Riwaya magnum22

MAGNAM22

Sehemu 10

Amata akazungumza kwa makini sana.
“Umenena Amata, wanaweza kuwa Kenya tena Mombasa…”
“Yeah! Chiba nakuamini sana, ihifadhi hii info, mi naenda kwanza Kunduchi nikaanzie kazi huko,” Amata akamwambia swahiba wake huku akiinuka tayari kwa safari.

KUNDUCHI RESORT
Kamanda Ama akawasili katika hoteli hiyo na kuegesha gari mahala pake. Hatua zake ndefu ndefu zikamfikisha katika kaunta ya hoteli hiyo nzuri nay a kisasa. Mapokezi hapo akakaribishwa na wahudumu wa wili wa kike wenye tabasamu la bashasha. Akawasabahi na moja kwa moja akamuulizia kijana yule anayemtaka. Haikuchukua muda kuitiwa kwani alikuwa upande mwingine wa hoteli hiyo. Kijana huyu mwembaba, mrefu mwenye tabasamu na maneno ya kuvutia na utani uso kifani alikutana uso kwa uso na Amata.
“Naitwa Justus!” amata akajitambulisha, “tunaweza kuongea kidogo?” akamuuliza.
“Bila shaka kaka yangu, kwanza kabisa mi naitwa Umar,” akajitambulisha kwa jina moja tu. Kisha wakavuta hatua hadi karibu na bwawa kubwa la kuogelea.
“Mr Umar, mimi ni mgeni hapa kwenu, na shida yangu kubwa ni kuwa namtafuta mtu huyu, je umewahi kumuona hapa?” akamwonesha picha ya Amanda.
“Aaaaaaahhhhhh!!!! Huyu?” Umar kama kawaida yake akachanusha tabasamu pana usoni pake.
“Huyu mwanamke kanishinda, na wewe upo kwenye listi?” Umar akauliza. Kamanda Amata akabaki na kigugumizi kwa sekunde kadhaa akijiuliza kichwani mwake.
“Listi ya nini?”
“Aaaaaa yule mzungu ni mtalii wa ngono, mpaka vigogo hapa wamekuja sana kumgonga,” akaeleza.
“Vigogo?”
“Ee yule nani yule alikuwa balozi huko Emirate huko…”
“Aaaa Balozi Bailhani?”
“Yes!”
“ Achana na hayo, mi nataka nijue huyu mwanamke yuko wapi?” akamuuliza.
“Alikaa hapa kama siku tatu hivi…”
“ Sikia Umar, yule mwanamke kaingia nchini bila kibali, tunamtafuta…”
“Ah mzee we kumbe ni imigresheni?”
Mazungumzo kati ya wawili hawa yakachukua kama nusu saa hivi, Umar akaeleza mengi anayoyajua juu ya mwanamke huyo, nyendo zake na watu kadhaa aliokuwa nao karibu. Kwa namna moja kwa Amata mazungumzo haya yalimpa faida lakini pia yakamwachia maswali; je ni kweli alikuwa akifanya mapenzi na watu hao aliyotajiwa au kulikuwa na jambo lingine, hakupata jibu mara moja kwa kuwa huko chumbani waikuwa wao wawili tu yaani mwanamke huyo na mgeni wake.
Hata Balozi Bailhan? Akajiuliza.
“Kwa hiyo amecheck out lini?”
“Mh huyu katoroka, hajatuaga wala nini yaani hata sisi hapa hatuelewi kaondoka ondoka vipi,” Umar akaeleza.
“Asante kwa maelezo yako, umenisaidia sana, nitakutafuta wakati mwingine hata tupate kinywaji kidogo,” akamtania.
“Usijali kaka, hata wewe unakaribishwa hapa kupumzika na shemella wetu,” naye akamtania, wakaagana wakipeana mikono kisha Amata akampa kadi kazi yake.
“Kwa lolote, waweza kunipigia,” akamwambia.
“Asante,” akashukuru kisha kila mmoja akachukua njia yake.
Ndani ya gari lake kamanda Amata akachukua kijitabu chake kidogo na kuandika jina Bailhani akapiga mstari na kuunganisha na jina bandia la mwanamke yule ambaye mpaka dakika hiyo hawakupata jina halisi. Kisha akaondosha gari lake na kurudi mjini.
* * *
Amata alikutana na Chiba na Gina mchana huo kwa chakula cha mchana katika hoteli ya Double Tree. Pamoja na chakula hicho mazungumzo ya hapa na pale yalikuwa yakiendelea mahala hapo.
“Hujanipa mchapo wa Kunduchi,” Chiba akamwambia Amata.
“Huko poa tu, yule kijana kanipa umbeya wa kutosha, lakini katika mazungumzo yetu na yeye nimeweka akilini jina moja tu na nataka nilifanyie kazi…”
“Jina gani asee?” Chiba akauliza.
“Balozi Bailhani. Inasemekana alikuwa akimwona mara kadhaa akija pale na mwenyeji wake ni huyu mwanamke, jamaa anasema kuwa balozi huyo alikuwa anakula mzigo,” Amata akasema.
“Mmmm labda, lakini swali ni kwamba walikutana vipi au walifahamiana wapi?” Chiba akamalizia.
“Siyo la kuliacha hilo ee, Gina mama, kazi yako hiyo!” Amata akasema.
“Eeeee muda wa kula bwana, ngoja nimalize ndo unipe kazi,” Gina akalalama.
“Haya Malkia!” Amata akajibu na chakula kikaendelea kuliwa huku mazungumzo mengine yakiendelea.
“Nahitaji kwenda Angola,” akawaambia.
“Kumekucha….” Gina akadakia.
“Na makucha yake…” Chiba naye akamalizia.
“Ee lazima tujue ulinganifu wa mambo haya ili nijue kama naingia kazini kumsaka mshenzi huyu basi nimsake kwa nguvu zote,” akawaambia.
“Sure!” Chiba akaunga mkono.
“Kuna vitu nahitaji kuvijua kutoka Angola, nikivipata hivyo nikioanisha na Ivory Coast kazi imeisha… hayawani hawa…. Umesema wapo watatu ee…”
“Ee ni watatu,”
“Lazima wapatikane iwe kwa jasho au machozi…” Amata akawaambia wakti akimalizia chakula chake.
“Safari lini?” Gina akauliza.
“Ikiwezekana kesho niwe Luanda na Mungu akipenda kesho hiyo hiyo nigeuke kurudi Dar…” akawaambia.
“Amata, ukiingia Luanda nakuhakikishia hutopenda kurudi Dar badala yake utaendelea kwenda Ivory Coast,” Chiba akamwambia.
“Ikibidi, itakuwa hivyo,”
“Basi kabla hujaondoka twende shamba nikakufanyie identification, sina imani sana na kazi ya safari hii maana tunamuwinda muwindaji,” Chiba akamwambia. Wote wakatoka na kuingia garini, safari ikaanza kuelekea Shamba huku wakimuacha Gina akifanya utaratibu wa usafiri wa Kamanda wa usiku huo.

SHAMBA
Wakiwa katika Safe House au Shamba kama inavyojulikana, Kamanda Amata na Chiba walikuwa katika chumba maalum chenya mitambo anuai.
“Natakiwa kukuwekea identification Chip, ili kila utakapokwenda nikuone na iwe rahisi kukufuatilia…” Chiba akamwambia Amata.
“Aaaa ila haka kadude kanauma asee,”
“Ni kweli lakini hatuna jinsi, safari hii nitakuweka pajani,” China akamwambia Amata huku akifungua mkoba maaumu wenye mashine ya kubeba kifaa hicho. Ni kitu kama bunduki au sijui tuite bastola, kazi yake kubwa ni kuweka mwilini mwa mwanadamu micro chip inayowasiliwana kwa satelite na kuonesha ni wapi mtu huyo alipo kwa wakati huo. Kamanda Amata akatulia na Chiba akafanya hivyo kama ambavyo anafanya siku zote.
“Assssss ah! Shit!” Amata akapiga kite cha maumivu wakati chip hiyo ikisukumwa ndani kwa nguvu na mashine ile.
“Weka mkono wako hapa,” Chiba akamwambia. Naye akaweka mkono katika kitu kama bangili kubwa kilichounganishwa na mashine hiyo, kisha Chiba akatazama kwenye kompyuta yake na kujaribu kuviunganisha vitu hivyo viwili.
“Aaaaaa hapo sawa, sasa nakuona mubashara, upo Gezaulole, Kigamboni,” Chiba akasema na kuanza kufunga mkoba wake. Si kwamba alikuwa anamwona kama alivyo, bali alimwona kwa alama ya dot nyekundu inayowakawaka katika ramani na kuonesha ulipo.

LUANDA - ANGOLA
KATIKA UWANJA wa ndege wa kimataifa wa Quatro de Fevereiro, Kusini kabisa mwa Mji Mkuu wa Angola, Luanda, Kamanda Amata aliwasili na ndege ya shirika la Kenya ‘Kenya Airways’. Akainua uso wake na kutazama anga la nchi hiyo, moyo wake ukamkaribisha katika jiji hilo, la kupendeza kwa macho na fahari zake.
“Boa noite senhor!” (habari za jioni mheshimiwa) akasikia salamu kutoka nyuma yake, Amata akageuka na kugongana macho na mtu mmoja, mwembaba wa wastani, ana nywele nyingi zilizochanganika na mvi, ndevu za wastani zilikipendezesha kidevu chake.
“Boa noite, como você está?” (nzuri hujambo?) akamjibu salamu yake, kisha wakapeana mikono kama kawaida ya Waafrika kunesha kwamaba sisi ni kitu kimoja.
“Bem-vindo em Luanda, você precisa de um imposto?” (Karibu Luanda, unahitaji huduma ya taksi?) yule mzee akamkaribisha Amata na kumtupia swali. Kwa haraka haraka Kamanda Amata akamsoma machoni na kumwelewa mara moja mzee huyo, hakuwa na mawaa yoyote.
“Sim! Preciso de um imposto, você pode me levar para o hotel Alvalade?” (Ndiyo, ninahitaji taksi, unaweza kunipeleka Hoteli ya Alvalade?) akakubali na kumuuliza huku tayari wakianza kunyayua mguu kwa hatua ya kwanza kuelekea kwneye maegesho ya uwanja huo.
“Claro que eu posso!” (Bila shaka ninaweza!) yule mzee akajibu na wote wakaendelea kutembea bila kuongea chochote mpaka katika gari hilo. Lilikuwa gari la kawaida sana, si zuri la kutisha bali tunaweza kuliita la kawaida.
“Dakika ngapi tutakuwa pale?” akamuuliza kwa Kireno cha kubabaisha.
“Kama kumi au chini ya hapo kama hakutakuwa na msongamano barabarani…”
“Na hapa ni kama kwetu Dar es salaam?” Amata akamuuliza.
“Oh unatokea Dar es salaam, Tanzania? Ninapenda sana nchi hiyo na ninapenda kufika kabla sijafa…” yule mzee akaongea kwa furaha sana baada ya kujua kuwa mwenyeji wake anaipenda nchi yake. Gari lile likawashwa kwa shida kidogo likagoma kuwaka.
“Ossshhhh!!! Matatizo yameanza!” akalalama.
“Vipi, bovu?” Amata akauliza.
“Aaaaa vijana hapa wanatumia sana uchawi, hawataki mimi nipate pesa,” akaendelea kulalamika.
“Usiamini uchawi, gari lako ni bovu, mi nasukuma we uliwashe!” Amata akamwambia na kutelemka chini, akaenda nyuma ya gari hilo na kulisukuma peke yake, sekunde chache likawaka, akarudi na kuketi kwenye kiti cha abiria.
“Tunaweza kwenda!” akamwambia na yule mzee akatia gia ya kwanza na kuondoka zake kupitia Barabara ya Revolução de Outubro na kunyoosha moja kwa moja mpaka kwenye mzunguko na kuchukua ile Barabara ya Cmte Gika. Dakika chahe tu kweli waliingia katika hoteli hiyo kubwa ya nyote tano. Kamanda Amata akachomo noti mbili za Kwanza 5000 kila moja. Mzee yule badala ya kuzipokea akabaki akitetema mikono.

“No, ninyingi sana hizi kwa sfari ya kilomiti tatu,” akasema.
“Najua, ninakupa kwa sababu nataka umpelekee chakula kizuri mama yangu leo, usijali kwani kesho nitakuhitaji asubuhi hapa,” Amata akamwambia ma mzee yule akampatia mgeni wake kadi kazi yake kwa minajiri ya mawasiliano.

Kamanda Amata akavuta kijibegi chake na kuingia ndani ya hoteli hiyo ya kisasa inayoonesha kuwa na starehe zote za msingi ambazo mwanadamu angehitaji.
“Karibu Alvalade Hotel, karibu Luanda!” mwanadada mrembo aliyekuwa ndani ya suti nadhifu kabisa alimkaribisha kijana huyu mtanashati, mwenye siha ya kiume na mwili uliojengeka kimazoezi kwa wastani. Kwa kumtupia jicho alihisi kama amekutana na kijana wa ndoto zake, akajikuta akikosa neno na kubaki kumwemwesa midomo yake.

“Signorita!” Amata akaita huku mezani akiwa tayari ameweka karatasi inayoonesha booking yake na kadipesa yake aina ya MasterCard.

“Oooh! Ulikwsihaweka booking,” akasema mwanadada yule huku akichukua ile karatasi na kugeukia upande wa kompyuta yake. Dakika kama mbili baadae tayari akawa na kadifungushi kwa ajili kufungua mlango wa chumba chake.

“Twende nikuoneshe chumba chako!” yule mwanadada akamwambia Amata na kutoka upande wa pili, kisha wakafuatana na kuingia kwenye lifti na kupanda mpaka ghorofa ya saba, wakatoka kwenye lifti na kuingia chumba namba 11A.

“Hiki ni chumba chako Mr Spark!” akamwambia Amata.
“Aaaanh hutaki kunionesha zaidi?”
“Kukuonesha nini?” yule mwanadada akajibu huku akiondoka zake na kumwachia Amata mtikisiko wa nyama za nyuma. Kama kuumbwa aliumbwa, mfupi, mwenye unene wa wastani, aliyebinuka kiunoni kuja chini, na fundi aliyeishona nguo aliyoivaa unaweza kusema kuwa kazaliwa nayo. Kabla hajaingia katika lifti akageuka nyuma na kutazama alipotoka, akagongana macho na Amata ambaye bado alikuwa kasimama nje ya mlango huo akimsindikiza kwa macho. Kamanda Amata akachukua mfukoni kadi kazi na kuiangusha sakafuni, kisha akapachika kadifungushi yake katika ushoroba mdogo wa kitasa cha mlango huo, kisha akabonyeza namba fulani na kufungua. Akaingia ndani kuufunga mlango nyuma yake, mara baada ya kuhakikisha usalama wa chumba hicho akavua nguo zake na kutwaa vazi la kuvalia na kujibwaga kitandani, haikuchukua muda akapitiwa na usingizi. Ni mara chache sana kwa Kamanda Amata kuingia hotelini na kupatwa na usingizi haraka kwa kuwa daima alikuwa akija kwa shari hivyo ama ulala kitini kwa tahadhari au kwa mang’amung’amu kwa kuwa hujiweka tayari kwa lolote. Lakini safari hii kwake iikuwa kama picnic tu ambayo hata mwili wake ulijikuta unataka kupumzika zaidi.

* * *
Asubuhi ya siku iliyofuata ilimkuta Amata katika gym ndani hoteli hiyo. Alikuwa akifanya mazoezi makali mpaka wengine walikuwa wakimshangaa lakini yeye hakujali bali aliendelea na mazoezi yake na kuhakikisha mwili umetona jasho la kutosha. Akaschukua taulo lake na kujifutafuta taratibu huku akimshukuru kiongozi wa darasa hilo la mazoezi.

Ndani ya chumba chake, aliingia maliwato na kujimwagia maji kisha akarudi kuvaa nguo zake maalumu za kazi, yaani suti safi aliyoinunua mara tu alipofika uwanja wa ndege wa Luanda. Akajitazama kwenye kioo na kugeuka huku na huko, waaaaaoh, amependeza mno. Akauvuta mkoba wake na kufungua vijifuko vya siri, akatoa baadhi ya silaha zake anazozijua yeye na kuzipachika katika mwilia wake, bastola yake aina ya PPK na kuipachika mahala pake. Akahakikisha yupo tayari kuondoka, akiwa anamalizia kuiweka sawa tai yake akasikia mlango ukigongwa kisha ukasukumwa na mtu ambaye hakumtegemea akaingia ndani akiwa na toroli yenye kifungua kinywa juu yake. Alipogeuka kumtazama akamtambua mwanadada yule yule aliyempokea jana na kumwongoza chumbani.

“Wewe ni Waitress au receptionist?” akamtupia swali lakini macho yake yote yalikuwa yakiangali kifua kizuri cha mwanadada huyo kilichopambwa kwa matiti ya saizi ya kati.
“Yote mawili, vipi kwani?”
“Nashangaa unaleta kifungua kinywa, isitoshe sikuagiza room service!” Amata akamwambia mrembo yule.
“Nimeamua nikuletee maana jana nilikuona umechoka sana, au hupendi?” akamwambi huku aking’atang’ata ulimi wake. Kamanda Amata akamtazama kwa jicho la kiu, kiu ya penzi.
“Sina muda wa kunywa chai!” akamwambia muhudumu yule.
“Ila una muda wa nini?”
“Wa kuondoka!” alipojibu hayo tayari mwanamke yule alikuwa amemaliza kazi ya kuandaa kifungua kinywa mezani. Akafungua mlango na kuondoka zake huku akimwacha Amata anatoa macho tu. Mara baada ya kuondoka mwanamke yule, Amata akatoka chumbani na kuchukua njia nyingine, akatelemka hadi chini huku tayari simu yake ikiwa sikioni kwa mawasiliano. Ijapokuwa hata yeye alimhusudu sana mwanamke huyo kwa siku ya kwanza tu kama ilivyokuwa kwa mhudumu yule lakini Amata hakutaka kuonesha udhaifu bali alitumia uanaume wake kuamua kuondoka huku roho ikitamani na kuijutia nafasi hiyo.

Katika maegesho tayari yule mzee wa siku ya jana alikuwa keshafika na kuegesha gari lake vizuri akilifutafuta ili ling’ae.
“Mzee!” Amata akaita kwa kutumia lugha ya Kireno. Alipolifikia gari akafungua mlango wa abiria na kuketi tayari kwa safari.
“Wapi asubuhi hii?”
“Condominio Bela Vista!” akamtajia mahala anapotaka kufika. Mzee yule akawasha gari, bila shida safari hii likakubali na kuondoka eneo hilo. Iliwachukua dakika kama arobaini hivi kufika katika jingo hilo la kifahari sana ambalo kila mtu alikuwa akijua na kutambua kuwa ni sehemu ya biashara hasa ya matajiri kuja kupumzika ama kuzungumzia biashara zao au kuja na vimwana kupunguza mawazo ilhali wake zao wamewaaacha nyumbani.

“Nisubiri hapa, nakuja!” Amata akamwambia yule mzee na kulifuata jingo hilo. Suti aliyovaa na mkoba aliyoubeba vilishabihiana haswa na mahali anapongia.

“Karibu sana, tunaweza kukusaidia!?” akaulizwa na kijana mmoja aliyekuwa nyuma ya dawati hilo la maulizo.
“Ndiyo, naweza kuonana na Bwana Fernades Pereira?” akauliza.
“Una miadi naye?”
“Bila shaka!” akawajibu na kuwapa kikadi kidogo ambacho Madam S alimpatia kwa siri.
Dakika tatu baadae, akachukuliwa na msichana mrembo, kwa kumtazama tu mavazi yake akajua kuwa ni katibu muhtasi wa mtu huyo. Wakaongozana pasi na kuongea mpaka katika ofisi fulani kubwa sana. Ofisi hii iliyokuwa tupu kabisa isipokuwa meza kubwa na viti viwili tu, na juu ya meza hiyo kulikuwa na simu moja ya kizamanai sana lakini ilioneka bado mpya kabisa.

“Você precisa esperar aqui, o Sr. Pereira vai se juntar a você em breve!” (subiri hapa, Mr Pereira ataungana nawe muda si mrefu) mwanadada yule akamwambia. Na Kamanda Amata akasubiri kama alivyoamuriwa, yule msichana wa kadiri ya miaka ishirini na tano au thelathini hivi akapotelea katika moja ya milango mingi iliyozunguka ukumbi huo. Sekunde hiyo hiyo akasikia mlango wa nyuma yake ukifunguka, alipogeuka akakutana uso kwa uso na mtu mmoja mwenye umbo kubwa, Mwafrika aliyevali suti ya kawaida tu, kwa huku kwetu tungeiita Kaunda Suit.

“Karibu sana Mr. Spark!” yule jamaa akamkaribisha Amata huku akiketi kitini na kumtaka Amata naye afanye hivyo.

“Yes! Tuna dakika chache sana za mazungumzo kama kumi na tano hivi, karibu…” yule jamaa akamwambia Amata huku akimkazia macho usoni.

“Nami nina jambo moja la kuzungumza nawe…”
“Ndiyo!”
“Nimetumwa kutoka Tanzania…”
“Najua!”
“Mkoba huu…” akauweka mezani “unatakiwa unatakiwa ndani yake ikae taarifa ya mauaji ya Rais wa Angola yaliyotokea miezi kama minne iliyopita,” akamwambia.
“Kwani mimi ndo’ nilimuua?” Perreira akauliza.
“Siyo wewe!”
“Ila…”
“Inajulikana kwamba tafutishi yote ya mauaji hayo wewe unayo, na hata jengo lililotumika ni lako, hivyo bila shaka una kimojawapo ama taarifa ya mauaji au mpango wa mauaji…”

Perreira akashusha pumzi ndefu na kumtazama kijana huyu ambaye hakuwa anaonesha hata tabasamu usoni mwake.

“Nani kakutuma hizo habari za kipumbavu?” akamuuliza Amata.
“Haina haja kujua ni mambo mawili tu yanayotakiwa kuwamo ndani ya mkoba huu,” Amata akajibu. Yule bwana akajifikicha macho na kisha kuyarudisha kwa Amata na ndipo alipojikuta akitazamana na domo la bastola aina ya PPK.

“Katika jumba hili, mtu huwa haingii na bunduki, wewe umewezaje?” Perreira akamuuliza Amata.
“Ndiyo ujue kwamba jumba lako halina ulinzi kama unavyofikiria,” Amata akajibu.
“Ok, ukinambi nani kakutuma, mimi nitakupa utakacho, huwa sina shida na watu wa serikali ila nataka nijue nani kakutuma…”
“Nimetumwa na AU…”
“Addis Ababba…”
“Yes!”
“Ok, nifuate, ila bunduki yako ihifadhi vizuri,” Perreira akamwambia kisha
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom