Nabii Johnson Petersburg (kurudi kwa kifo)

Skythelimit

Member
Jul 19, 2023
27
53
SEHEMU 1

Hapo zamani za kale enzi za akina nabii mfalme Daud huku Israel kulikuwepo na nabii mmoja kwenye himaya ya Uingereza aliyekuwa akijulikana kwa jina la nabii Johnson Petersburg (45) alimaarufu kama “sababu ya kifo” au jina lingine alikuwa akitambulika kama “mpasua vichwa”. Hii ni historia yake kabla hajawa nabii na namna alivyokuja kuwa nabii mkubwa kwenye zama zake hapo Uingereza.

Johnson Petersburg akiwa juu ya farasi amesimama alikuwa akitafakali ni kwa namna gani ataenda kukiteketeza kijiji cha West Norwich. Sababu ilikuwa kusemekana kijiji hicho kulea vijana chokoraa sana ambao hugeuka kusumbua watu wanapopita mtaani hapo. “Hivi hawa vijana wa huu mtaa wananifahamu kweli!? Dah… watajuta!” Mpasua vichwa alijisemesha hayo akiwa anaweka shoka yake vizuri kiunoni na kuamuru farasi yake kuondoka kuelekea kijiji cha west Norwich.
Mitaani west Norwich kulionekana vijana wasumbufu zaidi ya kumi wakileta fujo sokoni kwa wateja waliokuwa wakinunua mahitaji. Skatel “ we dada leta hiyo burger hapa unajua matumizi yake!” Skatel aliekuwa miongoni mwa makundi ya vijana hao akamunyanganya hiyo burger Jennie. Vijana wengine wakawa wanawapiga baba mmoja na mke wake na wakamnyanganga kikapu chake, akawaambia “Lakini vijana jambo hili mnalofanya jueni sio vizuri”
“utatufanya nini?”
“fanyeni yote ila msimuguse mke wangu”
Ahaa!.....ahaaa! Vijana hao wakacheka kwa kebehi huku wakimsukuma mke wa bwana huyo huko chini na kuaendelea kupiga huyo bwana huku wakichukua mikufu na mikate aliyokuwa nayo. “unaleta ujuaji hapa kula hiyo” maneno hayo aliyasema Raul huku akimsindikiza bwana huyo kwa buti kali la tumboni.
“haaa! Hu si uhungwana kutupigia wateja wetu”
“Jacob embu tulia ndugu yangu hawa vijana wana fujo sana” wauzaji wa sokoni walikuwa wanasemezana pembeni ya akina Jacob.
Jacob akawasikia na kuwafata “nyie wapumbavu mnasemajee!” kabla Jacob hajawarushia ngumi, malangoni kwa soko hilo akaanza kuona vijana wenzake watukutu wakishushiwa kipigo kizito. Mpasua vichwa Johnson alikuwa ameshaingia eneo hilo na anashusha kipigo kizito kwa hao vijana.
“kwenchi ninyi ebu kujeni hapa!” Johnson aliwaita hilo kundi la hao vijana likiongozwa na Skatel. “ hoya embu chomoa hizo panga” amri kutoka kwa Skatel akimuamuru Rogers kufungua mkeka uliokuwa na siraha zao za majambia. “hoya shika hilo” Rogers aliwarushia majambia kila mwanachama wake ambapo walikuwepo vijana kama kumi na tano. Johnson akachomoa kishoka chake kutoka kiunoni ili awaponde vichwa vyao. Haikupita dakika tano Johnson kuwa amewamaliza hao vijana kwa kipigo kizito kama kumsukuma mlevi, huku akipasua vichwa vyao kwa mikono na kishoka chake.
“Nini sasa huyu mpuuzi anafanya ndugu zangu anaua vijana wetu angali sisi tunamuungalia” baba yake Skatel uvumilivu ukamshinda alipoona mwanae kauwawa na Johnson. “Haiwezekani hao ndo vijana wanautulinda eneo hili kwa nini kawafanyia unyama huu!?” mfanyabiashara mwenzake na baba Skatel akarukia mada na wauzaji ndani ya soko hilo wakacharuka “hili haliwezekani” “hili haliwezekani” wafanyabiashara hapo sokoni hasa wanaume wakachukua visu ili wakapambane na bwana Johnson Petersburg.
Johnson akasema “sawa damu za mapuku yenu zinawita… uhh! Kujeni hapa”

Inaendelea.......
 
SEHEMU 2

Baba Skatel akasema “hao ni vijana wetu unaowaita mapuku!!!”

Wenzake wakarukia “ haiwezekani, haiwezekani!!”

Wauzaji hao wakamfuta bwana Johnson kama makondoo yanazama kuelekea mtoni. Walishangazwa na mkong’oto mzito waliokutana nao, huku wengi wakifa kwa kishoka hicho kilichojua kazi yake hapa duniani ni kutoa uhai wa watu tu.

Akinama hapo sokoni wakiwa wanalia wakaanza kumlaumu Johnson “ ondoka kwetu wewe ni muuaji” “umetuulia wame na watoto wetu, ondoka kwetu” akinamama hao waliendelea kumlaumu Johnson ambae kwa muda wote huo alikuwa amevaa nguo za ngozi kama askali wa jeshi la mfalme na akiwa kasimama kuwaangalia. Jennie ambae muda fulani nyuma alikuwa katoka kuzalilishwa na Skatel alikuwa akimuangalia Johnson kwa macho ya huba.

Johnson akawaambia hao akina mama “ sikilizeni akina mama, wame na watoto wenu wasisitizeni juu ya maadili na kuheshimu watu. Kijana hasipo zingatia maadili na nidhamu lazima ikabu ya mikono ya chuma itamfikia iwe angali hapa hapa duniani au kuzimu.” Akinamama wakashangaa, mama Bruno akasema “ oh! Kuwa na hofu ya Mungu we mwanaume!” Johnson akajibu “Mungu gani unamuongelea hapa, huyo huyo aliewatazama hapa nikiua wame zenu au yupo mwingine?” Johnson akiwa anaondoka Jennie akamkimbilia na kumwambia “ sa… samahani!......” Johnson akamwambia “ongea nakusikiliza”

“naomba twende nyumbani ukapumzike”

“ nyumbani wapi?”

“ nyumbani kwangu, maana inaonekana umetokea mbali na umetuondolea vijana wakorofi hapa sokoni”

“ sawa twende”

Nje ya soko Johnson Petersburg akampakia Jennie kwenye farasi yake na kuelekea nyumbani kwa Jennie. Ilikuwa yapata jioni kuelekea usiku ambapo Johnson walifika kwa Jennie.

“ Oh! Karibu kwangu shujaa” Jennie alimkaribisha Johnson ndani nyumbani kwake. “usijari!” Jennie akamuandalia maji ya kuoga Johnson akaenda kuoga, baadae Jennie akaandaa chakula mezani. “karibu mezani shujaa”

“asante sana naona vyakula kama vyote!

“ Yaah! Unajua unapokuwa na mtu jasiri kama wewe hivyo lazima kuongeza majonjo!”

“aha! Acha utani bana!” wakatabasamu wote, Johnson akamwambia “ ohh! Halafu kuna kosa nimelifanya…….”

“Kosa gani hilo shujaa?”

“nimeingia ndani kwa mtu hata sijauliza mwenyeji wangu jina lake, unakaa na nani hapa, isije kuwa nakula jasho la mwanaume mwenzangu humu!” Jennie baada ya kulizwa swali hilo picha ya kumbukumbu ilimjia kichwani mwake na akakumbuka kifo cha mchumba wake Bruno ambae walikuwa hajatambulishana kwa wazazi. Bruno ni miongoni mwa vijana waliokufa sokoni kwa kipigo kizito kutoka kwa bwana Johnson. Jennie akashituka “uh! Unasemaje shujaa!” Johnson akamwambia “ nakuona umeganda, shida nini?”

“ hapana shujaa kula twende tukalale”

“ ila nilikuuliza swali hapo awali, jina lako……!”

“ sawa nimekumbuka, jina langu naitwa sweet Diva humu ndani nimo pekee yangu” Jennie alidaganya jina.

“ wow! Binti mzuri hivyo unaishi pekee yako humu ndani….!”

“ Wala hata usijari nina zawadi yako chumbani kula haraka!” Jennie aliongea hayo huku akaondoa baadhi ya vyombo mezani na kuvipeleka jikoni. Akiwa jikoni Jennie picha ya mauaji ya Bruno ilimurudia huku na maneno mchache ambayo Bruno alipenda kumwambia “ mchumba wangu nakupenda, napambana ili nije nikuoe…..” Kabla Jennie ajamaliza hiyo kumbukumbu, Johnson alimuita kutokea sebuleni “ Sweet Diva nishakuwa tayari nakusibiri” Jennie katoka huko chumbani akiwa na nguo nyepesi ya kulalia, Johnson akamshika kiuno na kuelekea chumbani kwa ajili ya chakula kingine.

Itaendelea
 
SEHEMU 3
Asubuhi na mapema, Jennie alidamka mapema sana huku Johnson akiwa bado amelala huku akionekana kuchoka na shughuli ya usiku huo. Jennie akachukua kisu kikali kilicho kuwa pembezoni mwa kitanda alipokuwa amelala na kujiandaa kwa ajili ya kukisokomeza mwilini kwa bwana Johnson Petersburg. Kumbukumbu ya kifo cha Bruno kikapita tena kichwani mwake na akajikuta mwili umesisimuka huku akipeleka kisu tumboni mwa Johnson. “ nini hiki unafanya wewe kahaba” Johnson akatamka hayo huku kisu kikiwa kimemchana pembezoni mwa tumbo lake maana alipiga mkono wa Jennie. Jennie akamwambia “nakuchukia! Kwa sababu umeua mchumba wangu”
“mjinga wewe kuja hapa” Johnson akamshika Jennie akampiga kofi akayumba akaenda kudondokea ukutani. Jennie kutazama alikuwa na kisu bado mkononi, akakirusha kwa spidi kali kwa Johnson ila hakikumpata Johnson maana alikipangua kwa shoka lake alilokuwa nalo mkononi. “naona unataka kifo cha fajaa! Pokea kitu hicho!” Johnson alisema hayo huku akirusha shoka yake iliyoenda ikatua moja kwa moja kwenye shingo ya Jennie na hivyo kupoteza maisha yake. Johnson akachukua vitu vyake ili kupanda farasi yake aondoke.

Kule sokoni ambapo kuna uharibifu mkubwa uliotokea kutokana na mapigigano ya jana kati ya Johnson na vijana wa hapo west Norwich. Kikosi cha askali 20 kutoka kwa mfalme wa Uingereza kilitumwa maeneo hayo ili kije kuchunguza nini kimetokeo hapo. Baada ya kuulizwa wenyeji waliweza kusema sababu ya mapigigano yote hayo ni bwana mmoja wasiemjua katokea wapi, ila kaua watu wengi na kuelekea na nyumbani kwa Jennie. Asubuhi hiyo jeshi hilo likiwa na farasi wa vita likatoka kuja nyumbani kwa Jennie. “twendeni tutamkamata huko huko” askali Austin kiongozi alikuwa akiwaamuru maaskali wenzake kuelekea nyumbani kwa Jennie.
Johnson akiwa ndo anatoka ndani na kupanda farasi wake kwa mbali kidogo aliona kundi la askali likija upande alipokuwa. “hii ni hatari, ondoka….!” Johnson aliiamuru farasi wake na hivyo akatii na kuanza kukimbia kuelekea nje ya mji. “ huyo ni yeye ongeza mwendo tukamkamate” askali Austin aliwaamuru maaskali wake kumfukuza Johnson. Mbio za farasi zikashika kasi kuelekea porini kama tai aliyeona mawindo kutokea angani. Johnson alizidi kuwacha mbali kwa farasi wake. “ askali rusheni mishale anatuacha huyo” amri ya kamanda Austin kwa askali wake, wakarusha mishale lakini hakuna hata mmoja uliompata Johnson. “ ongezeni mwendo anatupotea huyo” pamoja na amri zote hizo askali hao hawakuweza kumshika Johnson na hivyo akawapotelea msituni. “ simameni” Austin aliwaamuru maaskali wake kusimama baada ya kuona hawawezi kumkamata Johnson, “Austin umefanya nini sasa… unakubali huyu Puju kutuzidi maarifa chifu!” kamanda Robert aliuliza, Austin akamjibu “ hapana huyo mtu kaingia msituni turudi tukajipange halafu tutamrudia tena”
“ tutamwambia nini mfalme kamanda”
“Hilo ni jukumu langu Robert, makamanda tunarudi Norwich” kamanda Austin aliamuru makamanda wake nao wakageuka kurudi mjini Norwich.
Msituni baada ya Johnson kugundua kwa umbali mrefu kutofatiliwa na askali yoyote alishuka kwenye farasi yake na kukaa chini ya mti pembezoni mwa kijito. Akiwa katulia hapo kwa mbali kidogo alisikia milio ya vitu kama viumbe vikicheza juu ya maji yanayo tiririka mtoni hapo. Akamfunga farasi wake vizuri baadae akachukua mishale na upinde aliokuwa nao shingoni na kuweka vizuri kiunoni shoka lake. Akashuka bondeni kuelekea mlio hiyo ilipotokea, kadiri alivyokuwa akisogea bondeni akagundua ni milio ya ndege aina ya Mabata bukini. Alivyopata upenyo wa kuchungulia majini kweli akayaona hayo mabata bukini yakiwa yanaji mwaya mwaya majini kwa raha zao bibi na bwana. Taratibu Johnson akasogea na kufyatua mshale uliompiga bata mmoja huku mwingine akiruka na kukimbia. Johnson akakimbia kwenda kumfata, akiwa anamchukua bata huyo kwa mbali Johnson akasikia mlio wa farasi kama kupata maumivu. Kwa kuwa Johnson ameshakaa na farasi yake Dovin kwa muda mrefu akagundua kabisa ni farasi wake. Johnson akatoka mbio kuelekea alipo muacha farasi wake, hakuamini macho yake alipokuta dubu kashamvunja miguu yote anataka kumtafuna. “oh Dovin wang.…….!” kabla Johnson hajamaliza kusema hayo huyo dubu alimuacha farasi huyo na kumkimbilia Johnson Petersburg. Johnson akamtupa yule bukini pembeni na kuanza kupambana na dubu. Dubu mwenye hasira kali, Johnson akamrushia shoka lake lakini halikumpata. Dubu huyu hapa akamfikia Johnson na kuanza kumchana chana kwa makucha yake, Johnson akaviringishana nae kuelekea bondeni. Kwa kuwa Johnson alikuwa na mishale mgongoni mwake akachomoa mmoja na kumchoma ubavuni kama mara tano, anachomoa na kuchomeka mpaka dubu huyo alipokufa. Johnson akainuka huku mwili wake ukiwa na majereha mengi ya mikwaruzo, mwili umetapakaa damu, akainuka kuelekea kwenye farasi wake. Maajabu akakuta farasi wake kesha kufa “ oh Dovin wangu.. hukunisubiri hata kwa dakika 10!” Johnson akatoa heshima za mwisho kwa farasi wake baadae akachukua siraha zake na bata wake kuelekea mapangoni kwa mlima uliokuwa karibu hapo. Usiku Johnson alikuwa yupo pangoni kakoka moto huku akimchoma bata wake, baada ya nyama kuwa tayari alianza kumla huku pia akijichua mwili uliokuwa umejeruhiwa na dubu.
 
SEHEMU 4

Asubuhi jeshi la mfalme lilikuwa parade kwa ajili ya majukumu ya kila siku. Mfalme Philip wa II (70 miaka) akatoka ndani ya kastri kwa ajili ya kupokea taarifa hasa fujo zilizotokea West Norwich. “ kamanda Austin nielezee kipi kimetokeo West Norwich” Kamanda Austin akajibu “mtukufu mfalme kuna mtu mmoja ambaye kasababisha fujo na mauaji hapo west Norwich”
“huyo mtu yuko wapi Austin?”
Huku Austin akikunja shingo kuangalia chini akajibu “mtukufu mfalme mharifu katupotelea msituni huko west Norwich” mfalme Philip II akatupa chini fimbo yake ya kifalme akasema “ni ujinga gani huu Austin umefanya!..... naambie umuhimu wako kuwa kamanda mkuu wa kikosi?” kimya kikatawala, pembezoni mwa uwanja wa kastri viongozi wa baraza walikuwa wamesima wakisikiliza kinachoendelea hapo. Mfalme Philip wa II akaendelea “sasa Austin kuanzia leo wewe sio kamanda wa kikosi hicho, Kamanda Lewis utachukua majukumu ya kuwa kamanda mkuu na hivyo utaongoza askali wako kwenda kumtafuna huyo mharifu” kamanda Lewis akasema “ nimepokea mtukufu mfalme”
Koridoni baada ya viongozi wale kutoka kwenye uwanja wa kastri, viongozi Albert na Leonard walikuwa wakijadiliana juu ya uongozi wa mfalme Philip II. “unajua huyu mzee tayari uongozi umeshamshinda Leonard”
“kwa nini Albert?”
“Si unaona jambo siriazi kama hili limemshinda”
“Kweli Albert, yaani kijiji kinavamiwa halafu mwalifu hapatikani”
“Unakumbuka tu juzi hapa masanduku ya dhahabu kutoka Wales yalipotelea njiani!”
Leonard akahitimisha kwa kusema “Albert kuna namna itatakiwa kufanya kumdhibiti huyu mfalme”
Usiku wa kalala, asubuhi kikosi cha kamanda Lewis kikawa kikifanya mazoezi kwa ajili ya kwenda kukabiliana na muharifu. Dastan (25) mtoto wa mfalme alikuwa hapo kambini akiangalia utayari wa kikosi cha Kamanda Lewis juu ya kwenda kumshika muharifu aliyeuwa wananchi wengi huko west Norwich. Dastan akasema “ Kamanda Lewis kuweni shupavu suala la uharifu huko west Norwich linamuumiza sana baba yangu” kamanda Lewis akajibu “ usiwe na mashaka mwana mfalme huyo nyang’au lazima tutamleta hapa.”
Ndani kwenye kastri, mfalme Philip II alikuwa amesima anaongea na kiongozi wake; mshauri mkuu bwana Albert. Mfalme Philip II akamwambia “unajua Albert kwa sasa napitia wakati mgumu sana, nimetoka kupoteza wananchi wangu wa west Norwich, dhahabu zangu kutoka Wales zimepotelea njiani, mfalme wa Ireland anataka nchi yangu ijisalimishe kwake…!” Albert akamjibu “Mfalme mimi naamini utayavuka yote bila shida yoyote”
“kivipi Albert?”
“Mfalme unacho kikosi imara sana ambacho kwa miaka mingi kimekuwa kikituletea ushindi”
“Kweli Albert?”
“kweli kabisa mfalme: wewe ni jemedari wa vita, simba wa milimani, ukiunguruma kishindo chako kinatikisa dunia, hakuna kama wewe na hayupo hatatokea!”
“ Safi sana Albert, mimi ndie mfalme hakuna zaidi yangu hapa duniani” maneno hayo ya mfalme Philip II aliyatoa na baadae kumuruhusu Albert kuondoka. “ngoja aendelee kujidaganya!” Albert aliyasema hayo akiwa anatoka mlangoni kwa mfalme Philip II.

Kule Msituni Johnson alikuwa na hekaheka za kuandaa mitego kwa ajili ya kuwadhibiti jeshi la mfalme Philip II ambao alijua lazima watamfatilia. Miti iliyochongwa vizuri kama mikuki ikawa imetegwa kwa ustadi mkubwa pembezoni mwa barabara.
 
SEHEMU 5

Kikosi cha makamanda kutoka kwa mfalme Philip II, kikiongozwa na Kamanda Lewis kilikuwa njiani kuelekea msituni kulikosemekana ndiko huyo mharifu alikokuwa akikaa. Farasi zikashika kasi kutoka Makao makuu ya mfalme kuelekea porini. Kwa mwendo kama wa masaa mawili, kikosi hicho cha makamanda 30 kikawa tayari kimeshafika msituni West Norwich na wakaanza kujipanga kwa namna gani kumvamia mharifu pangoni. Kamanda Lewis akasema “kamanda Wright na wenzako 10 piteni kule, na wewe kamanda Hanson pita njia hiyo na hawa askali 10….. ninyi mnifuate huku” kamanda Lewis akatoa amri hiyo na vikosi vikafuata. Kikosi cha Kamanda Wright kikiwa na siraha jambia na mishale kikachukua njia yake kuelekea kushoto, kikosi cha Kamanda Hanson chenyewe kikaelekea kulia. Kwa umakini sana wakati wa kutembea, kikosi cha kamanda Wright na Hanson wakajikuta wanachomwa na mikuki hiyo iliyotegwa njiani na hivyo wakafariki wote kabla hata ya kumkamata mharifu. Kilio cha makamanda hao kilimshitua kamanda Lewis na hivyo pamoja na maaskali kukimbia kwenda kuwaona. “Loh! Kamanda wangu…..!” kamanda Lewis alisema hayo akiwa anasikitika kuona kifo cha kamanda Wright. “Makamanda twendeni huyu pimbi hayuko mbali” kamanda Lewis akawahimiza maaskali wake waendelee mbele kumtafuta mharifu. Kwa mbele Johnson akiwa amekaa kwenye jiwe huku akitafuna mizizi ya miti. Lewis baada ya kumuona akasema “makamanda kuweni tayari, mharifu wetu yule pale!” makamanda 10 pamoja na yeye Lewis waliokuwa wamebaki wakamsogelea Johnson bila kujua hatari yake. Johnson alisimama na kuwafuata kama mshale. Mapigano yakachukua nafasi huku Johnson akitumia shoka lake, Lewis na makamanda wake wakitumia majambia yao kwa ustadi mkubwa. Mtu mmoja baada ya mwingine wale makamanda wakawa wanandondoka na kufa baada ya kukuta na shoka la Johnson. “wewe kijana utauweza kweli huu moto?” Johnson Petersburg akamuuliza swali hilo kamanda Lewis huku akiendelea kumshambulia. Kamanda Lewis akasema “lazima nikufikishe kwa mfalme”
“ unifikishe mimi kwa mfalme…..? Labda kwa mizimu ya kwenu….!” Johnson akaendelea kuwashambulia kamanda Lewis na mwenzake mmoja aliebaki. Muda mfupi kamanda mmoja wa Lewis akadondoshwa chini na kufa. Lewis akaongeza mashambulizi lakini akazidiwa uwezo na Johnson na hivyo kupoteza maisha. Johnson baada ya kujiridhisha kuwamaliza hao makamanda akabeba shoka lake na kuelekea pangoni kwake.
Usiku Johnson alikuwa kwenye pango lake akiota moto huku akichoma nyama kutokana na mawindo yake huko msituni. Baada ya kula akaenda kwenye kizimba chake akalala.
Hekaluni kwa mfalme kulikuwa na hekaheka nyingi kuhusu usalama wa hapo kutokana na vitisho kutoka kwa watawala wengine majirani zake. Lakini pia ilikuwa zimeshapita siku 7 tangu maaskali kutumwa msituni na bila kurudi kuleta mrejesho. Kiongozi Albert na Leonard walikuwa kwenye ofisi yao wakijadili namna ya kumuangusha mfalme Philip II. Albert akamwambia “unajua Leonard huyu mfalme wa ajabu sana, inawezekana vipi kijana wake kumpa mamlaka makubwa ya kukagua hazina ya dora huku ndo kwanza katoka kusoma!?”
“ata mimi nashangaa Albert”
“sasa sisi hatuna cha kupoteza tayari masanduku ma 4 ya dhahabu kutoka wales yapo mikononi mwetu”
“usiniambie Albert ulifanikisha hilo jambo?”
“Wewe tulio tu Leonard lazima tusimike mtu wetu hapa ambae atafuata matakwa yetu ya kiuongozi”
“ sasa twende kwanza kwenye kikao cha mfalme tumsikie ana jambo gani leo”
Kiongozi Albert na Leonard wakatoka chumbani humo na kuelekea kwenye ukumbi wa mfalme. Pamoja na viongozi wengine wakaungana nao na kuingia ukumbini. Baada ya kuingia ukumbini viongozi 20 mfalme na yeye pia akaingia, akakaa na kufungua majadiliano. Mfalme Philip II akamwambia “ndugu zangu karibuni mahala hapa, kuna machache ya kuwashirikisha. Kwanza niwambie kwamba juhudi ya kufatilia masanduku ma 4 ya dhahabu kutoka Wales imekuwa ngumu kwa sababu wavamizi wameyashikilia huko mpakani. Makamanda tuliowatuma kule West Norwich bado hawajarudi hivyo nitapeleka kikosi kingine kikaone nini kilichotokea huko. Na mwisho napenda kumtangaza kijana wangu Dastan kuwa mkuu wa makamanda katika hii dora ya Uingereza kwa sababu sasa naona ameshatosha kuwajibika kwa ajili ya dora hii”
Dastan akasimama na kusema “Asante ewe mtukufu mfalme”
Viongozi waandamizi wakajadiliana mmoja mmoja na kusema “ dhahabu imepotea? Makamanda wiki nzima hawajarudi?” Albert akavunja minong’ono na kusema “mtukufu mfalme wewe ni jabari la siasa sioni cha kukushinda hapo. Mimi nadhani ongeza kikosi cha makamanda wa kwenda West Norwich kupambana na huyo mharifu”
Mfalme akajibu “sahihi kabisa nitatuma makamanda 50 wakiongozwa na kijana wangu Dastan kwa ajili ya kumkabili huyo mtu anayeondoa amani maeneo hayo”
 
SEHEMU 6

Baada ya kutoka katika kikao hicho kikao Albert na Leonard walikuwa wakielekea kwenye majukumu yao ya kila siku. Albert akasema “sasa mfalme anatufinya kuhusu kuja kwa mwanae!”
“mwanae yupi tena Albert?”
“ Si yule Titus wa mke wake wa Wales!”
“ sawa nimemkumbuka, anakuja lini?”
“Ataingia hapa kesho!”
Usiku Dastan alikuwa kwenye mawazo mengi namna gani anaenda kumtafuta mharifu ambae bado hajamjua yupoje. “mwanangu usijali nimekupa makamanda wenye sifa za kumshambulia hata kiumbe kilicho chini ya ardhi, hivyo namna mtampata mtu huyo”
“Hapana tatizo baba” Dastan kijana wa mfalme akamjibu baba yake baadae akaaga na kwenda chumbani kwake.
Asubuhi kikosi cha Dastan kilikuwa kikijiandaa kwa ajii ya safari milimani west Norwich ambapo kunaaminika ndiko mharifu anapokaa. Kabla makamanda hawajaondoka, ugeni wa wa mtoto wa mfalme Philip II aliingia hapo kwenye makazi ya mfalme. Titus (33) mwana mfalme alikuwa ameingia kwa farasi wake akisindikizwa na walinzi wake. Mfalme Philip II akamuuliza mlinzi wake “ni nani huyo huko nje kaingia?”
“ ni mwanao Titus kaingia mtukufu mfalme!”
“ Lakini mbona huyu kijana nilimuzuia asije huku, imekuaje anisikilizi? Mfalme Philip II akashuka chini ili kuonana nae.
Kule kwenye makazi ya makamanda wakachukua farasi zao na kuondoka kwa mwendo kasi kuelekea msituni West Norwich. Chini ya uongozi wa Dastan, maaskali wa mfalme Philip II walikuwa wanaenda kuhakikisha wanamkamata mharifu wa msituni.
Mfalme alipomfikia kijana wake Titus kwa mama mwingine, alikataa salamu ya Titus nakumwambia “ unawezaje kuja kwangu bila taarifa?”
“Yaani kuja kwa mzazi wangu mpaka nitoe taarifa?”
Mfalme Philip II akamwambia “wewe na mama yako mliondoka hapa mmechoka kuishi humu ndani kama watumwa, sasa imekuwaje uje hapa?”
“ naona unapiga tu kelele!” Titus akamwambia hivyo mfalme
“ kijana wewe ni mpumbavu sana, sitaki kukuona hapa”
Albert aliekuwa hapa karibu akaingilia na kusema “ mtukufu mfalme hamna sababu ya kugombana na kijana wako……!”
“ Nani kijana wangu, huyo sio kijana wangu atafute pa kwenda kabla sijamfunga gerezani”
“ Mzee acha hizo!” Titus akajibu,
Kabla mfalme Philip II hajampiga kofi, kiongozi Albert akamvuta Titus na kuondoka nae kuelekea kwake, akasema “ngoja nimuondoe hapa mheshimiwa mfalme” baada ya Titus kuondoka na Albert, mfalme alibaki amesima huku walinzi wa Titus wakimfuata uelekeo wao. Mfalme Philip II akabaki anajiongelesha “yaani mtoto nilipomhitaji kwa ajili ya malezi mama yake alimkatalia, leo anakuja kunifanyia fujo kweli!” akiwa amesima hapo akamuona mlinzi wa hekalu nae kasimama kumwangalia “na wewe acha kushangaa nenda kwenye lango kule” mfalme Philip II akachapa miguu kurudi ndani.
Usiku kiongozi Albert na Leonard na Titus walikuwa pamoja ndani kwa siri. Albert akasema “ sasa wewe Titus mbona umekuja mapema sana?”
“Niliona ninyi mmekaa kimya sana” Titus akajibu,
“hapana tunapanga misheni kwa ueledi mkubwa sana” Leonard akajibu,
Albert akamuuliza Titus “hujatupa mrejesho kuhusu zile dhahabu zilozopotea Titus?”
“nipende kuwambia kwamba ile ramani ya msafara mliyonitumia, niliitumia na kuweza kukamata dhahabu zote za mfalme Philip”
 
SEHEMU 7

Wote wakapongezana kwa kusema “vizuri sana”, Titus akawaambia “nipo hapa kwa jukumu moja tu la kuhakikisha nachukua jukumu la kuwa mfalme wa Dora hili la Uingereza”
Leonard akajibu “sisi tupo hapa kukuhakikishia unafanikisha hilo”
Albert akasema “ ila nadhani Dastan anaweza kutuharibia huo mpango wa wewe kuwa mfalme….!”
Titus akajibu “huyo ni mtoto mdogo hanisumbui!”
Huko msituni West Norwich, Dastan na maaskali wenzake walikuwa wameshaingia kwenye maeneo ya kamanda Johnson Petersburg. Wakajipanga ili wamshike akiwa pangoni lakini walijikuta wanakufa kwa mitego aliyoitega Johnson. Hadi walipo baki makamanda makamanda 12, Johnson akatokezea na kuanza kuwashambulia. Dastan akasema “makamanda kuweni makini na huyu mtu…”
Johnson akajibu “kujeni hapa enyi mapuku” baada ya muda mchache wale makamanda walikuwa wanaogelea kwenye damu zao. Baada ya Johnson kuwamaliza makamanda wote alimpiga teke Dastan naye akandondoka chini, kabla hajamudondoshea shoka, Dastan akasema “usiniue mimi mwana wa mfalme”
“kwa hiyo mfalme Philip II kaamua kukutoa kafara wewe mwanae wa pekee…..!”
“hapana ila alitaka kujua wewe ni nani unayesumbua raia wake”
“ ahaa! Kumbe anataka kujua mimi ni nani…… sasa sitakuua, utarudi ukamwambie mimi ni yule kamanda aliyenifukuza jeshini, kayaharibu maisha yangu na sasa ninaishi mapangoni kama mbweya ila nitamtafuta mimi mwenyewe ili tuongee kianaume!”
Johnson akamnyenyua Dastan na kumpeleka kwenye farasi ili arudi kwa mfalme. Dastan akatoa ishara ya heshima akapanda kwenye farasi wake ili arudi kwa mfalme. Johnson akachukua siraha zake na kupandisha mlimani kwenye mapango anapoishi.
Ndani ya kastri kwa mfalme Philip II, kiongozi Albert, Leonard na Titus walikuwa kwenye jengo lingine wakijadili namna ya kumuondoa mfalme Philip II kwenye kiti cha kifalme. Titus akasema “ viongozi wangu sioni kuchakarika kwenu juu ya mimi kuwa mfalme wa Dora hii!”
Albert akajibu “ tupo vizuri kabisa kumbuka leo siku ya tano Dastan bado hajarudi”
Leonard akadakia “watakuwa wameshakufa hao!”
“Sasa baada ya mwana mfalme kufa, inabidi tuwaze kumpoteza mfalme Philip II” Albert aliongezea.
Wakiwa wanajadiliana wakasikia honi ya kuingia kwa mtu, mfalme akashuka chini kuelekea kwenye malango ya kastri, Leonard na Albert na wananchi wengine pia wakaelekea malangoni mwa kastri ili waweze kuona aliyeingia. Mfalme wa wananchi wengine hawakuamini kumuona Dastan akiwa kwenye farasi hoi bin taabani kwa majareha ya ya kipigo.
“mwanangu nani kakufanyia hivi……!” mke wa mfalme Philip akamuuliza Dastan mwanae. Dastan kabla hajajibu, mfalme Philip II nae akauliza “mwanangu sema nini kilitokea huko Msituni?”
“ni Johnson Petersburg baba..!” kila mtu akaduwaa baada ya kusikia jina hilo.
“yaani kamanda wangu niliemuajiri kwenye jeshi langu kanigeuka ni kuwa adui wa Dora la Uingereza!”
“anadai ulimfukuza jeshini kwa aibu bila kuzingatia haki zake”
“kwahiyo kaamua kuanzisha vita na mimi mfalme?”
“ ndio na anadai atateketeza makamanda wako wote”
Watu wakashangaa “kuteketeza makamanda wote!”
“viongozi tuonane ukumbini” mfalme Philip II akawaamuru viongozi wake waende ukumbini kujadili jambo hilo.
 
SEHEMU 8

Ukumbini kukaonekana kuwa na mawazo mseto, kundi moja likimtaka mfalme ashiriki kwenye mapigano na Johnson ili akamatwe, huku wengine wachache wakimuomba mfalme kupata na Johnson ili arudishwe kundini. Albert na Leonard waliojua uwezo mkubwa wa mapigano aliokuwa nao Johnson ndiyo wakawa wa kwanza kumtaka mfalme kwenda msituni akapambane na Johnson. Leonard akasema “mtukufu mfalme mimi naona kwa namna ulivyo jitegenezea ikhlasi naona nibora uende wewe huko Msituni na jeshi imara naamini huyo msaliti atapatikana”
“ Na mimi naona iwe hivyo” Albert akasapoti
Mfalme akauliza “wengine mnasemaje?”
“mtukufu mfalme kwa kuwa Johnson ni miongoni mwa raia wetu sioni busara kupigana nae twende tumfate huko msituni tusuruhishane tumrudishe kambini” kiongozi Josephat akapendekeza hivyo. Mfalme akakubaliana na wachache waliopendekeza wao la kupatana na Johnson ili kujenga umoja ndani ya Uingereza.
“Sasa naona maoni ya kupata na Johnson ndiyo muhimu, hivyo kesho kutwa mimi pamoja na viongozi wachache na makamanda wachache tutaelekea huko msituni West Norwich kumrudisha Johnson kambini.”
Baadhi ya viongozi waliotamani mfalme akashiriki vita ya msituni wakachukia uamuzi huo, wakatoka nje wakinung’unika. Hawa walikuwa viongozi Albert na Leonard, baada ya mfalme kuhitimisha kikao viongozi wote walitoka kuendelea na shughuli zao. Albert na Leonard muda mfupi wakawa ndani ambapo wamemuhifadhi Titus na hivyo wakawa wanajadiliana namna ya kukatisha ufalme wa Philip wa II. Albert akasema “mfalme anasisitiza juu ya kwenda msituni kupatana na Johnson”
“Kweli ndo kaamua hivyo!?”
Leonard akajibu “ni kweli Titus mfalme kapinga wazo la yeye kushiriki vita ili apambane na Johnson”
“siyo mbaya kifo chake kitamfuta huko huko west Norwich”
“Kivipi Titus”
“mimi na wewe(Albert) tutamfuta kwa nyuma kabla hajafika kwenye mlima aliko Johnson sisi tutamvamia huko”
“na habari ya mapatano na Johnson ndiyo itakuwa imeishia hapo” Albert akaongezea
“na mimi hapa kwenye kastri nitabaki kufanya nini?” Leonard akauliza
“wewe utabaki kupiga propaganda juu ya kifo cha mfalme na kunitangaza kama mfalme mpya nitakapoingia na mwili wa marehemu mfalme Philip” Titus akamjibu hivyo, Leonard akamwambia “lakini Titus husisahau kwamba mfalme Philip II ni baba yako, husimtendee kinyama!”
“mimi sijali, nachojua ni kwamba baba yangu alinitelekeza katika udogo wangu, hivyo sijali kitakachomtokea” Titus akahitimisha kwa kusema hayo na baada ya muda mchache wakatawanyika kwenda kuweka mambo sawa.
 
SEHEMU 9

Kule Msituni, wakati wa usiku Johnson alikuwa yupo kwenye pango lake akichoma nyama na kula. Wakati akila alikuwa akikumbuka namna watoto wake 2 pamoja na mke wake walivyo chukuliwa mateka na wavamizi. “oh mke wangu……!” akawa kama anafuta machozi akatandika akalala. Akiwa usingizi aliota ndoto iliyomuogopesha sana maana katikati ya ndoto aliona watu kama mizimu aina ya mazombi yakimfuata na kumkimbiza yakitaka kumtafuna. Akajitaidi kuyakimbia lakini ikafikia hatua akashindwa kukimbia, yakamukaribia ili yaanze kumtafuna. Lakini aliona ishara kama miale myeupe aliyopita katikati yao kama radi hayo mazombi yakaanguka yakafa. Akashituka huku mapigo ya moyo yakienda kasi sana. “duh nitakufa huku mapangoni!......... kesho nirudi mjini kwa mfalme” Johnson alijisemea hayo huku akipanga vifaa vyake kwa ajili ya safari.
Kulipo pambazuka, makamanda 10 wa mfalme pamoja na viongozi 2 walikuwa pamoja na mfalme kuanza safari ya kuelekea msituni West Norwich ili kuonana na Johnson. Wakapanda kwenye farasi kwa ajili ya kuanza safari yao kuelekea msituni.
Walipofika katikati mwa safari, mfalme ndani ya kikoteni kikivutwa na farasi alishangaa farasi zikisimama ghafla. Mara ghafla kipigo kikaanza kutembea kwa maaskali wake. Mapanga yakafanya kazi yake huku askali wa mfalme akifa mmoja baada ya mwingine.
“Kiongozi Linus tumeshatekwa hapa”
“naona hivyo mtukufu mfalme”
“ Tutafafanyaje sasa?”
“kamata upanga wako tuone namna ya kujiokoa hapa” kiongozi Linus na kiongozi Jailos wakateremka kutoka kwenye mkokoteni huo wakimuacha mfalme ndani yake. Wakatoka ili wapambane na kundi la wavamizi ambao walikuwa hawajawajua bado. Jailos na Linus wakiwa wanajiandaa kutumia majambia yao mishale ikatokea huko porini na kuwapiga wote wawili wakafa. Maaskali wa mfalme wakakatwa katwa na mapanga wakafa wote. Kundi la wavamizi wakiwa na askali 20 pamoja na watu 2 waliojificha nyuso zao kwa maski walioneka kulizunguka gari la mfalme. “makamanda mshusheni humo ndani ya gari” kiongozi 1 aliamuru, kabla mfalme hajashushwa alishuka mwenyewe na kuuliza “ ninyi ni nani na mnataka nini kwangu?”
“Shuka kwanza nchini ewe mpumbavu” kiongozi 1 akamjibu. Kamanda Colin akamvuta kutoka kwenye mkokoteni na kumdondosha chini mfalme.
“Leo ni siku yako ya mwisho, kama ambavyo hukuwatendea haki wengine na wewe pia leo utaonja mateso ya kiburi chako”
“Unaoneka wewe ni kijana unaenifahamu kwani wewe ni nani?”
“jina langu halitakusaidia chochote wakati huu, nachotaka saini kwanza hizi karatasi labda ndo unaweza kupata msamaha” kiongozi 1 akamwambia.
“siwezi kusaini karatasi nisizo zijua, kwani mnataka nini?”
Kiongozi 2 akamwambia kiongozi 1 “ mbona unachelewesha kazi kata shingo hiyo tutatumia vidole vyake kusaini baada ya kifo chake”
Mfalme akasimama kwa haraka ili amkate kiongozi 1, kiongozi 1 akamkwepa panga zikakutana, kiongozi 1 akamchana panga la paja mfalme akapiga magoti. Mfalme Philip II akiwa amechoka, amekata tamaa ya kutoka hapo mzima akainamisha kichwa ili kichinjwe. Kiongozi 1 akashika vizuri upanga wake akauinua juu ili akate kichwa cha mfalme. Panga likiwa juu kiongozi 1 alishangaa mkono wake ukiwa umechomwa mshale pasipo kujua umetokea wapi. Kiongozi 1 akiwa anagugumia maumivu, Kiongozi 2 akaamuru “makamanda kaa teyari mtego huu!” wakiwa bado wanashangaa mishale mingine akiwashukia makamanda. Kuangalia vizuri Johnson Petersburg alikuwa amewasili eneo hilo kwa farasi, Kiongozi 1 akakata mshale kipisi kikabaki ndani akajiandaa kwa mapigano. Johnson akashuka chini ya farasi, akashika shoka lake akawafata.
Kiongozi 2 akamwambia kiongozi 1 “huyo ndo Johnson Petersburg kuwa makini nae sana”
 
Hii ni lugha gani imetumika? Maana sijaelewa kabisa, mwanzoni nilidhani ni kiswahili
 
SEHEMU 10

Mfalme akasimama na kuanza na yeye kupambana upya kwa maumivu makali aliyo kuwanayo hakuweza kupambana. Johnson akawapiga wale wavamizi huku akimlinda mfalme. Kwa muda mchache Johnson akawa kawamaliza makamanda wote, kiongozi 2 akamfata ovyo ovyo akapigwa shoka ya bega, bega likaning’inia akafa. Akabaki kiongozi 1 ambaye kwa mateke ya Johnson yalimchosha na kumdondosha chini.
“ leo mtasema ninyi ni akina nani” Johnson akasema huku akimfuata kiongozi 1 iliamfunue maski yake.
“Tafadhali naomba usinivue maski hii……….!”
“Johnson mvue tu usimsikilize huyo nyang’au!” Mfalme akamwambia Johnson. Mfalme akiwa anasema hayo Johnson alikuwa tayari ameshika maski hiyo ya kiongozi 1 na kuivuta kwa nguvu uso ukabaki wazi.
Mfalme akasitajabu na kusema “Titus kijana wangu wewe ndo ulikuwa umeamua kuja kuniua!?”
Johnson akauliza “mfalme kumbe unamjua huyu?”
“Ndio ni mwanangu lakini kwa mama mwingine aliehamia kwao huko Wales”
“Sasa mfalme unasemaje kuhusu huyu msaliti?”
“dawa yake ipo hekaluni tukifa kule”
Mfalme akaenda akamtoa maski pia yule kiongozi 2, hakuamini kukuta ni mtu anaemfahamu “dah! Kiongozi Albert wewe ndo wa kunisaliti mimi…….”
“mfalme unamjua na huyo pia?”
“Alikuwa kiongozi wangu mwadamizi ambapo kila jambo langu muhimu lazima nimwambie yeye”
“Achana nae dawa ya msaliti ni mauti!
Johnson na mfalme wakamfunga Titus na kupanda nae kwenye farasi huku Johnson akiwakokota kurudi hekaluni kwenye makazi ya mfalme.
Mida ya jioni, msafara wa mfalme Philip II ukaingia hekaluni huku ukiongozwa na Johnson. Ngoma zikalia kuita watu, watu wakasimama kwenye malango ya mfalme. Johnson akasimamisha farasi na mfalme akashuka kwenye farasi huku akimvuta Titus. “ wananchi Titus ni msaliti alipapanga njama za kuniua mimi leo” mfalme Philip II akasema hayo. Mwana mfalme Dastan akamkimbilia akampiga kofi na akataka kuchomoa panga lake kwa ajili ya kumuua lakini baba yake akamzuia.
“sikiliza usifanye hivyo”
“lakini huyu ni msaliti baba kataka kukuua”
“adhabu yake ipo ni nzito tu”
Wananchi wakaanza kupigaga kelele “msaliti auawe! Msaliti auawe”
Mfalme akasema “wananchi tulieni tu adhabu yake inakuja, kamanda Boson mpeleke chumba cha mateso huko gerezani” Kamanda Boson akamchukua Titus akampeleka gerezani, lakini Leonard alionekana mtu wa wasiwasi sana baada ya kuangaza na kutomuona rafiki yake kiongozi Albert. Mfalme Philip II akaendelea kusema “kiongozi Albert aliekuwa kiongozi wa karibu kwenye baraza langu, alinigeuka na kupanga njama ya kuniua. Shukrani kwa kamanda Johnson Petersburg kufika kwa wakati na kuweza kuniokoa” wananchi wakapaza sauti na kumpongeza “Johnson shujaa wa Dora la Uingereza…….!” Wananchi wakiwa wanaendelea kupongeza mfalme Philip II alimchukua Johnson na wanafamilia wake wakaingia ndani.
Wakiwa ndani mfalme Philip II pamoja na Dastan walikuwa na maongezi na Johnson ambaye sasa karudi kwa mfalme. Mfalme akasema “Johnson karibu sana”

Inaendelea......
 
SEHEMU 11

“asante sana mtukufu mfalme”
“ Johnson nadhani tusahau yaliyopita tugange ya mbele”
“ni sahihi mfalme”
Dastan akasema “lakini Johnson uliponishika kule Msituni uliahidi kuja kulipa kisasi kwa baba kwa kukufukuza kwenye kikosi cha makamanda, isije ikawa unatafuta ukaribu kwa baba yangu ili umuue!?”
“Ningekuwa na shida ya kumuua baba yako ningemalizana nae mapema hata kabla ya Titus hajataka kumuua sina haja ya kufanya hivyo maana naamini niitaji kufanya kazi bado kwa uaminifu mkubwa”
“sasa Johnson achana nayo, utakuwa kamanda mkuu chini ya Dastan kuhakikisha usalama na amani katika imaya hii inadumu”
“Sawa mfalme” Johnson akakubali huku mfalme akimimina Divai kwenye grasi ili wanywe. Wote wakachukua na kuanza kunywa, wakiwa wanakunywa aliingia Rebecca (33) mpishi wa chakula cha mfalme. Rebecca binti mzuri sana wa umbo na sura aliingia na kumuita Dastan mwana mfalme. Johnson baada ya kugeuka na kuona uzuri wa Rebecca alijikuta akidondosha grasi ya divai na kuleta mshituko kwa wote.
Mfalme akasema “Johnson shida nini?”
“hapana mfalme najisikia tu kama kizunguzungu, siko vizuri”
“Dastan samahani njoo mara moja” Rebecca akaita
“sawa narudi baba” Dastan akaodoka kumfuata Rebecca, wakiwa nje ya mlango wa kuingia kwa mfalme pale walipo kuwa wamekaa. Rebecca akamwambia Dastan “mama yako sijui amelala, kajaribu kumuangalia umwambie aje jikoni nina shida nae” wakiwa bado Dastan na Rebecca wamesima hapo, Johnson baada ya kumuaga mfalme alipita eneo hilo ili aende kwenye makazi yake. “Johnson unaondoka?”
“Yah nitarudi baadae” Johnson akiwa jicho ajalitoa kwa Rebecca akajigonga kwenye ukuta uliokuwa mbele yake, Akina Dastan wakaguna.
“aisee! Sijui nini kinaendelea hapa kwa mfalme!” Johnson akaondoka huku akilalamika.
Asubuhi kulikuwa na kikao kwa mfalme, ndani ya kikao hicho Johnson alikuwa ndani kama mlinzi wa mfalme. Mfalme akasema “ ndugu zangu tumetambua msaliti wetu alikuwa miongoni mwetu……”
Akaendelea “Albert alikuwa kiongozi mkubwa tu lakini akapanga njema za kuniua”
Kiongozi Romeo akasema “alipanga jambo la ajabu sana!”
Mfalme akaendelea “sasa tumsahau huyo kwakuwa ameshakufa, mhahini Titus sijui tumfanyeje?”
Kiongozi Leonard akasema “mimi nadhani kwa kuwa wewe ni mfalme wa misamaha, mimi nadhani na yeye umsamehe!”
“Kivipi nimsamehe mtu aliyejaribu kuniua?”
Leonard akajibu “ulinzi wako umeonesha udhaifu mkubwa kama jaribio la kukuua limetokea kwa mtu wa huko huko kwenye familia yako.” Kwa kutamka hayo viongozi wengine wakastajabu, kamanda Johnson nae akakasirika.
Mfalme akamjibu “ kwa hiyo wewe Leonard ulitaka tumfanyeje Titus?”
“msamehe kama ulivyo mrudisha kundini huyo msaliti Johnson”
Baada ya kutajwa kwa hilo jina dhumuni la kikao likaingia doa. Mfalme akamwambia Leonard “Leonard naona unenda kasi sana, nakukumbusha Fikiri kabla ya kunena” kikao kikahitimishwa kwa kukubaliana Titus arudishwe Wales kwa mama yake na hivyo hasirudi tena Uingereza.
Nyakati za usiku, Johnson alikuwa akizunguka kuona usalama wa hekalu la mfalme, katika pita pita yake akakutana na Rebecca.
“wewe Rebecca unaenda wapi usiku huu?”
“ wewe unanihoji kama nani?”
“usalama wako ni muhimu hapa hekaluni”
“nalifahamu hilo”
“sasa samahani nilikuwa naomba tuongee!”
“Mbona mpaka sasa tunaongea Johnson” Johnson akajaribu kumwambia juu ya hisia zake lakini hakashindwa.
“ una….ju….a! au basi tu nisikupotezee muda nitakuandikia barua juu ya ninacho taka kukuambia”

Itaendelea.......
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom