mapengo junior
JF-Expert Member
- Jun 28, 2011
- 1,135
- 276
- Thread starter
- #81
SIMULIZI; BALAA
MWANDISHI; HALFANI SUDY.
SIMU; 0757 633010
SEHEMU YA THELATHINI NA NANE
Kundi la Six killers walikuwa wamejipanga vizuri sana huko Kilwa Kivinje. Kutokana na kutokuwepo kwa Tano, ratiba zao zilibadirika kidogo. Kazi ya kumuwinda Dokta Yusha sasa alipewa Sita. Huku waliobaki walikuwa wanalinda eneo la chumba cha kuhifadhia maiti ili operesheni yao ya kutoa mioyo iliyotarajia kufanyika usiku wa siku hiyo iende vizuri. Kwa bahati nzuri siku hiyo ilitokea ajari ya basi katika kijiji cha Somanga. Ajari ilioua watu thelathini na kujeruhi saba, Six killers walikuwa na uhakika wa kupata mioyo thelathini ambayo, mara mbili ya oda yao, bahati ilioje?
Saa moja usiku Dokta Yusha alielekea Kilwa Kivinje. Kwenda kuwaangalia watu aliowapenda sana. Ambao sasa walikuwa wagonjwa, Mkewe kipenzi Nasra, rafiki wa mkewe, Hasina na mkwe wake. Njiani roho ilikuwa inamdunda sana, bila kujua kwanini hali ile ilimtokea. Laiti Dokta Yusha angejua anayoenda kukutana nayo huko basi angeusikiliza moyo wake, Dokta Yusha alikuwa anaenda kwenye balaa kubwa sana!
Na moyo wake uliligundua hilo mapema sana. Lakini hakuusiliza moyo wake, au labda hakuuelewa moyo wake unamaanisha nini?
Nusu saa ilitosha kumfikisha Dokta Yusha Kilwa Kivinje. Na moja kwa moja alienda katika wodi waliolazwa wakina Nasra. Hali ya wagonjwa wale wawili ilikuwa vilevile. Mkewe kipenzi Nasra na rafiki wa mkewe
Hasina walikuwa wamelala katika usingizi ule mbaya, usingizi nzito usiojulikana mwisho wake. Huku Mzee Mpaukha naye akiwa kalala kwa kujifunika nusu shuka safi ya hospitali, shuka iliiyoiashia kifuani, uso ukiwa wazi. Dereva alikuwa amejifunika shuka la hospitali gubigubi sawa na mgonjwa mwengine aliyelala kitanda cha pili toka pale alikolala dereva.
Kumbe jirani yule alikuwa ni Sita wa Six killers, akiwa amejificha kwa kujifunika gubigubi katika kitanda kimoja katika wodi ile. akiwa amepania kummaliza Dokta Yusha kabla hajaenda katika jukumu lake lengine la usiku ule.
Dokta Yusha kama kawaida yake alienda kwenye kitanda alicholala mkewe kipenzi, Nasra, alimwangalia kwa muda mkewe, bado alikuwa katika hali ya kutia shaka. Alipiga hatua chache na kukisogelea kitanda cha Hasina, nae alikuwa taabani kwa ajari ile. Alisogea tena hadi kitanda alicholazwa Mzee Mpaukha, Mzee Mpaukha alikuwa amelala, hakutaka kumsumbua, alimshuhudia akipumua vizuri. Alikiangalia kitanda alicholazwa dereva wa Mzee Mpaukha, alimwona amejifunika gubigubi. Alikisogelea taratibu kile kitanda, alikuwa anasogea Huku akiiona kuwa kitanda cha pili kutoka kitanda cha dereva Musa nacho kulikuwa na mgonjwa aliyejifunika gubigubi kama Musa, alipanga kwenda kumwangalia nae, bila kujua dhamira mbaya ya mgonjwa aliyelala kitanda kile. Kitanda kililaliwa na Sita wa Six killers. Na lengo lake kuu ni kumuuangamiza Dokta Yusha...
ITAENDELEA KESHO MUNGU AKIPENDA.
MWANDISHI; HALFANI SUDY.
SIMU; 0757 633010
SEHEMU YA THELATHINI NA NANE
Kundi la Six killers walikuwa wamejipanga vizuri sana huko Kilwa Kivinje. Kutokana na kutokuwepo kwa Tano, ratiba zao zilibadirika kidogo. Kazi ya kumuwinda Dokta Yusha sasa alipewa Sita. Huku waliobaki walikuwa wanalinda eneo la chumba cha kuhifadhia maiti ili operesheni yao ya kutoa mioyo iliyotarajia kufanyika usiku wa siku hiyo iende vizuri. Kwa bahati nzuri siku hiyo ilitokea ajari ya basi katika kijiji cha Somanga. Ajari ilioua watu thelathini na kujeruhi saba, Six killers walikuwa na uhakika wa kupata mioyo thelathini ambayo, mara mbili ya oda yao, bahati ilioje?
Saa moja usiku Dokta Yusha alielekea Kilwa Kivinje. Kwenda kuwaangalia watu aliowapenda sana. Ambao sasa walikuwa wagonjwa, Mkewe kipenzi Nasra, rafiki wa mkewe, Hasina na mkwe wake. Njiani roho ilikuwa inamdunda sana, bila kujua kwanini hali ile ilimtokea. Laiti Dokta Yusha angejua anayoenda kukutana nayo huko basi angeusikiliza moyo wake, Dokta Yusha alikuwa anaenda kwenye balaa kubwa sana!
Na moyo wake uliligundua hilo mapema sana. Lakini hakuusiliza moyo wake, au labda hakuuelewa moyo wake unamaanisha nini?
Nusu saa ilitosha kumfikisha Dokta Yusha Kilwa Kivinje. Na moja kwa moja alienda katika wodi waliolazwa wakina Nasra. Hali ya wagonjwa wale wawili ilikuwa vilevile. Mkewe kipenzi Nasra na rafiki wa mkewe
Hasina walikuwa wamelala katika usingizi ule mbaya, usingizi nzito usiojulikana mwisho wake. Huku Mzee Mpaukha naye akiwa kalala kwa kujifunika nusu shuka safi ya hospitali, shuka iliiyoiashia kifuani, uso ukiwa wazi. Dereva alikuwa amejifunika shuka la hospitali gubigubi sawa na mgonjwa mwengine aliyelala kitanda cha pili toka pale alikolala dereva.
Kumbe jirani yule alikuwa ni Sita wa Six killers, akiwa amejificha kwa kujifunika gubigubi katika kitanda kimoja katika wodi ile. akiwa amepania kummaliza Dokta Yusha kabla hajaenda katika jukumu lake lengine la usiku ule.
Dokta Yusha kama kawaida yake alienda kwenye kitanda alicholala mkewe kipenzi, Nasra, alimwangalia kwa muda mkewe, bado alikuwa katika hali ya kutia shaka. Alipiga hatua chache na kukisogelea kitanda cha Hasina, nae alikuwa taabani kwa ajari ile. Alisogea tena hadi kitanda alicholazwa Mzee Mpaukha, Mzee Mpaukha alikuwa amelala, hakutaka kumsumbua, alimshuhudia akipumua vizuri. Alikiangalia kitanda alicholazwa dereva wa Mzee Mpaukha, alimwona amejifunika gubigubi. Alikisogelea taratibu kile kitanda, alikuwa anasogea Huku akiiona kuwa kitanda cha pili kutoka kitanda cha dereva Musa nacho kulikuwa na mgonjwa aliyejifunika gubigubi kama Musa, alipanga kwenda kumwangalia nae, bila kujua dhamira mbaya ya mgonjwa aliyelala kitanda kile. Kitanda kililaliwa na Sita wa Six killers. Na lengo lake kuu ni kumuuangamiza Dokta Yusha...
ITAENDELEA KESHO MUNGU AKIPENDA.