princewilly
JF-Expert Member
- Nov 30, 2017
- 259
- 526
NYEMO CHILONGANI.
SEHEMU YA 01
Wasichana zaidi ya kumi katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam walinyamaza ghafla huku macho yao yakimwangalia kijana mmoja ambaye alikuwa akipita mbele yao.
Mwendo wake ulikuwa wa taratibu sana, alitembea kwa kujiamini mno, alijua kwamba alikuwa mzuri wa sura, wanawake wengi walimbabaikia huku akizungumziwa sana midomoni mwao na ndiyo maana hata alipokuwa akitembea mbele ya wasichana, mwendo wake ulikuwa ni wa kunyata sana kana kwamba alikuwa akimsubiri mtu aliyekuwa nyuma yake.
Wote waliokuwa wakimwangalia walivutiwa naye, kulikuwa na wasichana ambao walitamani hata kumsimama kijana huyo na kuzungumza naye tu ili kesho waanze kuzusha kwamba walikuwa kwenye mahusiano ya kimapenzi pamoja naye lakini hilo halikuwezekana kabisa.
Kila mmoja alitulia na kumwangalia kwa makini kabisa, alikuwa kijana mwenye sura nzuri ambaye kila msichana chuoni hapo aliyemwangalia alitamani sana siku moja awe naye kimapenzi na kuwa mume wake wa ndoa. Kijana huyo aliitwa Richard Mawelle.
Richard alikuwa tofauti na vijana wengine, muda mwingi alikuwa kimya, hakuwa mzungumzaji hata kidogo, hakupenda mazoea na wasichana na ndiyo maana muda alipenda kujitenga huku kama ilikuwa ikitokea kuzungumza na watu wengine, basi alikuwa akiwafuata marafiki zake wawili, Robinson na Robert.
Wasichana walimbabaikia, mara kwa mara kulikuwa na ugomvi wa wasichana kwa wasichana, wengi walikuwa wakigombana kwa ajili yake, si kwamba walizungumza naye bali kujitamba mbele ya mashoga zao ndiyo hali iliyokuwa ikileta ugomvi katika chuo hicho.
Kulikuwa na makundi ya wasichana waliokuwa wakichukiana kisa Richard, kulikuwa na watu ambao kila walipoonana ilikuwa ni kugombana kisa kijana huyo ambaye wala hakuwa na taarifa na msichana yeyote yule.
Kutokupenda kwake wanawake kukamfanya watu kuanza kumfuatilia, walihisi kwamba kulikuwa na siri kubwa na nzito nyuma yake, ilikuwa ni vigumu kwa mvulana yeyote kutotaka kuwa kwenye mahusiano na msichana yeyote yule, hasa wasichana wengi warembo ambao walikuwa wakipatikana chuoni hapo.
Kwenye ufuatiliaji wao, hawakugundua kitu chochote kile, alikuwa mzima wa afya, hakuwa na urafiki na wanaume wengi, hao wawili, Robinson na Robert ndiyo walikuwa kila kitu kwake, alibadilishana nao mawazo na hata kujadili mambo mengi ambayo walitakiwa kufanya mara baada ya kumaliza chuo.
Kila siku Richard alikuwa mtu wa kupokea maboksi ya zawadi kutoka kwa wasichana mbalimbali, chuoni hapo ilikuwa ni kama ushindani, kila mmoja alitaka kumuonyeshea kijana huyo kwamba alikuwa akimpenda na alitakiwa kuuchukua moyo wake na kumfanyia lolote lile alilotaka.
“Richard...kwa nini unanifanyia hivi?” aliuliza msichana mmoja aliyeitwa Jesca ambaye alisimama mbele ya Richard.
Siku hiyo ilionekana kuwa kama muujiza, kijana huyo hakuwa akitoa nafasi ya kusimama na msichana yeyote yule, kwa Jesca ilikuwa ni bahati kubwa kwa kuwa alimkuta akifikiria mambo mengine kabisa, alimfuata kwa kushtukiza.
“Unasemaje?” aliuliza Richard huku akionekana kushtuliwa kutoka kwenye lindi la mawazo.
Msichana huyo akarudia maneno yake kwa mara nyingine huku Richard akimwangalia. Alitamani kumfukuza, hapo alipokuwa alikuwa akiwasubiria marafiki zake, Robinson na Robert ambao walipanga kuonana mahali hapo kwa ajili ya kuzungumza kitu cha muhimu sana.
Alisita kumfukuza kwa sababu kila mtu aliyekuwa canteen alikuwa akimwangalia yeye na msichana huyo ambaye aligoma kabisa kuondoka, alichokuwa akitaka ni kujua ukweli kama Richard alikuwa akimpenda au la.
Alichokifanya ni kusimama, akamshika mkono na kuanza kuondoka naye. Kila mmoja alishangaa, uondokaji wake haukuwa wa kawaida hata kidogo, ni kama kulikuwa na kitu kilichokuwa kikiendelea.
Waliokuwa wakitaka kuona mwisho wa mchezo ni kitu gani kingeendelea wakaanza kufuatilia kimyakimya, wale ambao hawakuwa mule canteen ambao walimuona Richard na msichana huyo wakiwa wameshikana mikono walipigwa na butwaa kwani kwa mwaka wa pili mfululizo walijaribu kuzungumza na Ricard lakini ilishindikana kabisa.
Siku hiyo ilikuwa ni kama kituko fulani hivi, safari yao hiyo iliishia katika bweni la wavulana ambapo moja kwa moja wakaelekea katika chumba alichokuwa akilala na kumuweka kitandani.
Jesca hakujua sababu ya kupelekwa mahali pale, alibaki akimshangaa Richard, alihisi kama kijana huyo alitaka kuzungumza naye lakini kwa jinsi alivyoonekana, hakuwa sawa kabisa.
“Jesca! Nisikilize kwa makini,” alisema Richard huku akimwangalia msichana huyo usoni.
“Sawa. Nakusikiliza baba,” alisema msichana huyo kwa adabu zote.
Richard alitaka kuzungumza kitu lakini akashindwa, alichokifanya ni kuchukua begi lake na kulifungua, humo akatoa kadi nyingi, maua, saa mpya, cheni na vitu vingine vingi ambavyo alitumiwa kama zawadi na wasichana mbalimbali chuoni hapo.
“Hebu niambie! Kati ya hawa wote na wewe nimkubali nani?” aliuliza Richard huku akimwangalia msichana huyo ambaye hakuwa akishangaa vitu vile kwani kwa jinsi Richard alivyokuwa mzuri wa sura, alistahili kuvipokea kutoka kwa wasichana hao.
“Richard....” aliita Jesca.
“Hebu nijibu kwanza! Nimkubali nani? Nyie mnanichanganya sana. Unajua mimi siangalia wanawake, mimi naangalia pesa, kichwa changu kinafikiria mambo mengi kuhusu pesa. Jesca, sina muda na wanawake,” alisema Richard huku akionekana kuwa na hasira mno.
Jesca alibaki kimya, alimwangalia Richard, kwa jinsi alivyokuwa akizungumza, mishipa ilivyomtoka ilionekana kabisa kwamba hakuwa na masihara hata kidogo, kile alichokuwa akimwambia ndicho ambacho alikimaanisha kutoka moyoni mwake.
Baada ya kunyamaza kwa sekunde kadhaa, Jesca akaanza kutabasamu, alijua dhahiri kwamba Richard alikasirika, hakutaka kumuona akiendelea kwenye hali hiyo na ndiyo maana akaamua kulitumia tabasamu lake kama silaha ya kumaliza hasira za Richard.
“Unacheka?” aliuliza Richard.
“Hapana! Natabasamu. Naomba nipige picha na wewe, nakuomba!” alisema Jesca huku akitoa simu yake aina ya iPhone X.
“Jesca....”
“Nakuomba,” alisema Jesca na kujivuta mbele ya Richard na kujipiga picha moja iitwayo ‘selfie’ kisha kuondoka mahali hapo.
Moyo wa Jesca ukauma mno, hakuamini kile alichokuwa ameambiwa. Alijiona kuwa msichana mrembo mno, alifuatiliwa na wanaume wengi lakini wote hao hawakuwa na nafasi kwake, mwanaume ambaye alikuwa akimpenda kwa mapenzi ya dhati alikuwa huyo Richard ambaye aliamua kumkataa na kumwambia kwamba hakufikiria mapenzi, moyo wake ulifikiria zaidi pesa.
Alitembea kwa kujiachia, kila mtu ambaye alimuona alipoingia ndani na Richard aliamini kwamba walimalizana vizuri na inawezekana kabisa msichana huyo alikubaliwa kwani hata tabasamu lililokuwa likionekana usoni mwake lilikuwa la matumaini tele.
Jesca aliamua kulitumia tabasamu lake kama kuficha kile kilichokuwa kimetokea ndani. Moyo wake ulikuwa kwenye maumivu makali mno, alilia kwa ndani lakini machoni mwake alionyesha kuwa na furaha kupita kawaida.
Alitembea mpaka kwenye bweni lao, akaingia mpaka chumbani na kulala kitandani kwake, hapo ndipo alipoanza kulia kwa uchungu mkubwa moyoni mwake.
Kwa miaka ishirini na mbili aliyokuwanayo alijiapiza kwamba ilikuwa ni lazima aendelee kuishi bikira mpaka siku ambayo angeolewa ili iwe zawadi kwa mume wake lakini kitu cha ajabu kabisa baada ya kuanza chuo na kumuona Richard, akaamua kuachana na ahadi yake kwa mume wake mtarajia hivyo kutaka bikira hiyo itolewe na kijana huyo.
“Richard! Kwa nini umenifanyia hivi?” aliuliza Jesca huku akiendelea kulia kama mtoto mdogo.
Wakati yeye akilia na kuomboleza, upande wa pili maisha ya Richard yalikuwa kama kawaida, alizoea kuyaona machozi ya wanawake, wale wachache ambao walibahatika kuzungumza naye wengi waliyatumia ili kumlaghai lakini msimamo wake ulikuwa uleule kwamba hakutaka kuwa na uhusiano na msichana yeyote yule mpaka pale ambapo angekuwa na pesa nyingi.
Kupendwa na wanawake haikuwa chuoni tu bali hata nyumbani kwao, Magomeni Mapipa Richard alikuwa gumzo, kila msichana aliyekuwa akimuona alimpenda, alivutiwa naye na kutamani kuwa naye lakini hali ilikuwa vilevile.
Wake za watu walikuwa kwenye wakati mgumu, hawakuweza kujizuia, waliwaambia wanawake wengine jinsi walivyokuwa wakimpenda kijana huyo ambaye hakuonekana kuwa na habari na msichana yeyote yule.
Ndoa nyingi zilitingishika, waume zao walikasirika lakini hawakuwa na la kufanya kwa kuwa walijua ukweli juu ya kijana huyo kwamba hakuwa mtu wa wanawake, aliishi maisha yake ya peke yake huku kila siku akiwaambia watu kwamba pamoja na umasikini aliokuwa nao na familia yake lakini kuna siku moja angekuja kuwa na pesa nyingi.
“Ipo siku. Iqram, ipo siku mshikaji wangu,” alisema Richard mara kwa mara alipokuwa akikutana na rafiki yake, Iqram Maduro.
“Itakuwaje?”
“Nitakuwa bilionea mkubwa sana!”
“Kama ni hivyo, nitafurahi, ila kwa nini usianze kuwa na mademu wa kishua? Angalia unavyofagiliwa, kwa nini usimchukue hata Amanda. Demu ana pesa, atakutoa,” alisema Iqram.
“Hujui kichwa changu kinafikiria nini. Iqram, sifikirii laki, milioni wala bilioni. Kichwa changu kinafikiria trilioni,” alisema Richard.
“Trilioni?” aliuliza Iqram kwa mshtuko.
“Ndiyo! Nisikilize! Kuna siku nitazipata hizi pesa. Nakuambia ukweli, kuna siku nitazipata, nitakuchukua na kukupeleka Paris kwenye mnara wa Eiffel na nitakwambia Iqram I made it,” alisema Richard huku akionekana kuwa na imani kubwa ndani yake.
“Utafanikiwaje?”
“Hahah! Nimezungukwa na vichwa viwili hatari sana, yaani vichwa hatari mno, utaona,” alisema Richard huku akimwangalia Iqram.
“Basi wote tuseme Insh allah!” alisema Iqram huku akitabasamu.
Je, nini kitaendelea?
Tukutane kesho hapahapa.
SEHEMU YA 01
Wasichana zaidi ya kumi katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam walinyamaza ghafla huku macho yao yakimwangalia kijana mmoja ambaye alikuwa akipita mbele yao.
Mwendo wake ulikuwa wa taratibu sana, alitembea kwa kujiamini mno, alijua kwamba alikuwa mzuri wa sura, wanawake wengi walimbabaikia huku akizungumziwa sana midomoni mwao na ndiyo maana hata alipokuwa akitembea mbele ya wasichana, mwendo wake ulikuwa ni wa kunyata sana kana kwamba alikuwa akimsubiri mtu aliyekuwa nyuma yake.
Wote waliokuwa wakimwangalia walivutiwa naye, kulikuwa na wasichana ambao walitamani hata kumsimama kijana huyo na kuzungumza naye tu ili kesho waanze kuzusha kwamba walikuwa kwenye mahusiano ya kimapenzi pamoja naye lakini hilo halikuwezekana kabisa.
Kila mmoja alitulia na kumwangalia kwa makini kabisa, alikuwa kijana mwenye sura nzuri ambaye kila msichana chuoni hapo aliyemwangalia alitamani sana siku moja awe naye kimapenzi na kuwa mume wake wa ndoa. Kijana huyo aliitwa Richard Mawelle.
Richard alikuwa tofauti na vijana wengine, muda mwingi alikuwa kimya, hakuwa mzungumzaji hata kidogo, hakupenda mazoea na wasichana na ndiyo maana muda alipenda kujitenga huku kama ilikuwa ikitokea kuzungumza na watu wengine, basi alikuwa akiwafuata marafiki zake wawili, Robinson na Robert.
Wasichana walimbabaikia, mara kwa mara kulikuwa na ugomvi wa wasichana kwa wasichana, wengi walikuwa wakigombana kwa ajili yake, si kwamba walizungumza naye bali kujitamba mbele ya mashoga zao ndiyo hali iliyokuwa ikileta ugomvi katika chuo hicho.
Kulikuwa na makundi ya wasichana waliokuwa wakichukiana kisa Richard, kulikuwa na watu ambao kila walipoonana ilikuwa ni kugombana kisa kijana huyo ambaye wala hakuwa na taarifa na msichana yeyote yule.
Kutokupenda kwake wanawake kukamfanya watu kuanza kumfuatilia, walihisi kwamba kulikuwa na siri kubwa na nzito nyuma yake, ilikuwa ni vigumu kwa mvulana yeyote kutotaka kuwa kwenye mahusiano na msichana yeyote yule, hasa wasichana wengi warembo ambao walikuwa wakipatikana chuoni hapo.
Kwenye ufuatiliaji wao, hawakugundua kitu chochote kile, alikuwa mzima wa afya, hakuwa na urafiki na wanaume wengi, hao wawili, Robinson na Robert ndiyo walikuwa kila kitu kwake, alibadilishana nao mawazo na hata kujadili mambo mengi ambayo walitakiwa kufanya mara baada ya kumaliza chuo.
Kila siku Richard alikuwa mtu wa kupokea maboksi ya zawadi kutoka kwa wasichana mbalimbali, chuoni hapo ilikuwa ni kama ushindani, kila mmoja alitaka kumuonyeshea kijana huyo kwamba alikuwa akimpenda na alitakiwa kuuchukua moyo wake na kumfanyia lolote lile alilotaka.
“Richard...kwa nini unanifanyia hivi?” aliuliza msichana mmoja aliyeitwa Jesca ambaye alisimama mbele ya Richard.
Siku hiyo ilionekana kuwa kama muujiza, kijana huyo hakuwa akitoa nafasi ya kusimama na msichana yeyote yule, kwa Jesca ilikuwa ni bahati kubwa kwa kuwa alimkuta akifikiria mambo mengine kabisa, alimfuata kwa kushtukiza.
“Unasemaje?” aliuliza Richard huku akionekana kushtuliwa kutoka kwenye lindi la mawazo.
Msichana huyo akarudia maneno yake kwa mara nyingine huku Richard akimwangalia. Alitamani kumfukuza, hapo alipokuwa alikuwa akiwasubiria marafiki zake, Robinson na Robert ambao walipanga kuonana mahali hapo kwa ajili ya kuzungumza kitu cha muhimu sana.
Alisita kumfukuza kwa sababu kila mtu aliyekuwa canteen alikuwa akimwangalia yeye na msichana huyo ambaye aligoma kabisa kuondoka, alichokuwa akitaka ni kujua ukweli kama Richard alikuwa akimpenda au la.
Alichokifanya ni kusimama, akamshika mkono na kuanza kuondoka naye. Kila mmoja alishangaa, uondokaji wake haukuwa wa kawaida hata kidogo, ni kama kulikuwa na kitu kilichokuwa kikiendelea.
Waliokuwa wakitaka kuona mwisho wa mchezo ni kitu gani kingeendelea wakaanza kufuatilia kimyakimya, wale ambao hawakuwa mule canteen ambao walimuona Richard na msichana huyo wakiwa wameshikana mikono walipigwa na butwaa kwani kwa mwaka wa pili mfululizo walijaribu kuzungumza na Ricard lakini ilishindikana kabisa.
Siku hiyo ilikuwa ni kama kituko fulani hivi, safari yao hiyo iliishia katika bweni la wavulana ambapo moja kwa moja wakaelekea katika chumba alichokuwa akilala na kumuweka kitandani.
Jesca hakujua sababu ya kupelekwa mahali pale, alibaki akimshangaa Richard, alihisi kama kijana huyo alitaka kuzungumza naye lakini kwa jinsi alivyoonekana, hakuwa sawa kabisa.
“Jesca! Nisikilize kwa makini,” alisema Richard huku akimwangalia msichana huyo usoni.
“Sawa. Nakusikiliza baba,” alisema msichana huyo kwa adabu zote.
Richard alitaka kuzungumza kitu lakini akashindwa, alichokifanya ni kuchukua begi lake na kulifungua, humo akatoa kadi nyingi, maua, saa mpya, cheni na vitu vingine vingi ambavyo alitumiwa kama zawadi na wasichana mbalimbali chuoni hapo.
“Hebu niambie! Kati ya hawa wote na wewe nimkubali nani?” aliuliza Richard huku akimwangalia msichana huyo ambaye hakuwa akishangaa vitu vile kwani kwa jinsi Richard alivyokuwa mzuri wa sura, alistahili kuvipokea kutoka kwa wasichana hao.
“Richard....” aliita Jesca.
“Hebu nijibu kwanza! Nimkubali nani? Nyie mnanichanganya sana. Unajua mimi siangalia wanawake, mimi naangalia pesa, kichwa changu kinafikiria mambo mengi kuhusu pesa. Jesca, sina muda na wanawake,” alisema Richard huku akionekana kuwa na hasira mno.
Jesca alibaki kimya, alimwangalia Richard, kwa jinsi alivyokuwa akizungumza, mishipa ilivyomtoka ilionekana kabisa kwamba hakuwa na masihara hata kidogo, kile alichokuwa akimwambia ndicho ambacho alikimaanisha kutoka moyoni mwake.
Baada ya kunyamaza kwa sekunde kadhaa, Jesca akaanza kutabasamu, alijua dhahiri kwamba Richard alikasirika, hakutaka kumuona akiendelea kwenye hali hiyo na ndiyo maana akaamua kulitumia tabasamu lake kama silaha ya kumaliza hasira za Richard.
“Unacheka?” aliuliza Richard.
“Hapana! Natabasamu. Naomba nipige picha na wewe, nakuomba!” alisema Jesca huku akitoa simu yake aina ya iPhone X.
“Jesca....”
“Nakuomba,” alisema Jesca na kujivuta mbele ya Richard na kujipiga picha moja iitwayo ‘selfie’ kisha kuondoka mahali hapo.
Moyo wa Jesca ukauma mno, hakuamini kile alichokuwa ameambiwa. Alijiona kuwa msichana mrembo mno, alifuatiliwa na wanaume wengi lakini wote hao hawakuwa na nafasi kwake, mwanaume ambaye alikuwa akimpenda kwa mapenzi ya dhati alikuwa huyo Richard ambaye aliamua kumkataa na kumwambia kwamba hakufikiria mapenzi, moyo wake ulifikiria zaidi pesa.
Alitembea kwa kujiachia, kila mtu ambaye alimuona alipoingia ndani na Richard aliamini kwamba walimalizana vizuri na inawezekana kabisa msichana huyo alikubaliwa kwani hata tabasamu lililokuwa likionekana usoni mwake lilikuwa la matumaini tele.
Jesca aliamua kulitumia tabasamu lake kama kuficha kile kilichokuwa kimetokea ndani. Moyo wake ulikuwa kwenye maumivu makali mno, alilia kwa ndani lakini machoni mwake alionyesha kuwa na furaha kupita kawaida.
Alitembea mpaka kwenye bweni lao, akaingia mpaka chumbani na kulala kitandani kwake, hapo ndipo alipoanza kulia kwa uchungu mkubwa moyoni mwake.
Kwa miaka ishirini na mbili aliyokuwanayo alijiapiza kwamba ilikuwa ni lazima aendelee kuishi bikira mpaka siku ambayo angeolewa ili iwe zawadi kwa mume wake lakini kitu cha ajabu kabisa baada ya kuanza chuo na kumuona Richard, akaamua kuachana na ahadi yake kwa mume wake mtarajia hivyo kutaka bikira hiyo itolewe na kijana huyo.
“Richard! Kwa nini umenifanyia hivi?” aliuliza Jesca huku akiendelea kulia kama mtoto mdogo.
Wakati yeye akilia na kuomboleza, upande wa pili maisha ya Richard yalikuwa kama kawaida, alizoea kuyaona machozi ya wanawake, wale wachache ambao walibahatika kuzungumza naye wengi waliyatumia ili kumlaghai lakini msimamo wake ulikuwa uleule kwamba hakutaka kuwa na uhusiano na msichana yeyote yule mpaka pale ambapo angekuwa na pesa nyingi.
Kupendwa na wanawake haikuwa chuoni tu bali hata nyumbani kwao, Magomeni Mapipa Richard alikuwa gumzo, kila msichana aliyekuwa akimuona alimpenda, alivutiwa naye na kutamani kuwa naye lakini hali ilikuwa vilevile.
Wake za watu walikuwa kwenye wakati mgumu, hawakuweza kujizuia, waliwaambia wanawake wengine jinsi walivyokuwa wakimpenda kijana huyo ambaye hakuonekana kuwa na habari na msichana yeyote yule.
Ndoa nyingi zilitingishika, waume zao walikasirika lakini hawakuwa na la kufanya kwa kuwa walijua ukweli juu ya kijana huyo kwamba hakuwa mtu wa wanawake, aliishi maisha yake ya peke yake huku kila siku akiwaambia watu kwamba pamoja na umasikini aliokuwa nao na familia yake lakini kuna siku moja angekuja kuwa na pesa nyingi.
“Ipo siku. Iqram, ipo siku mshikaji wangu,” alisema Richard mara kwa mara alipokuwa akikutana na rafiki yake, Iqram Maduro.
“Itakuwaje?”
“Nitakuwa bilionea mkubwa sana!”
“Kama ni hivyo, nitafurahi, ila kwa nini usianze kuwa na mademu wa kishua? Angalia unavyofagiliwa, kwa nini usimchukue hata Amanda. Demu ana pesa, atakutoa,” alisema Iqram.
“Hujui kichwa changu kinafikiria nini. Iqram, sifikirii laki, milioni wala bilioni. Kichwa changu kinafikiria trilioni,” alisema Richard.
“Trilioni?” aliuliza Iqram kwa mshtuko.
“Ndiyo! Nisikilize! Kuna siku nitazipata hizi pesa. Nakuambia ukweli, kuna siku nitazipata, nitakuchukua na kukupeleka Paris kwenye mnara wa Eiffel na nitakwambia Iqram I made it,” alisema Richard huku akionekana kuwa na imani kubwa ndani yake.
“Utafanikiwaje?”
“Hahah! Nimezungukwa na vichwa viwili hatari sana, yaani vichwa hatari mno, utaona,” alisema Richard huku akimwangalia Iqram.
“Basi wote tuseme Insh allah!” alisema Iqram huku akitabasamu.
Je, nini kitaendelea?
Tukutane kesho hapahapa.