrika.
Kwa maneno haya, nawahakikishia Watanzania na Wagambia na Waafrika wote kwa ujumla kuwa, Mwenyekiti wetu wa Umoja wa Afrika yupo salama, na mimi kama mnavyoniona, isipokuwa tumepoteza watu wawili; msaidizi wa Rais wa Gambia na mwanausalama kutoka Tanzania, Mwenyezi Mungu awalaze pema peponi.
Kwa kumalizia napenda kuwaambia wale waliojaribu kutekeleza ugaidi huu, kuwa sasa nawatangazia vita, popote walipo duniani, nitawakamta na tutawashughulikia ipasavyo. Kama wanasikia hotuba hii basi wasubiri kiama chao au wajiue kabla hatujawafikia, asanteni. Mungu ibariki Afrika Mungu ibariki Tanzania.”
Jaffer Bakhari, akavua miwani yake na kuzima luninga hiyo, akawatazama wasaidizi wake kwa zamu kisha akarudisha macho yake mbele.
“We have missed him!” (tumemkosa) akawaambia.
“I cannot believe, I know Martin Gupter, never miss the range…” (siwezi kuamini, namjua Martin Gupter hawezi kukosa shabaha) akajibu mmoja wao.
“Hawa watu wanacheza sana na sisi, kwa nini wanang’ng’ania ile ardhi? Hawataki kutuachia?” Jaffer akalalama, huku wafuasi wake wakiwa kimya kabisa, “Ok, kesho tutaondoka kwenda Dubai, pale tutakutana Embriyo nzima tutajua nini tunafanya,” akawaambia.
“Na hawa je? Martin na wenzake,” kijana mmoja akauliza.
“Kazi yao itaendelea, ila nitawaficha kwa muda na maelekezo yote nimeshawapa ya wapi wanatakiwa kwenda kujificha. Mambo yakitulia tutaanza tulipoishia… ninyi si mmesikia huyu Rais wa Tanzania anachosema, haya maneno si ya kupuuzia hata kidogo, hah hah hah nevey atafurukuta tu na kina Gupter lakini kamwe hawezi kuigusa Embriyo… san asana nayeye namweka kwenye hesabu, anatakiwa auawe!” Jaffer akawaambia navijana hao wakamkazia macho kumtazama kana kwamba ni mara ya kwanza kumwona. Tajiri huyu akampa ishara mmoja wa vijana hao naye akamkabidhi bahasha kubwa, akaiweka mezani. Dakika hiyo hiyo wanadada warembo wa Kiarabu wakaingia katika sebule hiyo na kutoa huduma za vinywaji na vitafunwa kwa watatu hao.
Simu ya Jaffer ikapiga kengele mara tatu, akaiinua na kutazama kwenye kioo, “wamekaribia, dakika kumi zijazo watakuwa hapa,” akawaambia akimaanisha Martin na wenzake.
VIII
Jioni hii, Kamanda Amata, Chiba, Gina na Madam S walikutana Ofisi ndogo kwa majadiiano mafupi juu ya siku nzima ilivyokwenda.
“Mmefanya kazi kubwa sana nyie vijana!” Madam akawaambia viajana wake, “lakini kazi ndiyo kwanzaaaaa inaanza, mheshimiwa Rais amesema anawataka hao watu ama wawe marehemu au wazima,” akawaambia.
“Kasema hivyo?” Chiba akauliza.
“Ndiyo! Tena kasisitiza sana kabla ya kuondoka kuelekea Dodoma,” akawajibu.
“Sawa! Ni wajibu wetu daima kuweka rehani maisha yetu, kama atakavyo atawapata ama wafu au wazima,” Amata akajibu. Muda wote huo, Gina alikuwa kimya kabisa, hakutaka kuongea wala kujibu swali. Saa kama mbili hivi zilifuata za mkutano mzito wa kupanga kazi.
“Kutokana na hili, mkutano wa dharula umeamua kuunda kikosi cha wapelelezi kwa ajili ya kuwaska wauaji au magaidi hawa,” Madam akawaeleza, “Lakini hata hivyo ofisi ya muda ya usalama ya AU itakuwa hapa Dar es salaam na wamesema wanataka idara ya usalama ya Tanzania ilifanyie kazi hili,” akawaambia.
“Sisi?” Chiba akauliza.
“Ndiyo, sisi, ukiona hivyo, wametuamini… wameona kazi yetu leo tu, wamekubali…” Madam S akawaambia na kutabasamu.
“Tunaanzia wapi kuwatafuta hawa watu?” Gina akasema kwa mara ya kwanza.
“Wewe wajua,”
“Wala usijali, tutapata tu pakuanzia, kama tumegundua target yao tutashindwaje kujua pa kuwapata?” Chiba akauliza.
“Mnajua, Mwenyekiti wa AU ambaye ndiye Rais wa Gambia ameridhia sisi kuingia kazini kwa siri, na tayari ametenga fungu la kutosha hata kabla hiyo ofisi haijaanzishwa rasmi… Amata you are the leader! Tunasubiri tu idhini ya wengine hasa Baraza la Usalama, ” akasema na kumtazama kijana huyu mtanashati mwenye sura ya upole iliyoficha ujasiri wa hali ya juu.
“Tena nimefurahi kwa hili, nina uchungu sana, naomba tu walibariki, watu wachache hawawezi kutuletea uumbavu wao nyumbani kwetu,” Amata akazungumza.
“Ok, zaidi ya hayo, tukapumzike, nitakuiteni kama kuna taarifa nyingine ila kwa sasa endeleeni na shughuli zenu za kawaida za kujenga Taifa,” Madam S akamaliza kuwaambia na kuagana nao.
* * *
Siku iliyofuata, Martin na wenzake waliabiri katika ndege ya shirika la Kenya na kuiacha ardhi ya Afrika Mashariki kuelekea mafichoni.
“Wakitupata wakatambike!” Fredy akamwambia Martin aliyekuwa kimya muda wote.
“Ni kweli,” akafungua kinywa chake kusema, “ lakini Tanzania wameitia doa kazi yangu kwa mara ya kwanza, mpaka sasa bado nawaza wamewezaje kugundua nyayo na mbinu zetu,” akaongeza kusema, “bunduki yangu nimeiacha nah ii inaweza ikaleta shida kwenye mipango mingine,” akamaliza na kuinua bia yake aina ya Heineken iliyokuwa katika kijimeza kidogo na kuimiminia tumboni mwake yote kama ilivyo.
“Afrika haina utundu wala teknolojia ya kugundua sisi ni nani na wapi tulipo, mi naona wazi kuwa hakuna kazi rahisi tuliyowahi kuipata kama hii ya safari hii,” Amanda akaongeza.
“Hapana, kazi nyepesi haiwezi kuingia doa kama hii, hii kwangu ndiyo kazi ngumu sana, na inaendelea kuniumiza kichwa,” akaeleza.
“Tulia The hunter!” Amanda akamwambia.
Muda mfupi baadae wakatangaziwa kuwa wanatua katika Uwanja wa Ndege wa Lungi jijini Free Town, Sierra Leone. Mara baada ya kutoka na kuuacha uwanja huo walichukua gari na moja kwa moja wakaelekea katika mji mdogo wa Waterloo ambako kulikuwa na nyumba moja ya mashambani waliyoitumia kujificha mara wamalizapo matukio yao.
SIKU TATU BAADAE
KAMANDA AMATA alisimama mbele ya bosi wake, wima kabisa, kwa ukakamavu wa kiaskari. Pembeni yake yaani upande huu na mwingine kulikuwa na Gina na Chiba, kati yao na Madam S kulikuwa na meza kubwa yenye vitendea kazi vya kiofisi.
“Nimewaita rasmi, hii hapa mbele yangu ni barua kutoka ofisi ya Mwenyekiti wa Umoja wa Nchi za Afrika kitengo cha usalama. Kimeiomba Tanzania ifanye kazi ya kuwasaka watu hawa waliojaribu kufanya mauaji ya marais, wakamatwe popote walipo duniani.
Niliitwa Ikulu, nikapewa barua hii, ikiwa na maana kuwa kazi hii imeletwa rasmi katika kitengo nyeti cha huduma hatari na za siri TSA, ifanyie kazi. Name nimesimama hapa kuwatuma kazi hiyo. TSA 1 !” akaita.
“HOT”
“Nakupa jukumu sasa, kiofisi ufike popote inapohisiwa watu hawa wapo, kimwili na kiroho kwa njia yoyote ile wakamatwe, ikibidi lolote lifanyike, clear?” Madam akamwambia.
“For my people, For my Nation … nipo tayari!” akajibu.
Madam S akainua kabrasha lililokuwa mezani kwake na kumkabidhi mikononi, naye akapokea kwa mikono miwili. Kabrasha lile lilikuwa limefungwa kwa karatasi laini inayoweza kuonesha mpaka upande wa pili. Kilichofungwa ndani ni faili moja lenye karatasi kama hamsini hivi na juu yake kulikuwa na maandishi makubwa yaliyosomeka, ‘MAGNUM 22’.
“Najua unajua nini unapaswa kutenda,” Madam S akamwambia na kuketi tena kitini, kasha vijana wake nao wakaketi katika viti vyao, “kama mnavyojua hii ni kazi nyingine nzito, kumsaka muuaji ni sawa na kuwinda, maana hata yeye anajua kuwa anasakwa na anajua ni nini afanye ili asikamatwe, lazima ujue hesabu za magazijuto, lakini ninaamini kuwa mtaweza. TSA 2 utabaki hapa utamsaidia kaka yako kwa kila anachohitaji kiteknolojia, hakikisha umpotezi kwenye rada yako. TSA 5 utakuwa tayari kwa usaidizi wowote utakaohitajika,” akamalizia kwa kuwaambia.
Baada ya hapo Kamanda Amata na Chiba wakainuka tayari kuondoka, wakaagana na Madam S na kutoka nje y ofisi hio huku lile kabrasha likiwa katika mfuko wa karatasi. Safari yao iliishia Gezaulole, Shamba, huku ndiko mambo yote hupikwa.
* * *
Katika meza yenye umbo la yai, vijana hawa wawili waliketi kwa kutazamana, Amata akaweka kabrasha lile mezani na kulichana ili kujua nini kipo ndani yake. Ni karatasi kadhaa zenye maelezo mengi yanayohusiana na kile kinachodhaniwa kuwa ni kisa cha watu hao kutaka kumdhuru Rais, zaidi ya hapo kulikuwa na taarifa fupi ya mauaji ya Angola na Ivory Coast. Kwa ujumla ndani ya bahasha hiyo kulikuwa na kazi mbili kubwa, moja ni kufanya uchunguzi kama mauaji ya Angola, Ivory Coast na shambulio la Dar e salaam vina mahusiano na muuaji ni mmoja? La pili ni kuwa kama ndiyo, basi askew na atiwe mbaroni kwa gharama yoyote ile na kama siyo basi huyu aliyehusika na shambulio la Dar es salaam atafutwe. Sambamba na hayo yote palikuwa na picha za maeneo ambako matukio hayo yalifanyika katika nchi zote tatu na tafutishi chache ambazo zilipatikana tayari ziliwekwa vielelezo vyake.
Kamanda Amata akashusha pumzi na kujiegemeza kitini.
“Vipi?” Chiba akamuuliza huku akilivuta lile kabrasha na kuanza kulipekua. Kamanda hakujibu swali lake bali alibaki kimya akitafakari hili na lile.
“Nafikiri nianzie wapi, Angola, Ivory Coast au wapi!” akajisemea.
“Hapa, anzia hapa na kutoka hapa utakwenda huko kote,” Chiba akamwambia, naye akatikisa kichwa juu chini.
“Kuna mengi unayotakiwa kuanza nayo hapa nyumbani,” akamwekea picha moja mezani, iliyomwonesha kijana mmoja mrefu mwenye shingo nyembaba na nywele kama za Kisomali hivi.
“Huyu ni nani?” Amata akauliza.
“Huyu ni mhudumu wa mapokezi katika hoteli ya Kunduchi, alinipokea kwa furaha sana na kwake nimepata jambo moja tu…”
“Lipi?”
“Alinambia kuwa mwanamke huyu ana wanaume wengi… sasa inabidi kujua wanaume hao labda tutapata picha Fulani ya kuwasaka…” Chiba akasema.
“Good! Huyu lazima nimuone leo hii, najua kutoka hapa nitaweza kujua nini kinafuata…”
“Sawa! Hilo la kwanza, hapa kuna mpango wa siri ambao uliniwezesha kukujuza kuwa tageti ya jamaa ipo wapi, na mara moja katika faii hili nililolifuma chumbani mwa yule mwanamke limeeleza kila kitu ,mpango mzima,”
“Unasema?!” Amata akahamaki.
Chiba hakujibu, akachukua simu yake na kumpa Kamanda Amata, naye akaipokea na kuanza kuperuzi faili lile, kila alipozidi kwenda zaidi alijikuta akipigwa na bumbuwazi.
Kumbe mpango upo hivi! Akawaza huku akiendelea kuchambua na vya chini, “kwa hiyo ina maana sasa watakuwa safarini kuelekea Sierra?” akauliza.
“Kama wamefanikiwa kutoka nchini, basi watakuwa tayari wamefika nchini humo, lakini mpaka sasa sijapata habari yoyote iwe kutoka Uwanja wa ndege au bandarini au Ubungo, hamna kitu, ina maana wapo ndani ya nchi hii,” Chiba akasema.
“Hapana Chiba, hawa jamaa nakuhakikishia wameshatoka nchini, unakumbuka lile gari lao walivyolitumbukiza baharini? Na polisi wanamaji wamesemaje, ‘hatujaona gari wala nini’ nahisi sasa lile gari lina uwezo wa kutembea majini tena chini kwa chini…”
“Aaaaa Amata kaka, kwani hapa tupo kwenye muvi za James Bond?” Chiba akatania.
“Habari ndo hiyo, watu kama hawa kutokana na wanachokifanya lazima wajipange sana katika kutoroka, tungelipata gari sawa, halipo baharini, liko wapi? Washasepa. Haya umeenda Kunduchi kwa yule mwanamke umepata nini, ameondoka saa ngapi na kwa vipi, kuna uwezekano kabisa kuwa lile gari limesafiri kutoka hapa na kumchukua yule mwanamke kisha wakatokomea kwa njia hiyohiyo na kuvuka mpaka…. Na ukiangali kama wametoroka kwa njia hiyo, basi watakuwa Kenya,” Amata
Sehemu 9
Mikikimikiki ilikuwa kwa watu sita tu kwa muda huu, hakuna mwingine aliyejua nini kinaendelea kaetika eneo hilo. Gina alikuwa akizungusha macho huku na kule kujua ni wapi mwanamke yule wa kizungu kapotelea, Chiba alikuwa akifanya juu chini kutafuta mawasiliano mengine ambayo aliyanasa yakiwaunganisha watu hao, Kamanda Amata akitaka kuhakikisha muuaji hafanikishi azma yake yeye akiwepo hapo. Upande wa pili, Martin Gupter akiwa anahaha kutafuta shabaha maridhawa kummaliza mtu wake, Fredy akiwa anajaribu kumpa tumaini Martin kumaliza kazi huku akijipanga ni jinsi gani ya kumuokoa mtu huyo, Amanda akiwa tayari katoweka ukumbini na kupotea kusikojulikana, ilikuwa ni shida. Wanausalama wengine wakiwa wanaendelea kufanya kazi zao za kiusalama wakiwa wanajua hali ni shwari kama walivyo hakikishiwa.
Kamanda Amata akaingia ndani ya jingo lile, akaifiki lifti na kujaribu kuibonyeza hapa na pale.
“Steppppssss!!!!” sauti ya Chiba akamfikia kutoka nyuma. Watu katika jingo hilo hawakuelewa kinachoendelea, wakaona ni kama moja ya muvi za Hollywood. Amata akakamata ngazi na kuanza kupanda kwa kasi huku akikimbia kuelekea juu, nyuma yake akifuatiwa na Chiba.
“Wana sekunde tano tu,” Chiba akamwambia Amata.
“Twendeeeee!!!!” Amata akapiga kelele na kuendelea kukimbilia kule juu.
* * *
Wakati picha ikiwa tayari kupigwa pale mbele ya jengo la mkutano, mabodigadi walikuwa makini kabisa kuangalia kila mtu na kila mpiga picha maana walikuwa wakijua kuwa aina ya budnuki huwa kama kamera. Gina akiwa anajua nini alichotumwa, akaivaa miwani yake na kuangaza huku na huko, miwani ile iliweza kusogeza taswira ya kila mtu anayekuwa mbele yake. Ni hapo alipoinua uso wake juu kutaza lile jingo baada ya kusikia mazungumzo ya Amata na Chiba. Kitu cha kung’aa kilimulika usoni mara moja akili yake ikamwonesha hatari, hakusubiri nini wala nini. Kutoka yeye mpaka pale waliposimama Rais wa Gambia na wa Tanzania ilikuwa ni kama mita nne hivi, na walinzi wengine walikuwa wamezunguka huku na huko. Alichosikia sikioni mwake ni jina lake.
“Dowwwwwwnnnnn!!!!!” akapiga kelele huku akijirusha mzima mzima na kuitawanya miguu yake hewani. Mguu mmoja ukatua kifuani mwa Rais wa Gambia na mwingine kifuani mwa Rais wa Tanzania, kutokana na nguvu ya kiki hiyo maraisa wale wte wakaenda chini. Mmoja wa walinzi wa Rais wa Gambia alikuwa makinia sana, wakati Gina akijichota kujiinua huku akipiga kelele, tayari alikwishachomoa bastola na kumlenga sawia, akaachia risasi mbili na zikamwishia Gina mgongoni. Gina akaenda chini pamoja na marais wale. Kingine kilichoshuhudiwa ni Aide de Camp wa Rais wa Gambia aliyesimama nyuma ya bosi wake akipigizwa mlangoni na damu nyingi zikimvuja shingoni, akaanguka akiwa hana uhai. Walinzi wa maraisa wakavamia eneo haraka na bundukia zikawa nje waziwazi, wanajeshi na polisi tayari wakazingira eneo na marais pamoja na wageni wakaondosha haraka katika eneo lile.
Madam S hakuwa mbali sana, alijishika kichwa alipomwona mlinzi yule akiinua bastola kumlenga Gina, hakuweza kufanya chochote lakini alitamani kuwahi au kumkataza, akachelewa.
Masikini binti yangu!!!! Akajisemea moyoni huku akijisika kichwani na mara baada ya viongozi wale kuondolewa, alishuhudia Gina akiwekwa kitandani huku akivuja damu mgongoni na kinywani, akiingizwa kwenye gari la wagonjwa pamoja na yule ADC wa Gambia.
* * *
Kamanda Amata alifika juu ya kabisa ya ghorofa, kwa mguu wake akaupiga mlango kwa nguvu nao ukafunguka na kujipigiza upande wa pili. Martin aliposikia kishindo hicho akageuka na kumwona jamaa huyo akimjia kasi, hakutaka kuipoteza nafasi. Akarudisha jicho kwenye lensi na kuweka shabaha, akapachika dole lake la shahada na kuvuta trigger, bunduki ile ikatema, na risasi ikahama kwa kasi kuelekea kule ilikoagizwa. Martin aliinuliwa na teke moja la nguvu lililotua ubavuni mwake, akabingirika na kusimama kabla hajakaa sawa, akajikuta akipata shambulizi la ghafla, akapepesuka na kushindwa kujielewa, kamanda Amata akaenda hewani na kumpa double kiki za kifua, zikamsumkuma na Martini akajigonga kwa nyuma kwenye ukingo wa ghorofa akayumba na kujirusha kwenda chini.
“Amejiuaaa!!!” Chiba akapiga kelele akiwa tayari kafika kwenye ule ukingo na bastola mkononi.
Martini alidaka waya wa umeme, akauachia na kudaka nyaya za simu, zikakatika, akashuka nazo mpaka kwenye jengo la pili, akaruka sarakasi maridadi kabisa na kujikuta chini. Dakika hiyo hiyo, gari lililokuwa likiendeshwa na Fredy likafunga breki kali na mlango wa ubavuni ukafunguka, Martini akajitoma ndani huku rsasi ya askari mmoja ikifumua kiatu chake. Fredy akapiga norinda na kuweka gari sawa, akabadili gia na kuondoka kwa kasi. Akafuata barabara ya kuelekea ikulu, na kisha kukamata ile ya Agha Khan kwa kasi ya ajabu, akanyoosha na kupitiliaza mpaka kwenye barabara ya Ocean na kupitiliza bila kukunja kutoka kwenye ukingo wa bahari gari lile likapaa hewani na kutua majini.
Askari waliokuwa wakilifukuza kwa pikipiki na gari ,ahiri za polisi, wakasihia hapo na kushuhudia gari lile likizama taratibu majini na kupoteleamo.
“Wamechagua kifo chao!” askari mmoja akasikika huku akipanda pikipiki lake tayari kwa safari ya kurudi.
Kamanda Amata na Chiba wakawasili eneo hilo na kukuta askari wale wakiwa wamezubaa kutazama majini.
“Vipi?” akauliza.
“Gari limetumbukia baharini na kuzama!”
“Wamechagua kifo chao!” mwingine akadakia.
Kamanda Amata akajua wazi kuwa upeo wao wa kufikiri umeishia hapo, akainua simu na kupiga kwa Inspekata Simbeye.
“Ee Kijana!” Inspekta akaitikia.
“Nahitaji boti na wazamiaji kama sita hivi wafike eneo lote la bahari ya Dar Es Salaam hususan Ocean Road mpaka Msasani na Kunduchi haraka nataka wajlitafute gari la jamaa wametumbukiza baharini,” akamwambia.
“Clear!” akajibu na kukata.
Amata na Chiba wakaingia garini na kurudi, hawakubakia eneo lile kwani tayari walikwishawapa kazi vijana.
“Dah! Washenzi wametuzidi kete!” Amata akasema huku akiendesha gari kwa kasi ya ajabu.
“Yule mwanamke atakuwa karudi Kunduchi, kwa sababu mizigo yake bado ipo pale…” Chiba akasema.
“Sasa ili kumuwahi, inabidi kutumia pikipiki,” Amata akamwambia wakati akisimamisha gari mbele ya ukumbi ule uliokuwa ukifanyika mkutano. Chiba akatelemka na moja kwa moja akaliendea pikipiki kubwa la polisi na kulipanda, baada ya mazungumzo mafupi na askari huyo, akaliwasha na kutokomea. Kamanda Amata akageuza gari na kurudi moja kwa moja mpaka Ofisi Ndogo ambako huko alikutana na Madam S akiwa kasawajika uso wote. Akaingia na kujitupa kitini mara moja, akiwa amechoka vibaya mno.
“Wapo salama?” akamuuliza Madam S.
“Yes, Gina amefanya kazi kubwa sana kuwasevu, alijitoa mhanga kiukweli,” Madam S akamsimulia Amata kilichojiri huku chini. Amata akabaki kustaajabu mambo yaliyofanywa na mwanamke huyo, “kwa hiyo mzima au amekufa?” akauliza kwa hamaniko kubwa.
“No ni mzima, bullet proof ilimsaidia sana, ila kama mlengaji angepiga kichwa hatungekuwa na Gina tena,” Madam S akamwambia, “Hata hivyo risasi ya muuaji imeondokana na maisha ya mtu…”
“Nani?”
“ADC wa Gambia…” akamjibu. Kamanda Amata akabaki kimya kwa sekunde kadhaa.
“Muuaji ametoroka, ni mwanaume wa Kizungu, bunduki yake ipo garini na risasi aliyotumia tuna ganda lake pia,” akamwambia.
“Lazima asakwe, popote duniani, na atiwe mkononi, endelea na Chiba mi ninaelekea Ikulu mara moja lakini tukutane hapa jioni nitawatumia taarifa” akamwambia na kuagana naye. Kamanda Amata akatoka na kuingia garini mwake akawasha na kuelekea Kunduchi ambako Chiba alikuwa ametangulia kwanza.
Huko Kunduchi Chiba aliwasili na kuweka pikipiki yake vizuri, hakusubiri kuuliza wa kusabahi mtu, mbio zake zikaishia katika mlango ule ule aliyoingia mwanzo, akanyonga kitasa bastola mkononi, akaingia, peupe, hakuna mtu. Akatazama kile chumba, hakuna mzigo hata mmoja. Akashusha bastola yake na kuiweka kiunoni mara akasikia vishindo vya watu nyuma yake alipotazama ni walinzi wa hoteli ile.
“Hamjamwona huyu mwanamke akitoka?” akauliza.
“Alitoka asubuhi sana hapa, na hajarudi,” mmoja akajibu huku mwingine akitazama huku na huko.
“Shit!” akachukua simu yake na kupiga namba fulani akaiweka sikioni.
“Hayupo, na kila kitu chake hakipo,” akamwambia Kamanda Amata.
“Ok rudi tukutane Hospitali ya Lugalo, Gina yuko pale” akamwambia.
“Yupo hospitali? Mzima au?” Chiba akauliza.
“Mzima kabisa,” Amata akamjibu lakini ilionekana wazi kuwa hakuridhika au kuamini jibu hilo.
* * *
Ndani ya Hospitali ya Lugalo jeshini, Gina alihifadhiwa ndani ya chumba cha peke yake, macho yake alikuwa ameyafumba na kubaki kimya kabisa. Kilichomgutusha ni mlango uliofunguliwa taratibu na watu wawili wakaingia ndani yake. Akafumbua macho yake taratibu na kutazama, aliwajua, Amata na Chiba.
Chiba alikuwa wa kwanza kukifikia kitanda cha mwanamke huyo na kumwacha Amata nyuma.
“Uko sawa?” akamwuliza.
“Ndiyo niko sawa, hakika ililikuwa ni pumzi yangu ya mwisho, nisingeweza kuwaona tena ndugu zangu na wapenzi wangu kama nyie,” Gina akasema huku akimkumbatia kwa nguvu Chiba na kisha Amata.
“Hauna majeraha yoyote? Au maumivu?” Amata akauliza.
“Ni hapa tu kwenye kiungo cha paja na kiuno kwa sababu nilianguka vibaya, ile risasi ilipoteza taiming yangu… vipi mmepata mshenzi yule?” akawauliza.
“Ah wapi! Wametoroka, wale jamaa wanaiujua kazi yao vyema sana, hawabahatishi,” Amata akajibu.
“Dah! Tunafanyaje?”
“Aluta continua, yaani mapambano yanaendelea. Kama hakuna la ziada wakuruhusu…” Amata akamwambia Gina huku akiketi juu ya kitanda kile.
“Wangeniruhusu mapema tu, ila niliwaomba wasubiri kidogo,” Gina akajibu huku akitoka kitandani na kuketi juu yake.
“Umekuwa shujaa Gina,”
“Ilibidi, kama ningechelewa kidogo tu basi rais wa gambia angekuwa hana uhai, nilijua wazi kuwa risasi ile ingenipata mimi na kutoniletea madhara, lakini yule mlinzi wa rais aliponifyatulia risasi ndipo akanipotezea malengo na badala yake ile risasi ikamwaribu vibaya ADC, amekufa, hana uhai,” Gina akajibu huku akiangusha machozi.
“Usilie Gina, hii ndiyo kazi yetu, uhai wetu u mkononi na tunauweka rehani siku zote, kumbuka kiapo chetu daima, for my people, for my nation,” Amata akamwambia.
* * *
Katika kilindi cha bahari, Martin, Fredy na Amanda walikuwa wakiendelea na safari yao. Chombo ambacho walikuwa wakikitumia ardhini kama gari la kisasa aina ya Lexus mara hii kilikuwa nyambizi ndogo ya kisasa aina ya Violina. Kama ni teknolojia, basi hapa ilitendewa haki kwani chombo kimoja kiliweza kubadilika mara tatu.
Mara baada ya kulitumbukiza gari hilo majini pale Ocean Road hakikuchukua hata dakika moja kumezwa na maji na kutoonekana tena. Kikiwa chini ya maji kiligeuka na kuwa nyambizi ndogo yenye kasi ya ajabu. Fredy alikiongoza na kwenda kukiweka katika pwani ya Kunduchi kama Boti ya kawaida mara baada ya kukiibua majini. Hawakukaa sana Amanda ambaye alitoroka katika ukumbi wa mikutano aliungana nao na safari ya kutoroka nchi ikaanza rasmi. Chombo kile kikazama tena majini na kusafiri chini kwa chini huku kikiongozwa kwa satelaiti ambayo iliwajulisha mahali walipo na upande gani wanaelekea.
“Asante sana Fredy,” Martin akashukuru.
“Asante ya nini?
“Ya nini? Fredy, kiukweli nilijua leo niko matatani, sijamwelewa yule jamaa…”
“Jamaa gani?” Amanda akadakiza swali.
“Kule ghorofani, nimepambana na mtu mmoja mwepesi sana wa mapigano, sikumjibu chochote kwa sababu nilijua wazi kuwa nikionesha umahiri wangu, nitapoteza muda na kuongeza nafasi ya kukamatwa, nikakubalia anipige name nilipopata upenyo ni kajirusha chini, si kwamba nilimkimbia bali wakati mwingine hata kukimbia ni silaha,” Akaeleza, “Nilikuwa nawaza nikifika chini nitawatoroka vipi askari na watu waliopo huko, bahati nzuri na wewe unafika, hakika ni pona yangu…” Kamalizia.
“Sasa tumefanikiwa kuua au?” Amanda akauliza.
“Sidhani, nilichokishuhudia ni mtu aliyeruka kuwaokoa wale marais, nafikiri kama ni kuua atakuwa amekufa mtu mwingine ila si mlengwa…” akamjibu.
“Safari hii tumekutana na wajuvi,” Fredy akawaambia, “sehemu zote tulizopita hatukuwa kujulikana wala nini lakini hapa nashangaa, yaani wana intelijensia ya hali ya juu, na hata bomu tulilotega kule nyumbani sidhani kama litafanya tuliyokusudia,” akamaliza kusema na kuhamishia macho yake katika luninga iliyokuwa mbele yake ikimwonesha ni wapi wanapita. Chombo hiki kilikuwa kikisafiri kilomita moja tu kutoka nchi kavu hivyo kamera yake ndogo ambayo huwa juu inaweza kupata picha nzuri na vizuri ya wapi wanapita.
“Tunakaribia kufika mpaka wa Tanzania na Kenya,” Fredy akawaambia.
“Oh asante Mungu, siitaki kabisa hii nchi…” Martin akawaambia, “tukivuka mpaka nambie,” akamwambia Fredy.
“Ili iweje?” Amanda akauliza.
“Ili ninywe pombe,” akajibu na kujilaza kitini.
“Mmmmm hapo sawa, jamani mkumbuke tunapiga nanga Mombasa, tajiri anatusubiri katika Hoteli ya Likoni High Class,” Amanda akawaambia wenzake nao wakaitikia.
* * *
HOTELI YA LIKONI HIGH CLASS
NDANI YA HOTELI hii, katika apatimenti inayojitegemea na yenye kila kitu cha thamani, watu watatu walikuwa wameketi kimya wakitazama matangazo ya luninga kutoka vituo vya Tanzania. Habari iliyokuwa ikitawala ni juu ya tukio la mchana wa siku hiyo la kukoswakoswa kuuawawa kwa marais wa Gambia na Tanzania kwa kuwa haikujulikana rasmi ni yupi aliyekusudiwa.
Sasa ilikuwa ni hotuba ya Rais wa Tanzania akihutubia taifa mubashara kupitia kituo hicho kutoka Ikulu ya Dodoma ambako yeye na mgeni wake walipelekwa kwa siri siku hiyo hiyo.
“…ni tukio ambalo hatukulitegemea, ni magaidi waliojaribu ama kuniua mimi au mwenzngu Rais wa Gambia na mwenyekiti wa Umoja wa nchi za Afrika.
Kwa maneno haya, nawahakikishia Watanzania na Wagambia na Waafrika wote kwa ujumla kuwa, Mwenyekiti wetu wa Umoja wa Afrika yupo salama, na mimi kama mnavyoniona, isipokuwa tumepoteza watu wawili; msaidizi wa Rais wa Gambia na mwanausalama kutoka Tanzania, Mwenyezi Mungu awalaze pema peponi.
Kwa kumalizia napenda kuwaambia wale waliojaribu kutekeleza ugaidi huu, kuwa sasa nawatangazia vita, popote walipo duniani, nitawakamta na tutawashughulikia ipasavyo. Kama wanasikia hotuba hii basi wasubiri kiama chao au wajiue kabla hatujawafikia, asanteni. Mungu ibariki Afrika Mungu ibariki Tanzania.”
Jaffer Bakhari, akavua miwani yake na kuzima luninga hiyo, akawatazama wasaidizi wake kwa zamu kisha akarudisha macho yake mbele.
“We have missed him!” (tumemkosa) akawaambia.
“I cannot believe, I know Martin Gupter, never miss the range…” (siwezi kuamini, namjua Martin Gupter hawezi kukosa shabaha) akajibu mmoja wao.
“Hawa watu wanacheza sana na sisi, kwa nini wanang’ng’ania ile ardhi? Hawataki kutuachia?” Jaffer akalalama, huku wafuasi wake wakiwa kimya kabisa, “Ok, kesho tutaondoka kwenda Dubai, pale tutakutana Embriyo nzima tutajua nini tunafanya,” akawaambia.
“Na hawa je? Martin na wenzake,” kijana mmoja akauliza.
“Kazi yao itaendelea, ila nitawaficha kwa muda na maelekezo yote nimeshawapa ya wapi wanatakiwa kwenda kujificha. Mambo yakitulia tutaanza tulipoishia… ninyi si mmesikia huyu Rais wa Tanzania anachosema, haya maneno si ya kupuuzia hata kidogo, hah hah hah nevey atafurukuta tu na kina Gupter lakini kamwe hawezi kuigusa Embriyo… san asana nayeye namweka kwenye hesabu, anatakiwa auawe!” Jaffer akawaambia navijana hao wakamkazia macho kumtazama kana kwamba ni mara ya kwanza kumwona. Tajiri huyu akampa ishara mmoja wa vijana hao naye akamkabidhi bahasha kubwa, akaiweka mezani. Dakika hiyo hiyo wanadada warembo wa Kiarabu wakaingia katika sebule hiyo na kutoa huduma za vinywaji na vitafunwa kwa watatu hao.
Simu ya Jaffer ikapiga kengele mara tatu, akaiinua na kutazama kwenye kioo, “wamekaribia, dakika kumi zijazo watakuwa hapa,” akawaambia akimaanisha Martin na wenzake.
VIII
Jioni hii, Kamanda Amata, Chiba, Gina na Madam S walikutana Ofisi ndogo kwa majadiiano mafupi juu ya siku nzima ilivyokwenda.
“Mmefanya kazi kubwa sana nyie vijana!” Madam akawaambia viajana wake, “lakini kazi ndiyo kwanzaaaaa inaanza, mheshimiwa Rais amesema anawataka hao watu ama wawe marehemu au wazima,” akawaambia.
“Kasema hivyo?” Chiba akauliza.
“Ndiyo! Tena kasisitiza sana kabla ya kuondoka kuelekea Dodoma,” akawajibu.
“Sawa! Ni wajibu wetu daima kuweka rehani maisha yetu, kama atakavyo atawapata ama wafu au wazima,” Amata akajibu. Muda wote huo, Gina alikuwa kimya kabisa, hakutaka kuongea wala kujibu swali. Saa kama mbili hivi zilifuata za mkutano mzito wa kupanga kazi.
“Kutokana na hili, mkutano wa dharula umeamua kuunda kikosi cha wapelelezi kwa ajili ya kuwaska wauaji au magaidi hawa,” Madam akawaeleza, “Lakini hata hivyo ofisi ya muda ya usalama ya AU itakuwa hapa Dar es salaam na wamesema wanataka idara ya usalama ya Tanzania ilifanyie kazi hili,” akawaambia.
“Sisi?” Chiba akauliza.
“Ndiyo, sisi, ukiona hivyo, wametuamini… wameona kazi yetu leo tu, wamekubali…” Madam S akawaambia na kutabasamu.
“Tunaanzia wapi kuwatafuta hawa watu?” Gina akasema kwa mara ya kwanza.
“Wewe wajua,”
“Wala usijali, tutapata tu pakuanzia, kama tumegundua target yao tutashindwaje kujua pa kuwapata?” Chiba akauliza.
“Mnajua, Mwenyekiti wa AU ambaye ndiye Rais wa Gambia ameridhia sisi kuingia kazini kwa siri, na tayari ametenga fungu la kutosha hata kabla hiyo ofisi haijaanzishwa rasmi… Amata you are the leader! Tunasubiri tu idhini ya wengine hasa Baraza la Usalama, ” akasema na kumtazama kijana huyu mtanashati mwenye sura ya upole iliyoficha ujasiri wa hali ya juu.
“Tena nimefurahi kwa hili, nina uchungu sana, naomba tu walibariki, watu wachache hawawezi kutuletea uumbavu wao nyumbani kwetu,” Amata akazungumza.
“Ok, zaidi ya hayo, tukapumzike, nitakuiteni kama kuna taarifa nyingine ila kwa sasa endeleeni na shughuli zenu za kawaida za kujenga Taifa,” Madam S akamaliza kuwaambia na kuagana nao.
* * *
Siku iliyofuata, Martin na wenzake waliabiri katika ndege ya shirika la Kenya na kuiacha ardhi ya Afrika Mashariki kuelekea mafichoni.
“Wakitupata wakatambike!” Fredy akamwambia Martin aliyekuwa kimya muda wote.
“Ni kweli,” akafungua kinywa chake kusema, “ lakini Tanzania wameitia doa kazi yangu kwa mara ya kwanza, mpaka sasa bado nawaza wamewezaje kugundua nyayo na mbinu zetu,” akaongeza kusema, “bunduki yangu nimeiacha nah ii inaweza ikaleta shida kwenye mipango mingine,” akamaliza na kuinua bia yake aina ya Heineken iliyokuwa katika kijimeza kidogo na kuimiminia tumboni mwake yote kama ilivyo.
“Afrika haina utundu wala teknolojia ya kugundua sisi ni nani na wapi tulipo, mi naona wazi kuwa hakuna kazi rahisi tuliyowahi kuipata kama hii ya safari hii,” Amanda akaongeza.
“Hapana, kazi nyepesi haiwezi kuingia doa kama hii, hii kwangu ndiyo kazi ngumu sana, na inaendelea kuniumiza kichwa,” akaeleza.
“Tulia The hunter!” Amanda akamwambia.
Muda mfupi baadae wakatangaziwa kuwa wanatua katika Uwanja wa Ndege wa Lungi jijini Free Town, Sierra Leone. Mara baada ya kutoka na kuuacha uwanja huo walichukua gari na moja kwa moja wakaelekea katika mji mdogo wa Waterloo ambako kulikuwa na nyumba moja ya mashambani waliyoitumia kujificha mara wamalizapo matukio yao.
SIKU TATU BAADAE
KAMANDA AMATA alisimama mbele ya bosi wake, wima kabisa, kwa ukakamavu wa kiaskari. Pembeni yake yaani upande huu na mwingine kulikuwa na Gina na Chiba, kati yao na Madam S kulikuwa na meza kubwa yenye vitendea kazi vya kiofisi.
“Nimewaita rasmi, hii hapa mbele yangu ni barua kutoka ofisi ya Mwenyekiti wa Umoja wa Nchi za Afrika kitengo cha usalama. Kimeiomba Tanzania ifanye kazi ya kuwasaka watu hawa waliojaribu kufanya mauaji ya marais, wakamatwe popote walipo duniani.
Niliitwa Ikulu, nikapewa barua hii, ikiwa na maana kuwa kazi hii imeletwa rasmi katika kitengo nyeti cha huduma hatari na za siri TSA, ifanyie kazi. Name nimesimama hapa kuwatuma kazi hiyo. TSA 1 !” akaita.
“HOT”
“Nakupa jukumu sasa, kiofisi ufike popote inapohisiwa watu hawa wapo, kimwili na kiroho kwa njia yoyote ile wakamatwe, ikibidi lolote lifanyike, clear?” Madam akamwambia.
“For my people, For my Nation … nipo tayari!” akajibu.
Madam S akainua kabrasha lililokuwa mezani kwake na kumkabidhi mikononi, naye akapokea kwa mikono miwili. Kabrasha lile lilikuwa limefungwa kwa karatasi laini inayoweza kuonesha mpaka upande wa pili. Kilichofungwa ndani ni faili moja lenye karatasi kama hamsini hivi na juu yake kulikuwa na maandishi makubwa yaliyosomeka, ‘MAGNUM 22’.
“Najua unajua nini unapaswa kutenda,” Madam S akamwambia na kuketi tena kitini, kasha vijana wake nao wakaketi katika viti vyao, “kama mnavyojua hii ni kazi nyingine nzito, kumsaka muuaji ni sawa na kuwinda, maana hata yeye anajua kuwa anasakwa na anajua ni nini afanye ili asikamatwe, lazima ujue hesabu za magazijuto, lakini ninaamini kuwa mtaweza. TSA 2 utabaki hapa utamsaidia kaka yako kwa kila anachohitaji kiteknolojia, hakikisha umpotezi kwenye rada yako. TSA 5 utakuwa tayari kwa usaidizi wowote utakaohitajika,” akamalizia kwa kuwaambia.
Baada ya hapo Kamanda Amata na Chiba wakainuka tayari kuondoka, wakaagana na Madam S na kutoka nje y ofisi hio huku lile kabrasha likiwa katika mfuko wa karatasi. Safari yao iliishia Gezaulole, Shamba, huku ndiko mambo yote hupikwa.
* * *
Katika meza yenye umbo la yai, vijana hawa wawili waliketi kwa kutazamana, Amata akaweka kabrasha lile mezani na kulichana ili kujua nini kipo ndani yake. Ni karatasi kadhaa zenye maelezo mengi yanayohusiana na kile kinachodhaniwa kuwa ni kisa cha watu hao kutaka kumdhuru Rais, zaidi ya hapo kulikuwa na taarifa fupi ya mauaji ya Angola na Ivory Coast. Kwa ujumla ndani ya bahasha hiyo kulikuwa na kazi mbili kubwa, moja ni kufanya uchunguzi kama mauaji ya Angola, Ivory Coast na shambulio la Dar e salaam vina mahusiano na muuaji ni mmoja? La pili ni kuwa kama ndiyo, basi askew na atiwe mbaroni kwa gharama yoyote ile na kama siyo basi huyu aliyehusika na shambulio la Dar es salaam atafutwe. Sambamba na hayo yote palikuwa na picha za maeneo ambako matukio hayo yalifanyika katika nchi zote tatu na tafutishi chache ambazo zilipatikana tayari ziliwekwa vielelezo vyake.
Kamanda Amata akashusha pumzi na kujiegemeza kitini.
“Vipi?” Chiba akamuuliza huku akilivuta lile kabrasha na kuanza kulipekua. Kamanda hakujibu swali lake bali alibaki kimya akitafakari hili na lile.
“Nafikiri nianzie wapi, Angola, Ivory Coast au wapi!” akajisemea.
“Hapa, anzia hapa na kutoka hapa utakwenda huko kote,” Chiba akamwambia, naye akatikisa kichwa juu chini.
“Kuna mengi unayotakiwa kuanza nayo hapa nyumbani,” akamwekea picha moja mezani, iliyomwonesha kijana mmoja mrefu mwenye shingo nyembaba na nywele kama za Kisomali hivi.
“Huyu ni nani?” Amata akauliza.
“Huyu ni mhudumu wa mapokezi katika hoteli ya Kunduchi, alinipokea kwa furaha sana na kwake nimepata jambo moja tu…”
“Lipi?”
“Alinambia kuwa mwanamke huyu ana wanaume wengi… sasa inabidi kujua wanaume hao labda tutapata picha Fulani ya kuwasaka…” Chiba akasema.
“Good! Huyu lazima nimuone leo hii, najua kutoka hapa nitaweza kujua nini kinafuata…”
“Sawa! Hilo la kwanza, hapa kuna mpango wa siri ambao uliniwezesha kukujuza kuwa tageti ya jamaa ipo wapi, na mara moja katika faii hili nililolifuma chumbani mwa yule mwanamke limeeleza kila kitu ,mpango mzima,”
“Unasema?!” Amata akahamaki.
Chiba hakujibu, akachukua simu yake na kumpa Kamanda Amata, naye akaipokea na kuanza kuperuzi faili lile, kila alipozidi kwenda zaidi alijikuta akipigwa na bumbuwazi.
Kumbe mpango upo hivi! Akawaza huku akiendelea kuchambua na vya chini, “kwa hiyo ina maana sasa watakuwa safarini kuelekea Sierra?” akauliza.
“Kama wamefanikiwa kutoka nchini, basi watakuwa tayari wamefika nchini humo, lakini mpaka sasa sijapata habari yoyote iwe kutoka Uwanja wa ndege au bandarini au Ubungo, hamna kitu, ina maana wapo ndani ya nchi hii,” Chiba akasema.
“Hapana Chiba, hawa jamaa nakuhakikishia wameshatoka nchini, unakumbuka lile gari lao walivyolitumbukiza baharini? Na polisi wanamaji wamesemaje, ‘hatujaona gari wala nini’ nahisi sasa lile gari lina uwezo wa kutembea majini tena chini kwa chini…”
“Aaaaa Amata kaka, kwani hapa tupo kwenye muvi za James Bond?” Chiba akatania.
“Habari ndo hiyo, watu kama hawa kutokana na wanachokifanya lazima wajipange sana katika kutoroka, tungelipata gari sawa, halipo baharini, liko wapi? Washasepa. Haya umeenda Kunduchi kwa yule mwanamke umepata nini, ameondoka saa ngapi na kwa vipi, kuna uwezekano kabisa kuwa lile gari limesafiri kutoka hapa na kumchukua yule mwanamke kisha wakatokomea kwa njia hiyohiyo na kuvuka mpaka…. Na ukiangali kama wametoroka kwa njia hiyo, basi watakuwa Kenya,” Amata