frema120
JF-Expert Member
- Jan 1, 2012
- 5,098
- 1,341
Rais JK kamteua Bwn RISHED BADE kuwa kamishina mkuu wa TRA Tanzania leo
===========================================================
===========================================================
![]()
Rished Bade
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete amemteua Bwana
Rished BADE kuwa Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA).
Kulingana na Katibu Mkuu Kiongozi Balozi Ombeni Sefue, uteuzi huu umaanza tarehe 06 Mei,
2014. Bwana BADE anachukua nafasi iliyoachwa wazi na Bwana Harry KITILYA ambaye alistaafu
tarehe 14 Desemba,2013.
Kabla ya uteuzi huo, Bwana BADE alikuwa Naibu Kamishna wa Mamlaka ya Mapato Tanzania
tangu Septemba,2012 na baadaye kukaimu nafasi ya Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Mapato Tanzania tangia Bwana Kitilya alipostaafu.
Kabla ya kujiunga na Mamlaka ya Mapato Tanzania, Bwana Rished BADE amewahi kufanya kazi
katika maeneo mbalimbali yaliyompa ujuzi na weledi mkubwa kwenye mambo ya fedha na mapato
kama ifuatavyo:-
Oktoba, 1995 – Mei, 2000 – Mkaguzi wa Benki za Biashara, Benki Kuu ya Tanzania.
Juni, 2000 – Juni, 2001 – Credit Manager, Akiba Commercial Bank.
Juni, 2001 – Septemba,2001 – Chief Financial Officer, Akiba Banking Corporation.
Septemba, 2001 – Machi, 2006 – Chief Operating Oficer, Barclays Bank (Uganda).
Januari, 2007 – Desemba, 2009 – Chief Executive Officer, Barclays Bank (Tanzania)
Desemba, 2009 – 2012 – Chief Financial Officer, (East and West Africa Cluster) Barclays Bank
Plc Emerging Markets.
Novemba, 2010 – Septemba, 2012 – Chief Executive Officer, Tanzania Mortgage Refinance
Company.
Bwana Rished BADE ana Shahada ya Kwanza ya Bachelor of Commerce and Management ya Chuo
Kikuu cha Dar es Salaam (1995); Shahada ya Master of Commerce in Banking and Finance ya Chuo
Kikuu cha Sydney (1999), na ni Certified Public Accountant (CPA).
Katika kumteua kuwa Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Mapato Tanzania, Mheshimiwa Rais ana
imani kubwa kwa elimu, uzoefu na weledi alionao, Bwana Rished Bade kwa kushirikiana na
watumishi wenzake, atatoa mchango mkubwa kwa Taifa kwa kuzidi kuimarisha Mamlaka hiyo na
kuboresha utendaji wake na hivyo kuongeza mapato ya Serikali kwa faida ya Taifa.
Imetolewa na:
Premi Kibanga,
Mwandishi wa Habari wa Rais Msaidizi,
Ikulu - Dar es Salaam.
Salute to all JF Great Thinkers..
Naamini waheshimiwa wengi tu wanakuja kuchungulia hapa JF na kujua yanayojiri ndani ya jamii.
Taarifa iliyopo ni kuwa TRA wamepata boss mpya, pasi na kujali elimu na ujuzi alionao, kamwe hawezi kujua kero zote zinazowakabili walipa kodi..ikiwezekana tumpe inputs,kero,ushauri ili kama ataweza kuzitafutia ufumbuzi well and good, kama hataweza basi ajue kuwa zipo na zinakera...huwezi kujua, kila mtu ana style ya utendaji kazi wake, wengine wanapenda ushauri na kuzifanyia kazi na wengine hawaambilikiz, jukumu letu ni kupiga mayowe tunapohisi the game is not fair..
1. Nimeona watu wengi humu wanalalamikia sana ushuru wa ku import gari nchini uko juu sana.
2. Andaa njia rahisi ya watu kulipa kodi,ushuru i.e online payments kadiri iwezekanavyo kuokoa muda na usumbufu wa kutoa rushwa..watu hawapendi kwenda TRA offices kukwepa usumbufu wa kubambikiziwa unfair taxes.etc
3. Annual motor vehicle licence fees inatuua Mr. Bade (you can not enrich poor people by making rich people poor - Ex U.S President A. Lincoln)
4. Viwango vya kodi na ushuru viwe reasonable na realistic ili zisiforce watu kukwepa kulipa that leads to tax evasion..fair taxes encourage taxpayers to pay voluntarily.
5. Tengenezeni website/blog yenu watu wapost complains zao humo.
Nawapisha wadau wengine muongeze hapo, nitarudi tena.
However, tunakutakia kila la heri Mr Bade.