indundidotcom
JF-Expert Member
- Mar 4, 2017
- 229
- 226
Weka tena mkuu
Mkuu Kulubule umeingia chaka, njoo chacha utumwagie vituzMwali anaenda Croatia na sivinginevyo
Aseee njoo udhihirishe hii kauluMwali anaenda Croatia na sivinginevyo
Mmmmmh! Mimi nilidhani kuwa kwa kuwa Timu yetu tuliyokuwa tunaishabikia imefungwa then ungeweka vipande ving zaidi ili tujisahaulishe kuhusu mpira.......MAGNUM22
Sehemu 12
Sasa nahitaji msaada wa jambo moja tu kutoka kwako…” akamwambia Jerry.
“Sema, na tutasaidiana kumtia mkononi mshenzi huyu!”
Kamanda Amata akatoa picha ya mwanamke wa Kizungu, akaiweka mezani, “katika tukio hilo, ulimwona mtu huyu ama anayefanana au mwanamke tu yoyote wa kizungu kama si akipita basi akitazama kinachoendelea au chochote kile?” Amata akauliza.
Jerry hakujibu, akaitazama ile picha kwa makini sana, kisha akamtazama tena Amata, wakatazamana, “ninamkumbuka hata kama ni miezi mine imepita, huyu mwanamke asubuhi ile, alikuwa akipita anafanya mazoezi ya jogging, nikamzuia na kumtaka apite upande mwingine, akatii wala hakuwa na ubishi, ndiyo ni huyu ama pacha wake, ila wanashahabiana,” akamwambia.
Kamanda Amata akachukua ile picha na kile kijimfuko akavirudisha kotini mwake.
“Spark! Vipi?” Costa akauliza.
Amata hakujibu, akamtazama Jerry, “Jerry, you people, mnafuga magaidi ilhali mnakaa na kunywa nayo,” akasema. Jerry akajikuta hana cha kusema akaendelea kumkodolea macho Amata.
“Kivipi?” Costa akauliza.
“Jerry, unamjua huyu?” akamuuliza akimaanisha kama anamjua Costantine.
“Yes, Costantine ni rafiki sana na mimi, tumefanya kazi hizi pamoja mara nyingi ila yeye sasa ni mpelelezi wa kujitegemea huko Costa Rica, alikuja hapa kwa minajiri ya kumsaka huyu mshenzi, na ni yeye aliyenigutusha mimi kuwa kuna uwezekano wa kutukia tukio la mauaji ya kiongozi hapa. Mara baada ya kunijuza nikalifikisha kunakohusika tukaanza kulifanyia kazi. Siku mbili kabla ya tukio sikumwona Costa, nikamtafuta sana pasi na mafanikio, nimeshtuka sana kumwona leo kwani nilikwishajua kuwa amekufa,” akaeleza.
“Washa TV,” Amata akamwambia Jerry, naye akafanya hivyo na habari waliyoikuta ni kuhusu Kisiwa cha Ilha Da Canzaga.
“What?” Jerry akajikuta anapigwa na butwaa baada kushuhudia moto mkubwa huko kisiwani huku jitihada za kuuzima zikiendelea.
“Samahani, naweza kwenda toilet?” Amata akaomba na kuoneshwa ni wapi choo kilipo. Akainuka na kuwaacha wawili hao wakiwa wamekodolea macho luninga, akafungua mlango na kuufunga.
Nusu saa ikapita, Amata hakurudi sebuleni, “hey! Mr Spark!?” akamuuliza Costa. Costa yeye hakujibu ila aliinuka na kuelekea chooni, akatikisa mlango, uko wazi, akausukuma huku akiita, hakuna mtu, kwenye tanki la maji ya kuflashi kuliandikwa kwa maka peni nyekundu.
Fernandes Perreira ndiye anayewasaliti! Costa akamwita Jerry naye akaja na kushuhudia maneno hayo.
“Ameondoka!” Jerry akasema.
* * *
MSAKO MKALI wa kumtia mkononi Amata ukaanzishwa ndani ya Jiji la Luanda, Fernandes Perreira mara baada ya jingo lake kule katika Kisiwa cha Ilha Da Canzaga kulipuliwa akajua tu hakuna mwingine zaidi ya mgeni wake aliyemtembelea na kutaka kupatiwa kabrasha la ‘SECRET ASSASSINATION’. Taarifa ikafika kwenye vyombo vya usalama na kazi ikaanza, akamatwe afikishwe panapohusika.
Fernandes Perreira alikuwa akizunguka huku na kule, nywele zimemsimama, hataki kungea na yoyote zaidi ya kufuta jasho tu, alichanganyikiwa, simu zilipigwa, akapokea, akaongea maneno machache tu, akakata. Wageni wengi, matajiri kwa viongozi wa serikali walimiminika kumpa pole kwa tukio hilo na baadhi yao ndiyo wakapata jazba ya kutaka mtu huyo asakwe mara moja.
Wakati yote hayo yakijiri, Kamanda Amata alikuwa akimlipa pesa dereva taksi wake, tayari kwa safari ya kurudi Tanzania, alijua kwa vyovyote lazima atakuwa hatarini tu, wakaagana na yule mzee huku akiwa amemwachia pesa nyingi tu. Kamanda Amata, akaingia katika ofisi ya ndege binafsi, bahati nzuri akapata ndege na kukodi, nusu saa baadae akaiacha Angola na kurejea Tanzania akiwa tayari keshapata jibu la moja na moja ni ngapi.
Kwakuwa timu yangu imefungwa mle nusu dozi