Riwaya: HOFU

RIWAYA: HOFU
MTUNZI: George Iron Mosenya
SEHEMU YA KUMI NA NANE
Akina nani hawa? Mbona sauti kama…..hata
mwili nao kama wa…..oooh!! ni yeye huyu ni
yeye…anafanya nini humu jamani. Mungu
wangu…” alitaharuki Inspekta John. Mara ule
upepo ukakoma.
John akatoa simu yake mfukoni aweze kupiga
picha walau moja tu ya umuhimu sana.
Akaseti simu yake isitoe mwanga wakati wa
kupiga ile picha na wala isitoe mlio wowote.
Upesi akaitega vyema!! Akiwa makini kabisa.
Lakini kosa moja tu likamgharimu. Simu yake
haikuwa imewekwa katika ukimya na muda
huohuo mkewe alimpigia simu maana usiku
ulikuwa unaingia na hajarejea nyumbani!!
Simu ikapiga kelele.
KIZUNGUMKUTI!!!!
******
Maeneo ya Nyihogo ndani ya mji wa Kahama.
Getonga na Rensho walichukua chumba kwa
kutumia pesa aliyokuwanayo Rensho na Getonga
asijue ni wapi ameitoa.
“Yule bwege wa kujifanya mchungaji alikuwa na
pesa sana…” Rensho alijisemea wakati wakiwa
ndani ya chumba walichokuwa wamechukua.
Getonga alimtazama bila kusema neno lolote.
“Saa sita kamili usiku niamshe we jamaa, nd’o
muda mzuri wa kumsaka huyo Salome….. kwa
wakati huu siwezi kujua pa kuanzia…we bwege
ungekuwa umenipa kitambulisho changu hata
nisingehangaika hivi!!”
“Nitakuamsha!!” Getonga alijibu kwa upole.
“Chukua simu yako katika pochi humo…ama ilete
hiyo pochi hapa” akazungumza Rensho. Kisha
akachukua kipochi chake na kuitoa simu ya
Getonga. Getonga aliduwaa na kutaka kuuliza ile
simu imefikaje pale lakini akahofia kumkera
Rensho. Akaipokea.
“Ole wako uwasiliane na mtu kabla hatujamaliza
kilichotuleta..,.. nimekupa useti alarm tu ya
kutuamsha saa sita basi!!”
Getonga akafanya kama alivyoamrishwa! Wakati
Rensho anapitiwa usingizi aliukunja mguu wake
na kuuweka juu ya mwingine, mapaja yake
meupe na laini yakachungulia nje.
Getonga akazikumbuka ndoto za marehemu
kadhaa ambao walikuwa wakiota mwanamke
mwenye mapaja meupe kisha ameyaacha nje
huku akiupandisha mguu mmoja juu ya mwingine.
Nalala na jini leo!! Getonga alijisemea huku hofu
ikimtawala zaidi
****
Jijini Dar es salaam, kabla Inspekta John Magege
hajatambua ni kitu gani afanye baada ya simu
yake kutoa mwanga. Wale watu tayari
walishamshtukia na yule mwanamke akawahi
kumdaka.
“Inspekta John Magege!! Kipi kimekuleta huku.
Mtoto mdogo kama wewe…” yule mwanamke
alimuuliza baada ya kumtambua.
“Lakini hata usingekuja bado tungekutana tu…
asante kwa kujileta mwenyewe kwa wakati…”
mwanaume alimtazama kwa kebehi na
kumwambia maneno yale, Inspekta aliyekuwa
ameketi chini alijikakamua na kuzungumza, “Mpo
chini ya ulinzi wa…” kabla hajamaliza alishtukia
akikwanguriwa vibaya mno na kitu ama mnyama
asiyemjua.
Sekunde nne nyuma alikuwa mzima wa afya na
uso unaong’ara lakini sekunde nne baadaye
alikuwa akiugulia maumivu makali na uso wake
ulikuwa unatokwa damu.
Kama ni kiumbe basi alikuwa ni paka.
“Hakuna amri za jeshi katika chumba hiki bwana
mdogo…na kwa vile umetutambua basi naweza
kukuahidi kuwa uhai wako upo mikononi
mwako…. Kiburi kitakufanya umfuate huyu
mwenzetu alipokwenda..” mwanaume mwenye
kitambi alimkoromea huku akimwonyesha maiti
ya mwenzao ambaye aliagizwa kwenda kusaka
damu kwa kuleta ajali ya maksudi katika basi.
Bahati mbaya akakutana na Rensho akaambulia
kifo.
“Watu wengine bwana…juzijuzi tu kilikuwa ki-
koplo sasa kupandishwa cheo na kuwa Inspekta
nd’o kujifanya unajua kufuatilia kila kitu….shenzi
taipu.” Mwanamke alimsimanga inspekta John.
“Haya hatupotezi wakati hapa….Mafaili ya kesi
hii yapo wapi na upelelezi wako umefikia wapi
Inspekta.” Bwana mwenye kitambi akaunguruma.
Inspekta John akanywea na kutambua kuwa
watu hawa hawakuwa wa kuwatishia neno ‘mpo
chini ya ulinzi’. Akalazimika kujibu. Alijibu kila
alichokuwa anakijua huku watu wale
wakimsikiliza.
Baada ya maelezo yake, wale watu wakanasa
mambo mawili makuu.
Kindo, yule mtu aliyepona katika sekeseke la
mauaji yale makubwa alikuwa bado hai huku
akimtaja RENSHO….
Pili kuna msichana mjini Kahama anayedhaniwa
kuwa ni mchuna ngozi amekutwa na maneno
katika makalio yake.
“I love KINDO”.
Huu ulikuwa mwangaza tosha, watu wale
wakatoweka pale upesi na kukubaliana kukutana
katika nyumba ya makamu mwenyekiti wao
baada ya muda mfupi.
“Huyu naye….” Mwanamke aliuliza huku
akimtazama Inspekta John
“Mfunge tu asije akatusumbua baadaye…”
mwanaume alijibu, John hakuelewa walimaanisha
nini. Alimtazama yule mwanaume ambaye
anamfahamu vyema akitegemea huruma yake
lakini haikuwa hivyo.
Baada ya nusu saa Inspekta John akiwa amevua
suruali yake na kuitupia begani huku shati lake
akilichomekea katika kibukta kifupi alichovaa,
alitoka mle ndani akiwa anacheka tu.
Mlinzi alimuona kuanzia mbali…. Hakutaka
kulisubiri lile balaa. Akajificha aweze kuona ni
kitu gani kinamtokea yule mbwana mjivuni wa
cheo.
Kupitia alipojificha alimuona Inspekta akilipita
gari lake na kuendelea kwenda mbele akiwa
anacheka vilevile kama alivyotoka.
****
Ulikuwa ni mwezi mtukufu wa Ramadhani, mwezi
maalumu kwa ajili ya mfungo wa takribani mwezi
mzima kwa ajili ya toba kwa dini ya kiislamu.
Waziri mkuu mstaafu ambaye pia alitajwa sana
kuwa ni mtarajiwa katika kugombea nafasi ya
uraisi baada ya miaka minne alikuwa chumbani
kwake huku nje kukiwa na mamia ya wananchi
ambao walikuwa wamekuja kufturu. Ilikuwa
kawaida ya bwana huyu kufanya jambo hilo kwa
wanachi si chini ya miamoja kwa siku. Tangu
mfungo ulipokuwa umeanza.
Kwa siku nyingine alikuwa akiungana nao na kula
pamoja lakini siku hii hakuonekana kabisa, hadi
alivyoingia baadaye sana na kuwapungia mkono
tu huku akionekana kuwa mwenye haraka sana.
Baada ya muda ugeni mwingine ulifuata, akaingia
diwani wa kata yao na mwanaume mwingine
ambaye alisemekana kuwa atakuwa meneja
kampeni wakati wa uchaguzi.
Hayo yote yeye mwenyewe muheshimiwa
hakuwahi kuyathibitisha na kila alipoulizwa
alicheka tu na kusema watu wasubiri muda.
Ndani ya chumba kimoja, watatu hawa
walikutanika na kuhakikisha chumba kimefungwa
kabisa.
“Nshomile….. weka mipango mezani sasa.”
Muheshimiwa waziri mkuu mstaafu Kimune Mune
alimuuliza mwenzake. Yule diwani akakaa vyema
akisubiri Nshomile aweze kuzungumza.
“Mipango iliyokuwepo ya mimi kumuagiza
marehemu ndani ya lile gari, tulitaka kumridhisha
muwezeshaji ili aweze kuingia katika vita hii na
atusaidie kutukamatia huyo Rensho na ku…”
“Mshomile hayo yamepita tayari tuweke mkakati
wa usiku huu huu ikiwezekana….” Diwani
alimkatisha Nshomile ambaye ni baba mzazi wa
Rensho.
“Hapa la msingi zaidi ni kwenda Kahama…
tukimpata huyo binti mwenye alama ya Kindo
makalioni lazima atatueleza Kindo yupo wapi,
tukimpata Kindo lazima tu atatuelekeza ni wapi
Salome yupo, akikamatwa yule ni kuondoa kile
kiumbe tumboni, kwisha habari yake Rensho
hapo…. Mtoto mdogo kama yule anatusumbua
hivi..” alitoa maelezo yake kwa kujiamini kabisa.
“Na kile kibwana Inspekta umekifunga vizuri
kweli asije akatuharibia, si unajua ninavyojulikana
mimi.” Kimune Mune, waziri mkuu mstaafu
alihoji.
“Magazeti ya kesho kutwa zitawekwa picha zake
nd’o utajua kama bado ni inspekta ama ni mtu
wa kupelekwa Milembe huko akakae na vichaa
wenzake.” Mzee Nshomile alijibu kwa nyodo huku
akiachia tabasamu hafifu.
“Haya tuna masaa kadhaa ya kufanya jambo hili,
mke wangu nimemwambia hatuhitaji usumbufu
tuna kikao cha muda mrefu..kwa hiyo
tunaondokea hapa na tutarudi wote kukutana
hapahapa. Tunaondoka sasa!! Tukumbuke kuwa
tukifanya mzaha, IKULU tunaikosa na hicho kitoto
tulichokilea sisi kitatuabisha hadharani!!” Waziri
mstaafu aliamuru. Kila mmoja akajiandaa na
kutoweka katika njia walizozijua wao.
Majira ya saa tano usiku walikuwa mjini Kahama
wakirandaranda huku na kule. Waligawana
sehemu za kufanyia msako ule usiku. Kwa nguvu
zao za maajabu kila mmoja akiwa na jina Kindo
mkononi akilisaka ni wapi lilipo.
Hawakuchoka watatu hawa licha ya kuruka hapa
na pale bila mafanikio, hatimaye katika kitongoji
cha Nyahanga nje kidogo ya eneo la kahama
mjini. Diwani mwanamke alihisi Kindo
aliyoiandika ikivutana kuelekea mahali,
akaifuatisha hadi katika bonde moja, akashuka
huko kwa kasi akalifukuzia windo lake, mbwa
walibweka sana lakini hakuwajali.
Hatimaye akafikia mahali na kukuta mtu akiwa
amejifunika.
Akamfunua haraka. Ana kwa ana akakutana na
mwanamke mwenye ujauzito unaoonekana
waziwazi, alikuwa amelala mithiri ya mtu
aliyepoteza fahamu ama amekufa kabisa.
Alianza kumtikisa kwa nguvu bila mafanikio,
hatimaye akamfunua nguo zake akamgeuza
nyuma… kwa utulivu kabisa kayaweka macho
yake sawa akisaidiwa na ile mbalamwezi
iliyokuwa inang’ara haswa. Akalisoma jina Kindo
katika makalio ya yule dada..
“Maskini na kimimba chake….” Alijisemea yule
diwani mwanamke huku akimvisha tena mavazi
yake.
Sasa naondokaje naye wakati amezimia sijui
amelala!! Alijiuliza.
Katika hoteli waliyolala Kindo na Rensho ile simu
ikalia kumaanisha kuwa muda ulikuwa umefika.
Kindo akamtikisha Rensho kidogo tu akaamka na
kuruka kisha akasimama wima.
“Shenzi taipu wamenisogelea wajinga hao….
Wamenisogelea….. wapo wapo….” Alihamanika
Rensho kisha akaufungua mlango na kutoka nje.
Huku nje alikimbia kidogo kisha akatoweka
kabisa.
Sekunde kadhaa akawa katika jalaa lililokuwa
bondeni kabisa.
Yule diwani akiwa anajihangaisha kumwamsha
Salome pale chini.
Rensho akawasili na hakuwa na wakati wa
kupeana salamu, akaruka hewani na kumchapa
teke kali la shingoni yule diwani. Hakumpa nafasi
ya kujibu mapigo wala kufanya sala yao haramu
ya kupotea kimiujiza. Akaruka tena na
kumchabanga ngumi kinywani, diwani akatema
damu. Akayumba na kumwangukia Salome
ambaye wqakati huu alishtuka na kusimama
wima, akabaki kuduwaa akishuhudia wanawake
wawili usiku wa giza kama ule wakipigana
makonde.
Rensho akataka kumuwahi Salome lakini diwani
naye akajirusha na kumkamata miguu yote miwili
Salome akatua chini kama gunia. Diowani
akamrukia na kumkata kofi kali sana la
mgongoni, Rensho akajikunja kwa maumivu na
hapohapo akafanikiwa kuutoa mguu mmoja
akaurudisha juu kisha ukatua katia sikio la yule
diwani. Diwani akalegea na kumwachia yule
binti….
“Mlinionea vya kutosha shenzi zenu!!” akasema
Rensho huku akiangaza ni wapi Salome yupo
tena.
Hisia hazikumpa kabisa.
Laiti kama angejua kuwa Salome ana maandhishi
yale, wala asingekawia kumtia mikononi. Lakini
hakujua juu ya hilo.
Hasira za salome kumponyoka mikoni mwake
akarejea kuzimalizia kwa yule diwani. Akamkaba
shingo yake kwa nguvu kisha……kisha akaikaba
hirizi yake na kuichomoa kwa nguvu zote.
Nshomile na waziri mstaafu wakatambua kuwa
hali si shwariu. Homa ya jiji Rensho ameharibu
tayari.
Kila mmoja akakimbia kivyake.
Majira ya saa tisa na nusu usiku walikuwa ndani
ya kile chumba.
Chini ulikuwepo mwili wa diwani wa kata.
Alikuwa maiti tayari.
Nshomile na waziri mstaafu, walikodoa macho tu
wasiamini kile walichokuwa wanakiona!!
KIZAAZAA!!!
 
SEHEMU YA KUMI NA TISA
Hasira za Salome kumponyoka mikoni mwake
akarejea kuzimalizia kwa yule diwani. Akamkaba
shingo yake kwa nguvu kisha……kisha akaikaba
hirizi yake na kuichomoa kwa nguvu zote.
Nshomile na waziri mstaafu wakatambua kuwa
hali si shwariu. Homa ya jiji Rensho ameharibu
tayari.
Kila mmoja akakimbia kivyake.
Majira ya saa tisa na nusu usiku walikuwa ndani
ya kile chumba.
Chini ulikuwepo mwili wa diwani wa kata.
Alikuwa maiti tayari.
Nshomile na waziri mstaafu, walikodoa macho tu
wasiamini kile walichokuwa wanakiona!!
KIZAAZAA!!!
MASAA MANNE YALIYOPITA!!
JIJINI DAR!
NAFSI ya mama Magege mke wa waziri mkuu
mstaafu hakuwa na amani kabisa. uvumilivu
wake alihisi unamponza.
Wasiwasi ulioishi katika nafsi yake, kwa siku hii
ulikuwa juu zaidi.
“Mume wangu na huyu diwani wana ajenda gani
ya siri eeeh!!” alijiuliza huku wivu ukichukua
nafasi kubwa zaidi.
Alijigalagaza kitandani lakini hakupata usingizi.
“Yeye si ndo mume wangu…… nataka kujua ni kitu
gani hicho wanachozungumza ambacho mimi
sitakiwi kujua. Kama ni siasa mbona alipokuwa
waziri tulikuwa tunaandamana kila sehemu?”
alijiuliza tena safari hii kwa sauti huku akirusha
miguu yake na kulivuruga shuka.
Uvumilivu ukakomea pale akasimama wima na
kuelekea katika chumba ambacho mumewe
alikiita cha siri, kwa ajili ya kuzungumza mambo
nyeti kabisa ya kisiasa ili aweze kuingia ikulu
baada ya miaka minne.
“Ikulu unataka kwenda unapanga mipango na
diwani? Upuuzi huu wasinifanye mjinga mimi…na
yule mzee Nshomile..macho yake yamejaa uongo
uongo tu…shenzi kabisa…” aliwaza huku akipiga
hatua kukielekea kile chumba.
“Mh! Lakini akinishtukia itakuwaje doh!
Watanidharau eeh!! Wivu wa uzeeni huu…..
mwee!!” alijionya wakati anataka kuyumbisha
mawazo yake.
Lakini nafsi nyingine ikamshinikiza aende liwalo
na liwe.
“Wakinishtukia nazuga kuwa nilikuwa naenda
stoo!!” Mama Magege akapata cha kuongopa
iwapo atafumwa akiwa karibu na eneo hilo
ambalo waliliita eneo la faragha kuu ya kisiasa.
Uoga ulimuingia kadri alivyozidi kukisogelea kile
chumba….awali alitegemea kusikia majibizano
baina ya watatu hao walioingia katika kile
chumba. Lakini ajabu ukimya ulikuwa wa kutisha
sana.
Ilikuwa yapata saa saba na dakika kadhaa za
usiku.
Hatimaye akakifikia kile chumba. Kwa
kumbukumbu zake ni kuwa mle ndani hakuna
godoro wala kitanda zaidi ya makochi na meza
kubwa.
Ukimya huu!! Wanafanya nini? Alijiuliza. Huku
akiwa ametega sikio lake mlangoni.
Hata kukoroma hamna? Alijiuliza.
Pepo la wivu likasemezana naye kuwa mumewe
yupo anafanya mapenzi na diwani!! Ujasiri wa
kufungua mlango kisharishari kwa nia ya
kufumania ukamuingia.
Akausukuma mlango…..
Mlango ukagoma kufunguka. Akajaribu kushusha
kitasa.
Hapo ukakubali amri, akasukuma kwa nguvu!!
Kimya!! Hakuna mshtuko wowote.
“Ahaa!! Wananichezea kamchezo eeh!! Kuna
mlango mwingine wamejitengenezea kwa ajili ya
kufanya uasherati wao. Wanapita bila mimi
kujua… pumbavu!!!” alihamaki mama Magege,
akaanza kusaka mlango huo wa ziada. Alihaha
huku na kule bila mafanikio. Hapakuwa na tundu
wala mlango wowote wa ziada.
“Washenzi hawa wamenipitaje hawa eeh!!
Magege umepita wapi wewe na wanaharamu
wenzako??” alijiuliza huku akifunga kanga yake
vizuri. Akatoka nje kuchungulia ni kwa namna
gani wangeweza kutoka bila yeye kujua.
Hakuiona hiyo namna.
“Tutaona nani mjanja leo…..” alizidi kuhamaki na
kuamua kufanya jambo ambalo baadaye liligeuka
kuwa mshikemshike na mwanzo wa kufumbuka
macho yake.
Mama Magege akaamua kujificha nyuma ya nlile
kochi kubwa kabisa ambalo aliamini kuwa hawezi
kuonekana. Aliamua kufanya hivyo ili aweze
kumuumbua mume wake.
Akajituliza pale bila kukata tamaa aliamini fika
kuwa watarejea kabla hapajapambazuka na
kuzuga kuwa walikuwa katika chumba hicho kwa
muda wote ule.
Subira yavuta heri!!
Naam! Ukafika wakati wa kupata matokeo ya
subira….
Ile subira ikaleta shubiri!!!
Kitu kikaanguka kwa nguvu ndani ya kile chumba
na kiza kikatanda ghafla.
Mama Magege kule alipojificha akatokwa na
mayowe bila kutarajia huku akijikurupua kutoka
mafichoni.
Alihaha huku na huko, hofu ikamfanya ausahau
hata mlango ulipokuwa.
Akaituliza akili yake na kujiona mpuuzi wa
mawazo kutokana na alichokuwa akikifikiria.
“Naogopa nini sasa?” alijiuliza……
Lakini kupitia dirisha akaona mwanga nje…
“Mbona umeme upo sasa halafu hu….” Kabla
hajamalizia kauli yake chumba kikapata mwanga.
“Au kuna shoti…” alijisemea tena na jicho lake
likahama hadi sakafuni.
“Mamaweeeeeee!!” alipiga makelele kwa sauti ya
juu sana. Alikuwa anatazamana ana kwa ana na
mwili uliokuwa uchi huku ukivuja damu. Mwili wa
Diwani!!
Nguvu zikamwisha mwilini!!
Akalegea na kujikuta akiketi pembeni ya ule mwili
akiwa hana la kufanya.
Ghafla likatokea jingine kubwa!!
Hajui kama walitoka ukutani ama walitoka darini!!
Mume wake mpenzi na mzee wa kuitwa Rensho
walitokeza ndani ya kile chumba wakiwa uchi wa
mnyama!!
Wakatazama jicho kwa jicho!!
Mama Magege akapoteza fahamu wakati waziri
mstaafu na Nshomile wakitumbua macho.
Rensho alikuwa amezua balaa haswa!!!
****
KAHAMA!
Chumba cha hoteli wilayani Kahama, Getonga
akiwa amefanikiwa kupata lepe la usingizi
alishtukia akiangukiwa na kitu kizito kifuani.
Akajaribu kujigalagaza huku akipiga kelele lakini
akaishia kupiga kelele katika kifua chake.
Alikuwa amezibwa mdomo!!
Na hata amacho yalipopata ufahamu vyema
alitambua kuwa alikuwa ana kwa ana na
mwanamke mwenye macho mekundu na hasira
kali.
Alikuwa ni Rensho!!
“Salome kanipotea…dakika mbili nimemuona na
dakika mbili baadaye kapotea… tunafanyaje
sasa… na wale wajinga wanamsaka…”
alizungumza Rensho. Na wakati huo aliuachia
mdomo wa Getonga.
Getonga akashusha pumzi kwa nguvu!!
“Sasa mbona umenivamia hivi Rensho hujui
naweza kufa….”
“Heri yako unayewaza kufa. Mimi nawaza
kufufuka sasa. Nataka kurudi katika asili yangu!!”
alijibu Rensho huku akikaa kitako.
“Halafu ukiogopa unafanana na kile kitoto chako
aisee!!” Rensho aliongezea huku akikaa vyema
katika kitanda.
“Yah! Tunafanana sana….” Alijikaza Getonga na
kujibu.
“Tunafanyaje juu ya kumpata Salome.” Akawa
makini tena Rensho na kuuliza.
Getonga akatulia kwa muda kisha akajibu
awezavyo.
“Ren.. mimi ninachofahamu juu ya Salome ni
kwamba ni binti ambaye alikuwa safarini,
akatekwa kisha kubakwa na vijana wawili kati ya
watatu waliomteka. Yule kijana ambaye
hakufanya huo unyama ndo alinisimulia.
Walipomaliza wakamtupa katika korongo moja ili
afe kama walkivyokuwa wameagizwa na mkuu
wao…. Baada ya hapo sijui lolote kuhusu Salome
ndugu yangu. Yaani vinginevyo mimi unanionea
tu….” Alijieleza kwa huzuni kuu.
“Mh! Huu ni utata mkuu na ni hatari kwangu na
hatari kwako. Wewe usiseme nakuonea wakati
umefanya njama ukachukua kitambulisho
changu…. Ok! Tunatakiwa kuangalia namna ya
kuiepuka hii hatari, kwangu mimi si tatizo kurudi
kuwa mtumishi wao lakini wewe watakuua na
familia yako yote…..” alikoma kidogo na
kuutazama uso wa Getonga jinsi ulivyotaharuki.
“Tunatakiwa kushirikia katika kumbukumbu hizi
walau tujue jambo moja ama mawili juu ya
Salome. Tukishayajua hayo tu basi huu mchezo
tunaumaliza mara moja kinabaki kitambulisho
tu…. Tena tunatakiwa kuwa makini kabla yule
bwege wa kuitwa Nshomile hajampata Salome.
Yaani akimpata tu, jiandae kufa kikatili kwa
kuchommwa moto kiungo kimoja baada ya
kingine…aisee majamaa yanaua vibaya yale kaka
yangu. Yaani yanakata mkono yanauchoma,
yanakata kamguu yanachoma…” Rensho
akamaliza kwa kucheka cheko la kupendeza,
wakati Getonga alikuwa ametumbua macho yake
kwa hofu kuu.
“He! Unakodoa mimacho…nd’o hivyo
wanavyokuua……” akamnaga, kisha akabadilika
tena, “Ok! Kaka, usiku huu tunatakiwa kufanya
jambo….unatakiwa uni’busti’”
“Ku’busti’ nd’o nini jamani…” aliuliza kinyonge.
“Unibusti nikumbuke walau mambo kadhaa juu ya
huyo Salome….”
“How..”
“Umesema?” Rensho akahoji….alikuwa hajaelewa
lugha iliyotumika.
“Aaah! Namaanisha kiaje sasa.”
“Kirahisi tu na vigumu vilevile…..” akavuta pumzi
kidogo kisha akalalamika kuwa anahisi njaa, kisha
akaendelea “Unatakiwa kufanya mapenzi na
mimi……” akasita tena na kumtazama Getonga
usoni.
“Usishtuke kusikia mapenzi, lakini unatakiwa
kuwa makini nikupe maewlekezo. Wakati
unafanya mapenzi na mimi sharti ni moja tu,
hakikisha unanisikiliza nitakachokuwa nasema na
ukinukuu..huo nd’o utakuwa mwanga wetu, hivyo
hutakiwi kunifanya kama mkeo ama hawara yako
yoyote yule, na kujikuta ukipoteza akili yako yote
usijue ni nimezungumza nini…..” Rensho
akashusha pumzi na kuweka kituo akimsubiri
Getonga aseme lolote.
Getonga alikuwa amepagawa kiakili, akaikumbuka
ndoto ya Maria kuwa anaota mtu anatokwa
damu, akakikumbuka kifo cha Inspekta Kisembe
kufa huku akivuja damu baada ya kutoka
nyumbani kwa Maria, kifo cha Sam nacho
kikamchanganya, Don na Dulla walikufa kwa
kuvuja damu…bila shaka baada ya kutoka
kufanya ngono. Sasa anaambiwa ashiriki katika
ngono na mtu huyu.
Hofu, uoga na kila aina ya mawazo ikamtawala
kijana huyu mwandishi maarufu anayesakwa jinni
Dar kwa kosa la kutoroka rumande alipokuwa
akikabiliwa na kesi nzito ya kushirikiana na
majambazi huku gari yake ikikutwa na silaha za
kivita.
“Aah! Rensho mbona sasa hiyo ngumu jamani..”
“Ok! Basi nadhani ni rahisi kufa kile kifo
nilichokwambia…..usiku mwema mi nalala.”
Rensho akajibu kwa jazba kisha akageukia
upande mwingine.
Nimeyakoroga!! Alijisemea Getonga huku
akijiuliza lipi ni sahihi.
Kubembeleza!! Ni hili aliliona sahihi zaidi.
Akaingia katika zoezi hilo.
“Ren, nahisi hujanielewa tu, unajua kabisa sitaki
kufa na sitaki kushuhudia familia yangu ikifa
namna hii. Nilichokuwa nataka ni walau kuuliza
maswali mawili matatu, halafu ukinijibu tu
tunafanya utakavyo kwa manufaa yetu!!”
alizungumza kwa sauti iliyojaa ushawishi.
“Hapo sasa umenena…. Neno moja lenye maana.
Haya uliza?”
“Ni madhara gani nitayapata nikikosea masharti.”
“Utakufa kwa kuvuja damu!!” Rensho alijibu kama
suala la kawaida kabisa. kisha akamalizia “kisha
nami nitapata ujauzito usiokuwa na kikomo
utanitesa hadi nitakaposalimu amri… kitu cha
msingi kuwa makini…na kwanini ujiandikie
kukosea wakati nimeshakueleza??”
Getonga alikuna kichwa, maji alikuwa ameyavulia
nguo tayari hakuwa na haja ya kuyaogopa. Aidha
yawe machafu ama masafi ni lazima ayaoge tu.
Kichwani mwake kilichomchanganya ni ule uzuri
wa Rensho.
Je? Ataweza kujiongoza akili yake, ule uhondo na
kusikia maneno atakayosema.
Kitanzi kilikuwa katika kichwa chake na chaguo
pia lilikuwa ni lake!! Aidha kujiua ama kukitengua
kitanzi kile.
Mtihani mkubwa sana!!!
Wakati anawaza haya, Rensho alizitoa nguo zake
zote na kulala chali kitandani,.
Ebwana wee!! Matiti kifuani hayakujua nini
maana ya kulala tangu yasimame yalikuwa
vilevile, rangi yake ya chungwa iliyafanya na
yaonekane kama chungwa lakini katika mfano wa
embe dodo, kile kiuno kilikuwa mahali pake na
kilibeba lile tumbo dogo la Rensho katika namna
ya kipekee huku mapaja ya wastani yakishangilia
hali ile. Chini ya magoti alikuwa na michirizi
fulani kama iliyoleta ukijani ukichunguza kwa
mbali. Michirizi ya huba.
Getonga akaupandisha uso na kuufikia uso wa
Rensho, akakuta binti yule akiwa amefumba
macho na kutoa tabasamu mwanana.
Maungo katika nguo ya Getonga yakaanza fujo,
akaanza kusahau kama walichotaka kufanya
kilikuwa ni tiba.
Akatamanika kingono.
Akaupeleka mkono na kumpapasa, ule ulaini wa
ngozi ambayo hakuwahi kuiona ikipakwa mafuta
ukamsaatajabisha!!
Rensho alikuwa na kila kitu kinachomfanya
aweze kuitwa mrembo.
“Hata mama Eva hapa haingii ndani!!” Getonga
alikiri huku unafiki akiweka kando…..
**GETONGA katika mtihani…. Anatakiwa
kum’busti’ RENSHO…..
Akikosea masharti tu… wamekwisha!!!!
ITAENDELEA…
 
SEHEMU YA ISHIRINI
etonga akaupandisha uso na kuufikia uso wa
Rensho, akakuta binti yule akiwa amefumba
macho na kutoa tabasamu mwanana.
Maungo katika nguo ya Getonga yakaanza fujo,
akaanza kusahau kama walichotaka kufanya
kilikuwa ni tiba.
Akatamanika kingono.
Akaupeleka mkono na kumpapasa, ule ulaini wa
ngozi ambayo hakuwahi kuiona ikipakwa mafuta
ukamsaatajabisha!!
Rensho alikuwa na kila kitu kinachomfanya
aweze kuitwa mrembo.
“Hata mama Eva hapa haingii ndani!!” Getonga
alikiri…..
Getonga akaiamuru akili yake kufanya kama
ilivyoagizwa, akaanza kumpapasa Rensho huku
akiwa ameiondoa tayari bukta yake.
Wakati anamkumbatia ndipo akakutana na
utofauti wa Rensho na ule wa mkewe mpenzi
‘mama Eva’.
Rensho hakuwa na joto hata kidogo, alikuwa wa
baridi sana.
Nimelala na maiti!! Alijisemea Getonga huku
akizidi kuzilazimisha hisia zake zisishuke kwa ni
kwa kushuka hisia asingeweza kufanya lolote.
Hatimaye akalifikia eneo husika!!
Loh! Rensho alikuwa bado bikira…..
Getonga akastaajabu, lakini hapo hapo
akakumbuka kuwahi kumsikia Kindo akidai kuwa
yule Rensho aliwahi kufa na kuzikwa akiwa na
miaka kumi tu. Lile wazo la kuwa analala na
maiti likajirudia tena, lakini akaendeleza jitihada
za kufanya kama alichoagizwa wakati huu
alilazimika kufumba macho na kuvuta hisia za
kuwa na mkewe kitandani!!
Rensho alikuwa hafanyi miguno wala hisia zozote
zile, ni kama hakuwepo pale kabisa kimwili.
****
Jijini Dar es salaam, mheshimiwa waziri mkuu
mstaafu na mwenzake mzee Nshomile wakiwa
wako uchi wa mnyama waliamua kufikia
maamuzi baada ya fumanizi lile ambalo
lilimaanisha kuwa siri zao zote zilikuwa nje
hatimaye. Na ilikuwa hatari sana kwa jambo hili.
Waziri mstaafu akaamua kumnyamazisha mkewe
kwa namna waliyojua wao ndani ya kile chumba
huku akitoa wazo la kumtafuta huyo mtu wa
kuitwa Kindo.
“Tunaanzia wapi kumpata sasa…” aliuliza mzee
Nshomile. Waziri msaafu akamwonyesha ishara
kuwa wanatakiwa kuondoka.
Nshomile akatii amri….
Wakatoweka na kuacha miili miwili ndani ya
chumba, mke wa waziri mstaafu na diwani
ambaye alikuwa ametokwa uhai tayari.
DAKIKA TANO BAADAYE!!
SAA KUMI ALFAJIRI.
Waziri mstaafu na mzee Nshomile walikuwa
katika wodi moja wapo ndani ya hospitali ya taifa
ya Muhimbili. Waliingia pale na kuruhusiwa muda
ule kutokana na heshima kubwa aliyokuwanayo
mheshimiwa waziri mstaafu.
Mavazi yao ya suti yalipendeza haswa.
Kwa waliowaona walinong’onezana kuwa harakati
zote zile ni kwa sababu mheshimiwa anataka
kuingia ikulu baada ya miaka kadhaa hivyo
alikuwa katika kuisaka hali ya kushawishi umma
ili apigiwe kura wakati wa uchaguzi mkuu.
Hawakujua kuwa walikuwa na lao jambo!!
Walipofika mapokezi waliomba kumwona
mgonjwa aliyefikishwa hapo masaa machache
yaliyopita aendaye kwa jina na John na cheo cha
Inspekta.
Inspekta John Magege, ambaye vyombo vya
habari usiku ule vilidai kuwa alikutwa akizurura
akiwa na mavazi yake begani.
Ikasadikika kuwa ni Malaria kali ilikuwa
imempanda kichwani.
Heshima ya waziri ikawapitisha tena bila kikwazo,
licha ya muuguzi kudai kuwa mgonjwa alikuwa
amechomwa sindano za usingizi. Walilazimisha
wakaingia baada ya mheshimiwa kumpigia simu
IGP ambaye alikuwa ni swahiba wake, IGP
akawapa ruhusa.
Kweli walimkuta akiwa amelala kiutulivu sana.
Katika wodi ile alikuwa yeye ndiye mgonjwa
pekee.
Waziri hakupoteza wakati, akaketi pembeni ya
kile kitanda kisha akamshika kichwa Inspekta
John ambaye hakuwa katika fahamu zake.
Akaanza kumuuliza maswali kadha wa kadha
hasahasa juu ya muonekano wa Kindo na kama
aliwahi kumuona hapo kabla.
Ajabu! Akiwa katika usingizi mzito aliyajibu
maswali ipasavyo na kudai picha ya Kindo baada
ya kuwa amekumbwa na lile janga ipo nyumbani
kwake, akaelezea vyema kabisa mahali nyumba
yake ilipo.
Picha ya Kindo! Ndo kitu pekee walichokihitaji
wawili hawa maana walipomchukua mwanzo kwa
ajili ya shughuli yao iliyoingia dosari hakuna hata
mmoja aliyeikariri sura yake.
Hata mzee Nshomile licha ya kukutana na Kindo
ana kwa ana hakukumbuka kuinasa sura yake
akilini.
Hivyo walikuwa wakiihitaji kwa udi na uvumba!!
Maelezo yalipowatosha wakatoweka huku
wakimpita muuguzi aliyekuwa ameuchapa
usingizi jirani na eneo la mapokezi.
Ikiwa ni saa kumi na dakika zipatazo arobaini,
walifunga safari hadi nyumba waliyoelekezwa na
Inspekta John Magege.
Mlinzi hakuwa kikwazo kikubwa kwao,
walimnyamazisha mara moja kisha wakaingia
ndani, wakaziba sura zao ili kuondoa mlolongo
wa kuhangaika kuwanyamazisha watu ambao
walikuwa wamewatambua.
Sebuleni walimkuta mke wa John Magege akiwa
bado yupo macho. Walipoingia akataka kupiga
kelele, Nshomile akamrukia na kumziba mdomo,
kisha swali moja tu.
“Chumba cha John kipo wapi?”
Huku akitetemeka akawaelekeza, waziri akaingia
upesi na kutuliza akili kisha akaanza kuisaka ile
picha hadi alipoipata.
Picha ikamrudishia kumbukumbu juu ya Kindo.
Akaihifadhi katika suti yake kisha akatoka na
kumpa ishara mwenzake.
Wakatoka!!
Saa kumi na moja alfajiri ulikuwa ni MSAKO
KINDO.
Sura yake ikakaririshwa vyema katika akili za
wawili hawa!!
Wakagawana maeneo ya jijini Dar es salaam
kumsaka mtu anayefanana na hiyo sura ya
Kindo.
*****
Rensho alianza kulalamika dakika kumi na tano
baadaye, kisha akaanza kukoroma huku akijikunja
huku na kule. Getonga hakumuachia aliendelea
kupalangana huku jasho likimtoka.
Hakuwa akipata ladha yoyote ile kama
alivyotegemea awali, ule ubaridi ukamfanya
ajilazimishe tu kufanya alichokuwa akikifanya.
“Kindo….muhimu sana. Kindo Muhimu sana……
Kindo muhimu sana….” Rensho aliendelea kurudia
yale maneno bila kuongeza neno jingine la ziada.
Getonga akatarajia mabadiliko lakini haikuwa
hivyo, aliendelea kusisitiza kuwa Kindo ni muhimu
sana.
Ghafla akatulia tuli kama alivyokuwa awali.
Getonga naye akaacha kufanya alichokuwa
anakifanya.
Hatimaye Rensho akayafumbua macho yake
kichovu, kisha akaangaza huku na kule kama
anayetoka kuamka.
“Nini kinatokea hapa …” aliuliza huku akijitazama
na kisha kujifunika na shuka.
“Umesema KINDO MUHIMU SANA…” Getonga
akamjibu.
“Kivipi muhimu…” akauliza swali lile ambalo
lilionekana kuwa gumu kwa Getonga.
“Wewe ndiye umesema sio mimi…na hukutoa
sababu…” alijitoa katika kujua akamrushia mpira.
“Ok! Ok ok…..hao hao…..hao….wanamtafuta
oooh!! Sijui kama tutawahi aaargh wanatuua
hawa…” Rensho alizungumza peke yake lakini
akiwa na mashaka makubwa sana.
“Akina nani?”
“Washenzi walafi wa madaraka haramu.” Alijibu
kwa ghadhabu.
“Kindo anamjua Salome…..sawa…Kindo ni
muhimu sana. Kindo anajua kaburi ambalo
nilizikwa miaka kama kumi na nne iliyopita..oooo
h!! mbona tulimuacha Kindo sasa. Wanamtafuta
hawa watu, wapo jirani kumpata ona…” alizidi
kulalamika.
Jambo la kufa miaka kumi na nne iliyopita…lilim
duwaza Getonga. Akajiuliza maiti gani huyu
anaishi huku amezikwa kitambo kirefu?
Hakupata jibu!!
“Wakimpata Kindo wamenimaliza. Mimi wewe na
familia yako,,,ooh! Wabaya watu hawa…. Kindo ni
mtu muhimu sana.”
“Sasa tunafanyaje?” aliuliza Getonga kwa uoga.
“Tuondoke tukajaribu bahati.” Alitoa jibu huku
akisimama wima, Getonga naye akasimama.
Rensho akamkumbatia kwa nguvu kisha kama
walivyotoweka na kufika Kahama wakatoweka na
kuingia jijini Dar es salaam.
Walilifikia lile jumba ambalo walitokea mwanzoni
na kuingia ndani Rensho akiwa mbele na Getonga
nyuma. Moja kwa moja katika chumba alichokuea
amefungiwa Kindo.
Lahaula! Kindo hakuwepo ndani yake!
Rensho akachoka, Getonga naye akasaidiana
naye kuchoka huku akiifikiria familia yake.
Rensho alijaribu kuvuta hisia zote juu ya hili
lakini hakuifanikiwa hata kidogo kupata ufumbuzi
juu ya ni wapi alikuwepo Kindo.
“Watakuwa wamemkamata tayari….. tumekwisha
ndugu yangu. Pole sana unaenda kuipoteza
familia yako.” Rensho alimwambia Getonga
pasipo kumtazama usoni.
Getonga akabaki kuduwaa asijue ni neno gani
linaweza kuyabadili mambo haya.
Wakiwa bado wanashangaa mara ghafla kama
upepo Rensho alipokea pigo kali katika mgongo
wake. Ile Getonga anageuka kujiuliza kulikoni
mara na yeye akachabangwa kofi kali usoni.
Akayumbayumba na kukaa chini huku maumivu
yakitambaa mwili mzima.
Rensho alipojiweka sawa akakumbata na pigo
tena kali katika mbavu zake.
“Mpumbavu mkubwa wewe ulidhani siku yako
haitafika…..muonevu mkubwa wewe.” Sauti ya
kike ikakoroma kutokea katika kigiza kidogo.
Kisha ikaingia katika mwanga.
“Ulikosea sana kuamini kuwa sitakuwa na la
kufanya, hayawani wa kike wewe. Na wewe
Malaya wa kiume leo utajuta kuzaliwa..” alizidi
kuonya yule mwanamke.
“Shit!” Rensho alitokwa na kauli ya mshangao,
lakini haukudumu sana mshangao ule. Mara yule
kiumbe mwingine wa kike akajirusha juu juu aliwa
ameunyoosha mguu wake, Rensho akakinga
mikono na kupangua pigo lile, maumivu
aliyoyapata pale akakiri kuwa alikuwa
anapambana na kiumbe hatari.
“We Malaya unaniangalia kama hunijui eeh!”
Getonga akatupiwa swali na yule kiumbe.
“Rensho huyu nanmi sasa…”Getonga akamuuliza
Rensho ambaye alikuwa ameanguka jirani kabisa
na mahli alipokuwepo yeye.
“Anaitwa Queen huyu ni….”
“Alaa! Nd’o huyu…” Getonga akastaajabu na hapo
akazikumbuka picha ambazo kumbe huyo aliwahi
kumrushia azitazqme huku akidai kuwa
ulimwenguni alikuwa msichana mrembo sana.
Kisha akalikumbuka ombi la yule kiumbe ambaye
wakati wanakutana alikuwa na mguu mmoja huku
akitokwa na harufu kali, pia hakuwa na sikio.
Sasa alikuwa mrembo haswa, na alikuwa na kila
kiungo chake.
“Mbona sasa ana mguu..”
“Bwege amejibusti na Kindo huyu hapakuwa na
mwanaume mwingine hapa…nilifanya makosa
kumwacha Kindo hapa. Eeeh!! Tumekwisha sisi,
anajua udhaifu wangu huyu atanisumbua sana.”
Rensho alijilaumu huku akiwa hajajua ni kitu gani
afanye.
“Wanaume ni washenzi sana nyie, washenzi wa
kutupwa. Na wewe Rensho ukaona kwamba
nitafaidi sana kuzaa na huyu bwana ukaamua
uondoke naye… sasa ngoja nikuonyeshe tofauti
yetu…” akasita kisha akageuka nyuma.. “Kin…..
Kindo wee!” akaita kimahaba.
Na hapo akaingia kijana nadhifu haswa, kiatu
chake kikiwa katika mng’aro mahsusi kabisa na
alikuwa akitabasamu.
Akafika na kujiweka ubavuni mwa Queen.
Rensho na Getonga wakatumbua macho yao.
“Mtabaki huku kwa wafu sisi tunaondoka na
kurejea ulimwenguni.” Alisema kwa nyondo.
Rensho akanyanyuka kwa hasira na kumvamia
lakini akakutana na ngumi nzito ya begani
akapiga mayowe na kumwangukia Getonga pale
chini. Kisha Quue akamrukia tena kwa nguvu
zote na kumchabanga teke kali gotini. Rensho
akapiga mayowe makali.
“Umenivunjaaaaa!!”
“Huniwezi Rensho wewe ulikuwa wa wakati ule….
Na bado nitavunja na hicho kichwa” Alitamba
huku akiufuta mkono wake uliompiga ngumi
Rensho.
“Bila kitambulisho sitamuweza tutakufa….tutak
ufa tu!!” Rensho alimnong’oneza Getonga huku
damu zikimbubujika mdomoni,
“Kwa hiyo….”
“Ngoja tuone anataka kutufanya nini…” alisema
kwa kukata tamaa
Ilikuwa yapata saa kumi na moja na dakika
hamsini za asubuhi ambapo mambo yalibadilika
tena.
Ndani ya lile jumba akaingia kiumbe mwenye
hasira kuu, Queen akiwa hajui lolote mara
akachapwa teke la mgongoni akayumba kidogo
na kutaka kujiweka sawa mara akachapwa ngumi
kali ya uso akabaki kuona maluweluwe.
Punde Kindo akasikika akipiga kelele.
Getonga na Rensho waliokuwa wamekaa chini
wakawashuhudia wanaume walioziba nyuso zao.
Baada ya udhibiti huo, wakazifunua nyuso zao.
Alikuwa ni waziri mkuu mstaafu na aliyemdhibiti
Kindo alikuwa ni baba yake mzazi na Rensho.
Mzee Nsomile!!
Rensho ana kwa ana na baba yake!!! Rensho
alimtazama kwa hasira lakini pale alipo goti
lilikuwa halifanyi kazi na mwili ulikuwa dhaifu.
Hasira pekee nd’o ilimuongoza na kuamini kuwa
anaweza kumdhibiti yule mzee.
Lakini alikuwa na maadui watatu, waziri, baba
yake pamoja na mtumwa aliyesaliti utumwa
Queen!!
HATARI!!!
ITAENDELEA
 
SEHEMU YA MWISHO PART ONE
Baada ya udhibiti huo, wakazifunua nyuso zao.
Alikuwa ni waziri mkuu mstaafu na aliyemdhibiti
Kindo alikuwa ni baba yake mzazi na Rensho.
Mzee Nshomile!!
Rensho ana kwa ana na baba yake!!! Rensho
alimtazama kwa hasira lakini pale alipo goti
lilikuwa halifanyi kazi na mwili ulikuwa dhaifu.
Hasira pekee nd’o ilimuongoza na kuamini kuwa
anaweza kumdhibiti yule mzee.
Lakini alikuwa na maadui watatu, waziri, baba
yake pamoja na mtumwa aliyesaliti utumwa
Queen!!
HATARI!!!
Nianze na nani sasa? Alijiuliza Rensho huku
akimlaani Queen kwa lile pigo ambalo lilitawanya
goti lake na kumfanya ashindwe kusimama.
Akapiga kite cha ghadhabu kuhu akiangaza
macho huku na kule kama kuna namna ya
kuweza kujinyofoa kutoka katika mikono ya watu
wabaya.
“Laiti kama mguu ungekuwa unafanya kazi
ningeweza hata kukimbia……lakini aah!! Huyu
kaka na familia yake wangekufa vibaya.” Alizidi
kuwaza na kuwazua.
Akiwa hajapata jibu sahihi, mara mzee Nshomile
alimpiga Kindo kwa kutumia kiganja chake
maeneo ya shingoni, akalainika na kupoteza
fahamu. Kisha akamfuata Rensho na kusimama
mbele yake.
Ili kuthibitisha hasira kali aliyonayo mbele ya yule
binti akamuuliza swali moja.
“Mimi nani yako?” akahoji kwa hasira.
“Sikufahamu.” Rensho alijibu kwa jeuri huku
akijua fika kuwa yule ni baba yake.
Mzee Nshomile bila kusogeza hatua nyuma
akanyanyua mguu wa kulia akamtishia kama
anamchabanga usoni. Rensho kwa kutumia
mikono akajaribu kuzuia lakini ghafla ule mguu
ukatua katika goti lililosambaratishwa na Queen.
Rensho akapiga mayowe makali ya kutangaza
maumivu.
Tendo lile la yule mzee kumsaga Rensho gotini
likamtia hasira Getonga akafanya kujitingisha
kidogo ili kutetea usalama wa Rensho lakini pale
pale alikatwa kofi kali ya usoni, uso ukawaka
moto na sekunde kadhaa mbele akaanza kutokwa
damu puani.
“Mwanadamu mpumbavu wewe hauna la kutuzuia
sisi…dunia hii ni yetu!” Waziri mstaafu ambaye
alikuwa amemdhibiti Queen alisema kwa kejeli.
Getonga akanyanyua macho yake
wakagonganisha na yule waziri mstaafu.
“Whaaat…Gerlad Getonga Mosenya….. son of the
bitch!!” akawaka kwa hasira yule mzee, Getonga
naye akaduwaa hakutegemea kuwa yulew
angeweza kuwa waziri mkuu mstaafu. Waziri
ambaye aliwahi kuingia katika mzozo na gazeti
ambalo Getonga alikuwa akiandikia makala.
Makala iliyomponda sana kuwa ni mbadhlifu wa
fedha na maamuzi yake hayajanyooka, makala
ambayo iliwapa nafasi wapinzani kukidhoofisha
chama tawala.
Mafahari hawa wanakutana katika dunia nyingine.
Ni aidha Getonga atoke hai na kwenda kuandika
makala kuwa raisi mtarajiwa ni mshirikina
amaafe ili kila kitu kiende salama.
“Njoo umshike huyu…mdhibiti kabisa” Waziri
alimwamuru Nshomile naye akatenda vile mara
moja.
Waziri akawa huru, akamsogelea Getonga
ambaye alikuwa akivuja damu bado.
“Ulikuja huku pia kuchukua habari eeh!” Waziri
alimdhihaki, kisha akaendelea, “ulinichafua
magazetini enzi nikiwa waziri…nasikitika kuwa
licha ya kukutanishwa na kupatanishewa ni
kwamba hadi leo sijawahi kukusamehe nina
hasira na wewe na leo nitazimisha ndoto zako
zote ulizonazo mshenzi wewe.” Alizungumza kwa
ghadhabu huku akiwa ameikaba shingo ya
Getonga.
Na kwa kitendo cha sekunde chache tayari
alikuwa amemchapa makofiu mawili makali.
Damu ikazidi kuvuja huku Rensho akiishia kuumia
tu asiweze kumsaidia Getonga.
“Babaaaa!” sauti ya mtoto mdogo ilisikika ikiita,
matukio yote yakasimama.
Masikio ya Getonga yakatambua kuwa huyo ni
Anitha alikuwa amesikia kilio chake kikuu cha
maumivu.
“Nani huyo?” Waziri alimuhoji Nshomile.
“Kama ni mwanadamu nyonga mara moja…”
alitoa amri Waziri . nshomile akiwa amemkaba
Queen alikubali alichoelekezwa na wakaongozana
kwenda sauti ya mtoto ilipotokea.
Queen alikuwa akimchukia Getonga lakini
hakuwahi kumchukia mkewe na hasahasa yule
mtoto, alimpenda sana.
Ile amri ya ukikamata nyonga ilimshtua na hasira
zikampanda hakuwa tayari kushuhudia kifo cha
yule mtoto.
Nshomile asiyekuwa na taarifa kabisa wala
mategemeo katika lile tukio, alijikuta akimlegezea
ukabaji Queen na kumpuuzia akimchukulia kama
wanadamu wengine.
Hilo lilikuwa kosa kubwa sana kwa mzee huyu na
ambalo lilizua varangati.
Queen aliinama ghafla na kujitoa katika mikono
ya Nshomile, kisha upesi akakunjuka teke kali na
kumchabanga mgongo akajibamiza katika vyuma
vilivyokuwa mbele yake.
Hapohapo akamrukia tena na kumpiga ngumi ya
kisogo kali sana, mzee Nshomile akaishia kuona
maluweluwe na kuanguka chini.
Queen akamnyakua Eva (mtoto wa Getonga) na
kisha akatimua mbio….. ile anafika mlangoni
akatambua kuwa bado yeye si mwanadamu
kamili na bado anamhitaji Kindo ili aweze
kumrejesha tena katika ubinadamu. Akakata
tamaa.
“Eva mpenzi…..” akamuita yule mtoto kwa sauti
ya chini.
“Bee dada..” Eva akaitika kwa sauti ya kitoto.
“Naomba unisikie na ujaribu tu kunielewa sawa
mama eeh! Unauona ule mlango pale..”
akamnyanyua kichwa na kumuelekezea kule,
“Kimbia nenda ukaufungue na uingie ujifiche
pale, usilie wala usipige kelele hata kidogo…
naenda kumleta baba sawa eeeh!!...sawa
mamangu?” alimsihi kwa sauti tulivu ili aweze
kuelewa.
Japokuwa alikuwa mtoto yale maisha ya utata
yaliyokuwa yanaendelea katika jengo lile na kile
kilio alichokisikia kutoka kwa baba yake tyari
alitambua kuwa kuna hatari kubwa eneo lile.
Akafuata aliyoelekezwa!!
Eva akaanza kukimbia kuelekea ule mlango
ulipokuwa, Queen alimtazama vyema ili afike
kabisa na kujifungia nyuma ya ule mlango.
Tabasamu likamtoka kwa wepesi wa yule mtoto
mdogo, akaufungua mlango, ile anatak kuingia
ajifungie tu likatokea jambo ambalo lilivuruga
utaratibu.
Katoka paka katika ficho lile, Eva akapiga kelele
za uoga.
Queen akabaki kukodoa macho akimtazama jinsi
Eva alivyokuwa anatapatapa.
Kelele za Eva zikamkurupua na mzee Nshomile
kutoka pale chini, kabla Queen hajajua afanye
nini alivisikia vishindo vya mwanadamu kusogea
katika eneo lile. Akajipanga kumkabili…..
Ila mwenzake alikuwa amejipanga zaidi,
mawenge yakamkumba baada ya kupondwa na
kitu kizito kisogoni. Ile anaugulia maumivu
akashtuka akiwa amebanwa mbavu zake mbili za
chini kwa nguvu mno. Alijaribu kufyatuka lakini
hakufanikiwa…maumivu yalikuwa makali mno.
Queen akaanza kulia kama mtoto mdogo. Lakini
kama ile haitoshi akapigwa ngumi kali kiunoni,
ngumi iliyopigwa kitaalamu kwa ajili ya kuvunja
tu!
Queen akalainika na kumwangukia yule bwana
huku akiendelea kuugulia.
Mzee Nshomile akamchukua begani kama mzigo
tu usiokuwa na thamani yoyote, kisha akamfuata
Eva pale alipo akamvuta mkono kwa nguvu sana
Eva akaanza kulia.
“Mwache mtoto wangu nasema?” sauti kutoka
katika ficho jingine ikatoka, Nshomile akaifuata
kwa tahadhari akamkuta mama yake Eva
(Anitha) akiwa amefungwa kamba mikono
yake….. akamfungua na kumpa pigo moja la
kulainisha.
Baada ya dakika kadhaa kwenye ukumbi wa
mapambano alikuwepo Nshomile na mwenzake
Waziri mstaafu huku mateka wao wakiwa
wameongezeka idadi.
Rensho, Getonga, Kindo, Queen, Anitha (mke wa
Getonga), Eva (mtoto wa Getonga). Ukumbi
ulikuwa umechafuka damu. Ni Eva pekee ambaye
alikuwa havuji damu.
*****
FAMILIA nzima ilikuwa ikimtazama Getonga, naye
hakuwa na la kufanya zaidi ya kujisikia vibaya
kukaidi ushauri aliopewa na mkewe kuwa ajiweke
mbali kabisa na mambo ya uandishi wa habari za
kipelelezi kwani ni hatari kwa maisha yake.
Alimtazama Anitha mkewe akamtazama na Eva.
Machozi yakamtiririka kwa uchungu mkuu,
uchungu wa kuamini kuwa baada ya vifo vyao
kama kweli kuna mahali watakutana basi
watamlaumu bila kumsamehe kamwe.
Ni heri wakutane duniani wakiwa hai, ataomba
msamaha na maisha yao ya ndoa yataendelea.
“We kinyamkera ulidhani kuwaua wenzeti nd’o
utatoka na wewe ukiwa hai ili ukatuaibishe dunia
sivyo?” Waziri alimuhoji Rensho aliyekuwa hoi.
“Sasa utashuhudia vifo vya hawa rafiki zako
mmoja baada ya mwingine halafu wewe utake
usitake utatimiza ulichotakiwa kutimiza….na
ukileta ubishi ni kifo cha moja kwa moja…wewe
ni mtoto na utabaki kuwa mtoto tu..” Nshomile
akaongezea.
Rensho hakujibu kitu alikuwa akihema juu juu tu
kutokana na maumivu makali hasahasa ya goti
lililotawqanyika.
“Queen, tunafanyaje sasa…’ hatimaye
alimnong’oneza Queen, ambaye naye alikuwa hoi
akiwa amevunjika kiuno.
“Wangetuachia hata dakika kumi tungebusti ila
bila hivyo, naona tunateketea hapa…” alijibu
akiwa amekata tamaa.
Mzee Nshomile alimfuata Eva akamshika mkono
na kumvuta akasimama wima.
“Niue mimi umuache mwanangu hai…” Getonga
akajikaza na kusema maneno yale ya kijasiri….
Waziri mstaafu akamrukia na kumchapa ngumi
kali juu ya jicho, akachanika vibaya mno. Damu
ikaanza kuvuja. Eva akaanza kulia kwa hisia kali
za kuona baba yake akiteseka.
Waziri na mwenzake hawakujali hayo.
Na wakati haya yakitokea ilikuwa yapata saa
kumi na mbili alfajiri.
Rensho aliwatazama kwa uchungu mkubwa
majeruhi waliomzunguka, alimuonea huruma hadi
Queen ambaye alihusika katika kulisambaratisha
goti lake wakiwa katika mapambano. Alijua kuwa
wote hawana nguvu za kuwadhibiti watu wale
lakini hata yeye alikuwa dhaifu sana…..
Rensho akajaribu bahati ya mwisho kabisa huku
akijisemea nafsini mwake, iwapo hiyo nayo
itashindikana basi tena atakuwa radhi kushuhudia
vifo vya mateso kwa watu wale.
“Muulize Kindo…. Salome jina lake la kikabila ni
nani…jibu muhimu na haraka” alimnong’oneza
Queen, Queen naye akamnong’oneza Anitha,
Anitha akamuuliza Kindo aliyekuwa hoi.
“Ndema” Kindo akamjibu kwa shida huku akiwa
na dakika takribani kumi tangu arejewe na
fahamu zake.
Jibu likamfikia Rensho!!
Akayafumba macho yake. Na kisha kuzua
mtafaruku baada ya kuanza kupiga makelele.
“Ndema weee….Ndema weeeee amka
Ndema….amka…mwili hauiwezi kuishi bila roho
na hata roho haiwezi kuishi bila mwili….Ndema
weeeee Ndema njoo sasa….. amka Ndema..”
“Pumbavu unasema nini wewe..” Waziri alimtusi
kwa ghadhabu huku akimwendea kwa kasi.
Nshomile alikuwa anajiandaa kukikata kichwa
cha Eva kwa kutumia kisu kikubwa.
Upepo haukuvuma sana hadi kusababisha
milango kuvunjika. Hilo liliwashangaza wote hadi
Rensho mwenyewe.
Lakini akaamini kuwa ukweli kabisa mwili
hauwezi kuishi bila roho.
Baada ya mlango ule kuvunja katikati ya ule
ukumbi akaingia mwanadada mwenye mimba…
macho yake yalitangaza hasira kali sana, ujumbe
ulikifikia kiumbe kilichokuwa katika tumbo lake.
“Salomeeee!!: Kindo alipiga kelele huku
akijitutumua ainuke lakini yule alikuwa salome
mwili tu, akili yake ilikuwa imevurugika vibaya
mno na alikuwa anachemkwa na hasira.
“Wewe ni nani mwanamke…” waziri mkuu
mstaafu alimuuliza. Lakini hakupata jibu badala
yake Salome aliendelea kuangaza huku na kule.
Waziri akamfuata kwa fujo akidhani kuwa itakuwa
rahisi kiasi kile.
Salome akajirudisha nyuma kidogo kisha
akafyatuka kichwa kikali sana katika kinywa cha
waziri, meno mawili ya mbele yakasalimu amri
akayatema huku akiugulia maumivu.
Mzee Nshomile akajirusha ili kumsaidia waziri,
Salome akajikunja kidogo lile teke kali likamkosa,
akajizungusha hewani na teke la mzunguko, mzee
Nsomile akainama likamkosa. Akataka kumpiga
Salome ngumi katikati ya mapaja lakini alikuwa
mwepesi sana akawahi kujirusha kisha kama
afanyavyo kondoo akamfuata hewani kwa
kutumia kichwa, ni heri aliwahi kukwepa kichwa
kile kisikutane na kifua chake maana angepasuka
pasuka kama ulivyopasuka ule mkono uliokutana
na dhahama ile. Nshomile akaugulia maumivu,
huku akisimama wina na kujaribu kumkabili
Salome huku akiwa na majeraha.
Salome alikuwa hajasema neno lolote lile….tangu
aingie katika kile chumba.
Waziri alijitutumua na kusimama akiwa nyuma ya
Salome akaandaa shambulizi kwa kutumia chuma
alichokiokota pale ndani.
Hakujua kama ni roho ipo katika utendaji na
inaona kila kona.
Akakitupa kile chuma kwa nguvu, nia ikiwa
kukitandika kisogo cha Salome….
Binti akainama chuma kikapita kwa kasi na
kumtandika Nshomile usoni akatokwa na yowe
kubwa kisha akaanguka chini.
Waziri akajirusha kwa kutanguliza miguu miwili
mzima mzima ili kumuwahi Salome lakini
haikuwa rahisi kama alivyodhani. Salome
akakwepa kidogo kisha baada ya waziri kutua
chini na yeye akajirusha hewani na kutua katika
magoti yake.
Hapo akatokwa na ukelele mkubwa wa huku
akiyasaga magoti ya waziri mkuu mstaafu.
Hali ikatulia huku Salome akiwa amefura kwa
hasira kali sana.
“Wamalize wamalizeee….” Rensho alimsihi
bSalome lakini akijua kuwa anazungumza na ile
roho ndani yake.
“Sitaua mtu …” Salome alijibu. Rensho akawa
mpole. Na wakati huohuo Salome alianguka chini
na kutokwa na ile hali aliyokuwanayo akabaki
kuwa Salome halisi.
Rensho alipogeuka kuangaza kushoto na kulia
akagundua kuwa kuna watu walikuwa
wamepungua…..
Kindo na Queen. Wako wapi hawa? Alijiuliza.
Na mara kindo na Queen wakaingia wakiwa
katika afya zao imara.
Walikuwa wamebusti tayari.
“Kindo..” Salome aliita baada ya kumuona Kindo
akiingia pale ndani.
Kindo akaingia katika mchecheto, ni kweli
alikuwa akimpenda sana Salome kwa dhati.
Lakini katika mazingira yale ili atoke salama
ilikuwa lazima ajihusishe na Queen.
“Ni nani huyu kwani?” Queen alihoji.
“Huyo ni mume wangu..” Salome alitoa jibu……
“Shhhh! Komea hapo hapo mwanamke.”
“Hey! Jamani tunatakiwa kuwa wamoja jamani,
ugomvi wa nini tena? Tunatakiwa kutoka humu
ndani..” Rensho aliyekuwa amekaa pale chini
alionya. Wakanyamza.
Lakini Queen alikuwa amefikiria jambo, hakuwa
tayari kutoka mle ndani huku akijua kuwa Kindo
si mali yake. Tayari alikuwa amekolea. Wivu wa
kimapenzi ukaanza kumshambulia.
Na hapo akafanya tendo la kipuuzi kuliko yote
aliyowahi kuyafanya.
BOFYA LIKE, TOA MAONI YAKO
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom