RIWAYA: Anga ya Washenzi na Gilbert Evarist Mushi

gilbert35

JF-Expert Member
Nov 20, 2021
247
474
Riwaya: Anga ya Washenzi
Imeandikwa na Gilbert Evarist Mushi
Phone: 0765824715.

Msimu wa Kwanza, Sehemu ya 01

SURA YA KWANZA

Jumatatu Tar 07/04/2022, Saa 04:00 Asubuhi.
Hali ya hewa ilikuwa ni ya baridi sana katika mji wa Moshi, maelfu ya watu walikusanyika katika uwanja wa chuo kikuu cha ushirika Moshi, kila mmoja alikuwa ndani ya makoti pamoja na masweta mazito kutokana na baridi kuwa kali. Kila mtu alikuwa makini kusikiliza Rais Mark anawaambia nini. Rais Mark alikuwa katika ziara yake ya kwanza kabisa tangu mwaka mpya wa 2022 uanze, na katika ziara hiyo mji wa Moshi ulibahatika kuanza mwaka na rais Mark. Maelfu ya watu waliokusanyika katika kiwanja hicho walikuwa bize kusikiliza maneno ya rais wao kipenzi, vyombo vya ulinzi na usalama navyo havikuwa nyuma, vilikuwa vikifuatilia kwa karibu kila tukio, huku helikopta ya jeshi la polisi nayo ikizidi kupiga ruti angani kuhakikisha usalama unakuwepo kwa asilimia zote.

Daniel Mwaseba alikuwa ni mmoja kati ya watu waliokuwa bize kufuatilia kwa karibu kila tukio lililokuwa likiendelea. Yeye ni mpelelezi nambari moja Nchini Tanzania na kipenzi cha wengi ndani na nje ya nchi hii. Yeye pamoja na timu mahususi kutoka idara ya usalama wa taifa walikuwa ndani na nje ya uwanja wa Ushirika, na jukumu lao kubwa lilikuwa ni kuhakikisha Rais wa nchi anamaliza ziara yake salama katika mji huu wa Wachaga. Muda wote macho ya Daniel hayakutulia sehemu moja, alikuwa akiyazungusha macho yake kila kona, aliyapeleka kaskazini, sekunde hiyohiyo akayapeleka kusini, akayatupia magharibi na hata mashariki aliyapeleka macho yake ilimradi tu kuhakikisha usalama unakuwepo katika viwanja hivi vya chuo kikuu cha ushirika Moshi. Katika sikio lake la kushoto Daniel alipachika kifaa maalumu ambacho kilimsaidia kuwasiliana na wenzake wakati wowote, katika mkono wake wa kulia alikuwa ameshikilia vyema miwani ya shetani iliyokuwa na uwezo wa kuona tukio lolote la mbali. Daniel Mwaseba alikuwa amesimama pembeni kidogo ya jukwaa walilokalia viongozi wa kidini.
Daniel Mwaseba aliyapepesa macho yake kwa sekunde tano tu kila kona, lakini hakuona tukio lolote la ajabu linaloweza kuathiri usalama wa ziara ile, sekunde ya sita akayahamishia macho yake hadi mbele kabisa aliposimama mheshimiwa rais Mark. Rais alikuwa bado anawahutubia wananchi.
Sekunde ya saba Daniel akayapeleka macho yake upande wa mkono wa kushoto wa rais Mark, upande huo waliketi viongozi mbalimbali wa serikali.

Macho ya Daniel yalitua katika mikono ya makamu wa rais, mh Eliud Sumbi ambaye muda huo vidole vyake vilikuwa bize vikichezea simu yake. Vidole vyake vilikuwa vikibonyeza simu kwa kasi ya ajabu, kasi ambayo ilimshtua Daniel ambaye umakini uliongezeka zaidi ya awali, akili yake ilimtuma aendelee kutazama kunani hadi makamu wa rais aonekane kubonyeza simu kwa kasi ile tena wakati ambao yupo kwenye ziara, akaona hii si kawaida kwa viongozi wa serikali kufanya vile wakati kama huu. Daniel aliamua kuyaegesha macho yake palepale alipoketi mheshimiwa Eliud Sumbi. Alifundishwa kutopuuzia jambo lolote akiwa mafunzoni miaka kadhaa iliyopita. Alifahamu fika kwenye ulimwengu wa kipelelezi hakupaswa kupuuzia jambo lolote ambalo linaweza kuwa la kijinga au dogo kwa mtu wa kawaida, na kila atakaloliona katika ulimwengu huu basi ni lazima liwe na matokeo chanya ama hasi.

Mheshimiwa Eliud Sumbi ambaye ni Makamu wa rais wa Tanzania alikuwa akiuchakata ujumbe katika simu yake. Kwa namna alivyokuwa akiuchakata ujumbe ule ilionekana wazi alikuwa na lengo la kuufikisha ujumbe huo haraka sehemu husika. Alipomaliza kubofya simu yake alipepesa macho yake kulia na kushoto, kulia kwake aliketi Waziri wa ulinzi Dk Edward Bavu, na upande wake wa kushoto aliketi waziri wa michezo Dk Janeth Julius. Aliwaona mawaziri hawa wapo bize kusikiliza mheshimiwa Rais anasema nini. Alipepesa tena macho yake mbele na nyuma yake, na hapo akayahamisha macho yake hadi juu ya jengo moja la ghorofa lililopo karibu mita Mia Tano kutoka alipo. Ghorofa ile ilikuwa ni hoteli maarufu inayoitwa Five star Hotel. Macho ya Eliud Sumbi yalitazama juu ya hoteli ile kwa sekunde tatu ndipo akaiweka simu yake katika mfuko wake wa koti la suti.

Daniel Mwaseba hakuwa nyuma, alikuwa bize akiyafuatilia macho ya Makamu wa rais kila yanapotazama, alimwona mheshimiwa makamu wa Rais akitazama upande wake wa kushoto, akamwona pia akitazama kulia, Daniel naye akatazama hukohuko alipotazama mheshimiwa Eliud Sumbi. Alipoyapeleka macho yake katika kilele cha hoteli ya Five Star, Daniel naye aliyapeleka macho yake huko pia, na hapo ndipo hisia zake zilizaa matunda, Hisia mbaya za kumtilia shaka mheshimiwa Eliud Sumbi kutokana na ubonyezaji wake wa simu wenye kutia wasiwasi, tena wakati ambao ziara ya Mkuu wa nchi ikiendelea.
Juu kabisa ya Ghorofa, Five Star Hotel Daniel Mwaseba alifanikiwa kuona kivuli kikijisogeza taratibu, Ilihitaji macho ya mwewe kugundua juu ya ghorofa kuna kivuli, lakini macho ya Daniel yaliweza kugundua juu ya ghorofa kuna kivuli kikijisogeza karibu, na yalifanikiwa pia kuuona mkono wa binadamu ukijichomoza taratibu.

"Daniel kama unanipata, angalia kwa makini angani, itazame ile helikopta inayoimarisha ulinzi angani. Mbona kama si ile iliyopangiwa? Hii kama rangi yake ya kijani imepoa sana" Sauti ilisikika kutoka kisikilizio kilichopachikwa katika sikio la Daniel

"Nam Elizabeth Neville, upo upande gani kwani?" Daniel aliachia swali huku mkono mmoja ukigusa kisikilizio kile, macho yake yalikuwa bado yakitazama palepale juu ya jengo la Five Star hotel. Kwa haraka aliyarudisha macho yake pale alipoketi Makamu wa Rais, alimwona mheshimiwa Eliud Sumbi akitazama saa yake ya mkononi. Daniel Mwaseba aliyarudisha tena macho yake kwa kasi hadi juu ya jengo la hoteli ya Five star. Sasa alimshuhudia mdunguaji aliyelala mithili ya nyoka akiiseti bunduki ya masafa marefu.

"Nipo hema la kusini Daniel, jaribu kuwasiliana na Chifu ameketi na jenerali Evance, amuulize Jenerali ili nasi tuweze kufahamu kama ana taarifa yoyote ya kubadilishwa kwa helikopta maana hii inashangaza, kiusalama si kawaida. Najiuliza kwanini wameweza kuibadilisha bila sisi kujulishwa, nina uhakika wamebadilisha helikopta maana hii ni tofauti na ile ya kwanza tuliyoiona" Sauti ya kike ilisikika ikieleza kupitia kisikilizio alichopachika Daniel katika sikio lake.

"Elizabeth Neville! Kumekucha" Aliropoka Daniel. Aliiona hatari inayokwenda kutokea.
"Kama juu ya hoteli ile kuna mdunguaji na angani kuna helikopta ambayo si ile tuliyofahamishwa jana, ina maana walio ndani ya helikopta hawamwoni mdunguaji? Hapa kuna mchezo unaendelea, Rais Mark ana maadui wengi kwa sasa na nisipokuwa makini atauwawa" alijisemea Daniel huku akipiga hatua za haraka haraka kuelekea alipoketi Chifu Abdallah Ntenga ambaye ni Mkurugenzi wa idara ya usalama wa taifa

"Daniel kuna nini? Nifahamishe Daniel kama nakupata" Sauti ya Elizabeth Neville ilipenya kupitia kisikilizio kile na kutua katika sikio la Daniel Mwaseba

"Kuna tatizo Elizabeth, nadhani kuna tukio limepangwa kutokea hapa, siwezi kukuambia moja kwa moja ni nini lakini tambua hii ziara ipo kwenye hatari. Sasa hivi ninaelekea alipo chifu, niambie upo wapi Elizabeth" alisema Daniel huku akizipiga hatua zake kuelekea alipo chifu Abdallah Ntenga.

"Daniel mimi nipo huku nje ya uwanja kabisa, nakuja huko ndani sasa hivi" alisema Elizabeth Neville, wakati huo Daniel Mwaseba alishafika karibu na sehemu alipoketi chifu Abdallah Ntenga. Chifu alikuwa ameketi pamoja na mkuu wa majeshi ya Tanzania, jenerali Evance, pamoja pia na mkuu wa jeshi la polisi, IGP Kilazi. Alipokaribia alimpa ishara Chifu na palepale alinyanyuka na kumfuata.

"Kuna jambo halipo sawa Chifu, helikopta inayoranda juu ni tofauti na ile tuliyoiona mwanzoni, ulipewa taarifa juu ya kubadilishwa kwake?" aliuliza Daniel. Chifu alionekana kushtuka sana

"Unasemaje Daniel! Wamebadili helikopta? Kivipi wabadili helikopta bila kutufahamisha? Ile nyingine tuliyoiona jana ikifanyiwa majaribio imepata dharura gani?" aliuliza Chifu katika hali ya kushangaa kwani haikuwa kawaida kubadilishwa baadhi ya mambo ya kiusalama bila wao kujulishwa kwanza. Wakiwa bado wamesimama palepale mlio wa helikopta ulisikika kwa mbali, wote kwa pamoja wakainua vichwa vyao angani kuitazama helikopta ile. Chifu alipeleka mkono wake mdomoni, Daniel naye alionekana kushika kichwa chake.

"Mungu wangu...! Si yenyewe hii" alisema Chifu

Kuna nini nyuma ya pazia?

Tuwe wote kesho tena panapo uhai
 
Cover
Screenshot_20220508-063831.jpg
 
Riwaya: Anga ya Washenzi
Imeandikwa na Gilbert Evarist Mushi
Phone: 0765824715.

Msimu wa Kwanza.
Sehemu ya 02

Wakiwa bado wamesimama palepale mlio wa helikopta ulisikika kwa mbali, wote kwa pamoja wakainua vichwa vyao angani kuitazama helikopta ile. Chifu alipeleka mkono wake mdomoni, Daniel naye alionekana kushika kichwa chake.

"Mungu wangu...! Si yenyewe hii" alisema Chifu

"Ile tuliyoiona mwanzoni ilikuwa na rangi ya Kijani ya kijeshi, lakini hii kama kijani yake inakaribia kufanana na kijani kibichi. Pia juu ya hoteli ya Five Star nimemwona mdunguaji akijisogeza na bunduki, Chifu naomba umuulize jenerali Evance kama ana taarifa za kubadilishwa ili tujue, pia naomba ufwatilie nyendo za mheshimiwa Eliud Sumbi, Elizabeth Neville anakuja sasa hivi wacha mimi niwahi katika hoteli ya five star" alisema Daniel huku akitazama upande ilipo hoteli ile.

"Unamzungumzia Eliud Sumbi huyuhuyu ambaye ni Makamu wa rais! Umeona kitu gani kwake? " Chifu alimtupia swali Daniel.

"Ndiyo mkuu, namzungumzia Mheshimiwa Eliud Sumbi, tukizidi kuchelewa ndio hatari inazidi kuwa kubwa, nikirejea nitakueleza kila kitu, Kuwa makini na kila hatua anayopiga Mhe Eliud Sumbi Chifu. Mimi nawahi" Daniel alisema huku akiondoka, alimwacha Chifu akiwa njia panda.
Muda uleule baada ya Daniel Mwaseba kuelekea Five Star hotel, Elizabeth Neville aliwasili na kumkuta chifu akiwa palepale.

"Chifu kuna nini? Daniel ameshafika hapa?" Elizabeth Neville aliachia maswali mawili mfululizo.

"Hebu nisaidie jambo moja Elizabeth, mimi naenda kuzungumza na mkuu wa majeshi ya ulinzi na Usalama, jenerali Evance juu ya kubadilishwa kwa Helikopta. Wewe fuatilia kwa karibu nyendo za makamu wa rais tujue ni nini anafanya. Kuwa makini usigundulike kama unampeleleza, fanya kimyakimya" Chifu alimwambia Elizabeth Neville baada ya kuwasili, akamwacha na kuelekea alipo Jenerali Evance

Miguu ya Daniel ilikuwa ikigusa na kuachia ardhi kwa uharaka sana, alikuwa akikimbia kama vile amechanganyikiwa. Lengo kubwa lilikuwa ni kuwahi ilipo hoteli ya five Star. Barabarani hakufanikiwa kuona gari wala mtu akitembea zaidi ya askari wa doria tu, barabara ilikuwa imepoa sana, shughuli za machinga, watembea kwa miguu hazikuwepo. Hii ilitokana na Rais wa nchi yupo ziarani karibu na mitaa hii.
Dakika mbili zilimfikisha Daniel Mwaseba ndani ya hoteli ya Five Star, kwa mwendo wa haraka akaelekea sehemu zilipo ngazi za kuelekea juu kabisa ya ghorofa. Aliziona ngazi, bila kuchelewa alianza kupanda kuelekea juu. Hadi kufika juu kabisa alizivuka sakafu nne za ghorofa.

Juu kabisa ya ghorofa kulikuwa na mwanaume mweusi mnene kiasi akiwa amejilaza kwa kutumia tumbo lake, alikuwa akikamilisha zoezi la kuunganisha bunduki yake kwa utulivu mkubwa, mwilini alivalia koti kubwa lenye rangi nyeusi, suruali ya jeans nyeusi pamoja na raba nyeusi huku kichwani akivalia kofia kubwa nyeusi iliyofunika macho yake. Kiufupi alikuwa ni mweusi kila kona ya mwili wake, kuanzia ngozi yake hadi mavazi. Labda ni viganja vya mikono tu havikuwa vyeusi lakini hatuwezi kujua kutokana na kizuia mikono (Gloves) alichokuwa amevalia. Baada ya kukamilisha zoezi lile alianza kumtafuta ndege wake aweze kumwekea shabaha. Jicho moja alilielekeza kwenye kioo kidogo juu ya bunduki ile, kioo ambacho kilimsaidia kuvuta picha ya mbali, kilimwezesha kuona kwa ukaribu. Kupitia kioo hicho aliweza kumwona Mheshimiwa rais Mark akiendelea na hotuba, taratibu mwanaume yule alianza kuisogeza bunduki yake kutafuta alipoketi makamu wa rais, akasita kuisogeza zaidi baada ya kumwona mheshimiwa Eliud Sumbi, alimwona akihangaika kubofya simu yake. Ilikuwa ni kama mtu anayeharakisha kucharaza ujumbe kwenye simu. Mwanaume huyu akaachana na Mhe. Eliud Sumbi na kuisogeza tena bunduki yake kuelekea upande wa kulia, upande ambao aliketi waziri wa Ulinzi. Alimwona Dr Edward Bavu akiwa makini kumsikiliza mheshimiwa rais. Mwanaume huyu akaisogeza bunduki yake vizuri na kuweka shabaha katika kifua cha waziri wa ulinzi, Dr Edward Bavu.
Taratibu bila hofu yoyote akakisogeza kidole chake hadi kunako sehemu ya kufyatulia risasi, akakikaza kidole chake tayari kwa kufyatua. Tayari kwa kumfyatua Waziri wa ulinzi, Dr Edward Bavu.
Lakini akijiandaa kufyatua risasi, saa yake ya mkononi ilitoa mtetemo mdogo uliobatana na mwanga mdogo wa bluu. Akasitisha zoezi la kumfyatua ndege wake, macho yake yakawa makini kutazama saa ile. Aliona ujumbe mdogo ulioingia katika saa ile ambayo haikuwa saa ya kawaida kama hizi tuzijuazo, Ulikuwa ni ujumbe ukitoka kwa mtu aliyehifadhiwa kwa jina la M.B

"Toka eneo hilo haraka!" ujumbe ulisomeka vile. Kwa kasi akaunyoosha mkono wake wa kushoto na kulivuta briefcase lake, akiwa bado amelala na tumbo aliifungua briefcase ile na kuiweka bunduki yake, akaanza kutambaa kwa tumbo kinyumenyume kwa tahadhari ya kutokuonekana. Akizidi kurudi nyuma kwa kutambaa na tumbo alihisi uwepo wa kizingiti nyuma yake, kizingiti kilichomfanya ashindwe kabisa kuendelea na safari yake ya kurudi kinyumenyume. Na Kizingiti hicho kilikuwa ni Daniel Mwaseba ambaye ni mpelelezi kutoka idara ya usalama wa taifa.
Daniel Mwaseba aliutega mguu wake wa kulia kwa makusudi katika kisigino cha mguu wa mwanaume yule.

"Tulia hivyohivyo. Zungusha mikono yako nyuma, ujanja wowote utakaoufanya nitaumwaga ubongo wako." Daniel alionya kwa sauti ndogo iliyosikiwa vyema na mwanaume yule.

"Sipo tayari kukamatwa kizembe, Sipo tayari..." Mwanaume yule alijionya. Katu hakuwa na shaka wala hofu yoyote ile, alijiamini atatoka mbele ya mtu aliyepo nyuma yake. Kwa utulivu mkubwa mwanaume yule aliipeleka mikono yake nyuma ya kiuno chake, akitafakari namna sahihi ya kumtoka mtu aliyeko nyuma yake. Hakujua kama aliyekuwa nyuma yake ni mpelelezi anayelitikisa bara la Afrika kila iitwapo leo katika magazeti kutokana na shughuli anayoifanya dhidi ya wahalifu, hakujua kama ni Daniel Mwaseba ambaye anachukiwa na kila aina ya wahalifu katika uso wa dunia hii.
Hakujua!
Daniel kwa tahadhari alichomoa pingu katika mfuko wa nyuma wa suruali yake, akaanza kuisogelea mikono ya jamaa pale chini, ili amtie pingu,
Eeh bwana, Thubutu...!
Teke zito lililopigwa kwa mtindo wa kubinuka lilitua katika kiuno cha Daniel kwa namna ambayo hakuitarajia. Lilikuwa ni teke zito na la ghafla lililomwangusha Daniel usawa wa mita moja kutoka alipo jamaa yule. Jamaa bila kuchelewa aliruka mithili ya nyani na kutua katika tumbo la Daniel Mwaseba pale chini. Mbali na tumbo la Daniel kukomaa lakini alihisi maumivu makali sana, maumivu ambayo hakutarajia kama atakutana nayo. Hapo akafahamu mpinzani wake hakuwa mtu wa masihara,

"Nisipokuwa makini nitakufa, jamaa anapiga mapigo ya kifo huyu" Daniel akiugulia maumivu pale chini alijionya, ghafla alianza kunyongwa na mikono migumu ya jamaa iliyoweka kambi katika shingo yake, jamaa alimkalia Daniel kisawasawa na alidhamiria haswa kumuua. Daniel akajitahidi kuitoa mikono ile lakini hakuweza, ilikuwa ni mikono migumu, mikono isiyokuwa na tofauti na ile mikono ya majasusi. Daniel alianza kuona nyotanyota zikikatiza mbele ya macho yake, hakupewa hata sekunde ya kuvuta pumzi. Daniel akajilegeza na ghafla kwa ghadhabu kubwa nguvu zote alizihamishia katika mguu wa kulia, akaukunja mguu wake na kulielekeza goti lake kwa kasi ya ajabu hadi katika kisogo cha mwanaume yule. Daniel alipigwa na butwaa baada ya kushuhudia mwanaume huyo akiwa bado imara akizidi kumnyonga, mwanaume yule hata hakutetereka kutokana na kupigwa kisogoni na goti lake. Badala yake mwanaume huyo aliinyoosha shingo yake kuelekea kulia kisha kushoto huku mikono ikiendelea kuikamata shingo. Daniel Mwaseba akizidi kunyongwa alikiri hii aliyokutana nayo ilikuwa ni anga nyeusi, kwa kuwa hakutegemea kama mwanaume yule angestahimili uzito wa goti lake ambalo laiti likikupata kama si kifo basi ni kulala usingizi unaofanana na kifo.

Daniel atatoka salama kweli? Hii ni Anga ya Washenzi, na msimuliaji wako ni Gilbert Evarist Mushi.
Riwaya hii ina Jumla ya Misimu minne. Kwa sasa upo Msimu wa kwanza na kwa atakayeuhitaji atalipia Tshs 1000 kwenda M pesa namba 0765824715. Nambari ya Whatsapp ni 0765824715 au 0621249611. Nitakutumia msimu wote na baada ha ya hapo tutausubiri msimu wa pili unaotoka jumatano kesho kutwa. Wengine tutaendelea hapahapa taratibu.
 
Riwaya: Anga ya Washenzi
Imeandikwa na Gilbert Evarist Mushi
Phone: 0765824715.

Msimu wa Kwanza. Sehemu ya 03
Daniel alipigwa na butwaa baada ya kushuhudia mwanaume huyo akiwa bado imara akizidi kumnyonga, mwanaume yule hata hakutetereka kutokana na kupigwa kisogoni na goti lake. Badala yake mwanaume huyo aliinyoosha shingo yake kuelekea kulia kisha kushoto huku mikono ikiendelea kuikamata shingo. Daniel Mwaseba akizidi kunyongwa alikiri hii aliyokutana nayo ilikuwa ni anga nyeusi, kwa kuwa hakutegemea kama mwanaume yule angestahimili uzito wa goti lake ambalo laiti likikupata kama si kifo basi ni kulala usingizi unaofanana na kifo.

Katika mkono wa Daniel Mwaseba, kidoleni kulikuwa na pete ya shaba, pete ambayo aliinunua akiwa mapumzikoni nchini Ujerumani miaka miwili iliyopita, pete hiyo haikuwa pete ya kawaida kama zilivyo pete nyingine. Pete hiyo ilikuwa ni silaha tosha kwa Daniel, silaha ambayo angeitumia kama atakuwa katika mazingira magumu ya kutetea uhai wake, mazingira kama haya anayokumbana nayo hivi sasa. Kwa kutumia kidole gumba aliikandamiza kwa nguvu pete ile aliyovalia katika kidole cha shahada, hapohapo ikajifyatua na sindano nyembamba ikajichomoza katika uso wa pete. Daniel akazikusanya nguvu zake katika mkono wa kulia uliovalia pete ile, akakunja ngumi yake na kuipeleka mara mbili mfululizo katika bega la jamaa. Jamaa aliendelea kumnyonga Daniel kwa sekunde tatu tu, sekunde ya nne jamaa alilegea na kumdondokea Daniel katika kifua chake, hapo Daniel akaanza kupambana kuivuta pumzi kwa fujo kwani ilibakia kidogo tu aende kuisalimu kuzimu.

"Kama isingekuwa hii pete leo ningekufa, inaonekana watu walio nyuma ya hili ni watu waliojipanga vyema" aliwaza Daniel huku akijitahidi kuvuta pumzi kwa shida. Ngumi mbili alizozipiga ziliishindilia pete katika bega na kupelekea sindano ile yenye sumu kumchoma jamaa.

"Sindano ina sumu kali sana, nisipofanya kitu jamaa atanifia hapa na sitapata chochote, hapaswi kufa hadi nijue katumwa na nani" Daniel aliwaza, haraka alitoa kichupa kidogo chenye maji ya rangi ya shaba katika mfuko wa koti lake, akaichana nguo ya jamaa pale begani alipokita pete ile. Aliona alama mbili zilizovimbia kwa matone madogo ya damu, alama ambazo bila shaka ni ile sindano ilipenyeza baada ya kupiga ngumi zile. Daniel akafungua kichupa kile na kudondoshea tone moja la maji yale ambayo yalikuwa ni maalumu kwa kupunguza kasi ya usambaaji wa sumu, kilichobaki ilikuwa ni yeye kumwaisha hospitalini ili kuuokoa uhai wake. Baada ya hapo alichomoa simu yake na kuitafuta namba ya daktari kutoka hospitali ya KCMC, alikuwa ni Dokta Yusha ambaye ni rafiki yake wa muda mrefu.

Dokta Yusha alikuwa akitoka katika chumba cha upasuaji baada ya kudumu huko kwa takribani lisaa limoja, Dokta Yusha alikuwa ni mmoja kati ya madaktari wakubwa na maarufu katika hospitali ya rufaa ya KCMC mjini Moshi. Alikuwa akizipiga hatua zake kuelekea katika ofisi yake, ndipo katika mfuko wa koti lake alisikia simu yake ikitoa mtetemo kuashiria kuna mpigaji. Aliitoa na kutazama kwa makini, alipoitazama alimfahamu mpigaji ni nani, akaipokea na kuiweka katika sikio lake la kushoto..

"Dokta Yusha habari? Naomba msaada wako haraka, kuna mtu wa muhimu sana hapa amezidiwa na sumu, ndani ya dakika kumi zijazo atanifia. Ni wa muhimu sana dokta, njoo na vifaa hapa five Star hotel juu ghorofani kabisa" Daniel alisikika simuni, na simu ikakatwa.
Dokta Yusha alielewa. Palepale aliingia katika ofisi yake na kuchukua kibegi chenye baadhi ya vitu ambavyo aliviona vitamsaidia aendapo, bila kubadili vazi lake la kidaktari alielekea nje na kuchukua usafiri wake. Kutoka pale hospitalini hadi ilipo hoteli ilimchukua dakika sita tu kutokana na barabara kutokuwa na foleni yoyote.
*******

Taarifa ya kubadilishwa kwa helikopta ilionekana kumshtua sana jenerali Evance, hakuwa amepata taarifa yoyote kutoka kwa vijana wake tangu awakabidhi kazi ya kuimarisha usalama. Ni jana tu alitoka kuzungumza na vijana wake watatu aliowapendekeza katika kazi ya kuzunguka na helikopta angani, na leo aliona helikopta angani ikizungukazunguka hivyo akaamini ni vijana wake kiasi kwamba hakuwa tena na wazo la kuwasiliana nao.

"Hebu ngoja niwasiliane nao kwanza nijue kulikoni hadi wabadilishe helikopta bila kuniambia" alisema Jenerali Evance ambaye ni mkuu wa majeshi ya Tanzania, palepale alitafuta namba ya kijana mmojawapo kati ya watatu aliowapa kazi hiyo. Alimpigia David. Simu iliita na baada ya sekunde tano ikapokelewa

"David mmefanya kitu gani na wala hamsemi? Kwanini mmebadili helikopta bila kutoa taarifa? Upumbavu gani huu mnafanya kinyume na utaratibu?" jenerali Evance alianza kufoka kwa ghadhabu baada ya simu ile kupokelewa

"Mkuu hata sielewi ni kitu gani kimetokea, tulipoingia ndani ya helikopta ili tuweze kuiwasha ilitokea hali ambayo hata siielewi, mimi na wenzangu wawili tulipitiwa ghalfa na usingizi mkuu, ndio kwanza nimetoka katika usingizi mzito mkuu. Wenzangu bado hawajazinduka, nimejaribu kuwaamsha lakini hawaonyeshi dalili ya kuamka kabisa, nahisi kuna mtu ametuchezea mchezo," David alieleza simuni

"Unasema nini! Ooh shiit..... Ina maana hii helikopta inayoranda angani sio nyie?" Jenerali Evance aliuliza kwa kuhamaki, Upande wa Chifu Abdallah hali haikuwa nzuri hata kidogo. Kitendo cha Evance kuuliza maswali kwa namna ya mshangao alibaini kwa sasa mambo hayapo sawa kabisa, na huu ulikuwa ni mwiba mchungu sana kwake na katika idara yake. Alimsogelea jenerali Evance apate kusikia maongezi yale kwa ukaribu zaidi

"Kuna hatari hapa, hii sehemu si salama kwa Rais wetu. ndio kwanza vijana wangu wanatoka katika usingizi wa kifo baada ya kusinzia ghafla wakati wakijiandaa kupanda helikopta, bila shaka walifanyiwa mchezo walipotaka kuiwasha helikopta" jenerali Evance alimwambia Chifu Abdallah, palepale alipiga hatua kuondoka lakini ghafla alishikwa mkono na Chifu Abdallah.

"Wewe ni mtu imara, hatupaswi kukurupuka katika hili. Tutume vijana wafuatilie ni nani yupo nyuma ya hili, hivi sasa napozungumza na wewe tayari vijana wangu wapo kazini kimyakimya kufuatilia nani ana nia ya kuvuruga ziara hii." aliongea Chifu Abdallah baada ya kumshika jenerali Evance mkono

"Hii ni hatari Bwana Abdallah, endapo likitokea la kutokea hapa sisi ndio tutatazamwa, lazima tufanye kitu" Jenerali Evance akamwambia Chifu Abdallah

"Nawaamini vijana wangu, muda si mrefu watanipa majibu mazuri, wewe tafuta kijana wako mmoja aungane na kijana wangu ili wafuatilie nani amefanya hili hadi hao vijana washindwe kupaisha helikopta angani, na hiyo iliyopo juu angani ifuatiliwe na wahusika wakamatwe"
Maneno ya Chifu Abdallah yakamtuliza Jenerali Evance kwa kiasi fulani, akachukua ushauri ule na palepale akaitoa simu yake kuisaka namba ya kijana wake mwingine anayemtumaini sana.

"Ngoja nimwite kijana wangu yupo hapahapa ziarani, naomba ashirikiane na kijana wako ili zoezi liende haraka. Huyu kijana wangu yeye ni mzuri sana kwa mapambano kuliko upelelezi, ni miongoni mwa wanajeshi waliorudi salama baada ya kumalizika kwa vita nchini Afrika ya Kati, kwa kuwa vijana wako ni hodari katika upelelezi naomba umuunganishe na vijana wako ili nguvu iongezeke, ninamwamini sana" Jenerali Evance anamwambia Chifu kwa unyenyekevu mkubwa.

"Ataambatana na Elizabeth Neville waifuatilie helikopta ile, mtaarifu aje sasa hivi maana mambo yanaweza kuharibika kama tutazidi kuchelewa"
Palepale Jenerali Evance anampigia Gilbert Mwaitika, ambaye ni mmoja kati ya wanajeshi hodari sana katika vita. Gilbert Mwaitika ni mtaalamu wa mapambano ya ana kwa ana, ya kutumia silaha, na hata ya mbinu za kikomandoo. Miaka kadhaa iliyopita mwanajeshi huyu alishiriki vyema katika misheni iliyoitwa Biashara ya Watoto, iliyoandikwa katika majarida na mwandishi mmoja, katika misheni hiyo mwanajeshi huyu alionyesha ukomavu wa hali ya juu katika kupambana na watu waliokuwa wakifanya biashara hiyo, jambo lililompelekea apande chati kutoka upolisi hadi kuwa mwanajeshi komandoo baada ya kwenda mafunzoni nchini Iraq. Na huko ndipo alipokamilika na kuwa komando.
Jenerali Evance alimpatia maelekezo Gilbert Mwaitika ni wapi alipo ili aje. Wakati huo chifu naye alimfuata Elizabeth Neville na kumpatia kazi mpya.

"Unaona pale aliposimama mkuu wa majeshi, Jenerali Evance? hebu nenda mfuate sasa hivi, kuna kijana atakuunganisha nae ili mfuatilie ile helikopta inayoranda angani" Chifu alimwambia Elizabeth Neville.
Kina Daniel watafanikiwa kujua chochote? Vipi kuhusu Helikopta inayoranda angani Elizabeth Neville na Gilbert Mwaitika watafanikiwa kuinasa? Ungana nami katika sehemu ijayo hapahapa. Msimu wa Kwanza sasa upo tayari, Ni kwa Tshs 1000 tu unaweza kuupata. Lipa kwenda M pesa namba 0765824715 kisha njoo whatsapp kwa namba 0621249611 au 0765824715 nikutumie.
 
Riwaya: Anga ya Washenzi
Imeandikwa na Gilbert Evarist Mushi
Phone: 0765824715.

Msimu wa Kwanza. Sehemu ya 04

"Unaona pale aliposimama mkuu wa majeshi, Jenerali Evance? hebu nenda mfuate sasa hivi, kuna kijana atakuunganisha nae ili mfuatilie ile helikopta inayoranda angani"

"Sawa Chifu" Elizabeth Neville aliitika na palepale alielekea mahali alipo jenerali Evance.

Alimkuta jenerali Evance akiwa na kijana mmoja aliyevalia magwanda ya kijeshi, mrefu kiasi mwenye mwili wa mazoezi.

"Elizabeth Neville, kutana na Gilbert Mwaitika. Ni kijana wangu ninayemwamini na kumkubali sana. Mtashirikiana kama alivyokuambia chifu, nadhani mnafahamu ni wapi pa kuanzia, mtafuteni David kwanza mtapata pa kuanzia." Jenerali Evance alisema, Elizabeth Neville na Gilbert Mwaitika walitazamana, wakasalimiana kwa ishara ya kupiga saluti

Upande wa pili alipo Chifu Abdallah Ntenga alionekana akiwasiliana na watu fulani kupitia kisikilizio alichokipachika sikioni. Alikuwa akiwasiliana na maofisa watatu kutoka idara anayoisimamia. Maofisa hao ambao walikuwa karibu sana na Mheshimiwa Rais wakimwekea ulinzi ni Gabriel, Godwin pamoja na Deusderi. Chifu aliwataka Maofisa hawa kumtazama mheshimiwa rais kwa karibu zaidi baada ya kuzuka kwa hali ya taharuki. Yote haya yalifanyika kimya kimya ili kuzuia hofu kwa wananchi na viongozi kwa ujumla ili ziara iweze kutamatika salama. Yote haya yalifanyika kwa weledi mkubwa chini ya usimamizi wa Chifu Abdallah Ntenga, mkurugenzi wa idara ya usalama wa taifa.

Wakati huohuo Mh Eliud Sumbi ambaye ni makamu wa rais alikuwa ametulia kitini akimtazama rais Mark aliyekuwa akizidi kuwahutubia wananchi. Mh Eliud Sumbi mbali na kutulia lakini alikuwa akijilaumu sana baada ya mpango wake kufeli, alipanga katika ziara hii aitumie kumsambaratisha waziri wa Ulinzi Dr Edward Bavu na alishamwandaa mtu maalumu wa kuifanya kazi hii. Alimleta nchini jasusi Ochewa Owechi kutoka nchini Kenya kwa gharama kubwa ili aje kuitenda kazi hii. Mheshimiwa Eliud Sumbi alimfahamu vyema Daniel Mwaseba. Alifahamu ni mtu ambaye hupenda sana kufukunyua mambo. Alipomwona Daniel Mwaseba akizungumza na Chifu na baadae kumwona tena Daniel akitazama upande wa Five Star hoteli aliona mpango wake unaelekea kufeli, alihisi wenda watu hawa wameshanusa harufu ya hatari. Alipomwona mkurugenzi wa idara ya usalama wa taifa akiteta na jenerali Evance aliona mambo yameshaharibika, ikambidi ahairishe mpango wake kwa kumtumia ujumbe Ochewa Owechi ili aweze kuondoka pale haraka. Hakuwa na shaka yoyote juu ya jasusi Ochewa Owechi, aliamini ujumbe aliomtumia kule ghorofani utakuwa umeshatekelezeka.
Lakini hakujua kama Daniel alishafanya yake, hakujua kama jasusi huyo kwa sasa yupo katika mikono ya Daniel Mwaseba

Kwa nini Mh Eliud Sumbi anataka kumuua Dr Edwin Bavu? Kuna lipi lililojificha? Ungana nami katika riwaya hii yenye visa vya ajabu, ni mimi mwandishi wako Gilbert Mushi.

*****

Ilimchukua dakika tano tu Dokta Yusha kufika juu ya ghorofa ile, na huko alimkuta Daniel Mwaseba amejiinamia pembeni ya mwili wa Jasusi yule.

"Ooh Mungu wangu! Ni sumu ya aina gani hii inamfanya mtu avimbe mwili mzima kiasi hiki? Sijui kama atapona huyu labda nijaribu tuu lakini sijawahi kuona sumu kama hii" alisema Dokta Yusha baada ya kusogea karibu. Alishangazwa na aina ya sumu iliyokuwa katika mwili wa mwanaume yule. Mwili wake ulivimba na kuwa mkubwa kama unga wa ngano uliotiwa amira na kukandwa kisha kuanikwa juani. Daniel Mwaseba aliinua macho yake kumtazama Dokta Yusha.

"Angeniua huyu, ilinibidi nifanye hivi bwana Yusuph Shaweji" Daniel alisema huku akitaja jina kamili la Dokta Yusha. Dokta Yusha bila kuchelewa alikishusha kibegi chake na kukitua chini, akakifungua na kuvaa gloves

"Mvue nguo ya juu, natakka abaki kifua wazi" Dokta Yusha alimwambia Daniel, Daniel Mwaseba alianza kumvua mwanaume yule koti alilovalia, akamvua na tisheti aliyovalia, tisheti hiyo ilikuwa na picha ya fuvu la binadamu kwa mbele.
Dokta Yusha alitoa visindano vingi vidogovidogo na kuvisokomeza katika kifua cha mwanaume yule, akavisokomeza na visindano vingine katika bega, sehemu ambayo ngumi za Daniel zilitua.

"Nisaidie kupanua kinywa chake," Yusha alisema huku akivuta majimaji kutoka kwenye kichupa kidogo kwenda katika bomba la sindano.
Daniel Mwaseba akatii kama alivyosema Dokta Yusha, akakipanua kinywa cha mwanaume yule,

"Mmh! Jamaa ana ulimi mweusi kama wa Ng'ombe, cheki na meno yake," Daniel alisema baada ya kukipanua kinywa cha mwanaume yule.

"Hahaha, hujawahi kumwona mtu mwenye ulimi mweusi? Huwa inatokea, kuna hali fulani ya kibaiolojia inasababisha hivi, kwa wengine ni kutokana na vyakula, na hata maji pia. ila kwa huyu nadhani ni kutokana na mazoezi, anaonyesha amekomaa kimazoezi mno, hali inayonipa matumaini wenda mwili wake unaweza pia kupambana na sumu hii isimshambulie kwa kasi sana" Dokta Yusha akamwelezea Daniel, taratibu akalibinya bomba lile la sindano kuelekea katika kinywa cha mwanaume yule, matone matatu ya mji yakatua katika ulimi wa mwanaume huyo.

"Hii isipomsaidia hatutakuwa na ujanja mwingine tena Daniel, laiti angekuwa mchovu kiafya tungekuwa hatunaye tena huyu hadi sasa, baada ya dakika tano nitavitoa hivyo visindano kisha tutampeleka hospitalini angalau akabadilishiwe na damu maana hii sumu imetapakaa sana mwilini na kuichafua damu yake kwa kiwango kikubwa sana, tutafanya hivyo kama hiki nachofanya hapa kitaleta dalili njema." alisema Dokta Yusha akimtazama Daniel. Daniel alibaki kumtazama tu bila kutia neno lolote, badala yake alisogelea brufcase ile iliyopo pembeni na kuifungua. Ndani aliona bunduki kubwa ya masafa marefu, miwani ya kumwezesha kuona mbali, pamoja na noti kadhaa za shilingi elfu kumi ya Tanzania. Akahamia katika koti la mwanaume yule, aliona paspoti. Akaikagua kwa makini
"Ni mkenya, jina lake ni Ochewa Owechi, umri wake ni miaka 43." Daniel alisema baada ya kuisoma paspoti ya mwanaume huyu.
"Sasa alikuwa na mpango wa kumpiga nani risasi?" Daniel alikuwa akijiuliza huku akizidi kukagua paspoti ile iliyoambatana na picha. Akaiweka paspoti ile katika mfuko wake. Akazipiga tena hatua hadi katika miguu ya mwanaume yule, akabonyea chini kidogo na kuvua buti zilizovaliwa na mwanaume huyo.

"Mmmh!" akaachia mguno huku mkono wake ukielekea puani kupambana kuidhibiti harufu nzito kutoka kwenye buti zile.

"Ona Daniel, angalia hicho kidude kimedondoka baada ya kumvua buti" alisema Dokta Yusha huku akielekeza mkono wake kilipo kidude hicho. Daniel akainama kidogo kukitazama.

"Kuna watu wanamfwatilia, Ni chipu ya kumwonyesha mahali alipo" Daniel alijibu baada ya kutazama, akaichukua na kutia katika mfuko wake. Dokta Yusha akamshangaa Daniel kwa kitendo cha kukitia mfukoni badala ya kuiharibu na kutupa, lakini Daniel alijua ni kitu gani anafanya

"Najua unashangaa kwanini hivi, ila kusudi langu ni kwamba kama kuna watu wanamfwatilia endapo wakiona kifaa hiki kimezimika ghafla watahisi huyu mtu ametekwa. Nafanya hivi kuwapoteza maboya kama watakuwa wanamfwatilia, muda ukifika nitakiharibu" Daniel Mwaseba alimweleza Dokta Yusha.
**********

Kwanini Makamu wa rais ana nia ya kumuua waziri wa ulimzi? Kuna nini nyuma ya pazia? Daniel atafanikiwa kupata chochote kwa mdunguaji aliyetiwa mikononi mwake?
ITAENDELEA KESHO
 
Riwaya: Anga ya Washenzi
Imeandikwa na Gilbert Evarist Mushi
Phone: 0765824715.

Msimu wa Kwanza.
Sehemu ya 05

"Kuna watu wanamfwatilia, Ni chipu ya kumwonyesha mahali alipo" Daniel alijibu baada ya kutazama, akaichukua na kutia katika mfuko wake. Dokta Yusha akamshangaa Daniel kwa kitendo cha kukitia mfukoni badala ya kuiharibu na kutupa, lakini Daniel alijua ni kitu gani anafanya

"Najua unashangaa kwanini hivi, ila kusudi langu ni kwamba kama kuna watu wanamfwatilia endapo wakiona kifaa hiki kimezimika ghafla watahisi huyu mtu ametekwa. Nafanya hivi kuwapoteza maboya kama watakuwa wanamfwatilia, muda ukifika nitakiharibu" Daniel Mwaseba alimweleza Dokta Yusha.
**********

Gilbert Mwaitika akiongozana na Elizabeth Neville walifika alipokuwa David na wenzake baada ya kupewa maelekezo kutoka kwa David mwenyewe. Walipofika waliwakuta kina David karibu na msitu uliopo pembezoni mwa kijiji kimoja kiitwacho Masama, mahali ambapo helikopta hiyo ililala usiku kabla ya ziara ya rais kufanyika. David alikuwa ana fahamu lakini wenzake wawili walikuwa bado wangali usingizini.

"Nimejaribu kuwaamsha sana lakini hawajaamka, japo kupumua wanapumua" David alisema baada ya kupiga salute mbele ya Gilbert Mwaitika. Alimwona pia Gilbert Mwaitika akiwa ameambatana na mwanamke mmoja aliyevalia shati ya mikono mirefu yenye rangi ya samawati na suruali nyeusi. Alimtambua Gilbert Mwaitika kwa kuwa waliwahi kuungana pamoja kwenda kupambana na waasi nchini msumbiji mwaka mmoja uliopita. Lakini Mwanamke aliyeambatana na Gilbert Mwaitika, David hakumtambua wala hakuwahi kumwona hapo kabla.

"Vipi kwa upande wako upo sawa?" Gilbert Mwaitika alimuuliza David, baada ya David kujibu yupo fiti na hajapata mushkari yoyote basi Gilbert Mwaitika alimtambulisha David kwa Elizabeth Neville.

"David, kutana na Elizabeth Neville. Huyu ni askari mpelelezi kutoka idara ya usalama wa taifa"

"Habari Elizabeth Neville, mimi ndiye David, David Taiwan" David alijitambulisha huku akiupeleka mkono wake kwa Elizabeth Neville kumsalimu.

"Nafurahi kukufahamu David, tupo hapa kwa ajili ya kazi ngumu kidogo, kuwafahamu waliowafanya mshindwe kuirusha helikopta angani, na kuifwatilia pia helikopta inayoranda angani" alisema Elizabeth Neville huku akipiga saluti mbele ya David, mkono wa David ukabaki na mshangao baada ya Neville kutoupokea mkono ule na badala yake kuachia saluti

"Hii helikopta tutaitumia, David utasubiri hapahapa maana hawa nimeshawaitia gari ya dharura kutoka jeshini na itafika muda si mrefu kuwachukua wote" alisema Elizabeth Neville huku akiwatazama wanajeshi wawili waliolala chini huku wakionekana kuzidiwa na usingizi.
Gilbert Mwaitika aliitoa barakoa maalumu ya kuzuia hewa chafu katika mfuko wa suruali yake, akaivaa kisha akaisogelea helikopta ile na kuanza kuikagua. Wakati huo Elizabeth Neville alikuwa anamtazama David kwa macho ya kipelelezi, macho yake yalikuwa kazini muda huo. Alishaanza kumtilia shaka David, na alipomuambia kuhusu msaada utakaokuja muda mchache ujao haikuwa kweli, hakupiga simu sehemu yoyote kuita gari ya kuja kuwachukua kina David.
Alikuwa na sababu kufanya hivyo.

Baada ya kuikagua helikopta ile kwa takribani dakika kumi, Gilbert aliridhika. Yeye pamoja na Elizabeth Neville waliwaacha kina David pale chini wakisubiri gari ya wagonjwa kama Elizabeth Neville alivyodai. Gilbert ndiye aliyekuwa rubani wa helikopta ile huku Elizabeth Neville akiwa pembeni yake, akiwa makini kutazama chini kila mahali kwa kutumia miwani ya shetani. Walizunguka angani zaidi ya mara tano lakini hawakuiona tena helikopta ile, walizunguka karibu mji wote wa Moshi lakini hawakuiona helikopta ile. Na hata mngurumo wake haukusikika tena.
Ilitoweka ghafla.

"Nadhani watu hawa kila hatua wapo karibu na sisi, haiwezekani tupaishe helikopta halafu ghafla wao watoweke, kuna mchezo hapa na inawezekana tunazungukana pia." alisema Elizabeth Neville

"Unahisi ni kina nani wanayafanya haya?" aliuliza Gilbert, akaweka umakini kumsikiliza Elizabeth huku akizidi kuiongoza helikopta ile,

"David na wenzake wawekwe chini ya ulinzi kwanza, wao wanaufahamu mchezo mzima"

"David? David huyu ambaye alizimishwa akasinzia asijue chochote?" Gilbert Mwaitika akamuuliza Elizabeth Neville kwa wakha mkubwa.

"Unadhani kuna mwingine zaidi ya huyu? Kama waliwekewa mtego wapate kusinzia wakati wanajiandaa kuirusha helikopta angani kwa nini yeye amewahi kuzinduka na wenzake bado hawajitambui? Lakini wote si makomandoo? Kwa kuwa wote ni wanajeshi basi kama hiyo dawa ya usingizi iliyotegwa kwao iliwalevya wangelala wote watatu hadi sasa, na pia kama ni kuzinduka wasingepishana sana. Ukijaribu kutazama hali halisi hivi sasa unaona David ni mzima kabisa, mwili wake hauonyeshi uchovu wowote ule. Lakini wenzake wawili wapo kama wafu. Kwanini iwe hivyo?" alieleza Elizabeth Neville huku akiendelea kupepesa macho yake kila kona.

" Umeongea kitu kizito sana Elizabeth, japo kinaweza kuwa na ukweli ndani yake, lakini hatuna ushahidi wa kumhukumu David moja kwa moja"

"Kwa sasa watakuwa ni watuhumiwa nambari moja, tukijiridhisha na uchunguzi wetu kwamba hawana hatia basi tutamwachia yeye na wenzake, au wewe unaonaje?" alisema Elizabeth na kuachia swali kwa Gilbert.
Gilbert Mwaitika alijaribu kutafakari huku akiwa makini kuiongoza helikopta. Zilipita sekunde arobaini za ukimya huku sauti pekee za mngurumo wa helikopta yao zikisikika katika masikio yao

"Naungana na hisia zako Elizabeth, David tangu anapigiwa simu na jenerali tayari alikuwa anajitambua. Tutaamini vipi kama ni kweli naye alitumbukia katika usingizi wa kifo kama wenzake? Mpigie Chifu atume askari wa kwenda kumkamata, tutaenda kumhoji tukiwa na Daniel pindi ziara ya rais itakapotamatika. Sisi tuendelee kuimarisha ulinzi angani" alisema Gilbert Mwaitika, palepale Elizabeth Neville aliwasiliana na Chifu kumweleza kila kitu. Chifu Abdallah naye akamshirikisha Jenerali Evance juu ya jambo lile, wote kwa pamoja wakaubariki mpango wa kumkamata David na wenzake wawili.

*********

David alibaki palepale alipoachwa na kina Elizabeth Neville. Pembeni yake wanajeshi wenzake wawili walikuwa bado usingizini wakiwa hawana dalili yoyote ya kuzinduka. Akiwa pale chini kwa mbali aliona magari mawili yakija walipo, akafurahi kuona msaada unakuja kwani alishaanza kuchoka kusubiri, lakini alitahamaki baada ya kuona gari zile kusimama mbali kidogo na pale walipo, wanajeshi watano waliovalia magwanda ya kijeshi wakateremka na kusogea kwa mwendo wa tahadhari wakiwa na bunduki zao mikononi.
"Wale wajinga wamenigundua nini!" David aliwaza huku akitafakari namna ya kuwakimbia wanajeshi wale.
-------------------

Kule ghorofani Dokta Yusha alikuwa akimalizia kuvichomoa visindano katika kifua cha mwanaume yule waliyemtambua kama Ochewa Owechi kama ambavyo hati ya kusafiria waliyoikuta katika koti lake ilivyoeleza. Alipomaliza zoezi lile alimtaka Daniel Mwaseba aubebe mzigo wake ili waelekee hospitali. Kwa umakini mkubwa walishuka na mwili ule bila kugundulika na mtu yoyote, isitoshe pia kwa bahati nzuri hoteli ile haikuwa na kamera za ulinzi ambazo zingeweza kuwarekodi.
Walikuwa wakishuka kwenye ngazi kutoka ghorofa namba nne na hatimaye waliifikia katika sakafu ya tatu ya ghorofa, kwa umakini mkubwa wakazikamata tena ngazi zinazowapeleka hadi ghorofa namba mbili. Ndipo Daniel Mwaseba alipotumia mkono mmoja tu ambao ni wa kushoto kumshika vyema Ochewa Owechi katika bega lake la kulia huku mkono wa kulia ukipambana kuitoa chipu ile iliyokuwa ikimwonyesha mahali Ochewa alipo. Alipoitoa mfukoni aliidondosha chini kwa makusudi. Chipu ile baada ya kudondoshwa chini ilianza kubiringika kutoka katika ngazi zile kuelekea ghorofa ya chini na kukwamia katika sakafu ya pili ya ghorofa, mbele kabisa ya mlango wa chumba cha kwanza cha ghorofa namba mbili, hatua chache kutoka ngazi ilipo. Maandishi ya juu katika mlango ule yalisomeka "EMERGENCY ROOM/ CHUMBA CHA DHARURA", na maandishi hayo yalikuwa yamepambwa kwa wino mwekundu.

David anaonekana analo jambo analifahamu. Je! Elizabeth Neville atafanikiwa kujua ni kitu gani? Kwa nini helikopta itoweke ghafla? Kuna lipi limejificha? Kesho tena njoo tuisome.

Kwa waliomaliza kusoma Msimu wa kwanza sasa ni wakati wa kuusoma msimu wa pili. Njoo whatsapp kwa namba 0621249611 au 0765824715
 
Riwaya: Anga ya Washenzi
Imeandikwa na Gilbert Evarist Mushi
Phone: 0765824715.

Msimu wa Kwanza.
Sehemu ya 06

Kina Daniel Mwaseba pamoja na Dokta Yusha walifika chini, kwa ustadi mkubwa walitoka hadi nje bila kutiliwa shaka yoyote. Wakaelekea hadi ilipopaki gari ya Dokta Yusha na safari ya kuelekea hospitali ya KCMC kumsafirisha Ochewa Owechi kwa ajili ya matibabu zaidi ilianza.
Daniel Mwaseba na Dokta Yusha walifika hospitalini baada ya dakika 7 na moja kwa moja mwili wa Ochewa Owechi ulipelekwa ghorofa namba mbili katika vyumba vya wagonjwa maalum. Mwili huo ulianza kushughulikiwa na Dokta Yusha mwenyewe, na shughuli ya kuitoa sumu ile iliendelea ikiwemo kuuongezea mwili ule damu na maji. Taratibu kadiri muda ulivyozidi kwenda mbele ndivyo mwili ule ulivyozidi kupungua, hali iliyoashiria sumu iliyokuwepo inazidi kupungua na hata kuisha kabisa.

"Itanibidi nirejee kule ziarani maana sijui ni kitu gani kinaendelea huko kwa sasa, hakikisha tu hakuna mtu anakisogelea hiki chumba, kuwa nae makini maana jamaa si haba huyu" alisema Daniel huku akimfunga mwanaume yule kwa pingu mguuni na mkononi, akaunganisha pingu ile na chuma kimojawapo kilichoungana na kitanda kile.

"Mfunge vizuri Daniel, maana naweza kuwa mbali halafu akapata upenyo wa kutoroka" alisema Dokta Yusha, alisimama pembeni akimtazama Daniel Mwaseba anavyomfunga jasusi yule kutoka nchini Kenya.

"Akifungua hapa nitaamini hadi mahospitalini uchawi upo. Hapa nimemfunga pingu na kamba juu, mikononi na miguuni, hizi ni kamba ngumu sana zisizokatwa kirahisi. Kuna polisi wawili pia nawaita waje kuimarisha ulinzi ndani ya chumba hiki, wakifika wasiingie hadi nitakaporejea mimi, hata nesi usimruhusu aingie, ikitokea hali ya tofauti naomba nijulishe Dokta" Daniel Mwaseba alisema akijiandaa kuondoka, kabla ya kuondoka alikumbuka kitu, aliusogelea mkono wa Ochewa na kuivua ile saa.

Akili ya Daniel ilikataa kama ile ni saa ya kawaida. Baada ya kuivua akaiweka katika mfuko wa suruali yake na kuuendea mlango.

"Pia nitalifwata na hilo briefcase Dokta," alimalizia Daniel, wakati huo alishapiga hatua kadhaa kuelekea mlangoni, akaufungua na kuondoka.

Dakika mbili baadae iliingia gari nyeusi aina ya Land Cruiser ya polisi hospitalini pale, walishuka vijana wawili waliovalia sare za polisi, bila kuchelewa waliwasiliana na Dokta Yusha. Dokta Yusuph Shaweji aliwapokea na kuwapeleka katika mlango wa chumba alicholazwa Ochewa Owechi

"Nadhani mlipatiwa maelekezo yote na aliyewatuma" alisema Dokta Yusha baada ya kuwafikisha hadi nje ya mlango wa chumba husika.

"Ndiyo, ametuambia tusitoke hapa hadi atakaporejea" alijibu mmoja kati ya polisi wale,

"Na pia tusiingie ndani wala kuufungua mlango" Polisi wa pili alijibu kwa ukakamavu. Dokta Yusha baada ya kuridhika na majibu yao aliwaacha na kuwaahidi angerejea baadae

***********

David alihamaki baada ya kuona wanajeshi wanne wakimsogelea na bunduki zao mikononi ambazo wamezielekezea kwake, akauinua mguu wa kushoto kama anataka kuipiga hatua, haieleweki ni hatua kurudi nyuma au kwenda mbele, lakini mguu ule ulibaki ungali umeinuliwa baada ya kusikika kauli ya kibabe kutoka kwa mmoja kati ya wanajeshi wale

"Tulia hivyo hivyo David, ukifanya lolote bila amri yetu tutakuumiza. Kwa usalama wako tu jisalimishe"
David akagundua miongoni mwa wanajeshi wale yupo pia Salum ambaye ni rafiki yake wa muda mrefu. Ni baada ya kuisikia sauti yake ikimuamuru ajisalimishe. Akafurahi kumwona Salum kwani aliamini asingekamatwa na rafiki yake mkubwa kama Salum, walikuwa ni marafiki walioshibana sana tangu utotoni hadi kufika wote jeshini.

"Kuna nini kinaendelea Salum? Mbona mnanijia na bunduki kama mhalifu?" aliuliza David akiinua mikono yake juu

"Sisi tumepewa oda tuje kukuchukua David, ulichokifanya hatukifahamu maana hata sisi tulipopewa oda hii tulishangaa kama ushangaavyo wewe" alijibu Salum ambeye ni rafiki yake, na pia ni mmoja kati ya wanajeshi waliokuja kumkamata

"Nani kawapatia oda ya kunikamata?"

"Amri imetoka kwa Jenerali Evance, nilipigiwa simu na kupewa amri hii. sina jinsi David, naelewa sana na nafahamu u rafiki yangu lakini hii ni amri kutoka juu" Salum alisema akimtazama David kwa macho ya huruma. Hakujua ni kosa gani rafiki yake alilifanya hadi kupewa amri ya kumkamata.

"Mnaonaje? Ni sawa kunikamata bila kosa lolote? Maana sijafanya lolote lile lililo kinyume na amri zetu, na wala sijui kwanini mnataka kunikamata, Kweli unanijia na bunduki Salum rafiki yangu ilihali nawe pia hujui kwa nini wanikamata?" David alizungumza huku akimtazama machoni Salum,

David alikuwa ni mjanja sana na mzoefu kumzidi hata Salum na wenzake waliokuja kumkamata. Alikuwa akijaribu kumlaghai Salum kwa maneno huku kichwani akitafakari namna sahihi ya kumtoka Salum na wenzake. Alijua kabisa wakimchukua kifuatacho ni nini, sheria zao zilikuwa wazi. Zilitanabaisha kama utakuwa msaliti lazima uuwawe tena kwa mateso makali.

David alikumbuka siku ya jana majira ya usiku kuna mtu alimjia na kumtaarifu makamu wa Rais anataka kuzungumza nae, alishtuka sana kwani ni jambo la kushangaza mtu kama yeye kuhitajika na makamu wa Rais, akajiuliza mheshimiwa Eliud Sumbi anataka kumwambia nini. Kweli alifuata maelekezo ya mtu yule, akapelekwa hadi kwa makamu wa rais ambapo huko alipewa dili lenye pesa ndefu, na endapo tu atalifanikisha dili hilo angepokea awamu ya pili ya fedha aliyoahidiwa, ilikuwa ni fedha ambayo hata siku moja hakuwahi kufikiri atakuja kuishika. Wanasema pesa ni mwanaharamu, hii ilimkuta pia David. Pesa aliyopatiwa na makamu haikuwa pesa ya kitoto, na pia aliahidiwa maisha mazuri na mjengo. Baada ya kukubali sasa kilichobakia ni utekelezaji, akatekeleza mpango huo na sasa yupo matatani.

"David hatupo tayari kukusikiliza, sisi tunafwata oda, geuka na zungusha mikono yako nyuma tafadhali. Hatupo tayari kutumia nguvu David" Salum alibwata, yeye na wenzake walimzunguka David na kumtia nguvuni, wakafanikiwa kumtia pingu na kuelekea naye kwenye gari. Ile gari ya pili walishuka watu wanne waliovalia mavazi ya kiuguzi, wakaibeba ile miili miwili ya wanajeshi waliozidiwa na usingizi, wakaipakia kwenye gari na safari ya kutoka kijiji cha masama kuelekea Njiro karibu na kiwanda cha Pepsi ilipo kambi ya jeshi ilianza.

****

Daniel alirejea uwanja wa chuo cha ushirika na kukuta ziara ya rais ipo karibu kutamatika. Rais Mark alishamaliza kuongea na wananchi, kilichokuwa kikiendelea ni msemaji mkuu wa serikali Bwana Amos Shemdowe alikuwa akitamatisha ziara hii kwa kumkaribisha mwigizaji maarufu wa bongo fleva nchini Tanzania, Young Chilwey aweze kutumbuiza.
Daniel Mwaseba aliangaza macho yake pale alipokuwa amekaa Chifu, alimwona. Alifuata uelekeo kumwendea chifu hadi pale alipo, Chifu Abdallah Ntenga alipomuona Daniel alinyanyuka kumfuata, wakatoka pembeni kidogo kuzungumza.

"Niambie Daniel, ulifanikiwa kumtia nguvuni yule mdunguaji?" aliuliza Chifu

"Nilifanikiwa japo amedhurika sana maana alikuwa na uwezo mkubwa, nimemwacha katika chumba maalum kule KCMC hospitali chini ya uangalizi." alieleza Daniel Mwaseba kwa utulivu mkubwa mbele ya chifu wake

"Umeweza kugundua tageti yake ilikuwa ni ipi?" aliuliza Chifu

"Sina uhakika sana, nadhani akizinduka tunaweza kumhoji akatueleza, japokuwa hati yake ya kusafiria inaeleza yeye ni raia wa Kenya"

"Jitahidi sana hizi taarifa zisizagae, fanyeni kimyakimya hadi mpate majibu kamili maana itazuka taharuki kubwa, pia pale hospitalini ni rahisi yeye kutoroka, kama umesema alikuwa na uwezo mkubwa basi pale si mahali salama, kama si kutoroka basi anaweza kutoroshwa maana anaweza kuwa na mtu au watu nyuma yake wanamfwatilia. Fanya jitihada umtoe pale na umwamishie sehemu isiyofikika. Vipi ulikagua mwili wake kujua kama ana kifaa cha kuonyesha alipo?"

"Ndiyo niligundua anacho, nilikitupia kulekule hotelini" Daniel Mwaseba alisema, baada ya hapo akamuuliza chifu kama amefahamu chochote kuhusu tukio la Helikopta kubadilishwa

"Elizabeth Neville amehisi kuna mchezo mchafu ulitendeka nyuma ya pazia, japo hajathibitish lakini mtuhumiwa ameshaanza kufwatiliwa, nadhani mtaonana baadae ili muweze kufwatilia kwa undani zaidi." Chifu Abdallah Ntenga alisema, palepale wakaagana huku Daniel akipanga kurejea tena kule hospitali alipolazwa Jasusi kutoka nchini Kenya.

Daniel Mwaseba alichukua moja ya pikipiki maalum ya jeshi la polisi iliyokuwa katika viwanja vya ushirika Moshi tayari kuelekea kule hospitalini alipomuacha jasusi Ochewa Owechi, Daniel Mwaseba aliamini kwa sumu ile iliyo ndani ya mwili wa jasusi huyo asingeweza kuzinduka ndani ya muda mfupi.

ITAENDELEA

Msimu wa pili sasa unapatikana kwa Tshs 1000 tu. Kama bado hujaumaliza msimu wa kwanza njoo whatsapp au inbox hapahapa Fb nikutumie. Ni kwa Tshs 1000 tu. Whatsapp namba 0765824715
 
Umelipia Msimu wa Pili wa Anga ya Washenzi na sijakutumia bado? Nicheki inbox nikutumie sasa. Msimu wa Pili ni , kama bado hujaumaliza Msimu wa Kwanza lipia 1000 ya Msimu wa pili nikupe Ofa ya Msimu wa Kwanza bure kabisa. Hii ni ofa kwa member wa group hili tu. Nambari ya Malipo ni M Pesa namba 0765824715
WhatsApp namba 0621249611
 
Riwaya: Anga ya Washenzi
Imeandikwa na Gilbert Evarist Mushi
Phone: 0765824715.

Msimu wa Kwanza.
Sehemu ya 07

SURA YA PILI
Katika chumba maalumu alichokuwa Ochewa Owechi, pale mlangoni walisimama polisi wawili waliokuwa makini kila sekunde, hawakutaka kosa lolote lijitokeze kwa kuwa walimfahamu vyema Daniel Mwaseba pindi mambo yanapoharibika. Walikuwa makini sana kuliko nyakati zote zile ambazo walishawahi kuwa lindoni.

Ndani ya chumba kile macho mawili ya Ochewa Owechi yalifunguka kwa ghafla baada ya kutoka katika usingizi wa kifo. Jasho lilikuwa likimchuruzika kwa kiasi kikubwa katika uso wake.

"Nyumbani... nyumbani" alitamka baada ya kuzinduka kutoka usingizi ule mbaya uliosababishwa na Daniel, bila shaka tungeweza kuuita ni usingizi wa kifo.
Jasusi yule alianza kuyatazama kwa makini mandhari ya chumba kile, akakigeuza kichwa chake uelekeo wa kushoto. Macho yake yalitua katika mkono wake wa kushoto, akautazama na mkono wa kuume pia, mikono yake yote miwili ilikuwa imefungwa kwa kamba na pingu, akajaribu kuichezesha miguu yake kwa namna ya kuitikisa, nayo ilikuwa imefungwa barabara.
Alitabasamu, moyoni alifurahi kujiona yupo huru. Pingu ile na kamba hazikuwa chochote kwake, pia ukimya wa chumba kile ulizidi kumpa ujasiri. Kwa haraka alikisogeza kichwa chake hadi katika mkono wa kushoto mahali palipochomekwa mrija unaosafirisha damu kutoka kwenye kimfuko kinachining'inia juu (dripu) hadi katika mshipa wake. Kwa kutumia meno yake aliuuma mpira ule na kuuchomoa kutoka katika mshipa wa mkono wake. Hakujali kuhusu damu zilizoanza kumtoka pale, hakujali kuhusu maumivu na uchovu wa mwili, alijali kwanza usalama wake ndani ya chumba kile. Uchovu na maumivu aliviweka kando kwanza.
Baada ya kukamilisha zoezi la kuchomoa mpira ule alikisogeza tena kichwa chake kilichojaa nywele zilizojisokota na kujitengeneza muundo wa pilipili, alikisogeza karibu kabisa na mkono wa kuume, mkono ambao pia ulifungwa imara kwa kamba na pingu, lakini alikisogeza kichwa chake karibu na mkono huo. Mkono wake ulikuwa kifungoni lakini vidole vya mkono huo kwake vilikuwa huru. Kwa kutumia vidole vile kwa hali ya tabu alianza kuzichokonoa nywele zake, ghafla waya mwembamba ukatoka ndani ya nywele zile ukielekea chini. Kwa kasi ya ajabu akageuza kichwa chake na kuudaka kwa kuubana na lipsi waya huo uliokuwa ukielekea chini. Laiti kama angechelewa ndani ya robo sekunde basi waya ule ungedondoka sakafuni na asingeweza kuuchukua kutokana na kamba na pingu alizofungwa pale kitandani. Baada ya hapo akakisogeza kichwa chake tena kitandani pembeni ya mto wa kulalia na kuuachia waya ule. Hapo akaukamata vizuri waya ule kwa kutumia meno ya mbele, meno hayo yaliubana vyema waya huo kiasi kwamba ilikuwa ni kama ameushika kwa mkono. Taratibu akausogeza mdomo wake hadi katika mkono wa kulia, ncha ya waya ule ikaelekea hadi lilipo tundu la pingu ile, mahali panapopitishwa funguo wa pingu. Amini usiamini sehemu inayopaswa kuingizwa funguo ya pingu uliingizwa waya, tena waya ambao ukamataji wake haukutegemea mikono, ni meno yalitumika.
Kichwa cha Ochewa kilikuwa kimejiegesha jirani na mkono ule, mbele ya pingu ile kwa takribani dakika mbili, alichezesha kichwa chake akikipeleka kushoto, kulia nako alikipeleka huku meno yake yakiendelea kuushikilia waya ule ilimradi tu uchokonoaji ule uweze kuifungua pingu. Dakika mbili zilikatika huku uso wake ukizidi kuchuruzika jasho jingi lililotokana na shughuli anayoifanya.
Kweli mvumilivu hula mbivu, hatimaye pingu ile ikafunguka, na hapo akaanza kuulegeza mkono wake, akakusanya mate ya kutosha mdomoni, mate yale akayapakaza katika mkono wake kwa kutumia ulimi, kuanzia kiganjani hadi katika sehemu ya mkono ilipopita kamba ile aliyofungwa, kabla mate hayajakauka akaanza kuuchezesha mkono ule huku akiulegeza kwa utaalamu wa hali ya juu, kujilegeza kule kuliufanya mkono wake uweze kunywea taratibu na kuwa mkono mdogo, hali iliyoifanya kamba ile ionekane kama haikukazwa. Na kwa urahisi tu aliutoa mkono huo ndani ya kamba ile, na hapohapo mkono wake mmoja ukawa huru baada ya kukaa kifungoni kwa muda mfupi. Mwili ulikuwa bado kifungoni lakini kitendo cha mkono wake kuwa huru kilimfanya Ochewa Owechi ajihisi huru zaidi. Ndani ya dakika mbili tu mkono wa pili na miguu yake miwili ilikuwa huru. Ochewa Owechi alianza kuusogelea mlango taratibu kabisa bila kutoa sauti, kwa mbali alisikia maongezi ya watu wawili wakijadiliana. Akageuka na kuupa mgongo mlango ule, akaanza kuzipiga hatua zake taratibu hadi lilipo dirisha la chumba kile, kwa bahati nzuri au mbaya muundo wa kioo cha dirisha lile ulikuwa na uwazi mkubwa wa kumruhusu mtu kupenya pindi tu kioo kikiwa wazi ama dirisha kufunguliwa. Hili lilimfurahisha zaidi Jasusi huyu
--------------------

Daniel Mwaseba aliwasili na pikipiki yake hadi eneo la ukumbi wa kupaki vyombo vya moto katika hospitali ya KCMC, alipoizima pikipiki ile alianza kuzipiga hatua zake harakaharaka kuelekea vilipo vyumba vya kupumzisha wagonjwa maalum, mahali alipopumzishwa Ochewa Owechi. Lakini kabla hajaingia akiwa upande wa nje aliyatupa macho yake hadi katika dirisha moja juu ghorofani, lilikuwa ni dirisha la chumba alicholazwa Ochewa Owechi. Daniel Mwaseba mbali na kuona kioo cha dirisha kikichezacheza kama vile kikifunguliwa, aliona pia kamba ndefu iliyotokezea pale dirishani ikishuka kuelekea chini. Akajua bila shaka mtu wake amekwishazinduka na yupo katika harakati za kutoroka. Alibadili uelekeo wake na kuelekea nyuma ya jengo lile, akajongea pembezoni mwa ukuta wa ghorofa ile hadi katika kona moja, kona ambayo ilikuwa ni umbali kama wa hatua tano hivi kutoka usawa wa dirisha lenye kamba ile. Akasimama hapo kumsubiri Jasusi yule aliyekuwa katika harakati za kushuka.

Ndani ya chumba kile Ochewa Owechi alifanikiwa kuunganisha kamba baada ya kuyachana mashuka kadhaa aliyoyaona ndani ya chumba kile, akaifunga vyema kamba ile katika mguu mmoja wa kitanda, akayatazama mazingira ya nje upande wa chini kupitia kioo kile pale dirishani, baada ya kuhakikisha usalama upo alifungua kioo cha dirisha na kuitupa kamba ile, taratibu akaikamata na kuanza kushuka nayo hadi chini kabisa. Kitendo cha kutua tu na kuikanyaga ardhi alishtukia akipigwa mtama uliompeleka chini. Akijiandaa kumkabili aliyempiga mtama aliwahiwa. Daniel Mwaseba alimuwahi kwa kumnyooshea bastola akimsihi aweze kutulia. Ochewa Owechi hakutarajia kitendo kile, aliukubali wepesi na umahiri wa mpinzani wake.

Dokta Yusha alitoka ofisini na kuelekea hadi katika chumba alichopumzishwa Ochewa, mlangoni aliwakuta vijana wale wakiendelea na lindo lao, wakimlinda Ochewa asiweze kutoroka ama kutoroshwa bila kujua alishatoka mle ndani. Yusha aliwajulia hali na kuufungua mlango ule...

Naam. Alipigwa na butwaa baada ya kuingia ndani ya chumba kile, chini sakafuni alishangaa kuona kamba pamoja na pingu zilizotumika kumfungia Ochewa, mpira wa dripu nao aliuona ukiwa sakafuni. Kitandani kulikuwa na vipande kadhaa vya mashuka vilivyochanwa, lakini hakumuona mwanaume yule. Aliwaita vijana waliopatiwa kazi ya kulinda chumba kile, walipoingia nao walipigwa na butwaa, wote kwa pamoja walitazama kamba iliyofungwa katika mguu wa kitanda kile ikielekea dirishani. Walipochungulia nje walimuona Daniel Mwaseba akiwa amenyoosha bastola yake kumwelekezea Ochewa, haraka nao wakatoka nje kuelekea kule chini.

Ochewa Owechi aliwaona watu watatu wakija upande walipo yeye na Daniel, wawili walikuwa ni wanaume waliovalia sare za polisi huku mmoja akiwa na mavazi ya kidaktari. Palepale alipata wazo la kujiokoa baada ya kuona nafasi finyu ya kutoroka. Alishika upande wake wa kushoto wa kifua chake, akaanza kuugulia maumivu kwa mtindo wa kutetemeka, jasho la ajabu lilianza kumtoka usoni na kumfanya Dokta Yusha ambaye alishafika karibu aweke mikono yake kichwani.

"Daniel huyu anatufia, moyo wake unaonekana kumuuma sana" Dokta Yusha alisema huku akizidi kumsogelea Ochewa aliyekuwa katika hali mbaya.

"Hapanaa! Usimsogelee Dokta," Daniel alipiga ukelele uliomfanya Dokta Yusha kusimama ghafla,
"wacha mimi nimwangalie" Daniel alisema huku akimsogelea Ochewa kwa tahadhari kubwa. Na wakati huo mwili wa Ochewa Owechi ulianza kutulia pale chini.

"Mtu ana hali mbaya wewe unahisi ni mchezo anatuchezea? Hahaha" Dokta Yusha alisema na kucheka kidharau, alimwona Daniel ni kama mtu asiye na ubinadamu. Lakini Daniel Mwaseba hakujali, alimsogelea Ochewa pale chini kwa tahadhari kubwa huku akimsihi Dokta Yusha kukaa mbali.

"Daniel wewe ni mnyama, kila muda unawaza tu hatari badala ya kuihisi, haya sasa huyo katulia, sasa sijui kafa ama kapoteza fahamu, yote haya ni sababu ya wewe. Dokta Yusha alisema huku akirudi nyuma kidogo na kumpisha Daniel Mwaseba. Daniel kwa tahadhari kubwa aliinama kidogo na kuunyoosha mkono wake kuelekea katika kifua cha Ochewa Owechi ili kusikilizia mapigo ya moyo.

ITAENDELEA

Bado tunaendelea na msimu wa kwanza.... Lipia Tshs 1000 tu kwa ajili ya msimu wa pili kisha njoo whatsapp nikutumie msimu wa pili nikuzawadie na msimu wa kwanza bure. Nambari ya Malipo ni M Pesa namba 0765824715, WhatsApp 0621249611
Tuma ujumbe mfupi ukisema Msimu wa pili wa Anga ya Washenzi nami nitakutumia na msimu wa kwanza pia kama ofa.
 
Leo Usiku katika Anga ya Washenzi

Daniel akazunguka hadi nyuma ya gari na kuibonyeza batani mahususi iliyopo katika mlango wa buti na kufungua.
Looh!..
Teke zito kutoka katika mguu wa Ochewa lilikipangusa kidevu cha Daniel Mwaseba na kumfanya Daniel ayumbe kiasi na kuelekea chini bila kutarajia, lilikuwa ni teke zito lililopigwa kwa kasi pindi tu Daniel alipoufungua mlango wa buti. Daniel akiwa pale chini alianza kutema damu, na meno yake mawili ya mbele yalikuwa yamelegea tayari. Daniel Mwaseba alinyanyuka kwa hasira, wakati huo Ochewa alisharuka na kutoka ndani ya buti.

Gilbert Mwaitika, Daniel Mwaseba mwenye hasira kuu pamoja na Mwanasheria Mlevi wakamzunguka Ochewa Owechi na kuanza kumsogelea.

Wakati huo Elizabeth Neville pamoja na Cara walishaingia ndani ya kambi hii mpya. Waliingia pasipo kujua ni kipi kinaendelea huko nje.

Ni Saa moja Usiku. Watag marafiki waje waisome.
Simulizi Za Gilbert ... Home of Novels
 
Back
Top Bottom