RIP: Shaaban Mloo is no more..

Mzee Mwanakijiji

Platinum Member
Mar 10, 2006
33,476
39,995
Mwananchi

MWANASIASA mashuhuri na muasisi wa Chama cha Wananchi (CUF), Shaaban Khamis Mloo, amefariki dunia katika Hospitali Kuu ya Mnazi Mmoja jana ambako alikuwa akitibiwa maradhi ya moyo.



Mloo alifariki dunia saa 2:00 asubuhi ambapo katika kipndi cha siku tatu alikuwa katika Chumba cha Wagonjwa Mahututi (ICU) alipokuwa akipata matibabu baada ya kuugua kwa muda mrefu.


Mloo alianza kuugua muda mrefu lakini hali yake ilikuwa haitabiriki na mara kwa mara alijikuta akilazimika kupelekwa hospitali.



Mkurugenzi wa Habari na Mawasiliano ya Umma wa Chama cha CUF, Salim Rashid Bimani amethibitisha kutokea kwa kifo hicho akifafanua kuwa marahemu Mloo alizikwa jana Shambani kwake katika kijiji cha Mfenesini, Mkoa wa Mjini Magharibi Unguja.



“Marehemu Mloo mwishoni mwaka jana, alilazwa ICU katika Hospitali ya Aga Khan, jijini Dar es Salaam kutokana na kusumbuliwa na maradhi hayo hayo ya moyo.


Alipata nafuu, lakini mwanzoni mwa wiki hii akazidiwa tena na ikabidi apelekwe Hospitali ya Mnazi Mmoja na kulazwa ICU pia,” alisema Bimani katika hali ambayo ilionyesha kuwa ana majonzi.



Alisema wanachama wa CUF wanatoa mkono wa pole kwa Mwenyekiti wa Chama cha CUF na familia ya marehemu, Mzee Mloo na wananchi wote wa Tanzania kwani kifo chake kitakuwa kimeacha pengo kubwa ndani ya chama hicho cha upinzani.


Alimuelezea Mloo kuwa alijitolea wakati wote kukitumikia chama chake cha CUF na changamoto zake zilikiwezesha kuwa na nguvu visiwani hapa.



Alisema licha ya kustaafu, Mzee Mloo alikuwa mstari wa mbele katika kutoa ushauri wa chama hicho na kukosoa kila alipobaini kuwa mwelekeo wa chama unakwenda isivyo.


Katika uhai wake, Mzee Mloo aliwahi kushika nyadhifa mbalimbali katika Serikali na katika Chama cha Mapinduzi (CCM), ikiwa ni pamoja na Katibu wa CCM Mkoa wa Pwani na Naibu Waziri wa Mawasiliano na Uchukuzi Serikali ya Mapinduzi Zanzibar.



Mzee Mloo alikuwa ni miongoni mwa Viongozi wa Vyama vya Wafanyakazi Zanzibar, kabla ya Mapinduzi na baada ya kuanza kwa Baraza la Wawakilishi, alikuwa Mjumbe wa Baraza hilo kwa vipndi kadhaa.



Mwanasiasa huyo mkongwe wa Zanzibar, akiwa na wenzake aliongoza harakati za kudai mageuzi ya kisiasa wakati huo akiwa na Ali Haji Pandu aliyekuwa mwanasheria mkuu wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar (SMZ), Hayati Maulid Makame, na Soud Yusuf Mgeni.


Kwa pamoja waliunda Kamati Huru ya Mageuzi ya Kisiasa (Kamahuru) kwa lengo la kuishinikiza SMZ ikubali mabadiliko ya kisiasa na kufuta mfumo wa chama kushika hatamu.

?Hata hivyo, Chama hicho baadaye kiliungana na Chama cha Wananchi Tanzania (CCWT) kilichokuwa kikiongozwa na Mwenyekiti wake, James Mapalala na kuzaliwa CUF ambapo hadi anamaliza uhai wake, Mzee Mloo alikuwa mwanachama wa chama hicho na kiongozi analiyeheshimika.



Mwanasiasa huyo maarufu Zanzibar kwa jina la “Kuchi”, alijiuzulu mambo ya siasa CUF mwaka 2002 na kubakia kama mwanachama wa kawaida na mshauri wa ngazi za juu wa chama hicho.



Mara baada ya kuanzishwa kwa Chama cha CUF, Mloo alikuwa Katibu Mkuu wa kwanza wa Chama hicho kabla ya kuwa Makamu Mwenyekiti wa CUF.


Marehemu Mloo ni miongoni mwa wanachama waliofukuzwa na CCM mwaka 1988 baada ya kuchafuka kwa hali ya hewa ya kisiasa Zanzibar.



Wengine waliofukuzwa ni Maalim Seif Shariff Hamad, Ali Haji Pandu, Khatib Hassan, Hamad Rashid Mohamed, Soud Yussuf Mgeni, Masoud Omar, Maulid Makame na Machano Khamis Ali.



Bimani alisema marehemu Mloo ataendelea kukumbukwa na CUF kuwa ni mfano wa mwanamageuzi asiyeyumba ambaye kwa wakati wote alitetea haki na usawa mbele ya jamii huku akiwa anajali sana kazi zake katika chama hicho.


Naye, Patricia Kimelemeta anaripoti kuwa Mwenyekiti wa CUF Taifa, Profesa Ibrahim Lipumba alisema kuwa Mzee Mloo alikitumikia chama hicho zaidi ya miaka nane, tangu mwaka 1992 hadi 2000 alipochukua nafasi ya umakamo mwenyekiti hadi alipostaafu mwaka 2004.



Taarifa hiyo ilieleza kuwa, CUF inamtambua Mzee Mloo sio tu kama kiongozi mstaafu wa Chama, bali mwasisi, mwanzilishi na mwanachama imara na shupavu katika siku zote za uhai wake.


"Atakumbukwa daima ndani na nje ya nchi kama mjuzi wa siasa za Zanzibar na za Tanzania kwa ujumla, mchapakazi na mtu aliyekuwa na ujasiri," alisema Profesa Lipumba kupitia taarifa hiyo.


Alifafanua kuwa kikao cha mwisho kuhudhuria ni mkutano mkuu wa nne wa CUF uliofanyika katika ukumbi wa Diamond Jubilee, Dar es Salaam, Februari 23 hadi 27 Februari, mwaka huu.


Taarifa hiyo ilieleza kuwa, kabla ya kustaafu aliwaaga wajumbe wa mkutano mkuu huo, februari 2004 kwa kuwapatia waraka maalum ambao uliandikwa ulisema:



“Nakuachieni Chama wajumbe wote wa mkutano mkuu huu wa leo, mukiwa na jukumu moja kubwa sana.


"Ingawa sisi tunastaafu, lakini tutaangalia kwa macho mawili utendaji wenu katika kata, matawi, majimbo, wilaya na taifa. Nakuachieni Chama kilichokamilisha theluthi mbili ya mtandao wake katika mikoa 26 ya Tanzania.


"CUF imeenea kila mkoa. Katika wilaya 130, CUF iko wilaya 117, katika vitongoji 38,000, CUF ina 20%, katika vijiji 11,600, CUF ina 15%. Mitaa yote 3,080, CUF ina 20%”,ilieleza sehemu ya waraka huo.
 
Mwenyezimungu amweke mahali pema na atuletee viongozi watakaoiga au kuwa na mfano kama wake.
 
Mmungu amhufirie madhabi yake na amuweke katika pepo karibu na yeye
Amin
 
Mwananchi

MWANASIASA mashuhuri na muasisi wa Chama cha Wananchi (CUF), Shaaban Khamis Mloo, amefariki dunia katika Hospitali Kuu ya Mnazi Mmoja jana ambako alikuwa akitibiwa maradhi ya moyo.



Mloo alifariki dunia saa 2:00 asubuhi ambapo katika kipndi cha siku tatu alikuwa katika Chumba cha Wagonjwa Mahututi (ICU) alipokuwa akipata matibabu baada ya kuugua kwa muda mrefu.


Mloo alianza kuugua muda mrefu lakini hali yake ilikuwa haitabiriki na mara kwa mara alijikuta akilazimika kupelekwa hospitali.



Mkurugenzi wa Habari na Mawasiliano ya Umma wa Chama cha CUF, Salim Rashid Bimani amethibitisha kutokea kwa kifo hicho akifafanua kuwa marahemu Mloo alizikwa jana Shambani kwake katika kijiji cha Mfenesini, Mkoa wa Mjini Magharibi Unguja.



“Marehemu Mloo mwishoni mwaka jana, alilazwa ICU katika Hospitali ya Aga Khan, jijini Dar es Salaam kutokana na kusumbuliwa na maradhi hayo hayo ya moyo.


Alipata nafuu, lakini mwanzoni mwa wiki hii akazidiwa tena na ikabidi apelekwe Hospitali ya Mnazi Mmoja na kulazwa ICU pia,” alisema Bimani katika hali ambayo ilionyesha kuwa ana majonzi.



Alisema wanachama wa CUF wanatoa mkono wa pole kwa Mwenyekiti wa Chama cha CUF na familia ya marehemu, Mzee Mloo na wananchi wote wa Tanzania kwani kifo chake kitakuwa kimeacha pengo kubwa ndani ya chama hicho cha upinzani.


Alimuelezea Mloo kuwa alijitolea wakati wote kukitumikia chama chake cha CUF na changamoto zake zilikiwezesha kuwa na nguvu visiwani hapa.



Alisema licha ya kustaafu, Mzee Mloo alikuwa mstari wa mbele katika kutoa ushauri wa chama hicho na kukosoa kila alipobaini kuwa mwelekeo wa chama unakwenda isivyo.


Katika uhai wake, Mzee Mloo aliwahi kushika nyadhifa mbalimbali katika Serikali na katika Chama cha Mapinduzi (CCM), ikiwa ni pamoja na Katibu wa CCM Mkoa wa Pwani na Naibu Waziri wa Mawasiliano na Uchukuzi Serikali ya Mapinduzi Zanzibar.



Mzee Mloo alikuwa ni miongoni mwa Viongozi wa Vyama vya Wafanyakazi Zanzibar, kabla ya Mapinduzi na baada ya kuanza kwa Baraza la Wawakilishi, alikuwa Mjumbe wa Baraza hilo kwa vipndi kadhaa.



Mwanasiasa huyo mkongwe wa Zanzibar, akiwa na wenzake aliongoza harakati za kudai mageuzi ya kisiasa wakati huo akiwa na Ali Haji Pandu aliyekuwa mwanasheria mkuu wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar (SMZ), Hayati Maulid Makame, na Soud Yusuf Mgeni.


Kwa pamoja waliunda Kamati Huru ya Mageuzi ya Kisiasa (Kamahuru) kwa lengo la kuishinikiza SMZ ikubali mabadiliko ya kisiasa na kufuta mfumo wa chama kushika hatamu.

?Hata hivyo, Chama hicho baadaye kiliungana na Chama cha Wananchi Tanzania (CCWT) kilichokuwa kikiongozwa na Mwenyekiti wake, James Mapalala na kuzaliwa CUF ambapo hadi anamaliza uhai wake, Mzee Mloo alikuwa mwanachama wa chama hicho na kiongozi analiyeheshimika.



Mwanasiasa huyo maarufu Zanzibar kwa jina la “Kuchi”, alijiuzulu mambo ya siasa CUF mwaka 2002 na kubakia kama mwanachama wa kawaida na mshauri wa ngazi za juu wa chama hicho.



Mara baada ya kuanzishwa kwa Chama cha CUF, Mloo alikuwa Katibu Mkuu wa kwanza wa Chama hicho kabla ya kuwa Makamu Mwenyekiti wa CUF.


Marehemu Mloo ni miongoni mwa wanachama waliofukuzwa na CCM mwaka 1988 baada ya kuchafuka kwa hali ya hewa ya kisiasa Zanzibar.



Wengine waliofukuzwa ni Maalim Seif Shariff Hamad, Ali Haji Pandu, Khatib Hassan, Hamad Rashid Mohamed, Soud Yussuf Mgeni, Masoud Omar, Maulid Makame na Machano Khamis Ali.



Bimani alisema marehemu Mloo ataendelea kukumbukwa na CUF kuwa ni mfano wa mwanamageuzi asiyeyumba ambaye kwa wakati wote alitetea haki na usawa mbele ya jamii huku akiwa anajali sana kazi zake katika chama hicho.


Naye, Patricia Kimelemeta anaripoti kuwa Mwenyekiti wa CUF Taifa, Profesa Ibrahim Lipumba alisema kuwa Mzee Mloo alikitumikia chama hicho zaidi ya miaka nane, tangu mwaka 1992 hadi 2000 alipochukua nafasi ya umakamo mwenyekiti hadi alipostaafu mwaka 2004.



Taarifa hiyo ilieleza kuwa, CUF inamtambua Mzee Mloo sio tu kama kiongozi mstaafu wa Chama, bali mwasisi, mwanzilishi na mwanachama imara na shupavu katika siku zote za uhai wake.


"Atakumbukwa daima ndani na nje ya nchi kama mjuzi wa siasa za Zanzibar na za Tanzania kwa ujumla, mchapakazi na mtu aliyekuwa na ujasiri," alisema Profesa Lipumba kupitia taarifa hiyo.


Alifafanua kuwa kikao cha mwisho kuhudhuria ni mkutano mkuu wa nne wa CUF uliofanyika katika ukumbi wa Diamond Jubilee, Dar es Salaam, Februari 23 hadi 27 Februari, mwaka huu.


Taarifa hiyo ilieleza kuwa, kabla ya kustaafu aliwaaga wajumbe wa mkutano mkuu huo, februari 2004 kwa kuwapatia waraka maalum ambao uliandikwa ulisema:



“Nakuachieni Chama wajumbe wote wa mkutano mkuu huu wa leo, mukiwa na jukumu moja kubwa sana.


"Ingawa sisi tunastaafu, lakini tutaangalia kwa macho mawili utendaji wenu katika kata, matawi, majimbo, wilaya na taifa. Nakuachieni Chama kilichokamilisha theluthi mbili ya mtandao wake katika mikoa 26 ya Tanzania.


"CUF imeenea kila mkoa. Katika wilaya 130, CUF iko wilaya 117, katika vitongoji 38,000, CUF ina 20%, katika vijiji 11,600, CUF ina 15%. Mitaa yote 3,080, CUF ina 20%”,ilieleza sehemu ya waraka huo.
Inna lillah wa inna ilayhi rajiuun, hakika sisi sote tunatoka kwa Muumba na kwake tutarejea.
Mungu amlaze mahala pema peponi, Mzee Mloo, ambaye ameondoka wakati tukiwa bado tunasubiri mapambazuko na mawio ya haki ya kweli visiwani.
 
RIP Shaaban Mloo, mpiganaji wa mabadiliko ya kweli Tanzania. Pole kwa ndugu na marafiki.
 
Mbele yako nyuma yetu, Mungu atupe amani ktk hili zito kwa nchi yetu,Amen
 
RIP Mzee Mloo, tutakukumbuka kwa mengi, ikiwemo busara, upendo na upole wako
 
Back
Top Bottom