FANANI MTENZI
Senior Member
- Jul 4, 2017
- 106
- 95
KOMBORA KIOTANI-1
Uwanja ulipambwa kwa tabasamu za wana nchiMagwaride kadhaa yameshapita kutoa heshma zao kwa mkuu wan chi aliyekuwa jukwaa kuu.Mavazi yaliyovaliwa hapa asilimia kubwa yalikuwa yakizalendo hasa kwa rangi zilizopo kwenye bendera ya taifa.Uzalendo ulitukuka baina ya taifa hili linalokumbuka siku ya uhuru wa taifa lao kutoka kwa wakoloni waliowatawala.Kiuhalisi taifa limeshapiga hatua kutoka kwa mkoloni.Kuimarika kiafya,elimu,ulinzi na mengine mengi.Lilikuwa taifa imara na linaendelea kuimarika japo kwa mapungufu kadhaa wa kadhaa.
Jeshi la taifa la KIOTA kwa sasa katika sherehe za uhuru lilikuwa linafanya mazoezi kuonesha wana nchi wake uimara na ukakamavu wa jeshi.Pia walikuwa wakimuhakikishia mkuu wan chi ulinzi uliotukuka.Vyama mbalimbali vya siasa vilikuwepo katika sherehe hii pamoja na viongozi wa kitaifa.Vilevile kulikuwa na mialiko ya mataifa ya kadhaa japo wengi wao walituma udhuru na kuleta wawakilishi wao katika uwanja wa taifa.Ulinzi ulikuwa umeimarishwa katika jiji kuu la nchi ambapo taifa lilikuwa linashuhudia maadhimisho haya.
Rais Kisusi akiwa ameketi meza kuu,pembeni yake alikuwepo mkuu wa majeshi upande mmoja na upande mwingine alifuata naibu rais wake na viongozi wengine.Waliteta na mkuu wa majeshi.
“Kinachofuata ni nini jeneral maana leo sijisikii vizuri sijui kwanini?”aliuliza rais Kisusi.
“Ni mwite daktari?”aliuliza jenerali Tindikali.
“Hapana aliniambia sina tatizo.”alijibu rais Kisusi.
“Itakuwa msongo wa mawazo mkuu.Usijali nchi ipo salama.”
“Na wasiwasi na uchaguzi ujao.Lakini sio kwa hilo ni kwamba roho inanienda mbio sana.”
“Kivipi mkuu?”
Walikuwa maswaiba wakuu tangu shuleni tofauti ni majukumu ya kazi lakini wote ni wazalendo wazawa wa taifa la Kiota walioamua kuitumikia nchi yao.
“Au ni vile majirani zako hawajaja?”
“Hapana Tindikali.”
“Au tuhairishe shughuli?’”
“No!Leo ni dhifa muhimu sana sidhani kama kuna haja ya mimi kuondoka ghafla.Ngoja niimalize then tutaondoka.Unajua file namba 13.14 linanitatiza sana kiasi nakosa Amani.”alisema rais Kisusi ambapo alipitisha kitambaa kufuta kijasho kilichokuwa kina msumbua.
“Lina ufumbuzi hakuna kidudu mtu atakayesumbua.”Alijibu jenerali Tindikali.Waligutushwa na mshereheshaji aliyekuwa akielezea makundi mbalimbali ya ulinzi yaliyokuwa yanafanya mazoezi.
“Halafu Mkuu kinachofuata ni Maonesho ya ndege mpya za kijeshi tulizo tengeneza.”
Rais alipitisha ulimi kwenye papi za midomo yake nakuachia tabasamu hafifu.Akaangalia juu kusubiri maonesho ya ndege.
“Ndege inaendeshwa na Kapteni Pilipili ya kwanza kabisa kufanya onesho lake.Inatoka makao ya Msanda.Mh RAIS unasikia sauti ikizizima uwanja mzima.Haya ni mafanikio chini ya utawala wako.Ni ndege yetu wenyewe MI fighter Jet ian uwezo wa kwenda kilomita mia tatu kwa saa.Ina beba makombora kwa kumshambulia adui.Kwa heshma mh rais Kaptein…”MC alikuwa anahutubia.
Kaptein Pilipili akiwa angani kuelekea uwanja wa taifa kuonesha ndege mbele ya rais wao.Alianza kuhisi mikono mkimtetemeka.Makao yakuongozea ndege yalikuwa yakiwasiliana naye kumpa maelekezo ya kipi cha kufanya.Lakini ghafla alipoingia kwenye anga la uwanja aliekeza ndege moja kwa moja kwenye meza kuu walimoketi Rais na watu wake.Halafu akabonyeza kitufe cha kuachia kombora lakini hakubonyeza la kuruhusu kombora kutoka bali mlango wa kombora ulibaki wazi.Na kwa kasi atakayoenda nayo mpaka kufika kwenye jukwaa halitakuwa limeanguka kutoka kwenye eneo lakuhifadhi bali kama ndege ikiwaka moto au kulipuka bila shaka kombora lingelipuka.Kasi yake ilikuwa ya sekunde.
“Mh Rais kaptein Pilipili ndo….”hata kabla hajamaliza tayari ndege ilipigiza kwa kasi kwenye jukwaa.Kishindo kizito kilikuwa kimejiri.Lakini wakati wa butwaa lile likiendelea kuna mlipuko mwingine ulitokea pale uwanjani!Mlipuko mzito.Moto ulipanda juu na moshi mzito kufuka.Kilio kilikuwa kimesikika kikubwa sana tena cha kuogofya kiasi watu walishtuka ambao hawakupatwa na mlipuko ule.Vikosi vya kijeshi vilivyokuwa pale uwanjani nakubahatika kukoswa na mlipuko ule vili taharuki kwa harka maana mshtuko uliotokea ni waaina yake.Vyombo vya habari kadhaa vilipoteza mawasiliano hasa kamera zilizokuwa karibu jukwaaani.Lakini kwa kamera zilizo mbali kidogo hazikupatwa na kadhaia hiyo.Mambo yote yalionekana mubashara kwenye vyombo vya habari.Taharuki iliyokuwepo katika taifa haikuwa na maeleoz!Nchi ya Kiota ilikuwa taabani.Na kwa haraka tu ilikuwa vigumu kujua ni wangapi walikuwa wamekumbwa na kadhia hii!Ilichukua muda kwa vyombo vya habari kuanza kutangaza kinachotokea uwanjani.Waliopo studio waliona kama ni sinema wana tazama lakini ukweli ni kwamba balaa kubwa lilikuwa limetokea.
Wakati simu zikipigwa maeneo mbalimbali huku vyombo vya ulinzi vikijitahidi kujua ni ktiu ganoi kimetokea hadi ndege ilyokuwa ikirushwa kwa maonesho ikapoteza mwelekeo nakuanguka jukwaa alimokuwamo Rais Kisusi.Jukwaa ambalo serikali nzima ilikuwemo!Ilikuwa maapema mno kubashiri tukio hili ambalo bichi sana!Nchi ya Kiota ilikuwa imesimama hakuna kilichosonga.Waliokuwa karibu na maeneo yale nje ya uwanja walianza kutimua ovyoo.Waliopo ndani walianza kutoka nje msongamano ambao ulisababisha purukushani hadi watu kubanwa chini nawengine kupoteza fahamu.
Taharuki!Taharuki kuu!
Taifa limetetemeshwa!Kiota imeanguka chini kwa kishindo!
****
Makao makuu ya jeshi!TRIANGLE
Meza kuu yahali ya hatari ilikaliwa na viongozi wa kijeshi waliokuwa wamebaki kambini.Kulikuwa taharuki.Hakuna kilichotulia kila mmoja aliongea lake.Simu ikipigwa huku na kule.
“Nimesema tuna tuna tangaza hali ya hatari nakuipeleka kwa kiwango cha DEFCON 3.”alisema kanali Rama.
“Hapana huna mamlaka yakupandisha hiyo amri.DEFCON 3 nikubwa sana wewe huoni ni mwenzetu ndokaangusha ndege.”alijibiwa na Major Kanda.
“Major huu siwakati wa mzaa Kiota imepigwa hatucheki na mtu vilevile nataka kujua ikulu nani anachukua napia nijue nani anajua hali ya rais na serikali nzima.Tukisubiri mambo yaendee kijinga tutapoteza nchi!Tuamue hapa hapa kufungulia vikosi vya kijeshi kuingia mtaani.Hivi.”
“wewe ni nani katika nchi uamuru upuuzi huuo!”
“Huna mamlaka hana mamlaka!”
“Pumbavu hujui lolote nimekufundisha kazi mimi.”
Kila mtu alikuwa na wasiwasi na hasira.Hakuna aliyejua ni uamuzi gani wakuchukua kwa wakati huo.Ilihitajika busara na amani ya hali ya juu.Nchi ilikuwa imetikiswa kwa pigo kubwa kuliko yote pona ya watu ilikuwa na wakati mgumu usio na maelezo yakuridhisha.Hali ilikuwa tete.Hakuna aliyemuamini mwingine.Mfumo mzima wa utawala uliingia dosari ya ajabu.Utamwamini nani?Aliyetekeleza mauaji ni nani?Kwa dhamira gani?Na mpango upi?Ni ajali?Lilikuwa swali lililoshibisha meza nzima ya eneo lile.
“Jamani hebu tutulie natuwe na uvumilivu wa hali ya juu.Nchi nzima inahitaji amani.”alisema moja ya wazee wa jeshi aliye na umri mkubwa.Ni mstaafu lakini mtu mwenye busara alishashinda medani kadhaa kwa juhudi zake jeshini pamoja na ushirikiano mbalimbali alioutoa jeshini.Vyeo Alisha vipata.Pamoja na mambo mengine,alikuwa mzalendo kwa taifa lake huru.Alilipenda.Alilijali nakulithamini kama kwa uzalendo uliotukuka.Mwili wake wenye ngozi iliyozeeka,sharubu zenye uzito halafu nyeupe pamoja na pua yenye mchongo ilimpa sura ya busara.Utuuzima dawa.
“Ni sawa nchi imepigwa pigo kuu.Hii ni ajali mbaya…”kabla hajamaliza alivamiwa kwa kauli zenye utata.
“Sio ajali!”
“Wewe mzee unazeeka vibaya utaitaje tukio hili ajali?Unaona kuna ushawishiwi wa ajali hapo?”
“Huu ni uvamizi tumepigwa na adui zetu.Haiwezekani rubani wa jeshi ambaye ni mwanajeshi aangushe ndege mahali alipo mkuu wa majeshi na amiri jeshi mkuu ambaye ni rais?Hii ni dharau kubwa sana na haivumiliki kamwe!Lile eneo lilikuwa na umma mkubwa.Kulikuwa na mazoezi ya kutosha yaliyofanyika kabla ya leo.Rubani alijua fika anachopaswa kusema sasa iweje adondoshe ndege hapo?”
Mzee Gwamaka alivuta pumzi ndefu na kuzishusha kwa muda akiangalia hali ya hewa kwa ujumla.Alifikiria kidogo kitu gani cha kufanya.Alizitafuta busara zake zilizojificha ndani ya mvi zake.Akapitisha ulimi kwenye baraza la mdomo wake kasha akasema,”Najua tukio lililotokea ni zito.Tena ni kubwa sana.Sio tukio la kawaida.Ni la hatari.Tumepata pigo!Kulalamika sio suluhu.Muhimu tumuombe Mungu atupe ujasiri.Hili sio jambo la mzaa kabisa.Ni jambo lenye huzuni isiyo na mipaka.Kupigwa tumepigwa kweli.Ila sio kwamba ni lazima tuanguke chini kwa pigo hili.”
Wakamsikiliza,wengine walishayaacha makoti yao purazai.
“Ni kweli serikali nzima imetikiswa hatujui nani kapona nani kafa?Bado ni maapema mno.Pamoja na umaapema wote huu hatuna budi kujipanga nakuwa tayari kukabiliana na lolote litakalo tokea.Tuchunguze kwanza,tujue ni nini halafu hali ya dharura itangazwe.Kila sekta iliyopo pale jukwaani ilikuwa na wawakilishi wake.Wengi wao wakiwa ni viongozi wa sekta hizo.Bila kuficha kuna sekta nyingi zenye pengo hivi tunavyozungumza.Zinahitaji wasimamizi wapya ili nchi iendelee.Inaweza kuwa siyo ajali bali ni kundi la kivamizi kwa lengo lakuiadabisha serikali yetu tukufu.Ndiposa natoa tamko kwamba tufuate protokali.Uchunguzi ufanyike wa haraka sana ila tuwe na bodi maalum yakufanya uchunguzi huu pamoja na shghuli za uokoaji.
Uwanja ulipambwa kwa tabasamu za wana nchiMagwaride kadhaa yameshapita kutoa heshma zao kwa mkuu wan chi aliyekuwa jukwaa kuu.Mavazi yaliyovaliwa hapa asilimia kubwa yalikuwa yakizalendo hasa kwa rangi zilizopo kwenye bendera ya taifa.Uzalendo ulitukuka baina ya taifa hili linalokumbuka siku ya uhuru wa taifa lao kutoka kwa wakoloni waliowatawala.Kiuhalisi taifa limeshapiga hatua kutoka kwa mkoloni.Kuimarika kiafya,elimu,ulinzi na mengine mengi.Lilikuwa taifa imara na linaendelea kuimarika japo kwa mapungufu kadhaa wa kadhaa.
Jeshi la taifa la KIOTA kwa sasa katika sherehe za uhuru lilikuwa linafanya mazoezi kuonesha wana nchi wake uimara na ukakamavu wa jeshi.Pia walikuwa wakimuhakikishia mkuu wan chi ulinzi uliotukuka.Vyama mbalimbali vya siasa vilikuwepo katika sherehe hii pamoja na viongozi wa kitaifa.Vilevile kulikuwa na mialiko ya mataifa ya kadhaa japo wengi wao walituma udhuru na kuleta wawakilishi wao katika uwanja wa taifa.Ulinzi ulikuwa umeimarishwa katika jiji kuu la nchi ambapo taifa lilikuwa linashuhudia maadhimisho haya.
Rais Kisusi akiwa ameketi meza kuu,pembeni yake alikuwepo mkuu wa majeshi upande mmoja na upande mwingine alifuata naibu rais wake na viongozi wengine.Waliteta na mkuu wa majeshi.
“Kinachofuata ni nini jeneral maana leo sijisikii vizuri sijui kwanini?”aliuliza rais Kisusi.
“Ni mwite daktari?”aliuliza jenerali Tindikali.
“Hapana aliniambia sina tatizo.”alijibu rais Kisusi.
“Itakuwa msongo wa mawazo mkuu.Usijali nchi ipo salama.”
“Na wasiwasi na uchaguzi ujao.Lakini sio kwa hilo ni kwamba roho inanienda mbio sana.”
“Kivipi mkuu?”
Walikuwa maswaiba wakuu tangu shuleni tofauti ni majukumu ya kazi lakini wote ni wazalendo wazawa wa taifa la Kiota walioamua kuitumikia nchi yao.
“Au ni vile majirani zako hawajaja?”
“Hapana Tindikali.”
“Au tuhairishe shughuli?’”
“No!Leo ni dhifa muhimu sana sidhani kama kuna haja ya mimi kuondoka ghafla.Ngoja niimalize then tutaondoka.Unajua file namba 13.14 linanitatiza sana kiasi nakosa Amani.”alisema rais Kisusi ambapo alipitisha kitambaa kufuta kijasho kilichokuwa kina msumbua.
“Lina ufumbuzi hakuna kidudu mtu atakayesumbua.”Alijibu jenerali Tindikali.Waligutushwa na mshereheshaji aliyekuwa akielezea makundi mbalimbali ya ulinzi yaliyokuwa yanafanya mazoezi.
“Halafu Mkuu kinachofuata ni Maonesho ya ndege mpya za kijeshi tulizo tengeneza.”
Rais alipitisha ulimi kwenye papi za midomo yake nakuachia tabasamu hafifu.Akaangalia juu kusubiri maonesho ya ndege.
“Ndege inaendeshwa na Kapteni Pilipili ya kwanza kabisa kufanya onesho lake.Inatoka makao ya Msanda.Mh RAIS unasikia sauti ikizizima uwanja mzima.Haya ni mafanikio chini ya utawala wako.Ni ndege yetu wenyewe MI fighter Jet ian uwezo wa kwenda kilomita mia tatu kwa saa.Ina beba makombora kwa kumshambulia adui.Kwa heshma mh rais Kaptein…”MC alikuwa anahutubia.
Kaptein Pilipili akiwa angani kuelekea uwanja wa taifa kuonesha ndege mbele ya rais wao.Alianza kuhisi mikono mkimtetemeka.Makao yakuongozea ndege yalikuwa yakiwasiliana naye kumpa maelekezo ya kipi cha kufanya.Lakini ghafla alipoingia kwenye anga la uwanja aliekeza ndege moja kwa moja kwenye meza kuu walimoketi Rais na watu wake.Halafu akabonyeza kitufe cha kuachia kombora lakini hakubonyeza la kuruhusu kombora kutoka bali mlango wa kombora ulibaki wazi.Na kwa kasi atakayoenda nayo mpaka kufika kwenye jukwaa halitakuwa limeanguka kutoka kwenye eneo lakuhifadhi bali kama ndege ikiwaka moto au kulipuka bila shaka kombora lingelipuka.Kasi yake ilikuwa ya sekunde.
“Mh Rais kaptein Pilipili ndo….”hata kabla hajamaliza tayari ndege ilipigiza kwa kasi kwenye jukwaa.Kishindo kizito kilikuwa kimejiri.Lakini wakati wa butwaa lile likiendelea kuna mlipuko mwingine ulitokea pale uwanjani!Mlipuko mzito.Moto ulipanda juu na moshi mzito kufuka.Kilio kilikuwa kimesikika kikubwa sana tena cha kuogofya kiasi watu walishtuka ambao hawakupatwa na mlipuko ule.Vikosi vya kijeshi vilivyokuwa pale uwanjani nakubahatika kukoswa na mlipuko ule vili taharuki kwa harka maana mshtuko uliotokea ni waaina yake.Vyombo vya habari kadhaa vilipoteza mawasiliano hasa kamera zilizokuwa karibu jukwaaani.Lakini kwa kamera zilizo mbali kidogo hazikupatwa na kadhaia hiyo.Mambo yote yalionekana mubashara kwenye vyombo vya habari.Taharuki iliyokuwepo katika taifa haikuwa na maeleoz!Nchi ya Kiota ilikuwa taabani.Na kwa haraka tu ilikuwa vigumu kujua ni wangapi walikuwa wamekumbwa na kadhia hii!Ilichukua muda kwa vyombo vya habari kuanza kutangaza kinachotokea uwanjani.Waliopo studio waliona kama ni sinema wana tazama lakini ukweli ni kwamba balaa kubwa lilikuwa limetokea.
Wakati simu zikipigwa maeneo mbalimbali huku vyombo vya ulinzi vikijitahidi kujua ni ktiu ganoi kimetokea hadi ndege ilyokuwa ikirushwa kwa maonesho ikapoteza mwelekeo nakuanguka jukwaa alimokuwamo Rais Kisusi.Jukwaa ambalo serikali nzima ilikuwemo!Ilikuwa maapema mno kubashiri tukio hili ambalo bichi sana!Nchi ya Kiota ilikuwa imesimama hakuna kilichosonga.Waliokuwa karibu na maeneo yale nje ya uwanja walianza kutimua ovyoo.Waliopo ndani walianza kutoka nje msongamano ambao ulisababisha purukushani hadi watu kubanwa chini nawengine kupoteza fahamu.
Taharuki!Taharuki kuu!
Taifa limetetemeshwa!Kiota imeanguka chini kwa kishindo!
****
Makao makuu ya jeshi!TRIANGLE
Meza kuu yahali ya hatari ilikaliwa na viongozi wa kijeshi waliokuwa wamebaki kambini.Kulikuwa taharuki.Hakuna kilichotulia kila mmoja aliongea lake.Simu ikipigwa huku na kule.
“Nimesema tuna tuna tangaza hali ya hatari nakuipeleka kwa kiwango cha DEFCON 3.”alisema kanali Rama.
“Hapana huna mamlaka yakupandisha hiyo amri.DEFCON 3 nikubwa sana wewe huoni ni mwenzetu ndokaangusha ndege.”alijibiwa na Major Kanda.
“Major huu siwakati wa mzaa Kiota imepigwa hatucheki na mtu vilevile nataka kujua ikulu nani anachukua napia nijue nani anajua hali ya rais na serikali nzima.Tukisubiri mambo yaendee kijinga tutapoteza nchi!Tuamue hapa hapa kufungulia vikosi vya kijeshi kuingia mtaani.Hivi.”
“wewe ni nani katika nchi uamuru upuuzi huuo!”
“Huna mamlaka hana mamlaka!”
“Pumbavu hujui lolote nimekufundisha kazi mimi.”
Kila mtu alikuwa na wasiwasi na hasira.Hakuna aliyejua ni uamuzi gani wakuchukua kwa wakati huo.Ilihitajika busara na amani ya hali ya juu.Nchi ilikuwa imetikiswa kwa pigo kubwa kuliko yote pona ya watu ilikuwa na wakati mgumu usio na maelezo yakuridhisha.Hali ilikuwa tete.Hakuna aliyemuamini mwingine.Mfumo mzima wa utawala uliingia dosari ya ajabu.Utamwamini nani?Aliyetekeleza mauaji ni nani?Kwa dhamira gani?Na mpango upi?Ni ajali?Lilikuwa swali lililoshibisha meza nzima ya eneo lile.
“Jamani hebu tutulie natuwe na uvumilivu wa hali ya juu.Nchi nzima inahitaji amani.”alisema moja ya wazee wa jeshi aliye na umri mkubwa.Ni mstaafu lakini mtu mwenye busara alishashinda medani kadhaa kwa juhudi zake jeshini pamoja na ushirikiano mbalimbali alioutoa jeshini.Vyeo Alisha vipata.Pamoja na mambo mengine,alikuwa mzalendo kwa taifa lake huru.Alilipenda.Alilijali nakulithamini kama kwa uzalendo uliotukuka.Mwili wake wenye ngozi iliyozeeka,sharubu zenye uzito halafu nyeupe pamoja na pua yenye mchongo ilimpa sura ya busara.Utuuzima dawa.
“Ni sawa nchi imepigwa pigo kuu.Hii ni ajali mbaya…”kabla hajamaliza alivamiwa kwa kauli zenye utata.
“Sio ajali!”
“Wewe mzee unazeeka vibaya utaitaje tukio hili ajali?Unaona kuna ushawishiwi wa ajali hapo?”
“Huu ni uvamizi tumepigwa na adui zetu.Haiwezekani rubani wa jeshi ambaye ni mwanajeshi aangushe ndege mahali alipo mkuu wa majeshi na amiri jeshi mkuu ambaye ni rais?Hii ni dharau kubwa sana na haivumiliki kamwe!Lile eneo lilikuwa na umma mkubwa.Kulikuwa na mazoezi ya kutosha yaliyofanyika kabla ya leo.Rubani alijua fika anachopaswa kusema sasa iweje adondoshe ndege hapo?”
Mzee Gwamaka alivuta pumzi ndefu na kuzishusha kwa muda akiangalia hali ya hewa kwa ujumla.Alifikiria kidogo kitu gani cha kufanya.Alizitafuta busara zake zilizojificha ndani ya mvi zake.Akapitisha ulimi kwenye baraza la mdomo wake kasha akasema,”Najua tukio lililotokea ni zito.Tena ni kubwa sana.Sio tukio la kawaida.Ni la hatari.Tumepata pigo!Kulalamika sio suluhu.Muhimu tumuombe Mungu atupe ujasiri.Hili sio jambo la mzaa kabisa.Ni jambo lenye huzuni isiyo na mipaka.Kupigwa tumepigwa kweli.Ila sio kwamba ni lazima tuanguke chini kwa pigo hili.”
Wakamsikiliza,wengine walishayaacha makoti yao purazai.
“Ni kweli serikali nzima imetikiswa hatujui nani kapona nani kafa?Bado ni maapema mno.Pamoja na umaapema wote huu hatuna budi kujipanga nakuwa tayari kukabiliana na lolote litakalo tokea.Tuchunguze kwanza,tujue ni nini halafu hali ya dharura itangazwe.Kila sekta iliyopo pale jukwaani ilikuwa na wawakilishi wake.Wengi wao wakiwa ni viongozi wa sekta hizo.Bila kuficha kuna sekta nyingi zenye pengo hivi tunavyozungumza.Zinahitaji wasimamizi wapya ili nchi iendelee.Inaweza kuwa siyo ajali bali ni kundi la kivamizi kwa lengo lakuiadabisha serikali yetu tukufu.Ndiposa natoa tamko kwamba tufuate protokali.Uchunguzi ufanyike wa haraka sana ila tuwe na bodi maalum yakufanya uchunguzi huu pamoja na shghuli za uokoaji.