ISABEL-ndani ya mpango hasi
ilipoishia...
Honi za hatari zilipigwa na geti likajifungua
lenyewe, bila kuuliza aliingia ndani kumkuta
Jomse akiwa kajiinamia huku mkono mmoja
ukiwa unaminyaminya mbavu zake. Kelele ya
mlango ilimfanya kushtuka na kuikamata bastola
yake tayari kwa kazi.
Oh Ton, bienvenue mon ami Jomse
alimkaribisha kwa lugha yao ya kifaransa, Ton,
kazi hii imeshatuelemea, yule bibi nimeshindwa
kummaliza, sijui itakuaje, sijui nimtafutie wapi,
amekuwa mbogo aliyejeruhiwa Jomse alipigisha
viganja vya mikono yake kwa ishara ya kukata
tamaa na kutikisa kichwa chake kushoto kulia.
Jomse, Anaconda ameuawa, nahisi si mwingine
ni Amata aliyefanya kazi ile Ton alifikisha
taarifa, Jomse alipatwa na mshtuko mkuu alibaki
midomo wazi na mikono ikimtetemeka, alipiga
ngumi mezani na meza ile ya kichina
iliyotengenezwa kwa cheapboard ailigawanyika
vipande viwili. Aliichukua bastola yake na
kuitazama kwa makini Kisasi alijisemea, akiwa
kaukunja uso wake kwa hasira.
Wangu Amata, wako Bibi, Meno ya Mamba
atabaki hapa kumlinda Isabel
endelea...
9
Kompyuta ya Kamanda Amata ilikuwa ikiisoma
flash aliyoichukua kule hotelini, siri nyingi na za
kutisha zilikuwa zikipita katika kioo cha
kompyuta ile, Amata alibaki kapigwa na butwaa,
akili ilimsimama na meno kumchezacheza, hapa
ndipo aligundua hatima ya mpango hasi ambayo
katika memory card aliyopewa na Isabel kipande
hiki hakikuwapo. Aliendelea kusoma na kupata
majina kadhaa ya madigala wa mpango huo
duniani, aligundua kuwa kumbe ni nchi za
Maghalibi ndizo zinazofadhili mapinduzi hayo
kwa faida yao wenyewe, Amata alizama katika
lindi la mawazo, akiwaza na kuwazua, akipanga
na kupangua.
Alipogeuka kuielekekea simu yake na ndipo
alipojikuta kuwa hayupo peke yake.
Tulia hivyo hivyo! sauti ilimkoromea kutoka
upande ule, Amata hakuwa na la kufanya
Simama taratibu aliamriwa na kutii bila shuruti
Kwa mwendo wa taratibu ongoza nje ya
nyumba yako kupitia geti kubwa, Amata
alifanya hivyo na kufika nje ambako aliikuta gari
ndogo aina ya Toyota Altezza ikiwa buti wazi
Ingia kwenye buti, ukileta matata nafumua
ubongo wako sasa hivi
Amata alitazama huku na huku Usijaribu kuleta
shida ingia twende, Kamanda Amata na ujanja
wake wote aliingia ndani ya buti ya gari hiyo,
Jomse aliruka kwa wepesi na kulifunga buti lile
Amata akiwa ndani, kisha akaingia garini na
kuondoka kwa kasi.
Kamanda Amata nimemtia mkononi Jomse
alikuwa akiongea kwa simu na mtu mwingine
Vema, hakikisha unamhifadhi vizuri mpaka amri
nyingine itapotolewa sauti ya kike kutoka
upande wa pili ilisikika
Sawa Madam, nitahakikisha hilo, hawezi
kunitoroka huu ndiyo mkono wa Shetani Jomse
alimalizia kauli yake.
Kamanda Amata akiwa ndani ya buti hakuweza
kujinyoosha kutokana na udogo wa buti lile,
aliuinua mkono wake wa kushoto uliokuwa na
saa kubwa ya kisasa akabofya kitu Fulani
pembeni mwa saa hiyo, kidoti chekundu kikawa
kinawakawaka juu ya kioo cha saa hiyo,
aliisogeza karibu na kinywa chake na kuongea
maneno Fulani, kisha akabofya tena sehemu
nyingine, sasa kidoti cha kijani kikawa
kinawakawaka, akatulia kimya butini akisubiri
hatima yake huku akihesabu kona ya kwanza
mpaka ya mwisho kulia ama kushoto.
Gari ilisimama, kamanda Amata alihisi geti
likifunguliwa na sauti zilizoongea kifaransa
zilimfikia masikioni mwake, alielewa yote
yaliyoongelewa, na baada ya sekunde kadhaa
gari ile iliingizwa ndani na geti kufungwa nyuma
yake, gari ikasimama
Kuwa muangalifu, hajafungwa huyo Jomse
alimuamuru Meno ya mamba ambaye alibaki
pale kuweka ulinzi kwa Isabel na jingo zima kwa
ujumla.
Huyo msichana mpumbavu ameamka? Jomse
aliuliza tena
Hapana bado hajaamka, na sijui kama ataamka
maana hali yake ni mbaya sana Meno ya
mambo alimjibu Jomse.
Ah Muache afe tu, ijapokuwa Madam Rose
alikuwa anamuhitaji lakini hatuna la kufanya
Jomse alimueleza Meno ya Mamba. Amata
aliposiki kauli hiyo aliumia sana kwa kuwa
aligundua kuwa Isabel lazima atakuwa
ametekwa na kuwekwa huku, na kwa vyovyote
atakuwa kwenye hali mbaya kutokana na mateso
makali.
Suka taratibu, usilete makeke, la, hii SMG
itakufumua vibaya na mwili wako utakuwa
chakula cha samaki usiku huu sauti kavu ya
Meno ya mamba ilisikika masikioni mwa Amata.
Kamanda Amata alishuka kutoka kwenye buti ya
gari ile na kusimama kwa miguu yake miwili,
mikono yake ikiwa juu aliona asifanye makeke
yoyote kwani alishajua kuwa Isabel yupo eneo
hilo, japokuwa kwake haingekuwa kazi ngumu
kuwadhibiti wote wawili.
Geuka nyuma yako na uongoze njia unayoiona
Amata alitii na kufuata kijia hiko huku mikono
yake ikiwa juu kama alivyoamuriwa. Hatua
chache alijikuta katika ubaraza mpana tu, ukiwa
na viti viwili na kighorofa kimoja, chini sakafuni
aliona mwili wa binadamu aliolala bila uhai,
Amata alipigwa na butwaa aliutazama mwili ule
kwa haraka haraka akagundua kuwa si
mwingine ni Isabel alikuwa amelala chini na
mwili wake kutupwa kama wa mbwa. Hasira kali
zilimshika Kamanda Amata hakujua afanye nini,
alitamani aukimbilie ule mwili kujua kama una
uhai au la, lakini alishindwa japo alikuwa
anaumia sana
* * *
Ikulu ya Dar es salaam
Mheshimiwa Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiwa
tayari katika suti yake ya kijivu na msafara wake
wa watu wa usalama, walijipangwa kwa safari
ya uwanja wa ndege, tayari kwa safari ya
Washington ambako alialikwa kwa mkutano
maalum na Rais wa Marekani Mheshimiwa
Barack Obama. Kila kitu kilikuwa
kimekwishapangwa, watu wa usalama tayari
walikuwa wameandaa kila kinachobidi kwa ajili
ya kutekeleza na kuhakikisha kuwa mheshimiwa
Rais anafika safari yake salama na kurudi
salama, ujumbe anaosafiri nao tayari ulikuwa
ndani ya ndege kule uwanja wa ndege terminal 1
wakiwa wanamsubiri tu mheshimiwa Rais.
5H-ONE, Gulfsream Aerospace G-V SP G550,
ndege ya serikali ya jamhuri ya muungano wa
Tanzania, inaomba njia kuruka saa tatu na
dakika thelathini usiku huu sauti ilisikika katika
chombo maalum cha muongoza ndege katika
mnara mkubwa wa kuongozea ndege ulio upande
wa kusini wa uwanja wa ndege wa kimataifa wa
Julius Kambarage Nyerere.
5H-ONE, Gulfsream Aerospace G-V SP G550,
unaruhusiwa kuruka kupitia upande wa
mashariki sauti ya muongoza ndege iliruhusu
kuondoka kwa ndege ya Rais baada ya
kuhakikisha anga yote ipo salama kabisa.
Wakiwa wameketi sawia na mheshimiwa Rais
katika kaofisi kake kadogo ndani ya ndege hiyo
tayari kwa sfari kuelekea DC Washington. Dakika
chache tayari ndege ile ilikuwa imeiacha ardhi ya
Tanzania na kupasua anga kwenda anga ya
kimataifa, ikiwa chini ya uangalizi wa Rubani
mzoefu Capt Maga Junior na wasaidizi wake
wawili.
Madam S, aliiangalia ndege ile inapopotelea
mawinguni upande wa Vingunguti, yeye na
wengine waliomsindikiza mheshimiwa Rais
walianza kuchukua magari yao tayari kwa kurudi
kwenye shughuli zao nyingine, mara alihisi saa
yake kubwa ya mkononi inamfinya kwa vijimeno
maalum vilivyo chini ya saa hiyo, alihisi kuna
kitu, akaingia haraka kwenye gari yake na
kubonyeza kitufe Fulani pembeni ya saa hiyo, mara ikaanza kupiga ukulele kwa sauti ya chini ikitoa kamkanda kembamba ka plastiki
kalikokuwa na maadishi Fulani.
Att:Hakikisha mheshimiwa Rais haondoki, hiyo ndege imetegwa bomu kwenye control box na italipuka akiwa angani, fanya hima, mimi nimetekwa na sijui nilipopelekwa, fanya hima Tena Sana Aisee , madam S alishuka kwenye gari akiwa kama aliyechanganyikiwa hakuwa anajua afanye nini, alichukua simu yake na kubofya namba Fulani.
Hallo, naomba urudi uwanjani haraka sana kuna dharula simu ilifika kwa waziri wa ulinzi aliyekuwa tayari amekwishaondoka lakini gari yake bado ilikuwa njia panda ya air port kuelekea mjini, dreva wa gari hiyo aina ya Toyota Land Cruiser V8 aliligeuza na kurudi uwanja wa ndege, mara gari zilizofuata nyuma, kwa kitendo kile nazo zilirudi hasa zile za usalama.
Madam nini tena? waziri wa ulinzi mheshimiwa Machura a,imuuliza Mdam S ambaye alimkuta nusu kachanganyikiwa akiongea peke yake. Akampa ule mkanda uliotoka katika saa yake, naye akausoma, akashika kichwa hakujua la kufanya. Walibaki wanahangaika akili zikiwa zimewaruka kwa kiasi Fulani, kizaazaa!
* * *
Kamanda Amata alisoma kipande cha mwisho cha mpango hasi katika flash disk aliyoichukua kule valley View Hotel, ikionesha kuwa baada ya mauaji ya watu muhimu, wa mwisho kabisa ni Rais wan chi ambaye atategewa bomu kwenye ndege yage yake itakayoruka tarehe 26 June 2013 saa tatu na nusu usiku, bomu hilo limepangwa kulipuka dakika arobaini na tano baada ya ndege kuruka, lilikuwa limetegwa kwenye control box inayosambaza umeme katika ndege hiyo ya kisasa kabisa ambayo hakuna nyingine kama hiyo Afrika, kwa jinsi walivyofunga bomu hilo ilikuwa ni pale rubani anaporuhusu magurudumu kurudi ndani ndipo nalo linajiwasha na kuanza kuhesabu dakika 45 tu na kulipuka.
Simama apo hapo! sauti ya Jomse ilimuamuru
Kamanda Amata. Meno ya mamba alimsogelea Amata ili amfunge katika kiti kilicho jirani hapo.
Kaa chini usilete fujo, muda wetu umeisha wa kuwa nchini kwenu, dakika chache tutakuwa ndani ya nchi yetu Jomse alimueleza Amata ambaye alishikwa na hasira kali, akihesabu dakika za bomu lile lililotegwa katika ndege ya Rais, hakujua kama itwezekana kuokoa janga hilo au la, alitamani kama yeye angekuwa pale uwanjani ahakikishe mwisho wake.
Alipohakikisha amemfunga barabara, Meno ya mamba aliirejesha bastola yake kiunoni na kutembea hatua chache na kumsukasuka Isabel kwa mguu wake, Isabel hakutikisika.
Mara simu ya Jomse iliita
Mission clear, popo ameruka, subiri majibu
Jomse alitoa cheko la dharau
Kamanda Amata, sasa dunia itatikisika kwa hofu kuu kwa kusikia mlipuko mbaya wa ndege ya Rais wako, ha ha ha ha alijigamba, Sisi ndiyo wanamapinduzi, unakumbuka Rwanda na Burundi mwaka 1994, tulimtungua Rais
Abiyarimana na mwenzake Ndadaye!? Mliiona kama hadith ee! Ni sisi na sasa tuko hapa Tanzania, kamwe hamuwezi kukomesha juhudi,nakuwekea TV hapa uone dakika 40 zijazo breaking news sauti hiyo ilimkosesha raha Amata alitamani amrukie na kumgata ama kumeza kabisa kiumbe huyo. Waziwazi Amata alifura kwa hasira, akaanza kuopumua kwa nguvu na kifua chake kipana kikipanda na kushuka, akiwatazama kwa macho ya hasira watu hawa wakati wanamuwekea TV mbele yake umbali wa mita kama saba hivi.
Jomse alichukua simu yake iliyokuwa mezani wakati huo na kubonyeza namba Fulani kisha akaweka sikioni.
Yes. Hello, kutoka point A mission Clear, panga vikosi kuanza kazi mara moja pindi nikikupa taarifa alikata simu na kuiweka mfukoni.
Unasikia we mbwa, tayari majeshi ya waasi yameshakaa katima mapori ya Nyakanazi, na mengine yapo hapa Dar, tukitangaza tu nchi inapinduliwa dakika moja tu, na wewe ukishuhudia halafu utakuwa maiti, na yule bibi kizee wako muda si mrefu ataletwa hapa, na mtu wa kuwaua yuko Burundi anakuja, ha ha ha ha! Jomse aliongea kwa daharau ya hali ya juu.
Kamanda Amata kwa nguvu zote alijinyanyua kitini na kukinyanyua kiti kwa miguu yake na kukirusha kwa kukipiga mbele, kumbe kiti kile kilikuwa hakijafungwa pamoja naye, kilinyanyuka kwa kasi na kutua kichwani kwa Meno ya mamba, akiwa sasa mikono yake iliyofungwa pamoja imebaki nyuma, alimuona Jomse akija kwa kazsi pale alipo, Kamanda Amata lijikunja kwa kuruka na kuipenyeza miguu yake ndani ya wigo wa mikono iliyofungwa kuelekea nyuma na sasa mikono ile ilikuwa mbele, alinyanuka kwa kazi na kupiga double kick iliyotua kifuani mwa Jomse na kumpepesua hata bunduki yake kumtoka mikononi na kudondokea mbali, alipotua tu sakafuni kwa miguu miwili alipigwa mtama wa nguvu ambao ulimnyanyua juu na kabla hajatua aliichanua miguu yake na kuwatandika wote wawili kila mmoja teke la nguvu la mguu wake. Meno ya mamba alitema meno kadhaa.
Kamanda Amata alijiviriga kutoka pale
alipokuwepo na kuiwahi bastola iliyokuwa chini,kabla hajafika alipigwa teke la sikio na kumfanya kupoteza uelekeo, alijigeuza chali na kumuona Jomse akiwa na shortgun mikononi mwake, Amata hakujali, akiwa bado yupo chini alimdiga Jomse teke la nguvu nyuma ya vivigino lililomfanya aanguke chali kama mzigo kabla hajatulia, mguu wa nguvu ulitu juu ya tumbo la Jomse, ukelele wa maumivu ulisikika, wakati Meno ya mamba akija kwa kasi kumkabili Kamanda Amata ambaye alikuwa amelala pale chini, alishuhudia kichwa cha Meno ya mamba kikitawanyika vibaya na mwili wake kurushwa mita kadhaa ukiwa hauna uhai. Gina akiwa bado hajasusha mkono wake wenye bastola aina ya Makarov, bastola ya kirussia iliyotengenezwa mwaka 1949 na bwana Nikolay Makarov na
kuanza kutumika rasmi mwaka 1951 ilishafanya kazi yake kama ilivyoamuriwa.
Freeze, bastard Gina alimuamuru Jomse
aliyekuwa akijaribu kujitutumua pale chini, Jomse alijifanya asikii na kutaka kuichuku ile short gun mara Makarov ya Gina ilicheua tena na kuvunja mkono wa Jomse, yowe la maumivu lilisikika.
Mara polisi kadhaa waliingia ndani ya jingo lile wakiongozwa na Inspekta Simbeye, walimfungua kamanda Amata na kumchukua Isabel baada ya kugundua kuwa bado alikuwa na uhai, haraka sana wakamkimbiza Hospitali ya jeshi la
wananchi Lugalo.
Naomba muhakikisehe huyu mtu anafika makao makuu ya polisi leo kwa mahojiano, mimi naelekea uwanja wa ndege kuna muasi mmoja bado hajakamatwa na hayupo hapa kamanda Amata alitoa amri huku akiingia katika gari ile iliyomleta, Toyota Altezza na kuigeuza kwa kasi na kuondoka eneo lile kuelekea uwanja wa
ndege.
:::Shughuli imeamka, ndege ya Rais
imeshapaa... kuna bomu ndani yake...
:::Madama S atafanya nini kulinusuru janga
hilo?
:::Kamanda Amata atawahi uwanja wa ndege?
:::Nini hatima ya ISABEL, TONTON na kisa
kizima.
Kwa kujua hayo na mengine yote usikose
chapisho lijalo