mapengo junior
JF-Expert Member
- Jun 28, 2011
- 1,135
- 276
- Thread starter
- #101
SIMULIZI; BALAA
MWANDISHI; HALFANI SUDY
SIMU; 0757 633010
SEHEMU YA AROBAINI NA NANE
Dokta Yusha alichoka, alikaa chini ili kusubiri kukiona kifo cha njaa jinsi kinavyokuwa.
Saa kumi kamili alfajiri ilimkuta Dokta Yusha akiwa macho. Alikuwa hajasinzia hata kidogo, muda wote alikuwa anafikiria namna ya kutoka katika chumba kile lakini hakupata namna ya kutoka.
Mara, alisikia tena kelele za mlango kwa nje, ishara kama ya mwanzo kuwa mlango ulikuwa unafunguliwa.
'Ama zake, ama zangu!'
Aliingia tena Sita, akiwa kashika bunduki aina ya SMG mkononi. Alisimama pale mlangoni na kumwangalia Dokta Yusha. Sita wa Six killers alikuwa ameenda kuhakikisha tu kama Dokta Yusha hajafanya ujanja wowote wa kujaribu kutaka kutoroka. Sita alimshuhudia Dokta Yusha akiwa amekaa palepale alipomwacha awali. Akadanganyika kwamba Dokta Yusha hajafanya kitu chochote kile cha kujaribu kutoroka.
Alijidanganya. Dokta Yusha alitafuta sana njia ya kutoka mle ndani lakini hakuipata.
Sita aligeuka nyuma ili arudi nje kuendelea na lindo lake.
Kwa kasi ya haraka Dokta Yusha alinyanyuka pale chini na kupiga hatua mbili kubwa sana, hatua zilizomfikisha mpaka pale mlangoni. Alipokuwa Sita wa Six killers.
Wakati Sita anataka kugeuka nyuma kujua sababu ya vishindo viwili alivyovisikia, alichelewa sana!
Alikuwa kakabwa vizuri sana na Dokta Yusha. Kabali maridadi iliyomtetemesha Sita na kuidondosha bunduki chini.
Dokta Yusha hakujari, alimvuta Sita kwa nyuma kwa nguvu. Mwanzoni Sita alijikomaza lakini baadae Ilibidi ajilegeze, maana kukomaa ilimaanisha kuumizwa zaidi na ile kabali.
Kujilegeza nako lilikuwa kosa kubwa sana alilolifanya Sita. Kosa ambalo atalijutia mpaka kesho, kama kuna maisha baada ya kilichomtokea pale. Dokta Yusha alimvuta Sita kwa nguvu na kujikuta akimsukumia pale katika kiti cha kifo!
Balaa!
Sita alibadirika naye, mwili ulibadirika sambamba na kiti, Ilikuwa ni rangi nyekundu mithili ya tanuru la moto!
ITAENDELEA KESHO MUNGU AKIPENDA.
MWANDISHI; HALFANI SUDY
SIMU; 0757 633010
SEHEMU YA AROBAINI NA NANE
Dokta Yusha alichoka, alikaa chini ili kusubiri kukiona kifo cha njaa jinsi kinavyokuwa.
Saa kumi kamili alfajiri ilimkuta Dokta Yusha akiwa macho. Alikuwa hajasinzia hata kidogo, muda wote alikuwa anafikiria namna ya kutoka katika chumba kile lakini hakupata namna ya kutoka.
Mara, alisikia tena kelele za mlango kwa nje, ishara kama ya mwanzo kuwa mlango ulikuwa unafunguliwa.
'Ama zake, ama zangu!'
Aliingia tena Sita, akiwa kashika bunduki aina ya SMG mkononi. Alisimama pale mlangoni na kumwangalia Dokta Yusha. Sita wa Six killers alikuwa ameenda kuhakikisha tu kama Dokta Yusha hajafanya ujanja wowote wa kujaribu kutaka kutoroka. Sita alimshuhudia Dokta Yusha akiwa amekaa palepale alipomwacha awali. Akadanganyika kwamba Dokta Yusha hajafanya kitu chochote kile cha kujaribu kutoroka.
Alijidanganya. Dokta Yusha alitafuta sana njia ya kutoka mle ndani lakini hakuipata.
Sita aligeuka nyuma ili arudi nje kuendelea na lindo lake.
Kwa kasi ya haraka Dokta Yusha alinyanyuka pale chini na kupiga hatua mbili kubwa sana, hatua zilizomfikisha mpaka pale mlangoni. Alipokuwa Sita wa Six killers.
Wakati Sita anataka kugeuka nyuma kujua sababu ya vishindo viwili alivyovisikia, alichelewa sana!
Alikuwa kakabwa vizuri sana na Dokta Yusha. Kabali maridadi iliyomtetemesha Sita na kuidondosha bunduki chini.
Dokta Yusha hakujari, alimvuta Sita kwa nyuma kwa nguvu. Mwanzoni Sita alijikomaza lakini baadae Ilibidi ajilegeze, maana kukomaa ilimaanisha kuumizwa zaidi na ile kabali.
Kujilegeza nako lilikuwa kosa kubwa sana alilolifanya Sita. Kosa ambalo atalijutia mpaka kesho, kama kuna maisha baada ya kilichomtokea pale. Dokta Yusha alimvuta Sita kwa nguvu na kujikuta akimsukumia pale katika kiti cha kifo!
Balaa!
Sita alibadirika naye, mwili ulibadirika sambamba na kiti, Ilikuwa ni rangi nyekundu mithili ya tanuru la moto!
ITAENDELEA KESHO MUNGU AKIPENDA.