Riwaya: Hekaheka

HEKAHEKA - 12

Bob nilikuambia kuwa Jacob Matata si mtu wa kumchukulia mzaha hata kidogo. Ona sasa inaonesha ameshafanya upelelezi wa kutosha hapa kwenye kambi aliyokuwepo bila nyie kujua. Siju watu wako walikuwa wanafanya nini. Sasa ni lazima muongeze ulinzi kwenye ukanda huu, nami nitaongea na marafiki zangu walioko kwenye vyombo vya usalama ili wanisaidie kulinda upande huu” Mzee Harken Kalm aliongea kwa hasira huku ngozi yake ikiwa imebadilika na kuwa nyekundu utadhani nini. Muda huu mzee huyu anaongea na Bob Sepeto mkuu wa walinzi wake, ilikuwa ni saa saba usiku. Hali ndani ya kambi hiyo ilikuwa shwari kabisa. Lakini si kwa upande wa walinzi na wana usalama wote wa kambi hiyo. Kwani dakika chache zilikuwa zimepita tangu pale yule mtu aliyekuwa ameuawa na Jacob na maiti yake kuwekwa kwenye mtumbwi ufukweni mwa bahari ilikuwa imeonekana. Hali hii iliwafanya watu hao wawe katika kutafuta wakidhani Jacob bado alikuwa maeneo hayo. Kilichowatia kiwewe zaidi ni ile salamu waliyoikuta imeandikwa kwenye mwili wa marehemu. Maandishi hayo yalisomeka hivi; ‘Jacob anasema siku zenu zinahesabika’ Kwa kumbukumbu alizokuwa nazo mzee Harken Kalm, hakuwahi kutishiwa na yeyote na wala hakuwa anapenda hiyo itokee. Leo ilikuwa ni mara ya kwaza, tena la kutia aibu ni kutoka kwa mwafrika mwenye umri mdogo, Jacob Matata.

Amri ya kutafutwa Jacob popote pale ilitolewa, huku yeyote ambaye angafanikiwa kumuua iliahidiwa kuwa angezawadiwa kiasi kikubwa cha pesa na mzee Harken Kalm.

*****

Dakika arobaini na tano zilipokatika ilikuwa kama wiki moja kwa Kalm, yalipokatika masaa mawili ilikuwa kama mwaka. Tayari alikuwa ameshakunywa mvinyo kiasi kikubwa. Muda ulikatika lakini pamoja na mzee Harken Kalm kusambaza vijana wake kila kona ya jiji hakuna aliyefanikiwa kumtia Jacob Matata machoni. Jitihada zilifanyika na maharamia hawa ili kujua yalipo makazi ya Jacob na nyendo zake. Wakuu mbalimbali wa usalama walitumika ili kujaribu kumuhujumu, lakini haikujulikana Jacob alikuwa akiishi wapi.

Kwake yeye maisha yalikuwa yakiendeshwa kama kawaida tena bila ugumu wowote. Alikuwa akiishi kwenye nyumba iliyokuwa ikilindwa masaa ishirini na nne na vijana wauaji wa mzee Harken Kalm. Walikuwa wameshajua nyumbani kwake na kwa hivyo muda wote walikuwa wakipalinda wakitegemea kumuona Jacob akija hapo.

Ni kweli Jacob alikuwa akilala ndani ya nyumba hiyo siku zote kwani ndiye aliyewapokea siku ya kwanza walipokuja. Walipokuja nyumbani hapo siku ya kwanza, vijana hao katili walimkuta mzee mmoja aliyekuwa amevaa miwani myeusi. Pasipo kujua kuwa ndiye Jacob Matata, walimuuliza yeye ni nani katika jumba hilo. Kwa vile Jacob alitegemea kuwa jamaa hao wangefika hapo alikuwa ameshawaandalia jibu la kuwaridhisha na kuwafanya wasione umuhimu wake na kumwacha kama mzee aliyekuwa amepewa hifadhi katika nyumba hiyo.

Jamaa hao hawakuwa wakiacha nyumba hiyo ibaki bila kuwa na mtu wa kuhakikisha kuwa Jacob asingeingia bila wao kuwa na taarifa. Mara zote alipouliza kama Jacob alikuwa ametokea, Bob Sepeto alipata jibu la kuwa “ ….hapana, isipokuwa yule mzee mwenye miwani myeusi ndiye ameingia kulala…” Hivyo alikuwa akiwadhihaki mara zote ambazo walikuwa wakikutana nae bila wao kumtambua.

Baada ya muda fulani Jacob akawa amefanikiwa kujenga urafiki na mmoja wa vijana wa mzee Harken Kalm. Kijana huyu alijulikana kama Ikwagama Zulu, mwenye asili ya Afrika ya kusini. Jacob alifuatilia na kugundua kuwa Zulu na wenzie walikuwa wakipenda kula kwenye mgahawa wa Jeff Inc fast food. Hivyo Jacob akionekana katika sura yake ya kizee akawa anapenda kwenda pale. Mara kwa mara gari la akina Zulu na wenzake ilipokuwa ikiegesha aliifuata na kujifanya kuomba msaada. Zulu akawa ni mwenye huruma kuliko wenzake kwa kuwa anapenda kuongea na mzee huyu ombaomba. Kwa tabia hii wakajikuta wakawa wameshajenga urafiki wa muombaji na mtoa msaada, huku wakiwa wamepeana majina ya babu na mjukuu.

Jacob alipoona ameshazoea sauti na matendo kadhaa muhimu ya Zulu, siku moja alijifanya kumtaka chemba ili ampe habari muhimu. Walitoka ndani ya mgahawa na kuelekea upande wa nyuma kwenye kichohoro. Ghafla Zulu alishangaa kumuona mzee huyu akiwa kabadilika na kuanza kumpa mapigo makali ambayo hayakuchelewa kuuchukua uhai wake. Baada ya kumuua zulu, Jacob alimvuta mpaka sehemu fulani ambapo alitoa kizibo cha tanki moja la kuhifadhi taka za chooni toka nyumba fulani ya jirani. Hapo aliuvuta mwili wa Zulu na kuutumbukiza humo. Alifunika tanki hilo na kuingia kwenye kona moja ambapo alitoa kikoba chake na kuvaa sura fulani aliyokuwa ameshaiandaa usiku uliopita. Alibadilisha nguo na kuvaa zile alizokuwa amemvua Zulu kabla hajamtumbukiza kwenye tanki. Hapo akawa ameshabadilika toka sura ya mzee ombaomba na kuwa Zulu mlinzi wa mzee Harken Kalm. Alifungua kikoba alichokuwa nacho, humo hakuhitaji chochote kikubwa zaidi ya vikasha kadhaa vilivyokuwa na ngozi za sura za bandia. Alivifutika vitu hivyo sehemu aliyijua yeye katika mwili wake. Kisha akachukua silaha alizokuwa amempora Zulu na vitambulisho vyake. Huyo akarudi pale alipokuwa amewaacha wenzie na Zulu. Mambo yote hayo yalifanywa na Jacob Matata kwa kasi na umakini mkubwa na hivyo kumchukua dakika chache tu.

Kwa Jacob aliona ametumia dakika chache, lakini haikuwa hivyo kwa wafanyakazi wenzie na Zulu. Kwa masharti ya kazi yao, mnapokuwa sehemu kwa kazi maalum hairuhusiwi kuwa mbali na wenzio bila sababu maalum. Hii ilifanyika hivyo ili kuondoa uwezekano wa kuhujumiana au mtu kutekwa pasipo wenzake kujua. Hivyo kiongozi wao hapo tayari alikuwa amewasiliana na Bob Sepeto mkuu wao na kumtaarifu juu ya lile lililokuwa limefanywa na Zulu siku hiyo.

Hivyo wakati Jacob alipokuwa anafika ili kujiunga tena na walinzi hao akiwa katika sura ya Zulu, ni wakati huo huo ambao watu wanne toka kwa Bob Sepeto walikuwa wameshawasili eneo hilo kumchukua Zulu. Kitendo cha Zulu kutokuwa na nidhamu na kutoweka bila taarifa katika wakati mgumu kama huu kilimchukiza sana Bob Sepeto. Kwa kuzingatia sifa za Jacob na utaalamu aliokuwa ameusikia hakumuamini tena Zulu. Hivyo alikuwa ameshatuma watu wake ambao ni maalum kwa kuua wafanyakazi wasio waaminifu. Hivyo wakati Jacob anafika kwa lengo la kwenda kuwahadaa wale watu na kujifanya kuwa ndiye Zulu, tayari wauaji toka kwa Bob Sepeto walikuwa wakimngojea tayari kwa kumuua.

Jacob alipoingia kwenye mgahawa alielekea pale walipokuwa wamekaa wenzie na Zulu, alipoangalia hakuona mtu. Kwa haraka sana alizungusha macho hapa na pale bila kuona yeyote kati ya wale jamaa. Ndio hakuona yeyote kati ya wale, lakini aliona kitu. Aliona macho ambayo kwa utaalamu aliokuwa nao aligundua kuwa yalikuwa na kila dalili ya hatari. Mbaya zaidi ni pale Jacob alipogundua kuwa macho hayo yalikuwa yakimfuatilia yeye kwa usiri mkubwa.

Ili kuhakikisha kuwa watu hao walikuwa mahali hapo kwa sababu yake, Jacob aligeuka na kujifanya kama vile anaelekea nje. Alitembea kwa hadhali kubwa huku mkono wake akiwa anaupeleka tayari kwa kutumia bastola yake.

Hawa ni nani tena, na wamejuaje kuwa ni mimi? Jacob alijiuliza huku akiwa tayari ameshafika mlangoni. Hakuwa na hakika kama watu hao walikuwa wanamtafuta kama Jacob au kama Zulu ambaye sura yake ilionesha hivyo. Alikuwa ameshatoka nje na kutaka kuvuka barabara, mara akasikia vishindo vya mtu aliyeonekana alikuwa akija kwa haraka. Alipotaka kugeuka akaona gari moja ikija kwa kasi upande ule aliokuwa amesimama. Hapo akajua kuna jambo na mambo yameiva.

Alikuwa na uwezo wa kuruka mapema lakini hakufanya hivyo kwa sababu moja kubwa, alitaka kuwafundisha hao jamaa. Gari ilikuja kwa kasi pale alipokuwa amesimama. Nusu sekunde baadaye eneo hilo lilindima kwa mlio wa breki ya gari hilo huku watu wakipiga kelele za hofu.

Wakati gari inafika miguuni Jacob alishahisi kuwa kulikuwa na mtu nyuma yake. Kwa wepesi wa ajabu alijipindua na kuruka hewani kwa kurudi nyuma. Wakati anatua tayari alikuwa upande wa nyuma wa yule mtu aliyekuwa ameinama nyuma yake, alimsukumia kwenye taili za gari ambalo taili zake zililalamika kwa kitendo cha dereva kujaribu kumkwepa mwenzie. Wao walitegemea Jacob ndiye angekuwa akisubiri taili imsage, lakini dereva alichanganyikiwa kuona kuwa mtu waliyetegemea kummaliza alikuwa ameruka kwa staili ambayo alikuwa hajawahi kuona na wakati huohuo akamsukumia jamaa yao kwenye mataili.

“Mmalizeni!!! Dereva wa gari lililokusudia kumgonga Jacob alipiga kelele. Wakati ukulele huo ukiishia hewani, risasi zilimiminika kuelekea pale alipokuwa amesimama Jacob. Kwa mshangao zilikuta hewa, kwani Jacob alikuwa amewahi na kujiviringisha chini. Bado akiwa anaviringika chini Jacob aliachilia risasi mfululizo ambazo ziliwamaliza jamaa wote.

Itaendelea kesho ama baadae inategemea tu.
 
HEKAHEKA - 12

Bob nilikuambia kuwa Jacob Matata si mtu wa kumchukulia mzaha hata kidogo. Ona sasa inaonesha ameshafanya upelelezi wa kutosha hapa kwenye kambi aliyokuwepo bila nyie kujua. Siju watu wako walikuwa wanafanya nini. Sasa ni lazima muongeze ulinzi kwenye ukanda huu, nami nitaongea na marafiki zangu walioko kwenye vyombo vya usalama ili wanisaidie kulinda upande huu” Mzee Harken Kalm aliongea kwa hasira huku ngozi yake ikiwa imebadilika na kuwa nyekundu utadhani nini. Muda huu mzee huyu anaongea na Bob Sepeto mkuu wa walinzi wake, ilikuwa ni saa saba usiku. Hali ndani ya kambi hiyo ilikuwa shwari kabisa. Lakini si kwa upande wa walinzi na wana usalama wote wa kambi hiyo. Kwani dakika chache zilikuwa zimepita tangu pale yule mtu aliyekuwa ameuawa na Jacob na maiti yake kuwekwa kwenye mtumbwi ufukweni mwa bahari ilikuwa imeonekana. Hali hii iliwafanya watu hao wawe katika kutafuta wakidhani Jacob bado alikuwa maeneo hayo. Kilichowatia kiwewe zaidi ni ile salamu waliyoikuta imeandikwa kwenye mwili wa marehemu. Maandishi hayo yalisomeka hivi; ‘Jacob anasema siku zenu zinahesabika’ Kwa kumbukumbu alizokuwa nazo mzee Harken Kalm, hakuwahi kutishiwa na yeyote na wala hakuwa anapenda hiyo itokee. Leo ilikuwa ni mara ya kwaza, tena la kutia aibu ni kutoka kwa mwafrika mwenye umri mdogo, Jacob Matata.

Amri ya kutafutwa Jacob popote pale ilitolewa, huku yeyote ambaye angafanikiwa kumuua iliahidiwa kuwa angezawadiwa kiasi kikubwa cha pesa na mzee Harken Kalm.

*****

Dakika arobaini na tano zilipokatika ilikuwa kama wiki moja kwa Kalm, yalipokatika masaa mawili ilikuwa kama mwaka. Tayari alikuwa ameshakunywa mvinyo kiasi kikubwa. Muda ulikatika lakini pamoja na mzee Harken Kalm kusambaza vijana wake kila kona ya jiji hakuna aliyefanikiwa kumtia Jacob Matata machoni. Jitihada zilifanyika na maharamia hawa ili kujua yalipo makazi ya Jacob na nyendo zake. Wakuu mbalimbali wa usalama walitumika ili kujaribu kumuhujumu, lakini haikujulikana Jacob alikuwa akiishi wapi.

Kwake yeye maisha yalikuwa yakiendeshwa kama kawaida tena bila ugumu wowote. Alikuwa akiishi kwenye nyumba iliyokuwa ikilindwa masaa ishirini na nne na vijana wauaji wa mzee Harken Kalm. Walikuwa wameshajua nyumbani kwake na kwa hivyo muda wote walikuwa wakipalinda wakitegemea kumuona Jacob akija hapo.

Ni kweli Jacob alikuwa akilala ndani ya nyumba hiyo siku zote kwani ndiye aliyewapokea siku ya kwanza walipokuja. Walipokuja nyumbani hapo siku ya kwanza, vijana hao katili walimkuta mzee mmoja aliyekuwa amevaa miwani myeusi. Pasipo kujua kuwa ndiye Jacob Matata, walimuuliza yeye ni nani katika jumba hilo. Kwa vile Jacob alitegemea kuwa jamaa hao wangefika hapo alikuwa ameshawaandalia jibu la kuwaridhisha na kuwafanya wasione umuhimu wake na kumwacha kama mzee aliyekuwa amepewa hifadhi katika nyumba hiyo.

Jamaa hao hawakuwa wakiacha nyumba hiyo ibaki bila kuwa na mtu wa kuhakikisha kuwa Jacob asingeingia bila wao kuwa na taarifa. Mara zote alipouliza kama Jacob alikuwa ametokea, Bob Sepeto alipata jibu la kuwa “ ….hapana, isipokuwa yule mzee mwenye miwani myeusi ndiye ameingia kulala…” Hivyo alikuwa akiwadhihaki mara zote ambazo walikuwa wakikutana nae bila wao kumtambua.

Baada ya muda fulani Jacob akawa amefanikiwa kujenga urafiki na mmoja wa vijana wa mzee Harken Kalm. Kijana huyu alijulikana kama Ikwagama Zulu, mwenye asili ya Afrika ya kusini. Jacob alifuatilia na kugundua kuwa Zulu na wenzie walikuwa wakipenda kula kwenye mgahawa wa Jeff Inc fast food. Hivyo Jacob akionekana katika sura yake ya kizee akawa anapenda kwenda pale. Mara kwa mara gari la akina Zulu na wenzake ilipokuwa ikiegesha aliifuata na kujifanya kuomba msaada. Zulu akawa ni mwenye huruma kuliko wenzake kwa kuwa anapenda kuongea na mzee huyu ombaomba. Kwa tabia hii wakajikuta wakawa wameshajenga urafiki wa muombaji na mtoa msaada, huku wakiwa wamepeana majina ya babu na mjukuu.

Jacob alipoona ameshazoea sauti na matendo kadhaa muhimu ya Zulu, siku moja alijifanya kumtaka chemba ili ampe habari muhimu. Walitoka ndani ya mgahawa na kuelekea upande wa nyuma kwenye kichohoro. Ghafla Zulu alishangaa kumuona mzee huyu akiwa kabadilika na kuanza kumpa mapigo makali ambayo hayakuchelewa kuuchukua uhai wake. Baada ya kumuua zulu, Jacob alimvuta mpaka sehemu fulani ambapo alitoa kizibo cha tanki moja la kuhifadhi taka za chooni toka nyumba fulani ya jirani. Hapo aliuvuta mwili wa Zulu na kuutumbukiza humo. Alifunika tanki hilo na kuingia kwenye kona moja ambapo alitoa kikoba chake na kuvaa sura fulani aliyokuwa ameshaiandaa usiku uliopita. Alibadilisha nguo na kuvaa zile alizokuwa amemvua Zulu kabla hajamtumbukiza kwenye tanki. Hapo akawa ameshabadilika toka sura ya mzee ombaomba na kuwa Zulu mlinzi wa mzee Harken Kalm. Alifungua kikoba alichokuwa nacho, humo hakuhitaji chochote kikubwa zaidi ya vikasha kadhaa vilivyokuwa na ngozi za sura za bandia. Alivifutika vitu hivyo sehemu aliyijua yeye katika mwili wake. Kisha akachukua silaha alizokuwa amempora Zulu na vitambulisho vyake. Huyo akarudi pale alipokuwa amewaacha wenzie na Zulu. Mambo yote hayo yalifanywa na Jacob Matata kwa kasi na umakini mkubwa na hivyo kumchukua dakika chache tu.

Kwa Jacob aliona ametumia dakika chache, lakini haikuwa hivyo kwa wafanyakazi wenzie na Zulu. Kwa masharti ya kazi yao, mnapokuwa sehemu kwa kazi maalum hairuhusiwi kuwa mbali na wenzio bila sababu maalum. Hii ilifanyika hivyo ili kuondoa uwezekano wa kuhujumiana au mtu kutekwa pasipo wenzake kujua. Hivyo kiongozi wao hapo tayari alikuwa amewasiliana na Bob Sepeto mkuu wao na kumtaarifu juu ya lile lililokuwa limefanywa na Zulu siku hiyo.

Hivyo wakati Jacob alipokuwa anafika ili kujiunga tena na walinzi hao akiwa katika sura ya Zulu, ni wakati huo huo ambao watu wanne toka kwa Bob Sepeto walikuwa wameshawasili eneo hilo kumchukua Zulu. Kitendo cha Zulu kutokuwa na nidhamu na kutoweka bila taarifa katika wakati mgumu kama huu kilimchukiza sana Bob Sepeto. Kwa kuzingatia sifa za Jacob na utaalamu aliokuwa ameusikia hakumuamini tena Zulu. Hivyo alikuwa ameshatuma watu wake ambao ni maalum kwa kuua wafanyakazi wasio waaminifu. Hivyo wakati Jacob anafika kwa lengo la kwenda kuwahadaa wale watu na kujifanya kuwa ndiye Zulu, tayari wauaji toka kwa Bob Sepeto walikuwa wakimngojea tayari kwa kumuua.

Jacob alipoingia kwenye mgahawa alielekea pale walipokuwa wamekaa wenzie na Zulu, alipoangalia hakuona mtu. Kwa haraka sana alizungusha macho hapa na pale bila kuona yeyote kati ya wale jamaa. Ndio hakuona yeyote kati ya wale, lakini aliona kitu. Aliona macho ambayo kwa utaalamu aliokuwa nao aligundua kuwa yalikuwa na kila dalili ya hatari. Mbaya zaidi ni pale Jacob alipogundua kuwa macho hayo yalikuwa yakimfuatilia yeye kwa usiri mkubwa.

Ili kuhakikisha kuwa watu hao walikuwa mahali hapo kwa sababu yake, Jacob aligeuka na kujifanya kama vile anaelekea nje. Alitembea kwa hadhali kubwa huku mkono wake akiwa anaupeleka tayari kwa kutumia bastola yake.

Hawa ni nani tena, na wamejuaje kuwa ni mimi? Jacob alijiuliza huku akiwa tayari ameshafika mlangoni. Hakuwa na hakika kama watu hao walikuwa wanamtafuta kama Jacob au kama Zulu ambaye sura yake ilionesha hivyo. Alikuwa ameshatoka nje na kutaka kuvuka barabara, mara akasikia vishindo vya mtu aliyeonekana alikuwa akija kwa haraka. Alipotaka kugeuka akaona gari moja ikija kwa kasi upande ule aliokuwa amesimama. Hapo akajua kuna jambo na mambo yameiva.

Alikuwa na uwezo wa kuruka mapema lakini hakufanya hivyo kwa sababu moja kubwa, alitaka kuwafundisha hao jamaa. Gari ilikuja kwa kasi pale alipokuwa amesimama. Nusu sekunde baadaye eneo hilo lilindima kwa mlio wa breki ya gari hilo huku watu wakipiga kelele za hofu.

Wakati gari inafika miguuni Jacob alishahisi kuwa kulikuwa na mtu nyuma yake. Kwa wepesi wa ajabu alijipindua na kuruka hewani kwa kurudi nyuma. Wakati anatua tayari alikuwa upande wa nyuma wa yule mtu aliyekuwa ameinama nyuma yake, alimsukumia kwenye taili za gari ambalo taili zake zililalamika kwa kitendo cha dereva kujaribu kumkwepa mwenzie. Wao walitegemea Jacob ndiye angekuwa akisubiri taili imsage, lakini dereva alichanganyikiwa kuona kuwa mtu waliyetegemea kummaliza alikuwa ameruka kwa staili ambayo alikuwa hajawahi kuona na wakati huohuo akamsukumia jamaa yao kwenye mataili.

“Mmalizeni!!! Dereva wa gari lililokusudia kumgonga Jacob alipiga kelele. Wakati ukulele huo ukiishia hewani, risasi zilimiminika kuelekea pale alipokuwa amesimama Jacob. Kwa mshangao zilikuta hewa, kwani Jacob alikuwa amewahi na kujiviringisha chini. Bado akiwa anaviringika chini Jacob aliachilia risasi mfululizo ambazo ziliwamaliza jamaa wote.

Itaendelea kesho ama baadae inategemea tu.
Iendelee mkuu.
Tuko hapa tunasubiria mkuu.
 
HEKAHEKA - 13

“Mmalizeni!!! Dereva wa gari lililokusudia kumgonga Jacob alipiga kelele. Wakati ukulele huo ukiishia hewani, risasi zilimiminika kuelekea pale alipokuwa amesimama Jacob. Kwa mshangao zilikuta hewa, kwani Jacob alikuwa amewahi na kujiviringisha chini. Bado akiwa anaviringika chini Jacob aliachilia risasi mfululizo ambazo ziliwamaliza jamaa wote.

* * *

Hii ilikuwa ni simu ya tatu kwa siku hii ya leo. Ilionekana kuwa mpigaji wa simu hii alikuwa ni mmoja. Muda ambao simu hiyo ilikuwa ikipigwa na ujumbe uliokuwa ndani ya simu hii vilimfanya Bi. Anita aamini kuwa mpigaji wa simu hii kama hakuwa ni shetani mwenyewe basi, bila shaka alikuwa ni mtu mwenye mawazo ya shetani. Alifikiri ni jinsi gani mtu huyu alijiamini kiasi cha kumpigia simu mara kwa mara kiasi hicho bila kuogopa. Alijaribu kufikiri sauti hii ambayo si ngeni sana kwake ilikuwa ni ya nani au aliwahi kuisikia wapi. Hakuweza kupata jibu lolote la kweli. Simu iliyokuwa ikitumika ilikuwa ni ile ya mezani, Bi. Anita hakuwa na uwezo wa kuona namba za mpigaji.

Baada ya kufikiri sana ndipo akaamua kumtuma mmoja kati ya vijana wake ili aende shirika la simu kuulizia mmiliki wa namba iliyokuwa imepigwa mara tatu kwenda ofisini hapo.

Muda mfupi mara baada ya Bi. Anita kumtuma mtu wake kwenda kuulizia juu ya mpigaji huyu, mara simu yake ya mezani iliita. Kabla ya kuinyanyua, Bi. Anita alichukua kifaa fulani ambacho kilikuwa maalum kwa ajili ya kunakili maongezi ya kwenye simu. Baada ya kuipachika sehemu fulani jirani na mkonga wa kuongelea na kusikilizia Bi. Anita aliipokea simu hiyo.

“Nani unaongea?” Aliuliza Bi. Anita kwa sauti ya kukereka kidogo.

“Ni yule rafiki yako anaeomba nafasi ya kukushauri” Ulijibu upande wa pili.

“Urafiki gani unaombwa pasipo na pande mbili kujuana? Huo si urafiki bali ni mtu mmoja anaemjua mwenzie kutaka kumteka asiyemjua mwenzie” Alisema Bi. Anita.

“Nashangaa sana pale unaposema kuwa hunijui ilhali kila leo unafikiri namna ya kupata nafasi ya kuonana na mimi, unanifahamu ila sema hujui niko wapi japo ningependa ujue niko wapi. Nashindwa kukujulisha kuwa niko wapi kwa vile bado hatujawa na mtazamo sawa, tukiwa marafiki unaruhusiwa kujua niko wapi.” Ilipofika hapo sauti hiyo ilisikika ikicheka kicheko cha kebehi. Kwa kushindwa kuficha chuki yake Bi. Anita alijikuta akifumba macho.

“Okay, pamoja na kuwa umekataa kusema jina lako na mahali ulipo lakini bado sikuelewi pale unaposoma kuwa nakufahamu ilhali sikufahamu, labda ungenikumbusha tuliwahi kuonana wapi, na ni mitazamo gani tunayotofautiana?” Bi. Anita aliuliza huku mtu wa upande wa pili akionekana mwenye furaha isiyo kifani. Sauti yake ilionesha hivyo.

“Ngoja kwanza nikukumbushe uliniona wapi, wiki mbili zilizopita saa kumi usiku ulikuja kuniona pale Benki ilipovunjwa na kuibiwa mabilioni ya Shilingi. Ni kweli kuwa hukuiona sura yangu lakini matendo yangu uliyaona, wiki moja baadae ulikuja kuniona pale mabilioni ya Shilingi ya kampuni ya kutengeneza bia yalipoporwa, ilikuwa ni saa tisa alasiri juzi usiku ulikuja kuniona pale Shinyanga katika tukio ambalo nilikuwa nimeenda kuchukua madini, japo nyie mnasema ni kuiba. Nasema tuna tofauti za kimtazamo kwa vile mara zote ambazo umekuwa ukija kuniona na kufanikiwa kuiona sura yangu kwa njia ya matukio yangu umekuwa ukionesha masikitiko na hasira kuu. Tofauti na mimi ambaye hata hivyo mara kwa mara nimekuwa nikiwa hatua chache sana toka pale unapokuwa umesimama. Kwani licha ya kuwepo kwenye matukio hayo kwa njia ya matendo lakini mara nyingi kiwiliwili changu huwepo kwa vile huwa na hamu ya kumuona rafiki yangu ambaye ni wewe.”

Kinachonishangaza ni kuwa mara zote umekuwa ukichukia pale ninapofurahi, unalia pale ninapocheka, unajiandaa kupigana sehemu ambayo naona inafaa nijiandae kusheherekea. Unalinda sehemu ambayo ningependa iwe wazi masaa ishirini na nne. Hizo ndizo tofauti za kimtazamo zilizopo kati yangu na wewe, lakini nadhani wakati umefika ambapo tunatakiwa kuzika tofauti hizo, kwani tusipofanya hivyo waweza kufa kwa shinikizo la moyo. Nimetangulia kusema kuwa najua kwa sasa unatafuta namna ya kukifikia kiwiliwili changu. Ningefurahi sana kuwa mwenyeji wako kwani kwa hivi sasa nimetoka kuchukua benki statement inayoonesha kuwa mamilioni ya pesa niliyochukua pale kampuni ya bia na benki tayari yameshaingia kwenye akaunti yangu. Pia nimepokea taarifa kuwa yale madini niliyochukua kule Shinyanga yameshapata mnunuzi.

Nasikitika kwa vile unataka niendelee kuwa maskini huku tukiwaachia wazungu watajirike. Nadhani ungeniona hapa nilipokaa ungechoka kabisa kwani watu wanaosubiri taarifa za mapato na matumizi ya pesa hizo wengine wana cheo kuliko cha kwako. Naamini unaweza kuwa mmoja wao, unaweza kuwa unapata mamilioni ya Shilingi kwa mwezi kwa kazi ngumu ya kuwa unaweka miguu juu ya meza na kustarehe, tofauti na sasa ambapo unapokea vishilingi vichache ilhali unakesha katika kutafuta namna ya kufika mahali nilipo na kuharibu starehe yangu na wakubwa wako.

Vipi rafiki umefikia wapi katika kutafuta mpenyo wa kunifikia, inashangaza kwa sababu badala ya kutumia muda wako kutafuta pesa, wewe unautumia katika kupanga mipango ya kuwaharibia wenzio wenye shida na pesa na wanaojua matumizi yake. Juhudi hizo ungezielekeza pengine bila shaka ungekuwa tajiri kama mimi na wale walio na mtazamo kama wangu. Oooh Samahani nimekuwa msemaji sana, ila kumbuka kuwa unawajibu wa kufanya jambo kwa ajili ya matukio haya usinyamaze kana kwamba huyaoni” Ilimaliza sauti hiyo kwa kicheko ambacho kilisaidiwa na vicheko vya watu wengine waliosikika kuwa walikuwa karibu sana na muongeaji.

“Kama ulivyosema kuwa tunatofautiana mtazamo, hivyo kwa vile wewe una maneno mengi wakati huu basi mimi sina maneno mengi ili kwamba wakati nitakapokuwa na maneno mengi, wakati kichwa chako kikiwa kinaelekea kwenye kitanzi tayari kwa kunyongwa, nawe hutakuwa na maneno mengi. Kwa sasa niache niendelee na kazi uayoiona kama kazi kichaa, wasalimie hao wanaovuna wasipopanda na kukusanya wasipotawanya. Waambie watalipa udhalimu wanaowafanyia watu waliowaamini na kuwapa heshima ya kuwaongoza kumbe wao wanawadhihaki” Maneno hayo Bi. Anita aliyaongea huku akiwa bado amefunika macho kutokana na uchungu. Hata hivyo maneno hayo yalipokewa kwa vicheko toka upande wa pili. Kisha Bi. Anita hakuona haja ya kuendelea kuhojiana na hao watu, hivyo akaazimia kukata simu. Wakati anataka kuweka chini mkonga wa simu kuna neno akalisikia, neno lenyewe lilikuwa ni “….Kesho Leaders Club saa tatu usiku….” Aliuweka chini mkono wa simu.

Maneno yaliyoongewa na huyu mtu anayejiita kama rafiki yaliutibuwa kabisa ubongo wa Bi. Anita, akajikuta anatamani sana kupokea taarifa toka kwa kijana wake juu ya mmliki wa namba ya simu iloyokuwa ikitumiwa na mtu anayejiita ‘rafiki’.

Alitulia tuli juu ya kochi lake kubwa huku akijaribu kuyatafakari maneno yote yaloyokuwa yakisemwa na ‘rafiki’. Alishangaa, kwani kwa uzoefu na utaalamu alionao ulionesha kuwa mara nyingi wahalifu hutafutwa na siyo kujileta kama huyu. Ikitokea kuwa amejileta basi ujue kuwa kuna hila imefichika ndani ya moyo wake na kuwa adui huyo ni moto wa kuotea mbali.

Alifikiri ni jinsi gani wizi huu mfululizo ulivyopelekea jeshi la polisi kupakwa matope na watu mbalimbali kwa kile kilichoosemwa kuwa lilikuwa limeshindwa kuhakikisha usalama wa watu na mali zao. Hali hii iliyopelekea mkuu wa jeshi la polisi na waziri wa mambo ya ndani wajiuzulu mara baada ya shutuma dhidi yao kuzidi.

Kuona hivyo Rais kwa kutumia njia ya siri kabisa aliweza kumtaarifu Bi. Anita juu ya haja yake ya kutaka ofisi fukuzi ijiingize katika kutafuta ukweli juu ya matukio haya ya wizi wa kimataifa.

Masaa machache tu mara baada ya kupokea jukumu hilo toka kwa Rais, Bi. Anita alipokea simu toka kwa mtu huyu anayejiita ‘rafiki’. Katika simu hiyo ya kwanza ‘rafiki’ alisema alikuwa anampongeza Bi. Anita kwa kupewa jukumu hilo gumu, la siri na la kitaifa.

Baada ya Bi. Anita kutafakari kwa kina juu ya ujumbe huo toka kwa ‘rafiki’ ndipo kwa siri akamtumia taarifa Rais kumtaka kutowasiliana nae kwa njia yoyote zaidi ya wao kuonana ana kwa ana. Bi. Anita alimueleza Rais kuwa sababu kuu yeye kufanya hivyo kuwa amegundua kuwa kuna mtu anavujisha siri. Alishangaa zaidi pale alipopokea simu ya pili toka kwa ‘rafiki’. Katika simu hii ‘rafiki’ alikuwa anampongeza Bi. Anita kwa kuwa makini na kubuni njia nzuri ya kuwasiliana na Rais. Kwanza Bi. Anita aliogopa lakini baadaye aliamua kufuatilia ili kujua juu ya mtu huyu anayejiita ‘rafiki’. Ndipo hapo akaamua kumtuma mtu kwenda shirika la simu ili kujua mmiliki wa namba ya simu iliyokuwa ikitumiwa na ‘rafiki’. Wakati akisubiri taarifa toka shirika la simu ndipo alipopokea simu hii ya tatu toka kwa ‘rafiki’, safari hii rafiki akiongea kwa kirefu.

“Bosi, watu wa simu wanasema namba hiyo ni ya biashara na inamilikiwa na msichana mmoja aitwaye Joyce” Alisema huyu kijana ambaye alionesha hofu hasa mara baada ya kuiona sura ya Bi. Anita. Sura ya Bi. Anita ilionesha wazi wazi hasira, ilikuwa ya baridi sana.

“Huyo Joyce wamesema anaishi wapi?”

“Wamesema wakati anakuja kuchukua namba ya sanduku la posta na hiyo namba ya simu ya biashara alijiandikisha kama anaishi kinondoni makaburini. Kwa hiyo hawajui kama bado anaishi hapo au alishahama, nimejaribu kuwaulizia kama wanajua sehemu yake ya biashara wakasema hilo hawajui”.

“Sawa hebu fanya utaratibu ili uweze kupata anapoishi kama ukimpata mlete hapa pasipo yeye kujua, nafikiri nikisema hivyo unanielewa”

“Ndio bosi” Alisema kijana huyo aliyeonesha kila dalili kuwa alikuwa mtii na tayari kufanya lolote aliloambiwa na bosi wake.

Kijana huyo alipoondoka, Bi. Anita alizama tena katika mawazo juu ya mtu huyu ajiitaye ‘rafiki’. Aliwaza mengi, Hatimaye akafikia pale ‘rafiki’ aliposema kuwa yuko na watu ambao wengine ni wana vyeo kuliko yeye Bi. Anita. Alifikiri juu ya mtazamo wa viongozi wengi wa Afrika pale wanapokabidhiwa madaraka na wananchi, wengi hudhani kuwa wamepewa nafasi ya kujinufaisha binafsi. Hivyo wanapoingia madarakani tu, husahau wajibu wao kwa wananchi na badala yake hutimiza wajibu kwa matumbo yao na uchu walionao.

Mawazo yake hayo yaligutuliwa baada ya sauti ya mtu aliyekuwa akibisha mlango.

“Ingia ndani” Alisema huku akiruhusu viganja kupita juu ya uso wake kwa staili ya kufuta, bila shaka hii ni dalili ya kuhama kimawazo na kurudi ofisini. Yule kijana aliyemtuma kwa Joyce binti mwenye namba za simu zilizokuwa zimetumiwa na ‘rafiki’ alikuwa amesharudi.

“Bosi, nimeenda lakini tofauti na matarajio yetu, sijamkuta Joyce tuliyekuwa tukimtaka. Badala yake nimekutana na maiti ya Joyce, pembeni yake nilikuta karatasi hii ambayo ina namba za sanduku la posta”. Alisema huku akimkabidhi Bi. Anita hicho kijikaratasi ambacho hakikuwa na lolote zaidi ya namba za sanduku la posta. Alipofika hapo Bi. Anita alivuta pumzi ndefu kisha akasimama.

“Sasa inabidi uwe makini zaidi, inaonesha hawa watu wanafuatilia kila tunalolifanya na inawezekana kuna mtu wa karibu sana anayewapa taarifa juu yetu. Mchukue Mike mwende mkaangalie kwenye hilo sanduku la posta kuna nini, ila narudia inabidi muwe makini kwani bila shaka kutakuwa na watu wanaowatazama. Pia mkiweza kumtambua yeyote anayewafuatilia itakuwa vizuri zaidi. Haya kazi njema”. Alisema Bi. Anita huku uso wake ukiwa umeelekezwa dirishani.

Jambo moja lilianza kuusumbua ubongo wa Bi. Anita, nalo si jingine ila ni lile la kujiona yuko uchi. Kwani inaonesha adui alikuwa akijua kila kitu kuhusiana na yeye.

Dakika kumi baadaye yule kijana wake aliyekuwa ameenda posta alikuwa tayari amerudi.

“Eeh yalikwendaje?” Aliuliza pale alipokuwa tayari ameshakaa.

“Hakuna cha ziada zaidi ya karatasi hii” Alisema huku akimkabidhi Bi. Anita ile karatasi aliyoichukua posta.

Kama kawaida ya mwandishi wa karatasi hizi, hakuwa na maneno mengi, safari hii alikuwa ameandika; NAMTAKA JACOB MATATA LA SIVYO JIANDAE BADO “PIGO LA MAUTI”. RAFIKI.

“Jacob!!! Jacob anahusiana vipi na mambo haya, na kwa nini wanamtaka?” Bi. Anita alijikuta akifoka huku akipiga ngumi juu ya meza.

Kwa mara ya kwanza ndipo mkuu huyu wa kitengo hiki maalum cha usalama alikumbuka kuwa zilikuwa zimepita situ kadhaa bila kumuona wala kusikia Sauti ya Jacob Matata.

Itaendelea
 
HEKAHEKA - 13

“Mmalizeni!!! Dereva wa gari lililokusudia kumgonga Jacob alipiga kelele. Wakati ukulele huo ukiishia hewani, risasi zilimiminika kuelekea pale alipokuwa amesimama Jacob. Kwa mshangao zilikuta hewa, kwani Jacob alikuwa amewahi na kujiviringisha chini. Bado akiwa anaviringika chini Jacob aliachilia risasi mfululizo ambazo ziliwamaliza jamaa wote.

* * *

Hii ilikuwa ni simu ya tatu kwa siku hii ya leo. Ilionekana kuwa mpigaji wa simu hii alikuwa ni mmoja. Muda ambao simu hiyo ilikuwa ikipigwa na ujumbe uliokuwa ndani ya simu hii vilimfanya Bi. Anita aamini kuwa mpigaji wa simu hii kama hakuwa ni shetani mwenyewe basi, bila shaka alikuwa ni mtu mwenye mawazo ya shetani. Alifikiri ni jinsi gani mtu huyu alijiamini kiasi cha kumpigia simu mara kwa mara kiasi hicho bila kuogopa. Alijaribu kufikiri sauti hii ambayo si ngeni sana kwake ilikuwa ni ya nani au aliwahi kuisikia wapi. Hakuweza kupata jibu lolote la kweli. Simu iliyokuwa ikitumika ilikuwa ni ile ya mezani, Bi. Anita hakuwa na uwezo wa kuona namba za mpigaji.

Baada ya kufikiri sana ndipo akaamua kumtuma mmoja kati ya vijana wake ili aende shirika la simu kuulizia mmiliki wa namba iliyokuwa imepigwa mara tatu kwenda ofisini hapo.

Muda mfupi mara baada ya Bi. Anita kumtuma mtu wake kwenda kuulizia juu ya mpigaji huyu, mara simu yake ya mezani iliita. Kabla ya kuinyanyua, Bi. Anita alichukua kifaa fulani ambacho kilikuwa maalum kwa ajili ya kunakili maongezi ya kwenye simu. Baada ya kuipachika sehemu fulani jirani na mkonga wa kuongelea na kusikilizia Bi. Anita aliipokea simu hiyo.

“Nani unaongea?” Aliuliza Bi. Anita kwa sauti ya kukereka kidogo.

“Ni yule rafiki yako anaeomba nafasi ya kukushauri” Ulijibu upande wa pili.

“Urafiki gani unaombwa pasipo na pande mbili kujuana? Huo si urafiki bali ni mtu mmoja anaemjua mwenzie kutaka kumteka asiyemjua mwenzie” Alisema Bi. Anita.

“Nashangaa sana pale unaposema kuwa hunijui ilhali kila leo unafikiri namna ya kupata nafasi ya kuonana na mimi, unanifahamu ila sema hujui niko wapi japo ningependa ujue niko wapi. Nashindwa kukujulisha kuwa niko wapi kwa vile bado hatujawa na mtazamo sawa, tukiwa marafiki unaruhusiwa kujua niko wapi.” Ilipofika hapo sauti hiyo ilisikika ikicheka kicheko cha kebehi. Kwa kushindwa kuficha chuki yake Bi. Anita alijikuta akifumba macho.

“Okay, pamoja na kuwa umekataa kusema jina lako na mahali ulipo lakini bado sikuelewi pale unaposoma kuwa nakufahamu ilhali sikufahamu, labda ungenikumbusha tuliwahi kuonana wapi, na ni mitazamo gani tunayotofautiana?” Bi. Anita aliuliza huku mtu wa upande wa pili akionekana mwenye furaha isiyo kifani. Sauti yake ilionesha hivyo.

“Ngoja kwanza nikukumbushe uliniona wapi, wiki mbili zilizopita saa kumi usiku ulikuja kuniona pale Benki ilipovunjwa na kuibiwa mabilioni ya Shilingi. Ni kweli kuwa hukuiona sura yangu lakini matendo yangu uliyaona, wiki moja baadae ulikuja kuniona pale mabilioni ya Shilingi ya kampuni ya kutengeneza bia yalipoporwa, ilikuwa ni saa tisa alasiri juzi usiku ulikuja kuniona pale Shinyanga katika tukio ambalo nilikuwa nimeenda kuchukua madini, japo nyie mnasema ni kuiba. Nasema tuna tofauti za kimtazamo kwa vile mara zote ambazo umekuwa ukija kuniona na kufanikiwa kuiona sura yangu kwa njia ya matukio yangu umekuwa ukionesha masikitiko na hasira kuu. Tofauti na mimi ambaye hata hivyo mara kwa mara nimekuwa nikiwa hatua chache sana toka pale unapokuwa umesimama. Kwani licha ya kuwepo kwenye matukio hayo kwa njia ya matendo lakini mara nyingi kiwiliwili changu huwepo kwa vile huwa na hamu ya kumuona rafiki yangu ambaye ni wewe.”

Kinachonishangaza ni kuwa mara zote umekuwa ukichukia pale ninapofurahi, unalia pale ninapocheka, unajiandaa kupigana sehemu ambayo naona inafaa nijiandae kusheherekea. Unalinda sehemu ambayo ningependa iwe wazi masaa ishirini na nne. Hizo ndizo tofauti za kimtazamo zilizopo kati yangu na wewe, lakini nadhani wakati umefika ambapo tunatakiwa kuzika tofauti hizo, kwani tusipofanya hivyo waweza kufa kwa shinikizo la moyo. Nimetangulia kusema kuwa najua kwa sasa unatafuta namna ya kukifikia kiwiliwili changu. Ningefurahi sana kuwa mwenyeji wako kwani kwa hivi sasa nimetoka kuchukua benki statement inayoonesha kuwa mamilioni ya pesa niliyochukua pale kampuni ya bia na benki tayari yameshaingia kwenye akaunti yangu. Pia nimepokea taarifa kuwa yale madini niliyochukua kule Shinyanga yameshapata mnunuzi.

Nasikitika kwa vile unataka niendelee kuwa maskini huku tukiwaachia wazungu watajirike. Nadhani ungeniona hapa nilipokaa ungechoka kabisa kwani watu wanaosubiri taarifa za mapato na matumizi ya pesa hizo wengine wana cheo kuliko cha kwako. Naamini unaweza kuwa mmoja wao, unaweza kuwa unapata mamilioni ya Shilingi kwa mwezi kwa kazi ngumu ya kuwa unaweka miguu juu ya meza na kustarehe, tofauti na sasa ambapo unapokea vishilingi vichache ilhali unakesha katika kutafuta namna ya kufika mahali nilipo na kuharibu starehe yangu na wakubwa wako.

Vipi rafiki umefikia wapi katika kutafuta mpenyo wa kunifikia, inashangaza kwa sababu badala ya kutumia muda wako kutafuta pesa, wewe unautumia katika kupanga mipango ya kuwaharibia wenzio wenye shida na pesa na wanaojua matumizi yake. Juhudi hizo ungezielekeza pengine bila shaka ungekuwa tajiri kama mimi na wale walio na mtazamo kama wangu. Oooh Samahani nimekuwa msemaji sana, ila kumbuka kuwa unawajibu wa kufanya jambo kwa ajili ya matukio haya usinyamaze kana kwamba huyaoni” Ilimaliza sauti hiyo kwa kicheko ambacho kilisaidiwa na vicheko vya watu wengine waliosikika kuwa walikuwa karibu sana na muongeaji.

“Kama ulivyosema kuwa tunatofautiana mtazamo, hivyo kwa vile wewe una maneno mengi wakati huu basi mimi sina maneno mengi ili kwamba wakati nitakapokuwa na maneno mengi, wakati kichwa chako kikiwa kinaelekea kwenye kitanzi tayari kwa kunyongwa, nawe hutakuwa na maneno mengi. Kwa sasa niache niendelee na kazi uayoiona kama kazi kichaa, wasalimie hao wanaovuna wasipopanda na kukusanya wasipotawanya. Waambie watalipa udhalimu wanaowafanyia watu waliowaamini na kuwapa heshima ya kuwaongoza kumbe wao wanawadhihaki” Maneno hayo Bi. Anita aliyaongea huku akiwa bado amefunika macho kutokana na uchungu. Hata hivyo maneno hayo yalipokewa kwa vicheko toka upande wa pili. Kisha Bi. Anita hakuona haja ya kuendelea kuhojiana na hao watu, hivyo akaazimia kukata simu. Wakati anataka kuweka chini mkonga wa simu kuna neno akalisikia, neno lenyewe lilikuwa ni “….Kesho Leaders Club saa tatu usiku….” Aliuweka chini mkono wa simu.

Maneno yaliyoongewa na huyu mtu anayejiita kama rafiki yaliutibuwa kabisa ubongo wa Bi. Anita, akajikuta anatamani sana kupokea taarifa toka kwa kijana wake juu ya mmliki wa namba ya simu iloyokuwa ikitumiwa na mtu anayejiita ‘rafiki’.

Alitulia tuli juu ya kochi lake kubwa huku akijaribu kuyatafakari maneno yote yaloyokuwa yakisemwa na ‘rafiki’. Alishangaa, kwani kwa uzoefu na utaalamu alionao ulionesha kuwa mara nyingi wahalifu hutafutwa na siyo kujileta kama huyu. Ikitokea kuwa amejileta basi ujue kuwa kuna hila imefichika ndani ya moyo wake na kuwa adui huyo ni moto wa kuotea mbali.

Alifikiri ni jinsi gani wizi huu mfululizo ulivyopelekea jeshi la polisi kupakwa matope na watu mbalimbali kwa kile kilichoosemwa kuwa lilikuwa limeshindwa kuhakikisha usalama wa watu na mali zao. Hali hii iliyopelekea mkuu wa jeshi la polisi na waziri wa mambo ya ndani wajiuzulu mara baada ya shutuma dhidi yao kuzidi.

Kuona hivyo Rais kwa kutumia njia ya siri kabisa aliweza kumtaarifu Bi. Anita juu ya haja yake ya kutaka ofisi fukuzi ijiingize katika kutafuta ukweli juu ya matukio haya ya wizi wa kimataifa.

Masaa machache tu mara baada ya kupokea jukumu hilo toka kwa Rais, Bi. Anita alipokea simu toka kwa mtu huyu anayejiita ‘rafiki’. Katika simu hiyo ya kwanza ‘rafiki’ alisema alikuwa anampongeza Bi. Anita kwa kupewa jukumu hilo gumu, la siri na la kitaifa.

Baada ya Bi. Anita kutafakari kwa kina juu ya ujumbe huo toka kwa ‘rafiki’ ndipo kwa siri akamtumia taarifa Rais kumtaka kutowasiliana nae kwa njia yoyote zaidi ya wao kuonana ana kwa ana. Bi. Anita alimueleza Rais kuwa sababu kuu yeye kufanya hivyo kuwa amegundua kuwa kuna mtu anavujisha siri. Alishangaa zaidi pale alipopokea simu ya pili toka kwa ‘rafiki’. Katika simu hii ‘rafiki’ alikuwa anampongeza Bi. Anita kwa kuwa makini na kubuni njia nzuri ya kuwasiliana na Rais. Kwanza Bi. Anita aliogopa lakini baadaye aliamua kufuatilia ili kujua juu ya mtu huyu anayejiita ‘rafiki’. Ndipo hapo akaamua kumtuma mtu kwenda shirika la simu ili kujua mmiliki wa namba ya simu iliyokuwa ikitumiwa na ‘rafiki’. Wakati akisubiri taarifa toka shirika la simu ndipo alipopokea simu hii ya tatu toka kwa ‘rafiki’, safari hii rafiki akiongea kwa kirefu.

“Bosi, watu wa simu wanasema namba hiyo ni ya biashara na inamilikiwa na msichana mmoja aitwaye Joyce” Alisema huyu kijana ambaye alionesha hofu hasa mara baada ya kuiona sura ya Bi. Anita. Sura ya Bi. Anita ilionesha wazi wazi hasira, ilikuwa ya baridi sana.

“Huyo Joyce wamesema anaishi wapi?”

“Wamesema wakati anakuja kuchukua namba ya sanduku la posta na hiyo namba ya simu ya biashara alijiandikisha kama anaishi kinondoni makaburini. Kwa hiyo hawajui kama bado anaishi hapo au alishahama, nimejaribu kuwaulizia kama wanajua sehemu yake ya biashara wakasema hilo hawajui”.

“Sawa hebu fanya utaratibu ili uweze kupata anapoishi kama ukimpata mlete hapa pasipo yeye kujua, nafikiri nikisema hivyo unanielewa”

“Ndio bosi” Alisema kijana huyo aliyeonesha kila dalili kuwa alikuwa mtii na tayari kufanya lolote aliloambiwa na bosi wake.

Kijana huyo alipoondoka, Bi. Anita alizama tena katika mawazo juu ya mtu huyu ajiitaye ‘rafiki’. Aliwaza mengi, Hatimaye akafikia pale ‘rafiki’ aliposema kuwa yuko na watu ambao wengine ni wana vyeo kuliko yeye Bi. Anita. Alifikiri juu ya mtazamo wa viongozi wengi wa Afrika pale wanapokabidhiwa madaraka na wananchi, wengi hudhani kuwa wamepewa nafasi ya kujinufaisha binafsi. Hivyo wanapoingia madarakani tu, husahau wajibu wao kwa wananchi na badala yake hutimiza wajibu kwa matumbo yao na uchu walionao.

Mawazo yake hayo yaligutuliwa baada ya sauti ya mtu aliyekuwa akibisha mlango.

“Ingia ndani” Alisema huku akiruhusu viganja kupita juu ya uso wake kwa staili ya kufuta, bila shaka hii ni dalili ya kuhama kimawazo na kurudi ofisini. Yule kijana aliyemtuma kwa Joyce binti mwenye namba za simu zilizokuwa zimetumiwa na ‘rafiki’ alikuwa amesharudi.

“Bosi, nimeenda lakini tofauti na matarajio yetu, sijamkuta Joyce tuliyekuwa tukimtaka. Badala yake nimekutana na maiti ya Joyce, pembeni yake nilikuta karatasi hii ambayo ina namba za sanduku la posta”. Alisema huku akimkabidhi Bi. Anita hicho kijikaratasi ambacho hakikuwa na lolote zaidi ya namba za sanduku la posta. Alipofika hapo Bi. Anita alivuta pumzi ndefu kisha akasimama.

“Sasa inabidi uwe makini zaidi, inaonesha hawa watu wanafuatilia kila tunalolifanya na inawezekana kuna mtu wa karibu sana anayewapa taarifa juu yetu. Mchukue Mike mwende mkaangalie kwenye hilo sanduku la posta kuna nini, ila narudia inabidi muwe makini kwani bila shaka kutakuwa na watu wanaowatazama. Pia mkiweza kumtambua yeyote anayewafuatilia itakuwa vizuri zaidi. Haya kazi njema”. Alisema Bi. Anita huku uso wake ukiwa umeelekezwa dirishani.

Jambo moja lilianza kuusumbua ubongo wa Bi. Anita, nalo si jingine ila ni lile la kujiona yuko uchi. Kwani inaonesha adui alikuwa akijua kila kitu kuhusiana na yeye.

Dakika kumi baadaye yule kijana wake aliyekuwa ameenda posta alikuwa tayari amerudi.

“Eeh yalikwendaje?” Aliuliza pale alipokuwa tayari ameshakaa.

“Hakuna cha ziada zaidi ya karatasi hii” Alisema huku akimkabidhi Bi. Anita ile karatasi aliyoichukua posta.

Kama kawaida ya mwandishi wa karatasi hizi, hakuwa na maneno mengi, safari hii alikuwa ameandika; NAMTAKA JACOB MATATA LA SIVYO JIANDAE BADO “PIGO LA MAUTI”. RAFIKI.

“Jacob!!! Jacob anahusiana vipi na mambo haya, na kwa nini wanamtaka?” Bi. Anita alijikuta akifoka huku akipiga ngumi juu ya meza.

Kwa mara ya kwanza ndipo mkuu huyu wa kitengo hiki maalum cha usalama alikumbuka kuwa zilikuwa zimepita situ kadhaa bila kumuona wala kusikia Sauti ya Jacob Matata.

Itaendelea
Tuendelee mkuu.
Tuko pamoja mkuu.
 
HEKAHEKA - 13

“Mmalizeni!!! Dereva wa gari lililokusudia kumgonga Jacob alipiga kelele. Wakati ukulele huo ukiishia hewani, risasi zilimiminika kuelekea pale alipokuwa amesimama Jacob. Kwa mshangao zilikuta hewa, kwani Jacob alikuwa amewahi na kujiviringisha chini. Bado akiwa anaviringika chini Jacob aliachilia risasi mfululizo ambazo ziliwamaliza jamaa wote.

* * *

Hii ilikuwa ni simu ya tatu kwa siku hii ya leo. Ilionekana kuwa mpigaji wa simu hii alikuwa ni mmoja. Muda ambao simu hiyo ilikuwa ikipigwa na ujumbe uliokuwa ndani ya simu hii vilimfanya Bi. Anita aamini kuwa mpigaji wa simu hii kama hakuwa ni shetani mwenyewe basi, bila shaka alikuwa ni mtu mwenye mawazo ya shetani. Alifikiri ni jinsi gani mtu huyu alijiamini kiasi cha kumpigia simu mara kwa mara kiasi hicho bila kuogopa. Alijaribu kufikiri sauti hii ambayo si ngeni sana kwake ilikuwa ni ya nani au aliwahi kuisikia wapi. Hakuweza kupata jibu lolote la kweli. Simu iliyokuwa ikitumika ilikuwa ni ile ya mezani, Bi. Anita hakuwa na uwezo wa kuona namba za mpigaji.

Baada ya kufikiri sana ndipo akaamua kumtuma mmoja kati ya vijana wake ili aende shirika la simu kuulizia mmiliki wa namba iliyokuwa imepigwa mara tatu kwenda ofisini hapo.

Muda mfupi mara baada ya Bi. Anita kumtuma mtu wake kwenda kuulizia juu ya mpigaji huyu, mara simu yake ya mezani iliita. Kabla ya kuinyanyua, Bi. Anita alichukua kifaa fulani ambacho kilikuwa maalum kwa ajili ya kunakili maongezi ya kwenye simu. Baada ya kuipachika sehemu fulani jirani na mkonga wa kuongelea na kusikilizia Bi. Anita aliipokea simu hiyo.

“Nani unaongea?” Aliuliza Bi. Anita kwa sauti ya kukereka kidogo.

“Ni yule rafiki yako anaeomba nafasi ya kukushauri” Ulijibu upande wa pili.

“Urafiki gani unaombwa pasipo na pande mbili kujuana? Huo si urafiki bali ni mtu mmoja anaemjua mwenzie kutaka kumteka asiyemjua mwenzie” Alisema Bi. Anita.

“Nashangaa sana pale unaposema kuwa hunijui ilhali kila leo unafikiri namna ya kupata nafasi ya kuonana na mimi, unanifahamu ila sema hujui niko wapi japo ningependa ujue niko wapi. Nashindwa kukujulisha kuwa niko wapi kwa vile bado hatujawa na mtazamo sawa, tukiwa marafiki unaruhusiwa kujua niko wapi.” Ilipofika hapo sauti hiyo ilisikika ikicheka kicheko cha kebehi. Kwa kushindwa kuficha chuki yake Bi. Anita alijikuta akifumba macho.

“Okay, pamoja na kuwa umekataa kusema jina lako na mahali ulipo lakini bado sikuelewi pale unaposoma kuwa nakufahamu ilhali sikufahamu, labda ungenikumbusha tuliwahi kuonana wapi, na ni mitazamo gani tunayotofautiana?” Bi. Anita aliuliza huku mtu wa upande wa pili akionekana mwenye furaha isiyo kifani. Sauti yake ilionesha hivyo.

“Ngoja kwanza nikukumbushe uliniona wapi, wiki mbili zilizopita saa kumi usiku ulikuja kuniona pale Benki ilipovunjwa na kuibiwa mabilioni ya Shilingi. Ni kweli kuwa hukuiona sura yangu lakini matendo yangu uliyaona, wiki moja baadae ulikuja kuniona pale mabilioni ya Shilingi ya kampuni ya kutengeneza bia yalipoporwa, ilikuwa ni saa tisa alasiri juzi usiku ulikuja kuniona pale Shinyanga katika tukio ambalo nilikuwa nimeenda kuchukua madini, japo nyie mnasema ni kuiba. Nasema tuna tofauti za kimtazamo kwa vile mara zote ambazo umekuwa ukija kuniona na kufanikiwa kuiona sura yangu kwa njia ya matukio yangu umekuwa ukionesha masikitiko na hasira kuu. Tofauti na mimi ambaye hata hivyo mara kwa mara nimekuwa nikiwa hatua chache sana toka pale unapokuwa umesimama. Kwani licha ya kuwepo kwenye matukio hayo kwa njia ya matendo lakini mara nyingi kiwiliwili changu huwepo kwa vile huwa na hamu ya kumuona rafiki yangu ambaye ni wewe.”

Kinachonishangaza ni kuwa mara zote umekuwa ukichukia pale ninapofurahi, unalia pale ninapocheka, unajiandaa kupigana sehemu ambayo naona inafaa nijiandae kusheherekea. Unalinda sehemu ambayo ningependa iwe wazi masaa ishirini na nne. Hizo ndizo tofauti za kimtazamo zilizopo kati yangu na wewe, lakini nadhani wakati umefika ambapo tunatakiwa kuzika tofauti hizo, kwani tusipofanya hivyo waweza kufa kwa shinikizo la moyo. Nimetangulia kusema kuwa najua kwa sasa unatafuta namna ya kukifikia kiwiliwili changu. Ningefurahi sana kuwa mwenyeji wako kwani kwa hivi sasa nimetoka kuchukua benki statement inayoonesha kuwa mamilioni ya pesa niliyochukua pale kampuni ya bia na benki tayari yameshaingia kwenye akaunti yangu. Pia nimepokea taarifa kuwa yale madini niliyochukua kule Shinyanga yameshapata mnunuzi.

Nasikitika kwa vile unataka niendelee kuwa maskini huku tukiwaachia wazungu watajirike. Nadhani ungeniona hapa nilipokaa ungechoka kabisa kwani watu wanaosubiri taarifa za mapato na matumizi ya pesa hizo wengine wana cheo kuliko cha kwako. Naamini unaweza kuwa mmoja wao, unaweza kuwa unapata mamilioni ya Shilingi kwa mwezi kwa kazi ngumu ya kuwa unaweka miguu juu ya meza na kustarehe, tofauti na sasa ambapo unapokea vishilingi vichache ilhali unakesha katika kutafuta namna ya kufika mahali nilipo na kuharibu starehe yangu na wakubwa wako.

Vipi rafiki umefikia wapi katika kutafuta mpenyo wa kunifikia, inashangaza kwa sababu badala ya kutumia muda wako kutafuta pesa, wewe unautumia katika kupanga mipango ya kuwaharibia wenzio wenye shida na pesa na wanaojua matumizi yake. Juhudi hizo ungezielekeza pengine bila shaka ungekuwa tajiri kama mimi na wale walio na mtazamo kama wangu. Oooh Samahani nimekuwa msemaji sana, ila kumbuka kuwa unawajibu wa kufanya jambo kwa ajili ya matukio haya usinyamaze kana kwamba huyaoni” Ilimaliza sauti hiyo kwa kicheko ambacho kilisaidiwa na vicheko vya watu wengine waliosikika kuwa walikuwa karibu sana na muongeaji.

“Kama ulivyosema kuwa tunatofautiana mtazamo, hivyo kwa vile wewe una maneno mengi wakati huu basi mimi sina maneno mengi ili kwamba wakati nitakapokuwa na maneno mengi, wakati kichwa chako kikiwa kinaelekea kwenye kitanzi tayari kwa kunyongwa, nawe hutakuwa na maneno mengi. Kwa sasa niache niendelee na kazi uayoiona kama kazi kichaa, wasalimie hao wanaovuna wasipopanda na kukusanya wasipotawanya. Waambie watalipa udhalimu wanaowafanyia watu waliowaamini na kuwapa heshima ya kuwaongoza kumbe wao wanawadhihaki” Maneno hayo Bi. Anita aliyaongea huku akiwa bado amefunika macho kutokana na uchungu. Hata hivyo maneno hayo yalipokewa kwa vicheko toka upande wa pili. Kisha Bi. Anita hakuona haja ya kuendelea kuhojiana na hao watu, hivyo akaazimia kukata simu. Wakati anataka kuweka chini mkonga wa simu kuna neno akalisikia, neno lenyewe lilikuwa ni “….Kesho Leaders Club saa tatu usiku….” Aliuweka chini mkono wa simu.

Maneno yaliyoongewa na huyu mtu anayejiita kama rafiki yaliutibuwa kabisa ubongo wa Bi. Anita, akajikuta anatamani sana kupokea taarifa toka kwa kijana wake juu ya mmliki wa namba ya simu iloyokuwa ikitumiwa na mtu anayejiita ‘rafiki’.

Alitulia tuli juu ya kochi lake kubwa huku akijaribu kuyatafakari maneno yote yaloyokuwa yakisemwa na ‘rafiki’. Alishangaa, kwani kwa uzoefu na utaalamu alionao ulionesha kuwa mara nyingi wahalifu hutafutwa na siyo kujileta kama huyu. Ikitokea kuwa amejileta basi ujue kuwa kuna hila imefichika ndani ya moyo wake na kuwa adui huyo ni moto wa kuotea mbali.

Alifikiri ni jinsi gani wizi huu mfululizo ulivyopelekea jeshi la polisi kupakwa matope na watu mbalimbali kwa kile kilichoosemwa kuwa lilikuwa limeshindwa kuhakikisha usalama wa watu na mali zao. Hali hii iliyopelekea mkuu wa jeshi la polisi na waziri wa mambo ya ndani wajiuzulu mara baada ya shutuma dhidi yao kuzidi.

Kuona hivyo Rais kwa kutumia njia ya siri kabisa aliweza kumtaarifu Bi. Anita juu ya haja yake ya kutaka ofisi fukuzi ijiingize katika kutafuta ukweli juu ya matukio haya ya wizi wa kimataifa.

Masaa machache tu mara baada ya kupokea jukumu hilo toka kwa Rais, Bi. Anita alipokea simu toka kwa mtu huyu anayejiita ‘rafiki’. Katika simu hiyo ya kwanza ‘rafiki’ alisema alikuwa anampongeza Bi. Anita kwa kupewa jukumu hilo gumu, la siri na la kitaifa.

Baada ya Bi. Anita kutafakari kwa kina juu ya ujumbe huo toka kwa ‘rafiki’ ndipo kwa siri akamtumia taarifa Rais kumtaka kutowasiliana nae kwa njia yoyote zaidi ya wao kuonana ana kwa ana. Bi. Anita alimueleza Rais kuwa sababu kuu yeye kufanya hivyo kuwa amegundua kuwa kuna mtu anavujisha siri. Alishangaa zaidi pale alipopokea simu ya pili toka kwa ‘rafiki’. Katika simu hii ‘rafiki’ alikuwa anampongeza Bi. Anita kwa kuwa makini na kubuni njia nzuri ya kuwasiliana na Rais. Kwanza Bi. Anita aliogopa lakini baadaye aliamua kufuatilia ili kujua juu ya mtu huyu anayejiita ‘rafiki’. Ndipo hapo akaamua kumtuma mtu kwenda shirika la simu ili kujua mmiliki wa namba ya simu iliyokuwa ikitumiwa na ‘rafiki’. Wakati akisubiri taarifa toka shirika la simu ndipo alipopokea simu hii ya tatu toka kwa ‘rafiki’, safari hii rafiki akiongea kwa kirefu.

“Bosi, watu wa simu wanasema namba hiyo ni ya biashara na inamilikiwa na msichana mmoja aitwaye Joyce” Alisema huyu kijana ambaye alionesha hofu hasa mara baada ya kuiona sura ya Bi. Anita. Sura ya Bi. Anita ilionesha wazi wazi hasira, ilikuwa ya baridi sana.

“Huyo Joyce wamesema anaishi wapi?”

“Wamesema wakati anakuja kuchukua namba ya sanduku la posta na hiyo namba ya simu ya biashara alijiandikisha kama anaishi kinondoni makaburini. Kwa hiyo hawajui kama bado anaishi hapo au alishahama, nimejaribu kuwaulizia kama wanajua sehemu yake ya biashara wakasema hilo hawajui”.

“Sawa hebu fanya utaratibu ili uweze kupata anapoishi kama ukimpata mlete hapa pasipo yeye kujua, nafikiri nikisema hivyo unanielewa”

“Ndio bosi” Alisema kijana huyo aliyeonesha kila dalili kuwa alikuwa mtii na tayari kufanya lolote aliloambiwa na bosi wake.

Kijana huyo alipoondoka, Bi. Anita alizama tena katika mawazo juu ya mtu huyu ajiitaye ‘rafiki’. Aliwaza mengi, Hatimaye akafikia pale ‘rafiki’ aliposema kuwa yuko na watu ambao wengine ni wana vyeo kuliko yeye Bi. Anita. Alifikiri juu ya mtazamo wa viongozi wengi wa Afrika pale wanapokabidhiwa madaraka na wananchi, wengi hudhani kuwa wamepewa nafasi ya kujinufaisha binafsi. Hivyo wanapoingia madarakani tu, husahau wajibu wao kwa wananchi na badala yake hutimiza wajibu kwa matumbo yao na uchu walionao.

Mawazo yake hayo yaligutuliwa baada ya sauti ya mtu aliyekuwa akibisha mlango.

“Ingia ndani” Alisema huku akiruhusu viganja kupita juu ya uso wake kwa staili ya kufuta, bila shaka hii ni dalili ya kuhama kimawazo na kurudi ofisini. Yule kijana aliyemtuma kwa Joyce binti mwenye namba za simu zilizokuwa zimetumiwa na ‘rafiki’ alikuwa amesharudi.

“Bosi, nimeenda lakini tofauti na matarajio yetu, sijamkuta Joyce tuliyekuwa tukimtaka. Badala yake nimekutana na maiti ya Joyce, pembeni yake nilikuta karatasi hii ambayo ina namba za sanduku la posta”. Alisema huku akimkabidhi Bi. Anita hicho kijikaratasi ambacho hakikuwa na lolote zaidi ya namba za sanduku la posta. Alipofika hapo Bi. Anita alivuta pumzi ndefu kisha akasimama.

“Sasa inabidi uwe makini zaidi, inaonesha hawa watu wanafuatilia kila tunalolifanya na inawezekana kuna mtu wa karibu sana anayewapa taarifa juu yetu. Mchukue Mike mwende mkaangalie kwenye hilo sanduku la posta kuna nini, ila narudia inabidi muwe makini kwani bila shaka kutakuwa na watu wanaowatazama. Pia mkiweza kumtambua yeyote anayewafuatilia itakuwa vizuri zaidi. Haya kazi njema”. Alisema Bi. Anita huku uso wake ukiwa umeelekezwa dirishani.

Jambo moja lilianza kuusumbua ubongo wa Bi. Anita, nalo si jingine ila ni lile la kujiona yuko uchi. Kwani inaonesha adui alikuwa akijua kila kitu kuhusiana na yeye.

Dakika kumi baadaye yule kijana wake aliyekuwa ameenda posta alikuwa tayari amerudi.

“Eeh yalikwendaje?” Aliuliza pale alipokuwa tayari ameshakaa.

“Hakuna cha ziada zaidi ya karatasi hii” Alisema huku akimkabidhi Bi. Anita ile karatasi aliyoichukua posta.

Kama kawaida ya mwandishi wa karatasi hizi, hakuwa na maneno mengi, safari hii alikuwa ameandika; NAMTAKA JACOB MATATA LA SIVYO JIANDAE BADO “PIGO LA MAUTI”. RAFIKI.

“Jacob!!! Jacob anahusiana vipi na mambo haya, na kwa nini wanamtaka?” Bi. Anita alijikuta akifoka huku akipiga ngumi juu ya meza.

Kwa mara ya kwanza ndipo mkuu huyu wa kitengo hiki maalum cha usalama alikumbuka kuwa zilikuwa zimepita situ kadhaa bila kumuona wala kusikia Sauti ya Jacob Matata.

Itaendelea
Aksante sana mkuu.....fanya hisani utuongezee japo nyingine tena, imekuwa na mvuto sana hii.
 
HEKAHEKA - 14

Kama kawaida ya mwandishi wa karatasi hizi, hakuwa na maneno mengi, safari hii alikuwa ameandika; NAMTAKA JACOB MATATA LA SIVYO JIANDAE BADO “PIGO LA MAUTI”. RAFIKI.

“Jacob!!! Jacob anahusiana vipi na mambo haya, na kwa nini wanamtaka?” Bi. Anita alijikuta akifoka huku akipiga ngumi juu ya meza.

Kwa mara ya kwanza ndipo mkuu huyu wa kitengo hiki maalum cha usalama alikumbuka kuwa zilikuwa zimepita situ kadhaa bila kumuona wala kusikia Sauti ya Jacob Matata.

Baada ya kusoma ujumbe huo ambao bila shaka ulikuwa umetoka kwa ‘rafiki’ ambaye bila shaka alijua kuwa utamfikia, mawazo ya Bi. Anita yaliweza kuona kila dalili ya hatari iliyokuwa mbele yake. Kwa jinsi alivyolichukulia swala hili alijiona kuwa anacheza na moto. Ofisi yake ilikuwa imesheeni kila aina ya wataalamu katika fani hii ya ukachero. Lakini makachero hawa walikuwa wanatofautiana kiuwezo na ngazi, hivyo akajiona mpumbavu kwa kuwa anamtuma huyu kijana kuanza kufuatilia jambo hili. Isitoshe yeye Bi. Anita kazi yake ni kupanga nani afanye nini wapi. Kazi yake haikuwa kufanya kazi bali kupinga nani afanye nini na kumpa mazingira na mamlaka ya kufanya hivyo. Hivyo akaona umuhimu wa kushughulikia suala hili.

“Asante nimepata ujumbe aliotaka niupate, waweza kwenda” Alisema Bi. Anita huku akinyanyua mkonga wa simu.

* * *

Kitendo cha kusikia kuwa Jacob Matata yuko katika harakati za kuweza kuifikia himaya yake hii kilimkera sana mzee huyu. Hivyo pamoja na kuwatuma vijana wake chini ya Bob Sepeto kumfuatilia Jacob Matata lakini pia aliamua kuwatumia vibaraka wake serikalini ili aweze kupata nyenendo za mpelelezi hatari Jacob Matata.

Hivyo kwa nyakati tofauti tofauti alianza kuulizia juu ya mpelelezi Jacob Matata. Hapo ndipo alipoweza kupata taarifa juu ya makazi ya Jacob Matata na kitengo alichokuwa akifanyia kazi. Hapo akaamua kutumia mbinu mbalimbali ili kuweza kumpata mtu huyu hatari.

Ni katika harakati zake hizo, ndipo mzee Harken Kalm simu yake ilifika kwa Mkuu wa Jacob Matata, Bi. Anita, na kujitambulisha kwa jina la ‘rafiki’. Katika hali ya kumtisha na kumshawishi Bi. Anita atoe taarifa za Jacob Matata, ndipo akamtumia ule ujumbe kwa njia ya posta.

* * *

Saa tatu kasorobo usiku, siku iliyofuata iliwakuta makachero kadhaa hatari toka ofisi fukuzi wakiwa tayari wanarandaranda maeneo ya ukumbi wa leaders club. Bi. Anita aliamua kufanya hivyo mara baada ya kubahatisha kumsikia mtu anayejiita ‘rafiki’ akiwaambia wenzie kuwa wakutane hapo saa tatu usiku huo. Hivyo alikuwa amewatuma ili kuweza kuangalia uwezekano wa kumpata huyo mtu aliyejiita ‘rafiki’.

Kwa upande wake mzee Harken Kalm au ‘rafiki’ kama alivyojitambulisha kwa Bi. Anita, alikuwa ameongea hivyo makusudi kabisa. Alijua fika kuwa kama Bi. Anita angesikia asingeacha kutuma makachero Leaders Club ili wajaribu kumkamata. Lengo lake ilikuwa ni kumuwinda mpelelezi Jacob Matata.

“Mkienda hapo hakikisheni mnaangalia kama Jacob atakuwa miongoni mwa makachero watakaotumwa pale leaders Club. Hivyo mkimuona mleteni akiwa hai au maiti yake” Hii ilikuwa ni sehemu ya mwisho ya maelezo ya mzee Harken Kalm kwa vijana wake chini ya uongozi wa Bob Sepeto mwenyewe.

Hivyo wakati makachero toka ofisi fukuzi wakiwa wanafanya doria maeneo hayo kwa siri, vijana toka kwa mzee Harken Kalm nao walikuwa katika msako wa kuona kama Jacob alikuwa maeneo hayo na kama alikuwepo wamkamate au kumuua. Vijana wa mzee Harken Kalm hawakuwa wakimjua kachero yeyote mwingine zaidi ya Jacob Matata ambaye walikuwa wamepewa picha zake. Lakini hii haikuwazuia kuweza kuwatambua makachero wengine waliokuwa eneo hilo. Hii ni kutokana na ujuzi waliokuwa nao juu ya makachero.


Jacob kwa upande wake alikuwa amepata taarifa za kuwa na watu wanomtaka hapo Leaders Club. Taarifa hizo alizipata kupitia kwa Bi. Anita. Bi. Anita alimtaka Jacob awepo mahali hapo ili kuona kama wangeweza kuwanasa jamaa hao. Yeye Jacob ndiye aliyekuwa wa kwanza kabisa kufika eneo hilo. Alikuwa ametafuta mahali pazuri na kuegesha gari alilokuwa amekuja nalo. Hivyo aliweza kuwaona makachero wenzake wakati wakiingia eneo hilo. Kama alivyotarajia makachero hao hawakuja na gari. Walikuja mmoja mmoja kwa miguu, aliangalia jinsi walivyokuwa wamejipanga.

Hata pindi kundi lingine la vijana wa mzee Harken Kalm linaingia Jacob aliweza kuona na kuhisi. Lakini hakuwa na papara, alijua fika kuwa alihitaji muda. Pamoja na zana nyingine za kazi mikononi mwake alikuwa ameshikilia picha kadhaa. Picha hizo ndizo zile alizokuwa amezichukua wakati ule alipokuwa ameenda kwenye kambi ya Koboyo. Hivyo kwa kutumia picha hizo aliweza kuwatambua baadhi yao waliokuwa wakifika eneo hilo usiku huo.

Jambo moja lilimfurahisha Jacob ni kuwa watu wa pande zote mbili hawakuweza kutambuana. Vijana wa mzee Harken Kalm hawakuashiria kuwajali sana makachero waliokuwa wakipishana nao, kadhalika makachero hawakuweza kujua kuwa watu waliokuwa wakipishana nao na wakati mwingine kuongea nao ndio walikuwa watu wabaya hasa.

Jacob Matata hakushuka toka ndani ya gari, mpaka pale ilipotimu saa sita na dakika ishirini usiku. Muda huo watu wote walikuwa wametokomea ndani ya ukumbi. Kila kundi likijaribu kuangalia uwezekano wa kumuwahi mwenzake. Ni wakati huo ambao Jacob aliangaza macho huko na huko bila kuona mtu. Alikusanya zana zake na kuzipakia sehemu mbalimbali za mwili wake. Taratibu na kwa hadhali kubwa kama mtu anayekwenda kupokea mkate wa Bwana, Jacob alishuka ndani ya gari na kulifunga kabla ya kuanza kuondoka.

Safari yake iliishia kwenye gari moja waliyokuwa wamekuja nayo vijana wa mzee Harken Kalm. Hapo kwa hadhali ya ziada alizunguka mpaka upande wa nyuma wa gari. Akafungua buti ya gari hiyo ili aweke vitu vyake na kisha mwenyewe aingie. Aliweka begi lake, kisha wakati anajiweka sawa ili aingie alishitukia sauti ikimwamuru tokea nyuma, “tulia hivyo hivyo, la sivyo utanilazimisha kutumia silaha yangu” alitii na kutulia maana aliweza kuuhisi ubaridi wa mdomo wa bastola kwenye kichwa chake.

Hiyo ilikuwa ni sauti ya Bob Sepeto ambaye hakuwa ameingia ndani kama wengine badala yake alijibanza sehemu ili kuweza kuona hali ya hapo nje. Alikuwa macho kama paka mwenye njaa. Aliweza kumuona na kumtambua Jacob, tangu pale aliposhuka kwenye gari na kuanza kuelekea kwenye gari hii ambayo Bob Sepeto na kundi lake walikuwa wamekuja nalo.

“Najua una hamu ya kuitumia na wala haina haja ya mimi kukulazimisha” Jacob alisema hayo huku akiwa anavuta muda wa kuangalia ni namna gani angeweza kujinasua hapo.

“Nadhani hunijui vizuri bwana Jacob, nimekuambia tulia hivyo ulivyo na nisingependa mahojiano na wewe” Bob alisema hayo kisha akaachilia konde zito lilotua shingoni kwa Jacob na kumfanya apepesuke. Kwa upande wake Jacob aliona kuwa hiyo ilikuwa nafasi yake ya pekee. Alijifanya kama anaetaka kuanguka kufuatia lile konde. Bob akafanya kosa jingine kwa kurudi nyuma nukta chache, kufumba na kufumbua teke la Jacob lilikuwa limetua kwenye mbavu zake, akateteleka.

Jacob akaja kwa judo kwa nia ya kummaliza Bob, akakuta Bob kisha jipanga na kuikwepa. Sasa wakawa wanatazamana damu ya Jacob tayari ikawa inachemka tayari kwa mapambano. Aliruka kama anaetaka kupaa na kuachia teke kali ambalo hata hivyo Bob aliliona na kuachia ngumi iliyompata Jacob. Kufuatia umahili huu ambao Bob aliuonesha, Jacob akajua kuwa alikuwa anapambana na mtu hatari hivyo ilimbidi kutumia ujuzi zaidi.

Hii ni riwaya yangu ya kwanza kuandika. Niliiandika mwaka 2004 na kuitolea kitabu mwaka 201x.

Itaendelea kesho, kama bado ina mvuto lakini. Salamu zenu toka Congo
 
HEKAHEKA - 14

Kama kawaida ya mwandishi wa karatasi hizi, hakuwa na maneno mengi, safari hii alikuwa ameandika; NAMTAKA JACOB MATATA LA SIVYO JIANDAE BADO “PIGO LA MAUTI”. RAFIKI.

“Jacob!!! Jacob anahusiana vipi na mambo haya, na kwa nini wanamtaka?” Bi. Anita alijikuta akifoka huku akipiga ngumi juu ya meza.

Kwa mara ya kwanza ndipo mkuu huyu wa kitengo hiki maalum cha usalama alikumbuka kuwa zilikuwa zimepita situ kadhaa bila kumuona wala kusikia Sauti ya Jacob Matata.

Baada ya kusoma ujumbe huo ambao bila shaka ulikuwa umetoka kwa ‘rafiki’ ambaye bila shaka alijua kuwa utamfikia, mawazo ya Bi. Anita yaliweza kuona kila dalili ya hatari iliyokuwa mbele yake. Kwa jinsi alivyolichukulia swala hili alijiona kuwa anacheza na moto. Ofisi yake ilikuwa imesheeni kila aina ya wataalamu katika fani hii ya ukachero. Lakini makachero hawa walikuwa wanatofautiana kiuwezo na ngazi, hivyo akajiona mpumbavu kwa kuwa anamtuma huyu kijana kuanza kufuatilia jambo hili. Isitoshe yeye Bi. Anita kazi yake ni kupanga nani afanye nini wapi. Kazi yake haikuwa kufanya kazi bali kupinga nani afanye nini na kumpa mazingira na mamlaka ya kufanya hivyo. Hivyo akaona umuhimu wa kushughulikia suala hili.

“Asante nimepata ujumbe aliotaka niupate, waweza kwenda” Alisema Bi. Anita huku akinyanyua mkonga wa simu.

* * *

Kitendo cha kusikia kuwa Jacob Matata yuko katika harakati za kuweza kuifikia himaya yake hii kilimkera sana mzee huyu. Hivyo pamoja na kuwatuma vijana wake chini ya Bob Sepeto kumfuatilia Jacob Matata lakini pia aliamua kuwatumia vibaraka wake serikalini ili aweze kupata nyenendo za mpelelezi hatari Jacob Matata.

Hivyo kwa nyakati tofauti tofauti alianza kuulizia juu ya mpelelezi Jacob Matata. Hapo ndipo alipoweza kupata taarifa juu ya makazi ya Jacob Matata na kitengo alichokuwa akifanyia kazi. Hapo akaamua kutumia mbinu mbalimbali ili kuweza kumpata mtu huyu hatari.

Ni katika harakati zake hizo, ndipo mzee Harken Kalm simu yake ilifika kwa Mkuu wa Jacob Matata, Bi. Anita, na kujitambulisha kwa jina la ‘rafiki’. Katika hali ya kumtisha na kumshawishi Bi. Anita atoe taarifa za Jacob Matata, ndipo akamtumia ule ujumbe kwa njia ya posta.

* * *

Saa tatu kasorobo usiku, siku iliyofuata iliwakuta makachero kadhaa hatari toka ofisi fukuzi wakiwa tayari wanarandaranda maeneo ya ukumbi wa leaders club. Bi. Anita aliamua kufanya hivyo mara baada ya kubahatisha kumsikia mtu anayejiita ‘rafiki’ akiwaambia wenzie kuwa wakutane hapo saa tatu usiku huo. Hivyo alikuwa amewatuma ili kuweza kuangalia uwezekano wa kumpata huyo mtu aliyejiita ‘rafiki’.

Kwa upande wake mzee Harken Kalm au ‘rafiki’ kama alivyojitambulisha kwa Bi. Anita, alikuwa ameongea hivyo makusudi kabisa. Alijua fika kuwa kama Bi. Anita angesikia asingeacha kutuma makachero Leaders Club ili wajaribu kumkamata. Lengo lake ilikuwa ni kumuwinda mpelelezi Jacob Matata.

“Mkienda hapo hakikisheni mnaangalia kama Jacob atakuwa miongoni mwa makachero watakaotumwa pale leaders Club. Hivyo mkimuona mleteni akiwa hai au maiti yake” Hii ilikuwa ni sehemu ya mwisho ya maelezo ya mzee Harken Kalm kwa vijana wake chini ya uongozi wa Bob Sepeto mwenyewe.

Hivyo wakati makachero toka ofisi fukuzi wakiwa wanafanya doria maeneo hayo kwa siri, vijana toka kwa mzee Harken Kalm nao walikuwa katika msako wa kuona kama Jacob alikuwa maeneo hayo na kama alikuwepo wamkamate au kumuua. Vijana wa mzee Harken Kalm hawakuwa wakimjua kachero yeyote mwingine zaidi ya Jacob Matata ambaye walikuwa wamepewa picha zake. Lakini hii haikuwazuia kuweza kuwatambua makachero wengine waliokuwa eneo hilo. Hii ni kutokana na ujuzi waliokuwa nao juu ya makachero.


Jacob kwa upande wake alikuwa amepata taarifa za kuwa na watu wanomtaka hapo Leaders Club. Taarifa hizo alizipata kupitia kwa Bi. Anita. Bi. Anita alimtaka Jacob awepo mahali hapo ili kuona kama wangeweza kuwanasa jamaa hao. Yeye Jacob ndiye aliyekuwa wa kwanza kabisa kufika eneo hilo. Alikuwa ametafuta mahali pazuri na kuegesha gari alilokuwa amekuja nalo. Hivyo aliweza kuwaona makachero wenzake wakati wakiingia eneo hilo. Kama alivyotarajia makachero hao hawakuja na gari. Walikuja mmoja mmoja kwa miguu, aliangalia jinsi walivyokuwa wamejipanga.

Hata pindi kundi lingine la vijana wa mzee Harken Kalm linaingia Jacob aliweza kuona na kuhisi. Lakini hakuwa na papara, alijua fika kuwa alihitaji muda. Pamoja na zana nyingine za kazi mikononi mwake alikuwa ameshikilia picha kadhaa. Picha hizo ndizo zile alizokuwa amezichukua wakati ule alipokuwa ameenda kwenye kambi ya Koboyo. Hivyo kwa kutumia picha hizo aliweza kuwatambua baadhi yao waliokuwa wakifika eneo hilo usiku huo.

Jambo moja lilimfurahisha Jacob ni kuwa watu wa pande zote mbili hawakuweza kutambuana. Vijana wa mzee Harken Kalm hawakuashiria kuwajali sana makachero waliokuwa wakipishana nao, kadhalika makachero hawakuweza kujua kuwa watu waliokuwa wakipishana nao na wakati mwingine kuongea nao ndio walikuwa watu wabaya hasa.

Jacob Matata hakushuka toka ndani ya gari, mpaka pale ilipotimu saa sita na dakika ishirini usiku. Muda huo watu wote walikuwa wametokomea ndani ya ukumbi. Kila kundi likijaribu kuangalia uwezekano wa kumuwahi mwenzake. Ni wakati huo ambao Jacob aliangaza macho huko na huko bila kuona mtu. Alikusanya zana zake na kuzipakia sehemu mbalimbali za mwili wake. Taratibu na kwa hadhali kubwa kama mtu anayekwenda kupokea mkate wa Bwana, Jacob alishuka ndani ya gari na kulifunga kabla ya kuanza kuondoka.

Safari yake iliishia kwenye gari moja waliyokuwa wamekuja nayo vijana wa mzee Harken Kalm. Hapo kwa hadhali ya ziada alizunguka mpaka upande wa nyuma wa gari. Akafungua buti ya gari hiyo ili aweke vitu vyake na kisha mwenyewe aingie. Aliweka begi lake, kisha wakati anajiweka sawa ili aingie alishitukia sauti ikimwamuru tokea nyuma, “tulia hivyo hivyo, la sivyo utanilazimisha kutumia silaha yangu” alitii na kutulia maana aliweza kuuhisi ubaridi wa mdomo wa bastola kwenye kichwa chake.

Hiyo ilikuwa ni sauti ya Bob Sepeto ambaye hakuwa ameingia ndani kama wengine badala yake alijibanza sehemu ili kuweza kuona hali ya hapo nje. Alikuwa macho kama paka mwenye njaa. Aliweza kumuona na kumtambua Jacob, tangu pale aliposhuka kwenye gari na kuanza kuelekea kwenye gari hii ambayo Bob Sepeto na kundi lake walikuwa wamekuja nalo.

“Najua una hamu ya kuitumia na wala haina haja ya mimi kukulazimisha” Jacob alisema hayo huku akiwa anavuta muda wa kuangalia ni namna gani angeweza kujinasua hapo.

“Nadhani hunijui vizuri bwana Jacob, nimekuambia tulia hivyo ulivyo na nisingependa mahojiano na wewe” Bob alisema hayo kisha akaachilia konde zito lilotua shingoni kwa Jacob na kumfanya apepesuke. Kwa upande wake Jacob aliona kuwa hiyo ilikuwa nafasi yake ya pekee. Alijifanya kama anaetaka kuanguka kufuatia lile konde. Bob akafanya kosa jingine kwa kurudi nyuma nukta chache, kufumba na kufumbua teke la Jacob lilikuwa limetua kwenye mbavu zake, akateteleka.

Jacob akaja kwa judo kwa nia ya kummaliza Bob, akakuta Bob kisha jipanga na kuikwepa. Sasa wakawa wanatazamana damu ya Jacob tayari ikawa inachemka tayari kwa mapambano. Aliruka kama anaetaka kupaa na kuachia teke kali ambalo hata hivyo Bob aliliona na kuachia ngumi iliyompata Jacob. Kufuatia umahili huu ambao Bob aliuonesha, Jacob akajua kuwa alikuwa anapambana na mtu hatari hivyo ilimbidi kutumia ujuzi zaidi.

Hii ni riwaya yangu ya kwanza kuandika. Niliiandika mwaka 2004 na kuitolea kitabu mwaka 201x.

Itaendelea kesho, kama bado ina mvuto lakini. Salamu zenu toka Congo
Tuendelee chief.
 
HEKAHEKA - 15

Kwa vile Jacob alikuwa amesimama jirani mno na Bob, kufumba na kufumbua Jacob alijikuta yuko chini. Bob alifanikiwa kumchota mtama wa staili ambayo wachina wameibatiza jina la ‘shishogh’.

Jacob alipoamka hakumkuta Bob, alikuja akitahamaki kuona gari aliyokuwa ameshaweka vitu vyake ikiwa inawashwa. Alisimama haraka na kutaka kukimbilia upande wa dereva. Alikuwa ameshachelewa, Bob alikuwa ameshatia gari moto na kuanza kuondoka kwa kasi.

Kuona hivyo Jacob Matata alifanya mambo matatu kwa wakati mmoja, alianza kukimbia kuelekea alipokuwa ameacha gari lake huku akiwa anakwepa risasi toka kwa Bob aliyekuwa anaondoka na gari kwa kasi huku akiachia risasi kuelekea alipokuwa Jacob.

Bob hakumuogopa Jacob, ila aliona ingemchukua muda mrefu na nguvu nyingi mpaka kumshinda Jacob. Hakuona kuwa pale ilikuwa ni mahali sahihi kwa ajili ya vita yao. Hivyo aliamua kutumia hila ili amvute Jacob Matata waende nae kwenye uwanja ambao aliamini kuwa wangeweza kuwa na nafasi nzuri ya kupambana.

Wakati gari ya Bob inatokomea gizani, tayari Jacob alikuwa ameshawasha gari na kuliondoa kwa kasi.

Milio ya mataili ya magari viliwashitua makachero wote waliokuwa ndani ya ukumbi wa leaders club. Kwa nyakati tofauti wote walitoka nje, lakini si wao tu walioshituliwa na milio hiyo bali hata watu wa kundi la Bob walishituka sana.

Walipotoka nje hawakuona lolote kwani wale mafahali wawili wakati huo tayari walikuwa mtaani wanafukuzana. Ni vijana wa Bob Sepeto ndio waliogundua tofauti, hawakuliona gari la bosi wao-Bob Sepeto.

“Bosi salama na uko wapi?” Mmoja alikumbuka kumuuliza Bob kwa njia ya simu.

“Ninaelekea mchangani lodge, njooni hapo baada ya kama dakika kumi toka sasa” sauti hii ya Bob ilikuwa ya utulivu kiasi kuwa isingekuwa rahisi kwa kijana wake huyu kuamini kuwa Bob alikuwa akiendesha gari kwa mwendo wa kutisha.

Jacob alifanikiwa kuliona gari la Bob Sepeto kwa mbali sana. Hii ilitokana na muundo wa gari hilo na kwa vile magari yalishapungua sana barabarani. Vinginevyo isingekuwa rahisi hasa kwa vile ilivyokuwa usiku.



Dakika chache baadaye, Bob sepeto ndiye aliyekuwa wa kwanza kuingia Mchangani Lodge. “Kuna mgeni wangu anakuja kuniulizia, mwambie niko namba 15A” alisema hayo alipokuwa anapita mapokezi. Hakugeuka kumuangalia yule binti wa mapokezi wala hakusimama, alipitiliza moja kwa moja kwenda kilipokuwa chumba namba 15A.

Sekunde kadhaa baadaye mpelelezi Jacob Matata aliingia, hakwenda mapokezi kuuliza, badala yake alipitiliza moja kwa moja. Alitembea taratibu kana kwamba mtu aliyekuwa na hakika na alipokuwa akienda. Jacob alifanya hivyo makusudi, maana alitegemea kuwa Bob Sepeto angekuwa katika mkao wa kumsubiri.

Huyo alitembea na kibaraza mpaka alipofika mwisho, akaingia kushoto na kukuta upenyo fulani kwa ajili ya mafundi wa hoteli hiyo. Hapo alibana na kusikiliza kwa makini, alitaka kujua kama kuna mtu alikuwa anamfuatilia. Alitulia hivyo kwa takribani dakika moja na ushee.

Bob Sepeto alikuwa chumbani ameshajiandaa kwa mpambano na mtu aliyekuwa amezisikia sifa zake nyingi. Damu yake ilikuwa inachemka tayari kwa pambano ambalo yeye aliamini kuwa lingekuwa zito. Dakika kumi na tano zilipita bila kuwepo na ishara yoyote ya Jacob kutokea. Bob alikuwa amejilaza kitandani huku akiwa ameshikiria gazeti. Ingekuwa ni mimi au wewe bila shaka yoyote tungeweza dhani kuwa alikuwa amezama katika habari zilizokuwa katika gazeti hilo, lakini haikuwa hivyo kwa Bob Sepeto. Alikuwa macho kama nini. Jacob aliyekuwa dirishani akimsanifu hasimu wake huyo nae aligundua kuwa Bob alikuwa makini sana, gazeti ilikuwa geresha tu. Baadaye Bob Sepeto alikuja gundua kuwa alikuwa amezidiwa kete kwa Jacob kufanikiwa kufika pale dirishani bila yeye kuwa na habari.

“Hongera, ingia ndani” Alisema Bob bila kugeuka wala kuangalia pale dirishani.

“Asante!” Alisema Jacob huku sasa akiwa anafungua dirisha ili aingie ndani. Haikuwa rahisi kuamini alifikaje pale.

Jacob alipoingia na kufika ndani, Bob aliweka gazeti pembeni tayari kwa kumpokea mgeni wake huyu ambaye hata hivyo aliingia katika staili ambayo hakuitegemea. Jacob alishatambua kuwa, Bob hakuwa mtu wa kuendewa kwa papara. Hivyo alipokanyaga sakafu ya chumba hicho alijisogeza kwenye kona moja ya chumba hicho kulipokuwa na kiti akakaa mkao egesha. Kwa jinsi chumba kilivyokuwa Bob alikuwa juu ya kitanda huku akiwa ameupa mgongo mlango. Kwa vile Bob alikuwa anatazamana na Jacob, hivyo Jacob alikuwa akitazamana na mlango pia.

Jacob alijitengeneza vizuri kwenye kiti na kuweka miguu katika mtindo wa nne. Sasa walikuwa wamekaa kama marariki waliokuwa wanaenda kwenye maongezi ya muda mrefu. Huku kila mmoja akiwa katika hadhari la hali ya juu kwa hasimu wake, Jacob alishangaa pale alipoona kitu kama chuma chembamba kinacheza kwenye kitasa cha mlango. Akawa chonjo zaidi. Bob aligundua tofauti katika macho ya Jacob, hivyo hisia mbili zikamjia kichwani. Kwanza alidhani ni danganya toto ya Jacob kumfanya ageuke na kutoa nafasi. Pili alidhani ni wale vijana wake aliowaamuru kuja hapo hotelini watakapoona amechelewa.

Sekunde chache baadaye Jacob alikuwa amerukia upande mwingine wa chumba huku mwili wa Bob ukiwa amelala pale kitandani na damu zikiwa zinatoka kisogoni kwake. Jacob aliwahi na kulenga usawa wa pale kilipokuwa kimetokeza kile chuma kilichotoa risasi iliyommaliza Bob. Jacob hakufanikiwa kummaliza. Haraka aliparamia mlango kwa lengo la kumuwahi muuaji wa Bob lakini alipofika nje ya mlango hakukuta mtu zaidi ya kijikaratasi kilichokuwa chini. Kabla ya kukiokota aliangalia huku na huko, ili kuangalia kama kulikuwa na mtu alikuwa amemtega. Alikiokota kiaina na kuangalia kilikuwa na nini. NAMTAKA REGINA KWA BEI YOYOTE ILE, BANZI. Hayo ni maneno yaliyokuwa kwenye kikaratasi hicho. Kifo cha Bob na huo ujumbe viliitibua akili ya Jacob. Hivi kuna upande mwingine tofauti na hawa unaomuhitaji Regina? Alijiuliza huku akitokomea. Banzi ni nani na anahusika vipi katika kisa hiki? Jacob akatabasamu nakuachilia pumzi “Kazi ipo” akanong'ona.

Upo msomaji wangu?
 
HEKAHEKA - 15

Kwa vile Jacob alikuwa amesimama jirani mno na Bob, kufumba na kufumbua Jacob alijikuta yuko chini. Bob alifanikiwa kumchota mtama wa staili ambayo wachina wameibatiza jina la ‘shishogh’.

Jacob alipoamka hakumkuta Bob, alikuja akitahamaki kuona gari aliyokuwa ameshaweka vitu vyake ikiwa inawashwa. Alisimama haraka na kutaka kukimbilia upande wa dereva. Alikuwa ameshachelewa, Bob alikuwa ameshatia gari moto na kuanza kuondoka kwa kasi.

Kuona hivyo Jacob Matata alifanya mambo matatu kwa wakati mmoja, alianza kukimbia kuelekea alipokuwa ameacha gari lake huku akiwa anakwepa risasi toka kwa Bob aliyekuwa anaondoka na gari kwa kasi huku akiachia risasi kuelekea alipokuwa Jacob.

Bob hakumuogopa Jacob, ila aliona ingemchukua muda mrefu na nguvu nyingi mpaka kumshinda Jacob. Hakuona kuwa pale ilikuwa ni mahali sahihi kwa ajili ya vita yao. Hivyo aliamua kutumia hila ili amvute Jacob Matata waende nae kwenye uwanja ambao aliamini kuwa wangeweza kuwa na nafasi nzuri ya kupambana.

Wakati gari ya Bob inatokomea gizani, tayari Jacob alikuwa ameshawasha gari na kuliondoa kwa kasi.

Milio ya mataili ya magari viliwashitua makachero wote waliokuwa ndani ya ukumbi wa leaders club. Kwa nyakati tofauti wote walitoka nje, lakini si wao tu walioshituliwa na milio hiyo bali hata watu wa kundi la Bob walishituka sana.

Walipotoka nje hawakuona lolote kwani wale mafahali wawili wakati huo tayari walikuwa mtaani wanafukuzana. Ni vijana wa Bob Sepeto ndio waliogundua tofauti, hawakuliona gari la bosi wao-Bob Sepeto.

“Bosi salama na uko wapi?” Mmoja alikumbuka kumuuliza Bob kwa njia ya simu.

“Ninaelekea mchangani lodge, njooni hapo baada ya kama dakika kumi toka sasa” sauti hii ya Bob ilikuwa ya utulivu kiasi kuwa isingekuwa rahisi kwa kijana wake huyu kuamini kuwa Bob alikuwa akiendesha gari kwa mwendo wa kutisha.

Jacob alifanikiwa kuliona gari la Bob Sepeto kwa mbali sana. Hii ilitokana na muundo wa gari hilo na kwa vile magari yalishapungua sana barabarani. Vinginevyo isingekuwa rahisi hasa kwa vile ilivyokuwa usiku.



Dakika chache baadaye, Bob sepeto ndiye aliyekuwa wa kwanza kuingia Mchangani Lodge. “Kuna mgeni wangu anakuja kuniulizia, mwambie niko namba 15A” alisema hayo alipokuwa anapita mapokezi. Hakugeuka kumuangalia yule binti wa mapokezi wala hakusimama, alipitiliza moja kwa moja kwenda kilipokuwa chumba namba 15A.

Sekunde kadhaa baadaye mpelelezi Jacob Matata aliingia, hakwenda mapokezi kuuliza, badala yake alipitiliza moja kwa moja. Alitembea taratibu kana kwamba mtu aliyekuwa na hakika na alipokuwa akienda. Jacob alifanya hivyo makusudi, maana alitegemea kuwa Bob Sepeto angekuwa katika mkao wa kumsubiri.

Huyo alitembea na kibaraza mpaka alipofika mwisho, akaingia kushoto na kukuta upenyo fulani kwa ajili ya mafundi wa hoteli hiyo. Hapo alibana na kusikiliza kwa makini, alitaka kujua kama kuna mtu alikuwa anamfuatilia. Alitulia hivyo kwa takribani dakika moja na ushee.

Bob Sepeto alikuwa chumbani ameshajiandaa kwa mpambano na mtu aliyekuwa amezisikia sifa zake nyingi. Damu yake ilikuwa inachemka tayari kwa pambano ambalo yeye aliamini kuwa lingekuwa zito. Dakika kumi na tano zilipita bila kuwepo na ishara yoyote ya Jacob kutokea. Bob alikuwa amejilaza kitandani huku akiwa ameshikiria gazeti. Ingekuwa ni mimi au wewe bila shaka yoyote tungeweza dhani kuwa alikuwa amezama katika habari zilizokuwa katika gazeti hilo, lakini haikuwa hivyo kwa Bob Sepeto. Alikuwa macho kama nini. Jacob aliyekuwa dirishani akimsanifu hasimu wake huyo nae aligundua kuwa Bob alikuwa makini sana, gazeti ilikuwa geresha tu. Baadaye Bob Sepeto alikuja gundua kuwa alikuwa amezidiwa kete kwa Jacob kufanikiwa kufika pale dirishani bila yeye kuwa na habari.

“Hongera, ingia ndani” Alisema Bob bila kugeuka wala kuangalia pale dirishani.

“Asante!” Alisema Jacob huku sasa akiwa anafungua dirisha ili aingie ndani. Haikuwa rahisi kuamini alifikaje pale.

Jacob alipoingia na kufika ndani, Bob aliweka gazeti pembeni tayari kwa kumpokea mgeni wake huyu ambaye hata hivyo aliingia katika staili ambayo hakuitegemea. Jacob alishatambua kuwa, Bob hakuwa mtu wa kuendewa kwa papara. Hivyo alipokanyaga sakafu ya chumba hicho alijisogeza kwenye kona moja ya chumba hicho kulipokuwa na kiti akakaa mkao egesha. Kwa jinsi chumba kilivyokuwa Bob alikuwa juu ya kitanda huku akiwa ameupa mgongo mlango. Kwa vile Bob alikuwa anatazamana na Jacob, hivyo Jacob alikuwa akitazamana na mlango pia.

Jacob alijitengeneza vizuri kwenye kiti na kuweka miguu katika mtindo wa nne. Sasa walikuwa wamekaa kama marariki waliokuwa wanaenda kwenye maongezi ya muda mrefu. Huku kila mmoja akiwa katika hadhari la hali ya juu kwa hasimu wake, Jacob alishangaa pale alipoona kitu kama chuma chembamba kinacheza kwenye kitasa cha mlango. Akawa chonjo zaidi. Bob aligundua tofauti katika macho ya Jacob, hivyo hisia mbili zikamjia kichwani. Kwanza alidhani ni danganya toto ya Jacob kumfanya ageuke na kutoa nafasi. Pili alidhani ni wale vijana wake aliowaamuru kuja hapo hotelini watakapoona amechelewa.

Sekunde chache baadaye Jacob alikuwa amerukia upande mwingine wa chumba huku mwili wa Bob ukiwa amelala pale kitandani na damu zikiwa zinatoka kisogoni kwake. Jacob aliwahi na kulenga usawa wa pale kilipokuwa kimetokeza kile chuma kilichotoa risasi iliyommaliza Bob. Jacob hakufanikiwa kummaliza. Haraka aliparamia mlango kwa lengo la kumuwahi muuaji wa Bob lakini alipofika nje ya mlango hakukuta mtu zaidi ya kijikaratasi kilichokuwa chini. Kabla ya kukiokota aliangalia huku na huko, ili kuangalia kama kulikuwa na mtu alikuwa amemtega. Alikiokota kiaina na kuangalia kilikuwa na nini. NAMTAKA REGINA KWA BEI YOYOTE ILE, BANZI. Hayo ni maneno yaliyokuwa kwenye kikaratasi hicho. Kifo cha Bob na huo ujumbe viliitibua akili ya Jacob. Hivi kuna upande mwingine tofauti na hawa unaomuhitaji Regina? Alijiuliza huku akitokomea. Banzi ni nani na anahusika vipi katika kisa hiki? Jacob akatabasamu nakuachilia pumzi “Kazi ipo” akanong'ona.

Upo msomaji wangu?
Nipo
 
HEKAHEKA - 15

Kwa vile Jacob alikuwa amesimama jirani mno na Bob, kufumba na kufumbua Jacob alijikuta yuko chini. Bob alifanikiwa kumchota mtama wa staili ambayo wachina wameibatiza jina la ‘shishogh’.

Jacob alipoamka hakumkuta Bob, alikuja akitahamaki kuona gari aliyokuwa ameshaweka vitu vyake ikiwa inawashwa. Alisimama haraka na kutaka kukimbilia upande wa dereva. Alikuwa ameshachelewa, Bob alikuwa ameshatia gari moto na kuanza kuondoka kwa kasi.

Kuona hivyo Jacob Matata alifanya mambo matatu kwa wakati mmoja, alianza kukimbia kuelekea alipokuwa ameacha gari lake huku akiwa anakwepa risasi toka kwa Bob aliyekuwa anaondoka na gari kwa kasi huku akiachia risasi kuelekea alipokuwa Jacob.

Bob hakumuogopa Jacob, ila aliona ingemchukua muda mrefu na nguvu nyingi mpaka kumshinda Jacob. Hakuona kuwa pale ilikuwa ni mahali sahihi kwa ajili ya vita yao. Hivyo aliamua kutumia hila ili amvute Jacob Matata waende nae kwenye uwanja ambao aliamini kuwa wangeweza kuwa na nafasi nzuri ya kupambana.

Wakati gari ya Bob inatokomea gizani, tayari Jacob alikuwa ameshawasha gari na kuliondoa kwa kasi.

Milio ya mataili ya magari viliwashitua makachero wote waliokuwa ndani ya ukumbi wa leaders club. Kwa nyakati tofauti wote walitoka nje, lakini si wao tu walioshituliwa na milio hiyo bali hata watu wa kundi la Bob walishituka sana.

Walipotoka nje hawakuona lolote kwani wale mafahali wawili wakati huo tayari walikuwa mtaani wanafukuzana. Ni vijana wa Bob Sepeto ndio waliogundua tofauti, hawakuliona gari la bosi wao-Bob Sepeto.

“Bosi salama na uko wapi?” Mmoja alikumbuka kumuuliza Bob kwa njia ya simu.

“Ninaelekea mchangani lodge, njooni hapo baada ya kama dakika kumi toka sasa” sauti hii ya Bob ilikuwa ya utulivu kiasi kuwa isingekuwa rahisi kwa kijana wake huyu kuamini kuwa Bob alikuwa akiendesha gari kwa mwendo wa kutisha.

Jacob alifanikiwa kuliona gari la Bob Sepeto kwa mbali sana. Hii ilitokana na muundo wa gari hilo na kwa vile magari yalishapungua sana barabarani. Vinginevyo isingekuwa rahisi hasa kwa vile ilivyokuwa usiku.



Dakika chache baadaye, Bob sepeto ndiye aliyekuwa wa kwanza kuingia Mchangani Lodge. “Kuna mgeni wangu anakuja kuniulizia, mwambie niko namba 15A” alisema hayo alipokuwa anapita mapokezi. Hakugeuka kumuangalia yule binti wa mapokezi wala hakusimama, alipitiliza moja kwa moja kwenda kilipokuwa chumba namba 15A.

Sekunde kadhaa baadaye mpelelezi Jacob Matata aliingia, hakwenda mapokezi kuuliza, badala yake alipitiliza moja kwa moja. Alitembea taratibu kana kwamba mtu aliyekuwa na hakika na alipokuwa akienda. Jacob alifanya hivyo makusudi, maana alitegemea kuwa Bob Sepeto angekuwa katika mkao wa kumsubiri.

Huyo alitembea na kibaraza mpaka alipofika mwisho, akaingia kushoto na kukuta upenyo fulani kwa ajili ya mafundi wa hoteli hiyo. Hapo alibana na kusikiliza kwa makini, alitaka kujua kama kuna mtu alikuwa anamfuatilia. Alitulia hivyo kwa takribani dakika moja na ushee.

Bob Sepeto alikuwa chumbani ameshajiandaa kwa mpambano na mtu aliyekuwa amezisikia sifa zake nyingi. Damu yake ilikuwa inachemka tayari kwa pambano ambalo yeye aliamini kuwa lingekuwa zito. Dakika kumi na tano zilipita bila kuwepo na ishara yoyote ya Jacob kutokea. Bob alikuwa amejilaza kitandani huku akiwa ameshikiria gazeti. Ingekuwa ni mimi au wewe bila shaka yoyote tungeweza dhani kuwa alikuwa amezama katika habari zilizokuwa katika gazeti hilo, lakini haikuwa hivyo kwa Bob Sepeto. Alikuwa macho kama nini. Jacob aliyekuwa dirishani akimsanifu hasimu wake huyo nae aligundua kuwa Bob alikuwa makini sana, gazeti ilikuwa geresha tu. Baadaye Bob Sepeto alikuja gundua kuwa alikuwa amezidiwa kete kwa Jacob kufanikiwa kufika pale dirishani bila yeye kuwa na habari.

“Hongera, ingia ndani” Alisema Bob bila kugeuka wala kuangalia pale dirishani.

“Asante!” Alisema Jacob huku sasa akiwa anafungua dirisha ili aingie ndani. Haikuwa rahisi kuamini alifikaje pale.

Jacob alipoingia na kufika ndani, Bob aliweka gazeti pembeni tayari kwa kumpokea mgeni wake huyu ambaye hata hivyo aliingia katika staili ambayo hakuitegemea. Jacob alishatambua kuwa, Bob hakuwa mtu wa kuendewa kwa papara. Hivyo alipokanyaga sakafu ya chumba hicho alijisogeza kwenye kona moja ya chumba hicho kulipokuwa na kiti akakaa mkao egesha. Kwa jinsi chumba kilivyokuwa Bob alikuwa juu ya kitanda huku akiwa ameupa mgongo mlango. Kwa vile Bob alikuwa anatazamana na Jacob, hivyo Jacob alikuwa akitazamana na mlango pia.

Jacob alijitengeneza vizuri kwenye kiti na kuweka miguu katika mtindo wa nne. Sasa walikuwa wamekaa kama marariki waliokuwa wanaenda kwenye maongezi ya muda mrefu. Huku kila mmoja akiwa katika hadhari la hali ya juu kwa hasimu wake, Jacob alishangaa pale alipoona kitu kama chuma chembamba kinacheza kwenye kitasa cha mlango. Akawa chonjo zaidi. Bob aligundua tofauti katika macho ya Jacob, hivyo hisia mbili zikamjia kichwani. Kwanza alidhani ni danganya toto ya Jacob kumfanya ageuke na kutoa nafasi. Pili alidhani ni wale vijana wake aliowaamuru kuja hapo hotelini watakapoona amechelewa.

Sekunde chache baadaye Jacob alikuwa amerukia upande mwingine wa chumba huku mwili wa Bob ukiwa amelala pale kitandani na damu zikiwa zinatoka kisogoni kwake. Jacob aliwahi na kulenga usawa wa pale kilipokuwa kimetokeza kile chuma kilichotoa risasi iliyommaliza Bob. Jacob hakufanikiwa kummaliza. Haraka aliparamia mlango kwa lengo la kumuwahi muuaji wa Bob lakini alipofika nje ya mlango hakukuta mtu zaidi ya kijikaratasi kilichokuwa chini. Kabla ya kukiokota aliangalia huku na huko, ili kuangalia kama kulikuwa na mtu alikuwa amemtega. Alikiokota kiaina na kuangalia kilikuwa na nini. NAMTAKA REGINA KWA BEI YOYOTE ILE, BANZI. Hayo ni maneno yaliyokuwa kwenye kikaratasi hicho. Kifo cha Bob na huo ujumbe viliitibua akili ya Jacob. Hivi kuna upande mwingine tofauti na hawa unaomuhitaji Regina? Alijiuliza huku akitokomea. Banzi ni nani na anahusika vipi katika kisa hiki? Jacob akatabasamu nakuachilia pumzi “Kazi ipo” akanong'ona.

Upo msomaji wangu?
Tuendelee chief.
Naona mambo yanazidi kunoga mkuu.
 
HEKAHEKA - 16

Sekunde chache baadaye Jacob alikuwa amerukia upande mwingine wa chumba huku mwili wa Bob ukiwa amelala pale kitandani na damu zikiwa zinatoka kisogoni kwake. Jacob aliwahi na kulenga usawa wa pale kilipokuwa kimetokeza kile chuma kilichotoa risasi iliyommaliza Bob. Jacob hakufanikiwa kummaliza. Haraka aliparamia mlango kwa lengo la kumuwahi muuaji wa Bob lakini alipofika nje ya mlango hakukuta mtu zaidi ya kijikaratasi kilichokuwa chini. Kabla ya kukiokota aliangalia huku na huko, ili kuangalia kama kulikuwa na mtu alikuwa amemtega. Alikiokota kiaina na kuangalia kilikuwa na nini. NAMTAKA REGINA KWA BEI YOYOTE ILE, BANZI. Hayo ni maneno yaliyokuwa kwenye kikaratasi hicho. Kifo cha Bob na huo ujumbe viliitibua akili ya Jacob. Hivi kuna upande mwingine tofauti na hawa unaomuhitaji Regina? Alijiuliza huku akitokomea. Banzi ni nani na anahusika vipi katika kisa hiki? Jacob akatabasamu nakuachilia pumzi “Kazi ipo” akanong'ona.

******

“Leta habari kijana, yamekwendaje?” Sauti nzito iliuliza.

“Kama kawaida mzee huwa sifanyi makosa, Bob Sepeto hatunaye duniani!” Alijibu kijana huyu kwa sauti ya kujivuna kidogo.

“Vizuri sana Banzi, sasa hebu anza kufuatilia nyendo za Jacob Matata, hakikisha hampati Regina wala hawafikii vijana wa mzee Harken Kalm. Nakutahadharisha, Jacob si mtu wa kumuendea ovyo” Ilimaliza sauti hiyo nzito na kukata simu. Sauti hiyo nzito ilikuwa ikitoka mdomoni mwa mwanaume mmoja wa makamo. Aliminya namba kadhaa kisha akaongea “enhe leta habari kijana, yamekwendaje?” Aliuliza huku macho yakiwa yametua darini.

“Hapa nilipo niko hatua sita toka alipokaa mrembo Regina!” Ulijibu upande wa pili.

“Vizuri, uliwahi kabla mambo hayajaharibika?” Sauti hii nzito iliuliza tena.

“Kabisa, nilikuta ndio wanamgombania, lakini hakuna aliyefanikiwa kumpata”

“Vizuri Ponte, bila shaka utafanikiwa kumleta Regina akiwa salama, nina hamu nae sana na ndiye atakayekuwa malkia wenu” Ilisema sauti hii nzito na kukata simu.

Alipomaliza kuongea na sehemu hizi alizozitaka, alikohoa kidogo na sauti yake hiyo nzito ikiacha ukulele fulani. Mikono yake mizito na yenye misuli iliyoshikana kama mti wa mnazi ilivuta droo ya meza. Alipochukua kalamu na karatasi aliandika jina la Jacob, Regina, Mzee Harken Kalm na Bi. Anita. Kisha akajiapiza “kwa vile nakupenda Regina, lazima nikuokoe na lazima baadhi ya hawa watu hapa niwamalize” Jamaa hili liliongea kwa kunong’ona katika sauti yake nzito.

Jina lake mtu huyu aliitwa John Kificho. Yeye ni rafiki wa damu wa mzee Harken Kalm. Japo shughuli zake zilikuwa za halali lakini hakusita kuwa na vijana wa kazi ili kuweza kumsaidia kulinda utajiri aliokuwa nao. Ni urafiki huu ndio uliomuwezesha kuwepo kwenye chumba cha mapumziko cha mzee Harken Kalm, siku ile wakati Regina akipelekwa akahojiwe. Kwa kupitia mitambo ya kisasa ya jumba hilo walikuwa wakiwaangalia Bob na Regina pindi wakiwa wanaelekea kwenye chumba cha mahojiano. Ghafla John akajikuta akivutiwa mno na jinsi msichana Regina alivyokuwa ameumbika.

Mzee Harken Kalm alipoondoka kwenda kumuhoji Regina huku nyuma John Kificho akajikuta akiapa kuwa lazima ampate msichana huyo mrembo. Hapo ndipo ilipoanza mipango yake ya kuhakikisha anampata Regina. Mipango yake hiyo ndio iliyopelekea kifo cha Bob Sepeto. Ni yeye aliyekuwa amemtuma mtu kwenda kummaliza Bob. Pia kwa haraka sana alipanga mipango ya kwenda kumuokoa Regina. Huko kwa ustadi mkubwa alifanikiwa kuingiza mtu bila kushukiwa na yeyote. Kazi yake haikuwa ngumu kwa sababu hakuwa na kazi ya kutafuta habari, zote alizipata toka kwa mzee Harken Kalm mwenyewe. Mtu wake alikuwa tayari ameshaingia sehemu ambayo alikuwepo Regina. Mtu huyo alijitambulisha kwa Regina kuwa ametumwa na Jacob.

“Usijali, muda wote niwapo katika eneo hili nitahakikisha usalama wako kwa sababu nimetumwa humu kwa ajili yako!!” Alisema kijana huyo huku akiyasoma macho ya Regina.

“Umetumwa kwa ajili yangu!!” Regina alionekana kushangaa.

“Ndio”

“nani huyo aliyekutuma kwangu mtu kama mimi?”

“Bosi wangu Jacob Matata, inatakiwa tutoke humu ndani” Alisema huyo kijana.

“Kutoka hapa!!!” Regina alishangaa.

“ndio, tena si siku nyingi toka leo!!” Alisema kijana huyo kwa kujiamini.

“kaka nadhani una matatizo ya akili, wadhani unaweza kutoka hapa ukiwa salama?” Regina aling’aka kidogo.

“Tusibishane lazima tushirikiane!!” Alisema kijana huyo huku akishusha pumzi nyepesi.

“Ushirikiano gani unaotaka kama si kuhatarisha maisha tu?” Alisema Regina katika hali ya kuweweseka kidogo.

“Ushirikiano kama wa kuoga pamoja leo jioni, na kuwa karibu yangu, si wa kupigana kama unavyodhani wala kuruka ukuta” Alisema kijana huyo huku akitabasamu.

“Sasa wadhani kwa kuwa karibu na wewe ama kuoga pamoja twaweza kutoroka ndani ya ngome hii? Ndio maana nimesema yawezekana una upungufu wa akili!!” Alisema Regina huku akioneka kuanza kupoteza imani juu ya mtu huyu.

“Je nikikuambia ndio, na ukafanya na kujikuta nje ya ngome utakuwa umepungukiwa nini?” Alihoji kijana huyo.

“waongea mambo yasiyowezekana, lakini sioni gharama ya kufanya mambo hayo mepesi uliyosema” Alisema Regina huku macho yake yakimsaili kijana huyo.

Baada ya mahojiano hayo kilifuata kimya baina ya watu hao. Vijana wengi waliokuwa ndani ya eneo hilo walikuwa wakimuangalia Regina kwa macho ya matamanio. Kijana huyu katika hali ya uficho ficho alitoa kijikaratasi fulani na kuanza kukisoma kwa makini. Regina aliona hali hiyo lakini hakutilia maanani, kwani alishaanza kumuona kijana huyu kama mtu wa ajabu ajabu tu.

Muda wa jioni ni muda ambao watu walioko katika jumba hili huutumia kwenda sehemu iliyokuwa na bwawa kubwa la kuogelea. Hapo waliogelea na kujaribu kutafuta furaha ambayo hata hivyo ilionekana kuwa mbali nao.

Yule kijana na Regina walikuwa ni miongoni mwa watu waliokuwa pembezoni mwa bwawa hilo.

“Naomba tuoge pamoja, ila naomba uwe mwepesi kufanya vile navyokuelekeza kufanya, ni rahisi tu na hamna hatari yoyote. Je unauzoefu gani wa kuogelea?” Yule kijana alimalizia kwa swali.

“Si mzuri sana wa kuogelea maana nimejifunza nilipofika katika jumba hili” Alijibu Regina.

“Okey, nitakusaidia, tutaenda kuogelea upande ule kule ambao hauna watu wengi”

Dakika chache baadaye wote walikuwa ndani ya maji upande ule aliotaka yule kijana. Waliogelea hivyo kwa dakika kadhaa, kabla kijana huyo hajapotelea kwenye maji. Regina alisubiri kwa muda mpaka akawa anataka kutoka, ndipo alipomuona kijana huyo akiibuka.

“Samahani kwa kukuacha kwa muda, nilikuwa naangalia njia, sasa hebu zama twende, uwe mwepesi kufuata nitakachokuambia” Regina hakubisha alizama. Alipofungua macho alishangaa kuona kuna vitu kama mitungi ya gesi miwili. Kidogo alishangaa kuona anashikwa kichwa na kuminyiwa kitu mdomoni. Alikuwa ni yule kijana akimvalisha mpira wa kusaidia kuvuta hewa nzuri toka kwenye mtungi. Walipokuwa wameshavaa wote, yule kijana alimuashiria Regina amfuate. Waliogelea hivyo hadi pembeni kabisa ya ya bwawa upande mwingine. Walipofika hapo, yule kijana alipapasa kwenye ukuta wa bwawa sehemu hiyo. Ilionesha hakufanikiwa kupata kitu. Alitoa kile kikaratasi chake cha nailoni ambacho kilikuwa na ramani, akaangalia kwa muda. Akapapasa sehemu fulani, safari hii alifanikiwa kuinua kufuli kubwa. Alitoa funguo kadhaa toka mfukoni na kuanza kuhangaika kufungua lile kufuli. Baada ya dakika kadhaa kufuli hilo lilifunguka. Akainua kitu kama mfuniko mkubwa huku akikabiliana na nguvu ya maji yaliyotaka kupita mara baada ya kuwa yamepata uwazi kutokana na nafasi iliyokuwa ikiachwa na mfuniko huo. Mara sehemu ile kulipokuwa na mfuniko kukawa na shimo kubwa liloanza kupitisha maji kwa kasi. Kijana huyo alisogea sehemu fulani akashika kitu kama koki ya maji. Akainyonga mpaka mwisho, bila shaka alitambua kuwa maji yaliyokuwa yakitoka yangesababisha upungufu wa maji kwa haraka, hivyo akaamua kufungulia maji ya ziada yaingie bwawani humo.

Alimvuta Regina na kumuelekeza atangulie kuingia kwenye mfereji ambao sasa ulikuwa ukipitisha maji kwa kasi sana. Kwanza Regina alisita, lakini alishitukia ameshikwa na mkono wenye nguvu kama chuma na kusukumiwa kwenye huo mfereji. Nguvu ya maji iliwachukua na kwa kasi na baada ya kama dakika mbili hivi wakajikuta wameingia kwenye maji yaliyoonesha kuwa kulikuwa na nafasi. Hapo kijana huyo alimwamuru Regina apande mgongoni. Safari hii Regina alitii, akapanda mgongoni huku mpira wa hewa ya oksijeni ukiwa bado unaning’inia. Jamaa huyo aliogelea kwa kasi ya kushangaza. Baada ya mwendo wa kama dakika ishirini hivi waliibuka.

Asante kwa kusoma, itaendelea kesho
 
Back
Top Bottom