Riwaya: 'hofu'

Riwaya: 'hofu'

Watatoka kwenye hili jumba la fk salama? Tupe vitu plzzz
 
Wasalaam wakuu,nasikitika kwa kuwaacha kwa muda mrefu nikiwaachia njaa kali. nimshukuru kwa kipekee kidi kudi kwa kuwapeni angalau hicho kidogo alichowapeni. namuomba aendeleze na akiweza kumalizia kabisa kwani nahis kuwapa kwa wakati riwaya hii itakua ni makwazo kwenu kwani muda niupatao ni usiku na saa nyingine usiku sana! kidi kudi nakuomba uendelee na mniwie radhi kwa niliowakwaza lkn daima nipo nanyi
 
Last edited by a moderator:
Wasalaam wakuu,nasikitika kwa kuwaacha kwa muda mrefu nikiwaachia njaa kali. nimshukuru kwa kipekee kidi kudi kwa kuwapeni angalau hicho kidogo alichowapeni. namuomba aendeleze na akiweza kumalizia kabisa kwani nahis kuwapa kwa wakati riwaya hii itakua ni makwazo kwenu kwani muda niupatao ni usiku na saa nyingine usiku sana! kidi kudi nakuomba uendelee na mniwie radhi kwa niliowakwaza lkn daima nipo nanyi

Haya Fanya mambo sasa wewe ndo sterling wetu sasa..#kidi kudi
 
Last edited by a moderator:
lkn Willy si ungetupia alipoishia kidi kudi halafu umwachie ukumbi aendeleze
 
Nikipata nafasi hata saa 9 usiku nitawarushieni kama kidi kudi bado atakua hajamalizia
 
Last edited by a moderator:
FUNGA KAZI

II

Willy aliporuka na kupitia dirishani, alimkuta George anamsubiri tayari. Alikuwa amewasha taa ambayo swichi yake ilikuwa karibu na dirisha hilo. George alikuwa amesimama. Alimwonyesha Willy ishara ya vita vya maninja. Pale pale Willy aligundua kuwa George alikuwa ninja. Bila kuchelewa Willy alipiga magoti na kuinamisha kichwa. Hiyo ilikuwa ishara na imani yao. Kwa kutumia viganja vyake, Willy 'alisema' sala ya ninja vidole vya mikono yake vinaingiliana na kuachama kama meno ya mamba. George naye alifanya vile vile kama Willy alivyofanya. Kama kawaida sala yao ilichukua kama muda wa dakika kumi. Ndipo vita kali ilipoanza.

III

F.K. alikimbia na kutoka nje ya nyumba. Alibana karibu na mlango akimsubiri Bon ambaye alikuwa anamfuata. Bon alitokea akikimbia F.K. alimtegea na kumkata ngwara. Bon alianguka chini. F.K. aliruka haraka na kumpiga Bon teke la ubavuni kabla hajasimama na kurudi chini. F.K. alimtupia teke la pili. Alikuwa na nia ya kumpiga kichwani, lakini Bon alikuwa macho. Aliudaka mguu wa F.K. na kumfanya aanguke chini Mara wote waliinuka na kukabiliana.

"Leo ndio mwisho wako F.K", Bon alisema.

"Hee, nyie hamjui nguvu ya Afrika Kusini kijeshi. Hata mkituua sisi haiwezi kuwasaidia. Zaidi ya hayo mtazidisha hasira ya makaburu. Hapo ndipo mtakapokiona cha mtema kuni. Vitendo vyenu vitafuatiwa na mashambulizi ya kutisha. Vitendo hivyo vitazisanya nchi zilizo mstari wa mbele na Afrika huru kwa ujumla kukoma ubishi. Kamwe hamtaichokoza tena serikali imara ya Afrika Kusini", F.K. alijigamba.

"La hasha! Sisi tutawaangamiza nyinyi vibaraka na majasusi wa makaburu. Baada ya hapo. Serikali ya Afrika Kusini itatambua kuwa Afrika sasa ni imara. Zaidi ya hayo, kipigo tutakachotoa kitawatia hamasa wapigania uhuru wa Afrika Kusini. Vile vile vijana mashujaa wa Afrika Kusini watapata moyo wa kuendelea kupambana kwa nguvu zaidi. Na lazima makaburu watasalimu amri.... Na sasa hivi kifo chako kimefika, msaliti wee", Bon alisema.

Mara Bon alimrukia F.K. na kumpa vipigo vinne vya haraka haraka. F.K. alipepesuka huku damu zikimtoka midomoni. Hapo hapo F.K. aligundua kuwa hakuwa na uwezo wa kupambana na Bon Sipele.

F.K. alikuwa anafikiri haraka ni nini cha kufanya. Mara aliona gari lilikuwa njiani kuelekea kwenye nyumba yake. Aliangalia taa zake, akagudua kuwa gari lile lilikuwa aina ya Benzi. Na zaidi ya hayo Benzi hilo lilikuwa la kwake mwenyewe F.K. Katika mawazo yake F.K. alifikiri kwamba Stumke alikuwa ndani ya gari hilo. Alidhani kuwa alikuwa amemtoroka Willy na kuwafuata AICC. Mawazo yake yalimdanganya. Hali hiyo ilitokana na woga mwingi uliokuwa umemwingia F.K. kwa mara yake ya kwanza alifikiria kifo na woga wake ukaongezeka. Kufumba na kufumbua F.K. alitimua mbio kuelekea kwenye gari hilo lililokuwa linakuja kwa mwendo wa kasi. Bon alishangazwa na mbio za F.K. Alianza kumfukuza. Mara alijiwa na mawazo kuwa huenda wale walikuwa adui. Hivyo alisimama na kujiweka tayari kwa mapambano ya ziada.

Wakati ule ule Mike alikuwa ameshika upanga wake mkononi. Alikuwa amemuua Hecke. Baadae alimfuata Bon ili kumuongezea nguvu. Alipotoka nje, alimwona F.K. anatimua mbio huku akifukuzwa na Bon. Hivyo Bon naye aliamua kuwafukuzia. Alipomwona Bon anasimama naye akasimama pembeni. Mike alihisi vile vile wale walikuwa maadui. Gari hilo lilizidi kuja kwa kasi. F.K. alilikimbilia kwa kasi pia. Alikuwa ameinua mikono juu kama ishara ya kutaka lisimame. Bon na Mike walibaki wamesimama kushuhudia tukio hilo. Kitendo kilichofuata, kiliwashangaza. Badala ya gari hilo kupunguza mwendo, lilienda kasi zaidi kuelekea kwa F.K. ambaye alijaribu kulikwepa. Hata hivyo lilimkumba.

"Eeeeh! Nakufa!", F.K. alisema maneno yake ya mwisho. Alipogongwa, alirushwa juu na kuangukia kwenye seng'enge.

Bon na Mike waliona gari hilo likisimama mahali pale lilipokuwa limeegeshwa gari la Mzee Hamisi. Wote wawili walifichama nyuma ya mti. Walishangaa zaidi kuona mtu aliyeshuka kwenye gari hilo alikuwa Nyaso.

"Nyaso", Bon alimwita. Mike akaelekea kule ilipoangukia maiti ya F.K.

"Willy yuko wapi?", Nyaso alihoji huku machozi yakimtoka. Pale pale Bon aliwakumbuka Willy na George. Mambo hayo yalikuwa yemetendeka haraka sana.

"He! He! Hapa... hapa", sauti zilisikika.

"wako huku", Bon alimshika Nyaso mkono wakaenda mbio. Walielekea kule sauti zilikokuwa zimetokea. Hata hivyo Bon alikuwa bado ameshangazwa kitendo cha msichana huyu. Ilikuwa vigumu kwake kuelewa jinsi Nyaso alivyomgonga na kumuua bwana yake halafu asijali. Utafikiri hakuna jambo lililokuwa limetokea; ama kwa Nyaso alikuwa amegonga mbwa!.

"Ni vigumu kuwaelewa wanawake", Bon alijisemea kimoyomoyo.

IV

Walifika sehemu walikokuwa Willy pamoja na George. Ilibidi Bon amshike Nyaso ambaye alikuwa ameshikwa na kiwewe. Sababu ilikuwa ni kwamba vita vya maninja vilikuwa vimeanza.

"Willy! Willy! Ooooh", Nyaso aliita.

"Nyamaza! Hivi ni vita vya maninja. Sikiliza Nyaso. Wote wawili ni maninja. Maana yake ni watu wenye ujuzi wa hali ya juu wa kupigana. Wote wawili wamehitimu mbinu za hali ya juu za mapigano ziitwazo ninja. Sheria yao inasema maninja wawili wakianza kupigana, watu wengine hukaa kando. Mapigano huisha babada ya mmoja wao kuuawa", Bon alimweleza Nyaso kwa haraka.

"Hivi unaweza kumwacha Willy auawe ati kwa sababu ya sheria?, mimi nakwenda kumsaidia", Nyaso alisema huku akijaribu kujitoa mikononi mwa Bon.

"Kama Willy atauawa mimi nitachukua nafasi yake. Hii ni "sanaa" ya mauaji, nayo ina miiko yake. Hata mimi mwenyewe ni ninja", Bon alisema huku akimwangalia Nyaso usoni. Kwa mara ya kwanza Nyaso aliona macho ya Bon yamegeuka na kuwa kama hayana uhai.

"Mimi sikujuwa kama watu walio hai wanaweza kuwa maninja. Nilidhani ni hadithi tu ama michezo ya sinema. Mpaka sasa siamini", Nyaso alisema huku machozi yakimtoka.
Willy na George walikuwa wametazamana. Bon alimshikilia Nyaso kwa nguvu zaidi. Alipogeuka nyuma alimwona Mike amejiegemeza kwenye ukuta. Alionekana kuwa na wasiwasi. Bon alipomwangalia Mike alitoa ishara kuonyesha kwamba F.K. alikuwa amekufa. Hapo hapo wote waligeuza macho yao kuangalia mapigano makali yaliyokuwa yameanza. Mbinu zilizotumika zilikuwa za hali ya juu. Hata Bon mwenyewe alikiri. Pamoja na yeye kuwa ninja. Alikuwa hajaona mapigano makali kama hayo.

"George aliruka juu. Kana kwamba alikuwa anatembea hewani, alirusha mateke kumi mfululizo. Willy aliyakwepa yote. Kabla hajatua chini. George alichomoa upanga kutoka mgongoni mwake. Akaanza kumkabiri Willy.

Mike alihamaki akataka kuingia kwenye uwanja wa mapambano. Bon alimpa ishara ya kuzuia. Nyaso aligeuka na kulala kifuani mwa Bon. Alihofia Willy angeuawa wakati wowote. George alirusha upanga wake mara saba. Nia yake ilikuwa ni kumkata Willy. Lakini hakuweza kufanikiwa. Willy alikuwa ni mwepesi kama unyoya. Ghafla George aliruka juu na kumkuta Willy hayuko tayari. Bon na Make walifumba macho. Ilikuwa vigumu kuamini jinsi Willy alivyojipindua. Upanga wa George ulimpita kwenye mkono. Ulichana shati yake na kumkata kidogo.

Damu ilianza kumtoka Willy. Hata George mwenyewe alishangaa jinsi Willy alivyokwepa upanga huo. Willy aliangalia damu yake. Hasira ilimpanda. Alisikia harufu ya damu mpaka ule upanga akauona si kitu kwake. Alichana shati lake na kulitupa. Halafu alimrukia George na kumpiga dhoruba ambayo hakuitarajia. Aliupiga mkono wake wa kulia ambao ulikuwa umeshika upanga. Upanga uliruka na kuanguka karibu na miguu ya Bon. Kishindo cha upanga kilimshitua Nyaso. Aligeuka na kushuhudia jinsi Willy alivyokuwa akimtandika yule kaburu.

"Willy alimpiga George mapigo matano mfululizo, ambayo yalimfanya achanganyikiwe.

"Willy, muuee! muuee", Nyaso alipiga kelele. Lakini George alijibu mapigo. Alimpiga Willy kichwa cha aina ya pekee mpaka wote wawili wakaanguka chini. George aliwahi kuinuka, mara hii alitoa kisu kirefu. Halafu alimrukia Willy ili ammalize. Lakini Willy alikuwa macho. Aliruka kutoka mahali alipokuwa na George akamkosa. Bila kuchelewa Willy akamtupia George teke la tumbo akaanguka chini. Katika kuanguka kisu kilimtoka mkononi. Willy alitumia nafasi hiyo. Alimpiga George pigo la pekee ambalo lilimbomoa kifua. George alijuwa amekwisha.

"Aaaa! Nakufa! Willy, heri ungenikata kichwa ili nife kwa heshima za kininja", George alisema Bon alimtupia Willy upanga. Willy alikata kichwa cha George kwa pigo moja.

Nyaso alikurupuka kutoka mikononi mwa Bon, alimkimbilia Willy na kumkumbatia.

Aaaah. Willy! Siamini", Nyaso alisema kwa sauti kali. Bon na Mike walibaki wameduwaa.

"Haya tutoke hapa haraka, kazi iliyobaki ni ya polisi", Willy aliamrisha. Nyaso alitoa kitambaa na kumfunga mkono Willy. Wote waliingia ndani ya gari la F.K. Ingawa lilikuwa limevunjika taa za upande wa kulia. Willy aliendesha na wote wakarudi mjini.

FUNGA KAZI

V

"Hallo!", sauti ilisikika kwenye simu.

Hallo, mimi naitwa Willy Gamba".

"Ndiyo mzee", Kamanda wa polisi wa mkoa alijibu kwa hofu. Alikuwa amepokea simu kutoka kwa Inspekta Jenerali wa Polisi kutoka Dar es Salaam. Alikuwa ameambiwa asitoke nyumbani mpaka Willy ampigie simu.

"Haya sikiliza. Rafiki yako F.K. amekufa. Vile vile kuna rafiki zake wamekufa. Mzee Hamisi naye amekufa na maiti yako nyumbani kwake. Tondo pia ni maiti. Yapo nyumbani kwake. Naamini sasa unajuwa cha kufanya", Willy alieleza, wakati wakitelemka kwenye gari, kamanda aliuliza.

"Mzee Hamisi amekufa. Amekufa saa ngapi".

"Kati ya saa tatu na nusu na saa nne", Willy alijibu.

"Hiyo haiwezekani. Mimi nilipata habari kuwa mnamo saa nne na robo Mzee Hamisi alikuwa kwenye jengo la mikutano la AICC", Kamanda alisema.

"Yeye mwenyewe ama gari lake?", Willy aliuliza.

"Eah! Askari wanaolinda huku waliripoti kuonekana gari lake. Halafu waliripoti kuwa chumba kilichotayarishwa kwa ajili ya mkutano kiliwashwa taa. Wao walifikiri Mzee Hamisi alikuwa anaangalia na kuhakikisha usalama, kama kawaida yake", Kamanda alijibu.

"Haya, wewe shughulikia taarifa niliyokupa na kwa heri", Willy alijibu na kukata simu. Mawazo ya Willy yalikuwa yanakwenda haraka haraka.

Willy alipiga simu kutoka hotelini kwake New Arusha Hotel. Alikuwa na wenzake akiwemo Nyaso.

"Anasema nini?", Bon alimuuliza Willy. Willy alimweleza maneno ya Kamanda.

"Kama ni hivyo F.K. na wenzake waliweza kuingia kwenye chumba cha mkutano. Na kama waliingia walifanya nini?", Mike aliuliza.

"Maneno yako ni kweli. Bila shaka walikuwa na sababu", Willy aliitika. Kisha aliinua simu na kupiga namba ya mwandalizi wa mkutano wa wapigania uhuru.

"Hallo".

"Hallo. Willy hapa".

"Lete habari. Nimekaa nikisubiri kwa hamu hata mate hayamezeki. Wazee wana wasiwasi mkubwa. Kwani wanapiga simu kila baada ya dakika kumi. Heri tupate taarifa yako. Vinginevyo, kabla ya asubuhi watakuwa wamekufa kutokana na ugonjwa wa moyo", mwandalizi wa mkutano alisema. Willy alimweleza kwa kirefu yote yaliyokuwa yametokea.

"Hure? Afrika huru imeshinda", alijibu kwa ghafla na furaha kubwa.

"Kwa hiyo mkutano utaendelea kesho kama ulivyopangwa. Waeleze wazee kwamba sasa kazi kwao, kazi yetu sisi vijana wao tumeimaliza", Willy alisema.

"Sijui watawashukru vipi", yule mtu alisema huku akionyesha furaha.

"Hivi si wewe unayeshughulikia maandalizi ya mkutano?", Willy aliuliza.

"Ndiyo".

"Basi, naomba tuonane huko. Sisi tunakwenda huku sasa hivi.

"Oke!".

"Haya sasa twendeni. Tayari nimepata wazo. Wewe Nyaso lala na kupumzika. Hayo uliyoyafanya yanakutosha kwa siku moja". Willy aliwaambia wenzake.

"Nani abaki hapa? tunakwenda wote", Nyaso alijibu huku tayari akiwa amefika mlangoni.



VI

"Tunaomba vitambulisho", askari wa ulinzi kwenye jumba la mkutano, AICC waliwaambia akina Willy. Willy alitoa kitambulisho chake. Mmoja wao alikiangalia na kushituka. Aliwaruhusu haraka huku akiwa kama anataka kupiga saluti. Walipoingia kwenye uwanja walikuta yule mtu wao ameshafika.

Alikuwa amekaa juu ya boneti ya gari akizungumza na askari mlinzi. Willy alimfahamisha kwa wenzake.

"Huyu mtoto umempata wapi?", aliuliza.

"Huyu ni kuruta wetu", Willy alijibu kwa mzaha. Wote walicheka, baadaye waliingia kwenye chumba cha mkutano. Mkutano ungeanza masaa machache kutoka wakati huo. Waliongozwa na yule askari mlinzi. Willy aligusa mlango ukafunguka.

"Mliacha mlango wazi?", Willy aliuliza.

"Nadhani", mwandalizi alijibu huku akiwasha taa. Wote waliangaza huku na huko.

"Kuna kitu chochote kigeni ambacho hamkukiacha humu ndani ama kukipanga?", Willy aliuliza.

Walizunguka kote halafu mwandalizi wa mkutano akasema.

"Naona ni kama vitu vyote viko kama tulivyoviacha".

"Kwani Willy unafikiri vipi", Bon aliuliza.

"Ni dhahiri kwamba iwapo F.K. na wenzake waliingia ndani. Halafu askari walinzi wakafikiri alikuwa ni Mzee Hamisi eti baada ya kuona gari lake. Bila shaka watu hao walikuja kufanya hujuma ndani ya chumba hiki. Ni lazima kuna kitendo wamekifanya. Ni kazi yetu sisi kufahamu kitendo gani. Baada ya hapo kazi yetu itakuwa imekwisha. Vinginevyo kazi yetu haijakamilika kamwe". Willy alisema.

"Maneno yako ni kweli tupu", Mike aliitikia.

Mara nyingine ni vigumu kuelewa jinsi gani mambo fulani hutokea. Kwa muda wote huo Nyaso alikuwa amesimama kimya. Alikuwa mbali kidogo na Willy ambaye wote walikuwa wakimsikiliza. Yeye alikuwa amevutiwa na jambo moja ndani ya chumba hicho. Vyombo vya kuzima moto hapo ukutani vilikuwa vimepangwa kisanii.

Vyombo hivyo vilikuwa vimepangwa juu ya ukuta. Kwa pande zote nne vyombo hivyo viliangaliana kimoja na kingine jumla ya vyombo vilikuwa kumi na nne.

"Willy", Nyaso aliita. Willy alimsogelea.

"Unasemaje mtoto?", Willy aliuliza.

"Yeyote yule aliyepanga hivyo vyombo vya kuzimia moto?", Willy aliuliza.

Yule mtu aliangalia ule mpangilio wa vyombo hivyo. Halafu alimwangalia Willy kwa mshangao. Pale pale wote wakawa wamegundua sababu ya mshangao wake. Pale pale walihisi jibu.

"Hapana, vyombo vyote vilikuwa chini. Na jumla yake vilikuwa vinne tu katika chumba kizima", alijibu kwa kufadhaika.

Wanaume walipanda juu. Mike alikuwa wa kwanza kugundua ni nini kilikuwa ndani ya vyombo hivyo".

"Willy, ujuzi na uzoefu wako umeisaidia Afrika huru. Majasusi walitega mabomu ndai ya vifaa hivi. Mabomu yenyewe yanaendeshwa na mitambo yenye saa", Mike alisema kwa masikitiko. Nyaso aliyasikiliza yote hayo. Lakini hakuamini masikio yake.

"Heri tumekuja na mtoto huyu. Kuja kwake kumetupa faida; kweli naawambia wanawake wazuri wanayo mashetani yao", Bon alisema kiutani. Lakini Nyaso hakuwa katika hali ya utani bali alibaki ameduwaa. Ungedhani kapigwa dafrao. Mambo yaliyokuwa yametendeka, yalikuwa yamemzidi kimo. Vyombo vyote vilitelemshwa. Nane kati ya kumi na nne vilikuwa na maboni ndani yake. Kwa kutumia ujuzi wao waliyategua kwa uanalifu mkubwa. Willy alimwendea Nyaso na kumbusu.

"Ahsante sana Nyaso. Nikumbushe kesho nikununulie pipi", Willy alisema.

"Ahsante, Nitaisubiri hiyo pipi. Lakini hata hivyo sasa hivi ni asubuhi", Nyaso alijibu. Willy aliangalia saa na kugundua ilikuwa ni karibu saa kumi na moja alfajiri.

"La, twende tukapumzike. Sasa ni saa kumi na moja. Kazi yetu tumeimaliza. Imebaki ya wazee", Willy alishauri.

"Sawa kabisa. Sasa tuseme wewe mwenzetu unakwenda na sisi ama ndio mambo yamekunyookea", Mike alimtania Willy.

"Eti unasemaje mtoto. Maana sasa neno lako kwangu ni sheria. Ukisema nife, nakufa. Ukisema fufuka, nitafufuka", Willy alimwambia Nyaso.

"Tuwarudishe hotelini. Halafu wewe utakuwa mgeni wangu. Unakumbuka kwamba uliniahidi kitu, na mpaka sasa hujatimiza ahadi yako", Nyaso alisema.

"Bwana weee, tulepeleke kwanza sisi halafu uende ukatimize ahadi. Ahadi ni deni", Mike alieleza.

"Ningekuwa na bahati kama ya Willy ya kumpata mtoto kama huyu, mimi nisingepoteza hata dakika, kwanza kabisa mtoto mwenyee siyo wa kawaida", Bon aliongeza.

"Eeh, jamani! Mnanifanya nione aibu", Nyaso alinena.

"Achana na hao. Ndivyo walivyo. Tutawapeleka kwanz halafu twende kula vyetu", Willy alisema.

"Ahsante mwenzetu. Tukebehi tu", Mike alijibu wote waliekea kwenye gari.

"Askari hakikisha hamtoki kwenye chumba cha mkutano", Bon aliwaagiza askari wanaolinda chumba cha mkutano AICC. Ambao walikuwa wanatweta kwa jasho kwani ilikuwa vigumu kwao kuamini kuwa chumba walichokuwa wakilinda kilikuwa na mabomu. Pamoja na hayo, kundi la akina Willy hawakuona ajabu wala kuogopa. Wao walikuwa wanafurahi kana kwamba hakuna jambo la hatari lililotokea. Walikuwa wanataniana kwenye hali ya hatari. Hata hivyo walijitahidi na kujibu.

"Ndio afande", walimwaga yule mwandalizi wa mkutano.

"Tutaonana baadaye. Kesho ni kazi kwenu wazee. Sisi kazi yetu tumemaliza. Tunakwenda kutumia matuna ya uhuru wa Afrika", Willy alisema kwa mzaha.

"Sijui niwashukru vipi, kazi yenu ni ukombozi kwa Afrika nzima, Afrika ina deni kubwa kwenu", alisema mwandaaji wa mkutano huku Willy na wenzake wakimuaga na kupanda gari kuondoka.

Waliingia ndani ya gari. Mwanga wa mapambazuko uliwaongoza vijana hawa shujaa wa Afrikal. Walikuwa tayari wamemfungia kazi kaburu. Walikuwa wameipa hamasa Afrika huru ili kusaidia wapigania uhuru wa Afrika Kusini.

Wakati wananchi walipokuwa wanaamka kutoka usingizini, mashujaa hawa ndio kwanza walikuwa wanakwenda kulala. Walikwenda kuota ndoto za kweli za ushindi dhidi ya utawala wa makaburu, ambaye ni adui namba moja wa Afrika. Makaburu...
 
wakuu kwa kuwa imebakia sehemu moja riwaya hii ifike tamati na kwa kazi kubwa aliyoifanya Willy Gamba 1 kuileta hii kitu hapa mnaonaje nikimpa heshima yake ya kuja mwenyewe kutamatisha?
 
Back
Top Bottom