ISABEL an action story
ilipoishia...
Madam S, IGP na waziri wa ulinzi hawakuamini
wanachosikia baada ya simu iliyopigwa na
Amata kumfikia Madam S kabla hajaondoka
katika eneo hilo la makao makuu ya JKT. Kila
mmoja alifurahi kwa furaha ya aina yake
Well done Kamanda Amata Madam S alisikika
akiyatamka hayo maneno.
Ok, tunamshukuru Mungu, sasa kesho asubuhi
wote tukutane tuelekee Tabora kwa ndege ya
kukodi waziri alimaliza na wote wakaagana
kuelekea walikotoka.
endelea...
***
G ari za jeshi ziliondoka kutoka kambi ya Kaliua
KJ 320B kuelekea eneo la tukio ili kuwasaidia
abiria wale kuwafikisha mjini, usiku kwa usiku
amri ilitolewa na kiongozi wa kambi hiyo na kazi
ilianza mara moja bila hata kchelewa.
Watu walikuwa ni wengi sana kiasi kwamba
ilipelekea wengine kubaki ili gari zingine zije
kuwasaidia, vijana wa jeshi la wananchi wa
Tanzania walifanya kazi yao vizuri sana na kwa
moyo wa kizalendo kuwasaidia abiria wale japo
kuwasogeza karibu na stesheni au kuwafikisha
kabisa.
Steshen masta wa Tabora aliamuru vibelenge
kadhaa kufuatana ili kuona hali ilivyo na ndani
ya kimojawapo mlikuwa na mkuu wa polisi wa
Tabora, stesheni masta mwenyewe na viongozi
wachache wa chama na serikali, wote walitaka
kwenda kujionea wenyewe kile kilichotokea.
Wakiwa bado njiani kwa mwendo wa taratibu,
kwa mbali waliweza kuona kitu kikubwa
kimezuia reli, operetta aliongeza mwanga wa taa
yake kubwa na kupiga honi nyingi lakini hakuona
dalili ya kitu hicho kuondoka mahali pale,
alipunguza mwendo na walipokaribia walikuta ni
injini ya treni iliyokuwa ikitoka Kigoma kuja
Tabora
Oh my God! stesheni masta alisikika akisema
kwa sauti. Operetta alisimamisha chombo chake
na wote wakashuka kuangalia hali hiyo, walikuta
injini ile ikiwa imeacha reli na kusimama kando
katika mawe wakati lile behewa lilikuwa
limeanguka na kuharibika vibaya. Waliteremka,
kwa kusaidiwa na kurunzi walizonazo waliweza
kulikagua behewa lile na injini ile, hawakukuta
madhara katika injini ile ila tu behewa lilikuwa
limeharibika vibaya. Baadhi ya polisi waliingia
ndani ya injini hiyo kuangalia hiki na kile
wakisaidiana na mafundi, katika chumba
kimojawapo ndani ya injini hiyo ndimo
waligundua mwili wa mzee kasimu usio na uhai,
waliutoa na kuuhifadhi vizuri kasha kuupeleka
katika kibelenge kile
Alikuwa operetta wetu mahili sana stesheni
masta alijikuta akisema mwenyewe huku
akiuangalia mwili ule, machozi yalimlenga
Kwa vyovyote atakuwa kafa kishujaa, kwani
mwili wake unaoneka umepigwa sana
aliongezea mkuu wa polisi mkoa.
Waliupakia mwili ule katika kibelenge lakini
hawakuweza kuendelea na safari kwa kuwa reli
ilikuwa imeharibika vibaya. Kwa uchunguzi wa
haraka walioufanya waligundua kuwa reli ile
ilikuwa imefunguliwa
Washenzi hawa walifungua reli! mmoja wa
mafundi alisema kwa sauti
Ha! Hawa walidhamilia, mpaka wamefungua reli,
no hii ni hujuma Mkuu wa polisi alizungumza
hayo huku mkononi mwake akiwa ameshika
moja ya nati kubwa zinazotumika kufungia reli
hiyo ya kijerumani.
Tungewapata hawa jamaa leo wangejuta
kuzaliwa mkuu wa polisi alisema kwa hasira
Unafikiri bado watakuwa kwenye treni
iliyobaki? Stesheni masta aliuliza
Sio rahisi, hii ni hujuma kabisa lazima walifanya
hivi ili kuwaokoa wenzao, lakini dunia ni ndogo
tutawatia mkononi mkuu wa polisi alimjibu
stesheni masta. Vijana wa polisi walijaribu
kuangalia huku na kule japokuwa ilikuwa ni giza
lakini mwanga wa taa kutoka katika kibelenge
kile uliwawezesha kuona vizuri, polisi mmoja
alipiga hatua chache pale mbele akaona kitu
kama karatasi ndogo iliyokuwa ikisukwasukwa
na upepo mdogo uliokuwa ukivuma eneo hilo,
akakitazama akataka kukiokota lakini akaona ni
upuuzi akaamua kuondoka zake. Walirudi katika
kibelenge kile lakini askari wane walibaki kwa
ajili ya ulinzi lakini pia walijua wahujumu wale
wangeweza kurudi hasa kufuata mafuta.
***
Amata ga Imba, alisimama pembeni akiliangalia
zoezi zima linavyoendelea la kuwahamisha abiria
wale kwa kutumia magari ya jeshi,
Kamanda, asante kwa kazi, wewe waweza
kwenda sisi tutamalizia, na ulinzi tutaimarisha
polisi mmoja alimwambia Amata.
Hamna shida, lakini nasikitika kuwakosa wale
washenzi japokuwa mmoja wao kajiua
mwenyewe, sasa hatujui walikuwa wangapi
Amata alimjibu yule polisi
Hawa jamaa hata mi sijui walikuwa wangapi,
nahisi ni yuleyule mmoja yule polisi alitoa jibu
na hisia zake
Kama ni yule peke yake basi! Lakini sidhani,
lazima wako wengine au lazima ana mtandao
mkubwa, usijali afande Amata alimaliza na
kuondoka eneo lile mpaka kwenye gari
mojawapo la kijeshi aina ya MAN ililokuwa
limeegesha hapo likipakia baadhi ya abiria.
Kichwa kilimzunguka Amata, hakutaka
kukubaliana na wazo lake kuwa mle ndani
kulikuwa na jambazi mmoja tu, kwake kama
mzoefu wa kazi ile alijuwa wazi lazima watakua
kikundi ama ndaniya treni ile au nje yake,
alimfikiria sana Isabel ambaye muda huo
alikimbizwa hospitali ili kuokoa maisha yake kwa
kuwa alijua wazi kuwa ni yeye pekee anayeweza
kutoa mwanga wa tukio zima. Amata alitoa
karanga zake na kuanza kurushia mojamoja
kinywani mwake huku akiwaza ili na lile, moyoni
akiomba na kusali Isabel apone ili azungumze
naye machache watakuwa washapata ile
memory card?alijiuliza, mara kwa mara
alipofikiria juu ya Isabel alishtuka kwa kuwa
hakuwa na uhakika kama atamkuta mzima alijua
wazi kuwa kama wale majambazi wana mtandao
mkubwa haitakuwa kazi kugundu Isabel alipo
lakini wamfuate wa nini wakati washapata
wanachotaka alijiwazia mh naomba asife
alijiomba mwenyewe na hapo alijikuta anaingiwa
na shauku ya kumuona Isabel japo asikie neno
moja kutoka kwake labda lintampa muelekeo wa
nini cha kufanya.
Walikuwa watatu bwana we hukuwaona vizuri
baadhi ya vijana abiria walikuwa wakibishana,
Amata alijiunga nao katika mazungumzo yao.
Yule tall sura yake sio ngeni kabisa, kama
namuonaona madukani pale Mwanga sokoni au
itakuwa namfananisha labda mwingine
aliongezea. Amata alivutiwa na mazungumzo
hayo alitulia kimya akijifanya kuchocheachochea
vikuni kwenye ule moto uliokuwa ukiwaka
taratibu ili kuwapa joto usiku ule.
Baada ya mazungumzo yale marefu Amata
alikuwa amehifadhi vitu fulanifulani kichwani
mwake ili labda itakapobidi vitamsaidia katika
upelelezi wake. Kufumba na kufumbua abiria
wote walikuwa wameondoshwa eneo lile, askari
wachache walibaki kulinda mabehewa yale na
mizigo ya watu. Amata alitazama saa yake
tayari ilikuwa inakaribia saa kumi na moja
alfajiri, kichwa chake bado kilikuwa kinawazua
mengi kikitoa hili na kuweka lile, moyo wake
haukuridhika hasa alipomkumbuka Mandi jinsi
alivyojiua kwa mbinu ya kijinga namna ile, alijua
wazo kuwa wapo wenzake lakini aliumiza kichwa
jinsi gain ya kupata ukweli mpango hasi
alikumbuka neno hili alilotumiwa na Isabel
kupitia facebook, Amata alipenda ajue hasa
undani wa mpango huo ni nini. Alitamani kama
ni upelelezi basi akabidhiwe yeye hilo faili kwani
alitaka kulipa kisasi cha kuumizwa Isabel.
***
5
Mwili wa Koplo Kibona ulikuwa umehifadhiwa
vizuri kabisa katika sanduku la kisasa
liliofunikwa kwa bendera ya polisi, maafisa wa
jeshi hilo waliovalia nadhifu kabisa walikuwa
wamesimama kwa mstari ulionyooka vizuri na
upande mwingine kulikuwa na waombolezaji
wengine. Kasisi alipomaliza ibada ya marehemu,
vijana sita waliovaria nadhifu vazi la kipolisi
walisoge karibu na sanduku lile kwa ukakamavu
wa hali ya juu mara ilipigwa buluji maalumu ya
kazi hiyo kabla ya kushusha sanduku lile
kaburini. Jeshi la polisi liliamua kumzika
kiheshima kwa sababu amekufa akiwa katika
harakati za kulilinda taifa, baada ya buluji ile
kumalizika zilipigwa risasi kadhaa hewani kisha
sanduku lile lilishushwa taratibu kaburini.
Amata alisimama kwa mbali akiwa ndani ya suti
yake nyeusi iliyomkaa vizuri, pembeni yake
alikuwa na Madam S wakifuatilia kwa karibu
kabisa matukio yote ya mazishi hayo.
Muda si mrefu shughuli ilikamilika na watu
kuanza kutawanyika wengine wakienda kumpa
pole mjane wa marehemu.
Isabel alihifadhiwa katika chumba maalum
chenye mitambo tiba ya hali ya juu iliyomsaidia
kupumua na mingine ikisoma mapigo ya moyo
wake jinsi yanavyoendelea, Isabel alilala kimya
katika kitanda kile chenye shuka safi lenye
maandishi ya buluu yaliyosomeka MSD, hakuwa
hata anatikisa mkono wla kupepesa macho
alitulia kabisa, mara kwa mara muuguzi alikuja
kumuona maendeleo yake huku akiandika vitu
fulanifulani katika faili lililopo karibu kabisa na
kitanda hicho
Mgonjwa anaendeleaje?sauti ilimuuliza kutoka
nyuma ya kichwa chake, yule muuguzi alistuka
sana alijua labda ni mzuka. Amata ga Imba
alitabasamu hasa alipogundua kuwa muuguzi
yule kapata mshtuko kwa hilo.
Anaendelea vizuri, ila bado hajarudiwa na
fahamu Muuguzi alijibu kwa utulivu. Amata
alilisogelea faili na kulisoma harakaharaka
japokuwa watu huamini kuwa muandiko wa
daktari ni mgumu kusoma lakini kwa Amata
haikuwa hivyo. Alielewa moja kwa moja
yaliyoandikwa, Isabel alivunjika mbavu nne za
kulia inaonekana alipigwa sana kwa mateke na
kitu kigumu sehemu za mbavu, amekutikana na
majeraha ya kichwani, fuvu lake limepata shida
kidogo kadiri ya uchunguzi imeoneka Isabel
alijigonga vibaya kwa paji lake la uso hivyo
kusababisha majeraha eneo hilo, damu nyingi
imepotea hasa kutokana na majereha
aliyoyapata, mkono wake wa kulia umevunjika
hivyo alikuwa tayari amefungwa muogo POP.
Amata alimwangalia Isabel kwa uchungu sana
machozi yalitaka kumtoka lakini hakuruhusu hali
hiyo itokee. Mitambo mingi ya kidijitali
iliyomzunguka Isabel ilikuwa ikitoa ushirikiano
wa hali ya juu kuhakikisha mambo
hayataharibika, aliporidhika alimuaga yule
muuguzi na kuondoka zake.
***
Siku 3 nyuma
NYUMBANI
KWA
KINA ISABEL
Mama na Baba wa Isabel walikuwa shambani
kwao huko Kasulu wakiendelea kulima ili
kuhakikisha watoto wao hawalali njaa katika
msimu wote wa mwaka, redio ya mbao aina ya
National ilikuwa chini ya mchikichi ikiendelea
kuwaburudisha. Wazee hawa ambao bado
walishikilia falsafa za Mwalimu Nyerere kuwa
kilimo ni uti wa mgongo hawakuchoka na kilimo
japokuwa bado walikuwa wakitumi dhana duni
jembe la mkono lakini hawakukata tama kwani
walikumbuka mkitaka mali mtaipita shambani.
Mama Isabel! Aaaah mama mi nimechoka
bwana napumzika Baba wa Isabel alimwambia
mkewe huku akitupa jembe pembeni na kuiendea
redio ile ambayo ilikuwa imetulia hapo bila ya
wasiwasi.
Ah Baba Isabel, unanitia uvivu mwenzio, na mi
naacha Mama Isabel naye alitupia jembe
pembeni na kwenda chini ya migomba alipoficha
viazi vyake ili kutafuna atulize njaa ambayo
wakati huo ilikuwa ikimtafuna kwelikweli.
Ngoma maarufu iliyopigwa na marehemu Moriss
Nyunyusa ilirindima ndani ya redio ile kushiri
taarifa ya habari ilikuwa mbioni kuwa hewani,
baba wa Isabel alitazama saa yake ilikuwa saa
saba mchana.
Tabora,
Watu wawili wameuawa na wengine wawili
kujeruhiwa kwa risasi katika treni iliyokuwa
ikitoka Kigoma kuelekea Dar es salaam jana
usiku, dulu za kiusalama zimesema treni hiyo
ilivamiwa na majambazi ambao hawajajulikana
idadi yao na kusababisha vifo hivyo. Kamanda
wa Polisi mkoa wa Tabora amethibitisha kutokea
tukio hilo na amesema waliouawa ni askari polisi
Koplo Kibona na operetta wa treni hiyo mzee
Kasimu, eitha mkuu wa polisi huyo amethibitisha
majeruhi wawili walioumizwa vibaya na
kukimbizwa Muhimbili kwa matibabu kuwa ni
askari polisi konstebo Kirama na msichana
mmoja mwanafunzi aliyetambulika kwa jina moja
tu la Isabel, mpaka sasa hakuna mtu yeyote
anayeshikiliwa na polisi ila uchunguzi
unaendelea
Taarifa ile ilimshtua baba wa Isabel, alianza
kuhema kwa haraka haraka akamuita mkewe,
hali haikuwa nzuri, kilimo kilisitishwa, mama wa
Isabel akaanza kuagua kilio kilichowafanya
majirani waanze kukusanyika uko huko
shambani.
Mwanangu Isabel, jamani nifanyeje mimi, Oh
Mungu we
kilio kilitawala mama wa Isabel
hakuweza kujizuia kulia, alilia sana hata
kupelekea kuzimia mara kwa mara.
Mama nyamaza, si wamesema yupo hospitali
dada mkubwa wa Isabel alimbembeleza mama
yake
Wanatudanganya, mwanagu mimi atakuwa
ameshakufa, nimlilie nani mimi Mama wa Isabel
hakuweza kutulia kwa haraka, muda mfupi
nyumba ilikuwa imejaa watu kujua kulikoni, Baba
wa Isabel alishafikishwa katika hospitali ya
mission Kabanga maana BP ilipanda ghafla.
Taarifa za treni hiyo zilisambaa sana na kwa
haraka, watu wengi walisikitishwa kwa tukio hilo
Yaani hawa ni wakutia moto tu! mmoja wa
vijana aliyaongea maneno hayo kwa sauti
akionesha jinsi ambavyo angependa majambazi
hao waadhibiwe.
Siri imefichika, hakuna anayejua nini kipo nyuma
ya tukio hilo, mh kazi ipo...
Hali ya Isabel ni mbaya, unafikiri atapona?
je serekali ya Tanzania itaamua nini juu ya hili?
Usikise chapisho lijalo...