Riwaya: Kiguu na njia

Riwaya: Kiguu na njia

SURA YA KUMI NA NANE

Pilikapilika Za Moshi Na Arusha

Moshi na Arusha ni miji jirani sana, ikiwa imetenganishwa kwa umbali wa kilometa 75 tu na hivyo kufanya safari toka mji huu hadi ule iwe takriban dakika sitini kwa gari lisilo na matatizo.
 
SURA YA KUMI NA TISA

Pembe Za Faru

Wanasema ‘za mwizi arobaini’. Sisi hatukuzihitaji arobaini hizo. Siku ya tatu tu, toka tulipoanza shughuli hizo, ilitosha kabisa kututia hatiani.
 
SURA YA ISHIRINI

Jela miaka ishirini

Mfikirie mtoto mdogo sana wa kiume, aliyeondoka kwao zamani sana kuiokoa roho yake, mtoto ambaye alifuatana na babu yake, wakavuka misitu na nyika, milima na mabonde, mito na mabwawa hadi nchi ya mbali. Huko mtoto aliona nuru mpya elimu. Akaanza kusoma huku akiwa na matumaini.
 
SURA YA ISHIRINI NA MOJA

Mfungwa Asiye Na Mikono Toka Musoma

Wanahistoria wanatukumbusha kuwa adhabu ya kifungo, ambayo mimi na wenzangu gerezani humu tulikuwa tukiitumikia, ilianzishwa huko Ulaya yapata miaka 300 iliyopita. Awali ya hapo mhalifu, au mtuhumiwa aliyepatikana na hatia ama alinyongwa ama alitoswa baharini au kuachwa katika visiwa vya mbali visivyo na watu.
 
SURA YA ISHIRINI NA MBILI

Toka Gerezani Hadi Zanzibar.

Mfungwa hana kauli. Mfungwa hana hiari. Mara tu ukishahukumiwa wewe si wewe tena, ni mali ya mtu mwingine. Utafuata matakwa na hiari yake hadi mwisho wa kifungo chako.

tika gereza jingine la aina yake.
 
Back
Top Bottom