Ripoti ya tume ya maadili ya Philip Mangula iko wapi?

Kwangu mimi Mangula ni kiongozi wa mfano daima. Mangula ndiye aliyeijenga CCM na kuiwezesha kumuongezea kura Mkapa mwaka 2000 na pia kumpa kura za kumwaga Kikwete mwaka 2005. Lakini pamoja na jitihada zake nyingi alizozifanya kwa maslahi ya chama chake akaishia kutoswa na Kikwete. Nina uhakika Mangula angekuwa bado yupo CCM CHADEMA wasingefurukuta maana mzee alikuwa ni mtaalamu wa propoganda hasa. Ninakumbuka pale aliyakatalia mataifa ya magharibi kuingilia mgogoro wa Zanzibar. Na akafanikiwa kuingia kwenye mazungumzo ya muafaka na CUF. Hata kama hayakuwa na mafanikio, angalau yalisaidia kuleta hali ya utulivu Zanzibar.

Inasikitisha sana kuona nyota yake inazimwa kirahisi kiasi hiki. Laiti isingekuwa ni hofu ya kukolimbwa naamini Mangula angeweza hata kwenda CHADEMA akakijenge CHADEMA pia. Lakini Mungu amemlipa sana. Naamini huko Africa kusini atakuwa analipwa vema kuliko hata angekuwa bongo.
 
  • Thanks
Reactions: FJM
Hata kama angelikuwepo. Watanzania si kama zamani. Nyie mnafikiri ni Mabwege tu wa kubebwa kama watoto.

Mtaji mkubwa wa Chadema ni matatizo ya Wananchi yanayotokana na ukilaza wa CCM/mwamko wa Watz. Sasa kama Magamba wako busy kujitajirisha na nchi inauzwa kila siku, unafikiri watu wataacha kutafuta mbinu wajinasue na matatizo?

Kama Kikwete angelikuwa kiongozi mwenye kujali, basi mengi tunayosema leo wala tusingelisema. Ila sasa, watu wazuri wote kwa sasa hawatakiwi CCM. Sasa unategemea Mangula angelibaki? Ilikuwa lazima atoswe. Yamebaki mazee yenye fikra za kuleta watoto wao wawe Marais.
Kila hali inaonyesha kuwa Kikwete aliletwa na Mwinyi na nafikiri lengo ilikuwa ni Kikwete amuachie Mwinyi mtoto awe Rais. Sijajua kama watamfanya awe Rais wa Tanzania au Zanzibar...... Zenji wanamfaa ili huko nako mabomu yalipuke maghalani.
Kwangu mimi Mangula ni kiongozi wa mfano daima. Mangula ndiye aliyeijenga CCM na kuiwezesha kumuongezea kura Mkapa mwaka 2000 na pia kumpa kura za kumwaga Kikwete mwaka 2005. Lakini pamoja na jitihada zake nyingi alizozifanya kwa maslahi ya chama chake akaishia kutoswa na Kikwete. Nina uhakika Mangula angekuwa bado yupo CCM CHADEMA wasingefurukuta maana mzee alikuwa ni mtaalamu wa propoganda hasa. Ninakumbuka pale aliyakatalia mataifa ya magharibi kuingilia mgogoro wa Zanzibar. Na akafanikiwa kuingia kwenye mazungumzo ya muafaka na CUF. Hata kama hayakuwa na mafanikio, angalau yalisaidia kuleta hali ya utulivu Zanzibar.

Inasikitisha sana kuona nyota yake inazimwa kirahisi kiasi hiki. Laiti isingekuwa ni hofu ya kukolimbwa naamini Mangula angeweza hata kwenda CHADEMA akakijenge CHADEMA pia. Lakini Mungu amemlipa sana. Naamini huko Africa kusini atakuwa analipwa vema kuliko hata angekuwa bongo.
 
Dah! Huyu mangula amepotea katika jukwaa la siasa..JK anaonekana ni mtu wa kulipa visasi sana.
 
Inasemwa kwamba kati ya makosa makubwa aliyoyafanya Mr JK ni kumtoa mangula Ukatibu Mkuu!! Its a BIG MISTAKE EVER FOR JK NA SERIKALI YAKE.
 
Hata kama angelikuwepo. Watanzania si kama zamani. Nyie mnafikiri ni Mabwege tu wa kubebwa kama watoto.

Mtaji mkubwa wa Chadema ni matatizo ya Wananchi yanayotokana na ukilaza wa CCM/mwamko wa Watz. Sasa kama Magamba wako busy kujitajirisha na nchi inauzwa kila siku, unafikiri watu wataacha kutafuta mbinu wajinasue na matatizo?

Kama Kikwete angelikuwa kiongozi mwenye kujali, basi mengi tunayosema leo wala tusingelisema. Ila sasa, watu wazuri wote kwa sasa hawatakiwi CCM. Sasa unategemea Mangula angelibaki? Ilikuwa lazima atoswe. Yamebaki mazee yenye fikra za kuleta watoto wao wawe Marais.
Kila hali inaonyesha kuwa Kikwete aliletwa na Mwinyi na nafikiri lengo ilikuwa ni Kikwete amuachie Mwinyi mtoto awe Rais. Sijajua kama watamfanya awe Rais wa Tanzania au Zanzibar...... Zenji wanamfaa ili huko nako mabomu yalipuke maghalani.
Kuna jamaa yangu nilikuwa napiga naye story those days Mangula akiwa katibu mkuu wa CCM, aliniambia Mangula ndiyo think tank ya Taifa. Kwamba alikuwa ana uwezo hata wa kumwagiza Mkapa afanye hili au lile. Halafu Mkapa naye akawa anamfurahia sana namna ambavyo mawazo yake yalikuwa yanatekelezeka.

Lakini naamini sana kwamba katika kipindi hiki cha Kikwete, kama Mangula angekuwa ndiye katibu mkuu wa CCM ni either angeresign au angefukuzwa, kwa kuwa Kikwete anataka aonekane yeye yupo juu ya kila kitu. Hapendi wachapakazi na anapenda sana kuonekana kwa watu. Kwa hiyo asingependa kabisa aamrishwe na Mangula kutekeleza baadhi ya mambo. Nafikiri wote mnakumbuka vizuri kampeni za CCM za wakati ule wa akina Mangula. Na mnaweza kutofautisha na hizi za mwaka jana.

CCM wamepoteza Kichwa mhimu sana. Kuna haja ya kumwomba ajiunge na CHADEMA. Pengine atatupa tips mhimu za kuimaliza CCM. Ngoja nitakwenda kumuongelesha nione anasemaje.
 
Kuna jamaa yangu nilikuwa napiga naye story those days Mangula akiwa katibu mkuu wa CCM, aliniambia Mangula ndiyo think tank ya Taifa. Kwamba alikuwa ana uwezo hata wa kumwagiza Mkapa afanye hili au lile. Halafu Mkapa naye akawa anamfurahia sana namna ambavyo mawazo yake yalikuwa yanatekelezeka.

Lakini naamini sana kwamba katika kipindi hiki cha Kikwete, kama Mangula angekuwa ndiye katibu mkuu wa CCM ni either angeresign au angefukuzwa, kwa kuwa Kikwete anataka aonekane yeye yupo juu ya kila kitu. Hapendi wachapakazi na anapenda sana kuonekana kwa watu. Kwa hiyo asingependa kabisa aamrishwe na Mangula kutekeleza baadhi ya mambo. Nafikiri wote mnakumbuka vizuri kampeni za CCM za wakati ule wa akina Mangula. Na mnaweza kutofautisha na hizi za mwaka jana.

CCM wamepoteza Kichwa mhimu sana. Kuna haja ya kumwomba ajiunge na CHADEMA. Pengine atatupa tips mhimu za kuimaliza CCM. Ngoja nitakwenda kumuongelesha nione anasemaje.
Kuna version nyingine niliosikia ni kwamba Mangula alikuwa ame compile, kwa kushirikiana na UWT, madhambi ya Kikwete na jinsi alivyopata utajiri wa haraka---corruption. Ile ripoti ilikuwa itolewe mbele ya kikao kikuu cha kujadilia wagombea. Lakini ripoti hiyo ilizimwa na Mkapa kwa kusema kuwa hakuna aliye msafi ndani ya CCM. Hilo likawa anguko la Mangula baada ya Kikwete kuteuliwa kuwa mgombea. Pia si kweli kuwa Mkapa alimtaka Salim. Ni yeye aliyesema kuwa hawezi kumwachia nchi Mwarabu.
 
Kuna version nyingine niliosikia ni kwamba Mangula alikuwa ame compile, kwa kushirikiana na UWT, madhambi ya Kikwete na jinsi alivyopata utajiri wa haraka---corruption. Ile ripoti ilikuwa itolewe mbele ya kikao kikuu cha kujadilia wagombea. Lakini ripoti hiyo ilizimwa na Mkapa kwa kusema kuwa hakuna aliye msafi ndani ya CCM. Hilo likawa anguko la Mangula baada ya Kikwete kuteuliwa kuwa mgombea. Pia si kweli kuwa Mkapa alimtaka Salim. Ni yeye aliyesema kuwa hawezi kumwachia nchi Mwarabu.
Duh, kumbe kuna mengi behind the scene. Nilipopigia mstari sikuwa najua kabisa kama kuna habari hiyo. Hii kali kwakweli.
 
Salim ahamed salim alistahili kuwa rais wa tanzania baada ya mkapa, cha kushangaza zilitumika nguvu nyingi toka zanzibzr, kesho utawasikia urais zamu yetu kwa sasa, nadhani kwa kumkataa salim, wasipate tene nafasi hiyo
 
msema hovyo nimerudi baada ya kukaa mafichoni kwa muda mrefu kidogo nikipanga mipango ya maandamano makubwa ya kumng'oa ngeleja na rais wake. Kwa bahati mbaya inteligensia yetu imetutonya kwamba tayari intelijensia ya polisi ilikuwa inatufuatilia kwa karibu na hivyo tungeweza kuishia jela kabla ya maandamano kuanza. Tunajipanga kwa strategy mpya kwa sasa.

Lakini leo nimekuja na hili kubwa ambalo nimelipata kutoka vyanzo vya uhakika ndani ya ccm. Ni kwamba kisa cha mangula kutoswa na kusahaulika kabisa ni kutokana na mangula kugoma kumpa jk form ya kugombea urais. Inasemekana mangula katika uzoefu wake alikuwa anamjua kikwete kama mtu asiye na uwezo wa kuongoza nchi, lakini anayependwa sana na watanzania. Mangula alijua katika hali yoyote, kama kikwete angefanikiwa kupata form lazima angeshinda urais, na namna pekee ya kumuengua ilikuwa ni kumnyima form.

Inasemekana mwinyi (ali hassan) ndiye aliyemkomalia mangula plus mkapa kwamba wampe jk form akakataliwe na wananchi. Katika targeti yao, mkapa na mangula walitaka salim a salim ndiye achukue urais na si kikwete. Lakini kutokana na ubabe wa mwinyi na hofu ya kwamba kama mwinyi angeamua kuside na kikwete kungeleta mpasuko ndani ya chama, basi ikabidi akina mangula waruhusu jk achukue form ya urais. Na matokeo yake ndiyo haya tunayoona sasa. Kikwete anaendesha nchi hovyohovyo.

Shida zote tunazozipata watanzania, chanzo ni mwinyi. Ndiyo maana jk alitumia muda mwingi sana kumshukuru mwinyi katika hotuba yake ya kwanza bungeni. Habari ndiyo hiyo.



aisee kama ni mwinyi basi sitoshangaa hii nchi anaongoza na akili za salma kikwete unakumbuka huyu mwinyi nyerer alimtolea uvivu rais anafanya kazi kwa mawazo yamkewe pale mama siti mwinyi alipodondoka na makontena kadhaa ya jenereta natumaini kama yupo huko bandarini wanaumizana hivi sasa ...duh kazzi ipo na maaskofu maapadre ndio wanazidi kudai katoka kwa bwana mi huyo bwana naitaji kumjua yupi nimejaribu kusali kila sala lakini siso huyu bwana yesu tunae mjua nanyi viongozi wa kanisa acheni kujizalilisha na shida zenu mkichoka kuongea kama mmnazeeka kaeni kimywa watoto wenu watalishwa na mungu tu na alaaniwe amtegemeaye mwanadamu
 
CCM ilikufa siku wamemtoa Philip Mangula na kumuweka Yusuf Makamba. The party will NEVER be what is it was before. Zamani ulikuwa ukimuona Mangula kwenye gari unasimama na kumuangalia vizuri - kama celebraty fulani hivi. It is very unfortunate wengine wote waliofuata Mukamba na Mukama wanaonekana kama majambazi. Na kuna kipindi mtu unajiuliza hivi huyu Mukama mtu na heshima zake alikubalije kufanya kazi ya ukatibu hiki chama cha wasanii?
 
Jamani kiongzi wa Tanzania asisifiwe kuikomboa nchi za kusini mwa africa, bali asifiwe kwa kuwakomboa wananchi wake waishio bila kazi. Wala asisifiwe kwa kuwavimbia mataifa ya maghalibi, bali asifiwe kwa kumwaga wasomi wengi mitaani. HUyuMangula acha tuu atoswe na Kikwete. Kwanza naye aliikana dini na aliuhusudu sana ukomunisti wa Cuba. Alifikia mpaka kufuga ndevu kama kastro au samora. Kama haya ya kutoswa na kikwete ni ya ukweli, basi nampa hongera sana kikwete.Cha maana huyo mangula alichowafanyia wananchi hakijulikani kabisaa.
 
..Sakata la mzee Philip Japhet Mangula ni kubwa kiasi chake, hasa zinapotajwa siasa za majitaka za sisiemu. Kwa kuwa Mangula alikuwa katibu mkuu wa sisiemu baada ya akina Horace Kolimba na Lawrence Gama, alimjua vema sana JK. Lilipotokea suala la uchaguzi wa mwaka 2000, Mangula alimpa negative credits JK katika preliminary assessment, kwa kuwa alimjua kuwa ni mtu wa mzaha asiyeweza kufanya maamuzi katika chama. Negative credits za JK pia zilitoka kwa mzee Malecela. Lakini kwa kuwa Rostam na wenzake kwenye sisiemu mtandao walikuwa wamepenyeza rupia kwa wajumbe wa NEC na CC, JK alipita kwa kura nyingi. Sasa suala ni kwamba, baada ya vikao hivi vya NEC na CC, JK alivujishiwa habari kwamba Mangula alimnyima credits kwamba hafai kuwa rais wa nchi! Visa vikaanzia hapa. Baada ya JK kuwashinda Mark Mwandosya na Salim Ahmed katika kura za mwisho (baada ya kubadili kanuni za chama kwa hila) akapitishwa kuwa mgombea na kisha kushinda uraisi!
Mnamo mwaka 2007 katika uchaguzi mkuu wa viongozi wa sisiemu, kundi la mtandao (likiongozwa na JK) likafanya kila hila kuwaondoa katika nafasi za chama watu ambao haliivi nao na kisha kuwapachika watu wao. Mwathirika wa kwanza akawa ni katibu mkuu wa chama, mzee Mangula, ambaye alitunza kwa uaminifu nidhamu ya chama kwa kipindi chake chote. Mwathirika wa pili akawa waziri mkuu mstaafu, mzee Malecela, aliyekuwa makamu wa mwenyekiti kwa miaka kumi ya utawala wa Mkapa. Vurugu haikuishia hapo. Baada ya Mangula kuonja shubiri kidogo, akajitosa kuwania uenyekiti wa chama kwa mkoa wa Iringa. Huku nako wanamtandao walikuwa washamtangulia kwa rushwa na visasi. Huku akapambanishwa na Mheshimiwa Deo Sanga (aka Jah People, kwa sasa ni mbunge), huyu alikuwa diwani wa kata ya Makambako enzi hizo. Akamshinda Mangula katika uchaguzi huo, uliokuwa vurugu tupu! Tangu hapo mheshimiwa Mangula hajasikika sana katika siasa za chama, ingawa yupo akiendelea na shughuli zake za kilimo kijijini kwake Kinenulo Imalinyi Njombe. Kutokana na kuyumba kwa chama tangu enzi za katibu Makamba, akina JK na kundi lake wanashindwa kumfuata Mzee Mangula kwa ushauri, kwa sababu bado anakumbuka walivyomfanyia hila mwaka 2007 na wao mtandao wnaona aibu kwa waliyomfanyia. Kipimo walichompimia Mangula ndicho wanachopimiwa sasa, ingawa cha kwao kimejazwa, kimeshindiliwa na sasa kinasukwasukwa. Historia itajiandika
Hakika sisiemu watamkumbuka mtu huyu.
 
Idimi,
Nimekukubali. Lakini kumbukumbu zangu ni kwamba Mangula aliondolewa ukatibu mkuu mara tu baada ya Kikwete kuukwaa uenyekiti wa CCM.
 
Idimi,
Nimekukubali. Lakini kumbukumbu zangu ni kwamba Mangula aliondolewa ukatibu mkuu mara tu baada ya Kikwete kuukwaa uenyekiti wa CCM.
Mhe Jasusi, uko sahihi kabisa, Mkapa aliachia uenyekiti wa sisiemu kabla ya muda kamili wa kuachia nafasi hiyo haujafika, akamuachia mwenyekiti wa sasa mhe. Kikwete, ambaye aliitumia nafasi hiyo effectively kuwaondoa wale asiowataka. Hope unakumbuka vizuri jinsi wanamtandao walivyovuruga uchaguzi wa mwaka 2007 katika ngazi zote, na vurugu zile hazijaisha, wanamtandao wanajipanga kwa uchaguzi mkuu wa chama mwakani. Wale wasioiva na JK (kutoka makundi ya Sumaye, Mwandosya na Salim) ndo wanataka kumvua uenyekiti, ili asiwe na nguvu katika chama, picha ndo kwanza inaanza. Kiini hasa cha kuvuana magamba ni juhudi za kutaka ku-deal na hao wanaotaka kumpoka hilo rungu. Anayeua kwa upanga hufa kwa upanga pia.
 
Idimi nimekuvulia kofia mkuu. Nimeridhika sana na taarifa ulizozileta hapa. Kwa bahati mbaya sana sikuweza kureact mapema kwenye hizi hoja kwa kuwa sikuwa na umeme kwa zaid ya wiki nzima. Ulikuwa unakuja usiku unaondoka asubuhi.
Ila Mangula atabaki kuwa shujaa daima, maana alikuwa ni kiona mbali cha nchi.
 
Mhe Jasusi, uko sahihi kabisa, Mkapa aliachia uenyekiti wa sisiemu kabla ya muda kamili wa kuachia nafasi hiyo haujafika, akamuachia mwenyekiti wa sasa mhe. Kikwete, ambaye aliitumia nafasi hiyo effectively kuwaondoa wale asiowataka. Hope unakumbuka vizuri jinsi wanamtandao walivyovuruga uchaguzi wa mwaka 2007 katika ngazi zote, na vurugu zile hazijaisha, wanamtandao wanajipanga kwa uchaguzi mkuu wa chama mwakani. Wale wasioiva na JK (kutoka makundi ya Sumaye, Mwandosya na Salim) ndo wanataka kumvua uenyekiti, ili asiwe na nguvu katika chama, picha ndo kwanza inaanza. Kiini hasa cha kuvuana magamba ni juhudi za kutaka ku-deal na hao wanaotaka kumpoka hilo rungu. Anayeua kwa upanga hufa kwa upanga pia.
Mkuu habari hizi nzuri sana hebu endelea kutupa zaidi..mwaka huu tutasikia mengi sana..bado wanavuana magamba, kuna kambi rasmi ya upinzani ndani ya ccm(ccj), bado matatizo kibao na ahadi hewa za ccm...
Mhe Jasusi, uko sahihi kabisa, Mkapa aliachia uenyekiti wa sisiemu kabla ya muda kamili wa kuachia nafasi hiyo haujafika, akamuachia mwenyekiti wa sasa mhe. Kikwete, ambaye aliitumia nafasi hiyo effectively kuwaondoa wale asiowataka. Hope unakumbuka vizuri jinsi wanamtandao walivyovuruga uchaguzi wa mwaka 2007 katika ngazi zote, na vurugu zile hazijaisha, wanamtandao wanajipanga kwa uchaguzi mkuu wa chama mwakani. Wale wasioiva na JK (kutoka makundi ya Sumaye, Mwandosya na Salim) ndo wanataka kumvua uenyekiti, ili asiwe na nguvu katika chama, picha ndo kwanza inaanza. Kiini hasa cha kuvuana magamba ni juhudi za kutaka ku-deal na hao wanaotaka kumpoka hilo rungu. Anayeua kwa upanga hufa kwa upanga pia.
Mkuu habari hizi nzuri sana hebu endelea kutupa zaidi..mwaka huu tutasikia mengi sana..bado wanavuana magamba, kuna kambi rasmi ya upinzani ndani ya ccm(ccj), bado matatizo kibao na ahadi hewa za ccm...
 
Back
Top Bottom