Riwaya - Balaa

Riwaya - Balaa

SIMULIZI; BALAA
Mwandishi; HALFANI SUDY
SEHEMU YA TISINI NA SITA

SIMU; 0757 633010

Sasa Daniel aliona muda wake wa kuuwawa umefika, ujanja wake umefikia kikomo. Kwa sasa amepatikana! Alikuwa ameingia sehemu hatari sana, zaidi ya hatari yenyewe. Aliwaza hayo, halafu akabadirika, alikuwa anawaza mawazo hasi, yeye alikuwa mti makini sana. Akaitupa kule dhamira ya kushindwa. Siku zote yeye alikuwa ni mshindi!
Daniel Mwaseba, alizungusha macho yake kuwaangalia watu wale watatu waliogeuka kama watoa roho kwake.
Jamaa wale wawili wakawa wanamwangalia yule jamaa wa katikati aliyekuwa ameishika bastola ya Daniel Mwaseba, imara kwa mkono wa kiume. Daniel akaona ile ndio nafasi pekee ya kuitumia, nafasi ya hatari sana, lakini ilibaki ile tu. Angafanya nini, Daniel Mwaseba alinyanyuka pale chini kwa haraka, asalalee! hakuwahi kufanya hata chembe alichotaka kufanya!
Ngumi ya nguvu toka kwa yule jamaa aliyekaa upande wa kulia ilitua katikati ya mwamba wake wa pua. Ngumi iliyompata sawia. Daniel alikaa tena chini bila kupenda. Damu sasa zikiwa zinachuruzika mithili ya bomba kutoka kwenye pua. Jamaa alikuwa anaangalia kwengine lakini aliuona ujanja ukiotaka kufanywa na Daniel Mwaseba.

Daniel akajua sasa amepatikana, wale majamaa hawakutaka kumpa nafasi yoyote ile ili afanye anachotaka kufanya. Walikuwa wepesi mithili ya umeme. Pale chini alishika tshirt yake na kuipangusa ile damu iliyokuwa inamtoka puani. Majamaa watatu walimwangalia Daniel Mwaseba kwa tuo, halafu kwa pamoja wote waligeuka nyuma.
Katika mlango uleule waliotokea wao kuna mtu mwengine alikuwa anatoka. Daniel Mwaseba nae aliacha kujifuta damu na kumwangalia mtu huyo aliyekuwa anaenda mahali pale. Jamaa alisogea kwa hatua za taratibu huku akinesa kwa madaha mpaka pale walipokuwa wamesimama wale majamaa watatu. Mgeni huyu mpya, mtembea kwa mdenguo. Kwa majina alikuwa anaitwa Don Genge. Mkuu wa vijana wale. Mtu katili kabisa kuwahi kutokea duniani. Na kwa bahati mbaya alikuwa anawaongoza vijana makatili sana!
Yule jamaa aliyepambana mwanzo na Daniel Mwaseba nae alisogea pale walipo wale wenzie, sasa walikuwa wanne na Don Genge watano. Macho kumi ya watu makatili yalikuwa yanamwangalia Daniel Mwaseba. Naam! Macho kumi toka kwa watu watano. Daniel Mwaseba alikuwa pale chini akipiga hesabu zake, akitafuta namna ya kujitoa pale lakini hakuona namna yoyote ile. Ama kwa hakika Daniel Mwaseba alikuwa amepatikana!


TUKUTANE KESHO MUNGU AKIPENDA.
 
Dr Yusha bado hajapata njia ya ngome akavamie na maaskari wamuokoe Dan?
Au hata Polisi wamfatilie jamaniiii
 
SIMULIZI; BALAA
MWANDISHI; HALFANI SUDY
SIMU; 0757 633010

SEHEMU YA TISINI NA SABA

"Hahaha Daniel Mwaseba, una bahati mbaya sana. Umejiingiza mwenyewe katika mdomo wa mamba. Umekifata kifo chako hapa! Huwezi toka salama mahali hapa, tunakuuwa Daniel na tunakutoa moyo!" Don Genge alisema kwa kujigamba sana. Daniel Mwaseba hakujibu kitu, alikuwa anawaangalia tu kwa zamu watu wale watano.

"Daniel Mwaseba, mpelelezi mahiri nchini Tanzania..." Sauti kutoka kule mlangoni ilisikika. Nayo ikitaja jina la Daniel. Daniel Mwaseba alinyanyua sura yake na kumwangalia mtu aliyotoa kauli hiyo, alimtambua vizuri sana. Alikuwa ni yule jamaa aliyepambana nae kule Kimbilio lodge, yule jamaa aliyejirusha katika gari la polisi likiwa katika mwendo mkali. Mhalifu mwenye roho ngumu ya paka!
Alikuwa anaitwa Tano!
Sasa kundi zima la Six killers lilitimia. Alikuwepo Moja, Mbili, Tatu, Nne, Tano na kiongozi wao Don Genge.
Kiukweli Daniel Mwaseba alikuwa katika balaa kubwa sana!

"Hahaha eti mpelelezi mahiri nchini Tanzania, mpelelezi mahiri anaingia kichwakichwa kwenye moto namna hii. Ulikuwa unajiona makini sana Daniel Mwaseba, eti Taifa la Tanzania linakutegemea hahaha, Tano ni mahiri zaidi yako. Kwa taarifa yako alikuwa anakuona ulivyokuwa unamfata. Huwezi kumfikia Tano wewe kiakili hata siku moja. Tumekushudia jinsi ulivyojirusha toka mtini. Huna akili za kutuzidi Six killers, huna hata kidogo" Don Genge aliongea kwa kujigamba na kumsifu kijana wake Tano.

Daniel Mwaseba aliwaangalia wale watu makatili sana. Aliudhika pia na majigambo yao, lakini kimoyomoyo Daniel Mwaseba alijisemea.

'Mtajuta'

"Tummalize sahivi Bosi, tusimcheleweshe" Moja alishauri.
"Hatuwezi kumuua haraka namna hiyo Moja, lazima afe kwa mateso makali sana!" Don Genge aliyasema maneno hayo huku akiachia teke kali lililonasa vizuri katika shavu la Daniel Mwaseba. Damu ziliruka hovyo! Daniel alipata maumivu makali sana, lakini hakutaka kuonesha mbele ya maadui zake. Alijikomaza na kwa bahati nzuri Daniel Mwaseba alikuwa mwalimu katika fani ya kuvumilia maumivu....

ITAENDELEA KESHO MUNGU AKIPENDA
 
SIMULIZI; BALAA
MWANDISHI; HALFANI SUDY
SIMU; 0757 633010

SEHEMU YA TISINI NA SABA

"Hahaha Daniel Mwaseba, una bahati mbaya sana. Umejiingiza mwenyewe katika mdomo wa mamba. Umekifata kifo chako hapa! Huwezi toka salama mahali hapa, tunakuuwa Daniel na tunakutoa moyo!" Don Genge alisema kwa kujigamba sana. Daniel Mwaseba hakujibu kitu, alikuwa anawaangalia tu kwa zamu watu wale watano.

"Daniel Mwaseba, mpelelezi mahiri nchini Tanzania..." Sauti kutoka kule mlangoni ilisikika. Nayo ikitaja jina la Daniel. Daniel Mwaseba alinyanyua sura yake na kumwangalia mtu aliyotoa kauli hiyo, alimtambua vizuri sana. Alikuwa ni yule jamaa aliyepambana nae kule Kimbilio lodge, yule jamaa aliyejirusha katika gari la polisi likiwa katika mwendo mkali. Mhalifu mwenye roho ngumu ya paka!
Alikuwa anaitwa Tano!
Sasa kundi zima la Six killers lilitimia. Alikuwepo Moja, Mbili, Tatu, Nne, Tano na kiongozi wao Don Genge.
Kiukweli Daniel Mwaseba alikuwa katika balaa kubwa sana!

"Hahaha eti mpelelezi mahiri nchini Tanzania, mpelelezi mahiri anaingia kichwakichwa kwenye moto namna hii. Ulikuwa unajiona makini sana Daniel Mwaseba, eti Taifa la Tanzania linakutegemea hahaha, Tano ni mahiri zaidi yako. Kwa taarifa yako alikuwa anakuona ulivyokuwa unamfata. Huwezi kumfikia Tano wewe kiakili hata siku moja. Tumekushudia jinsi ulivyojirusha toka mtini. Huna akili za kutuzidi Six killers, huna hata kidogo" Don Genge aliongea kwa kujigamba na kumsifu kijana wake Tano.

Daniel Mwaseba aliwaangalia wale watu makatili sana. Aliudhika pia na majigambo yao, lakini kimoyomoyo Daniel Mwaseba alijisemea.

'Mtajuta'

"Tummalize sahivi Bosi, tusimcheleweshe" Moja alishauri.
"Hatuwezi kumuua haraka namna hiyo Moja, lazima afe kwa mateso makali sana!" Don Genge aliyasema maneno hayo huku akiachia teke kali lililonasa vizuri katika shavu la Daniel Mwaseba. Damu ziliruka hovyo! Daniel alipata maumivu makali sana, lakini hakutaka kuonesha mbele ya maadui zake. Alijikomaza na kwa bahati nzuri Daniel Mwaseba alikuwa mwalimu katika fani ya kuvumilia maumivu....

ITAENDELEA KESHO MUNGU AKIPENDA

Daah! Unatupia kidogo kidogo sana mpaka mzuka unapungua mkuu
 
meona eeeh bora angekuwa anatupia mbili kwa siku

Yan we acha2, mapengo Jr tusaidie bhana Kwa upande huo Ni fupi sana halaf unatupia kidogo kidogo xana Fanya hata Mara 2 au 3 Kwa cku
 
Mm naona mapengo jr bora uache tu maana waswahili hatuekewi unapotuambia ipo jikoni inapikwa.mnataka awe anakaa na kutunga tu hii hadithi wakati hatuilipii yy atakula wapi asipofanya kazi nyingne akawa anatunga tu ili kutufurahisha?tuwe waelewa bhasi kha!
 
Mm naona mapengo jr bora uache tu maana waswahili hatuekewi unapotuambia ipo jikoni inapikwa.mnataka awe anakaa na kutunga tu hii hadithi wakati hatuilipii yy atakula wapi asipofanya kazi nyingne akawa anatunga tu ili kutufurahisha?tuwe waelewa bhasi kha!

Samahan ulishawahi somea uandishi au kuandika hata story ya page 40? Ukinijib tutaendelea maana inaonekana hauelew chochote Kwa upande wa uandishi
 
SIMULIZI; BALAA
MWANDISHI; HALFANI SUDY
SIMU; 0757 633010

SEHEMU YA TISINI NA NANE

Huko katika mji mdogo wa Kilwa Masoko usiku uleule ambao Daniel Mwaseba alikuwa anapata mateso makali sana kwa vipigo toka katika kundi hatari la Six killers, Dokta kijana, Dokta makini, Dokta mzalendo, Dokta Yusha alikuwa ameshahaha vya kutosha katika mitaa yote ya mji wa Kilwa Masoko kuwatafuta madaktari wale hatari kwa Taifa. Alijaribu kuwatafuta mahali mote ambako alikuwa anaamini wale madaktari makatili wanaweza kuweka maskani yao bila mafanikio yoyote. Tangu jioni ya siku ile alipotoka tu Kilwa Kivinje alianza kuwasaka, jioni ilipita bure na sasa usiku wa manane Dokta Yusha alikuwa bado anahaha. Alipita karika baa zote za Kilwa Masoko. Baa zilizokuwa hadharani na baa za vichororoni. Alijaribu pia kupita nje ya nyumba za kulala na kujaribu angalau kuwaulizia watu aliowakuta nje. Lakini hakupata fununu zozote za maana. Pamoja na hayo yote lakini Dokta Yusha hakutaka kabisa kuchoka ama kukata tamaa wakati akijua fika kwamba kuna watu walikuwa wanateseka mahali flani. Funguo pekee ya kufika huko ni kuwapata wale madaktari makatili watakaomfikisha kule porini.

Alitafuta sana, baadae aliamua kwenda kulala katika nyumba yake ya kulala wageni aliyofikia. Ndio....Alienda kulala katika nyumba ya kulala wageni ya Mikumi. Dokta Yusha aliingia chumbani kwake na kujitupa kitandani bila kufanya chochote. Hakuoga, hakubadili nguo wala kufunga mlango. Alilala chali kitandani huku usingizi ukiwa umempaa kabisa, alikuwa akiwaza na kuwazua nini cha kufanya. Baada kama ya dakika kumi za kutafakari Dokta Yusha aliamka. Aliona ule sio muda muafaka wa kulala. Dokta Yusha aliinuka pale kitandani na kuingia tena mtaani. Safari hii alikumbuka kufunga mlango. Alitoka nje ya nyumba ile ya kulala wageni. Hatua kumi na saba tu toka nje ya nyumba ile ya kulala wageni ya Mikumi, Dokta Yusha alikutana na kitu kilichomshangaza sana...

ITAENDELEA KESHO MUNGU AKIPENDA
 
SIMULIZI; BALAA
MWANDISHI; HALFANI SUDY
SIMU; 0757 633010

SEHEMU YA TISINI NA TISA

Dokta Yusha alipigwa na mshangao mkuu! Dokta Yusha alikutana uso kwa uso na Mwanasheria. Mlevi wa ajabu sana kutokea ndani ya mji wa Kilwa Masoko na Tanzania kwa ujumla. Mlevi aliyehusika mara kadhaa kuokoa maisha ya Dokta Yusha katika hali ya utani. Mlevi ambaye mchana aliachwa katika hospitali ya misheni ya Ndanda, cha kushangaza sasa usiku wa manane alikuwa katika mji wa Kilwa Masoko. Dokta Yusha alipatwa na mshangao mkuu. Mwanasheria mbele ya macho yake, hakuamini kabisa!

"Wewe Mwanasheria, upo huku, umekuja saa ngapi, umewaacha na nani wagonjwa?" Dokta Yusha aliuliza maswali mfululizo akiwa na wahka mkubwa.
"Nipo Dokta, jana na leo" pamoja na Dokta Yusha kuuliza maswali kwa hisia kubwa, lakini Mwanasheria alitoa jibu la utani.
"Mwanasheria!" Dokta Yusha aliita kwa ghadhabu.
"Rabeka Dokta"
"Acha utani Mwanasheria, umekuja lini hapa, sasa wagonjwa umewaacha na nani kule hospitali?" Dokta Yusha sasa aliuliza akiwa ametulia kidogo.
"Nimemwona Dokta Kilumba leo, tena sasahivi" Mwanasheria badala ya kujibu maswali ya msingi ya Dokta Yusha, yeye aliongea kitu kipya kabisa.
"Dokta Kilumba? Umemwona wapi?" Dokta Yusha nae alipatwa na fadhaha kusikia Mwanasheria ameonana na Dokta Kilumba. Miongoni mwa watu anaowatafuta kwa udi na uvumba tangu alivyoingia Kilwa.
"Nimemwona Dokta pale katika baa ya by night bar" Mwanasheria alisema huku akiionesha baa hiyo iliko kwa kidole chake. Haukuwa mbali sana na pale walikosimama, nyumba ya kulala wageni ya Mikumi hadi katika baa ya Masoko by night.

"Twende Mwanasheria, twende haraka" Dokta Yusha alishauri kwa sauti yenye uharaka.
"Usiwe na pupa Dokta, polepole ndio mwendo"
"Unajua sikuelewi Mwanasheria"
"Utanielewa Dokta Yusha. Hatuna haja ya kwenda pale na kumvamia, twende taratibu tujifiche sehemu na kuona uelekeo wake baada ya kutoka pale"
"Sawa Mwanasheria"

Dokta Yusha na Mwanasheria mlevi kwa mwendo wa taratibu kama alivyoshauri Mwanasheria walienda katika baa ya by night, lengo lao kuu ni kumuwinda Dokta zaidi Kilumba....

ITAENDELEA KESHO MUNGU AKIPENDA
 
Back
Top Bottom