Watanzania kwa nadharia hatujambo. Kwani Kenya wakati wanajenga SGR yao TZ walikuwa wapi, wakati Kenya Airways inatamba, ATCL walikuwa wapi, makampuni karibu yote ya kimataifa yameweka HUB zao Kenya hata BBC, CGTN n.k. Tumejaa nadharia kama washabiki wa Yanga na Simba, kila shabiki anaamini timu yake ni bora lakini hawajiulizi mbona hawashindi mechi za kimataifa! Acha kuandika kama shabiki wa chama cha kisiasa, magari kuharibu barabara ndio awamu hii umeanza kuona hilo tatizo, ni kama vile raia anaeshabikia majumba kubomolewa wakati kila mtu anajua serikali haina uwezo kuwajengea raia wake makazi. Hakuna kigeni ambacho Nyerere hakukifanya na vyote imebaki historia.