Rias Samia kununua kila goli la Yanga kwa Tsh. Milioni 20

Roving Journalist

JF Roving Journalist
Apr 18, 2017
2,812
11,989
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akishiriki Uzinduzi wa Mradi wa Minara ya Kurusha Matangazo ya Televisheni Ardhini(DTT) ya Kampuni ya Azam Media Limited, Makao Makuu ya Azam Media Limited- Tabata Dares Salaam leo tarehe 18 Mei, 2023.



Rais Samia Suluhu Hassan ametangaza kuongeza Fedha za Motisha kwa Yanga SC inayoshiriki michuano ya Kombe la Shirikisho Afrika kutoka Tsh. Milioni 10 hadi Tsh. Milioni 20 kwa kila goli la ushindi.

Uamuzi huo unafuatia ushindi wa Magoli 4-1 dhidi ya Marumo Gallants FC ya Afrika Kusini ulioipeleka Yanga SC katika Fainali ikiwa ni Timu ya kwanza kutoka Tanzania kufanikiwa kufika hatua hiyo lakini amesisitiza kuwa fedha hizo zitatolewa ikiwa magoli yataipa ushindi timu.

Pia, Serikali imetoa ndege itakayobeba mashabiki na wachezaji kama Sehemu ya kuwatia moyo ili wafanye vizuri zaidi. Ndege hiyo itawapeleka, kuwasubiri na kuwarejesha.

Ameipongeza Azam kwa uwekezaji mkubwa waliofanya kwenye Sekta ya Habari na Mawasiliano. Teknolojia hii waliyoanzisha haitaongeza ubora wa picha pekee, bali pamoja na wingi wa chaneli.

Mtoto.jpg

11928834-8c6f-4e32-9974-22603789826a.jpg

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akifurahia jambo wakati Mtoto Georgina Magesa (8) akiwa ameketi kwenye Kiti cha Rais mara baada ya kukutana naye katika hafla ya uzinduzi wa Minara ya kurusha matangazo ya Televisheni Ardhini (DTT) ya Azam Media iliyofanyika katika Ofisi zao zilizopo katika Barabara ya Mandela Jijini Dar es Salaam.


784336aa-29c7-46c5-a495-996ee567bce2.jpg

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akipokea zawadi ya King’amuzi kutoka kwa Mkurugenzi Mtendaji wa Azam Ndugu Abubakar Said Salim Bakhresa kwa ajili ya kuangalia maudhui mbalimbali ya Azam TV mara baada ya kuzindua mradi wa Minara ya kurusha matangazo ya Televisheni Ardhini (DTT) ya Kampuni hiyo kwenye hafla iliyofanyika katika Ofisi zao zilizopo Barabara ya Mandela Jijini Dar es Salaam tarehe 18 Mei, 2023.

08b5dfbb-a59d-4388-bfc8-246e01c25e72.jpg

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akizungumza na viongozi pamoja na Wafanyakazi wa Azam Media mara baada ya kufungua Minara ya kurusha matangazo ya Televisheni Ardhini (DTT) ya Kampuni hiyo kwenye hafla iliyofanyika katika Ofisi za Kampuni hiyo zilizopo Barabara ya Mandela Jijini Dar es Salaam tarehe 18 Mei, 2023.

Pia soma: Rais Samia kununua kila goli Tsh. Milioni 5 mechi za Simba, Yanga CAF
 
Sasa me najiuliza mbona enzi za Mwendazake hawakuwahi kumuita kuzindua vitu kama hivi.... Yan kila siku kuzindua taka taka mpya tu..

Kazi kweli kweli
 
Uzinduzi wa minara ya digital terrestrial television (DTT) transmitter network.

The uplink of Azam Media channels to satellite, which are then received by DTT towers for terrestrial transmission.

This ensures that all Tanzanian households have access to high-quality television at a minimal cost.

Leading in technology deployment and coverage using the latest standards in DVB-S2 and DVB-T2, ADBL will continue expanding its terrestrial infrastructure to reach remote areas.

Using state-of-the-art Downlink and Uplink Head End facilities and Network Operator Centres (NOC), we are responsible to manage and maintain the network and infrastructure of both DTH and DTT platforms.

Azam Digital Broadcast Limited (ADBL) has made significant investments in the deployment of DTT Towers and top-of-the-line equipment with its network situated in 26 strategic locations across Tanzania.

Source : https://bakhresa.com/azam-digital/
 
Uzinduzi wa digital terrestrial television (DTT) transmitter network.

The uplink of Azam Media channels to satellite, which are then received by DTT towers for terrestrial transmission.

This ensures that all Tanzanian households have access to high-quality television at a minimal cost.

Leading in technology deployment and coverage using the latest standards in DVB-S2 and DVB-T2, ADBL will continue expanding its terrestrial infrastructure to reach remote areas.

Source : https://bakhresa.com/azam-digital/
Kwa hi technology Azam media itakua zaidi ya TBC ni haki kwa Raisi kuenda kufungua kitu hicho kwa niaba ya wananchi wote tumepiga atua kubwa kwenye media
 
Sasa me najiuliza mbona enzi za Mwendazake hawakuwahi kumuita kuzindua vitu kama hivi.... Yan kila siku kuzindua taka taka mpya tu..

Kazi kweli kweli
Magufuli amewahi kuitwa na Azam kuzinduwa kiwanda Cha kuchakata embe na kuzikausha na pale pale akamwambia mi napenda wewe Bakhresa pia ujenge kiwanda Cha Samaki hapa Pwani eneo ntakupatia Mimi mwenyewe ila sikuona watu wanapiga kelele kama Leo.
 
Magufuli amewahi kuitwa na Azam kuzinduwa kiwanda Cha kuchakata embe na kuzikausha na pale pale akamwambia mi napenda wewe Bakhresa pia ujenge kiwanda Cha Samaki hapa Pwani eneo ntakupatia Mimi mwenyewe ila sikuona watu wanapiga kelele kama Leo.
Kiwanda cha sukali sio samaki na sukali ya azam imeanza kutoka tayari watu hawaoni umuhimu wa huyu jama ila wanatazama imani yake tu.
 
Tutaweza sasa kupokea matangazo ya televisheni kwa antenna zilizopo katika mapaa ya nyumba zenu au ndani ya kumbi za nyumba zetu bila kutumia dishi .

Mtaalamu anafafanua DTT

9 January 2019
Oscar Nichor, Chief Operations Officer (TV Broadcast) at K-Net, explains what is DTT (digital terrestrial television)
 
Back
Top Bottom