iddy eba
JF-Expert Member
- Aug 28, 2015
- 575
- 1,169
- Thread starter
- #21
SEHEMU YA TISA
Kisembe baada ya kufanikiwa kuidhibiti ile damu
kidogo, akavaa nguo zake hovyohovyo. Akatoka
nje na kuingia ndani ya gari lake, nia yake ikiwa
kuwahi huduma hospitali yoyote ile…
Haikuwa nyepesi kama alivyoweza kudhani!!
Asubuhi ya siku iliyofuata taarifa za kustua nchi
zikatapakaa.
Inspekta Juma Kisembe amekutwa amekufa
baada ya kuvuja damu nyingi akiwa ndani ya gari
lake kando kando ya barabara ya Mandela jijini.
Inspekta alikuwa akivuja damu katika sehemu
zake za siri!!
Kifo kama cha mume mwenzake wa siri kwa binti
Maria, Dennis!!
***
MWANDISHI AJIINGIZA KWENYE UTATA WA
HOFU!!
EBOLA….. watafiti wakatoa taarifa kuwa Inspekta
Kisembe amekufa kutokana na ugonjwa huo.
Ebola? Vyombo vya habari vikahoji!!
Ebola gani hiyo iliyomtoa damu sehemu moja tu
katika mwili wake!! Ebola humfanya mgonjwa
avuje damu katika kila tundu lililopo katika mwili
wake.
Hii Ebola ya Inspekta mbona ya aina yake!!
“Kwa hiyo tuwatangazie wananchi kuwa kuna
mlipuko wa gonjwa hilo hatari!!” mwandishi wa
habari akamchimba msemaji wa jeshi la polisi.
“Kutokana na taarifa ya daktari amesema
yawezekana ni Ebola maana ugonjwa mwingine
haujaonekana…”
“Lakini hata Gonorea nayo humtoa mtu damu
mkuu, huoni taarifa ya gonjwa la ebola bila
kuthibitishwa ni sawasawa na kuwajengea
wananchi hofu makusudi!!” mwandishi
akamchimba zaidi, kisha bila kumpa muda wa
kujibu akaongezea jingine, “ Na hawa wenzetu
akiwemo bwana Patrick Masawe na wao
wamekufa vifo vya aina hii… na hadi sasa maiti
hazijakabidhiwa kwa ndugu na kilichowaua
hamjakisema wazi, mbona hiki kifo cha mzee
Kisembe ufumbuzi wake umepatikana upesi sana
mheshimiwa?” mara simu ikakatwa!!
Mwandishi hakujisumbua kupiga tena maana
alijua imekatwa maksudi na hata mpata hewani
tena msemaji huyo aliyezidiwa na mzigo wa
maswali ya kuthibitisha uhakika wa kifo cha
inspekta Kisembe.
Hiyo ilikuwa kawaida ya wakubwa wakiulizwa
maswali magumu!!
Mwandishi yule akajinyoosha katika kochi
alilokuwa amekaa, kisha kitu kikamkuna ghafla
kuwa asipuuzie tukio hilo la inspekta kufa katika
hali ya kustaajabisha.
Akautazama ukuta kisha akafumba macho baada
ya kuiona picha kubwa ya msichana mrembo
kiasi ambaye amepauka haswa. Mwandishi
akamkumbuka Nadia, akaukumbuka mkasa wa
Usilie Nadia ulivyokuwa wa kusisimua, kitabu
chake ambacho kilimpeleka Musoma na kisha
kuishia Mwanza.
Akageuka upande mwingine akakutana na picha
nyingine iliyobuniwa haswa na kupendeza,
maandishi yakasomeka ‘Anti Ezekiel.’
Akalikumbuka tukio hili katika hekaheka zake za
uandishi.
Tukio ambalo almanusura liondoke na uhai wake,
badala yake mkewe na mama yake mzazi
wakapotelea katika tukio hilo.
Tukio hilo la kugundua mkakati kabambe wa
kuusambaza ushoga katika nchi ya Tanzania kwa
kuwateka watoto wadogo wa kiume kisha
kuwahifadhi katika ngome iliyojengwa ardhini na
kuwafundisha tabia za kishoga.
Ufumbuzi huu ulimfanya kuwa mtu maarufu na
wa kuheshimiwa!!
Akainama chini na kuzidi kuwashwa kufuatilia
tukio la kifo cha inspekta wa polisi na watu zaidi
ya kumi na tano. Wote kwa kutokwa damu
nyingi!!
Lazima kuna kitu hapa!! Aliwaza Gerlad Getonga,
mtunzi wa vitabu vya Usilie Nadia na kisha
akaandika kitabu cha kihistoria kile cha Anti
Ezekiel, mkasa wa kweli kabisa uliotaka
kuondoka na roho yake huko Iringa.
Alitamani sana kumshirikisha mkewe Anitha,
lakini akatambua kuwa lazima atakutana na
vikwazo vikali, kwa sababu tukio la Michigan
ambapo mkasa wa Anti Ezekiel ulimalizia wote
waliponea chupuchupu.
Getonga akaitazama picha ya Eva mtoto wake,
machozi yakamlenga lenga alipofikiria kuwa
atamuacha kwa muda wakati akilifuatilia kwa
ukaribu tukio hilo.
“Hapa hakuna hatari yoyote bila shaka ni katukio
kadogo tu..” alijipa moyo huku akipita maamuzi
ya kufuatilia mkasa huu tofauti na waandishi
wengine!!
Getonga akaondoka bila kuaga, tayari alikuwa na
vifaa vyake muhimu kwa ajili ya kazi hiyo.
Laiti kama angejua kuwa tukio lile sio dogo kama
adhaniavyo ni heri angejiepusha nalo!!!
Hakujua kuwa madhara yake ni ya papo kwa
hapo zaidi ya yaliyomkuta wakati akifuatilia
mkasa wa Anti Ezekiel.
Akajiingiza kichwakichwa pasi na hofu yoyote!!
****
Alikuwa amejitahidi na kuachana na matumizi ya
sigara, lakini pombe hakuweza kuiacha. Angalau
kwa siku chupa mbili kwa ajili ya kuichangamsha
akili yake kisha anaendelea na mambo mengine
halafu jioni anajumuika katika vijiwe vya kahawa.
Jioni hii akiwa amemaliza mizunguko ya siku
hiyo akitumia usafiri wa pikipiki binafsi alikuwa
amevuna mambo kadhaa ambayo yalimpa
mwanga juu ya wapi anaweza kuanzia.
Katika daftari lake dogo akaandika mambo hayo
kwa ufupi sana. Ambapo yeyote hata mkewe
akilikwapua daftari lile hakuna ambalo angeweza
kuambulia.
Kindo- Mwendawazimu anayetamka neno moja
tu! =Rensho. Huyu SIMJUI
Maria- inasemekana alikuwa hawara yake
Inspekta. =SIMJUI
Sarah- Rafiki kipenzi wa Maria. =SIMJUI
Kijana- alionekana katika nyumba ya Maria usiku.
=SIMJUI
“Kila mtu simjui! Duh pagumu hapa” Alijikuta
akisema kwa sauti ya juu.
“Unataka kumjua nani?” sauti ya Anitha
ikamkurupua kutoka katika mawazo yake.
“Baba naye kwa kuongea mwenyewe loooh!!”
sauti ya kitoto ya Eva ikapeperusha swali la
Anitha, wakajikuta wakicheka huku wakimtazama
Eva akijifinyafinya uso wake.
Getonga akarejea katika mawazo yake tena!!
Akalitazama daftari lake na kuendelea kusoma.
Deniss- alikuwa hawara wa Maria. =AMEKUFA!!
Inspekta Kisembe- alikuwa hawara wa Maria. =
AMEKUFA
“Mahawara nao wote wamekufa!! ” akajiuliza
safari hii hakutoa sauti nje.
Kuna kitu hapa!! Akamaliza kwa kujipigia makofi,
Eva na Anitha wasijue lolote linaloendelea.
Usiku huu ukapita Getonga akijipongeza kwa
kujua mambo kadhaa ambayo hakuyajua.
Asubuhi alichelewa kuamka!! Na alipoamka
alikutana na mkewe akiwa anacheka.
“Nini tena wewe kucheka asubuhi asubuhi..”
“Waandishi mna mambo nyie dah siwawezi. Ila
nashukuru hata ulivyojiweka mbali na mambo
hayo.”
“tumefanya kituko gani tena.”
“Si mwili wa Inspekta huyu aliyekufa kwa
ugonjwa wa Ebola….”
“Nani, Inspekta Kisembe ama…”
“Ehee huyohuyo… eti nimesikia magazetini kuwa
kuna raia wanadai kuwa marehemu amekutwa na
maneno gani sijui kwa hiyo inasemekana ni u-
freemanson umemuua dah!! Maiti hana la
kujitetea kwa kweli…” alisema haya huku akiwa
bado anatabasamu.
“Maneno tena? Wapi” Getonga aliendelea kuhoji
kwa shauku.
“Rensho sijui Renshi…ila wamesema ni jina lenye
herufi sita kwa hiyo ni Freemason…. Kweli
hamna dogo waandishi…”
Gerlad Getonga akauficha mshtuko wake,
akaguna na kuendelea na shughuli za kusafisha
kinywa chake.
Rensho!! Hilo neno nimewahi kulisikia wapi?
Akajiuliza kimya kimya huku akitamani kujiandaa
upesi akanunue hilo gazeti linalodai kuwa
Inspekta alikutwa na alama.
Baada ya kuoga alirejea chumbani, akachukua
kidaftari chake kidogo
Mstari wa kwanza kabisa wa harakati zake
akakutana na neno.
Kindo- chizi anayetamka neno Rensho pekee.
Upesi akaongezea maneno chini yake.
Rensho ni nani? Kisha akakihifadhi tena.
****
Gari dogo aina ya Toyota Carina lilisimama katika
maegesho ya magari yasiyokuwa rasmi maeneo
ya Kariakoo mtaa wa gerezani. Vioo vikashushwa
na aliyekuwa anaendesha gari hilo.
Akaangaza huku na kule akiwa ameinyoosha
shingo yake akaona alichohitaji kukiona, kisha
akairudisha gari nyuma kidogo akaiingiza
barabarani. Akaendesha kwa muda mfupi akafikia
sehemu ya kuosha magari!!
Akaliacha gari likiwa linaoshwa pale, akaingia
mtaa wa tatu kutoka pale. Akaifikia nyumba
ambayo siku iliyopita alielekezwa kuwa Maria
alikuwa anaishi pale. Akiwa na kofia yake ya
pama kichwani akajiundia uenyeji, hakutaka
kumuuliza mtu yeyote yule juu ya mahali
anapoelekea.
Akaufikia mlango na kuanza kugonga! Hakupata
majibu na bado hakukata tamaa akaendelea
kugonga kama yu mwenyeji sana wa eneo lile.
Baada ya kujihakikishia kuwa hakuna mtu wa
kuufungua ule mlango, mwandishi huyu
mashuhuri Gerlad Getonga akaamua kukishusha
kitasa ili ahakikishe kuwa Maria aliufunga kabla
hajaondoka. Mlango ukafunguka, akatazama
kushoto na kulia. Hapakuwa nna mtu
anayemtazama, akaanza kuita jina la Maria huku
akiingiza kichwa chake ndani katika mfumo wa
kuchungulia.
Chumba hakikuwa na mwanga sana, lakini kile
kitendo cha kuufungua mlango tu na kuangaza
huku na huko akakutana na kitambulisho. Upesi
akainama na kukikwapua kisha akauegesha
mlango tena na kutoweka akiwa anajiamini
kabisa ili kuleta imani kwa yeyote yule ambaye
atakuwa amemtazama.
Hakujua kwa nini amechukua kile kitambulisho na
hakujua ni cha nani lakini huo ukawa mwanzo wa
hekaheka ya ajabu kabisa!! Lakini hakujua kuwa
alichelewa sana kugundua.
****
HAKIKA alionekana kama mwendawazimu!
Jinsi alivyovaa, jinsi alivyokuwa akihangahika
kuchorachora huku na huko. Mwanamama mtu
mzima alikuwa jirani na kijana huyo.
Gerlad Getonga akawasalimia wote wawili. Kabla
mama hajajibu, yule mwendawazimu kimtazamo
akaropoka maneno ambayo yalikuwa muhimu
sana kwa Getonga.
“Rensho….Rensho!!”
Getonga akatikisa kichwa kisha akamsalimia
mama tena, mama akajibu kwa upole kabisa
akiwa na dalili zote za kukata tamaa.
“We nawe unataka unisumbue na maswali kama
wenzako halafu upotee usirudi tena… hamna la
kunisaidia nyie watu sijui waandishi” alilalama
baada ya Getonga kujitambulisha kuwa ni
mwandishi wa kujitegemea na anataka
wazungumze naye juu ya tukio lilomsibu
mwanaye.
Jibu lile lilimkwaza lakini alitumia utashi wa hali
ya juu kumshawishi yule mama mzazi wa kijana
aitwaye Kindo kuzungumza naye.
Ukumbi ukabaki kuwa wa mama Kindo
“Najuta kuitwa mama, lakini mbaya zaidi najuta
kuzaa kisichokuwa chema!” akasita kisha akakaa
sawa na kuendelea, “Kindo hakutaka kunisikiliza
mimi, kaamua kufunga ndoa na huyo Rebeka
sijui. Nikamkataza katakata na kumweleza wazi
kuwa binafsi sijaridhia suala lake la kumuoa huyo
binti na kuachana na Salome. …..” mama akasita
tena na kumgeukia mwanaye aliyekuwa
akitazama kitu asichokijua.
Kindo asiyesema neno zaidi ya ‘Rensho’ alikuwa
anatetemeka huku akiwa amekodoa macho yake,
Getonga naye akafuatisha macho ya mama ana
wote kusaidiana kumtazama Kindo.
Amekuwaje huyu naye!! Mama mtu alijiuliza.
Na hapo likatokea tukio la ajabu kabisa
liliwaduwaza wawili hawa. Kindo akaanza
kuzungumza!!
“Mpe….mpe… mpe upesi…mama mpeni…mpeni
mama.. kaka mpe upesi.” aliyasema haya huku
akimtazama Getonga…. Badala ya kushtuka
Getonga alifanya tabasamu, kwani aliamini kuwa
Kindo ameanza kurejewa na fahamu zake tena,
hivyo atanufaika naye hasahasa kwa kufanya
mahojiano na mwanadamu pekee aliyetoka akiwa
hai katika tukio la kustaajabisha na wanadamu
zaidi ya kumi na nne kuuwawa kinyama na
kilichowaua kisijulikane popote.
“Mama, wakija waandishi wengine usiwaruhusu
kuongea na Kindo sawa.. watamvuruga akili
yake. Mimi kama nilivyokwambia nina nia ya
kukusaidia.
“Sawa mwanangu… nita…” mama akakatishwa na
kelele za Kindo tena, “Mpe upesi nasema.. mpe
kama kipo.. mpe..” alitoa karipio Kindo, Getonga
akatabasamu huku akizidi kuamini kuwa ni
fahamu zinamrejea Kindo.
Na hekaheka za kukata na shoka zikaanzia
hapa!!
Kindo akamvagaa na kumwangusha chini huku
akimkaba kwa nguvu sana shingo yake huku
akimsihi kwa maneno hayohayo kuwa ampe
kama kipo.
Getonga akakakamaa na kujitoa katika mikono ya
ya Kindo kwa juhudi zote, akahema juu juu huku
akimtazama Kindo na kutoamini kitu kilichotokea.
Kabla hajapumua vizuri na kujiweka sawa tena
mara alimwona Kindo akizidi kuyakodoa macho,
halafu akaanza kukifuatilia kitu ambacho Getonga
hakukiona.
Na wakati huo alimuona mama yake akiingia
ndani!!
“Mpe kaka.. mpe …mpe anaomba …mpe…”
aliyasema haya kwa sauti ya chini, Getonga
hakuelewa kitu. Lakini sasa alikuwa ameanza
kuingiwa na hofu!!
Wakati huohuo zikasikika kelele ndani ya nyumba
ya mama yake Kindo, alikuwa akilia kuomba
msaada. Getonga akatoka mbiombio mpaka
ndani kutazama kulikoni. Hapakuwa na kelele
tena.
Akakutana na sebule isiyotamanika kuitazama,
hata kama ni filamu ya kutisha lakini hii ilikuwa
maradufu.
Kichwa katika stuli, mguu mmoja ukining’inia
darini, paja likiwa sakafuni, na..na…….
Ilitisha kutazama vinginevyo. Damu mbichi
ilikuwa imetapakaa!!
Mama Kindo alikuwa ameuwawa kinyama ndani
ya sekunde kadhaa!!
Riadha aliyotimka Getonga mwenye kitambi cha
pesa hakuwahi kukimbia namna ile, alijikwaa
akaanguka akasimama, akaongeza mwendo.
Akapotea njia na kujirekebisha tena, akajitapikia
lakini hakujali!!
Kila aliyemtazama alihisi kuwa yawezekana ni
kibaka ama anayerukwa na akili. Lakini hakuna
aliyemjali, kila mmoja alikuwa na shughuli zake.
Hii ikawa siku ambayo Getonga asingeweza
kuisahau aidha kwa kuishi ama kwa kuwa
kuzimu.
Ukawa mwanzo wa moyo kudunda kwa kasi kila
mara, mwanzo wa kuikosa amani ya nafsi na
mwanzo mwingine wa kuishi kama kivuli, kivuli
kinachoogopa na kuogopwa pia!!
Mwanzo wa kujutia maamuzi!!
***Ni kitu gani kimehusika katika kifo hiki cha
mama yake Kindo….
**Na nini alichokiona Kindo!!!
MWANDISHI KAJIINGIZA KATIKA
ASIYOYAJUA….NINI KITAMTOKEA!!
Je atatupatia jibu na kutuliza HOFU YETU!!!
Kisembe baada ya kufanikiwa kuidhibiti ile damu
kidogo, akavaa nguo zake hovyohovyo. Akatoka
nje na kuingia ndani ya gari lake, nia yake ikiwa
kuwahi huduma hospitali yoyote ile…
Haikuwa nyepesi kama alivyoweza kudhani!!
Asubuhi ya siku iliyofuata taarifa za kustua nchi
zikatapakaa.
Inspekta Juma Kisembe amekutwa amekufa
baada ya kuvuja damu nyingi akiwa ndani ya gari
lake kando kando ya barabara ya Mandela jijini.
Inspekta alikuwa akivuja damu katika sehemu
zake za siri!!
Kifo kama cha mume mwenzake wa siri kwa binti
Maria, Dennis!!
***
MWANDISHI AJIINGIZA KWENYE UTATA WA
HOFU!!
EBOLA….. watafiti wakatoa taarifa kuwa Inspekta
Kisembe amekufa kutokana na ugonjwa huo.
Ebola? Vyombo vya habari vikahoji!!
Ebola gani hiyo iliyomtoa damu sehemu moja tu
katika mwili wake!! Ebola humfanya mgonjwa
avuje damu katika kila tundu lililopo katika mwili
wake.
Hii Ebola ya Inspekta mbona ya aina yake!!
“Kwa hiyo tuwatangazie wananchi kuwa kuna
mlipuko wa gonjwa hilo hatari!!” mwandishi wa
habari akamchimba msemaji wa jeshi la polisi.
“Kutokana na taarifa ya daktari amesema
yawezekana ni Ebola maana ugonjwa mwingine
haujaonekana…”
“Lakini hata Gonorea nayo humtoa mtu damu
mkuu, huoni taarifa ya gonjwa la ebola bila
kuthibitishwa ni sawasawa na kuwajengea
wananchi hofu makusudi!!” mwandishi
akamchimba zaidi, kisha bila kumpa muda wa
kujibu akaongezea jingine, “ Na hawa wenzetu
akiwemo bwana Patrick Masawe na wao
wamekufa vifo vya aina hii… na hadi sasa maiti
hazijakabidhiwa kwa ndugu na kilichowaua
hamjakisema wazi, mbona hiki kifo cha mzee
Kisembe ufumbuzi wake umepatikana upesi sana
mheshimiwa?” mara simu ikakatwa!!
Mwandishi hakujisumbua kupiga tena maana
alijua imekatwa maksudi na hata mpata hewani
tena msemaji huyo aliyezidiwa na mzigo wa
maswali ya kuthibitisha uhakika wa kifo cha
inspekta Kisembe.
Hiyo ilikuwa kawaida ya wakubwa wakiulizwa
maswali magumu!!
Mwandishi yule akajinyoosha katika kochi
alilokuwa amekaa, kisha kitu kikamkuna ghafla
kuwa asipuuzie tukio hilo la inspekta kufa katika
hali ya kustaajabisha.
Akautazama ukuta kisha akafumba macho baada
ya kuiona picha kubwa ya msichana mrembo
kiasi ambaye amepauka haswa. Mwandishi
akamkumbuka Nadia, akaukumbuka mkasa wa
Usilie Nadia ulivyokuwa wa kusisimua, kitabu
chake ambacho kilimpeleka Musoma na kisha
kuishia Mwanza.
Akageuka upande mwingine akakutana na picha
nyingine iliyobuniwa haswa na kupendeza,
maandishi yakasomeka ‘Anti Ezekiel.’
Akalikumbuka tukio hili katika hekaheka zake za
uandishi.
Tukio ambalo almanusura liondoke na uhai wake,
badala yake mkewe na mama yake mzazi
wakapotelea katika tukio hilo.
Tukio hilo la kugundua mkakati kabambe wa
kuusambaza ushoga katika nchi ya Tanzania kwa
kuwateka watoto wadogo wa kiume kisha
kuwahifadhi katika ngome iliyojengwa ardhini na
kuwafundisha tabia za kishoga.
Ufumbuzi huu ulimfanya kuwa mtu maarufu na
wa kuheshimiwa!!
Akainama chini na kuzidi kuwashwa kufuatilia
tukio la kifo cha inspekta wa polisi na watu zaidi
ya kumi na tano. Wote kwa kutokwa damu
nyingi!!
Lazima kuna kitu hapa!! Aliwaza Gerlad Getonga,
mtunzi wa vitabu vya Usilie Nadia na kisha
akaandika kitabu cha kihistoria kile cha Anti
Ezekiel, mkasa wa kweli kabisa uliotaka
kuondoka na roho yake huko Iringa.
Alitamani sana kumshirikisha mkewe Anitha,
lakini akatambua kuwa lazima atakutana na
vikwazo vikali, kwa sababu tukio la Michigan
ambapo mkasa wa Anti Ezekiel ulimalizia wote
waliponea chupuchupu.
Getonga akaitazama picha ya Eva mtoto wake,
machozi yakamlenga lenga alipofikiria kuwa
atamuacha kwa muda wakati akilifuatilia kwa
ukaribu tukio hilo.
“Hapa hakuna hatari yoyote bila shaka ni katukio
kadogo tu..” alijipa moyo huku akipita maamuzi
ya kufuatilia mkasa huu tofauti na waandishi
wengine!!
Getonga akaondoka bila kuaga, tayari alikuwa na
vifaa vyake muhimu kwa ajili ya kazi hiyo.
Laiti kama angejua kuwa tukio lile sio dogo kama
adhaniavyo ni heri angejiepusha nalo!!!
Hakujua kuwa madhara yake ni ya papo kwa
hapo zaidi ya yaliyomkuta wakati akifuatilia
mkasa wa Anti Ezekiel.
Akajiingiza kichwakichwa pasi na hofu yoyote!!
****
Alikuwa amejitahidi na kuachana na matumizi ya
sigara, lakini pombe hakuweza kuiacha. Angalau
kwa siku chupa mbili kwa ajili ya kuichangamsha
akili yake kisha anaendelea na mambo mengine
halafu jioni anajumuika katika vijiwe vya kahawa.
Jioni hii akiwa amemaliza mizunguko ya siku
hiyo akitumia usafiri wa pikipiki binafsi alikuwa
amevuna mambo kadhaa ambayo yalimpa
mwanga juu ya wapi anaweza kuanzia.
Katika daftari lake dogo akaandika mambo hayo
kwa ufupi sana. Ambapo yeyote hata mkewe
akilikwapua daftari lile hakuna ambalo angeweza
kuambulia.
Kindo- Mwendawazimu anayetamka neno moja
tu! =Rensho. Huyu SIMJUI
Maria- inasemekana alikuwa hawara yake
Inspekta. =SIMJUI
Sarah- Rafiki kipenzi wa Maria. =SIMJUI
Kijana- alionekana katika nyumba ya Maria usiku.
=SIMJUI
“Kila mtu simjui! Duh pagumu hapa” Alijikuta
akisema kwa sauti ya juu.
“Unataka kumjua nani?” sauti ya Anitha
ikamkurupua kutoka katika mawazo yake.
“Baba naye kwa kuongea mwenyewe loooh!!”
sauti ya kitoto ya Eva ikapeperusha swali la
Anitha, wakajikuta wakicheka huku wakimtazama
Eva akijifinyafinya uso wake.
Getonga akarejea katika mawazo yake tena!!
Akalitazama daftari lake na kuendelea kusoma.
Deniss- alikuwa hawara wa Maria. =AMEKUFA!!
Inspekta Kisembe- alikuwa hawara wa Maria. =
AMEKUFA
“Mahawara nao wote wamekufa!! ” akajiuliza
safari hii hakutoa sauti nje.
Kuna kitu hapa!! Akamaliza kwa kujipigia makofi,
Eva na Anitha wasijue lolote linaloendelea.
Usiku huu ukapita Getonga akijipongeza kwa
kujua mambo kadhaa ambayo hakuyajua.
Asubuhi alichelewa kuamka!! Na alipoamka
alikutana na mkewe akiwa anacheka.
“Nini tena wewe kucheka asubuhi asubuhi..”
“Waandishi mna mambo nyie dah siwawezi. Ila
nashukuru hata ulivyojiweka mbali na mambo
hayo.”
“tumefanya kituko gani tena.”
“Si mwili wa Inspekta huyu aliyekufa kwa
ugonjwa wa Ebola….”
“Nani, Inspekta Kisembe ama…”
“Ehee huyohuyo… eti nimesikia magazetini kuwa
kuna raia wanadai kuwa marehemu amekutwa na
maneno gani sijui kwa hiyo inasemekana ni u-
freemanson umemuua dah!! Maiti hana la
kujitetea kwa kweli…” alisema haya huku akiwa
bado anatabasamu.
“Maneno tena? Wapi” Getonga aliendelea kuhoji
kwa shauku.
“Rensho sijui Renshi…ila wamesema ni jina lenye
herufi sita kwa hiyo ni Freemason…. Kweli
hamna dogo waandishi…”
Gerlad Getonga akauficha mshtuko wake,
akaguna na kuendelea na shughuli za kusafisha
kinywa chake.
Rensho!! Hilo neno nimewahi kulisikia wapi?
Akajiuliza kimya kimya huku akitamani kujiandaa
upesi akanunue hilo gazeti linalodai kuwa
Inspekta alikutwa na alama.
Baada ya kuoga alirejea chumbani, akachukua
kidaftari chake kidogo
Mstari wa kwanza kabisa wa harakati zake
akakutana na neno.
Kindo- chizi anayetamka neno Rensho pekee.
Upesi akaongezea maneno chini yake.
Rensho ni nani? Kisha akakihifadhi tena.
****
Gari dogo aina ya Toyota Carina lilisimama katika
maegesho ya magari yasiyokuwa rasmi maeneo
ya Kariakoo mtaa wa gerezani. Vioo vikashushwa
na aliyekuwa anaendesha gari hilo.
Akaangaza huku na kule akiwa ameinyoosha
shingo yake akaona alichohitaji kukiona, kisha
akairudisha gari nyuma kidogo akaiingiza
barabarani. Akaendesha kwa muda mfupi akafikia
sehemu ya kuosha magari!!
Akaliacha gari likiwa linaoshwa pale, akaingia
mtaa wa tatu kutoka pale. Akaifikia nyumba
ambayo siku iliyopita alielekezwa kuwa Maria
alikuwa anaishi pale. Akiwa na kofia yake ya
pama kichwani akajiundia uenyeji, hakutaka
kumuuliza mtu yeyote yule juu ya mahali
anapoelekea.
Akaufikia mlango na kuanza kugonga! Hakupata
majibu na bado hakukata tamaa akaendelea
kugonga kama yu mwenyeji sana wa eneo lile.
Baada ya kujihakikishia kuwa hakuna mtu wa
kuufungua ule mlango, mwandishi huyu
mashuhuri Gerlad Getonga akaamua kukishusha
kitasa ili ahakikishe kuwa Maria aliufunga kabla
hajaondoka. Mlango ukafunguka, akatazama
kushoto na kulia. Hapakuwa nna mtu
anayemtazama, akaanza kuita jina la Maria huku
akiingiza kichwa chake ndani katika mfumo wa
kuchungulia.
Chumba hakikuwa na mwanga sana, lakini kile
kitendo cha kuufungua mlango tu na kuangaza
huku na huko akakutana na kitambulisho. Upesi
akainama na kukikwapua kisha akauegesha
mlango tena na kutoweka akiwa anajiamini
kabisa ili kuleta imani kwa yeyote yule ambaye
atakuwa amemtazama.
Hakujua kwa nini amechukua kile kitambulisho na
hakujua ni cha nani lakini huo ukawa mwanzo wa
hekaheka ya ajabu kabisa!! Lakini hakujua kuwa
alichelewa sana kugundua.
****
HAKIKA alionekana kama mwendawazimu!
Jinsi alivyovaa, jinsi alivyokuwa akihangahika
kuchorachora huku na huko. Mwanamama mtu
mzima alikuwa jirani na kijana huyo.
Gerlad Getonga akawasalimia wote wawili. Kabla
mama hajajibu, yule mwendawazimu kimtazamo
akaropoka maneno ambayo yalikuwa muhimu
sana kwa Getonga.
“Rensho….Rensho!!”
Getonga akatikisa kichwa kisha akamsalimia
mama tena, mama akajibu kwa upole kabisa
akiwa na dalili zote za kukata tamaa.
“We nawe unataka unisumbue na maswali kama
wenzako halafu upotee usirudi tena… hamna la
kunisaidia nyie watu sijui waandishi” alilalama
baada ya Getonga kujitambulisha kuwa ni
mwandishi wa kujitegemea na anataka
wazungumze naye juu ya tukio lilomsibu
mwanaye.
Jibu lile lilimkwaza lakini alitumia utashi wa hali
ya juu kumshawishi yule mama mzazi wa kijana
aitwaye Kindo kuzungumza naye.
Ukumbi ukabaki kuwa wa mama Kindo
“Najuta kuitwa mama, lakini mbaya zaidi najuta
kuzaa kisichokuwa chema!” akasita kisha akakaa
sawa na kuendelea, “Kindo hakutaka kunisikiliza
mimi, kaamua kufunga ndoa na huyo Rebeka
sijui. Nikamkataza katakata na kumweleza wazi
kuwa binafsi sijaridhia suala lake la kumuoa huyo
binti na kuachana na Salome. …..” mama akasita
tena na kumgeukia mwanaye aliyekuwa
akitazama kitu asichokijua.
Kindo asiyesema neno zaidi ya ‘Rensho’ alikuwa
anatetemeka huku akiwa amekodoa macho yake,
Getonga naye akafuatisha macho ya mama ana
wote kusaidiana kumtazama Kindo.
Amekuwaje huyu naye!! Mama mtu alijiuliza.
Na hapo likatokea tukio la ajabu kabisa
liliwaduwaza wawili hawa. Kindo akaanza
kuzungumza!!
“Mpe….mpe… mpe upesi…mama mpeni…mpeni
mama.. kaka mpe upesi.” aliyasema haya huku
akimtazama Getonga…. Badala ya kushtuka
Getonga alifanya tabasamu, kwani aliamini kuwa
Kindo ameanza kurejewa na fahamu zake tena,
hivyo atanufaika naye hasahasa kwa kufanya
mahojiano na mwanadamu pekee aliyetoka akiwa
hai katika tukio la kustaajabisha na wanadamu
zaidi ya kumi na nne kuuwawa kinyama na
kilichowaua kisijulikane popote.
“Mama, wakija waandishi wengine usiwaruhusu
kuongea na Kindo sawa.. watamvuruga akili
yake. Mimi kama nilivyokwambia nina nia ya
kukusaidia.
“Sawa mwanangu… nita…” mama akakatishwa na
kelele za Kindo tena, “Mpe upesi nasema.. mpe
kama kipo.. mpe..” alitoa karipio Kindo, Getonga
akatabasamu huku akizidi kuamini kuwa ni
fahamu zinamrejea Kindo.
Na hekaheka za kukata na shoka zikaanzia
hapa!!
Kindo akamvagaa na kumwangusha chini huku
akimkaba kwa nguvu sana shingo yake huku
akimsihi kwa maneno hayohayo kuwa ampe
kama kipo.
Getonga akakakamaa na kujitoa katika mikono ya
ya Kindo kwa juhudi zote, akahema juu juu huku
akimtazama Kindo na kutoamini kitu kilichotokea.
Kabla hajapumua vizuri na kujiweka sawa tena
mara alimwona Kindo akizidi kuyakodoa macho,
halafu akaanza kukifuatilia kitu ambacho Getonga
hakukiona.
Na wakati huo alimuona mama yake akiingia
ndani!!
“Mpe kaka.. mpe …mpe anaomba …mpe…”
aliyasema haya kwa sauti ya chini, Getonga
hakuelewa kitu. Lakini sasa alikuwa ameanza
kuingiwa na hofu!!
Wakati huohuo zikasikika kelele ndani ya nyumba
ya mama yake Kindo, alikuwa akilia kuomba
msaada. Getonga akatoka mbiombio mpaka
ndani kutazama kulikoni. Hapakuwa na kelele
tena.
Akakutana na sebule isiyotamanika kuitazama,
hata kama ni filamu ya kutisha lakini hii ilikuwa
maradufu.
Kichwa katika stuli, mguu mmoja ukining’inia
darini, paja likiwa sakafuni, na..na…….
Ilitisha kutazama vinginevyo. Damu mbichi
ilikuwa imetapakaa!!
Mama Kindo alikuwa ameuwawa kinyama ndani
ya sekunde kadhaa!!
Riadha aliyotimka Getonga mwenye kitambi cha
pesa hakuwahi kukimbia namna ile, alijikwaa
akaanguka akasimama, akaongeza mwendo.
Akapotea njia na kujirekebisha tena, akajitapikia
lakini hakujali!!
Kila aliyemtazama alihisi kuwa yawezekana ni
kibaka ama anayerukwa na akili. Lakini hakuna
aliyemjali, kila mmoja alikuwa na shughuli zake.
Hii ikawa siku ambayo Getonga asingeweza
kuisahau aidha kwa kuishi ama kwa kuwa
kuzimu.
Ukawa mwanzo wa moyo kudunda kwa kasi kila
mara, mwanzo wa kuikosa amani ya nafsi na
mwanzo mwingine wa kuishi kama kivuli, kivuli
kinachoogopa na kuogopwa pia!!
Mwanzo wa kujutia maamuzi!!
***Ni kitu gani kimehusika katika kifo hiki cha
mama yake Kindo….
**Na nini alichokiona Kindo!!!
MWANDISHI KAJIINGIZA KATIKA
ASIYOYAJUA….NINI KITAMTOKEA!!
Je atatupatia jibu na kutuliza HOFU YETU!!!