Mshana Jr
Platinum Member
- Aug 19, 2012
- 360,924
- 831,405
- Thread starter
- #321
Mmmh... Ila wasingemuua bali wangempa ulemavu wa kudumu.... Wanaobisha hawajawahi kukutwa na haya majanga
Anaekataa uchawi haupo, basi na aendelee kukataa vivyo hivyo. Nakupeni visa kadhaa vilivyowahi kutokea katika maisha yetu(Kifamilia).
Mnamo mwaka 2005 zikiwa zimebaki siku takribani 4 kufika Xmas, kuna mjukuu wa kwanza wa mama, alianza kuwa anaanguka, hapa ndipo nilipochoka. Humuoni akianguka, ila unamuona akijikung'uta tu kutoka chini.
Kile kitu kiliwashinda aliokuwa anacheza nao(wadogo zetu) wakamwambia mama, mama akajifanya mkali, anamwambia aache upumbavu wake wa kujiangusha, atampiga. Dogo akamwambia, bibi miguu haina nguvu na mimi sijiangushi! Mama akamwambia hebu njoo ukae hapa nione kama utaanguka, dogo akaenda kukaa mbele ya mama. Kidogo tukamuona anajikung'uta vumbi kutoka chini, mama akasema umefanyaje!!!? Hapo sasa wote tupo tunamuangalia.
Hatujakaa sawa, tukamuona tena anainuka kutoka chini, mama akasema tuingine ndani, ile kuingia ndani, tukamuona mlangoni anainuka kutoka chini, tukaingia ndani, akawa anaangalia juu pande zote za ndani akiwa amekaa kwenye kiti, mama nikamwambia aache ukali wake kwani hautasaidia chochote kujua ukweli wa unaosumbua.
Usiku ukafika tukalala, hali ikawa ile ile. Mama akanambia hebu mchukue mpeleke kwa fulani(huyo nloagizwa kwake alikuwa ni mganga wa majini alokuwa akitutibia nyumbani). Nikafika, nikamueleza, akachukua vitu vyake akaanza kumkanda miguu, akagunaaa, akasema huyu mbona Miguu imeshakufa! Ni ya baridi kabisa, ila haina shida nitapambana nayo. Akamkanda pale akanambia kaeni mpumzike kidogo, ukiondoka usiage wala kumsemesha yeyote ila ukifika nyumbani umwambie dada(mama sasa) aje jioni nataka aongee na Maimuna. Nikasepa nikafika hom, mama nikampa ujumbe jioni akaenda.
Akaenda kilingeni, yule mganga akapandisha, Maimuna kaja wakaanza kupiga stori hapo akamwambia kuna watu wanataka kumuua huyo mjukuu, asipofanya juhudi basi xmas ya mwaka huo itakuwa na msiba, mama akaelekezwa cha kufanya, akafanya huku dogo akaendelea na maisha fresh mpaka leo na yeye sasa hivi ana mtoto.




