Ripoti ya Kifo cha Mwangosi

Ripoti ya Kifo cha Mwangosi

Nimeisoma kwa makini ripoti hii ya kifo cha Mwangosi hakika imeniliza, imeniuma sana. Hakika pamoja na machozi yangu nukuu hizi zimenichefua sana.


“Baada ya kuvunjwa kwa ghasia,Mwangosi alikimbilia walipo polisi na kitu kama bomu kikarushwa na kundi la watu waliokuwa wanakimbia na kumlipua Mwangosi“ – Gazeti la Habari Leo


“Kilichosababisha kifo cha Mwangosi ni kitu kilichorushwa na kundi la watu.Polisi wanachunguza” – Gazeti la Mwananchi


“ Hii ni amri na polisi hairuhusu maswali zaidi kuhusu suala hili” – RPC Kamuhanda


Nukuu hizi katika ripoti hii zimenikera sana sana. Magazeti ya Mwananchi na Habari Leo yamemsaliti Mwangosi. Inakera sana. Inakuaje chombo cha habari tena chenye ripota kwenye eneo la tukio kije na nukuu kama hii iliyojaa utumbo na uzandiki? Yaani mazingira ya tukio yanavyoelezwa na ripoti hii gazeti linawezaje kuja na propaganda ya kipuuzi kabisa kuwa Mwangosi aliuawa kwa kutupiwa kitu kizito?

Lakini nukuu hiyo ya Kamuhanda ndiyo ujinga mkuu katika ripoti hii. Kwa mentality hizi za Jeshi la Polisi hakika tutegemee maafa makubwa zaidi.

Hakika MCT wamefanya kazi kubwa inayostahili pongezi na wameweka kumbukumbu sahihihi ingawa Jeshi la Polisi lililozoea kuua raia badala ya kuwalinda halitakoma kufanaya hivyo as far as limeweka weledi wote pembeni na kukubali kutumika kisiasa.

Madamu kasi ya CCM kudondoka ni kubwa kadri upinzani unavyozidi kuijitanua tutegemee msuguano na vifo vingine vingi maana Jeshi la Polisi sasa limebadilika na kuwa Idara ya Ulinzi ndani ya CCM na limejikabidhi jukumu kubwa la kudhibiti wapinzani.Tusubili tuone ingawa daina huwezi kushindana na umma unaotaka mabadiliko maana hakika umechoka.



Ripoti hii imeniliza, imeniuma sana. Siwezi kuendelea zaidi. R.I.P Mwangosi.
 
Wana JF heshima mbele,
Report ya Mauaji ya Mwangosi imetolewa hadharani leo,wenye data kamili tunaomba tuijadili,naona kama imekwepeshwa na kupindishwa sababu ya kesi iliyopo mahakamani!
Pesa zimeliwa,hakuna litakalofanyiwa kazi!
 
mambo mengi kwenye hiyo ripoti nilishayasoma sana kwenye vyombo vya habari. Tusubiri na hiyo ripoti nyingine ambapo nahisi itakuwa imechenga wee bila ukweli.
 
MUHUSIKA MKUU WA HAYO MAUWAJI NI M4C, CCM haihusiki! soma vizuri report.

m4c ndio iliompiga bomu? Unaongea kama humjui mungu? Unajiona we ni mungu mtu mwenye mamlaka ya kuamuru au kifurahia kifo cha mwenzio? Mwogope mungu kakabau dada sijui.
 
Ripoti imetoka polisi walimpiga na kumtesa Marehemu Daudi mwangosi kabla ya kumuua na bomu la machozi.

Chagonja ni muongo! mzandiki! ana fikra mgando! aliudanganya umma kuwa mwangosi aliuwa na kitu kizito.
 
Ulitegemea la muhimu kutoka kwa watuhumiwa wanaojichunguza?
 
Hii si ripoti bali upuuzi. Kwanini polisi waue watuhumiwe na wajichunguze na kutoa ripoti? Hapa hamna kitu bali mauza uza
 
Hapa ndio hutamani Chadema wawe wanatuambia wananchi wakishika dola kesi zote hizi zinafufuliwa na ikibidi wawe na kitengo cha kukusanya ukiukwaji wote wa haki za binadamu.

Nataka kisasi kwa yote haya! Bila kisasi damu hizi zitakuwa zimeenda bure!!!
 
:spy:WAUNGWANAAAAAAA hii ni danganya toto,na ni UPUMBAVU MTUPU.Kama ni kamati ya ukweli kwa nini isitoe itimisho lenye mapendekezo.KAMA WANAJUA SUALA LIKO MAHAKAMANI ni kwa nini iliundwa hiyo kamati?wasituhadae watz,sasa hatudanganyiki.
 
Kifungu kimojawapo cha ripoti kama mapendekezo kinasema hivi:"-Kufanya marekebisho ya Sheria ya Vyama vya Siasa Na. 5 ya 1992 ili kuweka wazi shughuli za Vyama vya Siasa baada ya Uchaguzi Mkuu. Lengo ni kuwa Shughuli za Siasa zihamie Bungeni kujadili na kuhoji mipango ya Serikali na matumizi ya rasilimali za nchi. Kwa kufanya hivyo wananchi watapata nafasi kufanya kazi za maendeleo."
Naona huu ni utapeli wa fedha zetu kwa kuandaa tume mfu...chama cha siasa kitaachaje kujiimarisha eti shughuli za kisiasa zisubiri wakati wa uchaguzi....huu ni ushenzi wa hali ya juu na ukosefu wa weledi. Wametumwa na chama tawala kusema haya ili chama tawala kipumue kidogo kutopoteza uhalali wake kwa wananchi. Nadhani mmechelewa kwa hili!
 
Ripoti imetoka polisi wanahusika na kifo hiki.

my take! wafuatao wajiuzulu au wawajibishwe mara moja.
1.IGP Said Mwema
2.Paul Chagonja
3.Kamuhanda
 
Theophil Makunga!!! Hii nchi inatia aibu sana!!! bro saini yako hiyo?
 
Poti sijakuelewa bado, ina maana uko hapa kusubiri tume ndio zikwambie ni nani alimuuwa Mwangosi? ina maana tangu siku ya kwanza hujui Mwangosi ameuliwa na nani? umenisikitisha sana halafu wewe una access na Internet vipi wale ndugu zako kijijini?

FFU.jpg
Nilijua kuwa wao ndio wamemuondoa Duniani ila kutokana na ubababishaji wa waliokuwa wakitoa habari walichanganya ila sasa hii tume angalau imejaribu kwenda ndani zaidi na kutoa picha inayoeleweka. Hivyo ndio maana nikasema wao polisi ndio waliomuua japo mi si mahakama ila kutokana na uchunguzi wa hii tume sihitaji tena mahakama inipe majibu
 
"Kamati ya Ushirikiano kati ya Jeshi la Polisi na Waandishi wa Habari iliyoanzishwa mwaka 2008 ifufuliwe." alafu? What the fu*****ck!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!
 
"Kuhusu operesheni ya uzuiaji wa mkutano wa CHADEMA usio halali Kijijini Nyololo tarehe 02 Septemba 2012, Jeshi la Polisi lilitekeleza wajibu wake ipasavyo na kutumia nguvu sahihi."

Shiiiiiiiiiiiiiiiiiit!!!!
:smash:
 
Tanzania bwana! sasa kwanini report ni ya kiingereza?
Mkuu wamefanya vema kuweka katika lugha zote mbili ili iwasaidie watu wa mataifa mbalimbali ambao Kiswahili hakipandi kusoma na kuelewa unyama uliotokea, kumbe ni kazi nzuri ya kuiweka katika lugha zote mbili. Kumbuka Balozi mbalimbali zinapenda kujua hili jambo.
 
wabheja sana n00b ngoja niagize kiccm(kiroba) kimoja na maji ya safari nianze kuipitia nukta kwa nukta ingawa haitakuwa na impact kimatokeo tofauti na ingekuwa imeundwa ile ya kijaji na vasco da gama.
 
Hii kamati ya Dr. Nchimbi fake kabisa, yaani inatia kichefuchefu
 
Back
Top Bottom