Riwaya - Balaa

Riwaya - Balaa

SIMULIZI; BALAA
MWANDISHI; HALFANI SUDY
SIMU; 0757 633010

SEHEMU YA ISHIRINI NA MBILI

Usiku uleule Tano alienda Kilwa Masoko. Kummaliza Mwanasheria. Alijua kumuacha hai Mwanasheria basi habari juu ya kidonda kilichoibuka ghafla katika kifua cha mama Mpaukha itaendelea kusambaa. Ilikuwa ni lazima kumuuwa Mwanasheria ili kumziba mdomo milele !

Usiku wa saa nne usiku ulimkuta Mwanasheria akinywa bia katika baa ya Tiga Tisa. Alikunywa bia nyingi sana. Tangu saa kumi na mbili jioni alikuwa hapo akipata ulabu.

Meza ya tatu toka pale alipokaa Mwanasheria kulikuwa na mgeni. Mgeni aliyewasiri pale majira ya saa tatu usiku. Mgeni huyo alikuwa makini kwa kila alichokuwa anakifanya Mwanasheria. Mgeni huyo hakuwa mwengine ila ni Tano wa Six Killers. Alikuwa anamsubiri mwanasheria anyanyuke ili akamfanye alichotaka kwenda kumfanya.

Saa tano usiku Mwanasheria alinyanyuka pale kwenye kiti. Tayari kuelekea nyumbani kwake. Alisogea taratibu kwenye gari yake, alipanda na kuliwasha. Safari kwenda nyumbani kwake ilianza. Tano naye alitoka pale Tiga Tisa. Alichukua pikipiki yake na kulifuata gari la Mwanasheria kwa nyuma.
Mwanasheria alikuwa amelewa hasa. Alipoteza kabisa umakini na hakutambua kabisa kama alikuwa anafuatwa. Alifika nyumbani kwake na kuingia ndani. Kutokana na ulevi Mwanasheria alijikuta amelala katika sofa pale sebuleni.

Tano alipaki pikipiki yake kwa nje. Alifika hadi mlangoni katika nyumba ile ya Mwanasheria. Kwa bahati mbaya nyumba ile haikuwa na fensi.
Kwa kutumia funguo malaya alifungua mlango wa sebule wa Mwanasheria. Ilikuwa ni kazi ndogo sana, kazi iliyodumu kwa dakika tatu. Alifungua mlango na kumkuta Mwanasheria amelala pale sebuleni kama mzoga. Alichomoa kisu chake mkononi. Kwa mwendo wa kunyata akawa anamsogelea pale sofani.
Akamtikisa kidogo, Mwanasheria hakuamka, alikuwa amelewa sana pombe. Alimtikisa tena. Nia ya Tano ni kumuamsha Mwanasheria ili kumjua mtu wa pili aliyedakia ile simu wakati yeye anaongea na Dokta Yusha. Lakini Mwanasheria hakuamka.
Tano aliamua kuua tu, akijipa moyo atamjua tu huyo mtu. Alirudisha nyuma ule mkono uliishika kisu, kwa nguvu aliungiza katika tumbo la Mwanasheria, akatoa akaingiza tena. Alirudia mara nne.Mwanasheria akakata roho akiwa amelewa.

Tano alitoka nje huku akiwa na furaha tele. Bila kujua kama alimuua mtu asiye sahihi. Yeye alimuua Mwanasheria wa Halmashauri ya wilaya ya Kilwa, Ndugu Juma Ngozi. Wakati Mwanasheria aliyeongea na Dokta Yusha, Mwanasheria mlevi alikuwa kilabuni wakati ule, akinywa pombe na kupigizana kelele na kina mama Kindumba...

ITAENDELEA MUNGU AKIPENDA.
 
SIMULIZI; BALAA
MWANDISHI; HALFANI SUDY
SIMU; 0757 633010

SEHEMU YA ISHIRINI NA TATU

Usiku uleule Tano alirudi Kilwa Kivinje. Kuendelea na kazi yake ya ulinzi pamoja kumuwinda Dr Yusha. Maana usiku wa siku hiyo pia, ilikuwa lazima waipata mioyo kumi na tano katika chumba cha kuhifadhia maiti. Alifika Kivinje mishale ya saa tano usiku. Na kuikuta kazi ya kutoa mioyo imeshaanza.

Asubuhi mji wa Kilwa Masoko uliamka na taarifa mbaya tena. Taarifa ya kifo cha Mwanasheria wa Halmashauri ya wilaya Kilwa, Ndugu Alex Mwasola. Mwasola alikutwa ameuwawa nyumbani kwake. Muuza maziwa ndiye aliyekuwa mtu wa kwanza kushuhudia maiti ya Mwasola. Alikuwa na ratiba ya kumpelekea maziwa kila siku. Siku hiyo aligonga sana mlango nje, aliposukuma mlango ulifunguka na alipoingia ndani, alilakiwa na maiti ya bosi wake. Mwili wa Mwanasheria Mwasola, umelala juu ya sofa huku ukiwa umetapakaa damu kifuani. Alirudi nyuma na kuondoka bila kuaga. Hakumsimulia mtu kuhusu tukio lile, muuza maziwa aligeuka bubu.

Halmashauri ya wilaya ya Kilwa, katika ofisi ya Mwanasheria watu walikuwa wamejaa. Ilikuwa siku ya kazi kwahiyo watu walijaa kufata huduma katika ofisi hiyo, watu wengi walikuwa wamekaa nje ya ofisi hiyo kwa kadri ya saa tano, bila Mwanasheria kutokea. Walijaribu kumpigia simu lakini simu yake iliita bila kupokelewa. Bahati mbaya Mwasola alikuwa hajaoa na wala hakai na mtu yeyote nyumbani kwake. Ilibidi atumwe mlinzi kwenda kwa Mwanasheria kumwangalia. Ilipo ofisi ya mwanasheria na mtaa wa National hakukuwa mbali sana. Yule mlinzi aliyetumwa kwa Mwanasheria alikutana na balaa.
Picha mbaya kama aliyokutana nayo Muuza maziwa. Mwili wa Mwanasheria ukiwa umelala sofani huku kisu kikiwa kinaning'inia kifuani mwake, na damu zilizoanza kukauka kifuani. Yule mlinzi alishindwa kuvumilia, alipiga makelele, makelele yaliyowajaza kwa kasi majirani...

ITAENDELEA MUNGU AKIPENDA.
 
SIMULIZI; BALAA
MWANDISHI; HALFANI SUDY
SIMU; 0757 633010

SEHEMU YA ISHIRINI NA TATU

Usiku uleule Tano alirudi Kilwa Kivinje. Kuendelea na kazi yake ya ulinzi pamoja kumuwinda Dr Yusha. Maana usiku wa siku hiyo pia, ilikuwa lazima waipata mioyo kumi na tano katika chumba cha kuhifadhia maiti. Alifika Kivinje mishale ya saa tano usiku. Na kuikuta kazi ya kutoa mioyo imeshaanza.

Asubuhi mji wa Kilwa Masoko uliamka na taarifa mbaya tena. Taarifa ya kifo cha Mwanasheria wa Halmashauri ya wilaya Kilwa, Ndugu Alex Mwasola. Mwasola alikutwa ameuwawa nyumbani kwake. Muuza maziwa ndiye aliyekuwa mtu wa kwanza kushuhudia maiti ya Mwasola. Alikuwa na ratiba ya kumpelekea maziwa kila siku. Siku hiyo aligonga sana mlango nje, aliposukuma mlango ulifunguka na alipoingia ndani, alilakiwa na maiti ya bosi wake. Mwili wa Mwanasheria Mwasola, umelala juu ya sofa huku ukiwa umetapakaa damu kifuani. Alirudi nyuma na kuondoka bila kuaga. Hakumsimulia mtu kuhusu tukio lile, muuza maziwa aligeuka bubu.

Halmashauri ya wilaya ya Kilwa, katika ofisi ya Mwanasheria watu walikuwa wamejaa. Ilikuwa siku ya kazi kwahiyo watu walijaa kufata huduma katika ofisi hiyo, watu wengi walikuwa wamekaa nje ya ofisi hiyo kwa kadri ya saa tano, bila Mwanasheria kutokea. Walijaribu kumpigia simu lakini simu yake iliita bila kupokelewa. Bahati mbaya Mwasola alikuwa hajaoa na wala hakai na mtu yeyote nyumbani kwake. Ilibidi atumwe mlinzi kwenda kwa Mwanasheria kumwangalia. Ilipo ofisi ya mwanasheria na mtaa wa National hakukuwa mbali sana. Yule mlinzi aliyetumwa kwa Mwanasheria alikutana na balaa.
Picha mbaya kama aliyokutana nayo Muuza maziwa. Mwili wa Mwanasheria ukiwa umelala sofani huku kisu kikiwa kinaning'inia kifuani mwake, na d ht 4 kwa sikuamu zilizoanza kukauka kifuani. Yule mlinzalishindwa kuvumilia, alipiga makelele, makelele yaliyowajaza kwa kasi majirani...

ITAENDELEA MUNGU AKIPENDA.

uongeze plz
 
SIMULIZI; BALAA
MWANDISHI; HALFANI SUDY

SEHEMU YA ISHIRINI NA TANO

Walimkuta Mwanasheria ameuwawa!
Illikuwa majonzi na kilio kikubwa sana kwa majirani.
Baada ya muda mfupi, askari Polisi waliwasiri. Haikujulikana hata ni nani aliyewapigia simu Polisi hao.
Walianza kufanya uchunguzi mle ndani, baadae wakauchukua mwili wa Mwanasheria na kuupeleka hospitali kwa ajili ya uchunguzi zaidi.

Muda mfupi tu habari za kifo cha Mwanasheria zikasambaa Kilwa nzima. Zilisambaa mpaka kilabuni na kumfikia Mwanasheria mlevi.

Taarifa za kuuwawa kwa Mwanasheria zilimstua sana Mwanasheria mlevi. Alilala kilabuni siku ile Mwanasheria. Na aliyemletea taarifa za mauaji hayo ni rafiki yake kipenzi katika ulevi, mama Kindumba.

"Mwanaaa" Mama kindumba aliita kilevi huku akifupisha jina la Mwanasheria.
"Nambie mama kindumba" Mwanasheria nae aliitikia kwa sauti ya kilevi pia.
"Umesikia wajina wako kauwawa!"
"Nani tena?"
"Mwanasheria"
"Mama kindumba unaumwa nini, Mwanasheria si mimi hapa" "Mwanasheria wa ukweli bana"
"Unaamaanisha Bwana Mwasola?"
"Ndiyo huyo huyo"
"Haaaa!"
"Ndo hivyo wamemkuta kapigwa bonge la kisu nyumbani kwake"
"Aisee, lakini poa bora nibaki Mwanasheria peke yangu"

Mwanasheria mlevi alitia mzaha uliomchekesha kila mtu pale kilabuni. Bila kujua balaa iliyoko ndani yake..
"Ngoja nimpigie Dokta Yusha alikuwa rafiki yake sana"

Simu hiyo ya Mwanasheria kwenda kwa Dokta Yusha ilizua kizaazaa kipya..

ITAENDELEA
MUNGU AKIPENDA
 
SIMULIZI; BALAA
MWANDISHI; HALFANI SUDY
SIMU; 0757 633010

SEHEMU YA ISHIRINI NA SITA

"Hallo Dokta Yusha "
"Nambie Mwanasheria"
"Una taarifa za msiba Dokta"
"Nani tena amefariki Mwanasheria?"
"Mwanasheria Mwasola ameuwawa!
" Acha utani Mwanasheria, Mwasola ameuwawa! "
"Kachomwa kisu Dokta"
"Etiiiii"
"Ndiyo hivyo Dokta"
"Nakuja Masoko sasa hivi, ahsante sana kwa taarifa Mwanasheria"
Simu ikakatwa.

Dokta Yusha aliipokea simu ile akiwa katika benchi la wagonjwa. Lakini mtu wa pembeni yake hakuwa mgonjwa, alikuwa ni Tano wa Six killers, katika harakati zake za kumuwinda Dokta Yusha. Alisikia kila kitu alichoongea Dokta Yusha, huku akishangazwa na taarifa kwamba Mwanasheria kauwawa ilhali Dokta alikuwa anaongea na Mwanasheria.

Dokta Yusha alinyanyuka pale kwenye benchi, akiwa na Lengo la kwenda Kilwa Masoko kwenye msiba. Alipanda gari yake na kuondoka bila ya kujua kama kuna mtu alikuwa anamfata nyuma kwa kutumia pikipiki. Sasa Tano aliamua kuumaliza mchezo, kumuua Dokta Yusha kisha kwenda Kilwa Masoko kumuua huyo Mwanasheria mpya!
Hii inaitwa LIWALO NA LIWE! Tano aliona mchezo unaelekea kubaya, aliamua kuumaliza leo!

Walipofika karibu na kijiji cha Mpara gari la Dokta Yusha lilipata tatizo la kiufundi, lilizima ghafla na kusimama. Ilikuwa bahati mbaya kwa Dokta Yusha..na bahati nzuri sana kwa Tano wa Six killers.

ITAENDELEA KESHO MUNGU AKIPENDA.
 
SIMULIZI; BALAA
MWANDISHI; HALFANI SUDY
SIMU; 0757 633010

SEHEMU YA ISHIRINI NA NANE.

Dokta Yusha alisimamisha gari. Na kuanza kulikagua, Tano nae alisimama pale na pikipiki yake.
Hatari ilikuwa inamkaribia Dokta Yusha!

"Vipi tena kaka" Tano aliuliza huku alimsogelea Dokta Yusha.
"Gari linanisumbua kidogo" Dokta alijibu huku akilichungulia gari lake kwa chini, uvunguni.
"Ngoja nikusaidie kidogo"
"Sawa"

Dokta Yusha alifanya kosa, kukaribiana na Tano, tena wakiwa wawili porini lilikuwa ni kosa kubwa sana. Tano hakuelekea kwenye gari, Tano alimfata Dokta Yusha pale chini. Dokta Yusha alimtazama yule jamaa na kuingiwa na woga kidogo, alishangaa jinsi ya yule dereva pikipiki alivyokuwa anamfata kwa kasi, tena kishari!
Dokta Yusha nae alisimama, alijipanga kwa shari yoyote.

Tano alitoa kitu kwenye mfuko wa ndani wa koti, ilikuwa bastola!
Sasa Dokta Yusha hakuwa na mshangao tena, alikuwa makini. Kitu ambacha Tano alikuwa hajui, Dokta Yusha alikuwa amepitia mafunzo ya uaskari kabla ya kuwa dokta, mafunzo ya uaskari magereza huko Kiwira, Mbeya. Na kufanya kazi kama askari magereza mkoani Mtwara. Dokta Yusha hakuwa mgeni kuitumia bunduki, hakuwa mgeni wa kutazamana na bastola. Ndio maana bastola aliyooneshwa na Tano haikumtisha kabisa, zaidi ilimuongezea umakini.

Tano yeye alimchukulia Dokta Yusha kama raia wa kawaida, raia ambaye atatetemeka baada ya kuoneshwa bastola, au labda atajikojolea baada ya kuona bastola ikimuelekea usoni mwake.
Lakini haikuwa hivyo kwa Dokta Yusha!

Tano na Dokta Yusha walikaribiana sana, Tano alifanya kosa la kiufundi, alimkaribia sana Dokta Yusha na ukaribu ule ulizua jambo!

Dokta Yusha alirudisha nyuma mguu wake wa kulia, na kuuleta mbele kwa kasi na nguvu kubwa sana!
Mtindo wa kuupeleka mguu namna ile huitwa teke!
Teke lile la Dokta Yusha lilifika ulipokuwa mkono wa Tano ambao ulikuwa umeshika bastola, bastola ilisukumwa kwa kasi na kujisweka pembeni ya barabara. Sasa Dokta Yusha na Tano walibaki mikono mitupu, wakitazamana kama majogoo!

ITAENDELEA JIONI MUNGU AKIPENDA.
 
SIMULIZI; BALAA
MWANDISHI; HALFANI SUDY
SIMU; 0757 633010

SEHEMU YA ISHIRINI NA TISA

Tano alitabasamu, alifurahi sana na ujanja aliouonesha Dokta Yusha, alimuona kama amejipalia mkaa wa moto, Tano alijiweka vizuri kimapambano!

Dokta Yusha naye hakutetereka, hakutetemeka, alimwangalia jinsi Tano alivyosimama na kupanga ngumi, yeye alikuwa amesimama tu kawaida.
Tano alimfata Dokta Yusha kwa kasi kwa teke lilikuwa linaelekea tumboni kwa Dokta Yusha, kwa kasi ya ajabu Dokta Yusha alijisogeza pembeni kidogo, kukwepa lile teke. Tano akapita kwa kasi na lile teke lake hadi pembeni mwa barabara kwenye nyasi fupi. Tano alisimama tena huku akiwa amefura kwa hasira, kukwepa vile na Dokta Yusha ilikuwa ni dharau kubwa sana kwake, akajipanga tena upya, kwa bahati mbaya alikuwa anaongozwa na hasira. Ni kosa kubwa sana katika mapambano kuongozwa na hasira.

Dokta Yusha alicheka kwa sauti kubwa kwa dharau, alicheka kwa lengo la kuzidi kumtoa Tano wa Six killers mchezoni, na kweli kicheko kile kilipokelewa tofauti kabisa na Tano muuaji, kicheko kiliibadirisha ile hasira ya Tano na kuigeuza kuwa jazba!
Dokta Yusha alifanya vile makusudi, kwa jinsi alivyomuona amesimama Tano na jinsi alivyopanga ngumi, alijua Tano siyo wa kiwango chake. Tano alikuwa mahiri zaidi yake. Sasa alikuwa anatumia mbinu ya kumpandisha hasira Tano ili apoteze umakini, huku yeye akifikiria namna ya kujiokoa na alifanikiwa tena kwa hilo!

Tano alifura kwa hasira na jazba ya hali ya juu. Moyoni mwake kulikuwa kunafukuta!

Alirusha ngumi kwa mkono wake wa kulia, ngumi ya nguvu iliyorushwa na mtu mwenye nguvu, Dokta Yusha alijaribu kuikwepa, lakini hakufanikiwa kuikwepa yote, mkwaruzo wa ngumi ile ulimpata kidogo katika sehemu ndogo ya mbavu ya kushoto, alisikia maumivu kidogo, lakini hakutaka kuonesha kama alisikia maumivu, Tano hakusubiri, ngumi ya kushoto sasa ilikuwa inaelekea katika mwamba wa pua wa Dokta Yusha, kwa kasi na umakini Dokta Yusha alifanya mambo mawili ya kustaajabisha sana...

ITAENDELEA KESHO MUNGU AKIPENDA.
 
SIMULIZI; BALAA
MWANDISHI; HALFANI SUDY

SEHEMU YA THELATHINI.

Dokta Yusha, aliikwepa ile ngumi, huku nae akipiga ngumi yake kwa nguvu iliyotua barabara katika mbavu za Tano!
Tano hakuamini kasi aliyoitumia Dokta Yusha kukwepa ngumi ile, pia hakuamini uzito wa ngumi wa Dokta Yusha, sasa tano akajua anapambana na mtu anayejua anachokifanya. Hakujiuliza tena, sasa aliamua kupiga mapigo ya kifo, mapigo ambayo yakimgusa mpigwaji yanaondoka na roho yake....Balaa!
Tano alianza na teke lilikwenda kwa kasi kama umeme, teke liliombatana na uzito wa kilo kadhaa. Dokta Yusha aliliona teke lile, teke liliolekezwa shingoni kwa lengo ya kuondoka na shingo yake, aliinama kidogo, teke likapita, ila upepo wa teke lile ulimyumbisha Dokta Yusha na kumdondosha chini, akiwa amelala pale chali, tano aliruka juu na kushuka chini huku akiwa amekitanguliza kifuti cha mguu wake wa kushoto, kifuto kilichoelekezwa katika upande wa kushoto wa kifua dokta Yusha, pale unapokaa moyo!
Dokta Yusha alijisogeza kidogo pale chini akiwa amelala vile vile, na kifuti cha dokta Yusha kutua katika lami, nguvu iliyoambatana na kifuti kile, na kutua kwenye lami ngumu, goti la Tano liligeuka palepale!
Tano alitoa ukelele mkubwa sana. Dokta Yusha alisimama na kwenda pale alipolala Tano huku akiwa amelishikia goti lake.
Dokta Yusha alijisachi mfukoni, na kutoa simu yake ya mkononi. Aliitafuta namba ya OCD ya kilwa, na kumpigia. Alimuelekeza kila kitu kilichotokea pale barabarani, na OCD alimwambia kwamba watafika askari pale baada ya muda mfupi.

Tano hakuwa na ujanja wowote, alikaa pake huku akilia, akisubiri hatma yake, mambo yalikuwa yameshaharibika..

ITAENDELEA KESHO MUNGU AKIPENDA.
 
SIMULIZI; BALAA
MWANDISHI; HALFANI SUDY
SIMU; 0757 633010

SEHEMU YA THELATHINI MOJA

Baada ya muda mfupi gari la polisi lilifika, likiwa na askari polisi sita waliovaa sare zao safi za jeshi la Polisi, wakiwa imara na bunduki mkononi kila mmoja. Walimbeba Tano na kumpakia nyuma ya gari ile ya Polisi. Dokta Yusha alipanda mbele ya gari ile, na safari ya kuelekea kituo cha polisi Masoko ilianza.

Dakika kumi zilitosha kuwafikisha askari wale wakiwa na Tano wa Six Killers katika kituo cha Polisi cha Masoko. Askari wawili walimshusha Tano msobemsobe, hawakujari kabisa makelele yake aliyokuwa anayapiga kutokana na maumivu akiyoyapata kutoka na maumivu ya kwenye goti. Kwa bahati mbaya askari wale hawakuwa na huruma kwa Tano, kwa kuwa hawakuwahi kufundishwa kumuonea huruma Mhalifu katika mafunzo huko chuoni Moshi.
Tano aliingizwa ndani ya kituo cha Polisi tayari kwa kuanza kuhojiwa.

Na alivyowekwa tu katika sakafu ya Polisi alikumbana na maswali mfululizo toka kwa askari wale. Kila askari alikuwa anauliza swali lake kwa sauti kubwa na ukali.
Tano alihisi kama wanampigia kelele, hakujibu kitu, alinyamaza kimya!

Dokta Yusha yeye aliitwa ofisini kwa mkuu wa upepelezi Wilaya. Alieleza kila kitu kilichotokea tangu alipopokea ile simu ya Mwanasheria mlevi. Simu iliyomtaarifu juu ya msiba wa Mwanasheria wa Halmashauri ya wilaya ya Kilwa, nae kuamua kwenda kilwa Masoko kwenye msiba.

Dokta Yusha alivyomaliza maelezo yake tu hapohapo wakatumwa askari kwenda kumkamata Mwanasheria. Mkuu wa upelelezi wa wilaya alihisi Mwanasheria mlevi anahusika na mbinu zile chafu!
Askari walewale waliomleta Tano waliingia tena kazini kumtafuta Mwanasheria mlevi popote alipo...

ITAENDELEA MUNGU AKIPENDA.
 
SIMULIZI; BALAA
MWANDISHI; HALFANI SUDY
SIMU; 0757 633010

SEHEMU YA THELATHINI NA MBILI

Mwanasheria bado alikuwa kilabuni, hana hili wala lile. Alikuwa anakunywa pombe huku akiongea neno kila linalomjia kichwani mwake. Bila kujua kama askari sita wenye silaha walikuwa njiani wanaelekea pale kilabuni kumkamata yeye, akituhumiwa kupanga mauaji ya Dokta Yusha!

Ghafla! Vumbi lilitimka pale kilabuni, gari ya Polisi lilifunga breki kali sana! Askari walikuwa wameshuka kabla hata ya breki ile. Walishuka kwa mbwembwe na bunduki zao mikononi. Walevi walitimka mbio, pombe zote ziliwatoka vichwani.

Mwanasheria mlevi hakusogea hata hatua moja, alikuwa ameshazungukwa na askari polisi watatu. Midomo ya bunduki ikielekezwa kichwani kwake!
Mwanasheria hakuwa jasiri kama Dokta Yusha, yeye alikuwa anatetemeka, hakuweza kuuzuia kabisa mkojo usimtoke.
Kuelekezwa bunduki kichwani kwake ? Hakuwahi kufikiria hata siku moja.
Alikosa la kusema, askari walimuamuru asimame, na kumuelekeza pa kuelekea, ndani ya gari ya Polisi. Alifika ndani ya gari, na kukaa chini bila kuambiwa..machozi yalimtoka na kudondoka katika sakafu ya bodi ya gari ile. Askari hawakulijari lile chozi, hawakuwa na muda wa kulijari chozi la Mhalifu, walidandia gari na kuondoka kwa kasi kubwa sana, safari kituo cha Polisi Masoko.

Walipofika kituo cha Polisi, Polisi hawakuuliza, ilikuwa ni mateke, ngumi na vifuti kwa Mwanasheria mlevi. Polisi walikuwa wanampiga Mwanasheria bila kujua kwanini wanampiga, na Mwanasheria nae hakujua kwanini anapigwa!
Mwanasheria alipoteza fahamu kituo cha polisi !

ITAENDELEA KESHO MUNGU AKIPENDA.
 
Naanza kona dalili za kutuambia umepata mfadhili amekuambia utoe kitabu. Kama hamna uhakika wa kumaliza kusimulia hadithi zenu kwa nini mnaziweka hapa? Mnakera sana.
 
Back
Top Bottom