Riwaya: Hekaheka

HEKAHEKA - 17

Alimvuta Regina na kumuelekeza atangulie kuingia kwenye mfereji ambao sasa ulikuwa ukipitisha maji kwa kasi sana. Kwanza Regina alisita, lakini alishitukia ameshikwa na mkono wenye nguvu kama chuma na kusukumiwa kwenye huo mfereji. Nguvu ya maji iliwachukua na kwa kasi na baada ya kama dakika mbili hivi wakajikuta wameingia kwenye maji yaliyoonesha kuwa kulikuwa na nafasi. Hapo kijana huyo alimwamuru Regina apande mgongoni. Safari hii Regina alitii, akapanda mgongoni huku mpira wa hewa ya oksijeni ukiwa bado unaning’inia. Jamaa huyo aliogelea kwa kasi ya kushangaza. Baada ya mwendo wa kama dakika ishirini hivi waliibuka. Regina alipofungua macho alijikuta akiangalia sehemu kama kisiwa hivi kilichokuwa mbele yao, upande mwingine ulikuwa ni bahari. Japo maji yalikuwa marefu, lakini waliweza kusimama na kutembea taratibu kuelekea nchi kavu.

“Hongera mrembo kwa kuwa mtii, nadhani umeamini sasa kuwa haikuwa kazi ngumu kutoka katika ile ngome” Alisema yule kijana walipokuwa wanatoka ndani ya maji. Regina kwa vile alikuwa amechoka sana, hakujibu kitu bali alimuangalia tu kijana wake huyu wa ajabu. Alifikiria ni nini kingefuata. Kwa vile walikuwa wamechoka sana, walijilaza hapo ufukweni ili kupata nguvu mpya. Wakiwa wamejipumzisha hivyo, mara vishindo vya watu vilisikika vikija upande huo waliokuwepo.

“Vipi mmeshaleta usafiri” Alisema yule kijana bila kugeuka wala kuangalia watu waliokuwa wamekuja.

“Ndio, ila bosi ana wasiwasi kweli kila dakika anapiga simu kuulizia” ilijibu sauti nyuma yao.

Regina alikurupuka na kugeuka haraka. “usijali, hawa wamekuja kutusaidia” sauti ya yule kijana ilimtoa hofu kwa mara nyingine. Toka hapo walitembea umbali fulani kabla ya kukutana na kijinjia ambapo gari aina ya Range Rover ilikuwa imeegeshwa. Waliingia humo na safari ya kwenda kwenye himaya ya John Mficho ilianza.


* * *

Haikuchukua muda mrefu kabla mabadiliko hayajaonekana. Maji ya bwawa yalipungua kwa kasi ambayo iliwashitua walinzi wa jumba la mzee Harken Kalm. Mara moja kikundi cha wataalamu ndani ya jumba hilo walianza kutafuta chanzo cha upungufu huo. Haikuchukua muda mrefu kugundua kuwa kuna sehemu ilikuwa imefunguliwa. Iliwachanganya zaidi kugundua kuwa haikuwa bahati mbaya, bali aliyefungua alikuwa ametumia funguo kufungua eneo hilo.

Asubuhi siku iliyofuata mambo mawili yalifanyika katika jumba hilo. Moja walitumwa vijana kwenda kufanya doria katika mwambao wote wa bahari eneo hilo. Pili kiliitishwa kikao cha haraka ili kujadili hali ya mambo ilivyokuwa inakwenda.

“Ningependa kujua kama kuna mgeni yeyote aliyeingia humu ndani katika siku tatu zilizopita” Alisema mzee Harken Kalm katika sauti ya utulivu wa mashaka. Ndani ya chumba hiki cha kikao kulikuwa na wakuu wa ulinzi na vikosi mbali mbali vya mzee Harken Kalm. Ili kujibu swali hilo ilibidi mtaalamu wa kuendesha mitambo ya kuangalia eneo hilo asimame na kutoa maelezo.

“Kuna mgeni mmoja tu aliyeingia humu siku ya jana, mgeni huyu aliletwa kwa taratibu za kawaida. Alikuwa ni kijana ambaye aliletwa ili kuwa miongoni mwa watu wanaotoa mbegu. Ukiacha huyo, basi ni rafiki yako John Mficho, huyu alikuja juzi na kuondoka mida ya mchana. Sijajua kama hili linaweza kuwa na uhusiano wowote na tatizo tulilo nalo?” Alimaliza jamaa huyu na kuketi kitini.

“Ndio yaweza kuwa na tatizo!! Hebu mtu akaangalie kama huyo kijana yupo. Ningependa kuwatahadharisha jambo moja, tangu kuingia kwa msichana Regina katika himaya hii kumekuwa na matatizo makubwa, matatizo haya kama mjuavyo ni kuwa msichana huyo alikuwa na uhusiano wa kimapenzi na mpelelezi hatari Jacob Mtata, bila shaka wote mnamfahamu Jacob Matata, hata kama hamumfahamu lakini mmeshapata kuzisikia habari zake. Tumekuwa katika harakati za kumuwinda lakini bila mafanikio. Mtu huyu amefanikiwa hata kumuua mtu kama Bob Sepeto, sasa ningependa kupata ushauri wenu tufanyeje ili kukabiliana na hali hii?” Alisema mzee Harken Kalm huku macho yake yaking’ara kwa hasira.

Mjumbe mmoja alisimama na kutoa maoni yake; “mimi naona ili kufuta kabisa kuwepo kwa tisho lolote, ni vema tukaangamiza kila mwenye kujua kuhusu sisi, hii ina maana kuwa mtu huyu Jacob Matata, Regina na yeyote atakayegundulika basi amalizwe” Mjumbe huyo alimalizia maelezo yake.



“Nyote mnisikilize kwa makini….” Alianza mzee Harken Kalm. Wakati ameanza hivyo, kijana mmoja kati ya vibaraka wake alikohoa kidogo. Ndani ya nukta chache mzee Harken Kalm aliutoa uhai wa kijana huyo kwa risasi tatu za kichwa. Kwa mzee huyo hilo lilikuwa ni kosa lililostahili kifo. Ukimya ulitanda katika ukumbi huo huku marehemu akipiga miguu katika hali ya kukata roho. Hakuna aliyeguna wala kujitingisha, ilikuwa kana kwamba hakuna lililokuwa limetokea.

“Habari nilizopata hivi punde ni kuwa, yule kijana aliyeingia humu ndani ametoweka pamoja na Regina, kikosi cha Paka mtakuwa na jukumu la kufuatilia hawa watu hadi wapatikane. Kuna watu wanawasubiri hapo nje wakiwa na taarifa za pa kuanzia katika kazi yenu. Haya ondokeni, nadhani mnajua maadili ya kazi yenu.”

“Kikosi cha Tai, mtakuwa na kazi ya kuhakikisha uhai wa Jacob matata unakatishwa. Sina mengi ya kueleza maana wote mna taarifa za kutosha juu ya adui yenu. Nimewachagua ninyi kwa kuzingatia uwezo wenu.”

“Kikosi cha mbwa weusi mtakuwa na kazi ya kuhakikisha usalama wa jengo hili, hii ikimaanisha ni pamoja na kujua kijana yule alifanikiwaje kwa urahisi namna ile kuweza kuingia na kumtorosha msichana Regina bila kushitukiwa na mtu.”

“Kama kawaida kunguru mtakuwa na kazi ya kuunganisha taarifa toka vikosi vyote, sitegemei uzembe, wala makosa yoyote. Ningependa kuona hali inakuwa shwari ndani ya muda mfupi. Haya tawanyikeni” Alimaliza mzee Harken Kalm, kisha akapotelea ardhini.

* * *

Makundi yote yalitawanyika. Wa kwanza kufikiwa alikuwa ni mpelelezi Jacob Matata. Kama ilivyoamuriwa, kundi la Tai ndilo lililokuwa na wajibu wa kummaliza Jacob. Kundi hili lilimfikia Jacob muda mfupi tu wakati anatoka kwenye kikao cha dhalura kilichokuwa kimeitishwa na Mkurugenzi wa ofisi fukuzi Bi. Anita. Ilivyo ni kuwa wakati Mzee Harken Kalm alipokuwa akifanya kikao na vikosi vyake ni wakati huo huo ambapo ndani ya ofisi fukuzi kulikuwa na mkakati mzito. Bi. Anita alikuwa ameandaa vijana wake hatari katika oparesheni nzito ya kulivamia jumba la mzee Harken Kalm. Ilipangwa kuwa Jacob ndiye angeongoza kikosi cha kwenda huko usiku huo.

Hivyo wakati Jacob anaelekea kwake sinza, ndipo alipoingia kwenye macho ya Tai waliokuwa katika harakati za kumsaka. Alipofika nyumbani, alikuwa sambamba na Tai pasipo kujua. Aliingia ndani na kuanza kufanya maandalizi tayari kwa kazi ya usiku. Alijua ingekuwa ni moja kati ya kazi ngumu ambazo amewahi kuzifanya, lakini ilibidi kukabiliana nayo. Ile kujua kuwa angeonana na mscihana Regina ilikuwa ni moja ya sababu zilizokuwa na msukumo mkubwa wa kumfanya awe na hari ya kwenda katika uwanja wa mapambano.

Wakati Jacob Matata akiwa amezama katika kupanga namna ambavyo angeongoza oparesheni hiyo ngumu ya kuvamia jumba la mzee Harken Kalm usiku huo mara alisikia kitu kama mchakacho. Japo ulikuwa ni mchakacho mdogo sana lakini kwa mtu kama Jacob ulikuwa wa kutosha kumfanya achukue tahadhali. Hivyo alijiweka sawa. Mtu aliyefanya mchakacho huo hakudhani kama ungekuwa mkubwa masikioni kwa Jacob Matata. Hivyo akaendelea na harakati zake za kutafuta chumba alichokuwa mpelelezi Jacob Matata. Alipofika chumba fulani, alitega sikio ili kusikiliza kama kulikuwa na mtu. Huyu alikuwa ni mmoja wa vijana wa kundi la Tai. Akiwa katika kuchungulia alishitukia mdomo wa bastola ukigusa shingo yake. Akataka kugeuka lakini alichelewa kwani sauti tayari ilishayafikia masikio yake “tulia hivyo hivyo, na fuata nitakavyokuambia” alisema Jacob huku akimsukuma huyo kijana wa Tai. Wakati akifanya hivyo, Jacob nae alihisi kitu cha baridi kikigusa sikio lake “sheet!, usilete ujanja tuko wawili huku, nenda hadi chumba namba tatu” Sauti ilimwamuru.

Alikuwa na uwezo wa kujitetea lakini hakuona ni busara kufanya hivyo, kwani watu hawa walionekana kutokuwa wauaji bali walitumwa kumchukua tu. “hata mngekuwa kumi, isingekuwa lazima kuniambia hivyo, mwanaume mzima hujiamini!” Alisema Jacob katika hali ya kuonesha kuwa hakuwa mtu wa kutishiwa ovyo.

Jacob aliongoza hadi chumba kile alichokuwa ameelekezwa. Chumba namba tatu ndicho alichokuwa amekaa akipanga kazi ya usiku. Hivyo ilikuwa ni ishara kuwa aliyemuamuru hivyo alikuwa ameshamuona kabla.

Waliingia ndani ya chumba hicho. Jacob akaamriwa kukaa. Akakaaa bila kipingamizi huku akijaribu kusoma mawazo ya vijana hao.

“Bwana Jacob, nashangaa kuona kuwa uliyeko mbele yengu ni tofauti na mtu ambaye nimekuwa nikisikia habari zake, badala ya mtu mkorofi, katili, miraba mine namuona mtu mtiifu, mpole, na mwenye mwili wa kawaida tu. Ila sijajua bado ukweli wa hivi nikuonavyo, lakini nitakapokuwa nimemaliza mahojiano na wewe ndipo naweza kupitisha kile ambacho macho yangu yananiambia, bila shaka utatoa ushirikiano katika mazungumzo haya, au siyo bwana Jacob?” Alisema kijana huyo kwa sauti tulivu lakini ambayo ilikuwa na chambechembe za ukatili ulioleta harufu ya hatari puani kwa Jacob.

“Labda kabla sijakuambia kuwa nitakuwa tayari au la, ningependa kujua sababu hasa ya kuniingilia bila ridhaa yangu?” Jacob aliuliza swali la kijinga.

“Ni kwa sababu tumelazimika kufanya hivyo na aliyetutuma!”

“nani aliyewatuma” Jacob alihoji zaidi.

“si lazima umjue. Ningependa kujua mambo kadhaa kabla sijakuacha uendelee na shughuli zako!” Alisema kijana huyo.

“Inategemea kama nitaweza kuwajibu” Jacob alisema.

“je unamfahamu msichana aitwaye Regina?” Sauti iliyouliza swali hili haikuwa tena ile ya utulivu bali ya muungurumo fulani.

“Ndio, namfahamu” Jacob alijibu.

“je unajua yuko wapi kwa sasa?”

“amesafiri leo asubuhi?”

“Hujajibu swali, nimeuliza yuko wapi?” Alirekebisha.

“si unajua kaka Kiswahili ni kigumu, okey kwa sasa hayuko mahali popote zaidi ya kuwa ndani ya ndege!”

“Amesafiri lini?” Aliuliza jamaa huyu huku akiongeza umakini zaidi. Swali hili lilikuwa gumu kwa Jacob Matata, kwani ilikuwa wazi kuwa kukosea kujibu uongo wake ingebainika. Maelezo yake yote yalikuwa ni ya kubuni tu.

“Ana dakika arobaini na tano tangu ametoka kiwanja cha ndenge cha mwalimu Nyerere!” Alisema hayo huku akimuangalia huyo kijana usoni. Uso wa kijana huyo ulionyesha kuridhika.

“Nairobi atakaa kwa muda gani?” Alihoji tena huyo kijana.

“Amesema inategemea na mambo aliyoenda kushughulikia?” Jacob alizidi kubuni.

“Ameenda kushughulikia nini?”

“Hakuniambia?” Jacob alijibu huku akiangalia jinsi hao jamaa walivyokuwa wamekaa. Mpaka sasa kulikuwa na vijana wapatao sita, hawa wote walikuwa ni kikosi cha Tai.

“Waweza kuniambia Regina alikuwa wapi siku tatu zilizopita?” Jamaa huyo aliuliza tena.

“Kwa muda nilikuwa sijaonana nae, ila jana jioni usiku ndio nilionana nae na akanipa taarifa za hiyo safari”

“Mlionana nae wapi?”

“Nilimuona akiwa njiani wakati nikiendesha kuja nyumbani”

“Alikuwa na nani wakati mnakutana?”

“Alikuwa ameegesha gari, nje alikuwa peke yake, hivyo siwezi sema kama alikuwa peke yake au la kwani yawezekana ndani ya gari kulikuwa na mtu” Jacob alizidi kubuni, lakini sasa akiwa anachoka kwa maswali kuwa mengi.

“Kama wiki moja iliyopita, ulionekana ukiwa kambi ya kaboya, je ulikuwa umeenda kufanya nini?” Jamaa aliuliza swali hili huku akitoa ishara fulani kwa vijana wake. Hivyo kijana mmoja alitoka chumbani humo. Mwingine aliingia sekunde chache baadaye, bila shaka kuchukua nafasi yake.

“Nadhani aliyeona alifananisha, kwani sijawahi kwenda kambi ya Kaboya” Jacob alisema huku akijua kuwa mambo yameanza kuiva.

“Kwani iko wapi hiyo kambi?” Jacob aliwahi kuuliza.

“Si lazima ujue?” Alijibiwa.

“Ila kwangu mnataka kujua, bila kunipa nafasi ya kujua kuhusu nyie. Nyie ni nani?” Hatimaye Jacob aliuliza.

“Kikosi cha Tai” alijibiwa.

“Kikosi cha Tai! Jina zuri, nimeshawahi kulisikia mahali” Jacob alisema hayo huku akishanga kuona wote walikuwa ndani ya chumba hicho wakiwa wameanza kutawanyika kushika nafasi katika kona za chumba.

“Sikiliza bwana Jacob, nasikitika kukuambia kuwa una muda mfupi sana wa kuishi na ilivyo ni kuwa hakuna namna utaweza kukwepa kuuawa hapa, nachoweza kukushauri kufanya ni kuomba sala yako ya mwisho” Alisema jamaa huyo huku akichomeka bastola mahali pake na kuchomoa kisu.

“Ningependa nikuue kwa kisu badala ya risasi, hii ni kutokana na ushirikiano ulioutoa katika maongezi yetu” Alisema jamaa huyo huku tabasamu angavu likichanua usoni kwake.

“Sawa, lakini kabla hamjaniua ningependa niache ujumbe mfupi kwa mpenzi wangu, ili akija apate maelezo muhimu juu mali zangu” Jacob aliomba.

“Hilo hutaruhusiwa kufanya” Alisema huyo jamaa huku akiwa anaweka sawa kisu chake.

Jacob alijiweka sawa ili kuweza kuiokoa roho yake toka katika mauti iliyokuwa mbele yake.

* * *

Wakati Jacob akiwa anatazamana na mdomo wa mauti, ndani ya jumba la John Kificho hali ilikuwa ni shangwe tupu. Tangu kuwasili kwa msichana Regina pamoja na yule kijana aliyefanikiwa kumtorosha katika jumba la mzee Harken Kalm, kumekuwa na sherehe za kumfanya Regina awe malkia. John Kificho alikuwa ameandaa sherehe hiyo ya kumfanya Regina awe mke wake, hiyo ilimaanisha kuwa angeitwa malkia wa jumba hilo.

Hakukuwa na uchaguzi kwa msichana Regina. Kwake hakuona tofauti ya kule alikotoka na hapo, japo hapo kulikuwa na unafuu kidogo. Kwa Regina, John Kificho hakuwa na mvuto wowote kwake, lakini kwa vile hakuwa na hiari ilimbidi akubaliane na lolote alilotakiwa kufanya. Ilikuwa wazi kuwa kukataa lolote ilikuwa ni kualika kifo chake.

Wakiwa katikati ya sherehe, mara simu ya mkononi ya John Kificho iliita.

“Aah kijana leta habari!!” Sauti nzito ya John iliunguruma.

“Bosi, hapa nilipo niko nyumbani kwa Jacob Matata, nashangaa kuona kuwa kuna jamaa wamemuweka kati sijui wanataka nini toka kwake. Unanishauri nipambane nao au niache wammalize Jacob?” Uliuliza upande wa pili.

“Kidogo nimebadili mawazo, ningependa kummaliza Jacob huku Regina akiwa anajua kuwa Jacob amekwisha, hivyo ni vema sisi tummalize katika njia ambayo Regina atajua kuwa Jacob hayupo tena duniani na wakati huo huo Regina aamini kuwa tumejaribu kuyaokoa maisha ya Jacob. Hivyo fanya namna kumuokoa Jacob kisha nitakuelekeza cha kufanya” Alimaliza John Kificho huku moyo wake ukiwa umeshinikizwa kwa furaha. Aliona mambo yanamnyookea.

“Sawa bosi nitakupigia dakika chache zijazo” ulijibu upande wa pili na kukata simu.

Itaendelea leo kama ikiwezekana.....
 
HEKAHEKA - 18

Kidogo nimebadili mawazo, ningependa kummaliza Jacob huku Regina akiwa anajua kuwa Jacob amekwisha, hivyo ni vema sisi tummalize katika njia ambayo Regina atajua kuwa Jacob hayupo tena duniani na wakati huo huo Regina aamini kuwa tumejaribu kuyaokoa maisha ya Jacob. Hivyo fanya namna kumuokoa Jacob kisha nitakuelekeza cha kufanya” Alimaliza John Kificho huku moyo wake ukiwa umeshinikizwa kwa furaha. Aliona mambo yanamnyookea.

“Sawa bosi nitakupigia dakika chache zijazo” ulijibu upande wa pili na kukata simu.

* *

Akili ya Jacob ilikuwa katika mahesabu ya kujumlisha kutoa na kuzidisha, alipokuja kugawanya tayari alikuwa amesharuka. Wakati Jacob akiruka, upande nje ya chumba walichokuwa kilisikika kishindo cha mtu akianguka. Hii ilimsaidia sana Jacob, kwani baadhi ya watu ilibidi wakimbilie nje na kuacha wachache tu humo ndani. Nje ilisikika hali ya mapigano makali, huku ndani Jacob alikuwa akisuguana na waliobaki akiwemo yule kiongozi wao.

Ulikwa ni mpambano mkali, ambapo mpaka unakwisha Jacob alikuwa hoi huku adui zake wakiwa marehemu. Alikuwa ameshinda kwa taabu sana kwani jamaa hao walikuwa ni wazuri wa kutosha. Alijivuta na kusimama kwa kusaidiwa na kiti. Akiwa anajiweka sawa, mlango ulifunguliwa. Hakuwahi hata kujiweka sawa kabla hajatazamana na mdomo wa bastola. Alikuwa ni kijana wa John Kificho.

“Toka nje” Jamaa aliamuru. Jacob alijikongoja.


* * *

Dakika chache baadaye gari iliyokuwa imembeba Jacob ilikuwa ikitambaa juu ya barabara moja ya jiji la Dar es salaam. Ndani kulikuwa na vijana kadhaa wa John Kificho. Walishika barabara ya Sam Nujoma, Ubungo, Mabibo, Buguruni, uwanja wa taifa. Walipofika hapo, vitambaa vya madirishani vilifunika na hivyo Jacob hakujua waliingia wapi. Walipofika eneo ambalo bila shaka ndio ilikuwa mwisho wa safari yao, mlio wa honi ulisikika. Ulisikika mlio wa geti kufunguliwa.

Aliposhuka alijikuta yuko eneo la wazi, lakini kulikuwa giza tupu. Ilikuwa kama ukumbi mkubwa usiokuwa na viti wala chochote. Hali ilikuwa kimya kabisa eneo hilo. Hatua kama hamsini hivi toka lilipokuwa gari lao, kulionekana mwanga wa taa. Lakini tofauti na matarajio yake, haikuamriwa yeye kupelekwa huko. Aliingizwa kwenye chumba fulani. Ilibidi kupita milango mitatu kabla ya kufikia chumba hicho. Jumba hili lilikuwa na ulinzi wa kutisha. Walinzi wake wote walionekana wakiwa makini, huku wakiwa wamewezeshwa kwa silaha za kisasa mno.

Jacob alijikagua na kuona jinsi alivyokuwa ameumia. Ilikuwa dhahiri kichwani mwake kuwa kulikuwa na makundi mawili aliyokuwa akipambana nayo. Hakujua kundi jingine lilikuwa na lengo gani nae. Hakuwa na shaka kuwa kundi la kwanza lilikuwa na lengo la kuficha ukweli fulani juu ya msichana Regina.

Mpaka anajiandaa kwenda kuvamia nyumbani kwa mzee Harken Kalm, Jacob alikuwa akiamini kuwa msichana Regina angekuwa ndani ya jumba hilo la mzee Harken Kalm. Lakini kufuatia mahojiano yake na mtu aliyekuwa ameongoza kundi la kuja kumteka ilionesha kuwa Regina alikuwa ametoweka katika himaya ya hao jamaa. Ameenda wapi na amewezaje kutoka? Hayo ni baadhi ya maswali ambayo Jacob matata alihitaji kupata majibu yake. Pia hakujua hawa watu walikuwa na lengo gani. Alikumbuka kifo cha Bob Sepeto, akahisi kuwa kundi hili laweza kuwa linahusika. Kwa nini?

Siku ya kwanza ilipita kwa mateso makubwa sana. Hakuna aliyekuwa amekuja kumuona wala kumpa chakula. Chumba hicho kilikuwa kichafu na hivyo kuwa makazi ya chawa, viroboto na papasi wenye njaa kali. Hewa ilikuwa ndogo sana. Japo hali ya maumivu ilikuwa imetoweka, lakini njaa ilikuwa ikimsumbua sana. Alichoweza kufanya ni kujinyooshanyoosha viungo ili kujiweka fiti. Watu kama hawa ndio maana huitwa makomandoo.

Siku ya pili jioni mlango wa chumba ulifunguliwa. Taa ndogo iliyokuwa ukutani iliwaka na kutoa mwanga hafifu sana. Kwa vile Jacob alikuwa amekaa kwenye giza kwa zaidi ya masaa 72, mwanga huo ulikuwa tosha sana kwake. Mara mbele yake alisimama jamaa mmoja aliyeonekana kushiba kiasi cha kutosha. Jamaa hilo halikuongea kitu. Lilipoingia tu, mlango nyuma yake ulifungwa. Jacob alisimama ili kuona jamaa huyu alikuwa ametumwa kufanya nini. Macho yao yalipogongana ndipo Jacob alipogundua kuwa jitu hilo lilikuwa si salama kwa hali yoyote. Lilizidi kumsogelea. Japo alikuwa na njaa, Jacob ilibidi ajiweke tayari kwa lolote. Lilipokuwa kama hatua tatu hivi toka alipokuwa Jacob, jitu hilo lilibadirika na kuwa mbogo kwa mapigo makali. Lilimpelekea mapigo makali sana ambayo kama si ustadi wa Jacob kuyakwepa, basi agekuwa kwenye ulimwengu mwingine. Mara kadhaa Jacob alijaribu kupeleka mashambulizi hakuambulia chochote. Jamaa alikuwa fundi katika kupigana. Dakika saba zilikatika huku hali ikiwa ngumu sana ndani ya chumba hicho. Kwa vile alikuwa na njaa, ukichanganya na ufundi wa hilo jamaa, Jacob alijikuta amechoka sana. Jamaa halikupunguza kasi ya mashambulizi wala halikuonesha dalili yoyote ya kuchoka.

Taratibu, nguvu zilianza kumpa mkono Jacob kama miale ya jua inavyopotelea mawinguni nyakati za jioni. Hali hii ilipelekea kupungua kwa uwezo wake wa kukabiliana na mpinzani wake. Jamaa lilipeleka wimbi zito la mateke na ngumi kwa Jacob, kwa vile alikuwa amepungukiwa uwezo, baadhi ya mapigo yakaanza kumuingia. Dakika chache baadaye, akawa kama gunia la kufanyia mazoezi. Mwisho fahamu zilimtoka Jacob, hakujua hata wakati jamaa hilo lilipotoka chumbani humo.

Fahamu zilipomjia alijikuta akiwa amelala ndani ya chumba hicho huku wale wadudu ambao ni wakazi wa chumba hicho wakiwa wanamfanyia sherehe. Alijaribu kusimama, akasimama. Mwili ulikuwa umedhohofika sana kutokana na njaa pamoja na kipigo alichokuwa amepata. Hakuweza kujua kama ilikuwa ni muda gani wakati huo, hakujua kama ilikuwa ni mchana au usiku. Pia hakuweza kujua kama ilikuwa imemchukua muda gani mpaka pale fahamu zilipokuwa zimemrudia. Alijinyoosha viungo kwa kutembea hapa na pela, aliruka kidogo na kufanya mazoezi mepesi. Alijua hili ndilo lilikuwa ndani ya uwezo wake na hakupenda kuuacha mwili uvunde kabisa maana ingemfanya awe katika hatari zaidi.

Siku ya tatu, Jacob alikuwa katika hali mbaya zaidi. Njaa, mshambulizi ya wadudu kwenye chumba hicho, na yale ya yule jamaa yalimfanya adhoofu kiasi cha kusikitisha. Wenyeji wa chumba hicho yaani, viroboto, papasi na chawa walionesha kuanza kuneemeka. Wengi afya zao zilibadirika ghafla tangu pale Jacob alipokuwa ameingia ndani ya chumba hicho. Muda fulani ulipofika mlango wa chumba hicho ulifunguliwa. Ile taa yenye mwanga hafifu iliwashwa kama ilivyokuwa jana. Mtu aliingia, Jacob alipomtazama alitambua kuwa ni lile jamaa. Mwili ulimsisimka na hasira iliyochanganyika na chuki juu ya jamaa huyu ilimkaba kooni. Alitamani angekuwa katika uwezo wake wa kawaida ili alifundishe adabu jitu hilo.

Kama kawaida, lilimsogelea taratibu huku likiwa na tabasamu la uovu usoni kwake. Jacob alijiweka sawa huku hali ya mwili wake ikiwa dhaifu kiasi cha kusikitisha. Jamaa hilo halikuwa na hata chembe ya huruma, lilianza kumshambulia Jacob kwa namna ya kuua. Jacob alitumia nguvu zake zote alizokuwa amebaki nazo kujaribu kujihami. Lakini hakuweza kufanya hivyo kwa muda mrefu. Hakuwa amebakiwa na nguvu kabisa. Ninaposema jamaa hilo linapiga, ninamaanisha. Ni jitu lililofundishwa kupiga na linajua kupiga sehemu ya kupiga. Kwa mara nyingine fahamu zilimtoka Jacob. Angekuwa ni mtu wa hivi hivi tu, tayari angekuwa ameshapewa jina la marehemu. Kama ilivyokuwa jana yake, hakuweza jua wakati jitu hilo lilipotoka mule chumbani.

*****

Tofauti na siku nyingine, aliporejewa na fahamu, Jacob alijikuta yuko kwenye chumba kimoja kizuri sana. Alikuwa amelazwa juu ya kitanda cha wagonjwa huku akiwa amefunikwa shuka na kufungwa vizuri sehemu alizokuwa ameumia kutokana na kipigo. Jambo moja lililomtia shaka ni namna alivyokuwa amefungwa mdomo wake. Hakuwa na uwezo wa kuufunua wala kusema lolote. Ndani ya chumba hicho hakukuwa na mtu yeyote zaidi ya msichana mmoja mrembo aliyekuwa amekaa pembeni yake.

Msichana huyo aliachia tabasamu mara alipogundua kuwa Jacob amefumbua macho. Jacob alimuangalia msichana huyo katika hali ya kumsoma. Hakuwa msichana mgeni sana machoni kwake, ila hakukumbuka mara moja kama alimuona wapi. Msichana mwenyewe alionekana kuwa anamfahamu Jacob, alitamani kusema kitu lakini alisita pale mlango wa chumba hicho ulipofunguliwa. Watu wanne waliingia, wote wakiwa ni wanaume. Walionekana kuwa ni watu watanashati na walioneemeka kwa pesa. Japo baadhi husema pesa huwezi kuiona usoni, lakini kuna nyuso ambazo hutangaza wazi kuwa hapa pesa ipo. Jamaa hao waliingia kimya kimya, huku msichana aliyekuwa chumbani humo akipewa ishara ya kutoka nje.

Walionekana kuongea kitu, Jacob alishangaa ni kwa nini hakuweza kusikia. Alitaka kujigusa sikio ili aone ni nini kilisababisha asiweze kuwasikia jamaa hao. Ile kutaka kuinua mkono ndipo alipogundua kuwa alikuwa mefungwa vizuri na kwa ustadi mkubwa katika kitanda hicho alichokuwa amelazwa. Hakuwa na ujanja zaidi. Jamaa hao hawakukaa muda mrefu, huku nyuso zao zikionesha kuridhika na namna Jacob alivyokuwa, walitoka na kufunga mlango nyuma yao.

Japo alikuwa katika chumba kizuri, lakini hali yake ilikuwa mbaya. Aliweza kuisikia njaa ikiongea tumboni mwake. Njaa hiyo ilipelekea maumivu makali ya kichwa, na kwa vile alikuwa amelazwa hali amefungwa kikamilifu damu haikuwa inazunguka vizuri mwilini. Hilo lilipelekea sehemu baadhi za mwili kufa ganzi. Hakuwa anajua hatma yake ingekuwa nini. Alijua wazi kuwa kwa jinsi mambo yalivyokuwa yamefanyika isingekuwa rahisi kwa mtu yeyote kujua yuko wapi na hivyo kuja kumuokoa. Hapo alijikuta akimuomba Mungu amsaidie.

Masaa manne baada ya wale jamaa kuwa wameondoka, mlango wa chumba hicho ulifunguliwa. Mtu wa kwanza wa pili wa tatu na wanne kuingia alikuwa mwanaume, wa tano alikuwa msichana. Japo ilikuwa ni siku nyingi zimepita lakini haikumchukua Jacob hata sekunde arobaini kutambua kuwa msichana aliyeingia alikuwa ni Regina. Kwa mara ya kwanza tangu aingie ndani ya himaya hii Jacob alijikuta akitabasamu. Regina alipomuona Jacob alishindwa kujizuia, machozi yalimtoka na akaenda ili amkumbatie. Hakujua ni namna gani, lakini teke la jamaa mmoja lilimpeleka chini. Sekunde iliyofuatana nayo alishuhudia jamaa aliyempiga teke Regina akiwa chini huku damu zikibubujika kifuani kwake kufuatia pigo la risasi.

“Pole mpenzi, nadhani huyu alikuwa amesahau kuwa malkia wa himaya hii hakutakiwa kufanyiwa hivyo” John Kificho alisema huku akimkumbatia Regina. Hakupendezwa na kitendo cha mmoja wa walinzi wake kumpiga teke Regina. Haikuwa lengo lake kuonesha kuwa alikuwa anamchukia Jacob.

“Regina, nitafanya kila niwezalo kuhakikisha kuwa Jacob anarudi katika hali yake, Daktari anayemuhudumia amesema kuwa Jacob ana hali mbaya sana kufuatia shambulio alilopata, hivi sasa hawezi kusikia wala kuongea. Ila nitajaribu kila niwezalo kuponyesha maisha yake, hii ni kawaida yangu ya kusaidia maisha ya watu” John Kificho alisema huku akiwa anachezea nywele za Regina. Regina alitingisha tu kichwa kama ishara ya kukubaliana na yaliyosemwa na Kificho. Regina alitamani apewe muda wa kuongea na kukaa na Jacob lakini haikuwa hivyo. Muda mfupi baadaye alitakiwa kutoka ndani ya chumba hicho kwa kisingizio kuwa daktari alitaka apewe nafasi ya kufanya kazi yake.

John Kificho na kundi lake walipotoka, aliingia mtu mwingine. Jacob hakuchelewa kumtambua mtu huyu. Alikuwa ni yule jamaa ambaye amekuwa na kazi ya kumpa kipigo tangu aingie ndani ya himaya hii. Jamaa huyo alitoa lile tabasamu lake la dhihaka, kisha akaparamia kitanda alichokuwa amelazwa Jacob. Alianza kumfungua kwa kasi, tena bila huruma ya kujali hali ya Jacob. Kipigo kikali kilifuata baada ya kufunguliwa. Hali ya Jacob ilikuwa dhaifu sana. Njaa ya siku tatu iliyoandama na kipigo kilichonyooka cha kila siku pamoja na mashambulizi ya wadudu kwenye chumba alichokuwa anafungiwa vilitosha kumfanya awe dhaifu. Alilaani sana hali hii iliyokuwa inamkuta, aliamini kuwa ilikuwa aibu kwake kunyanyaswa kiasi kile na mtu kama yule. Aliomba itokee muujiza ajikute yuko katika hali nzuri ili aweze kukabiliana na huyu jamaa.

Kipigo kile kilimfanya apoteze fahamu kwa mara nyingine katika siku hiyo. Alipolejewa na fahamu alijikuta yuko kwenye kile kitanda kizuri sana, lakini akiwa amefungwa kama awali. Mfungaji alikusudia Jacob asiwe na uwezo wa kuinuka wala kuongea. Pembeni yake alikuwa ni yule msichana ambaye hakuwa mgeni sana machoni kwake. Kama ilivyokuwa mwanzo, msichana huyo alipoona Jacob kafungua macho, alitabasamu. Alionekana kunong’ona kitu lakini Jacob hakuweza kusikia. Vifaa maalum alivyowekewa masikioni vilimfanya asiweze kusikia hata kidogo.

Yule msichana alimsogelea Jacob karibu zaidi. Akabandua vile vifaa vya kumfanya asisikie.

“Unajisikiaje mpenzi” sauti tulivu ya huyo msichana iliongea. Jacob aliposikia hiyo sauti, mara moja kumbukumbu zilimjia. Alikumbuka kuwa huyo alikuwa ni Evelyn au Eve kama alivyokuwa amezoea kumuita. Jacob alitaka kujibu lakini alishindwa. Mdomo wake ulikuwa umefungwa. Hivyo aliitikia kwa ishara ya macho tu.

“Pole sana, leo nitajitahidi kufanya mpango wa kukuletea chakula. Hawajui kama tunafamiana, nilifanikiwa kutoka katika jumba la mzee Harken Kalm, nimeajiliwa hapa kama muuguzi. Nashukuru kwa kuwa nimepata nafasi ya kukuonesha kuwa nakupenda” Eve alisema hayo huku akiwa amekaa pembezoni mwa kitanda. Macho yake yalionesha dhahiri upendo aliokuwa nao juu ya Jacob. Kufuatia maneno hayo ya Eve, Jacob alitabasamu. Alifurahi kusikia mpango wa Eve kumletea chakula, alihitaji chakula kuliko kitu kingine chochote kwa wakati huo. Ndoto za yeye kutoka hapo zilianza kumjia. Japo hakujua nje kulikuwa na ulinzi kiasi gani, lakini alijua fika kuwa ulinzi wa kuweza kumzuia yeye akiwa kamili haukuwepo. Alihitaji kuwa kamili, si kupewa silaha ndio awe kamili. Alihitaji chakula ili mwili wake urudiwe na nguvu. Hakujali juu ya majeraha kutokana na kipigo toka kwa jamaa ambalo limekuwa likifanya hivyo.

Kitendo cha Jacob kushindwa kuongea kilimsikitisha zaidi Eve. Hivyo kwa haraka alirudisha vile vifaa masikioni mwa Jacob, kisha akarudi alipokuwa awali. Dakika chache baadaye kitu kama kengele kilitoa mlio. Eve akampungia mkono Jacob na kutokomea nje. Hapo hakuonekana mtu yeyote ndani ya chumba hicho hadi asubuhi siku iliyofuata. Ilikuwa ni siku ya sita kwa mpelelezi Jacob Matata kuwa katika kifungo hiki cha kutisha. Hakujua watu hawa walikuwa na lengo gani kwake, japo alianza kuhisi mauti.

Itaendelea
 
HEKAHEKA - 18

Kidogo nimebadili mawazo, ningependa kummaliza Jacob huku Regina akiwa anajua kuwa Jacob amekwisha, hivyo ni vema sisi tummalize katika njia ambayo Regina atajua kuwa Jacob hayupo tena duniani na wakati huo huo Regina aamini kuwa tumejaribu kuyaokoa maisha ya Jacob. Hivyo fanya namna kumuokoa Jacob kisha nitakuelekeza cha kufanya” Alimaliza John Kificho huku moyo wake ukiwa umeshinikizwa kwa furaha. Aliona mambo yanamnyookea.

“Sawa bosi nitakupigia dakika chache zijazo” ulijibu upande wa pili na kukata simu.

* *

Akili ya Jacob ilikuwa katika mahesabu ya kujumlisha kutoa na kuzidisha, alipokuja kugawanya tayari alikuwa amesharuka. Wakati Jacob akiruka, upande nje ya chumba walichokuwa kilisikika kishindo cha mtu akianguka. Hii ilimsaidia sana Jacob, kwani baadhi ya watu ilibidi wakimbilie nje na kuacha wachache tu humo ndani. Nje ilisikika hali ya mapigano makali, huku ndani Jacob alikuwa akisuguana na waliobaki akiwemo yule kiongozi wao.

Ulikwa ni mpambano mkali, ambapo mpaka unakwisha Jacob alikuwa hoi huku adui zake wakiwa marehemu. Alikuwa ameshinda kwa taabu sana kwani jamaa hao walikuwa ni wazuri wa kutosha. Alijivuta na kusimama kwa kusaidiwa na kiti. Akiwa anajiweka sawa, mlango ulifunguliwa. Hakuwahi hata kujiweka sawa kabla hajatazamana na mdomo wa bastola. Alikuwa ni kijana wa John Kificho.

“Toka nje” Jamaa aliamuru. Jacob alijikongoja.


* * *

Dakika chache baadaye gari iliyokuwa imembeba Jacob ilikuwa ikitambaa juu ya barabara moja ya jiji la Dar es salaam. Ndani kulikuwa na vijana kadhaa wa John Kificho. Walishika barabara ya Sam Nujoma, Ubungo, Mabibo, Buguruni, uwanja wa taifa. Walipofika hapo, vitambaa vya madirishani vilifunika na hivyo Jacob hakujua waliingia wapi. Walipofika eneo ambalo bila shaka ndio ilikuwa mwisho wa safari yao, mlio wa honi ulisikika. Ulisikika mlio wa geti kufunguliwa.

Aliposhuka alijikuta yuko eneo la wazi, lakini kulikuwa giza tupu. Ilikuwa kama ukumbi mkubwa usiokuwa na viti wala chochote. Hali ilikuwa kimya kabisa eneo hilo. Hatua kama hamsini hivi toka lilipokuwa gari lao, kulionekana mwanga wa taa. Lakini tofauti na matarajio yake, haikuamriwa yeye kupelekwa huko. Aliingizwa kwenye chumba fulani. Ilibidi kupita milango mitatu kabla ya kufikia chumba hicho. Jumba hili lilikuwa na ulinzi wa kutisha. Walinzi wake wote walionekana wakiwa makini, huku wakiwa wamewezeshwa kwa silaha za kisasa mno.

Jacob alijikagua na kuona jinsi alivyokuwa ameumia. Ilikuwa dhahiri kichwani mwake kuwa kulikuwa na makundi mawili aliyokuwa akipambana nayo. Hakujua kundi jingine lilikuwa na lengo gani nae. Hakuwa na shaka kuwa kundi la kwanza lilikuwa na lengo la kuficha ukweli fulani juu ya msichana Regina.

Mpaka anajiandaa kwenda kuvamia nyumbani kwa mzee Harken Kalm, Jacob alikuwa akiamini kuwa msichana Regina angekuwa ndani ya jumba hilo la mzee Harken Kalm. Lakini kufuatia mahojiano yake na mtu aliyekuwa ameongoza kundi la kuja kumteka ilionesha kuwa Regina alikuwa ametoweka katika himaya ya hao jamaa. Ameenda wapi na amewezaje kutoka? Hayo ni baadhi ya maswali ambayo Jacob matata alihitaji kupata majibu yake. Pia hakujua hawa watu walikuwa na lengo gani. Alikumbuka kifo cha Bob Sepeto, akahisi kuwa kundi hili laweza kuwa linahusika. Kwa nini?

Siku ya kwanza ilipita kwa mateso makubwa sana. Hakuna aliyekuwa amekuja kumuona wala kumpa chakula. Chumba hicho kilikuwa kichafu na hivyo kuwa makazi ya chawa, viroboto na papasi wenye njaa kali. Hewa ilikuwa ndogo sana. Japo hali ya maumivu ilikuwa imetoweka, lakini njaa ilikuwa ikimsumbua sana. Alichoweza kufanya ni kujinyooshanyoosha viungo ili kujiweka fiti. Watu kama hawa ndio maana huitwa makomandoo.

Siku ya pili jioni mlango wa chumba ulifunguliwa. Taa ndogo iliyokuwa ukutani iliwaka na kutoa mwanga hafifu sana. Kwa vile Jacob alikuwa amekaa kwenye giza kwa zaidi ya masaa 72, mwanga huo ulikuwa tosha sana kwake. Mara mbele yake alisimama jamaa mmoja aliyeonekana kushiba kiasi cha kutosha. Jamaa hilo halikuongea kitu. Lilipoingia tu, mlango nyuma yake ulifungwa. Jacob alisimama ili kuona jamaa huyu alikuwa ametumwa kufanya nini. Macho yao yalipogongana ndipo Jacob alipogundua kuwa jitu hilo lilikuwa si salama kwa hali yoyote. Lilizidi kumsogelea. Japo alikuwa na njaa, Jacob ilibidi ajiweke tayari kwa lolote. Lilipokuwa kama hatua tatu hivi toka alipokuwa Jacob, jitu hilo lilibadirika na kuwa mbogo kwa mapigo makali. Lilimpelekea mapigo makali sana ambayo kama si ustadi wa Jacob kuyakwepa, basi agekuwa kwenye ulimwengu mwingine. Mara kadhaa Jacob alijaribu kupeleka mashambulizi hakuambulia chochote. Jamaa alikuwa fundi katika kupigana. Dakika saba zilikatika huku hali ikiwa ngumu sana ndani ya chumba hicho. Kwa vile alikuwa na njaa, ukichanganya na ufundi wa hilo jamaa, Jacob alijikuta amechoka sana. Jamaa halikupunguza kasi ya mashambulizi wala halikuonesha dalili yoyote ya kuchoka.

Taratibu, nguvu zilianza kumpa mkono Jacob kama miale ya jua inavyopotelea mawinguni nyakati za jioni. Hali hii ilipelekea kupungua kwa uwezo wake wa kukabiliana na mpinzani wake. Jamaa lilipeleka wimbi zito la mateke na ngumi kwa Jacob, kwa vile alikuwa amepungukiwa uwezo, baadhi ya mapigo yakaanza kumuingia. Dakika chache baadaye, akawa kama gunia la kufanyia mazoezi. Mwisho fahamu zilimtoka Jacob, hakujua hata wakati jamaa hilo lilipotoka chumbani humo.

Fahamu zilipomjia alijikuta akiwa amelala ndani ya chumba hicho huku wale wadudu ambao ni wakazi wa chumba hicho wakiwa wanamfanyia sherehe. Alijaribu kusimama, akasimama. Mwili ulikuwa umedhohofika sana kutokana na njaa pamoja na kipigo alichokuwa amepata. Hakuweza kujua kama ilikuwa ni muda gani wakati huo, hakujua kama ilikuwa ni mchana au usiku. Pia hakuweza kujua kama ilikuwa imemchukua muda gani mpaka pale fahamu zilipokuwa zimemrudia. Alijinyoosha viungo kwa kutembea hapa na pela, aliruka kidogo na kufanya mazoezi mepesi. Alijua hili ndilo lilikuwa ndani ya uwezo wake na hakupenda kuuacha mwili uvunde kabisa maana ingemfanya awe katika hatari zaidi.

Siku ya tatu, Jacob alikuwa katika hali mbaya zaidi. Njaa, mshambulizi ya wadudu kwenye chumba hicho, na yale ya yule jamaa yalimfanya adhoofu kiasi cha kusikitisha. Wenyeji wa chumba hicho yaani, viroboto, papasi na chawa walionesha kuanza kuneemeka. Wengi afya zao zilibadirika ghafla tangu pale Jacob alipokuwa ameingia ndani ya chumba hicho. Muda fulani ulipofika mlango wa chumba hicho ulifunguliwa. Ile taa yenye mwanga hafifu iliwashwa kama ilivyokuwa jana. Mtu aliingia, Jacob alipomtazama alitambua kuwa ni lile jamaa. Mwili ulimsisimka na hasira iliyochanganyika na chuki juu ya jamaa huyu ilimkaba kooni. Alitamani angekuwa katika uwezo wake wa kawaida ili alifundishe adabu jitu hilo.

Kama kawaida, lilimsogelea taratibu huku likiwa na tabasamu la uovu usoni kwake. Jacob alijiweka sawa huku hali ya mwili wake ikiwa dhaifu kiasi cha kusikitisha. Jamaa hilo halikuwa na hata chembe ya huruma, lilianza kumshambulia Jacob kwa namna ya kuua. Jacob alitumia nguvu zake zote alizokuwa amebaki nazo kujaribu kujihami. Lakini hakuweza kufanya hivyo kwa muda mrefu. Hakuwa amebakiwa na nguvu kabisa. Ninaposema jamaa hilo linapiga, ninamaanisha. Ni jitu lililofundishwa kupiga na linajua kupiga sehemu ya kupiga. Kwa mara nyingine fahamu zilimtoka Jacob. Angekuwa ni mtu wa hivi hivi tu, tayari angekuwa ameshapewa jina la marehemu. Kama ilivyokuwa jana yake, hakuweza jua wakati jitu hilo lilipotoka mule chumbani.

*****

Tofauti na siku nyingine, aliporejewa na fahamu, Jacob alijikuta yuko kwenye chumba kimoja kizuri sana. Alikuwa amelazwa juu ya kitanda cha wagonjwa huku akiwa amefunikwa shuka na kufungwa vizuri sehemu alizokuwa ameumia kutokana na kipigo. Jambo moja lililomtia shaka ni namna alivyokuwa amefungwa mdomo wake. Hakuwa na uwezo wa kuufunua wala kusema lolote. Ndani ya chumba hicho hakukuwa na mtu yeyote zaidi ya msichana mmoja mrembo aliyekuwa amekaa pembeni yake.

Msichana huyo aliachia tabasamu mara alipogundua kuwa Jacob amefumbua macho. Jacob alimuangalia msichana huyo katika hali ya kumsoma. Hakuwa msichana mgeni sana machoni kwake, ila hakukumbuka mara moja kama alimuona wapi. Msichana mwenyewe alionekana kuwa anamfahamu Jacob, alitamani kusema kitu lakini alisita pale mlango wa chumba hicho ulipofunguliwa. Watu wanne waliingia, wote wakiwa ni wanaume. Walionekana kuwa ni watu watanashati na walioneemeka kwa pesa. Japo baadhi husema pesa huwezi kuiona usoni, lakini kuna nyuso ambazo hutangaza wazi kuwa hapa pesa ipo. Jamaa hao waliingia kimya kimya, huku msichana aliyekuwa chumbani humo akipewa ishara ya kutoka nje.

Walionekana kuongea kitu, Jacob alishangaa ni kwa nini hakuweza kusikia. Alitaka kujigusa sikio ili aone ni nini kilisababisha asiweze kuwasikia jamaa hao. Ile kutaka kuinua mkono ndipo alipogundua kuwa alikuwa mefungwa vizuri na kwa ustadi mkubwa katika kitanda hicho alichokuwa amelazwa. Hakuwa na ujanja zaidi. Jamaa hao hawakukaa muda mrefu, huku nyuso zao zikionesha kuridhika na namna Jacob alivyokuwa, walitoka na kufunga mlango nyuma yao.

Japo alikuwa katika chumba kizuri, lakini hali yake ilikuwa mbaya. Aliweza kuisikia njaa ikiongea tumboni mwake. Njaa hiyo ilipelekea maumivu makali ya kichwa, na kwa vile alikuwa amelazwa hali amefungwa kikamilifu damu haikuwa inazunguka vizuri mwilini. Hilo lilipelekea sehemu baadhi za mwili kufa ganzi. Hakuwa anajua hatma yake ingekuwa nini. Alijua wazi kuwa kwa jinsi mambo yalivyokuwa yamefanyika isingekuwa rahisi kwa mtu yeyote kujua yuko wapi na hivyo kuja kumuokoa. Hapo alijikuta akimuomba Mungu amsaidie.

Masaa manne baada ya wale jamaa kuwa wameondoka, mlango wa chumba hicho ulifunguliwa. Mtu wa kwanza wa pili wa tatu na wanne kuingia alikuwa mwanaume, wa tano alikuwa msichana. Japo ilikuwa ni siku nyingi zimepita lakini haikumchukua Jacob hata sekunde arobaini kutambua kuwa msichana aliyeingia alikuwa ni Regina. Kwa mara ya kwanza tangu aingie ndani ya himaya hii Jacob alijikuta akitabasamu. Regina alipomuona Jacob alishindwa kujizuia, machozi yalimtoka na akaenda ili amkumbatie. Hakujua ni namna gani, lakini teke la jamaa mmoja lilimpeleka chini. Sekunde iliyofuatana nayo alishuhudia jamaa aliyempiga teke Regina akiwa chini huku damu zikibubujika kifuani kwake kufuatia pigo la risasi.

“Pole mpenzi, nadhani huyu alikuwa amesahau kuwa malkia wa himaya hii hakutakiwa kufanyiwa hivyo” John Kificho alisema huku akimkumbatia Regina. Hakupendezwa na kitendo cha mmoja wa walinzi wake kumpiga teke Regina. Haikuwa lengo lake kuonesha kuwa alikuwa anamchukia Jacob.

“Regina, nitafanya kila niwezalo kuhakikisha kuwa Jacob anarudi katika hali yake, Daktari anayemuhudumia amesema kuwa Jacob ana hali mbaya sana kufuatia shambulio alilopata, hivi sasa hawezi kusikia wala kuongea. Ila nitajaribu kila niwezalo kuponyesha maisha yake, hii ni kawaida yangu ya kusaidia maisha ya watu” John Kificho alisema huku akiwa anachezea nywele za Regina. Regina alitingisha tu kichwa kama ishara ya kukubaliana na yaliyosemwa na Kificho. Regina alitamani apewe muda wa kuongea na kukaa na Jacob lakini haikuwa hivyo. Muda mfupi baadaye alitakiwa kutoka ndani ya chumba hicho kwa kisingizio kuwa daktari alitaka apewe nafasi ya kufanya kazi yake.

John Kificho na kundi lake walipotoka, aliingia mtu mwingine. Jacob hakuchelewa kumtambua mtu huyu. Alikuwa ni yule jamaa ambaye amekuwa na kazi ya kumpa kipigo tangu aingie ndani ya himaya hii. Jamaa huyo alitoa lile tabasamu lake la dhihaka, kisha akaparamia kitanda alichokuwa amelazwa Jacob. Alianza kumfungua kwa kasi, tena bila huruma ya kujali hali ya Jacob. Kipigo kikali kilifuata baada ya kufunguliwa. Hali ya Jacob ilikuwa dhaifu sana. Njaa ya siku tatu iliyoandama na kipigo kilichonyooka cha kila siku pamoja na mashambulizi ya wadudu kwenye chumba alichokuwa anafungiwa vilitosha kumfanya awe dhaifu. Alilaani sana hali hii iliyokuwa inamkuta, aliamini kuwa ilikuwa aibu kwake kunyanyaswa kiasi kile na mtu kama yule. Aliomba itokee muujiza ajikute yuko katika hali nzuri ili aweze kukabiliana na huyu jamaa.

Kipigo kile kilimfanya apoteze fahamu kwa mara nyingine katika siku hiyo. Alipolejewa na fahamu alijikuta yuko kwenye kile kitanda kizuri sana, lakini akiwa amefungwa kama awali. Mfungaji alikusudia Jacob asiwe na uwezo wa kuinuka wala kuongea. Pembeni yake alikuwa ni yule msichana ambaye hakuwa mgeni sana machoni kwake. Kama ilivyokuwa mwanzo, msichana huyo alipoona Jacob kafungua macho, alitabasamu. Alionekana kunong’ona kitu lakini Jacob hakuweza kusikia. Vifaa maalum alivyowekewa masikioni vilimfanya asiweze kusikia hata kidogo.

Yule msichana alimsogelea Jacob karibu zaidi. Akabandua vile vifaa vya kumfanya asisikie.

“Unajisikiaje mpenzi” sauti tulivu ya huyo msichana iliongea. Jacob aliposikia hiyo sauti, mara moja kumbukumbu zilimjia. Alikumbuka kuwa huyo alikuwa ni Evelyn au Eve kama alivyokuwa amezoea kumuita. Jacob alitaka kujibu lakini alishindwa. Mdomo wake ulikuwa umefungwa. Hivyo aliitikia kwa ishara ya macho tu.

“Pole sana, leo nitajitahidi kufanya mpango wa kukuletea chakula. Hawajui kama tunafamiana, nilifanikiwa kutoka katika jumba la mzee Harken Kalm, nimeajiliwa hapa kama muuguzi. Nashukuru kwa kuwa nimepata nafasi ya kukuonesha kuwa nakupenda” Eve alisema hayo huku akiwa amekaa pembezoni mwa kitanda. Macho yake yalionesha dhahiri upendo aliokuwa nao juu ya Jacob. Kufuatia maneno hayo ya Eve, Jacob alitabasamu. Alifurahi kusikia mpango wa Eve kumletea chakula, alihitaji chakula kuliko kitu kingine chochote kwa wakati huo. Ndoto za yeye kutoka hapo zilianza kumjia. Japo hakujua nje kulikuwa na ulinzi kiasi gani, lakini alijua fika kuwa ulinzi wa kuweza kumzuia yeye akiwa kamili haukuwepo. Alihitaji kuwa kamili, si kupewa silaha ndio awe kamili. Alihitaji chakula ili mwili wake urudiwe na nguvu. Hakujali juu ya majeraha kutokana na kipigo toka kwa jamaa ambalo limekuwa likifanya hivyo.

Kitendo cha Jacob kushindwa kuongea kilimsikitisha zaidi Eve. Hivyo kwa haraka alirudisha vile vifaa masikioni mwa Jacob, kisha akarudi alipokuwa awali. Dakika chache baadaye kitu kama kengele kilitoa mlio. Eve akampungia mkono Jacob na kutokomea nje. Hapo hakuonekana mtu yeyote ndani ya chumba hicho hadi asubuhi siku iliyofuata. Ilikuwa ni siku ya sita kwa mpelelezi Jacob Matata kuwa katika kifungo hiki cha kutisha. Hakujua watu hawa walikuwa na lengo gani kwake, japo alianza kuhisi mauti.

Itaendelea
Tuendelee mkuu.
 
HEKAHEKA - 19

Kitendo cha Jacob kushindwa kuongea kilimsikitisha zaidi Eve. Hivyo kwa haraka alirudisha vile vifaa masikioni mwa Jacob, kisha akarudi alipokuwa awali. Dakika chache baadaye kitu kama kengele kilitoa mlio. Eve akampungia mkono Jacob na kutokomea nje. Hapo hakuonekana mtu yeyote ndani ya chumba hicho hadi asubuhi siku iliyofuata. Ilikuwa ni siku ya sita kwa mpelelezi Jacob Matata kuwa katika kifungo hiki cha kutisha. Hakujua watu hawa walikuwa na lengo gani kwake, japo alianza kuhisi mauti.



* * *



Ilikuwa ni siku ya nne yenye mashaka na uchungu kwa mkuu huyu wa kitengo fukuzi. Mpaka wakati huu vijana wake walikuwa wameshafanya kila liwezekanalo kuhakikisha kuwa wanajua alipo mpelelezi mwenzao Jacob Matata. Lakini mpaka inafika asubuhi hii hakuna hata fununu walizokuwanazo juu ya Jacob. Kutokana na maiti walizozikuta nyumbani kwa Jacob siku Jacob alipotoweka, ilikuwa wazi vichwani mwao kuwa Jacob hakuwa amechukuliwa kwa heri. Ilikuwa hakika kuwa kabla ya kuchukuliwa yalikuwa yametokea mapambano makali yaliyopelekea kuuawa kwa watu hao. Jacob yuko hai au maiti? Kama yuko hai, atakuwa sehemu gani? Maswali haya yamekuwa yakijirudia rudia kichwani kwa Bi. Anita mkuu wa Ofisi Fukuzi.

Siku ile kabla ya kutoweka kwa Jacob, ofisi hiyo ilikuwa imeandaa operesheni kubwa ya kwenda kwenye jumba la mzee Harken Kalm. Operesheni hiyo ingeongozwa na Jacob Matata mwenyewe. Lakini kitendo cha kutoweka kwake ilikuwa ni wazi kuwa wasingeweza tena kwenda, kwani ni Jacob aliyekuwa akipajua mahali walipokusudia kwenda. Hivyo ofisi yote ilikuwa imekumbwa na ubaridi wa kutisha.

Mpaka kufikia siku hii, Bi. Anita alikuwa ameshapiga simu kila sehemu aliyodhani kungekuwa na tetesi. Lakini Jambo moja lilikuwa likija kwa mbali- Jacob yuko hai japo yawezekana kuwa katika shida.



* * *



Kila mmoja kwa lengo lake alikuwa katika jitihada zake. John Kificho alikuwa amekufa katika kumpenda msichana Regina, hivyo alikuwa katika jitihada za kuuteka moyo wa msichana huyo. Kwa sababu asizozijua, mpelelezi Jacob Matata alijikuta mikononi mwa John Kificho. Hakuwa anamjua Kificho lakini alikuwa katika hali mbaya na alitakiwa kufanya kitu ili kujinasua katika mikono hiyo hatari.

Regina alishatambua nia ya Kificho kumtaka, lakini hakujua kuwa Kificho hakuwa na lengo la kumsaidia Jacob Matata. Hivyo alianza kumuamini Kificho na kumchukulia kama mtu mwenye huruma ajabu. Pamoja na hayo, moyo wa Regina ulikuwa katika mapenzi mazito kwa mpelelezi Jacob Matata.

Mzee Harken Kalm kwa upande wake alikuwa amechanganyikiwa, kutoweka kwa Regina na kutoonekana kwa Jacob Matata aliona kuwa ni hatari kwa himaya yake. Hivyo alikuwa akifanya kila njia kuhakikisha anampata Jacob na Regina, ambao aliamini kuwa walikuwa na siri zake.

Bi. Anita mkuu wa kikosi cha siri cha ofisi fukuzi, ameamua kuacha ofisi na kuingia uwanja wa mapambano kuongoza kundi la vijana wake kuhakikisha wanampata Jacob na kusambaratisha himaya ya mzee Harken Kalm. Alikuwa makini kufuatilia na kutaka kujua Jacob yuko wapi, kwani aliamini kuwa kwa vyovyote Jacob yuko hai.



Tamaa. Ni tamaa iliyosababisha mzee Harken Kalm, apokee simu hii. Alikuwa ndani ya chumba maalum ndani ya himaya yake, akisubiri taarifa yoyote nzuri juu ya msako uliokuwa ukiendelea. Tangu kutoweka kwa Regina na kutoonekana kwa Jacob Matata, mzee huyu amekuwa hana amani huku akijiona hayuko salama kabisa. Kikosi cha Tai, kikosi cha Paka na kikosi cha Mbwa weusi vyote vilikuwa vimesambaa katika maeneo mbali mbali kuhakikisha Jacob na Regina wanapatikana.

Simu hiyo haikulia muda mrefu kabla mzee Harken Kalm hajainyanyua na kunong’ona

“Leta habari” Alisema hivyo akiwa na hakika kuwa huyu alikuwa ni mmoja wa vijana wake.

“Shikamoo mzee!” Ulisema upande wa pili. Mzee Harken Kalm hakuitikia, badala yake akasema.

“Siko kwa hilo, labda unalingine nikusaidie!” Kadhalika sauti ya mzee Harken Kalm ilitoka katika hali ya kunong’ona.

“Sihitaji msaada wako ila nipo kukupa msaada!” Ulijibu upande wa pili katika sauti nzito, tulivu ya raha.

“Shiit, unaweza nisaidia nini wewe? Kwanza umepataje hii namba?” Mzee Harken Kalm aliongea tena kwa kunong’ona. Aliongea hivyo huku akiwa anajiandaa kuweka simu chini. Hakuwa amependezwa na maongezi ya mtu huyu asiye mfahamu.

“Ni juu ya Jacob na Regina!!” Kwa ile sauti nzito, tulivu ya raha mtu wa upande wa pili alisema. Ilikuwa wazi kuwa mtu huyu alikuwa akisema maneno hayo kwa raha mno.

“Wamefanyaje?” Mzee Harken Kalm aliukumbatia zaidi mkono wa simu, huku ngozi yake ikibadilika na kuwa nyekundu.

“Najua walipo!” Ulisema upande wa pili.

“wako wapi?” Mzee Harken Kalm alinong’ona zaidi kana kwamba alikuwa na mtu chumbani humo.

“umeulizia hatua ya mwisho, kuna hatua kabla ya hilo swali” ulisema upande wa pili kwa sauti ya pozi.

“Una hakika na usemayo?” Harken Kalm alinong’ona

“asili mia moja!”

“hatua gani sijauliza”

“Pesa”

“Siyo pesa, nitakupa fedha. Sema uko wapi na nikupateje?” Mzee Harken Kalm aliongea huku akiminya kitufe fulani. Mara walikuja vijana wawili, walisimama wakisubiri amri zaidi toka kwa mzee Harken Kalm.

“Sawa, kesho asubuhi nitaenda benki kuangalia kama utakuwa umeniwekea hizo pesa au fedha kama unavyoita. Nikizikuta nitawaelekeza mahali mtakapo wachukua watu wenu” Ulisema upande wa pili, kisha mtu huyo alitaja namba za akaunti yake ya benki kisha akakata simu.

Simu ilipokatwa, mzee Harken Kalm aliwageukia vijana wake, kisha akanong’ona “Nataka kujua hii simu imepigwa kutoka wapi na habari kamili za mpigaji” alipomaliza alibonyeza kitufe fulani akapotelea ardhini. Jitihada zilifanyika kuhakikisha mpigaji wa simu hiyo anajulikana. Lakini masaa kadhaa yalikatika bila mafanikio, ilikuwa ni ujumbe tosha kwa mzee Harken Kalm kuwa mpigaji wa simu alikuwa mtu aliyejiandaa na si vinginevyo.



Taarifa kuwa vijana wake walishindwa kujua sehemu aliyokuwepo mtu aliyepiga simu na kutaka ampe pesa ili amuambie Jacob na Regina walipo, zilimfanya Mzee Harken Kalm apate hamu ya kusikiliza tena sauti ya huyo mtu. Akiwa kwenye chumba chake cha siri kilicho chini ya ardhi, alibonyeza kitufe fulani kilichokuwa pembeni ya redio yake, mara sauti za mazungumzo waliyofanya na huyo mtu kwenye simu zilitokea tena. Alisikiliza kwa makini tena na tena. Kilichomfanya arudie kusikiliza ni sauti ya mtu huyu aliyempigia, haikuwa ngeni masikioni kwa Harken Kalm.

"shiiiit, Banzi!!!!!!!!” Alisonya kwa hasira.

"Mshenzi huyu bado yuko hai?” alijisemea kwa mshangao. Mzee Harken Kalm baada ya hapo aliwasha Laptop yake. Humo alifunua mafaili kadhaa kisha akatulia huku akisoma taarifa fulani. Alichukua kijtabu chake kidogo akaandika vitu fulani kisha uso wake ukaonesha tabasamu fulani. akasimama na kutoka katika chumba hicho. Alipita vyumba kadhaa ambavyo vyote vilikuwa sehemu ya ardhini ambayo ni mzee Harken Kalm pekee aliyekuwa anajua namna ya kuingia huko. Alitembea hivyo hadi alipofika kwenye mlango uliokuwa umeandikwa ‘Contact the world’ hapo alibonyeza namba fulani mlangoni hapo na mlango ukafunguka. Chumba hiki kilikuwa kipana angavu na kilichosheheni vifaa mbali mbali vya mawasiliano. Hapo Harken Kalm, aliwasiliana na huyu akaacha, akampigia yule, akakunja uso akakata simu, akamtumia ujumbe huyu, ujumbe ulipojibiwa akatabasamu, akapiga na kupiga, akaandika ujumbe na kusoma mwisho akaonekana kuchoka...ni wakati anaelekea kutaka kutoka chumbani humo ndipo akawa kama aliyekumbuka kitu. Akachukua mashine fulani na kuingiza namba kadhaa. Mashine ilitoa milio...Ngriiiiiih ngriiiiii ngriiiiii, kama mara sita hivi.

“Old friend!!!” Harken Kalm alisema kwa sauti chovu iliyochanganyika na matumaini kwa mbali.

“Ben, umejichimbia wapi?” Harken Kalm alihoji baada ya upande wa pili kuwa kimya

“Najipa nafasi Harken Kalm!” Upande wa pili ulijibu.

“Nahitaji huduma yako Ben kama uko sawa!”

“Unajua kuwa wewe siwezi kukukatalia” Upande wa pili ulijibu kasha ukaongeza.

“Ndio Kalm nikusaidie nini?”

“Unaweza jua Banzi yuko wapi kwa sasa?” Kalm aliuliza.

“Kuna sehemu fulani anakula bata” Upande wa pili ulijibu.

"Sikiliza Ben, nilikuambia kuwa kuna kazi nataka nikupe, sasa nakupa kazi, alipo Banzi ndipo alipo Jacob Matata na Binti mmoja aitwaye Regina. Sasa nakupa kazi ya kuwamaliza wote watatu, utatumia njia gani na namna gani hiyo sitaki kujua, nataka ukinipigia simu uniambie kuwa kazi tayari nami nitafanya mambo yangu” Harken Kalm alisema huku sauti yake ikiwa na mchanganyiko wa uchungu na hasira kama ladha ya maziwa ya mgando yaliyo haribika.

“Hiyo kazi ni ngumu sana, unajua hapo unaniambia nifanye kazi ya kuwamaliza makomandoo wawili, unajua fika uwezo wa Banzi na Jacob, najua fika kwa sasa hawako pamoja, kwa vyovyote ilivyo Jacob atakuwa mateka wa Banzi. Wewe mzoefu wa mambo haya, bila shaka unajua itakuwa hatari kiasi gani, hivyo hilo lazima ulizingatie kwenye malipo la sivyo nikimaliza kuwaua wao utafuata wewe” Sauti ya upande wa pili iliongea, iliongea kwa kuunguruma na mikwaruzo kama kawaida yake.

“Ben mimi na wewe hatujakutana barabarani bana” Harken Kalm alisema.

“Yeah, nadhani unajua ni kwa nini nafanya hivi, sihitaji pesa Harken Kalm, ila nahitaji kumuenzi baba yako. He was a good man” Upande wa pili ulisema.

Waliagana simu ikakatwa.

“Dawa ya moto ni moto, si maji, Ben ataumaliza mchezo” Harken Kalm alijisemea huku uso wake ukipata matumaini.



* * *



Baada ya mazungumzo na Harken Kalm, mwili wa Ben ulisisimka, alitabasamu, tabasamu baridi, picha ya Jacob Matata na Banzi zilimjia kichwani, aliwaangalia kila mmoja kwa zamu, kisha akaelekea kwenye friji na kutoa karoti moja akaanza kutafuna huku anazunguka sebuleni kwake.



Ben alikuwa Komandoo, komandoo kamili kwa maana ya kuhitimu. Mafunzo ya mtaani alipokuwa akingali mdogo, baadae alipojiunga na jeshi baada ya kufeli kidato cha nne, kisha kuwa miongoni mwa vijana kumi na tano waliochukuliwa kwenda Cuba kwa mafunzo baada ya urafiki wa Nyerere na Castro kuwa umekolea. Kwa vile alihitimu kwa kiwango cha kutisha, mwalimu wake wa kichina alimfanyia mpango wa kujiunga na shirika moja la siri nchini china ambalo lilikwa likitoa huduma ya uuaji ‘assassination service’. Alijiunga na shirika hilo kwa siri na kuwa miongoni mwa wauaji wa kuogopwa japo sura yake na jina lake halisi halikuwa likijulika. Watu wengi duniani hasa mashirika ya kijasusi na kigaidi yalimjua kwa jina moja tu – Kiroboto.



Mwaka 1995 alipata ujumbe wa siri kuwa alihitajika kwenda Siera Lione ambako mtu mmoja maarufu alikuwa katika harakati za kuuchukua urais wa nchi hiyo. Japo mtu huyo alikuwa mwanajeshi, lakini alitaka kuwa na mlinzi wake ‘special’ mbali na wanajeshi. Hivyo alikubali kulindwa na wanajeshi, lakini kwa sababu ambazo zilikubaliwa na waliokuwa wakitaka kumuweka madarakani, ilibidi atafutwe mtu special. Majina mengi yalipendekezwa ndani na nje ya bara la Afrika, lakini jina moja tu lilipita, nalo ni Kiroboto.



Moja kati ya masharti aliyopewa Kiroboto ili kupata kazi hiyo, ilikuwa ni kuua wazazi wake wote ili atakapokuwa katika kutimiza majukumu yake kitu muhimu kwake iwe ni huyo Rais mtarajiwa tu. Kwa Ben au Kiroboto kama alivyofahamika, mambo mawili yalikuwa muhimu sana kwake, pesa na wanawake. Alipenda pesa kama roho yake na pia alipenda wanawake kama mwili wake mwenyewe. Hivyo kwa kuzingatia kiasi cha pesa alichokuwa ameahidiwa kwa kazi ile, haikumpa shida kuja Tanzania na kuwamaliza wazazi wake wote wawili kwa risasi. Baada ya hapo akarejea Siera Lione na kuianza kazi yake ya kuulinda uhai wa aliyekuwa Rais mtarajiwa wa nchi hiyo wakati huo. Kweli alikuwa Kiroboto, kwani hadi mkataba wake ulipokwisha kila mmoja alinyoosha mikono kuwa jamaa alikuwa kiroboto. Cha mwisho kilichompa umaarufu zaidi duniani, ni pale mtu aliyemlinda kwa miaka mitano alipoona ameshachukua madaraka ya Urais, kwa siri alisitisha mkataba na Kiroboto. Kwa vile jeshi lilikuwa halimpendi na waliona tayari ameshakuwa na siri nyingi za nchi hiyo, hivyo wakaamuru auawe. Kikatumwa kikosi cha watu ishirini kufanya kazi hiyo. Ndani ya siku mbili watu wote hao waliuawa, tena si kwa risasi bali kwa mkono wa Kiroboto huku yeye mwenyewe akifanikiwa kuondoka nchini humo na kiasi kikubwa cha fedha na almasi ambazo alipewa kama zawadi na Rais aliyekuwa madarakani.



Kwa sasa Ben si mtu mwenye shida ya fedha, ila kuna kitu kinausumbua moyo wake, nacho ni kisasi, wala hakuwahi kuchukua kazi nyingine baada ya kupata utajiri ule toka Sierra Lione. Fununu za kuwa Harken Kalm ndio damu pekee iliyobaki toka kwa kingozi yule wa Sierra Lione zilimfikia Ben. Pia hakuchelewa kujua kuwa Harken Kalm alikuwa akifanya biashara haramu, lakini alijiapiza kumlinda kwa namna yoyote ile. Aliona hiyo ndio ingekuwa njia pekee ya yeye kulipa fadhila kwa kiongozi yule aliyempa utajiri alio nao sasa. Kwa siri sana Ben alijitambulisha kwa Harken Kalm, na kumwambia kuwa yupo kama atamuhitaji. Walitambuana. Hivyo simu hii ya kuomba msaada toka kwa Harken Kalm aliichukulia kwa uzito unaotakiwa. Alitamani kujikumbushia michezo yake, ila damu ilimsisimka zaidi alipotambua kuwa mchezo huu utamkutanisha na Jacob Matata na Komandoo Banzi. Ben and Jacob walikuwa miongoni mwa wale vijana waliokwenda Cuba. Wakati yeye alitoroshwa baada ya mafunzo kuisha, Jacob yeye alirejea Tanzania. Si kwamba Ben alikuwa mzuri zaidi ya Jacob, ila kilichomfanya mwalimu wa kichina amchukue Ben ni kwa vile alikuwa katili sana. Hivyo aliona kazi ya kuwa muuaji maalum wa kuajiriwa ingemfaa zaidi. Jacob alikuwa vizuri zaidi kimafunzo ila alikuwa na utu hivyo hakufaa kupelekwa kuwa muuaji.



Kila mmoja alishasikia sifa za mwenzake, Ben alijua kuwa Jacob Matata ni mpelelezi asiyeshindwa, na Jacob alishazisikia sifa za Kiroboto hasa ile habari ya namna alivyotoroka Sierra Lione ilimsisimua sana.



* * *



Huyu yeye anaitwa Gaucho, anamiliki kituo cha kufanyia mazoezi - Gym, maeneo ya Kimara Baruti. Leo hii hakufungua kituo chake. Si kwamba hakupenda kufungua au hakuwa na wateja, la hasha, alikuwa na wateja wengi, na wengi walishampigia kelele kwa nini huwa hafungui siku za Jumamosi. Jumamosi ingekuwa ni siku nzuri kwake kufungua kwa vile watu wengi ndio huwa na nafasi ya kufanya mazoezi, lakini asingeweza kufanya hivyo kwa sababu ya mtu mmoja tu, ndio mtu mmoja, mteja mmoja tu ndiye ambaye alisababisha Gaucho asiwe anafungua kituo chake siku ya Jumamosi.



Mteja huyo alijitambulisha kwa Gaucho kwa jina moja tu, Ben. Siku Ben amekuja ofisini kwa Gaucho hapo kwenye kituo cha mazoezi, alionekana kama mtu aliyepotea njia. Muonekano wake - mavazi, macho, usafi na uongeaji wake vilimfanya Gaucho atake kumuondoa haraka eneo hilo la ofisi yake. Walipoanza maongezi kidogo hali ikawa tofauti.

“Naitwa Ben.....” Sauti nzito iliyo na mikwaruzo ilisema huku macho makali yakiusanifu uso wa Gaucho.

“Sema nikusaidie nini” Gaucho alijibu kwa kukereka kidogo.

“Nahitaji sehemu ya kufanyia mazoezi.....”

“Mazoezi gani unayotaka kufanya wewe, ..na, ..na....unadhani hii sehemu ni muafaka kwako?”

Kabla ya kujibu, Ben aliminya vidole vyake, ule mlio wa vidole kuminywa ulitoka kwa fujo na kisha ukasika mlio huo huo toka miguuni.

“Sikiliza bwana....nani sijui?” Ben alitaka kujua jina.

“We sema tu shida yako” Gaucho akadharau hata kujitambulisha.

“Nataka nitumie kituo chako kwa ajili ya mazoezi, na nikifanya mazoezi sihitaji mtu mwingine awe ndani.... nahitaji kuwa peke yangu siku nzima......”

“Hilo halitawezekana bwana......” Gaucho alimkatisha Ben.

“Ben” Ben alimsaidia Gaucho kukumbuka jina lake.

“ndio Bwana Ben, haiwezekani kufunga kituo kwa ajili yako, yaani niwashe umeme, viyoyozi vyote vifanye kazi na mashine zote ziwe zimewashwa halafu ukumbi wa mazoezi uwe wewe tu Ben, huo ni ukichaa mkubwa.......” Gaucho alitaka kuendelea lakini alikatizwa na Ben.

“Miye nitakulipa mara mbili ya hela ambayo huwa unakusanya kwa siku” Sauti ile nzito yenye mikwaruzo ilitamka na kmfanya Gaucho ashituke kidogo.

“Wewe unaweza kufanya hivyo?” Gaucho aliuliza kwa dhalau.

“Sema ni shilling ngapi?” Ben alisisitiza.

“shillingi laki moja na nusu kwa siku” Gaucho alisema huku akiwa anataka kuinuka maana alijua mwisho wa maongezi yao ulikuwa unafika.

“Basi mie nitakupa laki nne kwa kila siku nitakayokuja kwenye mazoezi” Ben alisema huku akijitengeneza kitini.



Hicho ndicho kilimfanya Gaucho awe tayari kutia pamba masikioni kila wateja wake walipomsihi awe anafungua kituo siku ya Jumamosi.



Gaucho hakuwa anaamini macho yake pale Ben alipokuwa akianza mazoezi. Alikuwa ni kama anayeangalia filamu za wapiganaji wa kichina. Ben alikuwa anabadilika kabisa na kuwa kiumbe mwingine, staili zake za maozezi ya kupigana, kunyanyua vitu vizito na utumiaji wa vifaa ndani ya ukumbi wa mazoezi vilimfanya amuogope sana na kufuta mtazamo aliokuwa nao juu ya Ben. Aliamini huyu Ben kama si Ninja basi ni Komandoo.



Ben mwenyewe alilidhika na hilo, alihitaji siku moja ya mazoezi badala ya kuulaza tu mwili wake nyumbani akiwa anashinda akiangalia filamu mbali mbali. Haikutokea tu Ben akaamua kuanza mazoezi, laah. Ujumbe aliopokea siku nne zilizopita toka kwa Harken Kalm ndio uliomfanya aende kwa Gaucho kuomba kituo cha mazoezi. Ile simu kuwa anatakiwa awamalize Jacob na Banzi ndio iliyomfanya Ben au Kiroboto aanze mazoezi hayo ya kuweka mwili safi.

********


Tofauti na Banzi ambaye aliyepiga simu kwa mzee Harken Kalm, kumtaka pesa, huyu yeye alikuwa amejaa tamaa ya mapenzi. Mapenzi yalimfanya Eve awe katika harakati za siri za kutaka kumtorosha mpelelezi Jacob Matata toka katika himaya hii ya John Kificho. Alikuwa ameshaangalia kila namna ya kufanya lakini hakuwa amefanikiwa. Alikuwa na hakika kuwa siku ambayo angefanikiwa kutoroka katika himaya hiyo akiwa na Jacob Matata basi angeanza maisha mapya na Jacob.

Ni tamaa ya kutaka kumtorosha Jacob ilimfanya atengeneze urafiki na komandoo Banzi. Maana jamaa huyo ndiye aliyemtorosha Regina toka katika jumba la mzee Harken Kalm na ndiye pia aliyemfuata Jacob Matata kumleta katika jumba hili la John Kificho. Kutokana na uwezo alionao katika kupigana, Komandoo Banzi anaheshimiwa sana na John Kificho.

“Mambo Eve?” Banzi alisabahi wakiwa katika sehemu ya kulia chakula ya John Kificho ndani ya jumba hili.

“Poa tua…… nani sijui?”

“Banzi, Komandoo Banzi!”

“Oooh Komandoo!!! Kwa maana ya kufuzu jeshini au wa sifa fulani, maana siku hizi kuna makomandoo wengi?”

“Komandoo wa vyote, maisha, jeshini, shida na……?” Banzi alisita kabla hajaendelea.

“Mbona hujamalizia?” Eve alisahili.

“wa mambo mengi kama nilivyosema!! Ha ha ha ha! Basi” alisema kwa kicheko huku akimuangalia Eve kifuani.

Kimya kilipita kila mmoja akionekana kutafakari yake. Kisha Eve alinyanyua uso wake na kumuangalia Banzi huku akitengeneza nywele zake.

“Huonekani kama wewe ni Komandoo wa chochote kati ya ulivyovitaja!” Eve alichokoza.

“Ungependa kuona alama gani ya ukomandoo?”

“ukomandoo wa jeshi ningetegemea kuona mtu sugu, wa kutisha na mwenye tabia za ajabu ajabu tu, lakini si kama wewe Banzi. Kadhalika ukomandoo wa shida huonekana hata usoni tu japo si rahisi kuelezea lakini huonekana” Eve alieleza kabla ya kuuliza.

“Kwani nini kinakufanya useme wewe ni komandoo wa shida?”

“Kwa sababu nadhani nimefuzu na naendelea kupambana nazo” Banzi alijibu.

“Mmmmmmh, unapambana nazo? Lakini kama umefuzu basi hazikupi shida na ni sehemu tu ya burudani zako!!!!”

“Aha ha ha ha ha tse tse!!!” Wote walicheka.

“Kila mtu ana shida ila kuna mambo yanayosababisha kuwe na utofauti katika kuzikabili.” Eve lisema kwa utulivu huku akimeza funda la juisi aliyokuwa akitelemshia chakula.

“Una maanisha nini?” Banzi alihoji.

“Kuna shida za kujitakia na kuna shida za kusababishiwa” Eve alifafanua.

“Mmmmh, naona u mwalimu mzuri!” Banzi alisifia.

“Kwa nionavyo mimi, shida za kujitakia ni nzuri kulikuo za kusababishiwa”

“Hebu elezea kidogo, maana sioni shida nzuri, shida zote ni mbaya.”

“Hapana kuna shida ambazo hufundisha na shida ambazo zinaua” Eve alizidi fafanua.

“Mmmmmm, naona muda wangu unanitaka kuwa mahali fulani, ila nimependa mada hii, natamani tungepata nafasi ya kuijadili zaidi, naomba pia tujaribu kutafakari tofauti ya shida na changamoto” Banzi alisema huku akinyanyuka. Huu ndio ukawa mwanzo wa mazoea ya Eve na Banzi.



Siku nyingine wakiwa katika mijadala yao kama hii Eve alileta mambo mapya.

“Banzi, hivi una umri gani rafiki yangu?”

“Duuuh, leo naona una mada nyingine mpya, mwezi wa kenda natimiza miaka 39!”

“Hongera sana kwa umri na unaonekana unatunza mwili wako vizuri!”

“Asante, japo nadhani nastahili pole au kupewa tahadhari”

“Kwa nini Banzi?”

“Umri wangu na mambo yangu haviendani?”

“Sijakuelewa”

“Jana nilikuwa naongea na mama yangu ambaye yuko taabani hospitali, alikuwa analalamikia kitendo cha mimi kutokuwa na mke wala watoto, anasema naishi kama ndege”

“Lakini hilo si suala la kukulaumu sana, kwani inawezekana unakamilisha mipango yako ili ufanye hivyo!” Eve alijibu kwa kusisitiza.

“Ingekuwa hivyo nadhani mama asingekuwa ananisema, lakini naweza sema mie ni kama mtu ambaye naishi tu na kutimiza malengo ya watu wengine kama John Kificho” Hapo ndipo mjadala mkali ukazuka wa jinsi watu wengine wanyotumiwa na taaluma za kufikisha malengo ya watu wengine ilhali wao wakiachwa kuwa wahanga wa gharama za mafanikio ya hao watu. Ni mjadala huu ndio uliowafikisha kugundua kuwa Eve na Banzi walikuwa na shida mbili tofauti. Wakati Banzi akiwa na shida ya fedha za kujenga maisha yake, Eve yeye hakuwa na shida ya fedha bali mpenzi. Walivyojiangalia, hakuna ambaye angeweza kuwa jibu la mwenzie, ila jambo moja walikubaliana baada ya mjadala mrefu, nalo ni kuwa kila mtu ana ufunguo wa kuelekea kutatua shida ya mwenzie.

Eve alikuwa na jukumu la kumpa Banzi wazo la kumsaidia kupiga bingo, ili hali Banzi alikuwa na kazi ya kutumia ukomandoo wake kufanikiwa kutekeleza wazo la Eve na kumsaidia Eve.

Eve alikuwa na shida ya kumpata na kummiliki Jacob Matata ilhali komandoo Banzi alitaka kutumia hali iliyopo kujinufaisha kwa kupata fedha nyingi.

“Sikiliza Banzi, mzee Harken Kalm anamtaka Jacob na Regina kwa udi na uvumba, John Kificho anakutegemea katika ulinzi na kutekeleza mipango yake ya siri. John Kificho anakulipa fedha kidogo sana tofauti na kazi unayomfanyia. Fanya kitu! Ila hakikisha nampata Jacob Matata akiwa hai”

“Huo ni mpango mgumu sana ila naona unamanufaa, ngoja nijaribu kubuni vitendo vyake nione utafanyaje kazi” Banzi alisema huku akikuna kichwa kwa tafakari.



* * *



Banzi ni Komandoo kama alivyomuambi Eve, si Komandoo wa kujiita bali ni wa kutunukiwa baada ya kufuzu mafunzo ya juu kabisa yanayomfanya mtu kuitwa jina hilo. Amewahi kufanya kazi nyingi za hatari, japo nyingi zikiwa ni nje ya nchi kama vile Holland, Ugiriki na Cambodia. Kwa sasa hakuna kitu anahitaji zaidi ya pesa, ndo maana serikali ilipomtaka baada ya kuhitimu mafunzo alikataa na kusema atakuwa anafanya kazi binafsi.



Ili kutekeleza mawazo aliyokuwa amepewa na Eve, simu ya kwanza kupiga ilielekea ofisini kwa mzee Harken Kalm, ikimtaka pesa ili apate taarifa za walipo Jacob Matata na Regina. Ni simu hiyo ndio ilimfanya mzee Harken Kalm atume vijana wake watafute wapi alipo mtu aliyepiga hiyo simu bila mafanikio.



Simu ya pili kupiga iliingia moja kwa moja ofisini kwa mkurugenzi wa ofisi fukuzi, Bi. Anita.

“Ennhe niambie habari uliyonayo?” Bi Anita alimuuliza Banzi.

“Ni kuhusu rafiki yangu Jacob Matata, najua alipo, kama hutajari napenda kuwa kwenye oparesheni itakayokwenda kumchukua”

“Banzi! Umesahau kanuni namba nne?”

“Samahani mama si unajua uzee. Kwa hiyo?”

“Cover 9” Alijibu Bi. Anita.

“Assurance?” Banzi alisema.

“asilimia mia!”

Jibu la mwisho ndilo lilimfanya Komandoo Banzi aende posta saa nane na dakika saba usiku ili kuangalia sanduku lake la barua kwa maelekezo toka ofisi fukuzi. Na kweli alikuta karatasi yenye mistari minne tu. “BANZI FANYA MNADA KWA AJILI YA KUFILISI MALI YA MDAIWA JACOB, BANKI ITALIPA SHS 716”. Komandoo Banzi alikunja hiyo karatasi na kuiweka mfukoni. Akaangaza angaza kama anayetafuta sanduku jingine la barua, alipoona namba 716 alifungua kwa kutumia funguo zake malaya na kuweka karatasi nyingine tofauti na ile aliyokuwa amechukua toka sanduku lake.

Aliondoka haraka eneo hilo la kuchukulia barua na kurudi alipokuwa ameegesha gari lake. Aliingia ndani ya gari na kutia moto, lakini gari haikuwaka. Wakati anataka kutafuta nini kimetokea alipigwa na kitu kama nyundo ya kilo tano kichwani akapoteza fahamu papo hapo.

Itaendelea
 
HEKAHEKA - 19

Kitendo cha Jacob kushindwa kuongea kilimsikitisha zaidi Eve. Hivyo kwa haraka alirudisha vile vifaa masikioni mwa Jacob, kisha akarudi alipokuwa awali. Dakika chache baadaye kitu kama kengele kilitoa mlio. Eve akampungia mkono Jacob na kutokomea nje. Hapo hakuonekana mtu yeyote ndani ya chumba hicho hadi asubuhi siku iliyofuata. Ilikuwa ni siku ya sita kwa mpelelezi Jacob Matata kuwa katika kifungo hiki cha kutisha. Hakujua watu hawa walikuwa na lengo gani kwake, japo alianza kuhisi mauti.



* * *



Ilikuwa ni siku ya nne yenye mashaka na uchungu kwa mkuu huyu wa kitengo fukuzi. Mpaka wakati huu vijana wake walikuwa wameshafanya kila liwezekanalo kuhakikisha kuwa wanajua alipo mpelelezi mwenzao Jacob Matata. Lakini mpaka inafika asubuhi hii hakuna hata fununu walizokuwanazo juu ya Jacob. Kutokana na maiti walizozikuta nyumbani kwa Jacob siku Jacob alipotoweka, ilikuwa wazi vichwani mwao kuwa Jacob hakuwa amechukuliwa kwa heri. Ilikuwa hakika kuwa kabla ya kuchukuliwa yalikuwa yametokea mapambano makali yaliyopelekea kuuawa kwa watu hao. Jacob yuko hai au maiti? Kama yuko hai, atakuwa sehemu gani? Maswali haya yamekuwa yakijirudia rudia kichwani kwa Bi. Anita mkuu wa Ofisi Fukuzi.

Siku ile kabla ya kutoweka kwa Jacob, ofisi hiyo ilikuwa imeandaa operesheni kubwa ya kwenda kwenye jumba la mzee Harken Kalm. Operesheni hiyo ingeongozwa na Jacob Matata mwenyewe. Lakini kitendo cha kutoweka kwake ilikuwa ni wazi kuwa wasingeweza tena kwenda, kwani ni Jacob aliyekuwa akipajua mahali walipokusudia kwenda. Hivyo ofisi yote ilikuwa imekumbwa na ubaridi wa kutisha.

Mpaka kufikia siku hii, Bi. Anita alikuwa ameshapiga simu kila sehemu aliyodhani kungekuwa na tetesi. Lakini Jambo moja lilikuwa likija kwa mbali- Jacob yuko hai japo yawezekana kuwa katika shida.



* * *



Kila mmoja kwa lengo lake alikuwa katika jitihada zake. John Kificho alikuwa amekufa katika kumpenda msichana Regina, hivyo alikuwa katika jitihada za kuuteka moyo wa msichana huyo. Kwa sababu asizozijua, mpelelezi Jacob Matata alijikuta mikononi mwa John Kificho. Hakuwa anamjua Kificho lakini alikuwa katika hali mbaya na alitakiwa kufanya kitu ili kujinasua katika mikono hiyo hatari.

Regina alishatambua nia ya Kificho kumtaka, lakini hakujua kuwa Kificho hakuwa na lengo la kumsaidia Jacob Matata. Hivyo alianza kumuamini Kificho na kumchukulia kama mtu mwenye huruma ajabu. Pamoja na hayo, moyo wa Regina ulikuwa katika mapenzi mazito kwa mpelelezi Jacob Matata.

Mzee Harken Kalm kwa upande wake alikuwa amechanganyikiwa, kutoweka kwa Regina na kutoonekana kwa Jacob Matata aliona kuwa ni hatari kwa himaya yake. Hivyo alikuwa akifanya kila njia kuhakikisha anampata Jacob na Regina, ambao aliamini kuwa walikuwa na siri zake.

Bi. Anita mkuu wa kikosi cha siri cha ofisi fukuzi, ameamua kuacha ofisi na kuingia uwanja wa mapambano kuongoza kundi la vijana wake kuhakikisha wanampata Jacob na kusambaratisha himaya ya mzee Harken Kalm. Alikuwa makini kufuatilia na kutaka kujua Jacob yuko wapi, kwani aliamini kuwa kwa vyovyote Jacob yuko hai.



Tamaa. Ni tamaa iliyosababisha mzee Harken Kalm, apokee simu hii. Alikuwa ndani ya chumba maalum ndani ya himaya yake, akisubiri taarifa yoyote nzuri juu ya msako uliokuwa ukiendelea. Tangu kutoweka kwa Regina na kutoonekana kwa Jacob Matata, mzee huyu amekuwa hana amani huku akijiona hayuko salama kabisa. Kikosi cha Tai, kikosi cha Paka na kikosi cha Mbwa weusi vyote vilikuwa vimesambaa katika maeneo mbali mbali kuhakikisha Jacob na Regina wanapatikana.

Simu hiyo haikulia muda mrefu kabla mzee Harken Kalm hajainyanyua na kunong’ona

“Leta habari” Alisema hivyo akiwa na hakika kuwa huyu alikuwa ni mmoja wa vijana wake.

“Shikamoo mzee!” Ulisema upande wa pili. Mzee Harken Kalm hakuitikia, badala yake akasema.

“Siko kwa hilo, labda unalingine nikusaidie!” Kadhalika sauti ya mzee Harken Kalm ilitoka katika hali ya kunong’ona.

“Sihitaji msaada wako ila nipo kukupa msaada!” Ulijibu upande wa pili katika sauti nzito, tulivu ya raha.

“Shiit, unaweza nisaidia nini wewe? Kwanza umepataje hii namba?” Mzee Harken Kalm aliongea tena kwa kunong’ona. Aliongea hivyo huku akiwa anajiandaa kuweka simu chini. Hakuwa amependezwa na maongezi ya mtu huyu asiye mfahamu.

“Ni juu ya Jacob na Regina!!” Kwa ile sauti nzito, tulivu ya raha mtu wa upande wa pili alisema. Ilikuwa wazi kuwa mtu huyu alikuwa akisema maneno hayo kwa raha mno.

“Wamefanyaje?” Mzee Harken Kalm aliukumbatia zaidi mkono wa simu, huku ngozi yake ikibadilika na kuwa nyekundu.

“Najua walipo!” Ulisema upande wa pili.

“wako wapi?” Mzee Harken Kalm alinong’ona zaidi kana kwamba alikuwa na mtu chumbani humo.

“umeulizia hatua ya mwisho, kuna hatua kabla ya hilo swali” ulisema upande wa pili kwa sauti ya pozi.

“Una hakika na usemayo?” Harken Kalm alinong’ona

“asili mia moja!”

“hatua gani sijauliza”

“Pesa”

“Siyo pesa, nitakupa fedha. Sema uko wapi na nikupateje?” Mzee Harken Kalm aliongea huku akiminya kitufe fulani. Mara walikuja vijana wawili, walisimama wakisubiri amri zaidi toka kwa mzee Harken Kalm.

“Sawa, kesho asubuhi nitaenda benki kuangalia kama utakuwa umeniwekea hizo pesa au fedha kama unavyoita. Nikizikuta nitawaelekeza mahali mtakapo wachukua watu wenu” Ulisema upande wa pili, kisha mtu huyo alitaja namba za akaunti yake ya benki kisha akakata simu.

Simu ilipokatwa, mzee Harken Kalm aliwageukia vijana wake, kisha akanong’ona “Nataka kujua hii simu imepigwa kutoka wapi na habari kamili za mpigaji” alipomaliza alibonyeza kitufe fulani akapotelea ardhini. Jitihada zilifanyika kuhakikisha mpigaji wa simu hiyo anajulikana. Lakini masaa kadhaa yalikatika bila mafanikio, ilikuwa ni ujumbe tosha kwa mzee Harken Kalm kuwa mpigaji wa simu alikuwa mtu aliyejiandaa na si vinginevyo.



Taarifa kuwa vijana wake walishindwa kujua sehemu aliyokuwepo mtu aliyepiga simu na kutaka ampe pesa ili amuambie Jacob na Regina walipo, zilimfanya Mzee Harken Kalm apate hamu ya kusikiliza tena sauti ya huyo mtu. Akiwa kwenye chumba chake cha siri kilicho chini ya ardhi, alibonyeza kitufe fulani kilichokuwa pembeni ya redio yake, mara sauti za mazungumzo waliyofanya na huyo mtu kwenye simu zilitokea tena. Alisikiliza kwa makini tena na tena. Kilichomfanya arudie kusikiliza ni sauti ya mtu huyu aliyempigia, haikuwa ngeni masikioni kwa Harken Kalm.

"shiiiit, Banzi!!!!!!!!” Alisonya kwa hasira.

"Mshenzi huyu bado yuko hai?” alijisemea kwa mshangao. Mzee Harken Kalm baada ya hapo aliwasha Laptop yake. Humo alifunua mafaili kadhaa kisha akatulia huku akisoma taarifa fulani. Alichukua kijtabu chake kidogo akaandika vitu fulani kisha uso wake ukaonesha tabasamu fulani. akasimama na kutoka katika chumba hicho. Alipita vyumba kadhaa ambavyo vyote vilikuwa sehemu ya ardhini ambayo ni mzee Harken Kalm pekee aliyekuwa anajua namna ya kuingia huko. Alitembea hivyo hadi alipofika kwenye mlango uliokuwa umeandikwa ‘Contact the world’ hapo alibonyeza namba fulani mlangoni hapo na mlango ukafunguka. Chumba hiki kilikuwa kipana angavu na kilichosheheni vifaa mbali mbali vya mawasiliano. Hapo Harken Kalm, aliwasiliana na huyu akaacha, akampigia yule, akakunja uso akakata simu, akamtumia ujumbe huyu, ujumbe ulipojibiwa akatabasamu, akapiga na kupiga, akaandika ujumbe na kusoma mwisho akaonekana kuchoka...ni wakati anaelekea kutaka kutoka chumbani humo ndipo akawa kama aliyekumbuka kitu. Akachukua mashine fulani na kuingiza namba kadhaa. Mashine ilitoa milio...Ngriiiiiih ngriiiiii ngriiiiii, kama mara sita hivi.

“Old friend!!!” Harken Kalm alisema kwa sauti chovu iliyochanganyika na matumaini kwa mbali.

“Ben, umejichimbia wapi?” Harken Kalm alihoji baada ya upande wa pili kuwa kimya

“Najipa nafasi Harken Kalm!” Upande wa pili ulijibu.

“Nahitaji huduma yako Ben kama uko sawa!”

“Unajua kuwa wewe siwezi kukukatalia” Upande wa pili ulijibu kasha ukaongeza.

“Ndio Kalm nikusaidie nini?”

“Unaweza jua Banzi yuko wapi kwa sasa?” Kalm aliuliza.

“Kuna sehemu fulani anakula bata” Upande wa pili ulijibu.

"Sikiliza Ben, nilikuambia kuwa kuna kazi nataka nikupe, sasa nakupa kazi, alipo Banzi ndipo alipo Jacob Matata na Binti mmoja aitwaye Regina. Sasa nakupa kazi ya kuwamaliza wote watatu, utatumia njia gani na namna gani hiyo sitaki kujua, nataka ukinipigia simu uniambie kuwa kazi tayari nami nitafanya mambo yangu” Harken Kalm alisema huku sauti yake ikiwa na mchanganyiko wa uchungu na hasira kama ladha ya maziwa ya mgando yaliyo haribika.

“Hiyo kazi ni ngumu sana, unajua hapo unaniambia nifanye kazi ya kuwamaliza makomandoo wawili, unajua fika uwezo wa Banzi na Jacob, najua fika kwa sasa hawako pamoja, kwa vyovyote ilivyo Jacob atakuwa mateka wa Banzi. Wewe mzoefu wa mambo haya, bila shaka unajua itakuwa hatari kiasi gani, hivyo hilo lazima ulizingatie kwenye malipo la sivyo nikimaliza kuwaua wao utafuata wewe” Sauti ya upande wa pili iliongea, iliongea kwa kuunguruma na mikwaruzo kama kawaida yake.

“Ben mimi na wewe hatujakutana barabarani bana” Harken Kalm alisema.

“Yeah, nadhani unajua ni kwa nini nafanya hivi, sihitaji pesa Harken Kalm, ila nahitaji kumuenzi baba yako. He was a good man” Upande wa pili ulisema.

Waliagana simu ikakatwa.

“Dawa ya moto ni moto, si maji, Ben ataumaliza mchezo” Harken Kalm alijisemea huku uso wake ukipata matumaini.



* * *



Baada ya mazungumzo na Harken Kalm, mwili wa Ben ulisisimka, alitabasamu, tabasamu baridi, picha ya Jacob Matata na Banzi zilimjia kichwani, aliwaangalia kila mmoja kwa zamu, kisha akaelekea kwenye friji na kutoa karoti moja akaanza kutafuna huku anazunguka sebuleni kwake.



Ben alikuwa Komandoo, komandoo kamili kwa maana ya kuhitimu. Mafunzo ya mtaani alipokuwa akingali mdogo, baadae alipojiunga na jeshi baada ya kufeli kidato cha nne, kisha kuwa miongoni mwa vijana kumi na tano waliochukuliwa kwenda Cuba kwa mafunzo baada ya urafiki wa Nyerere na Castro kuwa umekolea. Kwa vile alihitimu kwa kiwango cha kutisha, mwalimu wake wa kichina alimfanyia mpango wa kujiunga na shirika moja la siri nchini china ambalo lilikwa likitoa huduma ya uuaji ‘assassination service’. Alijiunga na shirika hilo kwa siri na kuwa miongoni mwa wauaji wa kuogopwa japo sura yake na jina lake halisi halikuwa likijulika. Watu wengi duniani hasa mashirika ya kijasusi na kigaidi yalimjua kwa jina moja tu – Kiroboto.



Mwaka 1995 alipata ujumbe wa siri kuwa alihitajika kwenda Siera Lione ambako mtu mmoja maarufu alikuwa katika harakati za kuuchukua urais wa nchi hiyo. Japo mtu huyo alikuwa mwanajeshi, lakini alitaka kuwa na mlinzi wake ‘special’ mbali na wanajeshi. Hivyo alikubali kulindwa na wanajeshi, lakini kwa sababu ambazo zilikubaliwa na waliokuwa wakitaka kumuweka madarakani, ilibidi atafutwe mtu special. Majina mengi yalipendekezwa ndani na nje ya bara la Afrika, lakini jina moja tu lilipita, nalo ni Kiroboto.



Moja kati ya masharti aliyopewa Kiroboto ili kupata kazi hiyo, ilikuwa ni kuua wazazi wake wote ili atakapokuwa katika kutimiza majukumu yake kitu muhimu kwake iwe ni huyo Rais mtarajiwa tu. Kwa Ben au Kiroboto kama alivyofahamika, mambo mawili yalikuwa muhimu sana kwake, pesa na wanawake. Alipenda pesa kama roho yake na pia alipenda wanawake kama mwili wake mwenyewe. Hivyo kwa kuzingatia kiasi cha pesa alichokuwa ameahidiwa kwa kazi ile, haikumpa shida kuja Tanzania na kuwamaliza wazazi wake wote wawili kwa risasi. Baada ya hapo akarejea Siera Lione na kuianza kazi yake ya kuulinda uhai wa aliyekuwa Rais mtarajiwa wa nchi hiyo wakati huo. Kweli alikuwa Kiroboto, kwani hadi mkataba wake ulipokwisha kila mmoja alinyoosha mikono kuwa jamaa alikuwa kiroboto. Cha mwisho kilichompa umaarufu zaidi duniani, ni pale mtu aliyemlinda kwa miaka mitano alipoona ameshachukua madaraka ya Urais, kwa siri alisitisha mkataba na Kiroboto. Kwa vile jeshi lilikuwa halimpendi na waliona tayari ameshakuwa na siri nyingi za nchi hiyo, hivyo wakaamuru auawe. Kikatumwa kikosi cha watu ishirini kufanya kazi hiyo. Ndani ya siku mbili watu wote hao waliuawa, tena si kwa risasi bali kwa mkono wa Kiroboto huku yeye mwenyewe akifanikiwa kuondoka nchini humo na kiasi kikubwa cha fedha na almasi ambazo alipewa kama zawadi na Rais aliyekuwa madarakani.



Kwa sasa Ben si mtu mwenye shida ya fedha, ila kuna kitu kinausumbua moyo wake, nacho ni kisasi, wala hakuwahi kuchukua kazi nyingine baada ya kupata utajiri ule toka Sierra Lione. Fununu za kuwa Harken Kalm ndio damu pekee iliyobaki toka kwa kingozi yule wa Sierra Lione zilimfikia Ben. Pia hakuchelewa kujua kuwa Harken Kalm alikuwa akifanya biashara haramu, lakini alijiapiza kumlinda kwa namna yoyote ile. Aliona hiyo ndio ingekuwa njia pekee ya yeye kulipa fadhila kwa kiongozi yule aliyempa utajiri alio nao sasa. Kwa siri sana Ben alijitambulisha kwa Harken Kalm, na kumwambia kuwa yupo kama atamuhitaji. Walitambuana. Hivyo simu hii ya kuomba msaada toka kwa Harken Kalm aliichukulia kwa uzito unaotakiwa. Alitamani kujikumbushia michezo yake, ila damu ilimsisimka zaidi alipotambua kuwa mchezo huu utamkutanisha na Jacob Matata na Komandoo Banzi. Ben and Jacob walikuwa miongoni mwa wale vijana waliokwenda Cuba. Wakati yeye alitoroshwa baada ya mafunzo kuisha, Jacob yeye alirejea Tanzania. Si kwamba Ben alikuwa mzuri zaidi ya Jacob, ila kilichomfanya mwalimu wa kichina amchukue Ben ni kwa vile alikuwa katili sana. Hivyo aliona kazi ya kuwa muuaji maalum wa kuajiriwa ingemfaa zaidi. Jacob alikuwa vizuri zaidi kimafunzo ila alikuwa na utu hivyo hakufaa kupelekwa kuwa muuaji.



Kila mmoja alishasikia sifa za mwenzake, Ben alijua kuwa Jacob Matata ni mpelelezi asiyeshindwa, na Jacob alishazisikia sifa za Kiroboto hasa ile habari ya namna alivyotoroka Sierra Lione ilimsisimua sana.



* * *



Huyu yeye anaitwa Gaucho, anamiliki kituo cha kufanyia mazoezi - Gym, maeneo ya Kimara Baruti. Leo hii hakufungua kituo chake. Si kwamba hakupenda kufungua au hakuwa na wateja, la hasha, alikuwa na wateja wengi, na wengi walishampigia kelele kwa nini huwa hafungui siku za Jumamosi. Jumamosi ingekuwa ni siku nzuri kwake kufungua kwa vile watu wengi ndio huwa na nafasi ya kufanya mazoezi, lakini asingeweza kufanya hivyo kwa sababu ya mtu mmoja tu, ndio mtu mmoja, mteja mmoja tu ndiye ambaye alisababisha Gaucho asiwe anafungua kituo chake siku ya Jumamosi.



Mteja huyo alijitambulisha kwa Gaucho kwa jina moja tu, Ben. Siku Ben amekuja ofisini kwa Gaucho hapo kwenye kituo cha mazoezi, alionekana kama mtu aliyepotea njia. Muonekano wake - mavazi, macho, usafi na uongeaji wake vilimfanya Gaucho atake kumuondoa haraka eneo hilo la ofisi yake. Walipoanza maongezi kidogo hali ikawa tofauti.

“Naitwa Ben.....” Sauti nzito iliyo na mikwaruzo ilisema huku macho makali yakiusanifu uso wa Gaucho.

“Sema nikusaidie nini” Gaucho alijibu kwa kukereka kidogo.

“Nahitaji sehemu ya kufanyia mazoezi.....”

“Mazoezi gani unayotaka kufanya wewe, ..na, ..na....unadhani hii sehemu ni muafaka kwako?”

Kabla ya kujibu, Ben aliminya vidole vyake, ule mlio wa vidole kuminywa ulitoka kwa fujo na kisha ukasika mlio huo huo toka miguuni.

“Sikiliza bwana....nani sijui?” Ben alitaka kujua jina.

“We sema tu shida yako” Gaucho akadharau hata kujitambulisha.

“Nataka nitumie kituo chako kwa ajili ya mazoezi, na nikifanya mazoezi sihitaji mtu mwingine awe ndani.... nahitaji kuwa peke yangu siku nzima......”

“Hilo halitawezekana bwana......” Gaucho alimkatisha Ben.

“Ben” Ben alimsaidia Gaucho kukumbuka jina lake.

“ndio Bwana Ben, haiwezekani kufunga kituo kwa ajili yako, yaani niwashe umeme, viyoyozi vyote vifanye kazi na mashine zote ziwe zimewashwa halafu ukumbi wa mazoezi uwe wewe tu Ben, huo ni ukichaa mkubwa.......” Gaucho alitaka kuendelea lakini alikatizwa na Ben.

“Miye nitakulipa mara mbili ya hela ambayo huwa unakusanya kwa siku” Sauti ile nzito yenye mikwaruzo ilitamka na kmfanya Gaucho ashituke kidogo.

“Wewe unaweza kufanya hivyo?” Gaucho aliuliza kwa dhalau.

“Sema ni shilling ngapi?” Ben alisisitiza.

“shillingi laki moja na nusu kwa siku” Gaucho alisema huku akiwa anataka kuinuka maana alijua mwisho wa maongezi yao ulikuwa unafika.

“Basi mie nitakupa laki nne kwa kila siku nitakayokuja kwenye mazoezi” Ben alisema huku akijitengeneza kitini.



Hicho ndicho kilimfanya Gaucho awe tayari kutia pamba masikioni kila wateja wake walipomsihi awe anafungua kituo siku ya Jumamosi.



Gaucho hakuwa anaamini macho yake pale Ben alipokuwa akianza mazoezi. Alikuwa ni kama anayeangalia filamu za wapiganaji wa kichina. Ben alikuwa anabadilika kabisa na kuwa kiumbe mwingine, staili zake za maozezi ya kupigana, kunyanyua vitu vizito na utumiaji wa vifaa ndani ya ukumbi wa mazoezi vilimfanya amuogope sana na kufuta mtazamo aliokuwa nao juu ya Ben. Aliamini huyu Ben kama si Ninja basi ni Komandoo.



Ben mwenyewe alilidhika na hilo, alihitaji siku moja ya mazoezi badala ya kuulaza tu mwili wake nyumbani akiwa anashinda akiangalia filamu mbali mbali. Haikutokea tu Ben akaamua kuanza mazoezi, laah. Ujumbe aliopokea siku nne zilizopita toka kwa Harken Kalm ndio uliomfanya aende kwa Gaucho kuomba kituo cha mazoezi. Ile simu kuwa anatakiwa awamalize Jacob na Banzi ndio iliyomfanya Ben au Kiroboto aanze mazoezi hayo ya kuweka mwili safi.

********


Tofauti na Banzi ambaye aliyepiga simu kwa mzee Harken Kalm, kumtaka pesa, huyu yeye alikuwa amejaa tamaa ya mapenzi. Mapenzi yalimfanya Eve awe katika harakati za siri za kutaka kumtorosha mpelelezi Jacob Matata toka katika himaya hii ya John Kificho. Alikuwa ameshaangalia kila namna ya kufanya lakini hakuwa amefanikiwa. Alikuwa na hakika kuwa siku ambayo angefanikiwa kutoroka katika himaya hiyo akiwa na Jacob Matata basi angeanza maisha mapya na Jacob.

Ni tamaa ya kutaka kumtorosha Jacob ilimfanya atengeneze urafiki na komandoo Banzi. Maana jamaa huyo ndiye aliyemtorosha Regina toka katika jumba la mzee Harken Kalm na ndiye pia aliyemfuata Jacob Matata kumleta katika jumba hili la John Kificho. Kutokana na uwezo alionao katika kupigana, Komandoo Banzi anaheshimiwa sana na John Kificho.

“Mambo Eve?” Banzi alisabahi wakiwa katika sehemu ya kulia chakula ya John Kificho ndani ya jumba hili.

“Poa tua…… nani sijui?”

“Banzi, Komandoo Banzi!”

“Oooh Komandoo!!! Kwa maana ya kufuzu jeshini au wa sifa fulani, maana siku hizi kuna makomandoo wengi?”

“Komandoo wa vyote, maisha, jeshini, shida na……?” Banzi alisita kabla hajaendelea.

“Mbona hujamalizia?” Eve alisahili.

“wa mambo mengi kama nilivyosema!! Ha ha ha ha! Basi” alisema kwa kicheko huku akimuangalia Eve kifuani.

Kimya kilipita kila mmoja akionekana kutafakari yake. Kisha Eve alinyanyua uso wake na kumuangalia Banzi huku akitengeneza nywele zake.

“Huonekani kama wewe ni Komandoo wa chochote kati ya ulivyovitaja!” Eve alichokoza.

“Ungependa kuona alama gani ya ukomandoo?”

“ukomandoo wa jeshi ningetegemea kuona mtu sugu, wa kutisha na mwenye tabia za ajabu ajabu tu, lakini si kama wewe Banzi. Kadhalika ukomandoo wa shida huonekana hata usoni tu japo si rahisi kuelezea lakini huonekana” Eve alieleza kabla ya kuuliza.

“Kwani nini kinakufanya useme wewe ni komandoo wa shida?”

“Kwa sababu nadhani nimefuzu na naendelea kupambana nazo” Banzi alijibu.

“Mmmmmmh, unapambana nazo? Lakini kama umefuzu basi hazikupi shida na ni sehemu tu ya burudani zako!!!!”

“Aha ha ha ha ha tse tse!!!” Wote walicheka.

“Kila mtu ana shida ila kuna mambo yanayosababisha kuwe na utofauti katika kuzikabili.” Eve lisema kwa utulivu huku akimeza funda la juisi aliyokuwa akitelemshia chakula.

“Una maanisha nini?” Banzi alihoji.

“Kuna shida za kujitakia na kuna shida za kusababishiwa” Eve alifafanua.

“Mmmmh, naona u mwalimu mzuri!” Banzi alisifia.

“Kwa nionavyo mimi, shida za kujitakia ni nzuri kulikuo za kusababishiwa”

“Hebu elezea kidogo, maana sioni shida nzuri, shida zote ni mbaya.”

“Hapana kuna shida ambazo hufundisha na shida ambazo zinaua” Eve alizidi fafanua.

“Mmmmmm, naona muda wangu unanitaka kuwa mahali fulani, ila nimependa mada hii, natamani tungepata nafasi ya kuijadili zaidi, naomba pia tujaribu kutafakari tofauti ya shida na changamoto” Banzi alisema huku akinyanyuka. Huu ndio ukawa mwanzo wa mazoea ya Eve na Banzi.



Siku nyingine wakiwa katika mijadala yao kama hii Eve alileta mambo mapya.

“Banzi, hivi una umri gani rafiki yangu?”

“Duuuh, leo naona una mada nyingine mpya, mwezi wa kenda natimiza miaka 39!”

“Hongera sana kwa umri na unaonekana unatunza mwili wako vizuri!”

“Asante, japo nadhani nastahili pole au kupewa tahadhari”

“Kwa nini Banzi?”

“Umri wangu na mambo yangu haviendani?”

“Sijakuelewa”

“Jana nilikuwa naongea na mama yangu ambaye yuko taabani hospitali, alikuwa analalamikia kitendo cha mimi kutokuwa na mke wala watoto, anasema naishi kama ndege”

“Lakini hilo si suala la kukulaumu sana, kwani inawezekana unakamilisha mipango yako ili ufanye hivyo!” Eve alijibu kwa kusisitiza.

“Ingekuwa hivyo nadhani mama asingekuwa ananisema, lakini naweza sema mie ni kama mtu ambaye naishi tu na kutimiza malengo ya watu wengine kama John Kificho” Hapo ndipo mjadala mkali ukazuka wa jinsi watu wengine wanyotumiwa na taaluma za kufikisha malengo ya watu wengine ilhali wao wakiachwa kuwa wahanga wa gharama za mafanikio ya hao watu. Ni mjadala huu ndio uliowafikisha kugundua kuwa Eve na Banzi walikuwa na shida mbili tofauti. Wakati Banzi akiwa na shida ya fedha za kujenga maisha yake, Eve yeye hakuwa na shida ya fedha bali mpenzi. Walivyojiangalia, hakuna ambaye angeweza kuwa jibu la mwenzie, ila jambo moja walikubaliana baada ya mjadala mrefu, nalo ni kuwa kila mtu ana ufunguo wa kuelekea kutatua shida ya mwenzie.

Eve alikuwa na jukumu la kumpa Banzi wazo la kumsaidia kupiga bingo, ili hali Banzi alikuwa na kazi ya kutumia ukomandoo wake kufanikiwa kutekeleza wazo la Eve na kumsaidia Eve.

Eve alikuwa na shida ya kumpata na kummiliki Jacob Matata ilhali komandoo Banzi alitaka kutumia hali iliyopo kujinufaisha kwa kupata fedha nyingi.

“Sikiliza Banzi, mzee Harken Kalm anamtaka Jacob na Regina kwa udi na uvumba, John Kificho anakutegemea katika ulinzi na kutekeleza mipango yake ya siri. John Kificho anakulipa fedha kidogo sana tofauti na kazi unayomfanyia. Fanya kitu! Ila hakikisha nampata Jacob Matata akiwa hai”

“Huo ni mpango mgumu sana ila naona unamanufaa, ngoja nijaribu kubuni vitendo vyake nione utafanyaje kazi” Banzi alisema huku akikuna kichwa kwa tafakari.



* * *



Banzi ni Komandoo kama alivyomuambi Eve, si Komandoo wa kujiita bali ni wa kutunukiwa baada ya kufuzu mafunzo ya juu kabisa yanayomfanya mtu kuitwa jina hilo. Amewahi kufanya kazi nyingi za hatari, japo nyingi zikiwa ni nje ya nchi kama vile Holland, Ugiriki na Cambodia. Kwa sasa hakuna kitu anahitaji zaidi ya pesa, ndo maana serikali ilipomtaka baada ya kuhitimu mafunzo alikataa na kusema atakuwa anafanya kazi binafsi.



Ili kutekeleza mawazo aliyokuwa amepewa na Eve, simu ya kwanza kupiga ilielekea ofisini kwa mzee Harken Kalm, ikimtaka pesa ili apate taarifa za walipo Jacob Matata na Regina. Ni simu hiyo ndio ilimfanya mzee Harken Kalm atume vijana wake watafute wapi alipo mtu aliyepiga hiyo simu bila mafanikio.



Simu ya pili kupiga iliingia moja kwa moja ofisini kwa mkurugenzi wa ofisi fukuzi, Bi. Anita.

“Ennhe niambie habari uliyonayo?” Bi Anita alimuuliza Banzi.

“Ni kuhusu rafiki yangu Jacob Matata, najua alipo, kama hutajari napenda kuwa kwenye oparesheni itakayokwenda kumchukua”

“Banzi! Umesahau kanuni namba nne?”

“Samahani mama si unajua uzee. Kwa hiyo?”

“Cover 9” Alijibu Bi. Anita.

“Assurance?” Banzi alisema.

“asilimia mia!”

Jibu la mwisho ndilo lilimfanya Komandoo Banzi aende posta saa nane na dakika saba usiku ili kuangalia sanduku lake la barua kwa maelekezo toka ofisi fukuzi. Na kweli alikuta karatasi yenye mistari minne tu. “BANZI FANYA MNADA KWA AJILI YA KUFILISI MALI YA MDAIWA JACOB, BANKI ITALIPA SHS 716”. Komandoo Banzi alikunja hiyo karatasi na kuiweka mfukoni. Akaangaza angaza kama anayetafuta sanduku jingine la barua, alipoona namba 716 alifungua kwa kutumia funguo zake malaya na kuweka karatasi nyingine tofauti na ile aliyokuwa amechukua toka sanduku lake.

Aliondoka haraka eneo hilo la kuchukulia barua na kurudi alipokuwa ameegesha gari lake. Aliingia ndani ya gari na kutia moto, lakini gari haikuwaka. Wakati anataka kutafuta nini kimetokea alipigwa na kitu kama nyundo ya kilo tano kichwani akapoteza fahamu papo hapo.

Itaendelea
Shukran mkuu mtzmweusi
 
Mkuu unenisababishia alosto kila muda natandika K-VANT nakusubilia wewe huyu kiroboto atakua sir nature !na na song la jinsi kijana
 
Mimi naomba kupatiwa hii riwaya kamili kwa whatsapp. Nitachangia ndugu zangu nimeitafuta sana sikuipata
0672 910 165
 
Back
Top Bottom