Riwaya magnum22

Riwaya magnum22

MAGNUM22

Sehemu 6

Rejea SASA…
Uwanja wa ndege wa Kimataifa wa LUNGI
FREETOWN – SIERRA LEONE
CHIBA WA CHIBA aliwasili katika uwanja huo mkubwa kabisa usiku wa saa nne, mara tu baada ya kutoka nje hakutaka kupoteza muda kwani alikuwa na mengi ya kufanya kichwani mwake, kubwa zaidi ilikuwa ni kumpata Kamanda Amata ambapo mpaka dakika hiyo alikuwa akijua kwa uhakika mkubwa kuwa yupo katika nchi hiyo kwa kufuata ishara ya GPS ya simu aliyotumia. Hoteli aliyoipenda na kuichagua ni ile ya Light House, mwendo kama wa saa moja hivi kutoka uwanja wa ndege. Saa sita hivi akawasili katika hoteli hiyo, akapokelewa na kupata chumba.
Ndani ya chumba hicho kulikuwa na kitanda kikubwa na kiti kimoja chenye meza ndogo, akabwaga vitu vyake na kuifuata bafu, akajimwagia maji kisha kurudi ndani ya chumba hicho. Saa ya ukutani kamwashiria kuwa ni karibu saa saba usiku, Chiba hakuwa hata na lepe la usinginzi.
Maadam nipo hapa, lzima kamanda apatikane! Akawaza wakati akiwasha laptop yake na kuanza kuweka hai mtandao yake anayoijua mwenyewe. Safari hii alipoitafuta ile namba hakuipata hewani hivyo hakuweza kujua ni wapia au upande gani ambao mtu wake atapatikana, akaachana na hilo na kuendelea kup-ekua hiki na kile mpaka usingizi ukampitia mezani hapo.
Asubuhi kulipokucha kabla ya kufanya chochote, kwanza alifungua tena kompyuta yake na kutafuta uelekeo wa namba ile ambayo Amata allitumia siku mbili nyuma. Haikumsumbua, baada ya kuingia kwenye mtandao wa simu za nchi hiyo na kuvunja kodi kadhaa za kizuizi, akafanikiwa na kugundua kuwa uelekeo wa namba ile ni mahalia panapoitwa Waterloo. Akazidi kuichimba katika mtandao ikamwonesha umbali na uelekeo mji huo. Shauku aliyokuwa nayo ilimfanya hata asitamani kupata staftahi. Moja kwa moja baada ya kujiweka sawa akafika mapokezi na kutafuta usafiri wa kukodi wa kuelekea huko aendako. Akapata gari za watalii na kuikodi.
“Muda gani kutoka hapa?” akamuuliza dereva.
“Ni kama saa moja na nusu hivi,” akajibiwa.
“Sawa, sasa twende kisha tutarudi baadae…” akamwambia na safari ikaanza kuelekea huko Waterloo, mji mdogo Kusini mwa Freetown. Ndani ya gari lile alikuwa ametulia kimya kabisa katika siti ya abiri akitazama mandhari ya nje, milima na misitu minene, vijiji na mambo mengine mengi. Mazungumzo machache tu yalitawala kati yao kama kulikuwa na ulazima. Saa moja na nusu haikuwa muda mrefu kwao, waliwasili katika mji huo mdogo na kusimama mahali.
“Hii ndiyo Waterloo… kama unavyoona ipo kandoni mwa mto mkubwa wa Lofa…” yule dereva akamwambia Chiba.
Chiba akaanza kucheka.
“Vipi mbona wacheka?” dereva akamuuliza.
“Mto Lofa? Sisi kwetu hilo jina ukimwita mtu lazima akufundishe adabu,” akamjibu huku akiinua tablet yake na kuangali uelekeo wa anakotaka kwenda.
“Nipeleke bandarini…”
Yule dereva akawasha gari na kuendelea na safari huku akipita katikati ya nyumba zilizochoka, barabara zenye matope na madimbwi makubwa ya maji.
Nilifikiri njia kama hizi ni kwetu Sumbawanga tu, kumbe hadi huku! Akawaza. Lile gari likasimama kando ya bandari ndogo na tayari watoto wanaouza samaki walifika dirishani kuchuuza biashara yao.
“Kaka hapa ndo’ bandarini, umesema mwenyeji wako anapatikana hapa?” dereva akauliza, Chiba akajifanya kama hajasikia nini kaulizwa akamwita kijana mmoja na kumuuliza.
“Unamjua mtu mmoja anaitwa Hamadou?” akamuuliza.
“Hamadou? Huyu mvuvi?” yule kijana akauliza ili kupata uhakika wa jibu atakalotoa.
“Ndiyo!” Chiba akajibu hata kama hakujua kuwa huyo mtu ni mvuvi.
“Ndiyo, hakuna mtu asiyemjua Hamadou hapa mjini, ni mtu mwema mwenye kumcha Mungu, na sasa yupo paleeeee, ile ni nyumba ya dada yake!” akajibu.
“Asante sana,” akamshukuru na kumpatia noti ya dola ishirini kisha lile gari likaenda mpaka kwenye nyumba ile.
Chiba akateremka na kubisha hodi kwa kuugonga mlango, ukafunguliwa na mwanamke mwenye sura ya mviringo iliyojaa nyama mashavuni mwake. Akaeleza shida yake na kukaribishwa ndani. Dakika tatu nne baadae hakuamini kumuona Kamanda Amata mbele yake, akainuka na kumkumbatia kwa nguvu mpaka kila mtu akawashangaa.
“Hamadou, huyu ni kaka yangu,” Amata akamtambulisha kisha akawatambulisha kwa Chiba. Baada ya maamkiano hayo, mazungumzo ya msingi yakafuatia.
Saa mbili zilizofuata, Chiba na Anata wakawa tayari kuondoka, dada wa Hamadou alishindwa kuficha hisia zake na kuangusha machozi. Amata akambembeleza na kumuahidi kurudi kumsalimu.
* * *
HOTELI LIGHT HOUSE – FREETOWN
“Pole sana Kamanda!” Chiba alimpa pole mara tu baada ya kufika katika chumba ambacho alipanga kwa ajili yake.
“Nimeshapoa, unajua ni baada ya kuwasiliana na wewe, juzi ndo nimejua kuwa nipo bado Sierra Leone, Chiba nimeingia mpaka kaburini,” akamweleza.
“Pole, mama yako mvi zimemwongezeka, Gina, yeye ndo akikukumbuka tu machozi, kwa ujumla tulichanganyikiwa, nimekuatafuta siku tano bila kulala kwa maana, kodi zako zote hazisomi,” Chiba akamwambia. Amata akavua shati na kumwonesha kidonda katika paja la mkono wake.
“Wametoa chip na kuiharibu vibaya, wameninyang’anya simu zote na kuzipondaponda, nikabaki mimi tu, mateso niliyoyapata, Chiba, acha kabisa nilijua siponi lakini Mungu mkubwa…”
“Umeokokaje?”
“Kuna marehemu alinisaidia maana sote tulikutana katika kaburi moja,” Amata akaeleza maelezo ambayo Chiba hata hakuyafahamu maana yake nini.
“Kaburini kivipi?”
“Wale jamaa wana kaburi ambalo mtu akifa wanamtupiamo, sasa walijua mimi nimekufa wakanitupia humo, na humondani nikakutana mtu ambaye alikuwa dakika zake za mwisho za kukata roho, huyu ndiye akaniokoa mimi. Alinipa ishara nichukiue mkanda wake, huu hapa!” akamwambia na kumpa ule mkanda, kisha akendelea wakati Chiba kauchukua ule mkanda, “alipokufa na mimi hali yangu ikawa mbaya sana, nikaufunga ule mkanda kinoni kumbe haukua mkanda wa kawaida bali ni rimoti ya bomu,” Amata akamwelezea Chiba kila kitu mpaka alipojikuta katika boti ya akina Hamadou.
“Mh! stori yako imekomaa braza!” Chiba akamwambia huku akiinuka na kumtazama jeraha lake la kisogoni.
“Nilipigwa na kitu kama nondo sijui panga, likanizimisha kabisa,” Amata akasema bila hata kuulizwa.
“Pole kaka, sasa hapa inabidi kufanya mpango wa kurudi nyumbani Tanzania kwanza,” Chiba akamwambia.
“Najua, ila hii kazi lazima iishe,” Amata akasisitiza.
“Ndiyo ila kwa sasa inabidi turudi, kwanza tukaufanyie checkup mwili wako kisha majukumu mengine yatafuatia,” Chiba akamwambia.
“Umesomeka!” Amata akajibu bila ubishi maana alijuwa kuwa Chiba ni mjumbe wa Madam S hivyo anachomwambia ndicho alichoshema Madam S.
“AU imeunda timu mpya ya upeleelezi katika hili…”
“Wamechemka!”
“Kwa nini?”
“Kaka huu mtiti mwingine, mimi nimefika tayari paleee ambapo wapo, kumbuka ile shughuli pale Dar, kumbuka lile timbwili kaka, mi nimefika huku nimejitoa sadaka na ndiyo hivi, sikuwa duniani kama siku tatu hivi na moja ya nyongeza.

















VI












MIEZI MIWILI ILIYOPITA
DAR ES SALAAM
BAADA YA MAUAJI yaliyotokea Angola na Ivory Coast kuutikisa Umoja wa nchi huru za Afrika, iliazimiwa kuongeza ulinzi kwa viongozi wake na ikawa hivyo. Kikao cha viongozi wa juu wa umoja huo kikapangwa kufanyika katika ukumbi wa Hoteli ya Kilimanjaro, na ajenda kubwa ya kikao hicho ilikuwa ni kuhusu mgogoro wa kiutawala katika nchi ya Somali land.
Iliaminiwa kuwa Tanzania ni nchi ya amani na usalama wa hali ya juu hivy, kikao hiki kilitakiwa kuwakutanisha marais sita na mawaziri kama kumi hivi ambao ndiyo hasa walikuwa na maamuzi ya mwisho kabisa katika hilo. Wakati wao wakipanga mpango huo wa kukutana Dar es salaam, kulikuwa na makundi mengine mawili nayo yakipanga mikakati juu ya kikao hicho hicho.
Mara baada ya taarifa kufika Ikulu, Rais akaona ni vyema sasa kuviweka vikosi vyake anavyoviamini kabisa kiusalama tayari. Mara baada ya kuzungumza na Mkuu wa Jeshi, Polisi na wengine wote hasa makachero wenye pua kali za kunusa. Jioni ya siku hiyo alimwita Madam S katika afisi yake nyeti na kuzungumza juu ya ujio huo.
“Kwa ujumla wageni wa kidiplomasia watakuwkama ishirini na mbili hivi na wale top kabisa watakuwa marais sita na mawaziri wawakilishi watatu na wengien watakuja kadiri ya kazi zao” akamwambia.
“Selina! Unajua kilichotokea Angol na Ivori Coast naomba uwe makini na vijana wako katika yale maeneo nyeti,” akamsisitizia.
Madam S alibaki kimya akimsikiliza huku akikumbuka hisia kali TSA 1 juu ya mauaji ya Rais wa Angola na Waziri Mkuu wa Ivori Cost, sipendi vitu kama hivyo vitokee katika nchi yangu, hakikisha mnafanya kazi, unaweka watu wako na kumkamata yeyote atakayeonekana kutaka kuharibu mkutano huu, kwa sababu pia ndiyo utakaoamua mchakato wa uchunguzi wa vifo hivyo,” akasisitiza huku akiipigapiga meza yake kwa ngumi.
Mara baada ya kutoka katika kikao hicho, Madam S aliwatumia ujumbe wa maandishi vijana wake na kuwataka nyumbani kwake Masaki kwa kula na kunywa usiku wa siku hiyo. Lakini lengo lake lilikuwa hasa kuzungumza nao juu ya kazi hiyo ambayo inawakabili ndani ya saa sabini na mbili zinazofuata.
* * *
Usiku wa siku hiyo, TSA wote walikutana nyumbani kwa Madam S kama walivyoitwa, kweli jiko kubwa la kuoka nyama lilikuwa limekokwa moto huku yeye mwenyewe akiwa bize kuwekaweka mafuta ili nyama iwe tamu, nzuri na laini.
“Leo Madam umeamua, umetuwekea mavitu si ya kifala,” Amata akamtania.
“Ee mle mnywe maana kazi yenyewe hii tufanyayo haina guarantee watoto wangu…”
“Aaaa kabisa,” Chiba akadakiza.
Kama ni swala la pombe kwa vijana hawa halikuwa la kuwasumbua vichwa, walikuwa na uwezo wa kunywa mpaka asubuhi lakini pale wanaptaka pombe ziwatoke huwatoka, wanajua wao ni kityu gani hupenda kula ambacho huwafaya warudi haraka katika hali yao ya kawaida.
“Sasa- mama- anatupatia- neno- linaloendana- na- kinywaji- hiki….,”Scoba akazungumza kilevi kidogo kisha akajitupa kochini. Madam S akawakusanya vijana wake nao wakasogea kwa karibu sana ili kuhakikisha ni nini hasa mwanamama huyo anataka kuwaambia.
“Wandugu, mi nimewaita hapa tufurahi, lakini zaidi ya hilo pia nataka niwajuze juu ya kazi yetu ya mbele hapahapa mjini tumeombwa tuitupie jicho. Tunajua kuwa hata kama tusingeombwa hii ni moja ya kazi yetu lakini ka sasa ni agizo kutoka kwa mheshimiwa Rais, hatuna budi kuitilia mkazo…” Kawaambia nao wakatikisa vichwa.
“Mkuu hataki nchini mwake yatokee ya Angola na Ivory Coast, anataka tutupe jicho kila mahala ili tuweze kujua kama kuna hila yoyote,” akaongeza.
“Sawa, unajua tunafanya hii kazi bila kujua kwa undani kabisa kama muuaji wa hawa watu ni mmoja na anaweza kuwa tayari yuko nchini, sisi tutatazama kesho kutwa wakati yeye tayari kaingia muda mrefu anatutazama tu…”
“…sijamaanisha keshokutwa ndo tuanze kazi, tukitoka tu hapa ndo kazi hiyo ianze kila mmoja akae kwenye kona yake ya kawaida na tuendelee kuwasiliana.” Madam S akamkatiza Amata.
“Nikirejelea mauaji ya Rais wa Angola najaribu kujenga mahusiano, na nikitafakari ujio wa wajumbe wa juu wa AU hapa Dar’ nahisi muuaji keshafika, maana muunganiko naupata kwenye chanzo cha mauaji na ule ujumbe wa video ambao tumeuona. Anasema ‘nataka AU iachie kipande cha Somali land kijitawale’. Kichwa kinaniuma Madam, ila tuwe tayari kwa lolote siku hizo,” Amata akaongeza kusema.
“Ndiyo, na ni la msingi sana!” akamalizia kusema.
“Ila wanausalama wa Angola na Ivori Cost nawafikiria sana, yaani wameshindwa hata kupata fununu? Maana mambo haya katika kuyachunguza inabidi ucheze na pande mbili tu, wasije wakajaribu hapa, lazima tuishangaze dunia kama tunavyoishangaza kila siku” Amata akaongea huku wenzake wakitikisa vichwa kumuunga mkono.
* * *
Msako wa wauaji ulikuwa ukiendelea kimya kimya katika nchi hizi mbili; yaani Ivory Coast na Angola. Nchi hizi mbili kila moja kwa wakati wake na kwa mtindo wake ilikuwa ikihaha kila kona ya nchi kusaka nani alifanya haya. Angalau kwa Ivory Coast, walikuwa na picha ya video iliyonaswa na na CCTV za hoteli ile ikimwnesha mtu anayehisiwa na kupewa utambulisho wa jina ‘UP’ yaani Unknown Person. Zaidi ya hapo walikuwa na cha kuzungumza walau kusema ‘mtu huyo aliingilia chumba namba 660 na kuwalaza usingizi wapenzi wawili. Lakini kwa Angola ikawa ngumu kujua hata uelekeo wa muuaji ulikuwa wapi.
Usiku wa Siku hii Amanda Keller alikuwa akijiandaa kwenda Uwanja wa ndege kumpokea Martin Gupter ambaye alibaki yeye tu kuwasili Dar es salaam ili kutekeleza mauaji ya tatu kadiri ya matakwa ya mteja wao. Walichotakiwa kufanya wakiwa katika jiji hili ni kuhakikisha wanapata taarifa zote za mkutano kwanza, kama zitakuwa zimeenda vyema kwa mteja nwao wasi zoezi lihairishwe na litakuwa limeenda ovyo basi aliyekusudiwa auawe. Fredy tayari alikuwa jijini karibu siku nne nyuma na alishapanga mambo yake yote tayari kwa kumsaidia Martin kukimbia. Amanda Keller aliwasili uwanja wa ndege wa Julius Nyerere saa nne za usiku, saa mbili kabla ya Martin kuwasili na ndege ya KLM. Alikuja muda huu makusudi ili kuona kama mtego wowote uwanjani hapo, alichopaswa kufanya ni kumpokea mgeni wake na mara moja kumkuimbiza hotelini anakotakiwa kufikia. Nje ya gari lake aliangaza macho huku na kule akisaidiwa na taa za maegesho zilizokuwa zikirusha mwanga wa dhahabu na kufanya eneo hilo kupendeza. Akavuta hatu na kuufikia uwanja huo haswa katika eneo la kusubiria wageni naye akajichanganya na watu waliokuwa katika eneo hilo wakisubiri ndugu na jamaa zao.
Saa sita usiku ilipotimia, dege kubwa la KLM liliwasili na kuingia maegeshoni tayari kuteremsha watu walioabiri katika shirika hilo. Martin Gupter alikuwa mmoja wapo wa abiria hawa. Siku hii alivaa kanzu ndefu ya Kiislam kutoka Oman, mkononi alikuwa na tasbihi aliyokuwa akiizungusha zungusha kwa vidole vyake, mkato wa ndevu zake, kwa vyovyote ungekupa shida ya kumtambua kuwa si mwarabu, alijua kujibadili na alijibadili haswa. Moyo ulimshtuka sana aliposikia tangazo ya kwamba abiria wte waliokuja na ndege hiyo wasubiri ndegeni kwa dakika kama kumi au kumi na tano.
Mh! Hii sijawahi kuishuhudia. Akawaza hukua akiendelea kuhesabu tasbihi kana kwamba anajua nini huwa wanasema katika hiyo. Akainua simu yake na kutuma ujumbe mfupi kwa mwenyeji wake.
‘Tumeambiwa tusubiri dakika kumi na tano kisha tutateremka, vipi nipe habari za huko duniani’
‘Huku shwari, nipo nje nakusubiri, sijajua kama kuna tatizo au ni nini!’ akajibiwa.
Baada ya dakika hizo kukamilika mlango ukafunguliwa na mmoja mmoja akaanza kuteremka. Martin Gupter akazishuka ngazi akiwa katikati ya watu, akavuta hatua na kuingia ndani ya uwanja huo kwa ukaguzi. Baada ya kuonekana kuwa pasipoti na vibali vyake hazina mawaa yoyote, afisa uhamiaji akamruhusu kupita huku wengine wakisubirishwa kwa sababu hii na ile.
Saa saba hii, usiku mnene, TSA walikuwa wamewasili uwanjani hapo kwa kazi maalumu mara tu baada ya kuachana na Madam S. Walitakiwa kuanza kazi mara moja, wakakubaliana kuwa kazi ya kwanza itakuwa ni katika Uwanja huo maana kwa vyovyo ni asilimi themanini wageni huingilia hapo. Ijapokuwa walijiuliza kama mwenye nia mbaya atashukia Kilimanjaro itakuwaje, wakaamua kupiga ngumi kichakani.
“Tumechelewa kuingia kazini, lakini si mbaya, kama kuna mmuaji basi mjue huwa anaingia si chini ya saa kumi kabla ya kutekeleza kazi yake,” Amata aliwaambia kabla hawajafika uwanjani hapo. Na mara baada ya kuwasili wakaingia katika afisi ya usalama ambapo huwa wanaonana na mtu mmoja tu, ni yeye pekee anayewajua watu hawa na kazi yao ijapokuwa naye anafahamu tu kuwa ni wanausalama, hajui kiundani zaidi.
Lulu alikuwa nyuma ya kompyuta kubwa katika afisi hii ambayo mtu huweza kuona kila kinachotukia katika uwanja huo. Ofisi hii inayoshughulika na maswala ya usalama wa uwanja huo, huwa haiingiwi na mtyu mwingine zaidi ya watu watatu tu; yaani Lulu na wengine wawili lakini mwanamke huyu alikuwa mtumishi wa Usalama wa Taifa Tanzania na aliwekwa hapa makusudi.
“Tunaanza na KLM,” Amata akamwambia Lulu.
“Mnenembia mapema kuna ndege nyingi sana leo zimeingia ukizingati huu mkutano, aaaa waandishi wa matelevisheni, maredio, magazeti wameshuka siku hii, nahisi mahoteli yamejaa,” akamjibu Amata ambaye alikuwa tayari ameshachagua siti na kuketi, huku Gina akiwa upande wa pili.
“Unajua, hisia zangu zimenituma nije usiku huu, nimezitii…” akasema huku akitupia macho kwenye luninga ambayo iliunganishwa na mashine ya xray inayokagua mizigo kwa kupiga picha kwa ndani na kuweza mtu kuona nini na nini kipo.
“Waruhusu!” akamwambia. Lulu akapiga simu na abiria wakaanza kupita kwa ukaguzi, Lulu na Gina wakatingwa kutazama abiria hao mmoja baada ya mwingine kama kuna sura watakayoitilia shaka huku Amata akaitzama mizigo tu inaypita katika mashine hiyo.
Ni mzigo mmoja, uliokuwa katikati ya mingine uikamtia shaka kijana huyu ambaye macho yake na akili hufanua kazi kwa haraka sana.
“Stop!!” akamwambia Lulu, naye akabonya kitufe kimoja na ile mashine ikasimama. Opareta wa mshine ile akaendele kubonya bonya kitufe lakini mashine haikuwa inatembea, hakujua kama kuna sehemu itakuwa imesimamishwa la. Dakika chache, mashine ile ikaanza kutembea tena.
“Gina, anaglia ni nani anachukua mzigo huo hapo,” akamwonesha kwa kidole kwenye luninga kubwa, naye akaanza kukodolea macho kwa makini. Amata hakumwambia mtu kama nini amekiona katika mzigo huo ila alitaka kujua tu ni nani kaupokea. Kutoka kwenye luninga ile, gina alimwona kijana aliyevalia Kiislam akiuchukua mzigo ule pamoja na mingine kisha akaipakia kwenye kitoroli tayari kutoka nje.
“Anatoka nje!” Gina akmwambia Amata.
“Mfuatilie!” kisha akamtzama Lulu, “we mwanamke, kamera za nje zinafanya kazi?” akamuuliza.
“Ndiyo, zote mpaka za Barabarani kuleeee zinafanya kazi,” akamjibu.
“Gina!” akaita, “hakikisha unajua mpaka taxi gani kapanda au gari gani,” akamsisitizia na msichana huyo akahakikisha anatimiza hilo.
Huko nje, Martin Gupter alikutana na mwenyeji wake, Amanda Keller, wakakumbatiana na kwa bashasha na kunyonyana ndimi kwa sekunde kadhaa ikiwa ni moja ya njia ya kuwafanya watu waelewe kuwa hao ni wapenzi kumbe hamna chochote. Baada ya hapo wakakokotana mpaka kwenye maegesho na kuingia ndani ya gari alilokuja nalo.
“Kila kitu kipo sawa?” akamuuliza Amanda.
“Yes!” Amanda akajibu huku akilitekenya gari lile na kuanza kuondoka taratibu.
Huku ndani, kamanda Amata akainuka kitini, “Vipi kuna ndege nyingine international kwa sasa?” akamuuliza Lulu.
“Hamna, ni mpaka kesho saa sita mchana!”
“Ok, kama kawaida, ukimshuku mtu tupatie taarifa haraka, tupo kwenye hatari sana siku hizi,” Amata akamwambia mwanamke huyo huku akitoka na Gina.
Wakiwa kwenye ngazi za kuteremka chini, Amata akamsimamisha Gina na kumtazama usoni, “umefanikiwa?” akamuuliza.
“Yes!”
Wakaendelea kutembea mpaka chini, Amata akamwongoza Gina mpaka ndani sehemu ya kufikia wageni, akaenda naye mpaka dirisha ambalo wanahisi huyo mtu alipita kwa ukaguzi wa pasipoti. Hapo wakamkuta mwanadada mmoja mrembo tu ameketi akiendelea kuweka mambo yake vizuri na taarifa pia.
“Samahani afande!” Gina akamwambia na kumwonesha kitambulisho chake cha polisi.
“Sisi ni polisi wa usalama hapa Uwanjani, samahani, kuna mgeni kapita hapa kwako, ni kijana amevaa kanzu hivi….”
“Ameshika tasbihi mkononi?” akamalizia mwanadada huyo.
“Yes!”
“Enhe….”
“Tunahitaji taarifa zake ambazo umekusanya tafadhali,” Gina akasema huku tayari mkono wake ukiwa ndani ya kidirisha kusubiri kama ni karatasi atapewa au ni kitu gani.
“Taarifa za mtu ni siri, nafikiri unajua…”
“…ndiyo najua!”
“Kwa hiyo kuna karatasi ya kusaini kabla hujazichukua,” akamwambia.
“Lete nisaini, fasta fasta basi,” Gina akamwambia kisha akapokea hiyo karatasi na kuisaini, akamrudishia, yule mwanadada akapriti karatasi fulani na kumpatia.
“Asante sana, msalimie shemeji….” Gina akamtania huku akicheka.
Safari yao ikaishia kwenye gari lao, wakaingia ndani na kujifungia kimya, gina akiwa nyuma ya usukani na Amata katika kiti cha abiria. Akampa lile karatasi, akalipokea na kulisoma vizuri kabisa.
“Abdulah El Marik, miaka 27, kutoka Oman…” akatamka Amata.
“Madumuni ya safari!” Gina akasema, nambie tafadhali.
“Sawa boss nitakwambia sasa hivi… mmmm likizo kwa mke wake Fatma Mansoor wa Kinondoni, unalingine Boss?” akamtania. Gina alikuwa macho mbele muda wote.
“Haiingii akilini hiyo, mwanaume katoka Oman kuja kwa mkewe Tanzania, mh! Halafu anakuja likizo, hapo moja jumlisha moja tatu,” Gina akamwambia Amata.
“Kwa hiyo…” Amata akamwangalia Gina huku akiikunja ile karatasi.
“N’na mashaka na hilo…”
“Wamechukua gari gani?” Amata akauliza.
“Gari binafsi, Lexus jeusi short chasis!” akamweleza.
“Ok, twende tukalale shamba!” Amata akamwambia na mwanamke huyo akaondoa gari kwa kasi na kuingia barabarani kuelekea mjini. Safari yao ilikuwa ya kuelekea Kigamboni mpaka Gezaulole ambako jingo lao la siri, ‘Safe House’ au wao hupenda kuliita ‘Shamba’ lilikuwako.
“Tukalale? Au tukafanye…”
“Tukafanye nini…”
“Umeshaanza, tukafanye kazi he!”
“Utafanya kazi mwenyewe mi nalala!” Amata akajibu huku akifyatua kiti na kujilaza.
* * *
Amanda akaegesha gari kando ya Barabara ya Nyerere kwenye service road nje ya jengo la Quality Group.
“Kuna njia mbili za kutekeleza mauaji ya kesho…” Amata akamwambia.
“Ipi na ipi?”
“Ama kudungua au kutumia mikono,” akamwambia.
Martin akakaa kimya kwa sekunde kadhaa akitafakari hilo aliloambiwa, “Amanda! Nahisi kazi ya safari hii itakuwa ngumu sana…” akamwambia.
“Kwa nini?” Amanda akauliza.
“Lazima watakuwa wamejipanga sana, baada ya bosi kuwatumia ule ujumbe ni kama kawaamsha…”
“Of coz, ulinzi upo tight sana, nimeshuhudia kila aliyeingia, ni kweli, inabidi tufanye kazi, kazi ya akili…” Amanda akamwambia.
“Anyway, twende hotelini kwako tukayaweke sawa,” Martin akamwambia Amanda kisha gari lile likaondoka tena kwa kasi ileile kuelekea mjini.
* * *
HOTELI YA GOLDEN TULIP
AMANDA, MARTIN na FREDY walikuwtana pamoja ndani ya chumba hiki ambacho kwacho mwanamke huyu aliweka makazi. Walikuwa mkononi na saa kama thelethini na nne hivi kujua kama waue au waondoke.
“Hii ni ramani ya Dar es salaam!” Amanda akawaonesha baada ya kufanya tafiti na kujifunza mengi ya jiji hilo, na kufanikiwa kupata ratiba nzima ya mkutano siku hiyo, na orodha ya nani na nani watakuwepo.
“Ukumbi wa mkutano ni huu, unaitwa Nyerere Conference, upo mita chache sana kutoka State House. Hili eneo limezungukwa na majengo au taasisi za serikali tu na ziko katika mpangilio maalum ambao ni vigumu kufanya shambulizi kama tulifikilialo…” Amanda akaeleza.
“Unamaanisha nini…”
“Namaanisha kuwa hii kazi hapa si ndogo, inahitaji akili ya ziada…” Amanda akasema huku Fredy akiwa kabaki kimya.
Martin akamgeukia Fredy na kumtazama, “tutatorokaje?” akamuuliza.
“Usijali, tutaondoka kwa njia ya maji,” akamwambia.
“Umeandaa boti?”
“Usijali, tutaondoka tu,” Fredy akawahakikishia. Kisha wote wakarudi kwenye ramani ile na kuendelea kuichambua.
“Amanda! Nafikiri hapa ni pazuri sana,” akamwoneshea jingo ambalo lipo mkabala na ukumbi huo wa mikutano ambalo limetenganisha na barabara na majengo kadhaa. Wakaingia kwenye Google Map na kulitazama jingo hilo.
“Yes! Hii ni target nzuri sana ndugu zangu, kama ni kuua lazima hawa watatokea mlango huu, sasa tazama hili jengo kwenye picha hii… ni refu kuliko mengine… lina ghorofa kumi na nne, nikikaa juu kabisa nina uhakika Napata shabaha nzuri hasa wakati wanapiga picha…” Amanad akatikisa kichwa kisha akachukua ratiba na kuitazama.
“Hah! Umejuaje kama kuna kupiga picha?”
“Nishasoma!” akamjiabu.
Baada ya mazungumzo na majadiliano hayo mipango ikasukwa vyema, siku ya pili ilikuwa ni siku ya kupanga mambo tu ikiwamo kutega vyombo vya kunasa sauti na kuangalia jingo hilo jinsi lilivyokaa ili kama umbali utakuwa ni tatizo basi watumie mbinu nyingine.
* * *
Usiku ule, Amata, Gina na Chiba walikuwa mezani wakizungumza jambo bila kujua kuwa upande wa pili wa bahari kuna wengine nao watatu kama wao wakiwa na mwanamke mmoja nao waikuwa wkipanga hayo hayo.
“Unajua, lazima tuwe makini sana na huu ugeni, na inabidi tufanye kazi kwelikweli maana hawa wauaji ni wajuzi, hatujawahi kuwaona sura wala kupata wasifu wao, sasa hapa ni hatari sana, lakini mi narudia tena huyu mtu lazima tumchunguze…” Amata akawaambia wenzake.
“Umegundua nini?” Chiba akamuuliza.
“Sikiliza, kati ya mizigo yake kuna mmoja una bunduki kubwa, kwa harakaharaka hata kama sijaijua ni aina gani ya silaha naihisi ni Magnum 22 riffle,” akawaambia.
“Sure?” Gina akauliza.
“Yes! Huyu lazima kesho jua lisilale, tupate habari zake zote….”
“Amata! You are right!” Chiba akainua macho yake kutoka kwenye kompyuta na kmshtua Amata.
“Nini Chiba?”
“Abdulah El Marik, ambao nawaona hapa wote hawamechi…. Alama zake za vidole haziendani na jina, wala sura inakataa, huyu aliyejifananisha naye, tayari ni marehemu!”
“Kwa hiyo?” Gina akauliza.
“Tulale, kesho tutaanza nay eye,” Amata akamwambia.
 
Asante ila jamani mtu ukisafiri si hauruhusiwi kusafiri na silaha. Kama hapo airport kwenye mashine imeonyesha ana silaha kwa nini ameruhusiwa kupita au huko alipotoka pia ameruhusiwa kupita.mmh utamu kolea
 
MAGNUM22

Sehemu 7

Siku iliyofuata…
Ujio wa rais wa Gambia ulikuwa asubuhi kwa sababu siku hiyo hiyo alitakiwa kutembelea sehemu kadhaa za jiji. Barabara ya Nyerere ilifungwa kwa takribani nusu saa hivi na kusababisha jiji zima kusimama. Ulinzi ulikuwa wa hali ya juu, askari wa mbwa na farasi walikuwapo achana na wale wa kawaida na wasiovaa sare. Kila mtu alishangaa kwa nini rais huyu apewe uinzi zaidi hata ya yule wa kwetu! Hawakuweza kupata jibu kamili bali kubabiababia tu; labda kwa sababu mgeni, hapana ni kwakuwa ni Mwenyekiti wa AU, kila mmoja akasema lake.
Asubuhi ya siku hiyo wanausalama walikuwa wametingwa kuhakikisha usalama wa kiongozi huyo, ujumbe uliotumwa na Jaffer Bakhari uliwapa tensheni ya kuongeza ulinzi wa siku hiyo.
Upande wa pili wa jiji hilo, mita chache kutoka Ikulu ambako mgeni huyo angefikia, Kamanda Amata aliegesha gari nje ya geti la kuingia ‘Ofisi Ndogo’, akateremka na kuingai akatika ofisi hiyo ambamo alimkuta Madam S akiwa ametingwa na kazi huku akipokea simu hii na ile.
“Karibu!” bakamkaribisha Amata, “vipi mbona kama una ari ya bjambo fulani?” akaongeza swali.
“Of coz! Ni hivi, jana usiku kwa ndege ya KLM kuna mtu kawasili nchini ambaye tunamshuku kwa hatari zote. Sasa wasiwasi wangu asije kuleta madhara kwani mpaka sasa bado tunamfuatili nyayo zake. Naomba uwasiliane na watu wa usalama huko uwanja wa ndege na kwenye msafara wake ili wawe na tahadhari zote…”
“Kwa nini unamhisi?” Madam akamuuliza.
“Katika begi lake kuna Magnum 22 rifle, halafu katumia sura ya bandia, na mwenye sura hiyo tumegundua kuwa ni marehemu…”
“Nyie vijana mshafika mbali hivyo!”
“Umetuambia tufanye kazi na ndiyo tulianza jana ile ile…” akamwambia.
“Sawa, hiyo ni habari njema na inabidi adhibitiwe kabla hajaleta madhara..” Madam S akasema hivyo huku akiwa tayari keshaweka simu sikioni na kuwasiliana na wahusika. Taarifa hiyo iliwasha moto usiotegemewa, wanausalama wakahaha wakipita kila jingo karibu na barabara ambayo rais huyo anategemewa kupita.
“Madam S akamwangalia kijana wake…”
“Una akili za ajabu sana, ina maana kama usingechukulia maanani maagizo yangu ya jana basi labda ntu huyo angetuletea madhara ambayo hatukuyategemea,” akasema.
Huko uwanja wa ndege hali ilikuwa tafauti baada ya kupata ujumbe huo, ilibidi wanausalama wajipange upya, baadhi ya wanajeshi wakachukua nafasi kwa ombi maalumu wakashika doria hapa na pale, wakitumia darubini kubwa na zenye nguvu kutoka juu ya majengo wakitazama kila mahali.
Saa mbili baadae, wanausalama wakaufikisha msafara wa rais huyo salama kabisa Ikulu, wakati huo Amata na Madam S walikuwa ndani ya gari karibu kabisa na kona ya mwisho ya kuingia Ikulu.
“Wamefika salama, asante Mungu!” Madam S akashusha pumzi ya nguvu.
Amata akainua simu na kumpigia Gina kujua upande gani wa jiji alipo.
“Nipo, Tazara junction!” akajibu.
“Fika ofisi ndogo mara moja!” akamwambia na kisha akashuka na kuliacha gari la mwanmama huyo.
“Kwa hiyo….” Madam S akataka kujua.
“Nitakutafuta jioni nikupe habari, naingia kazini kumsaka mshenzi yule,” akamjibu. Kamanda Amata mara baada ya kuachana na bosi wake akarudi ofisi ndogo na kuanza kupanga kipi cha kufanya. Nusu saa baadae Gina akaingia na kumkuta Amata akiwa anamsubiri. Alipomwona tu akasimama na kumshika mkono.
“Wapi sasa?” akauliza.
“Kazini, inabidi tumsake yule jamaa,”
“Sasa tunaanzia wapi?”
“Hata mi sijui,” Amata akajibu huku wakitoka na kuingia ndani ya gari tayari kwa safari.
* * *
Katika hoteli ya Al Huruba, Kariakoo, Martin Gupter alishituka usingizini, akatazama saa yake, tayari ilikuwa imetimu saa nne asubuhi, akainuka na kuwasha TV. Alichokutana nacho kilikuwa ni matangazo ya moja kwa moja kutoka Ikulu juu ya makaribisho ya ugeni huo mkubwa.
“Ameshafika!” akajisemea na kuingia maliwato, akajimwagia maji na kubaki Martin Guter halisi siyo wa kujibadili sura kama ilivyokuwa jana. Akachukua simu yake na kumpigia Amanda kutaka kujua yuko wapi. Mwanamke huyo akamwambia kuwa yupo mitaa ya katikati ya jiji akitalii na kusikiliza hili na lile kutoka kwa wananchi.
“Endelea kulala, nahitaji kukuona nina habari ya kushangaza kidogo,” akamwambia mgeni wake na kukata simu.

SHAMBA
“Nina habari ya kushangaza kidogo!” Chiba akarudia sentensi hiyo kwa sauti ya chini kisha akaendelea kucheza na kompyuta yake kwa hili na lile.
“Yes!” akashangailia na kuvuta kijitabu chake, akachukua kalamu na kuandika maneno mawili.
Kariakoo, Mtaa wa Sikukuu…
Kisha akaandika maneno hayo kwenye meseji na kuituma kwa Amata. Chiba alikuwa akifuatilia simu nyingi sana siku hiyo, ni hii iliyopigwa saa tano kasoro robo iliyomshtua kidogo kwa mambo mawili.
Kwa nini afiche habari hiyo? Ina maana ni siri, na simu hiyo yaani namba hiyo haijawahi kupigwa hapo kabla, haina historia kwenye mtandao ikiwa na maana ni namba mpya. Chiba akajishika nywele zake na kuzikuma nyuma mbele.
Hapa ni pazuri kuanzia! Akawaza.
Nahitaji kuwajua hawa, tema wameongea kiingereza tu, wazungu, ni akina nani? Akajiuliza. Chiba huwa hana mzaa akiamua kumfuatilia mtu kidijitali. Akainua simu yake na kupiga katika kampuni ya simu na baadae ikapokelewa na mtu aliyemtegemea.
“Asee! Kuna namba hii….” Akamtajia “…. Nataka kujua imesajiliwa lini na kwa jina gani” akauliza.
“Subiri kidogo niitazame!” akajibiwa, “usikate simu,” Chiba akaambiwa naye akatii kie alichoambiwa.
Hizi kazi hizi za kubahatisha hizi, majanga! Akajiwazia na wakati huo akasikia simu ikimwita… “Braza! Braza!”
“Sema!”
“Hiyo namba imesajiliwa siku nne zilizopita na mwanamama mwenye jina Elizabeth Mc Qued, katika ofisi yetu ya Mnazi Mmoja,” yule kijana akajibu, Chiba akaiandika pembeni na kumshukuru mtu huyo.
“Yes!” akajisemea. Huku akiinua simu na kumpigia Amata.
“Heee braza, wapi sasa?” akamuuliza.
“Nipo mitaa ya Msasani,”
“Kuna mzigo nahitaji uufatilie tujue ndani nje!” akamwambia.
“Sawa! Nasubiri….” Amata akajibu na kumpa ishara Gina kuegesha gari mahala pazuri. Kishs akachukua simu yake, haikupita hata sekunde kumi ujumbe ukaingia, akausoma kwa makini na kumpa simu Gina, naye akausoma pia.
“Kwa hiyo!”
“Twende Mnazi Mmoja sasa hivi,” Amata akamwambia Gina na ye’ akaingiza gari barabarani na kurudi mjini. Kutokana na foleni za barabarani hawakuweza kufika haraka, hivyo ilimpasa Gina kupita njia za vichochoroni na kufanikiwa kutumia kama saa moja na robo hivi kuwasili eneo husika.
Ndani ya ofisi hiyo kulikuwa na watu wengi sana, wao hawakujali, walichokifanya ni kuingia kwa meneja na kujieleza hasa ni nini wanachokifuata. Na baada ya kuonesha vitambulisho haikuwa tabu kupewa huduma. Yule meneja akaingia kwenye mtandao wao na kupekua hapa na pale na kuprinti fomu ambayo ina maelezo yote. Kamanda Amata akaitazama ile karatasi na maelezo yote kabisa, kisha akaitazama picha iliyokuwa katika karatasi hiyo.
“Elizabeth Mc Qued,” akatamka jina lake na kuitazama picha ya mwanamke huyo mwenye nywele ndefu zilizomwagika mabegani mwake. Macho yake yaliyoingia ndani kidogo yalimfanya aonekane kama mwanamke mwenye hasira. Akampa picha ile Gina kisha yeye akaagana na meneja huyo na kutoka nje tayari kwa safari. Wakiwa ndani ya gari, Amata akachukua ile karatasi na kuipiga picha kisha akamtumia Chiba.
“Ifanyie kazi!” akamwandikia kwenye meseji.
* * *
Chiba akiwa Shamba, akapokea taarifa ile kutoka kwa Amata na Gina, akaitazama kwa kina kisha akaingiza zile data katika kompyuta yake na kuiskani ile picha. Akajaribu kumtafuta mtu huyo kama anaweza kumpata kwenye mitandao ya kiusalama. Picha nyingi zikazunguka kwenye kompyuta ya Chiba kama dakika tano hivi na baadae ikasimama picha ya mwanamke anayefanana na yule kwa mambo mengi sana.
Angela Queen! Akasoma jina lililojitokeza kiooni, kisha akajaribu kuoanisha na picha ile aliyotumiwa na Amata. Jina la mwanamke huyo likawa linamjia kichwani mara kwa mara. Ijapokuwa mambo mengi hayakuonesha kushahabiana lakini Chiba alikuwa na shauku kubwa sana ya kumjua mwanamke huyo. Akainua simu yake na kumpa maelekezo ya wapi alipo mwanamke huyo.
Kutoka Mnazi mmoja Gina akawasha gari na kurudi mjini mpaka katikati ya Mtaa wa Azikiwe karibu na Mnara wa saa.
“Yupo hapo hapo, ningekuwa naweza kumwona ningewaambia, lakini hapa GPS yangu inanionesha kuwa anaelekea upande wa Posta Mpya,” Chiba akamwelekeza Amata na Gina. Amata akaangaza huku na huku asione mtu wa kumfananaisha, Gina naye vivyo hivyo.
“Hatumwoni!”
“Tazama vizuri!” Chiba akamwambia Amata, msako ukaendelea. Baada ya kuchunguza kwa makini, Amata akamshika Gina begani na kumpa ishara kuwa atazame upande wa jengo la posta. Mwanadada mmoja wa kizungu alikuwa akitembea harakaharaka, akiwapita watu huku akiwahi katika maegesho ya taksi pembezoni mwa benki ya CRDB. Macho ya Amata hayakubanduka kwa mwanamke huyo mwenye nywele ndefu, nyeupe.
“NI huyu kweli?” Gina akauliza.
“Ndo’ namwangalia” Amata akajibu huku akitoa simu yake.
“Unataka kufanya nini?” Gina akauliza huku akimtazama Amata nini anachotaka kufanya. Mara akamwona yule mzungu akiinua simu yake na kuiweka sikioni, mara akaitoa na kuirudisha katika mkoba wake.
“Ingia kwenye gari, uifuate ile taksi,” Amata akamwambia Gina. Wakaingia garini na kuondoka taratibu wakiifuata ile taksi. Baada ya kuzunguka picha askari wakachukua mtaa wa Makunganya, huko mbele wakapita mitaa kadhaa na kuivuka barabara ya Lumumba, wakachukua Mtaa wa Libya kuja upande wa Kariakoo. Wakati Gina akitaka kuvuka barabara ile tayari askari akasimamisha magari yanayotoka upande wa Mnazi Mmoja.
“Aaaaaaa shit!” Gina akapiga ukelele na kukanyaga breki kwa nguvu. Baada ya dakika kama tano hivi, yule askari akaruhusu magari ya upande wa Gina yapite. Kwa mwendo wa taratibu akaendesha katika Mtaa wa Libya na kuteremka kama anakuja Barabara ya Msimbazi, akakunja kushoto na kuangalia pembezoni kama ataliona lile gari, halipo. Baada ya kuufuata mtaa huo, mita kadhaa kabla ya Soko la Kariakoo akaliona limeegeshwa katika maegesho ya Hoteli ya Al Uruba.
“Egesha hapa!” Amata akamwambia huku tayari kafungua mlango wa gari. Wakatika Gina anaegesha yeye keshashuka, “nisubiri hapa!” akamwambia huku akikatisha barabara kuielekea hoteli hiyo. Tayari Kamanda Amata alikwishamuaona mwanamke yule kasimama kaunta hivyo hakutaka kupoteza nafasi hiyo. Akazikwea ngazi na alipofika mlangoni na yule mwanamke akawa anatoka akiwa na kijana mwingine wa Kizungu, wakapishana na Amata akafika kaunta na kusimama akitazamana na mhudumu wa kaunta hiyo.
“Nikuhudumie nini?” yule mhudumu akauliza.
Kamanda Amata hakujibu kwanza, akageuka nyuma kuwatazama watu wale, mara akasikia muungurumo wa gari na kuliona likipita kasi. Sekunde chache akamuona Gina naye katoka kasi kuwafuata, hakujali. Akageuka na kumtazama tena yule mhudumu, aliyekuwa akimalizia kufunga kitabu cha leja.
“Nahitaji kufika chumba namba 221,” akamwambia mwanadada huyo. Amata tayari alikwishapiga jicho na kuona chumba hicho kimepangwa na mwanamke, akajua kwa kuomba huko ni rahisi kupata ruhusa ya kuingia ndani yake. Lakini lengo lake hasa lilikuwa ni kufika chumba namba 119 ambacho ndicho alichofikia mzungu yule, na hili alilijua baada ya kuona funguo ya mwisho aliyoweka yule mwanadada kwenye shelfu yake. Amata akaruhusiwa, akazikwea ngazi mpaka ghorofa ya kwanza chumba namba kumi na tisa. Akasimama kwa muda na kuingia funguo yake isiyoshindwa kitu, akiwa tayari kavaa glovu mikononi, akauchezea ule ufunguo na mlango haukuleta kiburi. Amata akakaribishwa na chumba kipana chenye kitanda kimoja na kiti kimoja, begi kubwa lilikuwa ndani ya kabati ambalo mlango wake haukufungwa. Akaliendea na kutupa jicho ndani yake pasi na kugusa chochote. Macho yake tu yalitosha kukagua kila kionekanacho, hakukuwa na kibaya zaidi ya nguo tu. Zaidi ya hillo hakukuwa na kitu kingine katika chumba kile, Amata akageuka huku na huko, hakuona cha maana.
“Mh! Ni huyu au tumechanganya?” akajiuliza kwa sauti ndogo, kisha akausogelea mlango wa bafuni na kuusukuma taratibu, naaaam ni huku alipoikuta ile kanzu imefuliwa na kuanikwa.
“Yes! Nitakuwa mgeni wako usiku huu, humuhumu tutajua mbivu na mbichi!” akasema na kujitoa taratibu ndani ya chumba hicho, akatokomea nje.
* * *
Gina akajikuta anashindwa aende wapi, gari alilokuwa analifuatilia lilimpotea kwenye mataa ya makutano ya Barabara ya Bibi Titi, Ohio na Ally Hassan Mwinyi. Akatoa gari nje ya barabara na kuegesha kando ya jengo la Msalaba Mwekundu, akateremka na kuvuta hatua mpaka kwa askari wa usalama barabarani na kumuuliza kama ameliona gari hilo. Jibu alilolipata ni kuwa gari hilo limeelekea Mtaa wa Ohio. Akaingia tena garini na kuifuata barabar hiyo mpaka Mtaa wa Samora, hakuliona. Akachukua simu yake na kumpigia Amata.
“Vipi?”
“Wamenipotea!” Gina akajibu.
“Isiwe wamekugundua tu… maana kama ndivyo tutakuwa tumewagutusha…” Kamanda akamwambia Gina kwa simu hiyo.
“Hapana hawajanigundua,” akajibu.
“Ok usicheze mbali na mitaa hiyo, mgeni wetu wa jana ni yeye huyo, na lazima usiku huu tumfungie kazi,” Amata akamwambia Gina.
“Sawa Boss!” Gina akajibu na simu ile ikakatika.
* * *
Martin Gupter na Amanda Keller wakateremka na kuachana na taksi ile, wakavuka barabara na kupita kama mitaa mitatu hivi wakaingia kwenye Lexus Jeusi, humo wakamkuta Fredy akiwasubiri.
“Vipi? Kila kitu level?” Martin akauliza.
“Bila shaka, tutapata kila kinachoendelea katika mkutano huo, na hilo hapo mbele ndilo jingo letu la kulengea shabaha,” akamwambia Martin. Kijana huyo akalitazama kwa makini sana, “inabidi kujua njia za kuingilia bila kujulikana na mtu,” akasema.
“Usijali, nimepanda mpaka juu kabisa na picha nilizopiga ni hizi hapa!” akamwambia na kumpa simu yake kubwa atazame pande mbalimbali zinavyoonekana kutoka juu. Alipojiridhisha na picha hizo, akamrudishia Fredy simu yake.
“Nimeona!” akamwambia.
“Inachobidi kufanyika ni wewe kusubiri mpaka dakika ya tukio ikikaribia ndipo ujitokeze,” Amanda akaongeza kusema huku Fredy akiondosha lile gari mpaka barabara nyingine upande wa pili wa eneo la tukio. Akaegesha gari karibu na jengo lingine ambalo kwalo Fredy alijua kuwa halitakuwa na kash kash za ulinzi.
“Huku hawafiki, hivyo nitaweka gari hapa, mara tu baada ya tukio fika hapa haraka na ndipo tutakapoondokea, hakikisheni hamuachi alama yoyote nyuma kama tulivyofanya Angola na Ivory Coast.
“Nimekupata!” Martin akajibu na kujiegemeza kitini tena. Kwenye dashboard ya gari hilo saa ilisoma saa nane mchana.
“Sasa ni hivi, inabidi kuingia shimoni kwa sasa mpaka kesho saa nne asubuhi ndo awamu ya pili ya kazi yetu itafanyika. Baada ya mazungumzo hayo, Fredy akawasha gari na kuondoka.

VII
OFISI NDOGO
JIONI HIYO MADAM S alikutana na vijana wake ili kukusanya taarifa na tafutishi za siku nzima, kilichomfurahisha ni kwamba, vijana wake tayari walikuwa wamefanya kazi kubwa kuliko idara nyingine yoyote ya usalama katika ziara hii.
“Nawakubali!” akawaambia, “kwa hiyo huyu mnamhisi?” akaongeza swali.
“Kinachtufanya tumhisi ni kwa nini atumie jina la marehemu? Unajua wauaji wengi hupenda kutumia majina ya marehemu tena uhakikisha wamejua kila kitu kuhusu huyo mtu kisha utwaa jinale na kulifanyia kazi. Mpaka sasa huyu yupo kwenye tageti lakini kiuhalisia hatujui analengo gani la kufanya hivyo kwa sababu mpaka sasa hakitukia chochote…”
“Ndicho ninachodauti….” Madam S akaikata kauli ya Amata.
“Ila hatuwezi kumwacha!” Amata akasema.
“Siyo tu hatuwezi bali pia hatutakiwi kumwacha, ila naomba msimkamate kwa kuwa si kazi yenu, nataka mumfuatilie nyendo zake mjue hasa ni nini anafanya, ila msimwache kwa kuwa asije akaleta madhara….” Madam S akawaambia.
“Kesho ndiyo haswa siku ya kikao, sijui niwagawanye vipi, lakini naomba tu msiwe mbali na ukumbi wa mkutano kwani hatujui kipi ni kipi,” akaongeza kusema na kuwatzama viajana wake kwa zamu. Safari hii TSA haikuwa imekamilika kwani Scoba na Jasmini hawakuwepo kwatika timu kwa sababu za kikazi. Mara baada ya kikao hicho wakapeana mikakati ya nini cha kufanya usiku huo ikiwamo kumsaka yule anayejiita ‘Abdulah El Marik’.

USIKU WA SIKU HIYO
GINA aliegesha gari mtaa wa Pemba, nyuma tu ya hoteli ya Al – Uruba, “Here we are!” akamwambia Kamandal Amata aliyekuwa ameketi katika siti ya mbele.
“Yes! Kazi moja!” Amata akajibu huku akijiweka tayari, akapacjika bastola moja kiunoni huku akiweka silaha kadhaa sehemu tofauti za mwili wake. Shati lake jeusi na suruali ya rangi hiyo vilimkaa vyema kabisa, akachukua kofia aina ya ‘capello’ nyeupe akaiweka kichwani pake, tai ya rangi hiyohiyo nayo akaipachika shingoni.
“Nitakukuta haa baadae kidogo,” akamuaga Gina na kumpa busu zito la kinywani. Kisha akaondoka zake. Kwa hatua za harakaharaka akapita katikati ya maghorofa ya Wahindi na kujikuta kaibukia nyuma ya hoteli hiyo. Jukumu lililokuwa hapo ni kupanda kwa nje na kuibukia katika chumba hicho ambacho tayari alikuwa amekikariri jinsi kilivyokaa na upande kilichopo. Haikumuwia vigumu kwani alijua vyema jinsi ya kuifanya kazi hiyo. Akaikamata tai yake na kuvuta, akaitoa shingoni na kuitia mfukoni, akaivua kofia na kuigeuza ndani nje – nje ndani kisha akaivaa tena ikiwa ya rangi nyeusi. Kamanda Amata alitulia kimya kabisa kwenye kiambaza cha ukuta akisikiliza moyo na hisia zake kama kuna chochote ambacho kitamletea taabu muda huo, hakuna. Taratibu, akakamata ruva za kibaraza cha kwanza na kudanda kama nyani akihakikisha hafanyi kishindo cha aina yoyote ile kitakachosababisha watu kugutuka na kumharibia misheni yake. Dakika moja ilikuwa kubwa sana, tayari alikuwa amefika pale anapopahitaji, akatua kibarazani na kutulia akimya akiwa amepiga goti moja na sikio lake likisikiliza kwa makini kama ndani kuna mtu. Naam, sikio la Amata likafikiwa na sauti za watu wawili zikilalamika.
Muda muafaka! Akajisemea huku akiitoa bastola yake kiunoni na kuiweka tayari, akainuka taratibu na kusimama mkabala na mlango, mkono mwingine ukakamata funguo Malaya na kuitia tunduni polepole, akaizungusha kiasi kwamba hata watu walio ndani wasijue kama kuna kiumbe kinaingia ndani ya chumba hicho.
Kitendo cha mlango kufunguka ghafla ndicho kilichowafanya wawili wale wakatishe starehe yao na kukurpuka wakitaka kupiga kelele.
“Shhhhhhhh!!!!!!!!!” akawaaambi huku akiwa kawanyooshea bastola yake, “Mmepanga chumba hiki saa ngapi?” akawauliza.
“Sa- sa- a kumi jioni!” mwanaume akajibu huku akimeza mate.
“Shiit!” akang’aka na kuiweka bastola yake kiunoni, “samahani kuwavurugia starehe, kuna mtu niliyekuwa namtegemea kumkuta, sorry!” akawaomba msamaha na kutoka nje, akadanda kwenye ukuta wa kijibaraza na kuruka kwa ustadi mpaka chini, akatua bila kufanya ukulele, kisha akapenya kwenye njia zile zile na kulifikia gari. Akafungua mlango na kuingia ndani, akaketi huku akimtazama Gina.
“Go! Go! Go!!!!!!” akamwamuru na mwanamke huyo akaondoa gari kuufuata Mtaa wa Pemba mpaka Lumumba, akakunja kushoto na kurudi kama anakuja Umoja wa Vijana, kabla ya kufika makutano ya Barabara ya Lumumba na Morogoro akasimama na kutazama nyuma na kisha pande nyingine, usalama upo.
“Vipi?” akamuuliza Amata.
“Hayupo…”
“Hayupo?” akauliza kwa shauku ya kutaka kujua.
“Si ungemsubiri arudi….” Gina akasisitiza.
“Amehama chumba na si ajabu hata hoteli yenyewe,” Amata akajibu kwa kirefu.
“Oh come on!!!” Gina akahuzunika, “katuzidi akili, alijua kama tutamfuata au kahisi tu?” akauliza.
“Kujua kama tutamfuata labda kama ulimwambia wewe, lakini hivi hivi sijui kama anaweza kujua…” Amata akajibu na kutumbukiza utani humo humo. Gina akaamua kuliingiza gari barabarani na kuondoka zake. Muda huo Kamanda Amata akachukua simu ya upepo na kumpigia Chiba kumtaka afuatilie namba ile iko wapi kwa muda huo. Jibu alilopewa na Chiba lilimkatisha tamaa kabisa baada ya kuambiwa kuwa namba ile haisomi tangu saa saba mchana.
Saa saba mchana! Amata akawaza. Akili yake ikazunguka huku na huko lakini hakupata jibu la kuiridhisha roho yake. Akainua simu yake nyingine akapiga namba fulani na kuiweka sikioni.
“Yes, mtu wetu kapotea kwenye sight tangu saa saba!” akamwambia Madam S.
“Ok cha muhimu ni kuimarisha ulinzi wa nje, na tuombe kukuche salama, kama ana nia mbaya na kikao hiki basi na’ hakika tutamtia mkononi,” akamjibu na kukata simu.
Amata akaiweka simu ile mahala pake na kutulia kitini, akamtaka Gina kuendelea na safari mpaka nyumbani kwa Chiba, Msasani kwa Nyerere, wakaiacha Barabara ya Old Bagamoyo na kuingia kulia upande wa baharini mpaka kwenye jumba hilo.
“Karibuni wapendanao,” Chiba akawakaribisha Amata na Gina. Badala ya kujibu Gina akatabasamu na kumtazama Amata.
“Umesikia Amata….”
“Umeanza!” Amata akamjibu kisha wote wakaingia ndani.
Ndani ya sebule pana, Amata, Gina na Chiba waliketi kwa mazungumzo mafupi.
“Kwa nini atoroke?” Amata akauliza.
“Ndiyo hapo ninapokuwa na shaka na watu hawa, sasa tunao wawili, yule mwanamke na yule kijana aliyemchukua pale Al Uruba,” Amata akasema.
“Ndiyo, tunaunganisha mambo tu na moja na moja itakuwa mbili tu… uwanja wandege tulimshuku huyu kijana, nje ya uwanja wa ndege alilakiwa na huyu mwanamke, na sasa tumeona mchana huu akimchukua pale Al Uruba na kumpeleka sijui wapi… nafikiri sasa tuangalie ni wapi mwanamke huyu anaishi…” Amata akasema.
“Hilo ndo la mzingi kwa sasa,” Gina akaongezea.
“Anhaaaaa mawazo yamegongana, huyu mwanamke simu yake imewahi kuongea mara kadhaa Golden Tulip, nikiwa Shamba nimejaribu kufuatilia mazungumzo yale, nimegundua kuwa watu hawa hawaongei mambo yao kwa uwazi simuni bali hupanga kukutana ndipo huzunguza mipango yao… kwa nini wafiche? Hilo la pili, lakini lingine ni kuwa hawako wawili, hawa jamaa wapo watatu na ninahisi kuwa kwa sasa wapo pamoja ndiyo maana wameweza kuzima simu,” Chiba akaeleza.
“Watatu!” Gina akashangaa.
“Ndiyo, wapo watatu…”
“Haijalishi, twende Golden Tulip sasa,” Amata akawaambia wenzake huku akiitazama saa yake, saa saba usiku. Gina na Amata wakaingia garini na kuanza safari wakimuCha Chiba nyumbani kwake akiwa anawafuatilia kwa vifaa vyake vinavyoongozwa kwa satellite.
 
MAGNUM22

Sehemu 8

GOLDEN TULIP
SAA NANE USIKU, hoteli ya Kimataifa iliyojengwa kando kando ya Barabara ya Toure ilikuwa kwenye hali ya utulivu. Magari mengi yalikuwa maegeshoni na ni walinzi tu walikuwa wakipita huku na huko kuhakikisha usalama wa vyombo hivyo. Gina akaongoza gari mpaka katika maegesho ya hoteli hiyo.
“Tunawapataje?” Gina akamuuliza Amata huku akizima injini ya gari hilo.
“Tutatumia Soviet Method, kwani picha ya yule mwanamke huna?” Amata akamtupia swali Gina.
“Ipo!” Gina akajibu.
“Sawa, ichukue twende nayo,” Amata akamwambia Gina huku tayari keshafungua mlango na kuteremka nje. Gina naye akateremka na kumfuata, hatua zao zikawafikisha katika meza ya mapokezi ya hoteli hiyo. Katika ofisi hiyo kulikuwa na wanadada wawili waliovalia nadhifu na kupendeza kwelikweli.
“Karibu sana Golden Tulip, nikusaidie nini?” mmoja wa wale wadada ambaye beji juu ya kifua chake ilimtambulisha kama Esther Kwimba akawakaribisha.
“Asante sana, sisi ni maafisa uhamiaji tumekuja hapa tunamtafuta mtu huyu… je mmewahi kumuona? Akamwambia mrembo yule huku akimwonesha kitambulisho cha kazi hiyo. Mwanadada yule akachukua kitabu cha leja na kukiweka tena mezani.
“Alikuwapo hapa, lakini amecheck out, likizo yake imekwisha!” akajibu. Amata akamkazia jicho kana kwamba bado hajarizika na jibu hilo, “huamini au?” akaongeza swali.
“Si kwamba siamini, ila nataka unambie ni saa ngapi ametoka na nani?” Amata akampiga swali mwanadada yule. Akafunua kitabu cha wageni na kutazama mpaka kwenye jina lile, Angela Queen.
“Angela Queen, amecheck out saa 11 jioni ya leo,” akajibu mwanadada yule.
Kamanda Amata akamtazama Gina, “tumemkosa?” mwanamke huyo akauliza huku akiweka mkono wake shavuni kwa masikitiko.
“No!” Amata akajibu, kisha akaaga na kutoka na Gina mpaka kwenye gari.
“Hatuwezi kumkosa, kama ametoka saa kumi na moja ina maana kwamba ndege yake ni saa moja usiku au saa kumi na mbili jioni ….”
“Ikizidi sana saa mbili usiku,”
“Yes! Kwa maana hiyo hatuna budi kutazama kama kuna ndege ya kutoka nje ya Tanzania mida hiyo,” Amata akamwambia Gina. Gina hakutaka kuchelewa akainua simu na kupiga kwa Lulu kutaka kujua kama kuna ndege yoyote ya kutoka nje ya Tanzania, jibu ambalo alilipata ni kuwa ‘hakuna’. Akamtazama Amata kwa nukta kadhaa kisha akamwambia, “Atakuwa humuhumu nchini”.
“Usiseme nchini, kwa kusema hivyo ndiyo unazidi kumpoteza, sema humuhumu jijini…”Amata akaongezea.
“Wapi sasa?”
“Sijui!” akamjibu huku akijiegemeza kitini na mkono wake ukishikwa kichwa, ukimya ukatawala kwa nukta kadhaa kati ya wawili hawa.
“Gina!”akaita, “sasa naweka nguvu zangu kwa asilimia tisini kwa mwanamke huyu na hao wenzake, mchezo wanaufanya unanitia mashaka, naihisi hatari mbaya sana siku ya kesho,” akamwambia.
“Yaani…. Kama sijakuelewa flani hivi,” Gina akaonesha mashaka katika hilo.
“Nasema, hawa jamaa sasa inabidi tuwafungie kazi, naanza kuhisi hatari siku ya kesho,” akarudia kusema.
“Kwa hiyo!”
“Yaani hapa tulipofikia yatupasa kutoa taarifa panapohusika ili kuanzia asubuhi ulinzi uwe mkali kila kona. Akamwambia Gina huku akifunga mkanda wa gari lake. Tayari jogoo wa kwanza alikwishawika, huyu kwenye mila zetu tungemchinja kwa sababu kafanya hivyo kabla ya wakati.
“Kumekucha, twende tukalale,”
“Unataka cha asubuhi?” Amata akamtania.
“Toka hapa!!!!” akamwambia huku akiwasha gari na kuyaacha maegesho hayo taratibu.
* * *
SIKU ILIYOFUATA
PAMABAZUKO LA SIKU HII lilimkuta Kamanda Amata na Gina kitandani, ni sauti ya kengele ya mlango ndiyo iliyowakurupusha katika usingizi wao.
“Aaaaaaaahhhhhhhh!” Gina akainuka na kutwaa koti lake lililoshonwa kwa kitambaa kizito cha taulo. Akavuta droo na kuchukua bastola yake ndogo akaifutika katika mfuko wa ndani huku mkono wake ukiwa huko, akatoka chumbani na kuelekea sebuleni. Akafika na kuufungua mlango macho yakagongana na kijana muuza maziwa ambaye anamfahamu, daima huja kumletea bidhaa hiyo.
“Leo mbona umewahi sana?” akamwuliza.
“Nina safari saa tatu asubuhi ndo maana nimekuetea mapema, hata hivyo nilijua kuwa umetoka maana niliona gari inageuza hapa getini,” yule kijana akamwambia.
“Gari?”
“Eee gari moja ya bei mbaya sana, nyeusi hivi… lakini ilivyonipita kwa mbele nikaona kuna wazungu watatu…”
Gina akatahayari kwa maneno hayo, akajiuliza juu ya gari hilo, hakulijua.
“Ok! Labda walipotea njia!” akamwambia na kumshukuru, kisha akamwambia asubiri kidogo, akaingia ndani na kumletea shilingi elfu ishirini kama nauli kwa safari kwa kuwa kijana huyu huwa anamsaidia mara nyingi hata kazi za hapo nyumbani. Mara baada ya kurudi ndani akamkuta Kamanda Amata akiwa tayari ndani ya suti safi.
“Vipi baba?” akamuuliza.
“Vipi?! Kazi mama, unajua leo ni siku ngumu sana, by the way kijana anasema ni gari gani lilikuja?
“Ee mwanaume hupitwi, wivu tu, yaani ushakuja kusikiliza…”
“Ndiyo, lazima nijue nini kinazungumzwa,” Amata akajibu huku akifunga vifungo vya mikono ya shati lake.
“Ninapata wasiwasi, anasema kuna gari jeusi lilikuwa na Wazungu watatu ndani yake, nina wasiwasi kwa sababu huyu tunayemsaka hata pale uwanja wa ndege alitumia gari jeusi…”
“Hata Chiba alituambia kuwa anahisi wapo watatu,” Amata akamwambia, “kwa hiyo wamekuja mpaka nyumbani, wamepajuaje? Walikuwa wanatufuatilia?” akaongeza maswali yaliokosa majibu.
“Vaa tuondoke! Haraka!” Kamanda akamwambia Gina na ni nukta hiyo hiyo simu yake ikaita kwa fujo, akaichuku na kuitazama, Chiba.
“Ndiyo kaka!” akaitikia.
“Jiangalieni nahisi mpo hatarini, kwa usalama tokeeni mlango wa nyuma,” akamwambia kupiti asimu hiyo. Dakika ishirini baadae, Gina naye akawa tayari, safari ikaiva.
“Tutokee mlango wa nyuma!” Amata akamwambia Gina, naye hakubisha, wakatumia njia hiyo kutoka nje, wakakodi taksi na haraka wakaingia katikati ya jiji. Breki ya kwanza ilikuwa ofisi ndogo. Madam S alikuwa tayari ndani ya ofisi hiyo, zaidi ya yeye safari hii kulikuwa na mgeni mwingine zaidi, Inspekta Simbeye.
“Nilijua tu kuwa muda huu mtaingia, haya hatuna muda wa kupteza…” akawaambia huku akiwataka kuketi.
“Kumekucha na siku yetu ni hii, kwa ushirikiano wetu tutaweza kuzuia jaribio la mauaji ambalo lina tetesi ya kutokea,” Madam S akasema.
“Mauaji?” Amata akauliza.
“Ndiyo, Simbeye alikuwa hapa,”
Inspekta Simbeye, akiwa ndani ya nguo za kiraia, lakini mkononi mwake kukiwa na simu ya upepo, alikuwa ofisini hapo dakika chache tu zilizopita. Ni mara chache sana ya Inspekta huyu wa kudumu kuja katika ofisi hii, kazi zao daima hufanyika mahala popote wanapochagua.
“Amepata hii meseji…” akampa simu Amata.

“Tunajua, mnatufuatilia,
lakini mjue kuwa tumejipanga na
tutatekeleza azma yetu,
lazima Somali Land iwe huru.
Tunahitaji Ardhi ya mama zetu,”
Ni sisi Freedomfighter!”

Kamanda Amata, akairudisha simu ile kwa Madam S, “ndiyo tunawafuatilia, na leo hii tutawatia mkononi,” akamalizia kusema.
“Mh! Wajitangaza sasa,” Gina akasema.
“Wameona tayari mmegundua nyayo zao,” akajibu, “sasa nataka niwape mpango kazi wa kufanya,” akaongeza.
Madam S akajikohoza kusafisha koo, “tatizo hatujui ni wakati na saa ngapi na ni njia gani watu hao watatekeleza mpango wao,” akawaambia.
“Yes!!” wakajibu kwa pamoja.
“Good sasa mpango wa kwanza ni kuzuia mkutano kuanza saa tatu, tukague ukumbi mzima kama kuna mlipuko au kitu chochote ambacho kitahatarisha uhai wa mtu. Pili tukiruhusu mkutano ufanyike tuhakikishe tumekagua gari zote za viongozi hao kabla hawajapanda kuja ukumbini, na ukaguzi wa kila mtu anayeingia ukumbini, asiruhusiwe mtu kuingia na simu, saa, wala chochote kile cha mawasiliano au chuma. Naongeza kuwa viongozi wote wasile chakula wala kunywa maji kutoka katika hoteli hiyo…” Madam S akatoa muongozo wa kwanza, akamgeukia Simbeye.
“Inspekta nimemwambia kuwa ninathitaji vijana wake wa kikosi maalumu kuanza kuweka ulinzi kwenye ukumbi huo sasa, ili kuzuia mtu yeyote kuingia ndani ya eneo la ukumbi huo,” akawaambia. Baada ya hapo akachukua simu maalumu ya ofisi na kupiga mahala fulani pa siri, akatoa angalisho la kuzuia mkutano huo kwa muda. Hakutaja muda gani ila alieleza hilo na kutaka kuonana na Mkuu wa Itifaki ya mkutano huo haraka iwekanzvyo.
“Kamanda Amata, hakikisha unategua kitendawili hikl ndani ya dakika chache zijazo kwa kombat ya aina yoyote, Chiba utakuwa na Amata, lakini wewe unajua ni nini cha kufanya, fuatilia hii meseji ujue imetoka wapi nahitaji ndani ya dakika chache tu uwe umenipa jibu. Gina nataka ufanye kazi ndani ya ukumbi wa mkutano kwa siri, hakikisha hutambuliki kwa yeyote, najua unajua nini cha kufanya.
* * *
Madam S alikutana na Mkuu wa Itifaki katika ofisi yake ndani ya jengo la Wizara ya Mambo ya Ndani. Hakikuwa kikao bali ni kupeana maagizo juu ya nini cha kufanya katikma mkutano huo.
“Unajua kuzuia mkutano kwa muda usiojulikana tunajenga picha mbaya sana katika uso wa kimataifa, kuna wajumbe wa Commoniwealth na UN na jumuia nyingine kubwa ambazo kwazo sisi hutegemea mengi. Sasa wanajua saa mbili tunatakiwa ukumbini then mnachelewesha mambo, Wazungu hawa watatasusa mkutano…” akazungumza bwana yule aliyetuna kitini kama chatu aliyemeza mbwa.
“Achana na Wazungu, mambo ya Afrika lazima yaamuliwe na yafanywe kiafrika, mkutano umeahirishwa kwa sababu za kiusalama, kuna tetesi za umwagikaji wa damu katika mkutano huu, inaonekana wewe wapenda litokee siyo?” madam S akamwambia huku akiwa tayari kainuka kitini.
“Si napenda litokee, bali mambo ya kiitifaki hayaendi hivyo mama,” akamwambia.
“Sasa ni hivi, kikao kitaanza itakapotangazwa, na ikiwezekana, hakitakuwepo kwa kabisa au tutabadilisha ukumbi,” Madam S akamwambia.
“Kubadilisha ukumbi?” akauliza huku naye akijitahidi kusimama kuonesha msisitizo lakini tumbo lake likamzuia kufanya hivyo. Wakati huo Madam S tayari alikuwa keshafungua mlango anaondoka.
Katika mahoteli yote ambayo wageni wale walifikia kulikuwa na ulinzi mkali sana, askari wenye sare na wasio na nazo walikuwepo, kila mmoja akiwa ametingwa na kile anachotakiwa kufanya. Hali ilikuwa tete, vijana wa Usalama wa Taifa walikuwa hai hai kujaribu kugundua mpango huo kila eneo muhimu ambalo walilihisi, lakini kazi ilikuwa ngumu.
Asubuhi hiyo hiyo, Gina alitinga katika ukumbi wa mkutano kama alivyotakiwa kufika, katika lango kuu la kuingia katika eneo la ukumbi huo, aishuhudia askari wa FFU na baadhi wa JW wakiwa wameweka ulinzi mkali, waandishi wa habari na watu wengine ambao tayari walikuwa wamewasili, wakatakiwa kukaa mbali kidogo na eneo kwa kuwa kuna kazi iliyokuwa ikifanyika.
“Akuna cha bomu wala nini,” akasikika mtu mmoja akisema.
“Basi tu, tunataka kuonekana tuko makini na usalama hamna chochote, walishindwa Angola na Ivori Coast kuzuia mauaji ya viongozi itakuwa sisi….” Mwingine aisikika, huyu ni kati ya wale Watanzania wanajidharau na kutokujiamini. Barabara kadhaa zilifungwa tayari kuruhusu wageni wa mkutano huo kuwasili muda wowote.
Kati ya watu waliokuwa katika kundi la waandishi wa habari, alikuwapo Amanda Keller akifuatilia kila kitu kwa ukaribu kabisa. Na taarifa zote ambazo zilipatikana hapo, zilifika kwa Martin na Fredy moja kwa moja. Hakuna mtu ambaye alimjua mwanamke huyo kuwa ni ‘kidudu mtu’ kati ya watu hao, na kutokana na mchanganyiko wa waandishi Wazungu kwa Waafrika haikuwa rahisi kumjua.
* * *
Ndani ya hoteli ndogo ya Kunduchi Beach huko Kunduchi, Martin na Fredy walikuwa wakipata kifungua kinywa huku wakisika mengi kutoka kwa Amanda.
“Wanafikiri sisi ni wajinga kufanya kazi yetu kwa wazi hivyo?” Fredy akamuuliza Martin.
“Sisi ni profesheno, yani nitamtungua huyo jamaa mpaka wenyewe watashangaa, salama yao ni kuachia ambacho tajiri wetu anataka,” Martin akamjibu Fredy huku akiweka kikombe cha kahawa kinywani na kupiga funda moja kwa mruzi.
“Wanafanya ukaguzi kama kuna mlipuko wowote….”
“Hah! Hah! Hah! Hah! Waache wafanye mazoezi maana hakuna watakachopata…” Martin akazungumza, “ni risasi moja tu basi ambayo wanatakiwa kuitafuta na si bomu au kemikali au sumu ya kwenye chakula, na risasi hii ninayo mimi peke yangu tu, na ndiye ninayejua ni wakati gani wa kuiruhusu ifanye kazi yake, na wasipoangalia watakufa wao, tena kifo kibaya,” akamwambia Fredi huku mkononi akiirusharusha risasi moja kubwa.
Upande wa pili, Chiba alikuwa ndani ya gari lake akiendesha taratibu huku akijaribu kufuata mawasiliano fulani ambayo aiyahisi si ya usalama sana. Kutoka ndani ya gari hilo aliweza kusikia sauti ya Amanda ikipeleka taarifa mahali fulani. Alichokuwa anafanya yeye ni kufuata wapi mawimbi hayo yanaelekea kwa kuangalia nguvu yake kawenye chombo hicho. Sasa alikuwa tayari maeneo ya Tangi Bovu na signal ilimwonesha kuwa upande huo wa Bagamoyo ndiko mawimbi hayo yanakwenda.
“Nina uhakika wa kuwatia mkononi muda si mrefu, huyu mwanamke yupo huko mjini ila sijajua ni eneo gani, na inaonekana anajua information zote,” Chiba akamwambia Amata kwa kifaa chake maalumu ambacho hakiingiliani na mawasiliano yoyote ya huko duniani.
“Ngoja nijaribu kumgundua kama nitafanikiwa maana inaonekana anajua sana kujibadili,” Amata akamjibu Chiba, “na ukigundua ni wapi walipo, naomba unijulishe usifanye kitu, ili tuje tuwatie displin na wajue kuwa sisi si watu wa mchezo mchezo,” akaongeza kusema huku akiwa mita chache kutoka Hoteli ya Kepinski Kilimanjaro ambapo Mwenyekiti wa Umoja wa Afrika ambaye ni Rais wa Ganbia pamoja na marais wengine walifikia mahala hapo. Ulinzi wa hapo haukuwa wa kawaida, kila aliyeingia alikaguliwa mpaka maeneo nyeti kabisa ya mwili wake.
* * *
Mkurugenzi wa Idara ya Usalama wa Taifa akakutana kwa siri na Mkuu wa Itifaki, mara hii ndani ya Ikulu, yaani makao makuu ya Rais wa nchi.
“Mheshimiwa, sasa tunaweza kuruhusu shughuli ziendelee, vijana wanasema usalama upo mwingi tu, hakuna walichokigundua kibaya,” yule Mkurugenzi akamwambia Mkuu wan chi huku mwanaitifaki yule akitikisa kichwa kuafikia hayo.
Baada ya kutafakari kwa sekunde kadhaa, akawataka kusubiri, akawaacha sebuleni na kuingia ndani katika chumba chake cha siri, akainua simu yake na kupiga namba fulani, akampata Madam S ambaye yeye ndiye aliyekuwa na usemi wa mwisho wa Rais huyo.
“Hali ikoje huko?” akamuuiza.
“Vijana hawajagundua chochote kibaya, nimewapa taarifa watu wa usalama na itifaki kuwa sasa shughuli inaweza kuendelea lakini ulinzi ndiyo kitu cha muhimu sana,” akamjibu.
“Sawa! Asante, nategemea hautakuwa mbali na eneo,” akamwambia.
“Bila shaka, na nitaongeza minzi wa siri kwa mgeni wetu kwa kuwa siamini mtu zaidi ya viajan wangu tu,” Madam S akamwambia.
“Fanya hivyo,” Rais akamwambia na kukata simu.
Saa nne kamili, waandishi wakaruhusiwa kuingia ukumbini na wageni wengine, wakapangwa mahala pao tayari kwa mkutano huo. Dakika kama ishirini baadae, ving’ora vikasikika na gari za bei mbaya sana zikaingia mfululizo katika eneo la ukumbi huo na kuegeshwa mahala salama kabla vingozi kuruhusiwa kushuka. Walinzi maalumu kutoka nchi ambazo marais wao walikuwapo waizingira magari hayo pande zote, huku masikioni mwao wakiwa na vifaa maalumu vya mawasiliano. Hakuna aliyejua ni nani wanayewasiliana naye, ilikuwa siri yao. Saa nne na nusu wote kwa pamoja wakafungua milango na kuwateremsha viongozi hao kisha kuwaingiza ukumbini humo, lakini kati ya wote hao, rais wa Gambia ambaye ndiye haswa mwendesha mkutano hakuwapo. Yote haya Amanda alikuwa akiyaona yote na kuwapa taarifa watu wake.
Kule Kunduchi, tayari vijana wale walikuwa wakijiandaa kuondoka kuelekea mjini tayari kwa kazi waliyotumwa. Martin akiwa chumbani kwake, akafunga kila kilicho chake tayari kwa safari na Fredy vivyo hivyo. Baada ya kila kitu kukamilisha wakaweka kila kitu ndani ya gari na wao kujipakia tayari kwa safari.
Chiba alifika katika hoteli hiyo na kupishana na gari lile getini pasi na kulichunguza sana, akaingia na kuegesha la kwake ndani kisha akateremka mpaka mapokezi. Alikuwa na uhakika kabisa kwamba mawasiliano hayo yametoka hapo.
“Karibu Kunduchi Beach Resort!” akakaribishwa na kijana mmoja mrefu mwenye asili kama ya Kisomai hivi.
“Asante sana, ninauliza mwenyeji wangu kama nimemkuta,” Chiba akamwambia huku akitoa picha na kumwonesha. Yule kijana akaichukua na kuingalia mara moja tu, akamrudishia kisha akatikisa kichwa kushoto kulia.
“Vipi?” Chiba akauliza.
“Dah! Kaka umejipatia dodo nini…. Maana wanawake hawa Wakizungu ni wagonjwa sana wa mapenzi ya kiafrika….” akasema.
“Kajilengesha mwenyewe mi nifanye nini, kuna mwanaume anayekataa mwanamke wa Kizungu, kwa mfano wewe angeamua kukupa, ungekataa?”
“Aaaaa brazaaa si unajua tena, bahati za wachache hizo, nikiipata siiachi,”
“Sasa je! Chumba chake kiko wapi?”
“Namba 50, Impala!” akamjibu. Chiba akavuta hatua mpaka upande wa vyumba na kukagua mpaka akakipata hicho akitakacho. Akapiga jicho katika tundu la ufunguo, hakuna ufunguo, akili ya kwanza ikamwambia kuwa ndani humo hakuna mtu. Akatazama huku na kule yuko peke yake eneo hilo, akachukua funguo yake na kuipachika, akanyonga mara mbili kitasa kikakubali tekenyo hilo, ukafunguka. Chiba akakaribishwa katika chumba kipana cha mviringo kilichobeba samani za thamani.
Bila shaka hii ni suit! Akawaza na kuingia ndani taratibu kisha akaufunga mlango nyuma yake. Akaitazama saa yake na kuizungusha kwenye pete ya juu, akasubiri kama sekunde kumi hivi hakuna chochote. Akachukua kifaa chake cha mawasiliano na kuwasiliana na Amata, akampa taarifa kuwa yupo chumbani kwa mwanmke huyo. Kamanda Amata akampa ‘go ahead’. Chiba akapekua hapa na pale, akainua hiki na kile, katika meza moja akakutana na kadi sakima ndogo kabisa ‘micro chip’ akaitazama kwa mahaba na kuichukua kwa uangalifu mkubwa, akaipachka katika simu yake na kuhamisha mafaili yote katika simu hiyo, kisha akaichomoa na kuirudisha mahala palepale. Akafungua moja baada ya jingine kusoma japo vichwa vya mafaili hayo. Lakini wingi wake haikuwa rahisi kumaliza yote hayo. Akaendelea kupekua hapa na pale na ndipo akakutana na begi moja dogo, alipolifungua, akakutana na nwele bandia kama sita hivi za aina tofauti na midomo bandia, nyusi, kope mpaka mboni za macho.
Mshenzi huyu, ndo maana anatusumbua si ajabu hata wanaume wake nao hujibadili! Akawaza na kuviacha kama alivyovikuta. Katika kuendelea kupekua pekua hakukuta kitu zaidi, akaamua kutoka ndani ya chumba kile akakifunga na kurudi kaunta.
“Ah mara hii?” yule kijana akauliza.
“Hapana, nitarudi muda si mrefu kuna vitu nachukua nje hapo,” Chiba akajibu huku akielekea garini, akawasha na kuondoka. Akiwa njiani akaegesha mahala na kuchukua simu yake.
Inawezekana kuna faili za kushughulikia haraka kabla sijafika mjini! Akawaza, kisha akafungua ile simu na kupekua mafaili mengi mengi, lakini haya hakuwa na mvuto nayo ijapokuwa yalikuwa ni ya mipango mingi mingi tu. Katika karibu na kukata tama akakutana na faili moja lililoandikwa Magnum 22, kwanza akalipuuza, lakini baadae, akaamua kutazama nini kilichopo ndani yake. Hakuamini macho yake, taarifa za mipango yote ya mauaji zilikuwa humo, ijapokuwa hazikueleza mengi yaliyopita, ila zilieleza mpango mkakati wa mauaji ya Dar es salaam, na wakati gani wa kufanya mauaji hayo. Chiba alihisi jasho likimtiririka kwapani, lakini kilichompa faraja ni kuwa wauaji wanasubiri hatima ya mktano huo ndipo wauae endapo ombi lao litakuwa limekataliwa. Akaitupa simu yake kitini na murudisha gari barabarani kisha akaondoka kwa kasi sana kuelekea mjini. Akatazama saa yake, tayari ilitimu saa sita kasoro robo, akainua simu yake na kumpigia Amata.
“Nakupata Chiba!” Amata akaipokea.
“Mkutano umefikia ratiba gani sasa?” akamuuliza.
“Wapo kwenye speech ya mwisho, Mkuu wa Nchi anashukuru ugeni huo…” Amata akajibu kwa kuwa hata yeye alikuwa akisikiliza kupiti chombo maalumu, na hakuwa mbali na eneo hilo.
“Agenda ya Somali Land, imetengwa au la?”
“Chiba mbona unaniuliza maswali ambayo yananitatanisha?” Amata akaongea kwa ukali.
“Just nijibu…”
“Imekataliwa, na wamesema haiwezekani kuwa hivyo!” Amata akajibu.
“Sasa….”
“Chiba kikao kimeisha, ngoja nicheki nini kinaendelea…”
“TSA 1 muuaji atatumia Magnum 22 mpango wao ni kumdungua Rais wa Gambia kutokea juu ya ghorofa la TPSA, wakati wa kupiga picha ya pamoja,”
“What? Chiba!” Amata akaita huku akifungua mlango wa gari na kuubamiza, akainua macho kutazama ghorofa lile, hapo ndipo akagundua kuwa ni kweli kutoka juu ya jingo hilo unaweza kumpata kirahisi mtu akiwa katika mlango mkuu wa ukumbi ule.
* * *
Kwenye gari ambalo ndani yake kulikuwa na Fredy na Martin, walikuwa wakipata kila kitu kutoka katika mkutano huo. Amanda kutoka ndani ya ukumbi wa mkutano alikuwa akiwapeperushia mawasiliano yote, kila kilichokuwa kikizungumzwa na kuamuliwa. Mara baada ya agenda za mkutano kwisha, ikafuata hotuba fupi ya shukrani kutoka kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kama mwenyeji kuwashukuru wageni hao. Ni wakati huo Gina alipokuwa tayari kamhisi mwanamke yule aliyejipachika katikati ya wanahabari wa kimataifa, aliporudisha macho tena, hakumwona. Gina akahisi kupata ganzi na tayari viongozi walikwishamaliza mkutano, sasa walikuwa wakipeana mikono tayari kwenda nje kwa ajili ya picha ya pamoja.
“Wamekataa, hatuna budi kutekeleza tunalopaswa,” Fredy akamwambia Martin.
“Umeona mwenyewe jinsi jamaa wanavyotuandama, wamegundua nyayo zetu, tunapotoa mguu nao wanakanyaga…”
“Sekunde tano mbele yao tupo salama, na hakika hizo tano tutakamilisha kila kitu…”
“Amanda!”
“Nimeshamwambia jinsi ya kutoroka…” Fredy bakajibu.
Martin akateremka garini na mkoba wake, akavuka barabara na kulipita jingo la kwanza kisha akaingia lile la pili la TPSA, akaingia kwenye lifti na kwenda juu kabisa, huko akakiendea kibanda kidogo ambacho kilikuwa na mitambo yote ya kuongozea lifti hiyo, akaiharibu na kuzima umeme ndani ya jingo hilo. Harakaharaka akafungua mkoba wake na kuchomoa vipande vitatu vya bunduki, akaviunganisha kwa haraka na kuiweka tayari, risasi moja akipachika ndani ya bunduki hiyo, Magnum 22 riffle, akafyatua miguu yake na kulala chini kimya huku akijifunika tambara ambalo lilifanana rangi na sakafu ya eneo hilo na kuruhusu mdomo tu wa buduki kutokeza nje. Jicho lake likiwa tayari kwenye lensi yenye nguvu kabisa alikuwa akiwaona viongozi wale wakitoka nje huku ulinzi maduhubuti ukiwa umewazunguka. Kila alipojaribu kumuweka kwenye shabaha yule anayemtaka watu walikuwa wakipita hapa na pale na kumpoteza shabaha.
“Shabaha ngumu Fredy!” Martin akamwambia Fredy kwa chombo chao cha mawasiliano.
“Five seconds Martin,” Fredy akamjibu.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom