Ridhiwan Kikwete: Mimi si fisadi

Ridhiwan Kikwete: Mimi si fisadi

wiki mbili zilizopita alikuwepo kule kigamboni kusuluhisha wanaccm. matokeo yake kuna mwanachama wa ccm alidungwa nondo na kuzirai mbele yake. lakini media haikuripoti. nilimwona aliyefanyiwa hiyo ishu ana bendeji.

Source: mimi
 
hana lolote huyu,tabia za kikwere tuu, akikua ataacha, dunia ya leo hiyo mitindo haipo yani. tulizoea zamani kutishiwa na watoto wa yona,kina kippi, sijui mkurugenzi wa bandari mitoto yake, but miaka hii nooop!
 
hana lolote huyu,tabia za kikwere tuu, akikua ataacha, dunia ya leo hiyo mitindo haipo yani. tulizoea zamani kutishiwa na watoto wa yona,kina kippi, sijui mkurugenzi wa bandari mitoto yake, but miaka hii nooop!

Nchi yenye uongozi bora ni uongozi wa team work chini ya watu wenye busara zao waliokomaa akili, si uongozi wa kifamilia, TZ is Bagamoyo wala Chanika peke yake, haikuwapasa kuiona nchi kama sebuleni kwao, vilio vya wa TZ wote vita wainamia, nakuwa mafuriko ya sunami, yaani matone ya kila mTZ yakiunganiswa yatawatoa nchi ya Ikulu we ngoja 2, Riziki 1 asijione kafoka atamfikisha baba yake pabaya wakati utakapofika wakuondolewa mzingo wa sheria na kuulizwa kwa nini aliiweka nchi chini ya uchief wa kikwere?
Mungu si mkwere atasikia kiliocetu haki maji mengi yatawazoa 2.
Mungu ibariki TZ, Mungu mbariki DR, Slaa na TZ kwa ujumla.
 
Hivi mmesahau kuwa huyu dogo naye alikuwa moja ya mafisadi wa EPA?? kuna kampuni alifungua na kuchukua 3Bil.. Ila nasikia alirudisha vipi sijui..

JK ndiye anayempa kichwa sawa na mama salma.. sasa hawa tarehe 31 oct 10 wanarudi chalinze kuanza maisha ya kulima.. biashara za ikulu zinakwisha...
 
Kazi yetu kama wapigakura ni kuwafuta kazi CCM na Jk wake baada ya hapo tutawasikia wanaelekea wapi wababaishaji hawa? Na mali zetu tutahakikisha wanazirudisha na wasipokaa chonjo jela inawanukia kihaswaaaaaaa
 
tupa kule.babake ndo kamdanganya kuwa nchi ni yao ila mwisho wao jpili,mi ananitia asira,anyway cha kufanya ni kumpigia kura slaa
 
Baba yake akishindwa na yeye pia kwaheri, ningekuwa mimi ndo Ridhione nisingegusa kabisa hata hapo ikulu, ningehangaika na issue zangu tu. Mkapa watoto wake na mke hawakugusa hata siku moja siasa. Walikuwa busy na NGO na Kiwira.

Mkuu, sina mbavu!! lakini ni kweli, yeye hajapewa mandate yoyote na Watanzania. Ni ulimbukeni wa hali ya juu.
 
Ningelikuwa yeye ningeanza kufungasha virago,maana ikulu haitawahusu tena pale maana watanzania wanaenda kumfuta kazi baba-ke JK
 
wiki mbili zilizopita alikuwepo kule kigamboni kusuluhisha wanaccm. matokeo yake kuna mwanachama wa ccm alidungwa nondo na kuzirai mbele yake. lakini media haikuripoti. nilimwona aliyefanyiwa hiyo ishu ana bendeji.

Source: mimi[/QUOTE]

NImeipenda hii:thumb:
 
ANAPEWA KICHWA NA BABA YAKE SI AMEAMBIWA URAIS NI WA FAMILIA! NAMUONEA HURUMA MWISHO WAKE UTAKUWAJE TUTAKAPO MTANGAZA DR WA UKWELI SLAA KUWA NDIYE RAIS WA WATANZANIA SIO Familia :thumb:
 
Urais wa Kiwete ni wake na familia yake kataachaje kuwa na jeuri! mapaka katawatomasa mwaka huu kama wa-TZ hawatakuwa macho. na nyie kwanini mnakachelewesha kwa nini msikikate mtama!! Kama inawezekana kwa OCD kukatwa mtama mbele ya vijana wake akiwa na magwanda yake mnashindwaje kwa hako!!!! Wa-TZ tuungane tuwang'oe hawa Wakwere, sikujua kama Wakwere wana akili fupi kiasi hicho!! Hivi hajakua tu kakaanza kujitegemea?? Jamani!! AIBU
 
H@ki Ngowi

Je nikuwa Ridhiwani ampa tafu Masuni au Ridhiwani ndio anataka tafu kwa masauni ili Amsaidie baba yake.

Huu unafiki ni wa hali ya juu,ingawa wanasema hakuna adui wa kudumu kwenye siasa ila this was going personal .
 
Tafu gani hii wakati ngoma ndiyo inaisha hivyo, si kumeshakuchwa sasa! Na namna hii kutakuja kuwa na utawala wa sheria bongo kweli? Mtu ametuhumiwa kugushi, ananyang'anywa wadhifa alionao, baada ya hapo hakuna hatua yeyote inayochukuliwa. Sasa walewale waliomtuhumu eti wanampiga tafu!!! Du!
 
Wakili uchwara RIZIWANI anadhani uper second yake ya kuhonga ndo inampa credibility ya kukubalika.

huyu dogo anabebwa na dola kwani ningekuwa mimi makame au tendwa ningeshamuengua kikwete kwa kadhia ya huyu dogo
 
kikwete na chama cha kidini ccm wanaweka mahakama ya kadhi.....wanahubiri oic....viongozi ngazi za juu waislamu
 
kikwete na chama cha kidini ccm wanaweka mahakama ya kadhi.....wanahubiri oic....viongozi ngazi za juu waislamu

Usileta udini katika hoja ya msingi. Tumeshasema hatutaki udini hapa JF ni bora anzisha blog yako ya kueneza udini na kisha utalipa hasara yake mwisho wa vita ya kidini.

Hoja iliyo mbele yetu ni ya Ridhwan kumpiga tafu Msauni wewe unaamsha hisia za kidini hapa. Hufai kuishi Tanzania ni bora uende Sudan au Nigeria utaupata udini na majanga ya maafa yaliyotokana na vita ya kuhubiri udini.

Natamani nikutandike viboko 12 kwa ajili ya kuwapooza watanzania walioumizwa mioyo yao na post yako inayopandikiza udini na viboko vingine 12 ukawaonyeshe waliokutuma kupandikiza udini Tanzania.

Kama hutaki Mahakama ya Kadhi au OIC jenga hoja na sisi tutakusaidia kukubaliana au kutokukubaliana na hoja zako lakini katika hoja zako usionyeshe unataka kudhalilisha dini fulani iwe ukristo au uislamu.
Nia yetu wote iwe ni kujenga Tanzania yenye amani inayohubiri upendo wa dhati kati ya Waislamu na wakristo.

kama una lengo la kututenganisha kwa msingi wa dini hutufai kabisa kabisa nchini Tanzania.
 
kikwete na chama cha kidini ccm wanaweka mahakama ya kadhi.....wanahubiri oic....viongozi ngazi za juu waislamu


Binafsi nimeumizwa sana na post yako. katika ukiristo na katika mahubiri ya Yesu kiristo au katika kitabu kitakatifu cha Bibilia hakuna mahala ambapo dini hii inasema ili kumfikia Mungu kwanza utukane dini za wengine. Bwana Yesu ziku zote alihubiri upendo kwa binadamu wote na ni jukumu letu wakristo kuwakataa wakristo wenzetu wanaohubiri chuki kwa binadamu wenzao.

Kama kuna ukurasa, sura au mstari katika Bibilia ulioandikwa kutukana dini zingine au watu wasio na dini naomba kifungu hicho ili tung'oe mzizi wa fitina za kidini. Tusifanye mambo ambayo vitabu vyetu vya dini vinakataza kufanya.

Kama umekwazwa na jambo kutoka kwa wenzio wa dini ingine jenga hoja utasikilizwa.Epuka kutukana dini za wenzako zina thamani kama dini yako.

Katika ukristo upendo ni kila kitu kuelekea kwa mwenyezi Mungu.
 
kikwete na chama cha kidini ccm wanaweka mahakama ya kadhi.....wanahubiri oic....viongozi ngazi za juu waislamu

wee lazima utakuwa ubwabwa wewe, acha kabisa mambo yako ya udini we juha, mwehu us'o haya
 
Back
Top Bottom