SIMULIZI; BALAA
MWANDISHI; HALFANI SUDY
SIMU; 0757 633010
SEHEMU YA THELATHINI NA TATU
Wote wawili Tano na Mwanasheria walipelekwa kituo cha afya Masoko, chini ya ulinzi mkali sana wa askari Polisi.
Kama ilivyo kawaida katika hospitali nyingi Tanzania, wahalifu huwa hawapati huduma nzuri pindi wanapoumwa. Labda kwa kuwa wanakuwa hawana wauguzi wa kuwapa pesa wagonjwa
( hongo).
Hali hiyo iliwakuta Tano na Mwanasheria pale kituo cha afya Masoko. Waliachwa wamelala katika kitanda vyao wakiwa na pingu zao mikononi.
Saa kumi na mbili jioni, Mwanasheria alizinduka, ni kudra za Mungu tu ndizo zilimuasha. Mwanasheria hakupata huduma yoyote ile pale kituo cha afya. Mwanasheria aliamka na maneno yake, Mwanasheria aliamka na lawama za kutosha, lawama kwa Polisi, lawama kwa Serikali, lawama kwa mfumo mzima wa nchi, lakini lawama hazikusaidia, ukweli ulibaki palepale, Mwanasheria alikuwa amelala kitandani akiwa hoi bin taaban na pingu zake kitandani !
Tano wa Six killers naye alikuwa katika wakati mgumu sana, mguu wake ulikuwa umeumia vibaya sana, alikuwa anagugumia kwa maumivu. Lakini hakuwa na jinsi, alikuwa amelala katika kitanda kidogo cha kituo cha kituo cha afya akiwa dhooful hali, huku akiwa hana namna ya kuwapigia wenzie ili awataarifu kwamba alikuwa mahali pale, kwa kuwa simu yake ilikuwa katika kituo cha Polisi.
Kundi la six killers walikutana kwa kikao cha dharura. Kikao kilichokuwa kinaoongozwa na Don Genge mwenyewe, kikiwa na ajenda kuu mbili.
Ajenda ya kwanza ilikuwa ni makabidhiano ya mioyo kumi na tano iliyipatikana kwa siku ile ya pili. Mambo yalienda sawa, na Dokta Sharifa alikabidhi deli kubwa jekundu lenye mioyo kumi na tano.
Ajenda ya pili, ilikuwa inahusu kutoonekana kwa Tano. Masaa zaidi ya kumi na tatu Tano alikuwa hajaonekana, na siku yake ilikuwa haipatikani!
"Hii ni siku ya tatu ya Mpango huu, kwa asilimia 90 mpango wetu umeenda sawa, lakini Kwa bahati mbaya sisi hatufanyi kazi kwa asilimia 90. Huwa tunafanya kazi kwa asilimia 100, au zaidi ya hizo ikiwezekana. Tano hajulikani alipo, na hizo ndio asilimia 10 tulizozipoteza. Natoa masaa mawili, Tano akiwa hai au mwili wake uwe hapa!.
Baada ya masaa hayo mawili, tutaenda kutoa mioyo tukiwa na Tano kama atabahatika kuwa hai, mmebaki wa tano, hakikisheni mnarudi na Tano! Mnaweza kwenda..."
Six killers walitoka mle ndani kwa lengo kuu moja, kwenda kumtafuta muuaji aliyepewa namba Tano....
ITAENDELEA MUNGU AKIPENDA.