ISABEL
ndani ya mpango hasi
ilipoishia...
Tungekuwa tumekufa mimi na Madam S leo
Kwa nini? Gina aliuliza huku akimpa juice
kwenye bilauri. Amata alimueleza Gina tukio hilo,
Gina alionekana kuchoka kwa habari hiyo.
Gina, sina la kufanya hapa lazima niingie kazini
bila ruhusa Amata alimueleza Gina huku akivuta
kitabu chake cha kumbukumbu na kupekua
kurasa kadhaa, na kuandika vitu Fulani.
Gina, nashindwa nianzie wapi, naomba hata
wewe uwe makini na usitembee kizembe kama
kawaida yako, hakikisha muda wote unakuwa na
mawasiliano na mimi ili kujua nilipo na ulipo,
kimenuka mama alipokuwa akimaliza maneno
hayo, saa yake ilimfinya mkono kuashiri kuna
ujumbe uliokuwa ukiingia, aliinua mkono na
kubonyeza namba Fulani mara mkanda maalum
ukawa unatoka ndani ya saa hiyo ukiwa na
maadishi tukutane shamba haraka
iwezekanavyo mama anataka msaada Tena Sana
Aisee mkanda ule uliishia hapo na kukatika,
Amata alijiweka tayari.
Gina natoka, signal yetu iwe ileile, sawa?
Yes Sir! Gina alijibu kwa utani kama
kawaida yake. Amata alitoka na kuelekea
shamba.
endelea...
***
Gari ya wagonjwa ya Jeshi kutoka hospitali ya
Lugalo ilifunga breki mbele ya wodi ya mifupa
(MOI), vijana wawili waliovalia kombati za jeshi
na msichana mmoja waliteremka na kuielekea
wodi hiyo, jambo la kushtua! Polisi aliyekuwa
lindo alionekana kwenye kiti chake akiwa hana
uhai, yule kijana wa jeshi alimtazama yule polisi
mwenye bunduki mkononi, kisha akapitiliza ndani
akifuatiwa na mwenzake walipoingia ndani
walimkuta muuguzi akiwa chali juu ya meza
yake, tundu la risasi lilionekana wazi kifuani
mwake. Chumba hakikuwa na mtu,
walitazamana hawakujua la kufanya walitoka
ndani ya chumba hicho kwa kasi na kuripoti
haraka kambini, Isabel ametekwa.
Haraka gari za polisi zilifika eneo hilo lakini
habari hazikubadilika, Isabel alikuwa ametekwa.
Inspekta Simbeye alijishika kiuno, hakujua nini la
kufanya, aliusogelea ule mwili wa yule askari na
kuuangalia kwa makini, kisha akaingia ndani
ambako vijana wake walikuwa wakifanya mambo
mbalimbali ya kiusalama.
Ina maana we hukuona yeyote aliyekuja?
Inspekta Simbeye alimuuliza daktari wa zamu
jioni hiyo.
Hapana, mi nimetoka hapa niliacha kila kitu
sawa. Nashangaa hawa jamaa wameingia saa
ngapi
Uhhhhhh Inspekta Simbeye alishusha pumzi,
kisha akausogelea mwili wa yule muuguzi,
ilionekana wazi kuwa hata tukio lenyewe bado ni
bichi kwa kuwa jeraha lile la risasi lilikuwa bado
linavuja damu taratibu. Kazi ilikamilika na miili
yote ilihifadhiwa katika chumba cha kuifadhia
maiti.
Inspekta Simbeye alikuwa kwenye lindi la
mawazo Isabel anaweza kufanya hili? alijiuliza
sana kwa kuwa aliamini kuwa ulinzi aliouweka
wodini hapo ulikuwa makini lakini nini kimejiri
katika utekaji huo, lilikuwa swali gumu sana.
Simbeye aliuangalia ule mlango mkubwa wa
wodi hiyo, bado alikuwa haamini kilichotokea,
mbele yake aliiona kazi jinsi itavyomuia ngumu,
aliingia kwenye land cruiser ya Polisi na
kuondoka.
***
Kamanda Amata aliketi juu ya kochi kubwa na
upande wa pili kulikuwa na Madam S, pamoja
nao kulikuwa na watu wengine wawili.
Kamanda, mi nakwambia kwenye hili sakata
Isabel lazima anahusika Madam S alimsisitizia
Amata juu ya uhusika wake katika mpango hasi,.
Hapana Madam, mi nafikiri ngoja aondolewe
pale kisha tutaenda kuongea nae vizuri
Ok! Kamanda
Madam S alikatishwa na mlio
wa simu, akainua mkono wake na kuelekeza
sikioni.
Yes, nakusikia
Madam S alijibishana na sauti
ya upande wa pili
Eee? What? aliuliza kana kwamba kuna kitu
ambacho hajakielewa katika simu hiyo. Alishusha
mkono wa simu taratibu na kuupachika kwenye
kikalio chake, kisha akainua bilauri ya maji na
kujimiminia kinywani, alikunywa kama mtu
aliyekuwa na kiu ya jangwani, kisha macho yake
mawili yaliyofunikwa kwa miwani yalitua kwa
wale vijana wawili na kisha kwa Amata, akatikisa
kichwa kuonesha masikitiko yake.
Isabel alitamka.
Isabel? Kafanya nini? Amata aliuliza
Isabel katoroka, na isitoshe ameuwa muuguzi
na askari wa mlangoni.
Amata alishtushwa na habari hiyo ambayo
kwake ilikuwa ngeni sana na ya kutoaminiwa,
alisimama kitini na kuliendea dirisha kubwa
lililopo hapo, uso wake ulianza kushikwa na
taswira ya gadhabu, Madam yuko sahihi,
inaonekana Isabel ni mmoja wao, kamanda
Amata aligeuka na kumtazama Madam.
Lazima apatikane Kamanda alijikuta akitamka
maneno hayo bila mwenyewe kujua.
Kamanda, kazi imerudi mikononi mwetu kwa
ushirikiano na jeshi la polisi, ila wao watafuata
maelekezo kutoka kwetu, kazi njema vijana
Madam S alimaliza na kuelekea kwenye vyumba
vya kulala.
Kamanda Amata alitoka katika jumba lile kubwa
shamba akaingia kwenye gari yake na
kutokomea.
Tairi zake zilisimama moja kwa moja katika wodi
ya mifupa, kwa mwendo wa haraka alizivuta
hatua zake na kuingia kwenye lango kuu kisha
moja kwa moja akingia kwenye kijivhumba cha
wauguzi akawakuta watatu wameketi hapo.
Habari zenu wadada? Mimi ni afisa usalama
Amata alijitambulisha moja kwa moja bila
kujizungusha, poleni kwa msiba. Lakini naomba
mnisaidie kitu kimoja ili kukabiliana na jambo
hili
Karibu sana mmoja wa wauguzi hao
alimkaribisha
Ningependa kuona daftari la zamu zenu, hasa
wale waliokuwa wanamhudumia Isabel
Bila kusita muuguzi yule alivuta daftari kubwa na
kuliweka mezani, Amata aliangalia orodha ya
majina yale na akalifikia jina la muuguzi
aliyebadilishana zamu na marehemu Suzan
Crispin , alifunga lile daftari na kuwarudishia
Asanteni warembo alijibu
Kaka tutoe hata soda basi mmoja wa wauguzi
alitamka
Amata alitoa wallet yake na kutoa noti ya ya sh
elfu kumi nma kuwapatia, kisha akaondoka zake.
8
Madam S, alibaki akihangaika mawazoni mwake,
moyo wake ulijawa hasira, kila mara aliapa
kumsaka aliyeweka bomu kwenye gari yake,
lakini alimshukuru Mungu kwa kuwa amemuokoa
katika hilo. Alitafakari kwa muda mrefu akipanga
na kupangua lakini picha haikuja sawa sawa.
Polepole alianza kupata hisia na kujua wapi ni pa
kuanzia kazi, akiwa katika mawazo hayo
alipitiwa na usingizi.
Asubuhi ya siku iliyofuata
Madam S, aliliendea geti kubwa la gereji hiyo,
akasukuma kijimlango kidogo, hakikuleta matata
akaingia na moja kwa moja akafika ofisini.
samahani kuna kijana mmoja, jana asubuhi
alinitengenezea gari yangu, nina shida nae, ile
gari imekorofisha nataka akaiangalie madam
Limueleza fundi mkuu
Unamjua kwa jina?
Hapana ila nikimuona nitamjua kwa sura
Madam S pamoja na yule fundi walitoka na
kuingia eneo la kazi, haikuchukua muda
alimtambua kijana yule, baada ya mazungumzo
yote waliondoka pamoja. Madam S alipita
taratibu eneo la uwanja wa Taifa.
Unaijua ile gari iliyochakaa pale? alimuuliza
Hapana, ntaijuaje gari iliyoungua vile?
Ok, umejibu vizuri. Gari yangu jana imelipuliwa
kwa bomu kama umesikia kwenye redio au TV,
Madam akameza mate na kuendelea Sasa nina
wasiwasi mkubwa wewe ndiye uliyefanya kazi
hii, ya kuweka bomu na kutaka kuniua siyo?
Yule kijana akaonekana kuchanganyikiwa, alikaa
kimya kwa muda bila kujibu chochote.
Usiponipa ushirikiano, utalala pabaya leo
Mama, utanionea tu, labda gari imelipuka
kutokana na mfumo wa umeme
Hapana, mimi najua aina za milipuko, lile ni
bomu Madam S alitulia kisha akaendelea Najua
si wewe, ila nambie nani unamuhisi
Yule kijana alibaki kimya moyo ulimuenda mbio
hakujua nini cha kufanya katika hali hiyo.
Alijaribu kuvuta kumbukumbu ya siku ile ili
angalau ajue ni nani labda alifanya hivyo, Bro
Jose , alijiwazia mwenyewe.
Nafikiri nimekumbuka kitu mama, kama ni yeye
kuna bro mmoja tunamwita Bro Jose , mara
nyingi huwa anakuja pale gereji
Madam S akatikisa kichwa kuashiria kuwa
amekubaliana na kijana huyo.
Ok, uliona anafanya nini?
Alikuja pale, akawa anaisifia gari yako, mi
nikiwa narekebisa tairi, ye akawa mara anaingia
ndani ya gari mara anaagalia engine
Ok, zaidi ya hapo, hamna kingine?
Hapana
Sawa, sasa nitampataje huyo Jose?
Huyu Bro Jose ni ndugu na mwenye gereji yule
uliyekwenda ofisini kwake
Madam S, aligeuza gari na kurudi mjini, kisha
alichukua simu yake ya upepo na kuongea na
watu Fulani, alisimama mahali na mara land
cruise yenye vioo vyeusi ilikaribiana nao, vijana
wawili walishuka na kumchukua fundi gereji
kutoka katika gari ya Madam S na kumuingiza
kwenye ile Cruiser
Sikia, sikufanyii hivi kwa nia mbaya ila utajua
baadae, utaenda kupumzika sehemu mpaka
nitakavyokuachia Madam S alimueleza yule
kijana, na baada ya hayo Panda kwenye gari
alimuamuru kupanda kwenye ile cruiser, akiwa
ndani wale vijana walimvalisha kofia kubwa ya
sox ambayo ilimfunika uso wote , na hakuona
chochote kilichoendelea zaidi ya kupitiwa na
usingizi mzito.
***
Umejiingiza kwenye jambo lisilokuhusu
msichana! Jomse alimueleza Isabel ambaye
alikuwa hoi kwa kipigo kutoka kwa jamaa huyo.
Hata mkiniua, nina uhakika hamtafanikiwa,
taarifa tayari zipo kwenye vyombo vya usalama
na nijivunia kwa kufanya hilo, heri mimi nife
lakini niwaokoe maelfu wanaotarajiwa kufa hapo
mbeleni Isabel alizungumza kwa sauti ya
kwikwi huku damu zikimtoka mdomoni, mguu
wake uliokuwa umeanza kupona sasa
ulitoneshwa tena kiasi kwamba hata hakuweza
kusimama. Jomse alichukizwa na jibu la Isabel,
alimpiga mateke mengi na mikanda ya kijeshi
mpaka Isabel akapoteza fahamu kwa mara
nyingine.
Jomse, acha hasira utamuua bure tu huyu na
haitatusaidia lolote Tonton alimwambia Jomse.
Na we usiwe kama Mandi, badala ya kufanya
kazi uliyotumwa unaanzisha mambo mengine,
hata nikimuuua huyu mimi napata faida gani, afe
tu tutatupa maiti yake porini iliwe na mbwa
Jomse aliongea kwa hasira huku akirusha
mikono yake hewani na kuondoka hapo
Muacheni afe apo hapo aliwaeleza wengine na
wote wakaondoka katika chumba hicho na
kumuacha Isabel peke yake akiwa hana fahamu.
Ok! Tuzungumze yajayo, kazi karibu inakamilika
plan A, japo kuwa jana tumemkosa yule bibi
kizee (Madam S), kweli ni tukio baya kwa
upande wetu. Tunapofanya kosa moja
tunajiharibia wenyewe Jomse aliwaambia vijana
wake akiwemo Tonton, akawatupia macho
mmoja mmoja kisha akaendelea Jamaa wapo
tayari mipakani, wanasubiri tukamilishe plan A, ili
wao wamalize plan B, lakini kumkosa yule bibi
jana, naomba muwe makini sana Jomse
alimaliza na kujimiminia wine yake kinywani.
Kabla hajasusha bilauri yake simu iliita mfukoni,
akaitoa na kuiweka sikioni,
Yeah man aliitikia
Eh! Unasema?(...), kama atarudi ni wa
kumpoteza tu. We njoo huku watarudi hao
Jomse akashusha simu yake.
Jamaa wamemkusanya dogo kule gereji taarifa
hiyo iliwashtua wote, kila mtu alionekana
kuchanganyikiwa na hilo.
Du! Eee sasa hapo patamu, tukamilishe mpango
huu haraka iwezekanavyo Ton alitoa rai.
Walivunja kikao na kurudi kule walikomuacha
Isabel, wakamkuta bado amezirai, Jomse
akachuku maji ya baridi kwenye ndoo na
kummwagia.
Amka mpumbavu wewe, na wewe lazima
ukutane na Madam Rose akutie adabu Jomse
alifoka na kumuacha Isabel akijivutavuta pale
chini.
Ton alikuwa kimya sana, fikra zake zilimfanya
akose raha kabisa, aliingia kwenye gari yake
tayari kuondoka
Ngoja nikaonane na Suzan nimpe mzigo wake
narudi baadae Tona alimuaga Jomse
No. Ton usiende peke yako, uko uendeko
hakutabiriki,nenda na Anaconda akulinde Jomse
alitoa amri na ikafuatwa.
Punde si punde walifika katika hotel ya Valley
View, Anaconda akasuka kwanza na kuangali uku
na huko kisha akagonga kioo cha dirisha la
nyuma kuashiria kitu, Ton akashuka na moja
kwa moja akongoza kuelekea hotelini na
Anaconda akamfuata nyuma yake.
Tax nyeupe ilisimama nyuma kidogo ya gari ya
akina Ton, mwanadada mrefu kiasi, mwenye
mwili wa kawaida, aliteremka na baada ya
kuiweka miwani yake vizuri, alivuta hatua
taratibu kuielekea hoteli hiyo, alichukua lifti
kupanda ghorofa ya nne kisha akaelekea chumba
namba saba akagonga mlango kwa staili
aliyoelekezwa, na mlango ukafunguliwa.
Karibu Suzan Anaconda Limkaribisha
Upo peke yako? Ton alidakia kwa swali
Suzan alisita kidogo kujibu Ee nipo peke yangu
Ok haina haja kuchelewa, tunashukuru kwa kazi
uliyotufanyia. Na ujira wako huu hapa dola za
kimarekani elf moja Ton alipomaliza kuongea
hayo alimkabidhi kitita hiko Suzan, nae
akakisunda katika mkoba wake. Suzan
hakuamini kabisa anachokishuhudia, pesa zote
hizo kwa kazi ndogo, kazi ya kumsaliti Isabel.
Ok. Mi naomba niende Suzan aliaga na
kusimama tayari kuondoka
Ok Suzan, be carefull Ton alijibu na kumruhusu
Suzan kuondoka.
Suzan aliiendea tax iliyomleta na kuingia mlango
wa nyuma wa gari hiyo.
Ingia! Ukileta fujo nakumaliza Suzan
alitazamana na domo la bastola kutoka kwa
Gina, Gina hakuonesha uso wa masihara hata
kidogo
Ingia alirudia tena na Suzana akaingia ndani,
Gina alichukua mkoba wa Suzana huku mkono
mmoja ukiwa bado umeshikilia bastola ile,
aliupekua na kutoa na alipoiona simu yake
aliichukua kwa kutumia kitambaa maalum kisha
akaitia kwenye mkoba wake. Suzan akatiwa
pingu mikononi.
Haya endesha gari
Tunaelekea wapi?
Central police
Dreva aliondoa gari na kuelekea alikoagizwa.
Walipofika central Suzan alishushwa na Gina
akafuata nyuma yake.
Hifadhi huyu, naomba asihojiwe lolote mpaka
mpatapo amri nyingine Gina aliwakabidhi Suzan
polisi waliopo kaunta na kisha yeye akaongoza
kuelekea ofisi ya Inspekta Simbeye.
Kazi uliyonituma imekamilika afande Gina
aliongea kwa ukakamavu mbele ya bosi wake
Vizuri sana afande, waweza kwenda
nitawasiliana na wewe nitakapokuhitaji Inspekta
Simbeye alimueleza Gina, Gina akaonesha
ukakamavu wake kwa kubana mikono yake
miwili kuonesha heshima, kisha akageuka na
kuondoka.
***Haya kazi imeanza.... mpango hasi
matatani...
****Nini hatima ya Isabel?