Riwaya magnum22

MAGNUM22 22

Sehemu 11

akainuka na kuuendea mlango mmoja wapo huku nyuma akifuatwa na Amata, wakaingia mahali pengine tofauti na ile ofisi ya kwanza. Huku kulikuwa na watu wachache wake kwa waume waliokuwa kwenye mazungumzo, tunaweza ita ya falagha kwa maana usingeweza kusikia wanachoongea ila ungewaona wanaongea. Mlango mwingine ukawafikisha nje kabisa kwenye bustani nzuri na ya kupendeza, yenye maua aina aina na vitu vizuri vya kuvutia.

“Sikiliza,” Perreira akamwambia Amata na nukta hiyo hiyo mwanadada mmoja aliyevalia bikini akafika mahala pale akiwa na kitunga mkononi mwake, hakuwa Mhindi wala Mwarabu ila alikuwa na nywele ndefu mpaka makalioni, akafungua kile kitunga na Perreira akachukua sigara moja kubwa na kuiwasha kisha akaipachika kinywani na kuibana kwa midomo yake miwili. Baada ya kupiga pafu tatu kubwa na kuutoa moshi hewani akamtazama Amata kwa mara nyingine.

“Mimi ni mtu mwema sana, huwa nasaidia serikali nyingi kwa mambo mengi, nasaidia makundi mengi ya huduma za kibinadamu kwa mambo mengi, ila kwa hilo ulilotumwa, Mr. Spark nina wasiwasi sana… Mimi sina mpango wa mauaji, ila nina taarifa ya mauaji, lakini sikai nayo hapa taarifa nyeti kama hiyo. Tazama kuleeeeee, unaona kile kisiwa?” akamwambia. Amata akatazama na kukiona vyema kabisa.

“Pale panaitwa Ilha da Canzaga, itakupasa uende utamkuta mtu mmoja anaitwa Oliviera, mwambie nimekutuma akupe hiyo kitu, na ukiishaipata kwa sababu wengi wanaitafuta, utatakiwa ufanye juu chini uondoke katika jiji hili kabla hujang’anywa. Maana kuna watu wengi wako hapa Luanda wanataka kitu hicho hicho,” Perreira akamwambia. Na mara ukasikika mlio wa boti, ikasimama mbele kidogo baharini, na opareta wa chombo hicho alikuwa ni yule mwanamke aliyeleta sigara kwa Perreira.

“Tutaonana baadae, all the best!” Fernandes akamuaga Amata. Kamanda alipotaka kumpa mkono, yeye akachukua sigara yake nakuendelea kuvuta huku akigeuza kurudi ndani ya jumba lile.

Amata akatembea harakaharaka na kuingia ndani ya boti lile na safari ikaanza. Kamanda alijiegemeza katika kiti cha nyuma huku mwanamke yule akiwa kwenye usukani mbele yake akiedesha chombo hicho kwa kasi huku amesimama na kumfanya kijana huyu kusisimkwa mwili kila alipomtazama. Kiu kilimshika, akasimama na kumwendea pasi nay eye kujua, akafika nyumayake na kumkamata kiuno.

“What!!!” yule mwanamke akapiga ukelele mara baada ya kuhisi kuwa ameshikwa bila ridhaa yake.

“Mh mhhhhh, endelea na kazi, u mrembo sana bibie!” Amata akamwambia huku kidevu chake akiwa kakiegesha begani kwa mwanamke huyo.
“Kaa kitini tafadhali,” akasema yule mwanamke.
“Nitakaaje wakati wewe umesimama?” akamuuliza.
“Kwa hiyo?”
“Tukae wote,” akamwambia huku akimbusu nyuma ya shingo. Yule mwanadada akajikuta kwenye wakati mgumu sana.


KISIWA CHA ILHA DA CANZAGA
Kijana mmoja akaondoa jicho katika lensi kubwa ya bunduki ndani ya jengo moja la ghorofa mbili katika kisiwa hicho.

“Vipi?” mwingine akauliza.
“Huyu jamaa inaonekana anajua nini kinampata!”
“Kwa nini?”
“Si amemkumbatia Alegria, sasa nakosa shabahsa sahihi,” yule kijana akamwambia mwenzake, naye akaja na kuweka jicho kuangalia.

“Mh!” akaguna.
“Vipi?”
“Mwache afike, tutafanya kazi hiyo hapa hapa,” akasema.
Wale jamaa wakaendelea kuiangalia ile boti ikizidi kuja katika jumba hilo.
Katika boti lile, Amata bado alikuwa nyuma ya Alegria, akimpapasa kimahaba sehemu za kiunoni na juu kidogo ambapo panatengeneza umbo halisi la mwanamke.
“Sipendi kushikwa namna hiyo tafadhali,” Alegria akamwambia Amata huku mikono yake bado ikikamata usukani mdogo wa chombo hicho.
“Katika jingo hilo ndipo tunakwenda?” akamuuliza.
“Ndiyo!” mwanake yule akajibu. Amata akamwacha mwanamke huyo na kuketi tena kitini, akachukua miwani yake maalumu na kuivaa. Miwani hii ilikuwa na uwezo mkubwa wa kukuza vitu vilivyo kilomita moja kwa umbali na kumfanya mvaaji avitambue kwa urahisi. Alipohakikisha imemkaa vyema, akazungusha vijinobu viwili vilivyo upande huu na mwingine. Kamanda Amata macho yake yakagongana na mtu anyeshusha darubini na pembeni yake kuna bunduki kubwa ya kudungulia. Tayari walikuwa kama mita mia mbili hivi kufika katika ghorofa hilo, Akili ya Amata ikafanya kazi haraka na kuamua kwa kasi ya ajabu, akainuka kutoka kwenye kiti na kukanyaga batani ya mwendokasi na kuifanya ile boti iongeze kasi kwa ghafla kiasi kwamba Alegria alishindwa kuiongoza na kumuangukia Amata. Kijana huyo akamdaka na kumkumbatia huku mguu wake bado ukiwa kwenye ile batani.

“Unafanya nini wewe?” yule mwanamke akapiga kelele na kumpiga kipepsi Amata. Maumivu aliyoyasikia hayakuwa ya kawaida katika moja ya mbavu zake.
“Tuliaaa mwanamke!” Amata akamwambia na kumtupia upande wa pili, mwanamke yule akajiinua na kumtandika pigo moja matata, Amata akaona asiwe mjinga kwa tayari aliijua azma ya wenyeji wake, akatoa mguu kwenye ile batani na kumpiga ngwala Alegria, akaanguka vibaya na kujikuta akitumbukia baharini. Kamanda akarudisha mguu kwenye batani na injini ya boti ikavuma na kunyanyua chombo hicho mara baada ya kugusa mchanga. Boti ile ilipaa na kutua kwenye dirisha moja la kioo, ikaingia nusu na kuning’inia. Amata akaruka haraka nje na kutua sakafuni, mara risasi chache zikapiga sentimita chache kutoka pale alipokuwa ameangukia, lakini tayari alikwishabingirita na kuhama eneo kusudiwa. Alipotulia tayari bastola ilikuwa mkononi na alipofyatua shabaha yake haikupotea bure. Mtu mmoja akaanguka kama mzigo, na Amata akamuwahi na kummalizia kwa guu moja zito la shingo.

“To the ground floor!!!!” sauti kutoka ghorofa ya juu ikasikika, Amata akajiweka tayari, bastola mkononi, akajibana sehemu akisubiri kuona hao wanaoamriwa kuja upande wake. Punde tu akamwona kijana mmoja akiteremka kupiti ngazi ya mzunguko inayounganisha ghorofa ya juu na ile ya chini. Kamanda Amata akajua mara hii ameingia kwenye domo la mamba, akainua bastola yake na kufyatua risasi moja, shabaha maridhawa. Kijana yule akapiga yowe moja na kuanguka vibaya sakafuni. Amata akahama kutoka pale na kwenda upande mwingine kulikokuwa na maboksi makubwa ambayo hata hakujua nini kipo ndani yake, akatulia kimya kabisa.

Oliviera, kijana mshupavu wa mwili anayeaminiwa na mkuu wake Pereira, aliteremka taratibu huku mkononi mwake akiwa Shot Gun matata sana. Akaangaza angaza macho yake huku na kule akitembea hapa na pale kwa hadhari kubwa, fulana aliyoubana mwili wake ilionesha jinsi gani alikuwa ‘baunsa’. Kamanda Amata akaendelea kusubiri ili kijana huyo afike kwenye ‘kumi na nane’ zake.
Simpigi kwa risasi! Akasema moyoni huku akijiandaa kumpa shambulizi la dharula. Oliviera, akatazama na kutazama, hakuna mtu! Akaiweka sawa bunduki yake na kupiga ‘burst’, risasi mfululizo zikamwagika na kumua maboksi yale, kisha ukimya ukatawala.
“Vieira! Vieira!” sauti ya mwanamke ikaita kutoka nje.
“Alegria, ingia ndani, mshenzi huyu ametufanya vibaya…” Olivieira akamwambia mwanamke huyo.
“Amejificha humu ndani au amekimbilia wapi, sijui….”
“Shiiiit! Kamuua Joao!” Alegria akiwa na vazi lile lile la bikini, akamwendea marehemu pale chini na kumtikisa tikisa.
“Keshakufa,” Olivieira akasema.
“Kwa nini hamkumuua tangu tunakuja kama kawaida?” Alegria akamuuliza Olivieira.
“Huyu mshenzi ni mjanja, alijificha nyuma yako…”
“Hakikisha tunaitoa roho yake, maana kama akipata anachotaka ataharibu mambo!” mwanamke huyo akasema huku akichukua Shot Gun ya yule marehemu na kuikamata vyema. Muda wote huo, kamanda Amata alikuwa akiwatazama kutoka nyuma ya maboksi, pale alipo ni risasi kadhaa zilimpita karibu sana, kilichomuokoa ni kuwahi kulala chini. Kwa wakati huu alikuwa akisikiliza mazungumzo yote ya wawili hao, akajua kuwa marehemu anaitwa Joao, na pia kuwa anachokitaka kipo hapa.
Kumbe! Akawaza na kujiweka tayari kutoa shambulizi la dharula.
Hapa lazima mmoja afe na mwingine apate kipigo kitakachomlazimu kunipa kila kitu, shenzi sana! Akajisemea moyoni kisha akaanza kuchagua nani afe na nani abaki. Akimtaza Alegria, jinsi alivyoumbika hakutamani kabisa kumuua, lakini akajiuliza kama akibaki hai je aianajua kila kitu kilipo? Hakuoma haja ya kujiuliza hilo. Akaigiza mkono mfukoni na kutoa goroli tatu, akazirusha mja upande huu nyingine ule na nyingine katikati kwaribu kabisa na miguu yao, kisha yeye akahama haraka na kuelekea upande mwingine.
“Aaaaaaaaaaaaaiaiiiiiiiiiihhhhhhgggggghhhhh!!!!!” Oliviera akapiga kelele huku akimiminia risasi upande ule kwa minajiri ya kuua tu. Mwanamke yule naye akaungana naye kwa kufyatua risasi vilevile. Baada ya kama sekunde ishirini hivi, Olivieira akanyosha mkono na risasi zikakoma, kilichobaki ni harufu ya baruti tu. Oliviera akampa ishara ya mkono Alegria akimtaka kupita upande wa pili huku yeye akipita upande huu waibukie nyuma ya mabaoksi hayo. Kamanda Amata akajua wakitawanyika tu pale waliposimama itakuwa ngumu kuwashambulia. Akatumia nguvu zake zote na kuruka kutoka juu ya maboksi yale huku miguu yake ikimchangua mmoja baada ya mwingine. Oliviera alishtuliwa na kishindo cha Amata kuanda maboksi akatazama juu na kujikuta akikanyagwa na guu la uso, akayumba na kwenda kando wakati Alegria akienda chini na bunduki kumtoka mikononi.

Mara alipotua chini, Oliviera tayari alikwishajiweka imara, akamshushia konde moja zito, Amata akayumba kwa nyuma na kujikwaa kwenye mwili wa Joao na kuajikuta akitaka kuanguka kinyumenyume lakini akajiwahi. Oliviera alikuwa akimfuata Amata kwa kasi lakini alipomfikia tayari alijikuta kapoteza, kwani pigo moja la pili la tatu, yote ya karate yakamwacha hana hali. Jamaa huyo akainua pipa lililo karibu na kulirusha kwa nguvu, Amata akaruka sarakasi na kuliacha likipita chini. Alegria alijiokota kutoka pale chini kuokota ile bunduki, hata hakufanikiwa kuishika kwani alijikuta akiangukiwa na mtu juu yake.

“Tulia! Kahaba wewe!” Amata akaunguruma huku bastola ikiwa mkononi tayari ilikwshammaliza Oliviera.
“Nipe ninachohitaji haraka!” akamwamuru.
Alegria akarembua macho yake ili kumteka mwanaume huyo. Kama alifikiri Amata hudanganywa na wanawake kirahisi basi alikosea, risasi moja ikachimba milimita kama tatu hivi kutoka mguuni mwa mwanamke huyo.
“Nipe ninachotaka haraka kisha unirudishe kwa bosi wako,” akamwambia huku akimfuata taratibu. Mwanamke huyo mwenye bikini akajikuta hana kingine cha kumlaghai jamaa huyu.
Huyu ni nani? Akajiuliza.

“Huku, nifuate!” Alegria akamwambia Kamanda, kisha wakafuatana na Alegria akamzungusha mpaka upande wa nyuma.

“Inabidi twende bondeni,” akamwambia Amata.
“Bondeni wapi?” akamuuliza.
“Hicho unachokitaka, kipo bondeni,”
“Sitaki maneno, nipe ninachotaka,” Amata akasisitiza.
Pale aliposimama Alegria, pakafunguka na kuacha uwazi katikati, wakateremka na katika chumba walichopita, Amata akashtuka kukuta kuna mtu kafungwa minyororo miguuni na mikononi akining’inia.
“Shiit! Mfungue huyu!” akamwambia Alegria.
“Sina funguo, hiyo loki hufungwa kwa namba na namba hiyo anaijua Oliviera pekee, sasa si umeshamuua, kwa hiyo no way!” Alegria akajibu kwa dharau, Amata akavuta hatua moja na kumpiga kwa kitako cha bastola katikati ya paji la uso na kumpasua.
“Mfungue!!!” akamwambia. Alegria akajipapasa katika paji la uso, akashika damu inayotiririka, kisha akamtazama Amata.
Kama kuna kitu ambacho Kamanda Amata hakuwa anakipenda ni kuoneshwa dharau na mtoto wa kike. Akairudisha bastola mahala pake, kumfuata mwanamke huyo. Lakini kabla hajafanya atakalo, yule mwanamke akaliamsha dude kwa mapigo ya kutosha ya karate. Amata akayapangua yote kisha akamshushia moja la kilo nyingi na kumpeelka sakafuni. Kamanda akamuwahi huku tayari mkononi ana kisu kidogo amekwishakikunjua, akakididimiza kwenye nyama ya paja.
“Aaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaahhhhhh!!!!” Alegria akatoa yowe lililomstua yule mateka.
“Mfungue!!!” akamwambia na wakati huo tayari mkononi ana kisu kingine. Alegria akainuka kwa taabu na kutembea kwa kuushika ukuta huku damu ikimwagika kwenye paja lake, akaingia kwenye kile kuwazi na kubonya namba fulani kwenye kifaa maalumu, ile minyororo ikalegea na yule bwana akawa huru.
“Huyu ni nani?” akamuuliza.
“Mpumbavu kama wewe!” Alegria akajibu.
“Sawa, nioneshe ninachotaka,” akamwambia tena na mwanamke yule akaendelea kujikongoja mpaka kwenye mlango mwingine wenye kufuri.
“Hapa!” akamwambia Amata, naye hakufanya ajizi, akachukua bastola yake na kuifumua kisha mlango ukawa wazi. Kulikuwa na shelfu ya vitabu na kabrasha kadhaa. Amata akaingia ndani na kijichumba hicho na kuvuta hili na lile.

‘SECRET ASSASSINATION’ moja ya makabrasha lilikuwa limeandikwa hivyo.
“Thank you very much!” Amata akamwambia Alegria kisha akamwongoza kutoka nje wakampitia na yule bwana mwingine, Amata akamsaidia kumkokota mpaka pale kwenye boti lililonasa dirishani. Amata akalisukuma kutoka upande wa ndani nalo likajikita chini kwa upande wa nyuma, akatoka na kulivuta kwa nje, akalisukuma mpaka majini kwani hapakuwa mbali, kisha akamtaka mwanamke yule kushika usukani. Watatu hao wakaondoka taratibu na kutokomea baharini kurudi Condominio Bela Vista.

Palepale alipopandia boti ndipo liliposimama tena na Bwana Pereira akatoka nje kuwalaki. Mkononi mwa Amata kulikuwa na ule mkoba ambao ndani yake kuna lile kabrasha, akashuka nalo na kusimama wima. Kisha akageuka kwa Alegria na kuchomo kile kisu kutoka pajani. Pereira akaendeela kutazama Amata anavyomchomo kile kisu. Akakipangusa na kwa kitambaa kutoka mfukoni mwake na kukirudisha ndani ya koti la suti aliyoivaa.

“Umefanya nini?” Pereira akamwuulia Amata.
“Nashukuru kwa wema wako nimepata ninachokitaka, na nimempata rafiki yangu pia, good bye and see you soon!” Amata akamuaga na kuondoka na yule jamaa aliyechoka ambaye kwa mateso alibaki na nguvu aliyopewa na Mungu tu.

* * *

Kamanda Amata moja kwa moja alikwenda na mtu wake katika kliniki moja maarufu sana ambayo mzee yule, dereva wa taksi alikuwa anaijua na ndiye aliwapeleka. Katika kliniki hiyo, Amata akakutana na daktari mwanamama mtu mzima mwenye asili ya Kihindi, akamkabidhi mgonjwa huyo huku akimtaka asiruhusu kuonekana na mtu yeyote.

“Wala usiondoke, subiri hapahapa, ni masaa kama mawili au matatu tutakupa jibu na utaweza kwenda na mtu wako,” yule daktari akasema.
Kamanda Amata akasubiri. Baada ya saa mbili, kweli mtu yule alikuwa sawa, akitembea mwenyewe bila kushikiliwa, aliyeonekana kuwa na nguvu haswa.

“Na hizi ni dawa ambazo atatakiwa kunywa kwa wiki moja,” muuguzi akamwambia Amata kisha akazilipia na kuchukua majibu ya vipimo mbalimbali. Mtu huyo akatakiwa kurudi siku ya pili kwa matibabu zaidi au tuseme ya kina. Baada ya kutoka hapo, Amata na mtu wake wakaelekea mpaka Hoteli ya Alvalade ambako alimpangia chumba na kumpatia huduma zote ikiwamo mavazi na nyingine za kukandwa na kadhalika ili kumrudisha katika hali ya ubinadamu.

Baada ya saa mbili kupita, yule mtu akawa mwingine kabisa si yule aliyemwokoa kule kisiwani. Hakuwa kijana bali mtu wa makamo, mwenye mvi chache kichwani na ndevu zilizonyolewa kiufundi sana. Suti safi ya gharama ilitulia mwilini mwake, yote haya yalifanywa na Kamanda Amata lakini mpaka dakika dakika hii hakuna aliyemjua mwenzake, ni mtu huyu tu ambaye aliisikia japo sauti ya Amata lakini mwenzake hakusikia chochotebkutoka kwa mtu huyo.

* * *
Katika chumba namba 720, ndani ya Hoteli ya Alvalde, mtu huyu alisimama mbele ya kioo kikubwa akijitazama mwili wake uliositiriwa kwa suti ya gaharama.

“Ni nani huyu aliyeniokoa?” akajiuliza kwa sauti ndogo. Hakukuwa na wa kumjibu, akajitazama vidole vyake na kugundua kuwa kimoja kimekatika, hakipo kabisa, akatikisa kichwa.
“Walinikata kidole!” akajisemea tena. Akajaribu kutikisa mguu, unaweza kidogo japo bado una uzito au tuite ganzi.
“Miezi mine chini ya himaya ya washenzi hawa, bila Mungu wangeshaniua…” akajisemea.
Maneno yote haya aliyazungumza peke yake akiwa kasimama mbele ya kile kioo, mtu huyu aligundua udhaifu mkubwa wa mwili wake katika utendaji kazi. Jamaa hawa walimweka katika himaya yao kwa takribani miezi mine ilhali alikotoka walikuwa wakimtafuta na kusaidki kuwa kapotea au kafa kabisa. Akajaribu kuvuta kumbukumbu ya jinsi alivyoingia katika himaya ya washenzi hao hakukumbuka. Ubongo wake ulikuwa ukimleta mpaka anaingia kwenye gari, zaidi ya hapo ni giza na ukiwa.

Ngoh! Ngoh! Ngoh! Mbisho wa hodi ukamshtua kutoka katika mawazo yake. Akautazama mlango huo kwa chati huku kichwani mwake akijiuliza kama afungue au la.
Liwalo na liwe! Akajisemea na kuuendea mlango, akaufugua na macho yake yakagongana nay a Amata. Hakuongea kitu akajikuta akigwaya tu kwani hakumwona mtu huyo kutabasamu tangu alipomwokoa.

“Tunatakiwa kuondoka! Haraka!” Amata akamwambia.
Yule mtu hakujali kujiuliza imani yake yote ililala kwa kijana huyu ambaye ukiwaweka pamoja inaoneka wazi kuwa huyu ni mkubwa kama miaka mine au mitano kwa Kamanda. Akatoka na kumfuata Amata katika njia ya ngazi, kisha wakaachana na ngazi na kuchukua ukorido mrefu uliowatoa upande wa kumbi za mikutano huko wakateremka kwa ngazi nyingine mpaka chini kabisa, wakajikuta nyuma ya hoteli. Hawakujisumbua kuzunguka mbele, wakapita kwenye kijimlango kilichjengwa katika wigo wa hoteli hiyo na kuibukia barabarani, Amata akafungua mlango wa gari na kuingia ndani huku yule mtu akifuatia kisha wakaondoka kwa kasi.

Taksi ya akina Amata, ikawasili katika Nyumba ya Wageni ya Chicala iliyojengwa katika ghuba ya Total Angola.
“Hapa patatufaa!” akasema huku akitangulia kushuka na kuchukua mkoba wake kutoka katika siti ya nyuma. Hakujali kama mtu wake huyo anaelewa au haelewi. Kisha akamtazama yule mzee mwenye taksi ambaye mpaka dakika huyo hata yeye alikuwa akipelekwa pelekwa tu hajui nini kinaendelea.

“Sasa, we waweza kwenda, mimi nikikuhitaji nitakwambia, bado nina siku kama tatu hapa Luanda. Mtu yeyote akikuuliza kama niko wapi usimpe habari zangu sanasana nitumie meseji kwa siri na meseji hiyo aundike K.A, mi nitaelewa kuwa kuna mtu anakuuliza juu yangu. Akampa pes iliyotakata na kuagana naye.

Haikuwa Gesti ya hadhi kubwa ila si mbaya sana, wakapata chumba kiimoja chenye vitanda viwili na choo ndani. Ukikaa ndani ya chumba hiki na kutazama diridhani unakutana na Bahari ya Atlantiki na Kisiwa cha Ilha Da Canzaga unakiona kwa mbali sana ila kwa chombo kama darubini unaweza kukiona uzuri kabisa. Kamanda Amata akafunga mlango na kutupia mkoba wake kitandani kisha akaketi na yule mtu naye akaketi upande wa pili, yaani kwenye kitanda kingine. Kutoka katika meza ndogo pembeni yake, akanyakua simu iliyowekwa hapo na kuzungusha namba kadhaa kisha akaiweka sikioni. Baada ya kupokelewa upande wa pili, akaagiza whisky na bilauri mbili na kigudulia cha barafu. Haikupita muda mlango ukagongwa, akaufungua na mwanadada mfupi kibonge akaingia na kuweka kinywaji kile mezani kisha akaondoka zake. Amata akafunga mlango na kuketi huku akifungua kile kinywaji, moja ya bilauri akajimiminia na ile nyingine akampa rafiki yake ambaye hajawahi hata kusikia sauti yake.

Baada ya nusu saa ya kila mtu kupiga kama bilauli tatu hivi, Amata akafungua kinywa na kumuuliza, “ Wewe ni nani?”
Yule jamaa akamtazama Amata kana kwamba haelewi anachoambiwa.
“Naitwa Costantine!” akajibu kwa sauti ya kukwaruza sana kiasi kwamba Amata akajua wazi kuwa huyo jamaa ana shida kwenye mfumo wake wa sauti hasa kooni.
“Costantine?” Amata akarudia kwa kuuliza.
Mara hii kabla hajajibu akakohoa kwanza na kutikisa kichwa chake, “Yes! Costantine,” akajibu. Ukimya ukapita tena kwa jozi la sekunde, mara hii Amata akajua kwa nini mtu huyo hapendi kuongea kwani alihisi ana maumivu sana kwenye koo.
“Mimi naitwa Mr Spark kutoka Zambia…”
“Oooh Mr. Spark!”
Koh! Koh! Koh! Akakohoa mfululizo kisha akaendelea kusema, “Happy to know you… mimi nilikuwa nakufa polepole,” koh! Koh! Koh! “…lakini nashukuru umenileta tena duniani, umenipa nafasi ya pili ya kuishi,” akaongea kwa kirefu.
“Obrigado!” akamshukuru.
Costantine akainuka na kuelekea dirishani, akasimama na kuangalia upande wa baharini, kisha akachukua darubini ya Amata iliyokuwa juu ya meza, akatazama tena baharini.
“Ilha Da Canzaga!” akatamka. Kamanda Amata akainuka alipoketi na kumwendea pale dirishani, wakasimama pamoja.
“Unapaona vizuri?” akamuuliza.
“Yes!”
Kishapo, Amata akachukua simu yake na kufungua program fulani katika hiyo, wakati wote Costantino alikuwa akimwangalia anachofanya. Na mara mlipuko mkubwa ukaonekana kule kisiwani.
“Kila kitu kimeanguka!” Amata akasema. Costantine akatazama kisini na kushuhudia moto na moshi mzito, akageuka kwa Amata na kumtazama, akamwona akiirussha ile simu kitandani na kisha ye mwenyewe kujibwaga hapo na kujimiminia kinywaji.
“Who are you?” Costa’ akamuuliza.
“Mr. Spark… mwokozi wa wanyonge,” akamjibu.
“Kazi yako ni nini hasa hapa Angol?” Costa akaanza kumhoji Amata.
“Nilikuja kuiangusha Ilha Da Canzaga, bahati nzuri nimekuokoa na wewe lakini pia nilikuwa nahitaji hii…” akachomoa kabrasha lake mkobani na kumwonesha kwa mbali.
“A secret assassination!” akasoma.
“Yes! Sasa sikiliza, mimi nimemaliza na hatuna budi kuagana, lakini marafiki lazima wajuane kwa kina….”
“…Ndiyo, bila shaka…”
“Ulikuja kufanya nini Angola?” akamuuliza.
“Nilikuja kumsaka mtu mmoja muuaji anayetafutwa kila kona ulimwenguni, lakini mtandao wake ukahi kunitambua na wakaniteka na kujikuta nipo kule, hata sikuwa najua kama ni kisiwani mpaka nilivyoona tulipokuwa tunatoka,” Costa akasema.
“Muuaji?” Amata akauliza.
“Yes, muuaji mmoja profesheno… katika kumtafuta nikagundua kuwa ana misheni ya kufanya hapa Angola …”
“Lini ilikuwa atekeleze misheni hiyo….?” Amata akamkatiza kwa swali.
“Aaaaannnhhh huu ni mwezi gani, samahani!” Costa akauliza, kumbe hata hakuwahi kujua tarehe na miezi inakwendaje.
“September!” akajibiwa
“September?” khooo – kho! Akakohoa, “ina maana nimekaa miezi mine mateka?” akasema.
“Ni miezi mine iliyopita… huyu bwege anaitwa Martin Gupter ila hutumia majina mengi sana na sura nyingi za bandia kujificha, yeye hutumiwa na mitandao mikubwa ya mauaji ijapokuwa naye anatimu yake ya watu wawili wenye weledi mkubwa wa mbinu za kigaidi na mauaji, hayawajawahi kukamatwa wala kujulikana kwa majina halisi,” akamwambia Amata.
Akili ya Kamanda ikaanza kuunganisha matukio, akachekecha na kuchekecha, akaona kwa vyovyote vile kuna uwezekano mkubwa wa misheni yao kuwa moja ila ikatofautiana maudhui.
“Miezi mine ilopita, aliuawa rais wa Angola,” Amata akasema.
“Come on! Walifanikiwa? Hawa ni washenzi…” Costa akaongea kwa hasira kidogo.
Ina maana huyu jamaa anajua mengi juu ya hili! Amata akawaza na kubaki kimya kwa sekunde kadhaa akimtazama mtu huyo. Baada ya muda kidogo, Costantine akainua uso na kumtazama Amata.
“Martin Gupter ni muuaji hatarai sana, yeye amebobea katika assassination iwe ya moto au ya baridi. Anatafutwa, natafutwa na watu wengi ikiwamo mimi, nilipata siri ya kuwa wanakuja huku Angola ili kutekeleza mauaji ambayo wenyewe waliyaita ‘Mauaji ya Kihistoria’, nikiwa hapa nikawafuatilia sana mpaka nikajua ni wapi watafanyia shabaha yao, siku nilipokuwa nimepanga kumaliza mchezo nikajikuta matatani, nilikuwa nachukua gari kwenda eneo la tukio, ghafla nikapigwa na kitu kama bomba la chuma kichani, nikapoteza fahamu na kujikuta ndani ya chumba kile. Wao nao wakanitesa na kunipiga sana ili niwaambie ni nani kanituma…”
“Kwa hiyo ni hicho tu kilichokuleta Angola?” Amata akamuuliza.
“Hicho tu! Namhitaji Gupter nimtoe roho yake, nilishahesabu nimeshindwa lakini wewe umenipa nafasi nyingine na kwa nafasi hii lazima nimmalize,” akasema, “na wewe huna haja na huyu shetani?”
“Sina, ila ninachotaka sasa ni kukamilisha uchunguzi kama mtu aliyetaka kufanya mauaji Dar es salaam ni huyo huyo au la…”
“Tena?”
“Ee ila hakufanikiwa na risasi ikamuua mtu mwingine, sasa nataka kuhakikisha je muuaji huyu wa Angola na yule wa Dar es salaam ni mmoja? Amata akamwambia huyu mtu bila kumzungusha.
“Hiyo kazi ndogo, nitakupeleka kwa mtu mmoja ambaye anaweza kukusaidia kujibu maswali ya shida yako, kwa vyovyote atakuwa anajua nini kinaendelea”.
“Twende hata sasa!” Amata akasema huku akiwa tayari amekwishainuka.

Wakatoka nje na kufunga mlango kisha wakachukua taksi mpaka mtaa mmoja wa kimya sana, ni majumba makubwa na machache yaejipanga upande huu na ule.
“Tuache hapa!” Costantine akasema na lile gari likaingia pembeni, wakashuka na kulipa kisha likaondoka, wakalitazama kwa kulisindikiza mpaka lilipoishia kwenye upeo wa macho yao.
Kutoka hapo wakavuka barabara, na Costantine akaongoza njia mpaka katika jumba moja la kifahari. Muda wote huu, Costantini ndiye alikuwa mbele huku Amata akifuatia kwa karibu maana hakujua hata ni wapi kiukweli alikuwa akipelekwa.
Kelele za mbwa akibweka zilisikika ndani ya wigo wa jumba hilo, na kabla hata hawajabonyeza kitufe cha kengele, mlango ukafunguliwa na mtu mmoja wa makamo aiyevalia jinzi na fulana mchinjo akatoka na kulifuata geti hilo kwa mwendo wa haraka kidogo. Bila kuongea neno lolote akafungua geti na kuwapa ishara ya kuingia, wakafanya hivyo na bwana huyo akawaongoza mpaka sebuleni wakaketi.
“Yes! Nashindwa niseme nini, ni wewe au?” yule bwana akamuuliza Costantine, wala hakuwa na muda na Amata.
“Yes! Ni mimi, nilikuwa mikononi mwa mbwa kwa miezi karibu mine kwa mujibu wa kalenda,” Costa’ akaeleza.
“Nilijua umekufa, tumekutafuta sana, mpaka kwa waganga tumeenda, mwisho tukakubali kushindwa…”
“Mlikubali tu kushindwa, ila sikufa…” akamjibu kwa kumkatiza kile alichokuwa akiongea. Yule jamaa akampa ishara ya kumwita pembeni ili wazungumze machache.
“Hamna shida, ongea hapahapa!” Costa akasema huku akimtazama Amata, “Najua sijakutambulisha, huyu ni rafiki yangu, anaitwa Spark!” akamtambulisha Kamanda kwa mwenyeji wake kisha akafanya hivyo kwa Kamanda Amata, wakafahamiana na kupeana mikono.
“Nasikia mzee katunguliwa,” akaanzia hapo na Amata akawa kimya akaisikiliza tu.
“Yes! Tumeshasahau ila bado tuna kazi ngumu kwani baada ya kufanya uchunguzi na kuweka tafutishi zote pamoja lile kabrasha likaibwa, mpaka sasa badala ya kumsaka muuaji tunatafuta kabrasha,” akaeleza.
“Oh shit! Hamjapata chochote? Ni Gupter au ni nani?” Costa akauliza.
“Hatujang’amua ni nani mpaka sasa tumemwita jina ‘sweet killer’ kwa sababu anaua na hapendi kuacha chochote nyuma yake, bahati nzuri tu niliokote kitu hiki…” akainuka na kuiendea droo, akafungua na kuchukua kijimfuko cha plastiki akaenda nacho mezani na kukifungua ndani, akamwaga vitu viwili … “ganda la risasi lakini ni mita kama mia tatu kutoka eneo tunalolihisi muuaji alikuwako,” akaeleza.
“Naweza kulishika?” Amata akauliza.
“Yes, ila usitumie mkono tupu,”
“Sawa!” Amata akajibu na kutoa soksi za mikononi kutoka katika suti yake akavaa na kuinua lile ganda, akaligeuza kwa nyuma na kujikuta anapigwa na bumbuwazi.
Magnum 22 riffle! Akasoma kilichoandikwa kisha akampasia Costantine, naye akalipokea na kuatazama vizuri.
“Martin Gupter! Huyu ni Gupter, siri ya jamaa huyu ni kutumia aina moja ya bunduki, Magnum 22 riffle, nimepita kwenye kesi zake kama tatu hivi kati ya hizo wachunguzi wamegundua aina hii ya bunduki kutumika,” Costa akaeleza.
“Ungekuwa umefanikiwa kumpata, ungetusaidia sana, sasa utafanya nini, kwa ujumla si kwamab tumemkosa ila ni kazi sana kumpata,” yule jamaa akasema.
“Mh!” Costa akaguna, “Jerry! Huyu bwana naye anamtafuta Gupter naweza kusema hivyo,” akamwambia.
“Huyu? Mr Spark?” akauliza. Ni mara hii Jerry alimtazama Amata, akaondoa miwani yake na kuiweka kitini, akatikisa kichwa, “Unamtafuta Gupter, the sweet killer?” akamuuliza.
“Si kwamba namtafuta Gupter, kwa sababu mpaka sasa inabidi nijiridhishe kama ndiye ninayemtafuta. Si unajua kilichotokea Tanzania siku nne zilizopita!”
“Yes! Najua, na ninafuatilia kujua nini Tanzania inafanya kwa sababu tunaiamini sana kwenye maswala ya kijasusi, ila hatujasikia chochote,” Jerry akasema.
“Ninaanza kuona kuwa ni huyu aliyetaka kutekeleza mauaji ya Dar es salaam…”
“Kwa nini??” hii ‘kwa nini’ ikatoka kwa Jerry na Costa’ kwa mara moja. Kamanda Amata akaingiza mkono mfukoni na kutoa kijimfuko cha plastiki na kuweka mezani ganda la risasi kama lile lile.
“Shiiiiit!” Jerry akang’aka kwa kulitazama tu, kisha akamtazama Amata na kisha Costa.
 
Mkuu Kulubule nakuonaaaaaaaaaaaaaaaa, tafadhali tushushie mzigo mrefuuuuuuuuuuuuuuuuu huku tukivuta pumzi za kushuhudia mwali wa dunia anaelekea wapi kati ya France na Croatia
 
MAGNUM22

Sehemu 12

Sasa nahitaji msaada wa jambo moja tu kutoka kwako…” akamwambia Jerry.
“Sema, na tutasaidiana kumtia mkononi mshenzi huyu!”
Kamanda Amata akatoa picha ya mwanamke wa Kizungu, akaiweka mezani, “katika tukio hilo, ulimwona mtu huyu ama anayefanana au mwanamke tu yoyote wa kizungu kama si akipita basi akitazama kinachoendelea au chochote kile?” Amata akauliza.
Jerry hakujibu, akaitazama ile picha kwa makini sana, kisha akamtazama tena Amata, wakatazamana, “ninamkumbuka hata kama ni miezi mine imepita, huyu mwanamke asubuhi ile, alikuwa akipita anafanya mazoezi ya jogging, nikamzuia na kumtaka apite upande mwingine, akatii wala hakuwa na ubishi, ndiyo ni huyu ama pacha wake, ila wanashahabiana,” akamwambia.
Kamanda Amata akachukua ile picha na kile kijimfuko akavirudisha kotini mwake.
“Spark! Vipi?” Costa akauliza.
Amata hakujibu, akamtazama Jerry, “Jerry, you people, mnafuga magaidi ilhali mnakaa na kunywa nayo,” akasema. Jerry akajikuta hana cha kusema akaendelea kumkodolea macho Amata.
“Kivipi?” Costa akauliza.
“Jerry, unamjua huyu?” akamuuliza akimaanisha kama anamjua Costantine.
“Yes, Costantine ni rafiki sana na mimi, tumefanya kazi hizi pamoja mara nyingi ila yeye sasa ni mpelelezi wa kujitegemea huko Costa Rica, alikuja hapa kwa minajiri ya kumsaka huyu mshenzi, na ni yeye aliyenigutusha mimi kuwa kuna uwezekano wa kutukia tukio la mauaji ya kiongozi hapa. Mara baada ya kunijuza nikalifikisha kunakohusika tukaanza kulifanyia kazi. Siku mbili kabla ya tukio sikumwona Costa, nikamtafuta sana pasi na mafanikio, nimeshtuka sana kumwona leo kwani nilikwishajua kuwa amekufa,” akaeleza.
“Washa TV,” Amata akamwambia Jerry, naye akafanya hivyo na habari waliyoikuta ni kuhusu Kisiwa cha Ilha Da Canzaga.
“What?” Jerry akajikuta anapigwa na butwaa baada kushuhudia moto mkubwa huko kisiwani huku jitihada za kuuzima zikiendelea.
“Samahani, naweza kwenda toilet?” Amata akaomba na kuoneshwa ni wapi choo kilipo. Akainuka na kuwaacha wawili hao wakiwa wamekodolea macho luninga, akafungua mlango na kuufunga.

Nusu saa ikapita, Amata hakurudi sebuleni, “hey! Mr Spark!?” akamuuliza Costa. Costa yeye hakujibu ila aliinuka na kuelekea chooni, akatikisa mlango, uko wazi, akausukuma huku akiita, hakuna mtu, kwenye tanki la maji ya kuflashi kuliandikwa kwa maka peni nyekundu.

Fernandes Perreira ndiye anayewasaliti! Costa akamwita Jerry naye akaja na kushuhudia maneno hayo.
“Ameondoka!” Jerry akasema.


* * *
MSAKO MKALI wa kumtia mkononi Amata ukaanzishwa ndani ya Jiji la Luanda, Fernandes Perreira mara baada ya jingo lake kule katika Kisiwa cha Ilha Da Canzaga kulipuliwa akajua tu hakuna mwingine zaidi ya mgeni wake aliyemtembelea na kutaka kupatiwa kabrasha la ‘SECRET ASSASSINATION’. Taarifa ikafika kwenye vyombo vya usalama na kazi ikaanza, akamatwe afikishwe panapohusika.
Fernandes Perreira alikuwa akizunguka huku na kule, nywele zimemsimama, hataki kungea na yoyote zaidi ya kufuta jasho tu, alichanganyikiwa, simu zilipigwa, akapokea, akaongea maneno machache tu, akakata. Wageni wengi, matajiri kwa viongozi wa serikali walimiminika kumpa pole kwa tukio hilo na baadhi yao ndiyo wakapata jazba ya kutaka mtu huyo asakwe mara moja.

Wakati yote hayo yakijiri, Kamanda Amata alikuwa akimlipa pesa dereva taksi wake, tayari kwa safari ya kurudi Tanzania, alijua kwa vyovyote lazima atakuwa hatarini tu, wakaagana na yule mzee huku akiwa amemwachia pesa nyingi tu. Kamanda Amata, akaingia katika ofisi ya ndege binafsi, bahati nzuri akapata ndege na kukodi, nusu saa baadae akaiacha Angola na kurejea Tanzania akiwa tayari keshapata jibu la moja na moja ni ngapi.




Kwakuwa timu yangu imefungwa mle nusu dozi
 
Mwali anaenda Croatia na sivinginevyo
Unasubiriwa etView attachment 810260
IMG-20180715-WA0012.jpg
 
MAGNUM22

Sehemu 12

Sasa nahitaji msaada wa jambo moja tu kutoka kwako…” akamwambia Jerry.
“Sema, na tutasaidiana kumtia mkononi mshenzi huyu!”
Kamanda Amata akatoa picha ya mwanamke wa Kizungu, akaiweka mezani, “katika tukio hilo, ulimwona mtu huyu ama anayefanana au mwanamke tu yoyote wa kizungu kama si akipita basi akitazama kinachoendelea au chochote kile?” Amata akauliza.
Jerry hakujibu, akaitazama ile picha kwa makini sana, kisha akamtazama tena Amata, wakatazamana, “ninamkumbuka hata kama ni miezi mine imepita, huyu mwanamke asubuhi ile, alikuwa akipita anafanya mazoezi ya jogging, nikamzuia na kumtaka apite upande mwingine, akatii wala hakuwa na ubishi, ndiyo ni huyu ama pacha wake, ila wanashahabiana,” akamwambia.
Kamanda Amata akachukua ile picha na kile kijimfuko akavirudisha kotini mwake.
“Spark! Vipi?” Costa akauliza.
Amata hakujibu, akamtazama Jerry, “Jerry, you people, mnafuga magaidi ilhali mnakaa na kunywa nayo,” akasema. Jerry akajikuta hana cha kusema akaendelea kumkodolea macho Amata.
“Kivipi?” Costa akauliza.
“Jerry, unamjua huyu?” akamuuliza akimaanisha kama anamjua Costantine.
“Yes, Costantine ni rafiki sana na mimi, tumefanya kazi hizi pamoja mara nyingi ila yeye sasa ni mpelelezi wa kujitegemea huko Costa Rica, alikuja hapa kwa minajiri ya kumsaka huyu mshenzi, na ni yeye aliyenigutusha mimi kuwa kuna uwezekano wa kutukia tukio la mauaji ya kiongozi hapa. Mara baada ya kunijuza nikalifikisha kunakohusika tukaanza kulifanyia kazi. Siku mbili kabla ya tukio sikumwona Costa, nikamtafuta sana pasi na mafanikio, nimeshtuka sana kumwona leo kwani nilikwishajua kuwa amekufa,” akaeleza.
“Washa TV,” Amata akamwambia Jerry, naye akafanya hivyo na habari waliyoikuta ni kuhusu Kisiwa cha Ilha Da Canzaga.
“What?” Jerry akajikuta anapigwa na butwaa baada kushuhudia moto mkubwa huko kisiwani huku jitihada za kuuzima zikiendelea.
“Samahani, naweza kwenda toilet?” Amata akaomba na kuoneshwa ni wapi choo kilipo. Akainuka na kuwaacha wawili hao wakiwa wamekodolea macho luninga, akafungua mlango na kuufunga.

Nusu saa ikapita, Amata hakurudi sebuleni, “hey! Mr Spark!?” akamuuliza Costa. Costa yeye hakujibu ila aliinuka na kuelekea chooni, akatikisa mlango, uko wazi, akausukuma huku akiita, hakuna mtu, kwenye tanki la maji ya kuflashi kuliandikwa kwa maka peni nyekundu.

Fernandes Perreira ndiye anayewasaliti! Costa akamwita Jerry naye akaja na kushuhudia maneno hayo.
“Ameondoka!” Jerry akasema.


* * *
MSAKO MKALI wa kumtia mkononi Amata ukaanzishwa ndani ya Jiji la Luanda, Fernandes Perreira mara baada ya jingo lake kule katika Kisiwa cha Ilha Da Canzaga kulipuliwa akajua tu hakuna mwingine zaidi ya mgeni wake aliyemtembelea na kutaka kupatiwa kabrasha la ‘SECRET ASSASSINATION’. Taarifa ikafika kwenye vyombo vya usalama na kazi ikaanza, akamatwe afikishwe panapohusika.
Fernandes Perreira alikuwa akizunguka huku na kule, nywele zimemsimama, hataki kungea na yoyote zaidi ya kufuta jasho tu, alichanganyikiwa, simu zilipigwa, akapokea, akaongea maneno machache tu, akakata. Wageni wengi, matajiri kwa viongozi wa serikali walimiminika kumpa pole kwa tukio hilo na baadhi yao ndiyo wakapata jazba ya kutaka mtu huyo asakwe mara moja.

Wakati yote hayo yakijiri, Kamanda Amata alikuwa akimlipa pesa dereva taksi wake, tayari kwa safari ya kurudi Tanzania, alijua kwa vyovyote lazima atakuwa hatarini tu, wakaagana na yule mzee huku akiwa amemwachia pesa nyingi tu. Kamanda Amata, akaingia katika ofisi ya ndege binafsi, bahati nzuri akapata ndege na kukodi, nusu saa baadae akaiacha Angola na kurejea Tanzania akiwa tayari keshapata jibu la moja na moja ni ngapi.




Kwakuwa timu yangu imefungwa mle nusu dozi
Mmmmmh! Mimi nilidhani kuwa kwa kuwa Timu yetu tuliyokuwa tunaishabikia imefungwa then ungeweka vipande ving zaidi ili tujisahaulishe kuhusu mpira.......
 
MAGNUM22

Sehemu 13

SHAMBA

MADAM S akarudi tena mezani alipowaacha Amata na Chiba, akatua lile kabrasha na kuvuta kiti, akaketi na kusogeza kabrasha lile kwake.
“Vipi?” Kamanda akauliza.
“Umefanya kazi kubwa sana mwanangu, ndani ya kabrasha hili kuna kila kitu, mpango mzima wa mauaji na mpango mzima wa uchunguzi, sasa swali ni kwamba ina maana hawa jamaa wanajuana na pande nzote?” akauliza.
“Nafikiri hivyo kwa maana wangepataje taarifa ya uchunguzi uliofanywa na wapelelezi wa serikali? Na wamepataje mpango mzima waq mauaji ya siri ambayo Gupter na wenzake wameupanga? Huyu ni nyoka mwenye vichwa viwili…”
“Ndumi la kuwili,” Chiba akamkatisha Amata.
“Nimesoma ndani ya kabrasha hili, nimegundua kitu kingine ambacho wala hatuna budi kuumiza kichwa…”
“Kipi hicho? Maana mimi sijasoma chochote,” Amata akadakiza.
“Mauaji ya Waziri Mkuu wa Ivory Coast ni wao pia waliohusika, maana nimeona mpango mzima hapa ndani na hakika wametekeleza isipokuwa si kwa mbinu ambayo wameianisha humu, mpango wa tat undo ulikuwa hapa kwetu ambao kwa hakika umefeli kwa asilimia themanini na tano,” Madam S akawaeleza vijana wake.
“Enhe!”
“Sasa hapa kuna mpango wan ne ambao maelezo yake hayapo sawasawa yaani hayajakamilika, inaonekana watu hawa huweka hizi karatasi hatua baada ya hatua…” akaeelza.
“Kwa hiyo walipanga mauaji ya watu wane?” Chiba akauliza.
“Yes! Na wane hao ni ndani ya miezi sita, wakiwa na maana kuwa Afrika itashtuka na kuwasikiliza kila wasemacho,” Madam akawaambia.
“Sawa, nani wa nne?” Amata akarusha swali.
“Enheeee hicho sasa ndicho kitendawili ambacho yatupasa kukitegua, na huyu wan ne anatakiwa kuuawa katika miezi hii miwili, ni nani na ni wapi, kazi ipo!” Madam S akafunga lile kabrasha na kuliweka kando.

“Tupo kazini,” akawaambia, “Na safari hii mkubali tu kuifanya peke yenu sijui kama Jasmine na Scoba watawahi maana wana kibarua kizito kule Haiti,” akawaambia.

Ukimya ukatawala kwa sekunde chache, hakuna aliyemwongelesha mwenzake wala kumshtua, Amata akavuta kwake lile kabrasha na kufungua kurasa ya mwisho kabisa. Huko akakutana na maneno machache tu ya kuhusu mpango huo wa nne.
“Watakamilishaje mpango wan ne kama wa tatu wamefeli?” Amata akauliza.
“Mi na wewe hatujui, sisi cha kufanya ni kuhakikisha mpango huo haufanikiwi kabisa kama ambavyo tumeweza hapa,” Madam akasema.
“Siri ya mpango wa nne wanayo wao wenyewe, yatupasa kuwatia mkononi,” Kamanda akawaambia.
“Naam, hivyo mwanangu huna mapumziko, anza kujiandaa safari ya Sierra Leone kama Chiba alivyosema imewadia, nataka kwanza ukahakikishe umewapata na kutibua mipango yao kisha hakikisha unapata kujua ni nani anayewatuma, yuko wapi na wapo wangapi,” akamwambia.
“Bila shaka, nitahakikisha hilo linafanyika,” akajibu
“Asante sana!”
Kikao kikafungwa ikiwa tayari TSA 1 anakabiliwa na mtihani mwingine wa kuwasaka hawa jamaa wauaji. Ni tafutishi za Chiba ambazo aizipata kwenye ile micro chip chumbani kwa Amanda kule Kunduchi ailiyomhakikishia kuwa watu hao mara baada ya kila mauaji huenda kujificha huko Sierra Leone, katika mji mdogo wa Waterloo.

“Comrade!” Chiba akaita. Amata akamtazama swahiba wake, mwenye renki inayofuata chini yake yaani TSA 2, mbobezi wa ujasusi wa kimtandao, mkufunzi katika Chuo Kikuu cha Mlimani katika kitengo cha TEHAMA.
“Nambie comrade!”
“Una kazi ngumu kaka,” akamwambia.
“Sure, ila kama wewe upon a Gina pia naamini haitakuwa ngumu,”
“Unategemea kuondoka lini?”
“Hatutakiwi kuwapa muda mrefu washenzi wale, kwanza naamini mpaka sasa watakuwa wameshanganyikiwa kama wamepata habari ya Angola,” akamwambia Chiba.
“Na umewatetemesha haswa!”
“Na bado nitawasambaratisha kabisa…” Amata akasema huku akiinuaka na kuiendea moja ya kompyuta iliyo jirani naye ndani ya chumba hicho cha mawasiliano.
Jioni hiyo Kamanda Amata alifanikiwa kupata ndege ya shirika la Ethipian Airline ambayo ilimtaka kuondoka mchana wa saa sita wa siku inayofuata. Haikuwa mbaya sana kwake, cha muhimu tu ni kuwa alitakiwa kufika katika nchi hiyo na kumsaka Martin Gupter na watu wake.
“Naomba uendelee kuwachunguza watu hawa unipatie majina kamili, kama ingewezekana basi tungeweza kujua hata ni wapi katika huo mji wapo maana inawezekana wasiwepo kabisa hata Sierra Leone…”
“Kivipi?”
“Kwa sababu kama wao ni wajuvi wa mambo haya ya assassination, kwa kuwa wamefeli kwenye jaribio lao basi wanatakiwa wabadili mbinu zote zinazofuata, kwa maana ukikosa kutimiza lengo maana yake ni kuwa umeongeza uwezekano wa kukamatwa hivyo lazima ujifiche mahala pengine…” Amata akamwambia Chiba.
“Aaaaaaa mi sitaki wafanye hilo!”


* * *

SIERRA LEONE
KATIKA MJI MDOGO wa Waterloo, kando ya mto mkubwa wa Lofa, kulikuwa na jumba kubwa sana la ghorofa tatu ambalo lilijengwa katika ubavu wa mlima. Jumba hili kama ungelitazama ukiwa juu yam lima ungeliona ni la kawaida yaani si ghorofa, na kama ungekaa mtoni, maana yake bondeni ndipo ungeona kuwa ni ghorofa. Wakazi wa jumba hili walionekana mara chache sana, zaidi nji wafanya kazi wa bustani, shamba na mambo mengine, hawa ndo haswa ungewaona kuanzi asubuhi mpaka saa tisa alasiri, zaidi ya hapo huwa kimya na upweke wake.

Hakuna aliyemjua haswa mmilikiwa jumba hili, wala kumwona, japo tu walipata tetesitetesi kuwa ni malia ya tajiri mmoja wa Kiarabu ambaye yupo nchini humo kama mfanyabiashara mkubwa mwenye utajiri wa mafuta huko Saudia na sasa alikuwa tayari ameanza kuchimba mafuta katika Bahari ya Atlantiki.

Katika miezi sita hii wafanyakazi walishuhudia wageni wapya watatu; wanaume wawili na mwanamke mmoja, hawakuhoji kwa sababu hayakuwa yakiwahusu. Walikuwa wakikaa katika jumba hilo na kuondoka kisha wangekuja tena, vivyo hivyo.
Martin Gupter, Amanda Keller na Frederick waliweka kambi katika mjengo huu, wakipanga mambo yao ya siri na kuweka mipango yao ya kufichika ndani yake. Mkataba mnono wa tajiri Jaffery Bakhari uliwataka wajitenge na dunia kwa miezi takribani nane hivi ili wakamilishe misheni hiyo ambayo waliita ‘Secret Assasination’.
Mara tu baada ya kuikamilisha kazi ambayo almanusura iwagharimu maisha yao na kutibua kila kitu, walikuja tena katika jumba hilo ambalo Kamanda Amata alimwambia Chiba kuwa watakuwa wamefanya kosa kubwa kama watarudi Waterloo, na ndivyo walivyofanya.
Katika sebure kubwa yenye kila samani ya thamani watatu hawa waliketi wakijimiminia vinywaji vikali kwenye matumbo yao na kuzungumza hili na lile
“Nyie hamjanielewa,” Martin akawaambia wenzake.
“Si kwamba hatujakuelewa, ipo hivi, kushindwa kumuua Rais wa Gambia ni kupunguza usalama wetu, huwezi kujua ni nguvu gani watachukua kututafuta, hatukupaswa kurudi hapa,” Fredy akamwambia Martin.
“Ndo maana nimesema hamjanielewa, nilitaka turudi hapa makusudi kwa sababu kama watatuma mtu au watu kutuchunguza tulipo, na kama wamepata information yoyote juu yetu basi watakuja hapa na sisi itabaki kuwazika mmoja baada ya mwingine ndani ya kaburi letu. Cha kufanya ni kuweka tayari watu wetu katika maeneo myeti,” akawaambia.
“Umesomeka!” Amanda akajibu, “Na nina wasiwasi sana na Tanzania, hawa wanaweza kuamua kulivalia njuga…” akaongeza kusema.
“Of course, sasa inabidi tuwapate watu wote hatari wa Tanzania, inawezekana wakatuma mmoja wa hao, Fredy fanya hiyo kazi mara moja,” Martin akatoa amri na Frederick akaingia kazi na kuanza kuusaka mtandao wa serikali ili tu aweze kupenye ndani na kuufikia idara ya usalama. Mara simu ya Martin ikaanza kuita, akainyakua na kutazama, namba haikujionesha, hivyo hakujua ni nani anayepiga, akaifyatua na kuiweka sikioni. Akazungumza na mtu wa upande wa pili kama dakika kumi hivi, ni sura yake tu iliyokuwa ikibadilika badilika iliyowapa ishara Amanda na Fredy kuwa taarifa anayoipokea ni hatari. Baada ya mazungumzo hayo akakata simu na kuitupia kochini.
“Vipi?” Amanda akawa wa kwanza kuuliza huku Fredy akaiachana na ile laptop na kuwa tayari kusikiliza.
“Habari mbaya, yatupasa kuwa tayari na makini, tunaweza kuvamiwa any time…”
“…mbona sikuelewi…”
“Mambo yameanza Angola, Joao ameuawa, Oliviera ameuawa, yule mshenzi Costa ametoroshwa, na kisiwa cha Ilha kimeteketezwa kwa moto. Aliyeyafanya hayo inasemekana ni spy kutoka Tanzania, na kabrasha la S.A amelichukua…” Martin akaeleza.
“Mama yangu!” Amanda akang’aka, “inabidi tupange mbinu mpy a ya kujikinga haraka sana,” akasema na kabla hajamaliza mashine ya nukushi ikaanza kutoa ukulele wa kuashiri kuwa kuna jumbe unaoingia. Kweli, picha kubwa ya A4 ikajitokeza, Amanad akainyakua na kuitazama kisha akampa Martin na kisha Fredy, kila mmoja akaitazama kwa dakika au sekunde anazoona yeye zinamfaa.
“Huyu, huyu, huyu, nataka afie kwenye hili kaburi hapa,” Martin akasema.
Amanda akazidi kuitazama ile picha ya kijna arijali mtanashati aliyevalia suti na macho yake yakiwa yamefichwa kwa miwani.
“Amejitambulisha kwa Pereira kama Mr. Spark…” Martin akasema.
“Haina tabu tunamkaribisha Waterloo,” Fredy akajibu kauli ya Gupter na kuendelea kazi yake mtandaoni, safari hii badaal ya kuuchunguza ule mtandao wa serikali, sasa akawa anatafuta data zaidi za Mr Spark kama angeweza kupata.
“Ana bunduki yangu huyu,” Martin akasema, “ndiye binadamu wa kwanza aliyeumbwa na Mungu kufanikiwa kupata bunduki yangu, haiwezekani, unafikiri nitafanyaje kazi bila mtoto wangu? Tuna miezi miwili tu iliyobaki tukamilishe mkataba na Jaffery tukamate pesa nzuri ya kutuwezesha kumiliki Dreamliner, ila huyu anataka kutuharibia, ni nani huyu? Nitamzika akiwa hai hapa chini ya nyumba hii akakutane na wajomba zake,” Martin akasema huku akionekana wazi kuwa tayari kilevi kimeshaanza kumchukua.
“Naenda kulala, nikiamka tutapanga kazi ya siku tano tu ya kumuua mshenzi huyu!” akasema na kuipiga bilauri ukutani kisha akaingia zake vyumbani. Amata na Fredy wakabaki wakimtazama tu, hawakuwa na la kufanya juu ya hili. Mwanamke huyu wa kizungu, akajitupa kitini na kujiegemeza akionekana kusawajika uso kwa mawazo ya dharula yaliyomkuta.
* * *
SOMALIA
Katika Jiji la Mogadishu, ndani ya hoteli kubwa ya kisasa, Jaffery Bakhari alikuwa na kikao kizito kilichojumuisha watu wengine kama watatu hivi ukiachana na vijana wake watiifu. Dhumuni la kikao hiki lilikuwa ni kujadili musatakabali mzima wa kampeni yao.
“Tumekwama! Labda niseme hivyo,” Jaffer akawaambia wenzake.
“Gupter alituhakikishia kuwa kila kitu kitakwenda sawa, sasa nini kimetokea?” Mjumbe mwingine akauliza swali lakini hakuna aliyetoa jibu.
“Anyway, kampeni yetu haiwezi kusitishwa, itaendelea, cha muhimu ni kuiongezea muda. Kwa kuwa tulishawaangusha wawili, wakabaki wawili, nimeongeza mwingine na huyu ndiye hasa amekuwa mwiba kuliko nilivyotegemea,” Jaffer akasema.
“Nani?”
“Rais wa Tanzania. Mambo yote yameanza kuharibikia kwake, nimemweka kwenye orodha na kumpa kazi Gupter mwenyewe,” akawaambia swahiba zake nao wakabaki kutikisa vichwa juu chini.
“Kwa hiyo kutangaza uhuru wa Somalia ya Kusini hakutaweza kuwa kama tulivyopanga, sivyo?” akauliza mzee mmoja mwenye nywele nyeupe kuanzia kichwani mpaka kidevuni. Afya yake ilionekana njema kipesa ijapokuwa alikuwa akitembezwa katika kitimwendo.
“Tunahitaji uhuru wa Somalia ya Kusini haraka iwezekanavyo,” mjumbe mwingine akaongeza, “hatuwezi kubadili taratibu zet bali tuwaambie tuliowapa kazi kuwa tunahitaji mpaka kufiikia tarehe hii iwekama tulivyopanga hata kama ni kuwaua wote kwa siku moja sawa tu, wataomboleza na baadae watatulia sisi tutaipata nchi yetu,” akasema tena.
Kikao kilikuwa kirefu lakini mwisho wa yote walifikia muafaka na kukubaliana kumuondoa kwenye orodha yule wa Tanzania.
“Wakikataa kutupatia nchi yetu kikatiba basi jeshi letu litaingia katika mapambano mpaka tutakapoikomboa,” Yule mzee akasema tena na wote wakaafiki.
“Lakini hawa Watanzania lazima tuwatazame kwa jicho la pekee maana wametuharibia kabisa mpango…”
Baada ya saa kama tano hivi kupita, kikao kikamalizika na kupangwa tena pindi kazi ikikamilika. Watu hawa watatu wenye unasaba fulani walijiunga na kuwekeza pesa nyingi kwa minajiri ya kuikomboa ardhi ya Somalia ya Kusini kwa madai kuwa ni mali ya babu zao. Kutokana na hilo walipanda mbegu miongoni mwa watu wazawa wa upande huo kuwatenga na kuwanyanyasa wale wenye asili ya Kaskazini. Hali hii ikaleta mapigano ya wenyewe kwa wenyewe mpaka Umoja wa Nchi za Afrika ukaamua kuingilia kati. Viongozi wengi wakapiga kelele juu ya hali hiyo hasa walipogundua kuwa wa-Kusini hao wanataka ardhi yao na kujitenga na Kaskazini.
Tangu waanze harakati hizi, wajumbe hawa wa juu kabisa wamekutana mara tatu tu, na wao ndiyo huwa na maamuzi ya mwisho, hiki kifanyike na hiki kisifanyike. Mara hii walikataa kabisa kubadili muda wa kutangaza uhuru wa nchi yao mpya. Kama pesa kwao hazikuwa tatizo, waliwekeza na kuwekeza, tayari walikwishapanga serikali, wakaunda jeshi na kubakisha tu kutangaza uhuru, hata maboksi yaliyojaa bendera mpya yalikwishawasili.
“Kumbukeni, tuna miezi mitatu tu, wakatae au wakubali, na wakitaka usalama wakubali, wakitaka damu imwagike wakatae,” Jaffer akamaliza na kuagana na wenzake na kujihakikishia kuimaliza kazi iliyobaki kwa miezi hiyo miwili.
* * *
DAR ES SALAAM
USIKU huo huo, Kamanda Amata alikuwa bize kitandani na mpenzi wake Gina, kilichokuwa kikiendelea hapo sina haja ya kukwambia. Hata kama ungesikia miguno ungeelewa maana yake ni nini. Kila mmoja alikuwa akimwonesha ufundi na utundu mwenzi wake. Baada ya muda wa kutosha wa burudani hiyo kila mmoja akabaki hoi.
“Hapo sasa tumeagana,” Gina akamwambia Amata.
“Umefurahi?”
“Siyo kufurahi tu, nimeridhika pia, yaani hata ukikaa huko mwaka mmoja mi sina hamu kabisa,” akasema.
“Haya bwana!” Amata akajibu na kukurupuka kitandani, akaketi na kuegemea besela la kitanda.
“Gina, unamwamini Mungu?”
“Yes!”
“Uniombee, maana kila nikifikiria hii safari yangu moyo wangu unazizima kwa woga,”
“Usihofu Amata, utakwenda na utarudi ninaamini hivyo…” Gina akamweleza.
“Aaaaa sijui, nahisi kama hii ni safari yangu ya mwisho….”
“Usiseme hivyo dear, hatari ngapi umepona, itakuwa hii? Si mimi tu wala Madam S, ila Watanzania wote wanakuombea, wanajua kuwa u mtetezi wao hata kama hawajawahi kukuona,” Gina akamfariji kwa maneno matamu.
Kamanda, akanyanyuka na kuliendea kabati kubwa la vipodozi ambalo katikati lilikuwa na kioo kirefu.
“This is Kamanda Amata, Amata Ric, TSA 1, nahisi kabisa kuwa muda si mrefu nitakiacha cheo hichi…”
“We unaongea maneno gani leo?” Gina akang’aka na kuinuka kumfuata Amata pale pale aliposimama.
“Usiwaze, go and kill them all… nauamini mkono wako,” akampet-pet na kisha kumrudisha kitandani na kuendelea na burudani zao.

SAA SITA MCHANA
Siku iliyofuata
Gina aliegesha gari nje ya Uwanja wa Ndege wa Julius Nyerere, kutoka ndani ya gari hilo akashuka Kamanda Amata na kufuatiwa na Chiba. Gina alipotoka garini, wote watatu wakaongozana na kuingia ndani uwanja huo sehemu ya kuondokea na kuhakikisha wamemwacha Amata akiwa tayari ameshauvuka mlango wa ndege na kuingia ndani. Mara baada ya kuupunga mkono wa kwaheri, Gina akajikuta akiangusha machozi.
“Unalia nini?” Chiba akamuuliza.
“Ingependeza ningekwenda na Amata…” akajibu
“Hapana, hiyo kazi si levo yako mwache yeye aende na wewe utabaki hapa,” Chiba akamwambia huku akimshika mkono na kutoka naye nje mpaka kwenye gari lao. Ndani ya gari Chiba akaketi nyuma ya usukani kwa maana alijua wazi kuwa mwanadada huyo hawezi tena kufanya kazi hiyo kwani bado alikuwa akilia kwa vikwifukwifu.

IKULU YA TANZANIA
Wakati yote hayo yakiendelea, Madam S alikuwa na mazungumzo ya falagha na Mkuu wan chi ndani ya jingo tukufu la Ikulu ya Tanzania ambapo ndipo ofisi na makazi ya Rais. Hakukuwa na na lingine linalozungumzwa zaidi ya mkakati wa kuwasaka Gupter na wenzake kama ambavyo Mwenyekiti wa AU amewataka kufanya hivyo.
“Unaamini peke yake anaweza?” Rais akamuuliza Madam S.
“Kwani ni mara yakwanza kwa yeye kufanya kazi kama hii?” Madam naye akauliza swali.
“Aaaa noh! Ni wewe unayewaju vijana wako vyema, si mimi…”
“Mpaka sasa, kazi imeshaanza, kitendo cha kuwapotezea malengo yao na kushindwa kumuua mlengwa, tayari ni kazi kubwa, kwa vyovyote watakuwa wameshtuka na wanahitaji kujipanga upya,” Madam akasema, “kwa upande wa Angola keshagundua mpaka ni nani anayemtilia shaka kuwa amehusika kwa namna moja au nyingine kutimiza mauaji yale…”
“…alikwenda Angola?”
“Ndiyo, mbona karudi jana tu!” akajibu
“Na huko unasema – wapi sijui wapi…”
“Sierra Leone…”
“Yes!”
“Yaani tunavyoongea tayari yupo hewani…”
“Good ndiyo maana nakupenda, yaani unajua kupanga mambo yako mwenyewe…”
Mazungumzo, mikakati, vikapangwa ndani ya jengo hilo, Mkuu wa Nchi akakubaliana na Madam S juu ya maswala mengi ya kusalama nchini. Akapokea mapendekezo ya mabadiliko na mambo mengine mengi. Saa tisa mchana wakamaliza kikao hicho ‘nyeti’ na kila mmoja kurudi katika majukumu yake.
* * *

WATERLOO
MARTIN Gupter alizinduka usingizini, akaketi kitandani kwa dakika kadhaa kasha akachukua simu yake iliyokuwa juu ya mezxa ndogo na kuiangalia kama kuna ujumbe au mwito wowote uliofika. Hakuwa mbali na hisia zake kwani alama ya bahasha ilikuwa ikiwakawaka juu ya kioo cha simu hiyo kubwa. Akaifungua na kuusoma ujumbe huo, mara baada ya hapo akahisi ubaridi ukimpenya kuanzia utosini mpaka unyayoni, akainuka na kuelekea sebuleni ambako aliwakuta Fredy na Amanda wameketi sebuleni wakiangalia TV.
“Jamani, kumekucha!” Martin akawaambia.
Amanda na Fredy wakashtuka na kumtazama Martin, “Nini tena?” akauliza mwanamke huyo.
“Kuna mgeni anaingia usiku huu…”
“Sure?”
“Yes, nimepata ujumbe kutoka Dar, hivyo hatuna budi kutrace, hatutakiwi kumpa nafasi kabisa, maadam kaja, nataka afie kwenye kaburi la pamoja,” Martin akasema, Fredy na Amanda wakatazamana kwa sekunde kadhaa.
“Hakikisheni mnamtia mkononi kabla hajapumua katika Jiji la Free Town,” akaongeza na kuwaonesha picha katika simu yake.
“Ni huyu!?”
“Shenzi sana huyu, huyu ndiye kaharibu mpango wetu kule Tanzania, shetani mkubwa, naenda mwenyewe…” Fredy akasema huku akinyanyuka tayari kuondoka, Amanda naye akafuatia.
“Yaani we tulia, tunaenda kumleta, ndege gani wanasema?”
“Ethiopian Airline, inaingia saa sita usiku huu, mna saa kama mbili hivi,” Martin akawaambia.
“Usijali tunamuwahi na tunakuja naye hapa!” Amanda akaongeza kusema wakati akijiweka sawa kwa safari. Nusu saa iliyofuatia, Amanda na Fredy walikuwa tayari barabarani kuelekea Jijini Free Town, m
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom